Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kuhusu Utanganyika: Shetani Unayemjua ni Bora Kuliko Malaika Usiyemjua!

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 29
    1. #1
      LordJustice1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2011
      Posts : 2,069
      Rep Power : 2301
      Likes Received
      409
      Likes Given
      36

      Default Kuhusu Utanganyika: Shetani Unayemjua ni Bora Kuliko Malaika Usiyemjua!

      Wakuu,
      Watanzania wengi wamezaliwa baada ya Aprili 26, 1964 kwa hiyo hawaijui Tanganyika, wanasoma tu kwenye makabrasha. Kama hiyo si sahihi sasa basi Watanganyika walioishi Tanganyika huru iliyodumu kwa miaka takriban 4 (1961-1964) wanaijua vizuri Tanzania kuliko Tanganyika iliyodumu muda mfupi!
      Afterall, wanaoidai Tanganyika hawajui kwamba kuna Tanganyika za aina kadhaa:
      1. Tanganyika ya kabla ya Mjerumani ambayo haikuwa na mipaka (Pre-1884),
      2. Tanganyika ya Mjerumani ambayo ilikuwa na mipaka iliyojumuisha Rwanda na Burundi (1884-1919),
      3. Tanganyika ya Mwingereza ambayo haijumuishi Rwanda na Burundi (1919-1961),
      4. Tanganyika ya Nyerere ambayo ilidumu kwa muda mfupi (1961-1964),

      Kwa hiyo wanaoipigania "Tanganyika" ni ipi hasa na kwa nini? Hiyo Tanganyika mpya ina siri gani ambayo itatukwamua kwenye lindi la umaskini? Sio tukiipata hiyo "Tanganyika mpya" tutakuta ufisadi bado unatutafuna kisawasawa kama kawaida? Hivi Watz tumekosa kabisa viongozi wa kutusaidia kujua matatizo ya kweli ya nchi yetu na kuyamaliza "once and for all" badala ya kutuletea "mvinyo wa zamani ndani ya chupa mpya" huku tukiacha matatizo halisi ya ufisadi, wizi, mikataba mibovu, ahadi hewa, udini, kututafuna?

      Si afadhali kuendelea na shetani tunayemfahamu (Tanzania) kuliko kung'ang'ania malaika (Tanganyika) tusiyemfahamu? Maana tumeonjeshwa na WANAUAMSHO kwamba tatizo ni nyumba za Ibada, si Muungano!

      Tukiwasikiliza hawa jamaa tutacheza ngoma tusyoijua, tutahenyeshwa kisawasawa kama Wakenya wanavyohenyeshwa na Al-Shabaab! Mambo haya yaluanza kama mchezo kama yanavyoendelea kwenye Utawala wa JK na bahati mbaya kuna mkono wa Serikali kwenye vuguvugu ya Uamsho! Sasa hivi wamehamia kwa Dr Ndalichako, Sensa, nk. Kesho utasikia mengine mengi! Tuiache Tanzania yetu kama ilivyo, tu-focus kwenye "real issues!!"
      Nawasilisha!!
      Last edited by LordJustice1; 15th June 2012 at 23:16.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Janjaweed's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th January 2010
      Posts : 3,620
      Rep Power : 1129
      Likes Received
      1390
      Likes Given
      1541

      Default Re: Kuhusu Utanganyika: Shetani Unayemjua ni Bora Kuliko Malaika Usiyemjua!

      tunaifahamu tangannyika acha kutudhalilisha
      kwamwewe likes this.
      Kama Vipi nipotezee tu; ntakuboa....

    4. #3
      LordJustice1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2011
      Posts : 2,069
      Rep Power : 2301
      Likes Received
      409
      Likes Given
      36

      Default

      Quote By Janjaweed
      tunaifahamu tangannyika acha kutudhalilisha
      Tanganyika ipi unayoifahamu wewe?

    5. #4
      Nyetk's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th February 2012
      Posts : 1,028
      Rep Power : 682
      Likes Received
      574
      Likes Given
      590

      Default Re: Kuhusu Utanganyika: Shetani Unayemjua ni Bora Kuliko Malaika Usiyemjua!

      Shida ya "watanganyika" siyo "Tanganyika" kimsingi maana hurka ya watu wa bara ni wamoja zaidi kuliko hao wapiga mayowe. Bali shida ya " watanganyika" ni KUCHOSHWA NA KELELE ZISIZOISHA NA ZISIZO MANTIKI ISIPOKUWA UDINI TU! Bahati mbaya kwa wabara hawa viongozi wa serikali zote mbili ama ni ndumilakuwili, ama ni mazezeta ama hawana meno na matokeo yake wamechochea kwa namna nyingi uhasama huu wa udini.

