Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: CHADEMA kuwakataa viongozi wa CCM

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 37
    1. FJM
      #1
      FJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 7,179
      Rep Power : 2569
      Likes Received
      5331
      Likes Given
      4587

      Default CHADEMA kuwakataa viongozi wa CCM

      CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimetangaza rasmi kusitisha kuwapokea viongozi wa ngazi zote watakaohama kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) na vyama vingine, baada ya kutemwa katika kura za maoni kwa lengo la kutaka kuwania nafasi za uongozi ndani ya chama hicho.

      Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alitoa msimamo huo jana alipokutana na wanafunzi wa vyuo vikuu vitatu vya Udom, CBE na St John, katika hafla ya kuwaaga wenzao wanaomaliza masomo yao.

      Mbowe alisema kuwa, CHADEMA kinataka sasa kupata viongozi na wanachama wanaosukumwa na uzalendo wa kweli, na wanaoamini itikadi na sera zake, na si wanaotaka kukitumia kama ngazi ya kufanikisha malengo yao.

      Alisema wamejifunza kwa kiasi kikubwa hasara ya kuwapokea wanachama, na hasa waliokuwa viongozi wa vyama vingine dakika za mwisho, hususan wakati wa uchaguzi, hivyo kuanzia sasa hawapo tayari kufanya hivyo.

      Mbowe alisema wapo tayari na wanawakaribisha wanachama ama viongozi wa CCM ambao wanaona kuwa CHADEMA ni chama makini, kikomavu na wanaoamini kina malengo halisi ya kuikomboa nchi na kuwaletea maendeleo wananchi wote bila kujali itikadi ya vyama, dini, kabila ama eneo la nchi.

      “Wale wapambanaji waliochoshwa na matendo ya wenzao ndani ya CCM, na wanaoamini kwa dhati kabisa na kusukumwa na dhamiri ya kweli ya kupigania maslahi ya wanyonge, waje sasa.

      “Hakuna haja ya wao kusubiri hadi dakika za mwisho, na hasa pale wanapopigwa chini katika kura za maoni ndio waje. Wajue kuwa wakisubiri muda huo, hawataweza kupokelewa hata kama watakuwa ni wazuri namna gani,” alisema Mbowe

      Source: Tanzania Daima



      My take: Hii itasaidia sana kukwepa kadhia kama ya Shibuda. Na ingekuwa vizuri kwa kila chama. Haiwezakani leo uko chama hiki lakini kesho uko upande wa pili. Unasimamia nini? Tumeona Kenya jinsi siasa zimegubikwa na wakubwa kuhama hama kila mara. Mwishoni mnajikuta vyama vyote viko contaminated maana viongozi wanakuwepo si kwa sababu ya principle bali kuendeleza 'ulaji'. Thanks Shibuda - learned the hard way!

    2. RukaaJuu Final

    3. #2
      Bob G's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 5th October 2011
      Location : UK Manyasi
      Posts : 1,659
      Rep Power : 717
      Likes Received
      291
      Likes Given
      36

      Default Re: CHADEMA kuwakataa viongozi wa CCM

      Ni uamzi mzuri ingawa si mzuri sana, Issue nikuwa makini na watu wote wanaomba uongozi coz wengi wa viongozi na wanachama wanatokea vyama vingine, muhimu wanapojiunga nilazima ziwepo kanuni na taratibu za mtu kujiunga na CDM ambazo hazitakua zinabagua watu wengine kuruhusiwa na wengine kukataliwa kuomba kugombea.

      Mwaka 2010 CDM haikusimamisha wagombea majimbo yote, tatizo kulikua hakuna watu wa kugombea na inaweza tokea tena 2015 ni vipi watu wakaomba wakakataliwa wakati majimbo hayana wagombea?

      Nashauri namna nzuri itafutwe kukabiliana na wahamiaji toka vyama vingine coz wapo watu makini pia ktk vyama vingine waruhusiwe
      FJM likes this.

