Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mbunge CCM: Bajeti si yenyewe imechakachuliwa

    Report Post
    Page 1 of 5 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 95
    1. #1
      dosama's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th December 2010
      Posts : 736
      Rep Power : 573
      Likes Received
      296
      Likes Given
      1

      Default Mbunge CCM: Bajeti si yenyewe imechakachuliwa

      WAZIRI wa Fedha na Uchumi, Dk. William Mgimwa, anadaiwa kusoma hotuba ya bajeti iliyojaa kasoro nyingi, ikiwa ni pamoja na kukosekana kwa vipengele muhimu vilivyokubaliwa na Kamati ya Uchumi na Fedha.

      Kwa kufanya hivyo, waziri huyo sasa anashutumiwa kwa kuidharau na kukiuka kwa makusudi maagizo ya kamati hiyo yaliyokuwa na lengo la kuiboresha bajeti ili ilete manufaa kwa wananchi.

      Tuhuma hizo nzito zilitolewa jana na mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM), mbele ya waandishi wa habari, na kutangaza rasmi kuipinga bajeti hiyo kwa madai kuwa haina tija kwa wananchi wanyonge.

      Aidha alisema kuwa bajeti iliyosomwa bungeni ilikataliwa na kamati hiyo bungeni kutokana na kubaini kuwa ni mbovu na haikidhi vigezo na malengo ya kumkomboa Mtanzania maskini.

      Mpina ambaye ni mjumbe wa kamati hiyo, alisema kuwa walimtaka Waziri Mgimwa kwenda kuifumua upya na kufanya marekebisho, lakini serikali imekataa ikitoa sababu na visingizo vingi.

      Kwa kujiamini, Mpina alisema kitendo cha waziri Mgimwa kutojali mapendekezo yao, kimeifanya bajeti hiyo kuonyesha kuwa serikali haina nia njema ya kuboresha maisha ya Watanzania ambao kila siku wanapiga kelele juu ya kuwepo kwa umaskini uliokithiri.

      Mpina alisema kuwa anajua msimamo wake huo, unaweza kumletea matata ndani ya CCM, lakini akadai kuwa yuko tayari kwa lolote hata ikiwa ni kufukuzwa ndani ya chama hicho.

      Mpina alisema bajeti hiyo imejaa upungufu mwingi, ikiwemo kuelekeza fedha nyingi katika matumizi makubwa ambayo siyo ya msingi na kuyaacha mambo ya maendeleo.

      Alifichua kuwa bajeti hiyo, pia imekiuka makubaliano ya wabunge ya utekelezaji wa mpango wa miaka mitano wa maendeleo ambao unalenga kuboresha maisha ya Watanzania ambao wamekata tamaa kutokana na umaskini walionao.

      Mpina alibainisha kasoro nyingine kubwa kuwa ni ukiukwaji wa maagizo ya wabunge ambao waliitaka serikali kuhakikisha kila mwaka wa fedha inatenga sh tirilioni 2.7 kutoka katika fedha za ndani kugharamia miradi ya maendeleo na kutenga asilimia nyingine 35 ya bajeti kwa ajili hiyo.

      Mbunge huyo alisema pia katika makubaliano ya wabunge na serikali yaliyokiukwa katika bajeti hiyo ni kuhakikisha kuwa fedha za umma zilizotengwa kwa ajili ya shughuli za maendeleo hazitumiki kwa ajili ya mambo mengine.

      Mpina alizidi kufichua kuwa wakati wa kujadili mpango wa maendeleo wa miaka mitano, aliyekuwa Waziri wa Fedha Mustafa Mkulo, aliwahakikishia wabunge kuwa mambo hayo yangezingatiwa kikamilifu na fedha hizo zingetengwa kila mwaka, ikianza na bajeti ya mwaka huu.

      “Lakini ukisoma bajeti iliyowasilishwa na Waziri wa Fedha na Uchumi inaonesha kuwa matumizi ya kawaida yametengewa trilioni 10.5, sawa na asilimia 70, na matumizi ya maendeleo yametengewa trilioni 4.5, sawa na asilimia 30, wakati fedha za ndani zilizotengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo ni trilioni 2.2 tu, badala ya 2.7,” alisema.

