Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Serikali ya China kuijenga upya TAZARA kuanzia mwaka huu wa fedha 2012/2013

    Report Post
    Results 1 to 17 of 17
    1. #1
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,204
      Rep Power : 3555
      Likes Received
      3055
      Likes Given
      462

      Default Serikali ya China kuijenga upya TAZARA kuanzia mwaka huu wa fedha 2012/2013




      Na Joseph Ishengoma

      Wuhan, China

      Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China imekubali kuanza utekelezaji
      wa miradi miwili mikubwa nchini (Tazania) katika mwaka wa fedha
      2012/2013 ukiwemo ujenzi wa reli ya TAZARA kati ya Kapilimposhi Zambia
      na Dar es saalam.

      Mradi mwingine ni wa Makaa ya Mawe Ludewa na Chuma Liganga ambayo kwa pamoja itagharimu zaidi ya dola za Kimarekani bilioni 4.

      Akizungumza katika maHafari ya wanafunzi wa Tanzania wanaosoma

      katika vyuo vikuu mjini Wuhan, China, Balozi wa Tanzania katika Jamhuri
      ya Watu wa China Phillipo Marmo amesema, ujenzi wa miradi hiyo utaongeza
      ufanisi katika usafiri na usafirishaji pamoja na kukuza ajira kwa
      watanzania.


      "Mwaka huu wa fedha, zaidi ya waandisi 400 kutoka China watakwenda Tanzania kuifumua na kuijenga upya reli ya TAZARA," amesema.


      "Ujenzi huo utaboresha uimara wa reli na kupunguza muda wa kusafiri
      kwa kutumia reli hiyo katika maeneo inapotoa huduma tofauti na ilivyo
      sasa."


      Reli ya TAZARA iliyojengwa kwa msaada wa serikali ya Watu wa China
      kati ya mwaka 195 hadi 1975 imekuwa ikilalamikiwa sana na watumiaji
      wake kutokana na ubovu wa miundombinu yake, yakiwemo mabehewa, mataaluma
      na hata uongozi.


      Kuhsu miradi ya Makaa ya mawe na chuma, Balozi Mmo ameeleza kuwa
      miradi hiyo inayotarajiwa kukamilika ndani ya kipindi cha miaka miwili
      ujenzi wake takapoanza, itasidia kukuza uchumi wa Taifa na kuongeza
      ajira kwa Watanzania.


      "Nchi yenye chuma inakuwa na mwelekeo mzuri wa kuwa na viwanda vitakavyotoa ajira kwa wananchi wake," amesema.
      Kuhusu utalii, Balozi huyo amewataka wanafunzi Watanzania walioko China kuitangaza vema nchi yao ili kuongeza pato la taifa kutokana na China kuwa na idadi kubwa ya watalii kila mwaka.

      "China inatoa watalii milioni 100 kila mwaka, kati ya hao ni 10,000
      tu wanaoenda Tanzania. Lengo la serikali ni kuendelea kutangaza vivutio
      vya utalii tulivyonavyo ili angalau asilimia moja ya watalii wa hapa
      waende kwetu," amesema na kuongeza kuwa, "tukifanya hivyo tutaongeza
      ajira na kukuza uchumi kupitia nyanja ya utalii". Kati ya watalii
      milioni 100 kutoka china, watalii zaidi ya 300,000 wanatembelea Angola.


      Maelezo hayo ya Mhe Marmo yametokana na hotuba ya Mwenyekiti wa WUTASA Bi Fatma Waziri kwa mgeni rasmi kuwa uwepo wa wanafunzi wa Tanzania mjini Wuhan ni zaidi ya uanafunzi kwani wamekuwa wakiitangaza vivutio mbalimbali vya utalii kupitia maonesho ya utamaduni.


      Awali wahitimu katika riasala yao iliyosomwa na DR. Ally Ahmed Saburi wameiomba serikali kushughulikia kwa haraka maombi ya mikopo ya wanafunzi walioko nje ya nchi kwani wanafunzi wa Kitanzanai wanaotegemea mikopo kutoka bodi ya mikopo na
      serikali ya mapinduzi Zanzibar wanapata wakati ngumu na kuishi kwa shida
      kutokanana ucheleweshwaji wa fedha.