    4. FJM
      #3
      FJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 7,179
      Rep Power : 2569
      Likes Received
      5331
      Likes Given
      4587

      Default Re: CHADEMA kuwakataa viongozi wa CCM

      Quote By Bob G
      Ni uamzi mzuri ingawa si mzuri sana, Issue nikuwa makini na watu wote wanaomba uongozi coz wengi wa viongozi na wanachama wanatokea vyama vingine, muhimu wanapojiunga nilazima ziwepo kanuni na taratibu za mtu kujiunga na CDM ambazo hazitakua zinabagua watu wengine kuruhusiwa na wengine kukataliwa kuomba kugombea. mwaka 2010 CDM haikusimamisha wagombea majimbo yote, tatizo kulikua hakuna watu wa kugombea na inaweza tokea tena 2015 ni vipi watu wakaomba wakakataliwa wakati majimbo hayana wagombea? Nashauri namna nzuri itafutwe kukabiliana na wahamiaji toka vyama vingine coz wapo watu makini pia ktk vyama vingine waruhusiwe
      Bob, kupokea 'reject' ni hatari sana. Viongozi wanaoomba kujiunga kwa sababu wameshindwa upande mwingine ni wazi kabisa wajiunga ili kupata uongozi na hatari ni kuwa na mtu kama Shibuda. Bado Shibuda ni CCM damu damu na kama sio busara ya CHADEMA wangejikuta wanatumia muda mwingi kumjadili kwenye vikao badala ya kufanya mambo mengine.

      Watu wapime na waamue sasa you are either with party X or party Y. Lakini mchezo wa kamari uishe!

      Kuhusu kusimamisha wagombea 2015. Nadhani this time around CCM wanaweza kujikuta wanakosa mtu wa kumsimamisha kwenye baadhi ya majimbo. Chama hakiuziki kabisa na tayari mwaka huu wamekosa watu wa kugombea nafasi za ubalozi. Wamepuuza kero za wananchi mno hivyo inakuwa shida hata kwa mgombea kusema analeta mambo mapya.

    5. #4
      Tume ya Katiba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2012
      Location : Chumbuni-Zanzibar
      Posts : 2,690
      Rep Power : 0
      Likes Received
      542
      Likes Given
      273

      Default Re: CHADEMA kuwakataa viongozi wa CCM

      Quote By FJM
      CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimetangaza rasmi kusitisha kuwapokea viongozi wa ngazi zote watakaohama kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) na vyama vingine, baada ya kutemwa katika kura za maoni kwa lengo la kutaka kuwania nafasi za uongozi ndani ya chama hicho.

      Mbowe kavunja katiba ya CHAMA.

    6. #5
      Asterisk's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 1st June 2012
      Posts : 215
      Rep Power : 395
      Likes Received
      49
      Likes Given
      107

      Default Re: CHADEMA kuwakataa viongozi wa CCM

      mi kwa maoni yangu ni kwamba wawapokee lakin wawe members tuu. mpaka watakapowaona wamekomaa ndo wawape fursa ya kugombea.
      tukisema tuwakatae tu si nzuri coz kuna wengine wamesha kombolewa ki fikra na wapo tayari kikomboa nchi yao. je hao wakimbilie wapi??

    7. Miaka 50

    8. #6
      Mkulima wa Kuku's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th January 2011
      Posts : 711
      Rep Power : 566
      Likes Received
      242
      Likes Given
      208

      Default Re: CHADEMA kuwakataa viongozi wa CCM

      Nadhani tukisoma vizuri utakuta Mbowe anazungumzia wanaokuja ili kugombea uongozi; na imefafanuliwa wote wanakaribishwa ila si kuja tu kutaka uongozi. Nawapa big up kwa hilo! Hii itasaidia sana kupata wajenga chamabadala ya wajengea tumbo

    9. #7
      Duble Chris's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th May 2011
      Posts : 2,340
      Rep Power : 872
      Likes Received
      382
      Likes Given
      309

      Default Re: CHADEMA kuwakataa viongozi wa CCM

      Quote By Mkulima wa Kuku
      Nadhani tukisoma vizuri utakuta Mbowe anazungumzia wanaokuja ili kugombea uongozi; na imefafanuliwa wote wanakaribishwa ila si kuja tu kutaka uongozi. Nawapa big up kwa hilo! Hii itasaidia sana kupata wajenga chamabadala ya wajengea tumbo
      kama ni hili hapo sawa
      frustration is given by expectationdivide by
      outcome
      ie
      frustration = expectation/outcome


    10. #8
      mamajack's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st May 2012
      Posts : 1,153
      Rep Power : 583
      Likes Received
      275
      Likes Given
      71

      Default Re: CHADEMA kuwakataa viongozi wa CCM

      alway chadema ni chama makini and viogonzi wake wanamaamuzi ya busara.

      long live mwenyekiti makini.!!!!