      Kwa kifupi hoja ya watanganyika ni kiitikio cha wimbo wa wazenji chenye maana hizi:
      1. To let Zanzibar go kwa maana ya kuchoshwa na makelele yasiyoisha ya wazenji ili (watanganyika) watumie muda vizuri kuzungumza habari za maendeleo na siyo ujinga tu kila kukicha. .
      2. To root away the seed of hate and conflict kwa maana kuwa upumbavu huu sasa umeanza kutudhuru tukizingatia kuwa nchi haina serikali kwa sasa.
      Last edited by Nyetk; 16th June 2012 at 00:15.

    6. #5
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Kuhusu Utanganyika: Shetani Unayemjua ni Bora Kuliko Malaika Usiyemjua!

      Mbona huongelei kabla ya Mjerumani?
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      LordJustice1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2011
      Posts : 2,069
      Rep Power : 2301
      Likes Received
      409
      Likes Given
      36

      Default

      Quote By Nyetk
      Shida ya "watanganyika" siyo "Tanganyika" kimsingi maana hurka ya watu wa bara ni wamoja zaidi kuliko hao wapiga mayowe. Bali shida ya " watanganyika" ni KUCHOSHWA NA KELELE ZISIZOISHA NA ZISIZO MANTIKI ISIPOKUWA UDINI TU! Bahati mbaya kwa wabara hawa viongozi wa serikali zote mbili ama ni ndumilakuwili, ama ni mazezeta ama hawana meno na matokeo yake wamechochea kwa namna nyingi uhasama huu wa udini.

      Kwa kifupi hoja ya watanganyika ni kiitikio cha wimbo wa wazenji chenye maana hizi:
      1. To let Zanzibar go kwa maana ya kuchoshwa na makelele yasiyoisha ya wazenji ili (watanganyika) watumie muda vizuri kuzungumza habari za maendeleo na siyo ujinga tu kila kukicha. .
      2. To root away the seed of hate and conflict kwa maana kuwa upumbavu huu sasa umeanza kutudhuru tukizingatia kuwa nchi haina serikali kwa sasa.
      Tatizo lako (sio la "Watanganyika" kama unavyodai) unafikiri mambo yataenda smooth na tutaishi raha mustarehe tuki-"let Zanzibar go!" Umesahau kwamba au hujui kwamba Wana-Uamsho ni watu wanaotumiwa na Waarabu wanaoumezea mate ukanda wa Afrika Mashariki (including DSM, Tanga, Mombasa, nk)! Sasa unapodai "to let Zanzibar go" you don't know the move behind the curtain, unafikiri kuwa ni "Movement ya Kisiasa" kumbe ni "ya Kidini!" Umefika wakati wa kuona mbele zaidi ya pua yako!

    9. #7
      LordJustice1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2011
      Posts : 2,069
      Rep Power : 2301
      Likes Received
      409
      Likes Given
      36

      Default

      Quote By zomba
      Mbona huongelei kabla ya Mjerumani?
      Nani unayemtaka aongelee hiyo Tanganyika ya kabla ya Mjerumani (German East Africa?)

    10. #8
      kookolikoo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th March 2012
      Posts : 1,951
      Rep Power : 753
      Likes Received
      281
      Likes Given
      146

      Default

      Quote By LordJustice1
      Nani unayemtaka aongelee hiyo Tanganyika ya kabla ya Mjerumani (German East Africa?)
      hakukuwa na hiyo German East Africa. Baada ya Berlin Conference kulikuwa na Deutsche Ost Africa iliyojumuisha Tanganyika Rwanda na Burundi!

    11. #9
      asigwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2011
      Location : TANDHANIYA
      Posts : 4,389
      Rep Power : 1265
      Likes Received
      1209
      Likes Given
      1253

      Default Re: Kuhusu Utanganyika: Shetani Unayemjua ni Bora Kuliko Malaika Usiyemjua!

      duh kweli mukulu...watanzania wanaiomba tanganyika ili wawe wadanganyika

    12. #10
      Shine's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th February 2011
      Posts : 9,187
      Rep Power : 2429
      Likes Received
      946
      Likes Given
      377

      Default Re: Kuhusu Utanganyika: Shetani Unayemjua ni Bora Kuliko Malaika Usiyemjua!

