Ushauri wa bure kwa BAKWATA na waislamu wenzangu wote kuhusu kususia SENSA
Nimepata tabu kwa muda ili kujaribu kufikiri na kupata sababu na jibu la maana la waislamu kususia hesabu ya watu nchini yaani sensa. Bado sijaelewa idadi ya watu, ama hesabu ya watu inahusiana vipi na imani za kidini wakati wanaohesabiwa ni watanzania wenye dini mbali mbali walionea na kusambaa nchini kwetu.
Je! Serikali ikichakachua idadi kamili ya watu wa dini fulani na kutoa idadi tofati kutakuwa na faida gani? Je! idadi ndogo ya waumini inasababisha kupungua imani ya watu kwa dini yao? Ukiwa na imani unaweza kuwa na dini yako peke yako, au ya watu sita tu na bado ikawa dini bila ya halaiki ya watu.
Au lengo letu ni kushindana idadi na watu wa imani nyingine? Hiyo itakuwa na faida gani kwetu.
Ikiwa ni hivyo, ushauri wangu ni huu.
Tuiache sensa ya serikali ifanye kazi yake, tukubali kuhesabiwa. Baada ya hapo tufanye sensa yetu ya waislamu tu. Nina hakika kila mtaa haukosi kuwa na shekhe ambaye anaweza kupita na kujua idadi ya waislamu walio katika mtaa wake, ndani ya kipindi kifupi tunaweza kupata majibu kwa kupitia sensa yetu ya uhakika. Maustadhi na mashekhe wetu mbona mengi mnayapigania na kufanikiwa? Je, sensa maalumu kwa ajili ya waislamu tu, itawashinda?
Hakuna sababu ya kutaka kujua idadi yetu kwa kubebwa na sensa ya serikali wakati uwezo tunao watu wakihamasishwa. Huo ndio ushauri wangu, isije ikawa tunafanya mambo kinyume na demokrasia na matakwa ya jamii inayotuzunguuka.
Re: Ushauri wa bure kwa BAKWATA na waislamu wenzangu wote kuhusu kususia SENSA
By Free World
Juma Salaam,
Kwanza sina shaka juu ya uislamun wako kama wengine humu JF, wanaojifanya waislamu kumbe ni makafiri wazuri.
Kimsingi hata mimi binafsi siathiriki na sensa na matokeo yake.
lakini unapaswa kuangalia mbali zaidi ya hoja zako hapo juu. Wakristo wanataka Waislamu wafikiri kama wewe ulivyofanya, kwa hiyo itawahakikishia dhulma bila bughdha
Madai ya msingi ya Waislamu ni kuwa Wakristo kwa kuwa ndio wengi serikalini na kwenye ufanyaji maamuzi wanatumia mwanya wa kutokuwa na takwimu sahihi kuhalalisha wao kuwa wengi kila mahali.
kama idadi ya watu wa dini fulani sio issue, kwa nini izungumzwe ile ya makadirio?
Kama kuna haja ya kuwa na makadirio (estimates) kwanini kusiwe na real data?
Pia kuna confusion inayotokana na records za nyuma, mwanzo waislamu walikuwa majority TZ, leo kwa nini wawe 35%?
Mwisho KWA NINI TUNAOGOPA KUPIMWA? wakati tunasisitiza watu wakapimwe ukimwi! Hapa tunaogopa ukweli?
Kuna siri ndani ya Pazia.
Kama wao wangedai hilo saa hizi limeshaingizwa katika fomu zenu.
Re: Ushauri wa bure kwa BAKWATA na waislamu wenzangu wote kuhusu kususia SENSA
Kuna watu wa akili fupi wanadhani hii nchi ina dini mbili tu kiasi kila leo wapo majukwaani wanadai uwakilishi wa dini yao kwenye kila nukta. Hivi mmeshawahi kujiuliza kuna dini na madhehebu mangapi ambayo hayafungamani kiasi serikali iingize kwenye sensa viongozi wao, hiyo itakuwa tume au nchi nzima?
Kama kuna anataka kujua idadi ya waumini wa dini yake hiyo sensa afanye mwenyewe nyumbani kwake. Serikali haina haja ya kutujua kwa dini na ndio maana haijafanya utaratibu huo. Sasa hawa wanaopenda kuleta usumbufu wa kitoto sijui wanataka lipi kwenye sensa.
