Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Uhuru: Bajeti yakuna wengi!

    Report Post
    Results 1 to 20 of 20
    1. #1
      Landala's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th December 2010
      Posts : 562
      Rep Power : 539
      Likes Received
      122
      Likes Given
      25

      Default Uhuru: Bajeti yakuna wengi!

      Habari za leo wanajf,muda si mrefu nilikuwa napitia vichwa vya habari vya magazeti mbali mbali nikakuta kwenye gazeti la Uhuru likisema 'BAJETI YAKUNA WENGI'hivi watanzania wenzangu ni kweli hii bajeti ya 2012-2013 imekuna wengi au hili gazeti la CCM la uhuru linataka kupotosha umma ili kuitetea serikali yao ya magamba..

    2. Miaka 50

    3. #2
      Bornvilla's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 17th February 2011
      Posts : 634
      Rep Power : 0
      Likes Received
      141
      Likes Given
      0

      Default re: Uhuru: Bajeti yakuna wengi!

      Imeakuna wenyewe tu! Hakuna lolote! paye inazidi kupanda, we unategemea nini?

    4. #3
      BJEVI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2011
      Posts : 755
      Rep Power : 574
      Likes Received
      165
      Likes Given
      140

      Default Re: Uhuru: Bajeti yakuna wengi!

      HILI NI GAZETI MFU ,HATA HAYA INGAWA NI YA KWELI WAKIAANDIKA WATASEMA KINYUME.

      SOMA HAPA.


      Tangu kuingia kwa mchezo mchafu wa kikundi cha watu tena wachache kujihudumia na kutafuta utajiri kwa kuwauza wenzao, Tanzania si salama ingawa hakuna milio ya bunduki.

      Uliza. Yako wapi mapambano dhidi ya ujambazi, ufisadi (ugamba), biashara ya mihadarati, kurekebisha mikataba ya kijambazi ya uwekezaji ambao ni uchukuaji na uwajibikaji? Si siri.

      Kwa sasa Tanzania iko mikononi mwa maharamia tuseme majambazi hasa kiuchumi. Imefikia mahali majambazi yaitwayo wawekezaji yanakuja na kutuibia mchana kweupe kwa kushirikiana na wenzetu waroho wachache tuliwaamini.

      Uliza uwekezaji kwenye Shirika la Reli uliishia wapi ilipoingia kampuni ya Kihindi iitwayo RITES?

      Mijitu inakuja bila hata senti halafu eti inawekeza kwa kuilazimisha serikali iwape mikopo ili waendeleze mradi! Ni wawekezaji wangapi wanakuja na briefcases zao na makaratasi na kurejea kwao wakiwa na magunia ya dola?

      Uliza. Ni wawekezaji wangapi hasa kwenye madini wanamiliki ndege na viwanja binafsi vya ndege wanavyotumia kutoroshea madini yetu bila kukaguliwa?

      Ni wangapi wanachafua mazingira na hakuna anayewawajibisha?

      Hebu zidi kupiga mbizi kwenye uchafu huu uone mengi. Hakuna ujambazi wa wazi kama unaofanywa na makampuni ya simu kwa sasa.

      Wanakuja na kuweka mitambo chakavu halafu wanawatoza Watanzania viwango vya juu vya kutumia simu.

      Huwa najiuliza. Inakuwaje kupiga simu, kwa mfano, kutoka Canada kwenda Kenya nitozwe senti tano za dola na Tanzania nitozwe senti 27 za dola kwa dakika?

      Wakati viwango vya Kenya ni vidogo, mawasiliano baina ya Kenya, Uganda, Rwanda hata Burundi ni bora na rahisi wakati Tanzania ni utapeli mtupu.

      Mtu unapiga simu unaambiwa ongeza salio, mara namba ya simu haipo, mara simu inatumika mara hili mara lile.

      Kwanini hatusikii upuuzi huu tunapopiga nchi tulizotaja hapo juu kama hakuna namna?

      Ajabu ya maajabu, kila mwaka makampuni ya simu yanabadilisha majina ili kuendelea kufaidi msamaha wa kipuuzi wa kodi.