      Alisema kitendo cha serikali kutenga trilioni 2.2 badala ya trilioni 2.7 ambayo inaleta tofauti ya sh bilioni 500, iliyoainishwa awali katika mpango wa maendeleo, kimeifanya miradi mingi kutengewa fedha kidogo huku mingine mingi ikikosa fedha kabisa.

      “Kibaya zaidi katika bajeti hii, mapato ya ndani kwa sasa yameongezeka kwa trilioni 1.5, huku matumizi ya kawaida yakipanda kwa trilioni 1.9 wakati fedha za maendeleo zikipungua kwa bilioni 397.8 ikilinganishwa na mwaka wa fedha 2011/12.

      “Hapa inadhihirisha dhahiri kuwa serikali haina nia ya dhati ya kupunguza matumizi ya kawaida,” alisema Mpina.

      Mbunge huyo alizidi kusisitiza kuwa wakati serikali ikiendeleza matumizi makubwa yasiyokuwa na tija, Watanzania wengi wanakufa kwa kukosa matibabu kutokana na kukosekana kwa zahanati, dawa na waganga na wengine wakikabiliwa na ukosefu wa maji safi na salama, elimu bora kutokana na upungufu mkubwa wa madarasa na nyumba za walimu.

      Mpina aliongeza kuwa kwa kipindi kirefu serikali imekuwa ikitoa ahadi za kupunguza matumizi ya kawaida ili kuongeza kasi ya utoaji huduma na uwekezaji katika sekta zinazokuza uchumi na kupunguza umaskini.

      Alitoa mfano wa wizara mbili za Nishati na Madini na Fedha na Uchumi ambazo zimejipangia kiasi kikubwa cha fedha kwa matumizi aliyoyaita kuwa si ya lazima.

      Kwa Wizara ya Nishati na Madini, Mpina alibainisha kuwa imejitengea sh milioni 142 kwa mwaka huu wa fedha kwa ajili ya mafunzo ya nje, wakati mwaka jana ilitenga sh milioni 34, hivyo kuwa na ongezeko la milioni 108.

      Wizara hiyo itatumia sh milioni 567 kwa ajili ya mawasiliano, badala ya milioni 71.76 ilizotumia katika mwaka wa fedha 2011/12, wakati katika kile kilichoitwa Kitengo cha Utawala na Mawasiliano kitatumia sh bilioni 2.003 badala ya sh milioni 53.87 za mwaka jana.

      Nayo Wizara ya Fedha na Uchumi imejitengea sh milioni 582.3 kwa safari za wakubwa za ndani, katika Idara ya Utawala na Rasilimali Watu, wakati mwaka jana ilitumia sh milioni 283, na safari za nje itatumia sh milioni 874,wakati mwaka jana ilitumia sh milioni 532.


      Chanzo: Tanzania Daima
      Last edited by dosama; 16th June 2012 at 06:54.

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      kookolikoo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th March 2012
      Posts : 1,931
      Rep Power : 749
      Likes Received
      280
      Likes Given
      144

      Default

      nimemsikia ITV!

    4. #3
      WA-UKENYENGE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st October 2011
      Location : Inside a Smart Grid
      Posts : 2,411
      Rep Power : 5037
      Likes Received
      780
      Likes Given
      1781

      Default Re: Mbunge CCM: Bajeti si yenyewe imechakachuliwa

      Bora huyo mbunge kaamua kujilipua na bajeti!
      "The usual conclusion is that you can't put a price on a human life. But you can if you must".

    5. #4
      tedo's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 17th August 2011
      Location : uchochoroni
      Posts : 5,479
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1259
      Likes Given
      880

      Default Re: Mbunge CCM: Bajeti si yenyewe imechakachuliwa

      Shkamoo!

    6. #5
      MNYISANZU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2011
      Posts : 6,304
      Rep Power : 2017
      Likes Received
      591
      Likes Given
      76

      Default Re: Mbunge CCM: Bajeti si yenyewe imechakachuliwa

      Kasoma alama za nyakati!
      " Ni fahari sana kuwa Mkristo "

    7. Miaka 50

    8. #6
      MtamaMchungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th April 2011
      Posts : 1,539
      Rep Power : 806
      Likes Received
      710
      Likes Given
      64

      Default Re: Mbunge CCM: Bajeti si yenyewe imechakachuliwa

      Ukiona mabeki hawaelewani na viungo, ujue kinachofuatia ni kufungwa.
      Tuko, Kalumbesa, asigwa and 2 others like this.