      "Wanafunzi wanaotegemea mikopo ya serikali wanakuwa na maisha magumu kutokana na ucheleweshwaji wa mikopo au wakati mwingine kuikosa kabisa. Tunaomba serikali iliangalie jambo hili kwa ukaribu ili kuepusha aibu wanayopata wanafunzi wanaotegemea mikopo nje ya nchi," alisema Dr. Ally.

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,204
      Rep Power : 3555
      Likes Received
      3055
      Likes Given
      462

      Default re: Serikali ya China kuijenga upya TAZARA kuanzia mwaka huu wa fedha 2012/2013

      Phillip Marmo hajui hao watalii 300,000 wanaotembelea Angola wanavyo ichuja Mali Asili ya Angola, Sababu Mahoteli, Restaurant's, hadi Safaris zinamilikiwa na Wachina wanalipia kwa YUAN wakiwa CHINA wakifika Angola hawana pesa zozote wanaanza kutumia wameshalipia safari tangu CHINA, yaani hadi Malaya wa Mitaani ni Wachina, Angola kuna Wachina Wengi zaidi ya England, Wamechukua biashara kibao za locals... Bongo tujiandae

      Wanakuja tena kutengeneza Tazara, wataleta wataalau wao hawachukui wabongo ni wao na wanakula chochote kinachokimbia vichakani kwahiyo tutapoteza vidudu vyetu vyote huko Maporini wanapopitisha hiyo reli.

      Sijui kama kweli wataajiri wabongo kwenye viwanda vya CHUMA na COAL angalia Zambia; tutamlaumu Mzindakaya ndie yeye aliyewachagua hao wachina before Waswedish, Wanorway, Wajerumani
      RedDevil and Consigliere like this.

    4. #3
      Sungurampole's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 17th November 2007
      Posts : 704
      Rep Power : 728
      Likes Received
      121
      Likes Given
      555

      Default re: Serikali ya China kuijenga upya TAZARA kuanzia mwaka huu wa fedha 2012/2013

      Sijui kama ni habari njema!

      Nilipita mwaka 2009 Dar - Kapiri nikasikitika kuona ilivyochakaa kwa kutofanyiwa ukarabati -

      Swali - tutafanya nini hili lisijirudie?
      There is a higher court than courts of justice and that is court of conscience.

      It supersedes all other courts.
      Mohandas Gandhi

    5. #4
      Njowepo's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 26th February 2008
      Location : Santiago
      Posts : 7,601
      Rep Power : 22056
      Likes Received
      995
      Likes Given
      777

      Default re: Serikali ya China kuijenga upya TAZARA kuanzia mwaka huu wa fedha 2012/2013

      Hawa wakija 400 after 10 years mbona watakuwa laki nne!
      Enzi wanajenga TAZARA Jk alimudu kuwacontrol as hawakuja na wake zao na wengi walikuwa wafungwa na alihakikisha wanarudi kwao wote
      Sasa izi zama za akina Mrisho ndo basi tena.
      WB Tanzania lead economist Jacques Morisset said the GDP doubled in 10 years, but it has failed to produce any significant decline in poverty levels.

    6. #5
      RedDevil's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th April 2009
      Location : Hapa Hapa
      Posts : 1,455
      Rep Power : 803
      Likes Received
      269
      Likes Given
      512

      Default re: Serikali ya China kuijenga upya TAZARA kuanzia mwaka huu wa fedha 2012/2013

      Quote By Sungurampole
      Sijui kama ni habari njema!

      Nilipita mwaka 2009 Dar - Kapiri nikasikitika kuona ilivyochakaa kwa kutofanyiwa ukarabati -

      Swali - tutafanya nini hili lisijirudie?
      Huu ni ujuha mkuu, inamaana hili shirika lilikuwa likijiendesha kwa hasara? Kwa nini tusubiri hadi Wachina watujengee hii reli kwa manufaa yetu, hapa ndiyo viongozi wetu napowaona wasaliti wa kwanza. Na wanahitaji kufanyiwa uchunguzi wa kina kama kweli wapo madarakani kwa interests za nchi au ni mapapeti.
      "Never argue with stupid people, they will drag you down to their level and then beat you with experience" Mark Twain

    7. Miaka 50

    8. #6
      Wingu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th January 2011
      Posts : 3,973
      Rep Power : 1217
      Likes Received
      247
      Likes Given
      41

      Default

      Reli ya kati ndo muhimu kuliko hata hiyo wanayotaka kutusaidia ila tunashukuru kwa msaada wao