      Angalia mahoteli yenu yanavyobadili majina na wamilki kila baada ya miaka mitano ili kuendelea kufanya biashara bila kulipa kodi. Angalia watu wanavyouziana makampuni waliyookota Tanzania kwa bei ya kutupwa.

      Anayebishia hili ajikumbushe Richmond ‘ilijiuza’ kwa Dowans kwa bei gani ikilinganishwa na bei ya maandishi tu bila kulipa pesa iliyoianzishia biashara hii hewa.

      Leo tunaambiwa kuwa pesa tunayoilipa IPTL, kwa mfano inatosha kununua na kujenga mitambo bora na mikubwa kuliko tunayolipia.


      Je, kwanini tunaona kujikomboa ni dhambi wakati tukiabudia maangamizi kama haya ya IPTL na makampuni mengine mengi ya nishati.

      Je, hapa hakuna rushwa na ufisadi vya wazi? Je, wahusika hawajulikani? Nani anawagusa wala kuwashughulikia? Tunakwenda wapi?

      Imefikia mahali watu wakiuliza ni kwanini uchafu huu unaendelea wakati kuna mamlaka, wanakufa kwenye mazingira ya kutatanisha. Jiulize. Mbunge wetu mmoja alipatwa na nini baada ya kuhoji ni kwanini alikuwa akiona watumiaji wa mihadarati hadharani ambao wangeweza kutuonyesha wanakonunua madawa.

      Tufikie mahali tuambiane ukweli bila kuogopana wala kufichana. Bila kufanya hivyo na kubadilika nchi yetu itaishia pabaya.

      Ni juzi juzi serikali ya Mali imeangushwa kutokana na hasira za jeshi kushuhudia wauza unga wakiwa ndani ya serikali na serikali isifanye kitu kwa vile wakubwa zake walikuwa wakinufaika na uchafu huu.

      Je, sisi tu salama na hawa wauza unga na majambazi wa kiuchumi waliotapakaa nchini mwetu? Je, wananchi wataendelea kugeuzwa mbuzi wa shughuli kila mwaka?

      Huwa siachi kusema kuwa Watanzania ni viumbe wa ajabu hata kama hawana mikia au macho kisogoni.

      Maana ukiangalia kwa mfano, rasilimali zao zinavyoibiwa, wanavyolanguliwa huduma kama vile umeme, simu na mahitaji mengine na wakaendelea kuvumilia unashangaa hawa ni watu wa namna gani.

      Nani kwa mfano anakumbuka na kuhoji ile kashfa ya utoroshaji wanyama iliyotokea Novemba 24, 2010 ambapo ndege ya kijeshi ya Qatar ilifanikiwa kutorosha wanyama mbali mbali 130 kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro?

      Je, kama KIA wana uwezo wa kutorosha wanyama hai na wengi kiasi hiki wanashindwa nini kuingiza maelfu ya tani za unga?


      Ukitaka kujua nini namaanisha, watafute wafanyakazi wadogo na wa kawaida viwanja vya ndege uone walivyo matajiri wa kutupwa.

      Unadhani pesa hii wanaipata wapi kama si kuruhusu uchafu na jinai kama ile ya KIA......................

      Nenda TRA, Bandari, Uhamiaji. Mambo ni yale yale. Uchafu, uchafu mtupu. Nani anajali iwapo wanaofaidika wameweka watu wao kufanya kazi hiyo? mfano, vituo vyetu vya mipakani vimegeuzwa maduka ya wezi wachache kupitisha wamtakaye na wakitakacho bila kuulizwa na yeyote?

      Je, namna hii nchi itakuwa salama? Je, namna hii tunaweza kujisifu kuwa yaliyotokea Mali hayawezi kutokea huko tuendako ambapo wahusika wasiporekebisha hali hii wananchi katika hali yoyote wataamua ‘enough is enough’.

      Tumekuwa taifa la hovyo linalowazawadia watenda maovu!

      Uliza waliotimuliwa madarakani kwa kashfa wanalipwa pesa ya umma kwa kazi gani zaidi ya kupaswa kuwa mahakamani hata magerezani? Tumegeuka taifa la watenda maovu na waovu kirahisi hivi?