    11. #9
      Comi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd October 2011
      Posts : 963
      Rep Power : 578
      Likes Received
      156
      Likes Given
      2

      Default Re: CHADEMA kuwakataa viongozi wa CCM

      Lengo la mbowe si kwamba hawawapokea,la hasha watapokelewa isipokuwa hawatapewa kipaumbele katika nafasi za kugombea uongozi katika nafasi za juu kama ubunge,katibu wa mkoa/wilaya n.k

      wao watakuwa ni wanachama wa kawaida maana kama umekaa magamba miaka 20 na hakuna cha maana ulichokifanya katika jimbo lako wala huna uzalendo kwa wananchi utakuwa huna faida. Kauli ya mbowe inawahusu wale wapenda matumbo yao na wabinafsi kama shibuda

    12. #10
      Kurunzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2009
      Location : DAR ES SALAAM
      Posts : 1,956
      Rep Power : 891
      Likes Received
      386
      Likes Given
      147

      Default Chadema yapiga stop viongozi wa ccm kujiunga chadema.

      CHAMA Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimetangaza rasmi kusitisha kuwapokea viongozi wa ngazi zote watakaohama kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) na vyama vingine, baada ya kutemwa katika kura za maoni kwa lengo la kutaka kuwania nafasi za uongozi ndani ya chama hicho.

      Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alitoa msimamo huo jana alipokutana na wanafunzi wa vyuo vikuu vitatu vya UDOM, CBE na St John, katika hafla ya kuwaaga wenzao wanaomaliza masomo yao.

      Mbowe alisema kuwa, CHADEMA kinataka sasa kupata viongozi na wanachama wanaosukumwa na uzalendo wa kweli, na wanaoamini itikadi na sera zake, na si wanaotaka kukitumia kama ngazi ya kufanikisha malengo yao.

      Alisema wamejifunza kwa kiasi kikubwa hasara ya kuwapokea wanachama, na hasa waliokuwa viongozi wa vyama vingine dakika za mwisho, hususan wakati wa uchaguzi, hivyo kuanzia sasa hawapo tayari kufanya hivyo.

      Mbowe alisema wapo tayari na wanawakaribisha wanachama ama viongozi wa CCM ambao wanaona kuwa CHADEMA ni chama makini, kikomavu na wanaoamini kina malengo halisi ya kuikomboa nchi na kuwaletea maendeleo wananchi wote bila kujali itikadi ya
      vyama, dini, kabila ama eneo la nchi.

      “Wale wapambanaji waliochoshwa na matendo ya wenzao ndani ya CCM, na wanaoamini kwa dhati kabisa na kusukumwa na dhamiri ya kweli ya kupigania maslahi ya wanyonge, waje sasa.

      “Hakuna haja ya wao kusubiri hadi dakika za mwisho, na hasa pale wanapopigwa chini katika kura za maoni ndio waje. Wajue kuwa
      wakisubiri muda huo, hawataweza kupokelewa hata kama watakuwa ni wazuri namna gani,” alisema Mbowe.
      Andre02150 likes this.

    13. #11
      Safety last's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th March 2011
      Posts : 2,680
      Rep Power : 950
      Likes Received
      519
      Likes Given
      6

      Default Re: Chadema yapiga stop viongozi wa ccm kujiunga chadema.

      Tayari tuna wanachama miliöni 7 sasa wanaweza kwenda CUF/NCCR chadema kumejaa!

    14. #12
      Nabihu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 20th March 2012
      Posts : 166
      Rep Power : 395
      Likes Received
      17
      Likes Given
      0

      Default

      Sizitaki mbichi hizi
      Mbelwa Germano likes this.

    15. #13
      TIMING's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 20,087
      Rep Power : 12252
      Likes Received
      6015
      Likes Given
      6852

      Default Re: Chadema yapiga stop viongozi wa ccm kujiunga chadema.

      i think it is a good strategy... kama wanataka mabadiliko ya kweli wajiunge sasa, na sio kusubiri kura za maoni za ccm.... maana watakua wanataka uongozi na si mapinduzi ya kweli ya mtanzania wa kawaida
      Andre02150 and Mbelwa Germano like this.
      .....Ana sifa zote, nzuri na mbaya!!!

    16. #14
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Chadema yapiga stop viongozi wa ccm kujiunga chadema.

      1) Anamla vijembe Slaa.

      2) Anarukia hoja ya uzalendo.