    9. #7
      Uswe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Posts : 1,782
      Rep Power : 794
      Likes Received
      439
      Likes Given
      437

      Default Re: Serikali ya China kuijenga upya TAZARA kuanzia mwaka huu wa fedha 2012/2013

      sidhani kama ni habari ya kushangilia hii, Tanzania ni kama shamba la bibi, wachina waje watengeneze, (naomba kuazima lugha ya mheshimiwa mwakyembe) wapuuzi wanakuja kukwapua
      mbona sioni umeme, maji wala barabara, 30% PAYE na Kodi nyingine katika bidhaa, zinaenda wapi?

    10. #8
      Sungurampole's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 17th November 2007
      Posts : 704
      Rep Power : 728
      Likes Received
      121
      Likes Given
      555

      Default Re: Serikali ya China kuijenga upya TAZARA kuanzia mwaka huu wa fedha 2012/2013

      Quote By Mzinga
      Reli ya kati ndo muhimu kuliko hata hiyo wanayotaka kutusaidia ila tunashukuru kwa msaada wao
      Wamechagua TAZARA kwani wao ndiyo waliijenga sisi na ndugu zetu wa Zambia tukaifuja beyond repair! Wanasema hatuna vocabulary - maintenance katika lugha yetu ..sijui
      There is a higher court than courts of justice and that is court of conscience.

      It supersedes all other courts.
      Mohandas Gandhi

    11. KVM
      #9
      KVM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2011
      Posts : 471
      Rep Power : 513
      Likes Received
      175
      Likes Given
      70

      Default Re: Serikali ya China kuijenga upya TAZARA kuanzia mwaka huu wa fedha 2012/2013

      Quote By Sungurampole
      Sijui kama ni habari njema!

      Nilipita mwaka 2009 Dar - Kapiri nikasikitika kuona ilivyochakaa kwa kutofanyiwa ukarabati -

      Swali - tutafanya nini hili lisijirudie?
      Sijui ni wangapi mnajua uozo uliopo Tanzania, karibu kwenye mashirika yote yanayomilikiwa na serikali. wafanyakazi wa mashirika hayo wameyafanya ni miradi yao binafsi. Kwa mfano kuna miaka ya 80 nilisafiri na TAZARA kutoka Makambako kwenda DSM. Mabehewa yalijaa mizigo-magunia ya vyakula ya wafanyakazi ambao hawayalipii chochote. Vyumbani nako walikuwepo wasafiri wengi ambao walikuwa wanatumia ticket maalum amabzo hutolewa kwa wafanyakazi. Maana yake treni ilikuwa inasafiri kwa hasara! Hii imeendelea mpaka leo hii!

      Kama kweli Watanzania wana uchungu na nchi yao inabidi wafunguke na siyo kushabikia tu kuwa tunataka mashirika ya serikali. Sote tumesikia alichoona Mwakyembe kwenye safari yake ya Train ya Dodoma.

      Mimi ningependekeza kuwa serikali isimamie tu njia ya reli lakini iruhusu watu binafsi wenye uweze wa kununua vichwa vya train na mabehewa na ujuzi wa kusafirisha mizigo watumie hizo njia. Mbona ndivyo tunavyofanya kwenye barabara?

    12. #10
      Narubongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2010
      Posts : 1,886
      Rep Power : 810
      Likes Received
      842
      Likes Given
      680

      Default Re: Serikali ya China kuijenga upya TAZARA kuanzia mwaka huu wa fedha 2012/2013

      unajiita mwanaume halafu unakwenda kwa mwanaume mwenzako kumuomba msaada akutunzie watoto na mke eh eh eh.. hii kitu mimi siwezi kabisa maana anayekusaidia akienda kumtongoza mkeo ni lazima akubali tu., halafu ipo siku unaweza kuombwa makalio kabisa
      "Chadema kinatumia alama ya vidole viwili kama manati, manati kamwe haiwezi kuua tembo" Livingstone Lusinde (2012)

    13. #11
      Pakawa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th March 2009
      Posts : 1,150
      Rep Power : 750
      Likes Received
      166
      Likes Given
      170

      Default Re: Serikali ya China kuijenga upya TAZARA kuanzia mwaka huu wa fedha 2012/2013

      Wacha waje wajenge kwani usafiri huu utawasaidia wengi na ajali za barabarani zitapungua maana mabasi yamekuwa chinja chinja...Sisi tumeshindwa wacha wageni watuwezeshe si ndio tunavyotaka
      Hata itakuwa kwa kila mtu atakayeliita jina la bwana atampokea roho wa mungu' 'Niiteni nami nitaitika anasema bwana wa majeshi.'