    9. #7
      man maswi's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 2nd May 2012
      Posts : 5
      Rep Power : 356
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Mbunge CCM: Bajeti si yenyewe imechakachuliwa

      tukipata kama hawa watano wa CCM itakuwa pwaaaaaaaaaaaa kwa Peopleeeeeeeeee

    10. #8
      asigwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2011
      Location : TANDHANIYA
      Posts : 4,388
      Rep Power : 1264
      Likes Received
      1208
      Likes Given
      1253

      Default Re: Mbunge CCM: Bajeti si yenyewe imechakachuliwa

      Quote By MtamaMchungu
      Ukiona mabeki hawaelewani na viungo, ujue kinachofuatia ni kufungwa.
      kweli baba hii iliyoongea ina mantiki sana

    11. #9
      Katalyeba's Avatar
      Member Array
      Join Date : 20th April 2012
      Posts : 15
      Rep Power : 360
      Likes Received
      3
      Likes Given
      6

      Default Re: Mbunge CCM: Bajeti si yenyewe imechakachuliwa

      Tanzania wabunge wa kusema ukweli, kama mmekubaliana lakini waziri anafanya yake mwumbue hadharani.

      Kwa maelezo machache niliyoyasoma hapo juu hayahitaji uwe CCM wala CHadema kukakataa bajeti hiyo, swala Muhimu ni uzalendo. Tukubaliane kwamba tunahitaji wabunge waseme hapana tuanze na moja.

      Kilimo ndo kingetutoa lakini bajeti haisemi tufanye nini ili tuweze kutoka kwenye lindi la umasikini.

      Naomba wadau wa Jamii, tuwaombe wabunge wetu waikatae bajeti, ieleze katika kilimo zimepelekwa ngapi, na zinatafanya nini, siyo washa tu, watueleze wametenga shiling ingapi kwa ajili ya kilimo cha Umwagiaji, na nishati ya uhakika, nilimsikia Filiokujombe siku moja akiuliza, watanzania hawahitaji vitambulisho, kipambele ingekuwa Umeme wa uhakika, then ndo watuambie vitambulisho. Bravo mbunge Mpina..

      Tupo pamoja na wewe hata ukifukuzwa kwenye Ugamba, Mungu atakupigania, utarudi Bungeni kwa tiketi ya Makamanda.
      Kingo and Maundumula like this.

    12. #10
      Welu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th July 2011
      Posts : 257
      Rep Power : 449
      Likes Received
      54
      Likes Given
      1

      Default Re: Mbunge CCM: Bajeti si yenyewe imechakachuliwa

      Aache uongo, tangu wote mzaliwe ni lini mmeawahi sikia budget kuu ikagomewa. Mlishaambiwa na spika kwamba hiyo kitu haiwezekani. Nawahakikishia, watarap sana, watapinga sana huku wakiunga kwa 100%. mwisho tutaambulia mayowe ya ndiyoooooooooooooooooooooooooo oooo. Nani asiye juwa unafiki wa magamba.

    13. #11
      Msambaa mkweli's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 31st December 2011
      Posts : 152
      Rep Power : 403
      Likes Received
      26
      Likes Given
      1

      Default Re: Mbunge CCM: Bajeti si yenyewe imechakachuliwa

      Uwazi na ukweli. Vua Gamba.

    14. #12
      Njangula's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 20th October 2011
      Posts : 179
      Rep Power : 418
      Likes Received
      16
      Likes Given
      1

      Default Re: Mbunge CCM: Bajeti si yenyewe imechakachuliwa

      Angekuwa mpinzani nisingeshangaa CCM wangesema anatafuta umaarufu. Hii inaonesha kuna patriots wengi ndani ya chama tawala wenye uchungu na nchi hii. Jamaa alilosema ni jema kabisa tena amepinga ktk pre-budget meeting na tena ktk mkutano wa budget. Binafsi naipinga imeongeza matumizi yasiyo tija.
      Maundumula likes this.

