Ni kweli kabisa physics, nimesoma hoja za wachangiaji wote naona wote wanaopinga hili jambo kama vile kuna maslahi flani wanayatetea. Vinginevyo sioni ugumu wa suala hili hata kidogo, na kwa ujumla hoja zao hazina uzito wala mantiki. Nitazieleza hoja chache tu kama ifuatavyo:
1. Waislamu watafute idadi yao wenyewe: hoja hapa si kwamba waislamu wanataka idadi yao, bali wanataka idadi rasmi ya watanzania kwa dini zao. Wakijihesabu wao bado haitasaidia kujua makundi ya dini nyingine officially. Wengine wanadai kuwa dini si waislamu na wakristo tu kuna dini za asili na wapagani, tuambieni wapagani ni wangapi? dini asilia ni wangapi? Na hii ni takwimu ya kawaida tu kwa nchi na nchi nyingi duniani zina data hizi na zinapatikana kwenye sensa zao. (angalia country profiles za nchi katika websites za cia, undp, worldbank, n.k.). Hoja ni kuwa kipengele cha dini kikiwekwa itakuwa ndiyo official data ya Tanzania as of 2012. Sioni tatizo na nadhani wanaopinga na kujiona eti wamekwenda shule dunia itawacheka kwa kupinga jambo la kawaida mno.
1. Waislamu wakijua wako wangapi so what? Kwani wamarekani, waingereza, wajerumani, wa Indonesia n.k. tunajua idadi ya dini zao mbali mbali so what? kusema hivyo si maanishi kwamba haina maana ina maana na partly maana hiyo ndiyo inayowafanya wanaopinga waendelee kupinga. Maana yake ni kubwa mno baadhi yake ni kutuwezesha kufanya country and regional comparisons of religious groups na preveiling social relations which affect their lives and the way they relate with others. Mf. unasema Northern Ireland majority ni Catholics, while England majority ni Anglican. Vile vile unasema nchi yenye waislamu wengi duniani ni Indonesia n.k. Kwa nchi takwimu za dini zina maana sana hata kwa serikali kwa mfan; katika mipango miji ni serikali inayotayarisha maeneo ya matumizi mbali mbali kama makazi, biashara, taasisi, viwanda, na maeneo ya ibada (misikiti, makanisa). Maeneo ya ibada hutengwa kwa kuangalia idadi ya waumini wa dini husika. Usipojua idadi yao unaweza ukaweka eneo kubwa na kuyanyima matumizi mengine yanayohitaji ardhi zaidi, au ukaweka eneo dogo ambalo halitoshelezi mahitaji ya waumini na hivyo kuleta msongamno ambao baadae huleta mizozo isiyokuwa ya lazima.
3. Wakatoliki wanajua idadi yao: Kwani wakristu wote ni wakatoliki? mbona hamjasema Anglican, Lutheran, SDA, Assemblies of God nao wanajua idadi yao. Na hata hao wakatoliki mbona sijaona hata mmoja wenu amesema precisely wako milioni ngapi Tanzania, huko ndo kujua idadi yao. Na zaidi ya hayo wasio na dini nao wanaipataje idadi yao maana wao hawana kanisa la kuwafanya wahesabiane kwa matumizi yao ya kidini.
4. Serikali kuwafanyia waislamu sensa: Kilichopo ni kwamba serikali inataka kufanya sensa ambao ni utaratibu wa kawaida wa nchi kujua idadi ya watu wake kila baada ya miaka kumi. Wanachoomba waislamu ni kuingizwa kipengele cha kujua dini ya mtu katika sensa ambayo inataka kufanyika. Jambo hili haliongezi wala kupunguza gharama ya serikali kufanya sensa. Ingekuwa serikali imekwisha fanya sensa, halafu waislamu wanaomba ifanyike tena hapo kidogo ungeweza kusema wanataka kufanyiwa, lakini si hivyo.
5. Waislamu kutokusoma: Sioni mantiki ya kuingiza suala la kusoma katika hoja hii. Nadhani inataka kutumika kama kisingizio kukwepa au kupindisha hoja ya msingi. Siku zijazo nitaanzisha thread tujadili mnaposema waislamu hawakusoma maana yake hasa ni ipi, na hivi kweli sentesi hiyo ina nguvu leo kama ilivyokuwa mwaka 1961?
6. Totofautishe usomi na kufundishwa: Kuna tofauti kati ya msomi (intellectual) na aliyefundishwa (trainee/trained person). Trained person hufanya na kuamua mambo kwa kufuata vile alivyo fundishwa, wakati intellectual hufanya na kuamua mambo kwa kufuata real and genuine facts hata kama zitapingana na dini, kabila, kundi, mkoa au kanda anayotoka, n.k. Nikitazama michango katika hoja hii naona wachangiaji wengi wanafanana zaidi na trained person kuliko intelectuals, ingawa wanawalaumu waislamu kuwa hawakusoma. Nadhani kusoma kwenye manufaa ni kuwa intellectuals na sio trainees.
Mtanzania Makini
Follow Us Here