      Je, baada ya mchezo huu mchafu Tanzania itabaki nini? Tunaviandalia nini vizazi vijavyo iwapo tunafanya mambo kama mataahira kutokana na kufikiri kwa matumbo badala ya vichwa?
      muchetz, Evarm and Mzalendo80 like this.

    5. #4
      LiverpoolFC's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2011
      Posts : 6,707
      Rep Power : 11284
      Likes Received
      1483
      Likes Given
      574

      Default Re: Uhuru: Bajeti yakuna wengi!

      Hawa mafisadi tusiwahanye sana,kwn hakika siku zao zinahesabika!

    6. #5
      kapotolo's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 19th September 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 2,409
      Rep Power : 1196
      Likes Received
      1282
      Likes Given
      392

      Default Re: Uhuru: Bajeti yakuna wengi!

      Ni kweli imemkuna, Nape, Lusinde, Mukama, JK, Mwigulu and the Like, watanzania wasio magamba ni maumivu
      i pad3 likes this.
      Kiongozi shupavu hawezi kutumia mabavu kuongoza, ni kiongozi dhaifu tu ndio atatumia mabavu kuficha udhaifu wake - Jenerali Ulimwengu


    7. #6
      Nteko Vano's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th February 2012
      Location : Dar es salaam
      Posts : 428
      Rep Power : 450
      Likes Received
      90
      Likes Given
      26

      Default Re: Uhuru: Bajeti yakuna wengi!

      Quote By LiverpoolFC
      Hawa mafisadi tusiwahanye sana,kwn hakika siku zao zinahesabika!
      Funguka mkuu, zinahesabika kivipi?

    8. #7
      Daudi Mchambuzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th November 2010
      Posts : 6,207
      Rep Power : 2625
      Likes Received
      3000
      Likes Given
      13672

      Default Re: Uhuru: Bajeti yakuna wengi!

      ccm wanajitekenya wenyewe alafu wanacheka wenyewe.

    9. #8
      LiverpoolFC's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2011
      Posts : 6,707
      Rep Power : 11284
      Likes Received
      1483
      Likes Given
      574

      Default

      Quote By Nteko Vano
      Funguka mkuu, zinahesabika kivipi?


      Nteko Vano! Soma alama ya nyakati! Jamaa zako wako ICU.

    10. #9
      Ndibalema's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th April 2008
      Location : Mbagala
      Posts : 6,641
      Rep Power : 2010
      Likes Received
      1656
      Likes Given
      1635

      Default Re: Uhuru: Bajeti yakuna wengi!

      Chadema ikiingia madarakani, wamsweke jela huyu mhariri mkuu wa gazeti la Uhuru na vibaraka wa chini yake.

    11. #10
      Kibada's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 5th April 2012
      Posts : 122
      Rep Power : 384
      Likes Received
      16
      Likes Given
      38

      Default Re: Uhuru: Bajeti yakuna wengi!

      Acha iwakune magamba ili walale usingizi wa pono wakati upinzani unajipanga kuchukua nchi...

    12. #11
      Khakha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2009
      Posts : 963
      Rep Power : 694
      Likes Received
      209
      Likes Given
      81

      Default Re: Uhuru: Bajeti yakuna wengi!

      Quote By landala
      habari za leo wanajf,muda si mrefu nilikuwa napitia vichwa vya habari vya magazeti mbali mbali nikakuta kwenye gazeti la uhuru likisema 'bajeti yakuna wengi'hivi watanzania wenzangu ni kweli hii bajeti ya 2012-2013 imekuna wengi au hili gazeti la ccm la uhuru linataka kupotosha umma ili kuitetea serikali yao ya magamba..
      mkuu, imewakuna wao nyinyiemu kwenye masaburi yao.

    13. #12
      Mnwele's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 4th February 2010
      Posts : 103
      Rep Power : 493
      Likes Received
      49
      Likes Given
      8

      Default

      Bora Uhuru kuliko TBCCM maana wao leo ndo wametenda hovyo kabisa katika uchambuzi wa habari magazetini. Waliperuzi Uhuru, JambaLeo na Mtanzania. Ukweli ni kwamba magazeti makini yote leo yameandika kuhusu kupingwa kwa bajeti ndani ya CCM na kwa WTz from all walks of life.
      Wanaendelea kutumikia kafiri

    14. #13
      OSOKONI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th October 2011
      Posts : 3,650
      Rep Power : 1114
      Likes Received
      1003
      Likes Given
      762

      Default Re: Uhuru: Bajeti yakuna wengi!