Hivi kuna mwanaume wa kukataa kutoa taarifa kweli ikiwa kila mtu anafuatwa peke yake?
Re: Ushauri wa bure kwa BAKWATA na waislamu wenzangu wote kuhusu kususia SENSA
Mmehangaika sana jamani kujibishana na watu wa hii Dini, moslems will not change till the second coming of jesus! unajua kwanini? lililoandikwa katika Biblia ni lazima litimie. Baba wa uslam ni ish-mael yule mtoto wa Ibrahimu aliyemzaa na mjakazi wake mmisri, HAJIRI. [FONT=Georgia]Mungu liandika hivi: KATIKA MWANZO 16:12[/FONT]
He will be a wild donkey of a man; his hand will be against everyone and everyone's hand against him, and he will live in hostility toward all his brothers." (QUOTED FROM ENGLISH STANDARD VERSION)
KWA BIBLIA ZA KISWAHILI ANASEMA: naye atakuwa kama punda mwitu kati ya watU, Mkono wake utakuwa juu ya watu wote na mkono wa watu wote utakuwa juu yake, naye atakaa mbele yao ndugu zake wote
sasa katika kiswahili Maana imepotea angalia neno lenye rangi nyekundu kwenye kingreza "hostility" kwa tafsiri nzuri ni 1. a hostile (very unfriendly) disposition 2. a state of deep-seated ill-will
3. the feeling of a hostile person 4. violent action that is hostile and usually unprovoked
Sasa kwa tafsri hizo unaweza usiwalaumu hawa waislam, neno la mungu ni lazima litimie, angalia mataifa ya kiislam yanavyoishi na mataifa wanayoyaita yana wakristo, matendo wayafanyayo duniani. NK
NISIWACHOSHE REFERENCE ZA BIBLE NI NYINGI WAACHENI WAISLAM WANAITIMIZA MISTARI YA BIBLIA
Re: Ushauri wa bure kwa BAKWATA na waislamu wenzangu wote kuhusu kususia SENSA
By Kikwebo
Mkuu umeona enhe! hapa Wassira ni bonge la kiongozi mbele ya Wahafidhina wa CDM! ama kweli ni vigumu kutofautisha kati ya CDM, kanisa na CCM ! (pole Ritz).
Kikwebo.
Kuhesabiwa hiyo haiusiani na wassira tunchotaka tupate data kwaajili ya maendeleo zitatusaidia 2015 tukichukua nchi
Re: Ushauri wa bure kwa BAKWATA na waislamu wenzangu wote kuhusu kususia SENSA
By Dumelang
Sasa kwa tafsri hizo unaweza usiwalaumu hawa waislam, neno la mungu ni lazima litimie, angalia mataifa ya kiislam yanavyoishi na mataifa wanayoyaita yana wakristo, matendo wayafanyayo duniani.
Machafuko karibu yote yanayotokea kwenye nchi za kiislam yanasababishwa na nchi unazoziita za kikristo sasa wewe niambie huyo bwana aliye hostile hapo anayetajwa ni nani kati ya USA ,UK, Iran au Iraq?
Mkuu umeona enhe! hapa Wassira ni bonge la kiongozi mbele ya Wahafidhina wa CDM! ama kweli ni vigumu kutofautisha kati ya CDM, kanisa na CCM ! (pole Ritz).
Kikwebo.
Pole unanipa tena mie badala uwape Chadema jinsi CCM wanavyocheza na akili zao.
Re: Ushauri wa bure kwa BAKWATA na waislamu wenzangu wote kuhusu kususia SENSA
By ritz
Huu ushauri wako wa bure bora ukaenao utakusaidia mbeleni.
Hujajibu hoja zake unaongea kiswahili swahili tu kama waanzilishi wa mgomo wenyewe. Issue ni kwa faida ya nani na ili iwe nini. Wengi wenu akili zenu ndio kama hizi ulizotumia kujibu hoja hii kipuuzi na bado mnataka uwiano sawa serikalini.
