Ni kwa kutoa kauli kuwa Rais Kikwete ni dhaifu!
Amekataa kufuta kauli yake na ametolewa nje ya Ukumbi.
Ni kwa kutoa kauli kuwa Rais Kikwete ni dhaifu!
Amekataa kufuta kauli yake na ametolewa nje ya Ukumbi.
Mkitaka kujuwa hii nchi ilipofikia ni mahala pabaya, hapa Riziwani Kikwete kwenye Facebook eti anawaambia watu atajibu hoja zao kwa niaba ya Serikali, jamani msisubiri mpaka tuingizwe vidole vya haja kubwa ndio mjuwe tunatukanwa na kudhalilishwa, mwenye masikio na asikie na mwenye macho na aone, huu ni sehemu ya Udhaifu wa JK, ingalikuwa enzi za Mwalimu hawa kina Makongoro wasingethubutu kufanya upumbavu huu.
Ridhiwani Kikwete
MAJIBU YA MASWALI YANGU KWA NIABA YA MH.WAZIRI WA FEDHA
Mh.Spika, jana niliuliza swali na leo narejea hapa barazani kueleza kuwa sikupata majibu toka kwa mheshimiwa waziri lakini baadhi ya wajumbe walijibu haya na hii sehemu ya majibu yao.
A. Maana ya bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha ni, maelezo na mipango ya kimatumizi ya serikali katika ule mwaka wa fedha uliotajwa. kwa mfano, bajeti aliyoisoma juzi bwana Mgimwa (mb) ni mpango wa matumizi ya serikali ya jamhuri ya muungano kwa mwaka huu wa fedha. hivyo basi ni mataraji kwamba wabunge wangeelewa haya pasi kulalamika.
BE. si kweli kwamba serikali haina mipango ya utekelezaji wa bajeti yake. ikumbukwe juzi siku ya kwanza kabla bajeti haijasomwa , mheshiwa Steven Masatu Wasira (mb) alisimama mbele ya bunge tukufu na kutoa mpango wa kazi na jinsi serikali ilivyojipanga. hii ilimaanisha kwamba hali ya kiuchumi,changamoto na maeneo ambayo serikali itayaangalia ikiwa ni katika kutimiza utekelezaji wa ilani ambayo tuliinadi kwa wananchi mwaka 2010 ambayo tutakuja pimwa mwaka 2015.
CHE. Kuhusu wabunge kuwa hawajui mipango ya serikali yao, s la kweli. tatizo linalojitokeza ni uelewa juu ya nini majukumu ya wabunge inapokuja wenye kujadili bajeti. hili nalifananaisha na mtu ambaye anataka panga matumizi ya mfuko wa mtu wakati alimwambia kuwa nakupa siku kumi uwe umeshanilipa kiasi ninachokudai. serikali ya CCM ipo katika kutimiza madeni waliyowaambia wananchi kuwa wangewalipa ifikapo mwaka 2015. kwa lugha nyengine hata kama serikali ingesema kuwa bajeti ya mwaka huu wa fedha itajikita katika masuala mawili tu ya barabara na maji, wajibu wa wabunge ni kusema kuhoji kwa nini vtu vyengine havijawekwa. majibu yatakayolewa ndiyo majibu kwa maana ya kwamba serikali imepanga kutekeleza hayo. suala la kwamba sintopitisha bajeti kwa sababu vipa umbele vyangu havijawekwa hilo sasa ni tatizo la mmoja mmoja ambalo haliwezi wekwa ndani ya bajeti.
kubwa zaidi wasijisahau wabunge wakafikiri wanaweza semea matatizo yote ya nchi ndani ya bajeti ya mwaka mmoja tu wa fedha. kwa upande mwengin ni changamoto kwa serikali kuwaelelewesha wabunge juu ya utaratibu huu.
ushauri
wajikite kuangalia kama mpangilio na mgawanyiko wa fedha unaweza kusaidia kunyanyua au kuleta tija za kimaendeleo katika maeneo yaliyotajwa. maeneo mengine bajeti zitakaz fuata.
nawasilisha tujadili majibu ya hawa wananchi wazalendo , kama walivyojiita.
Division four point 29 = Masters Mzumbe University. Nape Nnauye is my role model.
Goes on bro! This country mics pp like u! Mnafiki tu uyo spika,kwan hajui kwamba mkubwa ni dhaifu?