      Quote By Nteko Vano
      Funguka mkuu, zinahesabika kivipi?
      zimebaki chache unaweza kuzihesabu kwa urahisi sana
      Narrow minded people discuss people,common minded people discuss events great minded people discuss ideas!!!

    15. #14
      democratic's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st November 2011
      Posts : 1,602
      Rep Power : 819
      Likes Received
      278
      Likes Given
      52

      Default Re: Uhuru: Bajeti yakuna wengi!

      imewakuna kwa sababu ina *****
      Kama damu inakusisimka unapoona haki ya mtu ikipokwa na uko tayari kuitetea kwa gharama yeyote, basi hakika wewe ni Comrade wangu-Che Guevara.


    16. #15
      GEMBESON's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 15th April 2012
      Location : Tanganyika
      Posts : 209
      Rep Power : 399
      Likes Received
      25
      Likes Given
      41

      Default Re: Uhuru: Bajeti yakuna wengi!

      Hakuna mtu aliyekunwa na Bajeti, labda mseme imewatekenya wengi....

    17. #16
      asigwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2011
      Location : TANDHANIYA
      Posts : 4,389
      Rep Power : 1265
      Likes Received
      1210
      Likes Given
      1253

      Default Re: Uhuru: Bajeti yakuna wengi!

      neno wengi lina maana ya kuanzia watu wawili na kuendelea..kama ilimkuna mwenyekiti pamoja na katibu mwenezi wake inatosha kuandika ni wengi

    18. #17
      Bongolander's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th July 2007
      Location : Tandale
      Posts : 4,035
      Rep Power : 1418
      Likes Received
      610
      Likes Given
      44

      Default Re: Uhuru: Bajeti yakuna wengi!

      Quote By BJEVI
      HILI NI GAZETI MFU ,HATA HAYA INGAWA NI YA KWELI WAKIAANDIKA WATASEMA KINYUME.

      SOMA HAPA.


      Tangu kuingia kwa mchezo mchafu wa kikundi cha watu tena wachache kujihudumia na kutafuta utajiri kwa kuwauza wenzao, Tanzania si salama ingawa hakuna milio ya bunduki.

      Uliza. Yako wapi mapambano dhidi ya ujambazi, ufisadi (ugamba), biashara ya mihadarati, kurekebisha mikataba ya kijambazi ya uwekezaji ambao ni uchukuaji na uwajibikaji? Si siri.

      Kwa sasa Tanzania iko mikononi mwa maharamia tuseme majambazi hasa kiuchumi. Imefikia mahali majambazi yaitwayo wawekezaji yanakuja na kutuibia mchana kweupe kwa kushirikiana na wenzetu waroho wachache tuliwaamini.

      Uliza uwekezaji kwenye Shirika la Reli uliishia wapi ilipoingia kampuni ya Kihindi iitwayo RITES?

      Mijitu inakuja bila hata senti halafu eti inawekeza kwa kuilazimisha serikali iwape mikopo ili waendeleze mradi! Ni wawekezaji wangapi wanakuja na briefcases zao na makaratasi na kurejea kwao wakiwa na magunia ya dola?

      Uliza. Ni wawekezaji wangapi hasa kwenye madini wanamiliki ndege na viwanja binafsi vya ndege wanavyotumia kutoroshea madini yetu bila kukaguliwa?

      Ni wangapi wanachafua mazingira na hakuna anayewawajibisha?

      Hebu zidi kupiga mbizi kwenye uchafu huu uone mengi. Hakuna ujambazi wa wazi kama unaofanywa na makampuni ya simu kwa sasa.

      Wanakuja na kuweka mitambo chakavu halafu wanawatoza Watanzania viwango vya juu vya kutumia simu.

      Huwa najiuliza. Inakuwaje kupiga simu, kwa mfano, kutoka Canada kwenda Kenya nitozwe senti tano za dola na Tanzania nitozwe senti 27 za dola kwa dakika?

