Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

    Report Post
    Page 1 of 16 12311 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 315
    1. #1
      Hutaki Unaacha's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 19th September 2010
      Posts : 9
      Rep Power : 456
      Likes Received
      355
      Likes Given
      0

      Default CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

      Wapendwa wanaJF,

      Kwanza niwaombe radhi kwa kukaa kimya kwa muda mrefu baada ya kutoa part II na kuahidi kuendelea kutoa part III ambayo ingekuwa ya mwisho. Ninajisikia vibaya kwa kukaa kimya bila kuwajulisha chochote. Mnisamehe kwa hilo. Ninafahamu wengi mtanielewa nikisema kwamba nimeacha kwa sasa kuendelea na ile series mpaka pale muda mwafaka utakapowadia tena. Kuna mipango mingi ambayo nilitaka kuielezea ya ndani zaidi (hasa kama ningefikia kwa Apson na Edward) ambayo kwa namna moja nyingine ingekuwa na matokeo ya aina mbili tu yaani kutengeneza mwanzo wa njia ya kuelekea kwenye ukombozi wa taifa letu au uvunjifu wa amani kubwa ambayo haikuwahi kutokea katika historia ya nchi yetu (nime-consider taifa kwanza ingawa ya kwangu ni tofauti na intelijensia ya mwema). Muda ukifika nitaleta habari yote ikiwa kamili na kwa hili sitakaa muda mrefu kama ambavyo huwa nafanya. Naomba tena mnielewe kwa hilo na kusema ukweli nawaomba radhi sana tena sana kwa hili.

      Lakini kuna hili ambalo imebidi nisiliache na kwa haraka haraka na mpangilio mbovu naomba nilitoe hasa kwa CHADEMA na rafiki zake. Mimi sio mwanachama wa chama chochote cha siasa. JK anakiri na ameendelea kukiri kwamba EL ameharibu mipango yake mingi sana. Analalamika sana jinsi ambavyo EL ameharibu strategies zake za kumweka mtu wake Ikulu. Kwa bahati mbaya sana JK amekuwa akishinikizwa na baadhi ya “washika dini” kumweka muislam kwenye urais wa 2015 kwa muda mrefu sasa. Niseme wazi kuwa sina shida na Islam na hata wakiongoza consecutively kwa miaka 400. Tatizo naliona pale ambapo dini inakuwa sifa. Na wapo waislamu wengi ambao hawaipendi tabia hii maana baadhi wanasema inawadhalilisha. Najaribu kutoa habari tu. Sitaki tuingie kwenye malumbano ya dini. I love my country. Mtu wa mwisho ambaye EL amemharibu ni Nundu..JK ameumia sana. Sikuwahi kumwona JK akiumia kiasi hiki baada ya mpendwa wake wa 2015 (Nundu) kuharibiwa. Nafahamu wengi watashangaa kumwona JK akihangaika kumweka Nundu 2015 akiwakilisha CCM. Nataka niseme wazi kuwa, yeye ndiye alikuwa anaandaliwa. Ninao ushahidi wa wazi kabisa. Nahodha, Hussein, Asharose (ambaye ame-underperform na “kufukuzwa” na Ban) etc wameonekana hawawezi kushindana na EL ndani ya CCM. Hata Emmanuel, Membe etc ambao labda wangeweza kutumika kushawishi kanisa hawawezi kushindana na EL ndani ya CCM.

      Kwa ufupi sana, ripoti iliyomfikia JK kutoka state department ilimnyong’onyeza JK pale ilipobainika wazi kuwa hakuna mwanaCCM ambaye atamshinda EL 2015. Baada ya kuona hakuna namna nyingine, mwezi uliopita JK na EL wamekutana karibu mara 4 na “kusameheana” ili kujenga mtandao wa kuendelea kuwa na mtu wao 2015 as a president..Katika mkutano ule ambao Rostam hakuhudhuria labda kwa sababu ya ugonjwa wa baba yake mzazi (anamuuguza baba yake kwa sasa), lengo lilikuwa ni kupanga mipango ya nini kifanyike ili CHADEMA wasishinde urais 2015. Katika mikutano yao, imeonekana kwamba, ni vigumu kumshinda Dr Slaa kwa kura (kumbuka huyu katika uchaguzi wa 2010 alipata 47.3% kama matokeo halisi kabla ya uchakachuaji wa kishamba kufanyika). Kwa maana hiyo mambo/alternatives yafuatayo yaliazimiwa (hili ni muhimu sana na ushabiki uwekwe pembeni ili muweze kunusuru chama chenu na mikakati yenu);

      1. Ule mpango wa kuipasua CHADEMA (unaohusisha viongozi wa dini walio karibu na CHADEMA au Slaa na kuratibiwa na idara kwa usiri wa hali ya juu) usitishwe kwa muda ili kuona kama mipango mingine itafaulu.