      Hata pamoja na yote hayo kauli uliyoitumia ktk title siyo njema fanya kuiondoa

    13. #11
      Makala Jr's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th August 2011
      Posts : 1,645
      Rep Power : 721
      Likes Received
      344
      Likes Given
      0

      Default Re: Kuhusu Utanganyika: Shetani Unayemjua ni Bora Kuliko Malaika Usiyemjua!

      Suala hapa siyo kuvunja muungano wala kuidai Tanganyika.Hiyo Tanganyika itakuwa chini ya nani? Mara kadhaa kumekuwa na maneno kuwa wakristo bara ni wengi zaidi kuliko waislamu,sasa vp tena hiyo Tanganyika kwa upande wenye waislamu wengi watakapoleta madai ya kuanzisha mikoa maalum ya kiislam? Hivyo suala la udini siyo la Tanganyika na Zanzibar bali hata ndani ya Tanganyika litakuwepo. Mtazamo wa kuita ni kelele madai ya wazenj ni UTOVU NI NIDHAMU.Nchi hii ikigawanyika kipuuzi-kipuuzi tu nasi tukawa tunachukulia kawaida iko siku tutaukumbuka wakati huu muhimu,ambao tunaweza kukaa na kujadiliana kwa amani juu ya Muungano.Mkisema tatizo ni udini na zenj ikabainishwa kuwa ni nchi ya kiislam then,waislam walioko bara mtawataka waende Zanzibar? Kiini cha tatizo siyo udini tu bali pia UTAWALA ULIOCHOKA WA CCM.Badala ya kuweka mambo wazi ili wananchi wajadili namna ya kuuboresha muungano wao wakaunda cjui tume ya kushughulikia kero za muungano then muungano ukatafsiriwa kuwa KERO.

    14. #12
      Crucifix's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 20th February 2011
      Posts : 1,569
      Rep Power : 0
      Likes Received
      430
      Likes Given
      321

      Default Re: Kuhusu Utanganyika: Shetani Unayemjua ni Bora Kuliko Malaika Usiyemjua!

      hoja yako ni hoja mfu kabisa; kuna kasoro nyingi za muungano ambazo mimi niliyezaliwa miaka ya sabini ninaziona na siwezi kuwa **** kwa kukumbatia makosa ya babu zangu. Waulize Sudan kusini waliozaliwa katika Sudan moja ni kwa nini waliamua kujiondoa, kisha uje tena na hoja yenye maana. Bora malaika nisiyemjua kwa kuwa siku zote malaika ni mwema, kulikoni shetani yoyote. Wewe na mashetani wenzakomnaopendelea muungano kwendeni zenu. Wana uamsho z'bar wana matatizo yao pamoja na njaa lakini sisi watanganyika una hoja za msingi kuidai Tanganyika yetu.

    15. #13
      Kasimba G's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2011
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 852
      Rep Power : 593
      Likes Received
      252
      Likes Given
      265

      Default Re: Kuhusu Utanganyika: Shetani Unayemjua ni Bora Kuliko Malaika Usiyemjua!

      Inafuatana unamsema malaika yupi? 1? Mungu au wa shetani? Kama ni wa Mungu hata usipomjua ni bora kuliko shetani!

    16. #14
      papason's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th September 2010
      Location : Choma Cha Nkola
      Posts : 875
      Rep Power : 616
      Likes Received
      154
      Likes Given
      164

      Default Re: Kuhusu Utanganyika: Shetani Unayemjua ni Bora Kuliko Malaika Usiyemjua!

      walai tena si bure! Wewe una lako jambo, sijui umetumwa na nani?

    17. #15
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Kuhusu Utanganyika: Shetani Unayemjua ni Bora Kuliko Malaika Usiyemjua!

      Quote By LordJustice1
      Nani unayemtaka aongelee hiyo Tanganyika ya kabla ya Mjerumani (German East Africa?)
      Mleta mada.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    18. #16
      Nyetk's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th February 2012
      Posts : 1,028
      Rep Power : 682
      Likes Received
      574
      Likes Given
      590

      Default Re: Kuhusu Utanganyika: Shetani Unayemjua ni Bora Kuliko Malaika Usiyemjua!