      Wakati viwango vya Kenya ni vidogo, mawasiliano baina ya Kenya, Uganda, Rwanda hata Burundi ni bora na rahisi wakati Tanzania ni utapeli mtupu.

      Mtu unapiga simu unaambiwa ongeza salio, mara namba ya simu haipo, mara simu inatumika mara hili mara lile.

      Kwanini hatusikii upuuzi huu tunapopiga nchi tulizotaja hapo juu kama hakuna namna?

      Ajabu ya maajabu, kila mwaka makampuni ya simu yanabadilisha majina ili kuendelea kufaidi msamaha wa kipuuzi wa kodi.

      Angalia mahoteli yenu yanavyobadili majina na wamilki kila baada ya miaka mitano ili kuendelea kufanya biashara bila kulipa kodi. Angalia watu wanavyouziana makampuni waliyookota Tanzania kwa bei ya kutupwa.

      Anayebishia hili ajikumbushe Richmond ‘ilijiuza’ kwa Dowans kwa bei gani ikilinganishwa na bei ya maandishi tu bila kulipa pesa iliyoianzishia biashara hii hewa.

      Leo tunaambiwa kuwa pesa tunayoilipa IPTL, kwa mfano inatosha kununua na kujenga mitambo bora na mikubwa kuliko tunayolipia.


      Je, kwanini tunaona kujikomboa ni dhambi wakati tukiabudia maangamizi kama haya ya IPTL na makampuni mengine mengi ya nishati.

      Je, hapa hakuna rushwa na ufisadi vya wazi? Je, wahusika hawajulikani? Nani anawagusa wala kuwashughulikia? Tunakwenda wapi?

      Imefikia mahali watu wakiuliza ni kwanini uchafu huu unaendelea wakati kuna mamlaka, wanakufa kwenye mazingira ya kutatanisha. Jiulize. Mbunge wetu mmoja alipatwa na nini baada ya kuhoji ni kwanini alikuwa akiona watumiaji wa mihadarati hadharani ambao wangeweza kutuonyesha wanakonunua madawa.

      Tufikie mahali tuambiane ukweli bila kuogopana wala kufichana. Bila kufanya hivyo na kubadilika nchi yetu itaishia pabaya.

      Ni juzi juzi serikali ya Mali imeangushwa kutokana na hasira za jeshi kushuhudia wauza unga wakiwa ndani ya serikali na serikali isifanye kitu kwa vile wakubwa zake walikuwa wakinufaika na uchafu huu.

      Je, sisi tu salama na hawa wauza unga na majambazi wa kiuchumi waliotapakaa nchini mwetu? Je, wananchi wataendelea kugeuzwa mbuzi wa shughuli kila mwaka?

      Huwa siachi kusema kuwa Watanzania ni viumbe wa ajabu hata kama hawana mikia au macho kisogoni.

      Maana ukiangalia kwa mfano, rasilimali zao zinavyoibiwa, wanavyolanguliwa huduma kama vile umeme, simu na mahitaji mengine na wakaendelea kuvumilia unashangaa hawa ni watu wa namna gani.

      Nani kwa mfano anakumbuka na kuhoji ile kashfa ya utoroshaji wanyama iliyotokea Novemba 24, 2010 ambapo ndege ya kijeshi ya Qatar ilifanikiwa kutorosha wanyama mbali mbali 130 kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro?

      Je, kama KIA wana uwezo wa kutorosha wanyama hai na wengi kiasi hiki wanashindwa nini kuingiza maelfu ya tani za unga?


      Ukitaka kujua nini namaanisha, watafute wafanyakazi wadogo na wa kawaida viwanja vya ndege uone walivyo matajiri wa kutupwa.

      Unadhani pesa hii wanaipata wapi kama si kuruhusu uchafu na jinai kama ile ya KIA......................

      Nenda TRA, Bandari, Uhamiaji. Mambo ni yale yale. Uchafu, uchafu mtupu. Nani anajali iwapo wanaofaidika wameweka watu wao kufanya kazi hiyo? mfano, vituo vyetu vya mipakani vimegeuzwa maduka ya wezi wachache kupitisha wamtakaye na wakitakacho bila kuulizwa na yeyote?