      2. JK ajiuzulu urais mnamo mwaka 2013 hivi ili chini ya Bilal na kwa muda mfupi mabadiliko makubwa yafanyike na CHADEMA waweze kujumuishwa katika serikali hasa Dr Slaa ili kujipanga kukimaliza CHADEMA kwa urais zaidi. Ingawa JK alihofia hii technique kwa maana ya Bilal but hii naona ina mkono wa “wafanyabiashara” wakubwa wa mataifa Fulani ambao wanataka biashara zao ziende vizuri kama JK ataondoka madarakani kwani akiendelea hataweza kumweka mtu wao ili aendelee kulinda 'maslahi Fulani'

      3. Katiba ijayo iruhusu serikali tatu na by any means ilazimike kuwa EL awe rais wa Tanganyika, Dr Slaa/CHADEMA wa Muungano (asiye na nguvu yoyote) na Shein aendelee Zanzibar.

      4. Moja ya watu wenye nguvu ndani ya CHADEMA ashawishike kugombea kama independent candidate (sio Zitto) na malipo yake yawe competitive na campaign yake 2015 iwe sponsored kwa gharama yeyote ile.

      CHADEMA kuweni makini sana na baadhi ya wajumbe wa kamati kuu ambao wanaweza kuwaharibia your way to 2015. Muda umeniishia kwa leo maana nasafiri muda si mrefu otherwise nikipata muda tena nitawapa updates. Thank you.

    2. Study Abroad

    3. #2
      The State's Avatar
      Member Array
      Join Date : 19th March 2012
      Posts : 15
      Rep Power : 364
      Likes Received
      23
      Likes Given
      0

      Default Re: CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

      Duh, Hutaki Unaacha akishakuja tu hali ya hewa nchini na JF huwa inabadilika kwa muda..Ngoja kwanza nikae chini ili nisome nikiwa nimepumzika..Mama watoto lete juice!
      Mkono, cicy, Baba Collins and 2 others like this.

    4. #3
      TANMO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Tanzagiza
      Posts : 5,045
      Rep Power : 7768
      Likes Received
      1806
      Likes Given
      3439

      Default Re: CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

      Kwamba JK atakubali kuachia madaraka kabla ya muda? Nitashangaa sana, he does not look like he can that easily leave that office...
      cicy likes this.

    5. #4
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7367
      Likes Received
      6149
      Likes Given
      22265

      Default

      Quote By Hutaki Unaacha
      ...CHADEMA kuweni makini sana na baadhi ya wajumbe wa kamati kuu ambao wanaweza kuwaharibia your way to 2015. Muda umeniishia kwa leo maana nasafiri muda si mrefu otherwise nikipata muda tena nitawapa updates. Thank you.
      Mkuu Hutaki Unaacha, karibu tena.

      Msamaha wako nimeuelewa na nimefarijika kukuona bado upo maana nilihisi watu wako wameisha kupotezea!.

      Tukija kwenye haya usemayo kuhusu Chadema na 2015, this is too good to be true!.

      Hata hivyo nasubiria!.
      KOMBESANA and Tumaini Makene like this.

    6. #5
      Sangarara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 3,291
      Rep Power : 1195
      Likes Received
      1178
      Likes Given
      1551

      Default Re: CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

      Quote By TANMO
      Kwamba JK atakubali kuachia madaraka kabla ya muda? Nitashangaa sana, he does not look like he can that easily leave that office...
      Anaweza, tena vizuri sana, Hataki shida yule ni muoga sana.
      TANMO, Mantuntunu and saddam like this.

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      Kocha's Avatar
      Member Array
      Join Date : 2nd March 2008
      Location : Kijitonyama,Dar es Salaam
      Posts : 96
      Rep Power : 591
      Likes Received
      25
      Likes Given
      42

      Default Re: CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

      Nashauri hizi habari zifanyiwe kazi ipasavyo na Intelijinsia ya CHADEMA, zisipuuzwe kwani itasaidia kuwa na uhakika wa ushindi 2015 inawezekana kuna ukweli ndani yake

    9. #7
      STIDE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st September 2011
      Posts : 800
      Rep Power : 554
      Likes Received
      268
      Likes Given
      0

      Default Re: CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

      Naiona Tanzania katika machafuko ya kisiasa!!

    10. #8
      Asprin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 8th March 2008
      Location : Psychiatric Ward
      Posts : 25,419
      Rep Power : 32071
      Likes Received
      14527
      Likes Given
      22033

      Default Re: CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

      Mambo ya kusadikika haya. Sijapata picha ya lolote kati ya haya kuwa litatekelezeka.

      Ngoja tu nisitake na niyaache
      Mkono, kamili and grndossy like this.

    11. #9
      Molemo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Posts : 8,390
      Rep Power : 10868
      Likes Received
      3772
      Likes Given
      426

      Default Re: CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

      Ee Mungu linusuru Taifa lako.
      Mafie PM and Tumaini Makene like this.

    12. #10
      Edson's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2009
      Posts : 7,308
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1799
      Likes Given
      433

      Default Re: CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

      baadhi ya mipango uliyoongelea ni kweli
      Ibambasi and Tumaini Makene like this.
      I'm Naturaly Evasive..