    14. #12
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,204
      Rep Power : 3555
      Likes Received
      3055
      Likes Given
      462

      Default Re: Serikali ya China kuijenga upya TAZARA kuanzia mwaka huu wa fedha 2012/2013

      Quote By Sungurampole
      Wamechagua TAZARA kwani wao ndiyo waliijenga sisi na ndugu zetu wa Zambia tukaifuja beyond repair! Wanasema hatuna vocabulary - maintenance katika lugha yetu ..sijui
      Katika Mkataba Zambia ina asilimia kubwa zaidi ya Tanzania na ukiangalia Kuanzia Mkurugenzi Mkuu na wakurugenzi wengi wa Maana ni lazima wawe Wazambia, Wazambia wametoa Dola Milioni 10 kwa matengenezo hii ni baada ya Sata kuchukua Madaraka.

    15. Nzi
      #13
      Nzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2010
      Location : 740 Park Avenue
      Posts : 3,313
      Rep Power : 21622
      Likes Received
      924
      Likes Given
      822

      Default Re: Serikali ya China kuijenga upya TAZARA kuanzia mwaka huu wa fedha 2012/2013

      Quote By Mzinga
      Reli ya kati ndo muhimu kuliko hata hiyo wanayotaka kutusaidia ila tunashukuru kwa msaada wao
      Mzinga, kama wanakuja kuchimba na makaa ya mawe, basi reli ya TAZARA itakuwa ni ya muhimu kwao kuliko ilivyo reli ya kati kwao na kwetu.
      "You can't make a scene if you don't have little green"-------Jim Carrey

    16. #14
      Ndahani's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd June 2008
      Location : Somewhere
      Posts : 9,646
      Rep Power : 4016
      Likes Received
      2940
      Likes Given
      5063

      Default Re: Serikali ya China kuijenga upya TAZARA kuanzia mwaka huu wa fedha 2012/2013

      Kuna vitu vinatia sana aibu...Tazara is one of those. Inasuasua kwasababu ni kama haina mwenyewe. Watu wanakula wasipofanyia kazi.
      Kwa upande wa china hawafanyi haya bure bure. Wamewekeza sana kwenye mining Zambia. Copper inakuwa rahisi kama itasafirishwa kwa kutumia reli hiyo. Tukumbuke pia chuma na copper ni hot cake kule kwao
      We are all inventors, each sailing out on a voyage of discovery, guided each by a private chart, of which there is no duplicate. The world is all gates, all opportunities.
      Ralph Waldo Emerson

    17. #15
      Black Bat's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th October 2007
      Location : Abbottabad
      Posts : 2,479
      Rep Power : 9580
      Likes Received
      682
      Likes Given
      575

      Default Re: Serikali ya China kuijenga upya TAZARA kuanzia mwaka huu wa fedha 2012/2013

      hahaaa watanzania kweli hii reli imejengwa na wachina ili wasafirishe chuma kutoka zambia kuja bandari ya dsm them wapeleke kwenye viwanda vyao huko china.. Ina maana hamjui????? Mnafurahia hapa bure tu .. mnafikiri kuwa mnajengewe bure bure tu.. Thubutuuu..
      No free lunch in our era

    18. #16
      Somoche's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th October 2010
      Posts : 1,861
      Rep Power : 813
      Likes Received
      345
      Likes Given
      338

      Default Re: Serikali ya China kuijenga upya TAZARA kuanzia mwaka huu wa fedha 2012/2013

      Serikali hii inaomba omba tuuu miaka yooote hata kurekebisha reli haiwezi....dead Nation!!!

    19. #17
      Mngendalyasota's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 22nd January 2011
      Posts : 138
      Rep Power : 449
      Likes Received
      40
      Likes Given
      0

      Default Re: Serikali ya China kuijenga upya TAZARA kuanzia mwaka huu wa fedha 2012/2013

      Kumbe kuna wazanzibar wanaotegemea mikopo kutoka serikali ya muungano? Samahani kwa kuwa nje ya topic.

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...