      Je, namna hii nchi itakuwa salama? Je, namna hii tunaweza kujisifu kuwa yaliyotokea Mali hayawezi kutokea huko tuendako ambapo wahusika wasiporekebisha hali hii wananchi katika hali yoyote wataamua ‘enough is enough’.

      Tumekuwa taifa la hovyo linalowazawadia watenda maovu!

      Uliza waliotimuliwa madarakani kwa kashfa wanalipwa pesa ya umma kwa kazi gani zaidi ya kupaswa kuwa mahakamani hata magerezani? Tumegeuka taifa la watenda maovu na waovu kirahisi hivi?

      Je, baada ya mchezo huu mchafu Tanzania itabaki nini? Tunaviandalia nini vizazi vijavyo iwapo tunafanya mambo kama mataahira kutokana na kufikiri kwa matumbo badala ya vichwa?

      Mkuu uliyoandika mengi ni kweli, lakini ni vizuri ukikumbuka kuwa huwa wezi kuwa mwislamu kuliko waislamu wa Mecca, au huwezi kuwa mkatoliki kuliko Papa. Kama boss wako mwizi, ina maana gani wewe kuwa mwadilifu? Unajua kabisa kuwa Kiongozi ni mwizi na anaiba pesa ambazo wewe unakusanya, kwanini na wewe usiibe?

      Ukiangalia thread nyingi hapa JF utaona kuwa yote unayosema yamesemwa sana, na conclusion iliyofikiwa ni kuwa mtaji wa CCM [unyonge wa wananchi kielimu] ni mkubwa. Hadi unyonge huo utakapoondolewa hakuna kitakachokuja badilika hata kelele zipigwe vipi. Mfano wazi ni wezi wa EPA wameibia mabilioni lakini wapo wanatesa mitaani tena na kutukejeli, lakini wanaoiba kuku kwa njaa wanapigwa hadi kufa.

      Ukisema ukweli yatakukuta kama yaliyomkuta Kolimba au kama yaliyomkuta Mwakyembe, ni bora na wewe uwe CCM chukua chako mapema na ukae kimya.

    19. BAK
      #18
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,666
      Rep Power : 44978
      Likes Received
      8396
      Likes Given
      8376

      Default Re: Uhuru: Bajeti yakuna wengi!

      Unategemea nini kiandikwe na gazeti la magamba kama siyo kuifagilia Serikali ya magamba? Eti bajeti imekuna wengi!!! Daaaaah!!!!
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    20. #19
      sam2000's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 11th August 2011
      Posts : 153
      Rep Power : 424
      Likes Received
      38
      Likes Given
      113

      Default Re: Uhuru: Bajeti yakuna wengi!

      Quote By Landala
      Habari za leo wanajf,muda si mrefu nilikuwa napitia vichwa vya habari vya magazeti mbali mbali nikakuta kwenye gazeti la Uhuru likisema 'BAJETI YAKUNA WENGI'hivi watanzania wenzangu ni kweli hii bajeti ya 2012-2013 imekuna wengi au hili gazeti la CCM la uhuru linataka kupotosha umma ili kuitetea serikali yao ya magamba..
      Hakuna tofauti kati ya gazeti hili na yale ya mia 300!!!

    21. #20
      Indume Yene's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th March 2008
      Location : Chumbani
      Posts : 2,151
      Rep Power : 4954
      Likes Received
      334
      Likes Given
      312

      Default Re: Uhuru: Bajeti yakuna wengi!

      Nafikiri gazeti la Uhuru hawajakosea, bajeti imekuna wengi vichwani. Mtu anapojaribu kutafuta jibu ambalo haliko karibu huwa anajikuna kichwani. Sasa hii bajeti ni kweli lazima watu wajikune vichwani maana haina majibu kabisa kwa watanzania especially walala puh na mimi nikiwemo. Tanzania haina vyanzo vingine vya mapato zaidi ya kupandisha kodi kwenye soda, bia, sigara......watu wakigoma kuvuta sigara na kunywa pombe sijui serikali itapata wapi hela. Na huko ndiko tuendako.

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...