    15. #13
      Kazi Deo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 28th July 2011
      Posts : 12
      Rep Power : 397
      Likes Received
      0
      Likes Given
      7

      Default Re: Mbunge CCM: Bajeti si yenyewe imechakachuliwa

      Hao ndio wanaohitajika sasa.Big up Mpina

    16. #14
      Makupa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 2,175
      Rep Power : 809
      Likes Received
      249
      Likes Given
      0

      Default Re: Mbunge CCM: Bajeti si yenyewe imechakachuliwa

      afadhali hoja nzito kama hii imetolewa na mbunge wa ccm

    17. #15
      vipik2's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th November 2011
      Posts : 364
      Rep Power : 450
      Likes Received
      79
      Likes Given
      74

      Default Re: Mbunge CCM: Bajeti si yenyewe imechakachuliwa

      Quote By Njangula
      Angekuwa mpinzani nisingeshangaa CCM wangesema anatafuta umaarufu. Hii inaonesha kuna patriots wengi ndani ya chama tawala wenye uchungu na nchi hii. Jamaa alilosema ni jema kabisa tena amepinga ktk pre-budget meeting na tena ktk mkutano wa budget. Binafsi naipinga imeongeza matumizi yasiyo tija.

      Utawaona baada ya Mtikila kushinda kesi yake huko Arusha na kiama cha CCM kitakuwa 2015, jiulize kwa nini Wabunge wengi wa CCM wanapigia chapuo mgombea binafsi hivi sasa? tayari wameshasoma alama za nyakati ukutani hivyo hawaoni shida kuja kumtosa CCM dakika za lala salama
      Tunasikitika kutangaza kifo cha ndugu CCM, Mazishi yatakuwa 2015 na habari ziwafikie ndugu wote mafisadi na shost wake CUF

    18. #16
      Malipo kwamungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2012
      Posts : 276
      Rep Power : 417
      Likes Received
      41
      Likes Given
      68

      Default Re: Mbunge CCM: Bajeti si yenyewe imechakachuliwa

      Wasiwasi wangu baada ya bajeti itafuata itikadi makini ya Jairo kuwapongeza wabunge wote kwa sherehe zitakazo fanyika ..... na kila 1 kuondoka na bahasha ya AHSANTE aah nanii siyo rushwa hii ni kama zamani tuliita takrima kwa waheshimiwa kutusaidia kupitisha bajeti yetu sisiemu twawala bana

    19. #17
      Nyakageni's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st February 2011
      Posts : 5,230
      Rep Power : 1537
      Likes Received
      764
      Likes Given
      52

      Default Re: Mbunge CCM: Bajeti si yenyewe imechakachuliwa

      mnafiki tu huyu!

    20. #18
      marejesho's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Location : MULA
      Posts : 3,364
      Rep Power : 13046
      Likes Received
      1553
      Likes Given
      1137

      Default Re: Mbunge CCM: Bajeti si yenyewe imechakachuliwa

      Safi sana!

    21. #19
      peter tumaini's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2012
      Location : DSM
      Posts : 575
      Rep Power : 483
      Likes Received
      86
      Likes Given
      54

      Default Re: Mbunge CCM: Bajeti si yenyewe imechakachuliwa

      Quote By Njangula
      Angekuwa mpinzani nisingeshangaa CCM wangesema anatafuta umaarufu. Hii inaonesha kuna patriots wengi ndani ya chama tawala wenye uchungu na nchi hii. Jamaa alilosema ni jema kabisa tena amepinga ktk pre-budget meeting na tena ktk mkutano wa budget. Binafsi naipinga imeongeza matumizi yasiyo tija.
      mkuu uko sawa, kama kitu hukubaliani nacho ni bora uonyeshe hisia zako hadharani kuliko kuwa mnafiki.

    22. #20
      peter tumaini's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2012
      Location : DSM
      Posts : 575
      Rep Power : 483
      Likes Received
      86
      Likes Given
      54

      Default Re: Mbunge CCM: Bajeti si yenyewe imechakachuliwa

      nampongeza kwa kusimamia anacho kiamini bila kujali gharama zake.

    23. Study Abroad
    Page 1 of 5 123 ... LastLast

    LinkBacks (?)


    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...