      Kuna kila sababu ya kuona kuwa, ingawa Slaa ana hamu sana ya kugombea tena, hatopewa fursa hiyo na Mwenyekiti Mbowe.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    17. #15
      Mtoto Wa Mbale's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th May 2011
      Posts : 420
      Rep Power : 494
      Likes Received
      143
      Likes Given
      1

      Default

      Quote By Asterisk
      mi kwa maoni yangu ni kwamba wawapokee lakin wawe members tuu. mpaka watakapowaona wamekomaa ndo wawape fursa ya kugombea.
      tukisema tuwakatae tu si nzuri coz kuna wengine wamesha kombolewa ki fikra na wapo tayari kikomboa nchi yao. je hao wakimbilie wapi??
      Hawatapokelewa kama wameshindwa kura za maoni ccm halafu wakaona wakihamia CDM watashinda. Kama wanadhani ccm hakiwafai, wasingoje wakati wa uchaguzi bali wajiunge sasa.

      Huo ni uamuzi wa busara sana. Naamini CDM imejipanga kusimamisha wagombea katika kila jimbo. Wako wasomi wengi na wapenda mabadiliko wanaoamini katika nguvu ya umma.

    18. #16
      Mungi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 23rd September 2010
      Location : Hapa!!!
      Posts : 10,186
      Rep Power : 24275
      Likes Received
      4680
      Likes Given
      2300

      Default Re: CHADEMA kuwakataa viongozi wa CCM

      Quote By Tume ya katiba
      Mbowe kavunja katiba ya CHAMA.
      na we unataka kujiunga CHADEMA baada ya kupigwa chini ADC? Chama cha kikundi cha Uamsho hicho!
      "Peace is not simply about the absence of violence. It is defined by the presence of fundamental liberties and the prevalence of economic opportunities."

    19. #17
      Technician's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th March 2010
      Posts : 796
      Rep Power : 624
      Likes Received
      191
      Likes Given
      163

      Default Re: Chadema yapiga stop viongozi wa ccm kujiunga chadema.

      Si kweli ,lazima itakuwa zaidi ya hicho kiwango chama kinaweza kujiendesha chenyewe bila kutegemea ruzuku maana yake kina wanachama wengi wanaoweza kutoa fedha za ada tuu zaidi ya 7bilion kwa mwezi basi kina wanachama zaidi ya 10milioni 500x7,000,000=3,500,000,000/= wametoka

      Quote By Safety last
      Tayari tuna wanachama miliöni 7 sasa wanaweza kwenda CUF/NCCR chadema kumejaa!
      The best lovers are those with well developed sensitivity and a wide imagination.

    20. #18
      paty's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th October 2010
      Location : never never land
      Posts : 1,025
      Rep Power : 975
      Likes Received
      270
      Likes Given
      62

      Default Re: Chadema yapiga stop viongozi wa ccm kujiunga chadema.

      idea nzuri, hii kitu ya kuwaza kwamba wakija CDM watapea nafasi ife kabisa, waende CHAUSTA,
      CHADEMA mwendo mdundo - T 2015 CDM

    21. #19
      Mbelwa Germano's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th May 2011
      Posts : 701
      Rep Power : 838
      Likes Received
      200
      Likes Given
      262

      Default Re: Chadema yapiga stop viongozi wa ccm kujiunga chadema.

      Quote By zomba
      1) Anamla vijembe Slaa.

      2) Anarukia hoja ya uzalendo.

      Kuna kila sababu ya kuona kuwa, ingawa Slaa ana hamu sana ya kugombea tena, hatopewa fursa hiyo na Mwenyekiti Mbowe.
      Sytem at work
      80 percent of problems are often due to 20 percent of the causes

    22. #20
      EMMANUEL NSAMBI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th October 2011
      Posts : 357
      Rep Power : 454
      Likes Received
      78
      Likes Given
      17

      Default Re: Chadema yapiga stop viongozi wa ccm kujiunga chadema.

      Quote By zomba
      1) Anamla vijembe Slaa.

      2) Anarukia hoja ya uzalendo.

      Kuna kila sababu ya kuona kuwa, ingawa Slaa ana hamu sana ya kugombea tena, hatopewa fursa hiyo na Mwenyekiti Mbowe.
      Hivi wewe uliwahi kusikia lini Slaa na Mbowe wakatofautiana?Mfumo wa cdm uko makini sna,wanajadili kwa pamoja na kutoa uamuzi kwa pamoja.Wanachokiamua wanakisimamia kwa pamoja tofauti na nyinyiem kila kundi lina mamlaka
      na uwezo wa kukisemea chama.

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...