    13. #11
      jogi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th September 2010
      Posts : 3,973
      Rep Power : 1209
      Likes Received
      965
      Likes Given
      247

      Default Re: CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

      kwani wakuu ule mkutano tulioambiwa ulifanyika kwa siri kati kub na jk unaweza kuwa classic info. ku-justify angalau kwa mbaaali maelezo ya Hutaki Unaacha?

    14. #12
      Ibrah's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd March 2007
      Location : TZ
      Posts : 2,883
      Rep Power : 1198
      Likes Received
      402
      Likes Given
      46

      Default Re: CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

      Hutaki unaacha, asante kwa nondo, sisi tunatafakari na kuangalia upepo uvumavyo.

      Kitu ninachokubali moja kwa moja ni Chadema kuweni makini, kila clue inayopatikana, kwa watu makini ni jambo la kufanyia kazi.
      Nani asiyejua kuwa kura za Dk Slaa zilichakachuliwa? CCM wanajua wazi kuchakachua kura za urais 2015 itakuwa kazi ngumu sana, na yawezekana matokeo ya uchakachuaji kura za urais 2015 yanaweza kuingiza nchi yetu kwenye historia na ukizingatia ICC imeshatinga Kenya, wanatutolea macho Tanzania.
      Jasusi and Tumaini Makene like this.

    15. #13
      dosama's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th December 2010
      Posts : 736
      Rep Power : 572
      Likes Received
      296
      Likes Given
      1

      Default Re: CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

      Manao copy habari yote acheni hizo tabia mnakera kwa sababu tushaisoma nawe unairudisha kama ilivyo

    16. #14
      Bhavick's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2011
      Posts : 314
      Rep Power : 449
      Likes Received
      56
      Likes Given
      8

      Default Re: CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

      Mungu tuokoe!
      Mafie PM likes this.

    17. #15
      kiraia's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2007
      Location : Kowamrasa
      Posts : 647
      Rep Power : 716
      Likes Received
      83
      Likes Given
      476

      Default Re: CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

      Hutaki unaacha hilo la mtu mwenye NGUVU ndani ya CHADEMA Kugombea kama private candidates nimelisikia baada ya CCM kuridhia mgombea Binafsi kwenye kikao kilichopita, ila huyo uliyesema siye watu wanasema ndiye anayeandaliwa kufanya hivyo.
      Invisible, Jasusi, jmushi1 and 4 others like this.
      The most dangareous position in which to sleep is with your feet on your office desk.

    18. #16
      Ritz's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 1st January 2011
      Location : Republic of Nauru
      Posts : 18,144
      Rep Power : 12552
      Likes Received
      5725
      Likes Given
      742

      Default Re: CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

      Quote By Hutaki Unaacha
      ...2. JK ajiuzulu urais mnamo mwaka 2013 hivi ili chini ya Bilal na kwa muda mfupi mabadiliko makubwa yafanyike na CHADEMA waweze kujumuishwa katika serikali hasa Dr Slaa ili kujipanga kukimaliza CHADEMA kwa urais zaidi. Ingawa JK alihofia hii technique kwa maana ya Bilal but hii naona ina mkono wa “wafanyabiashara” wakubwa wa mataifa Fulani ambao wanataka biashara zao ziende vizuri kama JK ataondoka madarakani kwani akiendelea hataweza kumweka mtu wao ili aendelee kulinda maslahi Fulani
      Haya twende kazi.
      "Kuna kontena la futi 40 lilobeba karatasi za kupigia kura limekamatwa Tunduma" Dk W. Slaa

    19. #17
      Mpangamji's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 12th May 2010
      Posts : 483
      Rep Power : 554
      Likes Received
      117
      Likes Given
      70

      Default Re: CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

      Ngumu kumeza! CDM endeleeni na taratibu zenu, msiweke nguvu nyingi kufuatilia ukweli au uongo wa haya mambo. Tricked
      KOMBESANA and Tumaini Makene like this.

    20. #18
      Comi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd October 2011
      Posts : 958
      Rep Power : 576
      Likes Received
      154
      Likes Given
      2

      Default Re: CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

      Hivi jamani laana inachukuaga mda gani mpaka ianze kazi? Maana mhh
      Mafie PM likes this.

    21. #19
      STIDE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st September 2011
      Posts : 800
      Rep Power : 554
      Likes Received
      268
      Likes Given
      0

      Default Re: CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

      Hutaki Unaacha, please kama ulivosema waipenda Tz, hebu onyesha uzalendo wako kwa kututafunia huyu alieandaliwa!! Ili tuwe nae makini. Please!!
      Tumaini Makene likes this.

    22. #20
      Royals's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th November 2011
      Posts : 1,000
      Rep Power : 579
      Likes Received
      215
      Likes Given
      4

      Default Re: CHADEMA kuweni makini sana, kilicho nyuma ya pazia hiki hapa!

      Heee. ukiona hivo ujue miti yote inateleza. Ujanja huo nduo ulioiangamiza Cuf.

    23. Miaka 50
    Page 1 of 16 12311 ... LastLast

    LinkBacks (?)


    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...