We hijawahi kuona refa anatoa kadi nyekundu kwa mchezaji wa timu mojawapo uwanjani then akijishtukia aliboronga anasawazisha kwa kutoa penati kwa timu pinzani? Kwa kifupi hakuwa fair kwa kuwaacha Lusinde na Nchemba waliotukana jana na leo bila ya kuwaadhibu; Hii siyo mara ya kwanza Spika kulalamikiwa kwa kupendelea wabunge wa ccm hata kwa mambo ya kipuuzi. Taasisi ya Uraisi ndo kitu gani mbele ya maslahi ya walioiweka madarakani????
Goes on bro! This country mics pp like u! Mnafiki tu uyo spika,kwan hajui kwamba mkubwa ni dhaifu? U -ccm ndo unamsumbua!
Kama Rais mpaka apewe kibali na CC ya chama chake ndio awaondoe mawaziri wabovu huyo ni dhaifu period. Katika hili hakuna sababu za kumnyooshea kidole Mnyika kuwa kapotoka, maana aliposema afafanue kwa nini kasema Rais ni dhaifu Ndugai kwa sababu anaelewa kuwa kauli hiyo ya Mnyika ni kweli kakataa ili asimuumbue mwenyekiti wa chama chake.
Hatutajua chochote iwapo hatutahoji na kudadisi
Hivi hili neno alilolisema Mnyika humu JF sio tusi? Mbona sijaona haka kaneno 'BANNED' kwa wanaorudia hili hili la Mnyika humu JF? Hili ni tusi 'jengo la posho' tu?
Uchakavu wa Mahakama si nafuu ya hukumu!
Ahahahaha, Magamba yalikuwa yanarusha mawe wakati yanaishi kwenye nyumba za vioo,tatizo lao wanatukana sana tena matusi ya nguoni na hawafanywi kitu, mtu akisema ukweli wanatumia wingi wao na madaraka ya spika kuwatoa nje,mi nadhani tuvumilie tu, bado kidogo sana tutafika cause 2015 sio mbali,tutafika tu, kwa mwendo wa farsi ama kinyonga.
Moto unaoteketeza misitu minene na mbuga za wanyama huaza kama spark. Pia jipu huanza kama kipele kidogo vile.
Mataizo yameanza kitambo kidogo, Awamu ya pili, tatu, na nne ni balaa.
Mzee ruksa alitoa ruhusa kila mtu kuchuma atakavyo watu wakachuma mpaka Lolyondo na Katabaro sasa havipo tena, mrema akajifanya kukamata biashara ya bi mkubwa pale airport sikaenada na maji nk nk.........watu wenye uwezo wakaneemeka.
Mkapa kaja na ufisadi ukijificha kwenye kivuli cha ubinafsishaji na ubia, mpuuzi kauza viwanda, madini, ardhi, mashirika ya uma nk. kashfa nzitonzito zikaanza kujitokeza (EPA, DEEP GREEN, Kagoda nk........) CCM wakiiba fedha nyingi kuhonga wapiga kura kupitia kashfa hizi. Lakini alidhibiti mfumko wa bei, alikusanya kodi na serikali ilikuwa na fedha. Alikuwa na jeuri ya kusema sitaki hiki nataka kifanyike kile, walau balaza lake la mawaziri lilikuwa stable ukilinganisha na awamu ya nne. Alikuwa mchafu aliejificha na uchafu wake mwingi umegundulika wamu ya nne.
Kikwete kaja na sifa nyingi, mzee wa ahadi nyingi zisizotekelezeka, maishabora kwa kila mtanzania maneno matupu, Nguvu zaid, ari zaidi na kasi zaidi imekuwa polepole zaidi ya konokono, Hana maamuzi , hukaa kimya akivizia upepo kupowa na kuchukuwa opotunity ya kuzuga watu, kiongozi ambaye serikali yake ameivunja takribani mara mbili-recod, shilingi imeyumba, maisha yamekuwa magumu kupita kiasai, mfumko wa bei usio na kiwango, polojo nyingi katika maandishi yasioendana na uhaliasia, anamapato zaidi ya wote wliomtangulia lakini anamatumizi ya ovyo kuliko wote waliomtangulia na serikali haina fedha- anavuna dhahabu kwa wingi, misitu kwa wingi, anauza ardhi kwa wingi, ameshindwa kuilinda shilingi, elimu imeshuka ubora kupita kiasi, afya imepoteza muelekeo.......(Anaomba sana nje)
Kizazi cha sasa ni tofauti na cha nyerere na mwinyi, sasahivi tumeelevuka, tunahitaji kujuwa mali zetu za asili na kodi zetu anakula nan na nani na kwa manufaa gani.