      Quote By LordJustice1
      Tatizo lako (sio la "Watanganyika" kama unavyodai) unafikiri mambo yataenda smooth na tutaishi raha mustarehe tuki-"let Zanzibar go!" Umesahau kwamba au hujui kwamba Wana-Uamsho ni watu wanaotumiwa na Waarabu wanaoumezea mate ukanda wa Afrika Mashariki (including DSM, Tanga, Mombasa, nk)! Sasa unapodai "to let Zanzibar go" you don't know the move behind the curtain, unafikiri kuwa ni "Movement ya Kisiasa" kumbe ni "ya Kidini!" Umefika wakati wa kuona mbele zaidi ya pua yako!
      Mkuu, kwa kawaida ukianzisha mada basi unajivika jukumu la kuratibu mjadala in a fair and objective manner. Kama mwanzishaji mada na kwa hiyo mwendeshaji majadiliano hukupashwa kuwa wa kwanza kurusha kauli za kashfa kwa wachangiaji. Hapo pekundu pamekutambulisha kama ifuatavyo:
      1. Una tabia ya udictator na unadhani uonavyo wewe basi ndiyo ukweli. Who are you hata ujidhani kuwa mtazamo wako ndiyo bora kuliko wa wengine?
      2. Wewe yumkini ni tunda na sehemu ya uozo ambao watanzania tunataka sasa kuuondoa. Mwenye akili timamu katu hawezi kukubaliana na kichwa cha habari ulivyokiweka: "Kuhusu Utanganyika: Shetani Unayemjua ni Bora Kuliko Malaika Usiyemjua!" Katika hili shetani ni nani na malaika ni nani? Unataka kusema kwa kuwa chama fulani (kwa mfano) ndo kimetawala miaka mingi hata kama kimepoteza dira na watu wanaona nchi inaenda vibaya tukiache kitawale milele kwa sababu ndiyo shetani tunayemjua? Infalibility ya muungno wa namna hii imeletwa na malaika yupi?


      Kama niliyoandika juu yako hapo juu hayakuhusu basi napata mashaka sana kama wewe kweli ni mtanzania na unayeishi ndani ya mipaka ya nchi hii.
      Last edited by Nyetk; 16th June 2012 at 14:28.
      kwamwewe likes this.

    19. #17
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Kuhusu Utanganyika: Shetani Unayemjua ni Bora Kuliko Malaika Usiyemjua!

      Kama umeshindwa kuuongelea Utanganyika kabla ya Mjerumani, jee, unaweza kutueleza maana ya Tanganyika? na jinaTanganyika limetoka wapi? kwani Tanzania tunajuwa ni Muhindi wa Tanga aliyetowa hilo jina. Tanganyika jee?
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    20. #18
      kwamwewe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2010
      Posts : 856
      Rep Power : 5406
      Likes Received
      99
      Likes Given
      125

      Default Re: Kuhusu Utanganyika: Shetani Unayemjua ni Bora Kuliko Malaika Usiyemjua!

      Quote By LordJustice1
      Tatizo lako (sio la "Watanganyika" kama unavyodai) unafikiri mambo yataenda smooth na tutaishi raha mustarehe tuki-"let Zanzibar go!" Umesahau kwamba au hujui kwamba Wana-Uamsho ni watu wanaotumiwa na Waarabu wanaoumezea mate ukanda wa Afrika Mashariki (including DSM, Tanga, Mombasa, nk)! Sasa unapodai "to let Zanzibar go" you don't know the move behind the curtain, unafikiri kuwa ni "Movement ya Kisiasa" kumbe ni "ya Kidini!" Umefika wakati wa kuona mbele zaidi ya pua yako!
      kwani kanisa linatumiwa na nani ?? waafrika ??? kwani uarabu ni udini ??

      wrong thought !!!wrong idea !!! wrong time!!! wrong place!!!

    21. #19
      babuwaloliondo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th March 2011
      Posts : 287
      Rep Power : 472
      Likes Received
      100
      Likes Given
      614

      Default Re: Kuhusu Utanganyika: Shetani Unayemjua ni Bora Kuliko Malaika Usiyemjua!

      unarecycle post za mwanakijiji
      The hottest places in hell are reserved for those who in times of great moral crisis maintain their neutrality.- JFK

    22. #20
      Mwiba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd October 2007
      Posts : 4,593
      Rep Power : 2085
      Likes Received
      223
      Likes Given
      19

      Default Re: Kuhusu Utanganyika: Shetani Unayemjua ni Bora Kuliko Malaika Usiyemjua!

      Yakhee inaposemwa Tanganyika ni hii Tanganyika tuliopatia Uhuru ya TANU na inaposemwa Zanzibar ni ileile waliyopata Uhuru ,maana kama utaihitaji hizo zingine basi mikoa ya Pwani yote itaenda Zanzibar ,angalia ukienda Mahakamani usije ukasema unaidai tanganyika ya Mjeru ,tutapoteza ukanda wapwani kwa kilomita kibao.
      Light travels faster than sound. This is why some people appear bright until you hear them speak.

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...