Kwa ufupi hatudanganyiki tunahitaji ukweli hapa ndipo penye matatizo, CCM na kikwete wanataka kuishi kwa mazoea kitu ambacho kwa jamii ya sasa hakiwezekani na hapa ndipo Kikwete anapopata challenge lazima ashambuliwe maana JIPU HUPASULIWA LIKISHAIVA SASA JAMII IMEIVA INAFAHAMU HAKI ZAKE ZA MSINGI.
Hashambuliwi kikwete kwa sababu ya dini yake la ila kwa matendo yake ya kutochukua hatua mara moja inapotakiwa kufanya hivyo, kucheka na kula na mafisadi mbaya zaidi kuwapigia kampeni majukwaani, ahadi za uongo pasi na kusoma alama za nyakati.
"Ikulu ni mahala PATAKATIFU,
mimi sikuchaguliwa kuja kupageuza kuwa pango la wala RUSHWA."
By J.K. NYERERE.
rais wetu ni hola kama anavoonekana![]()
rais asiyejua kwa nini nchi yake ni
maskini wakat ina raslimaki kibao
huo sio udhaifu??4leni za magari
jijin dsm rais anasema eti hayo ni
maisha bora! Huo sio udhaifu??
Kumteua mgonjwa mahututi kuwa
wa wazir asiyekuwa na wizara
maalumu isiyo na ofc! Huo sio
udhaifu?? Brother mnyika we si wa
kwanza kusema kikwete ni
dhaifu.hata nyerere alishawah
kusema 95 kwamba 'hatumchagui
m2 awe rais kwa sura yake.kwa
sababu haendi kuwa rais wa mamiss
2nataka rais mchapa kazi na
muadilifu'
anatia huruma
Taarifa: ile Propaganda mashine ya CCM Dr Benson Bana yupo studio za Clouds kwenye kipindi cha Jahazi, hapa huitajiki kuwa na Degree kujuwa yupo hapo studio kwa kazi gani na malipo yanatoka wapi.
Mimi binafsi nina aleji na hiyo redio wenye access tune Clouds mtatujurisha. najuwa hapo Dr Bana povu litamtoka haswa ili malipo yawe mazuri.
Division four point 29 = Masters Mzumbe University. Nape Nnauye is my role model.
hivi huyu Kikwete yupo hapa nchini?
Ninachohisi ni kua leo wakati bunge linaendelea Naibu Spika alidhani anaendesha kikao cha chaama ndio maana akajikuta anafanya kiroja cha kumtoa nje Kamanda Mnyika JJ
Kweli ni dhaifu. Wapi pesa za rada?, issue ya Jairo? EPA?, issue ya Yona na Mgonja? etc dhaifu*15tirioni za bajeti yake.
Laiti kama ungejua kuwa ule ni ustahimilivu, basi ndiyo ungekiri uwezo wa JK kama kiongozi. Watu wa aina ile unawategemea, LAKINI SIYO BUNGENI. tatizo hapa ni kwamba HANSARD za BUNGE haziwezi kuweka hayo katika kumbu kumbu, tena out of context. Mjadala unaoendelea ni Bajeti, siyo uwezo wa Rais. Hilo likijadiliwa Bungeni, basi uje mambo ni mazito sana. So JK atamwachia Speaker na Uongozi wa Bunge kumshughulikia Mbunge mtovu wa nidhamu, aliyeishiwa hoja.
Lakini nakwambia, ukitaka kujua nini kinamuudhi, mwambieni huyo Mh. Mnyika afanye tendo la kihaini, au hata aashirie tu ndiyo mtamtambua. Alishawaonya, "This smile may be quite deceiving".
Raisi hajulikani yu wapi wakati wowote anavuta mwewe anaenda kuangalia DEAD SEA kuhakikisha kweli kama hakuna kiumbe anaishi humo.....
Duh! Full practical hataki kusimuliwa.
Follow Us Here