Tafakari jipe majibu, kazi hapewi mtu ili kubalansisha dini kwamba 10 huku na 10 huku, kazi hutolewa kwa vigezo vya elimu na uwezo wa kuifanya. Sasa kwa mfano Waislamu wakiwa milioni 38 kati ya 45 ndio kigezo kwamba wawe wengi kwenye kazi kwa kuwa wao ni wengi mtaani?
Kama waumini wote
wangekuwa wanakwenda kuswali msikitini na wakristo wote kwenda
makanisani sensa ingekuwa nyepesi ..... naona kazi ya kwanza ya dini ni
kuwarejesha waislamu na wakristo wote kwenda nyumba za ibada ili wapate
sensa yao. wamrudie Mungu hesabu itakuwa rahisi wala hakutakuwa na haja
ya kuisumbua serikali ambayo idadi ya waumini wa dini haina umuhimu
katika kupanga maendeleo ya watu kama vile barabara, umeme,
maji.
Re: Ushauri wa bure kwa BAKWATA na waislamu wenzangu wote kuhusu kususia SENSA
By Kabembe
Taabu ya hawa wenzetu hata ukiwapa uongozi wa nchi,yaani Rais,makamu,waziri mkuu na mawaziri wote,makatibu wote,wakurugenzi wa idara wote,wakuu wa mikoa,wilaya wote,wakurugenzi wa mashirika ya umma wote na kadha wa kadha bado hawa jamaa zetu wataendelea kulalamika na kudai mfumo kristo unatawala,frankly is very hard to deal with these characters,they are funny and useless!
Mhh nina wasiwasi na uwezo wako wa kuangalia mambo na kupata uhalisia wake. Tatizo la waislamu si kutaka kupewa, Urais, au ukuu wa wilaya kama unavyosema, tatizo ni mfumo gani unamuweka mtu fulani mahali gani. Je ni mfumo wa haki??? Hili ndilo tatizo. Angalia kilichotokea juzijuzi tu baraza la mtihani, na aina ya majibu tuliyopata baada ya waislam kulalamikia matokeo ya mtihani, na baadaye majibu yaliyofuatia!!! Hii ni katika somo moja tu, je nani anajua nini kinaendelea katika masomo mengine???. Sioni kwa nini Serikali ikatae kuweka kipengele cha kumtambua mtu dini yake??
Re: Ushauri wa bure kwa BAKWATA na waislamu wenzangu wote kuhusu kususia SENSA
Walau basi Makanisa yanaweka kumbukumbu za waumini wao kwa daftari rahisi lenye majina ya waumini wanaoabudu kwenye kila nyumba ya ibada jumapili bila kuhitaji sensa au utaratibu wa kiserikali.
Waislamu hilo hamliwezi?Tangazeni tenda ya kuhitaji huduma za ushauri namna ya kujuanidadi yenu,tutawapa dozi ya ushauri mtupatie hiyo fedha
Last edited by KOMBESANA; 15th June 2012 at 17:24.
Reason: typo
Re: Ushauri wa bure kwa BAKWATA na waislamu wenzangu wote kuhusu kususia SENSA
By Sideeq
Sawa! lakini itambulike officially na Serikali.
Na kama serikali inaweza kugharimia ufanyaji wa sensa , vilevile hawa Masheikh watakaofanya hii kazi wagharimiwe na Serikali.
Nyie mbona mmezidi vya dezo sana?? kwanini msitumie pesa zenu kufanya sensa zenu..kwani wakristo wanapohesabiana huko makanisani hiyo kazi inagharamiwa na serikali?? mambo ya ajabu sana haya..hamna source of income??? taabu tupu..mahakama ya kadhi mnataka serikali ii gharamie , yaani belivers na non belivers wabebe mizigo ambayo sio yao..nani anataka pesa zake zikafanye kazi isiyo mhusu?? mahakama zenu sisi tuzigharamie...ajabu hii
Re: Ushauri wa bure kwa BAKWATA na waislamu wenzangu wote kuhusu kususia SENSA
By Maundumula
Machafuko karibu yote yanayotokea kwenye nchi za kiislam yanasababishwa na nchi unazoziita za kikristo sasa wewe niambie huyo bwana aliye hostile hapo anayetajwa ni nani kati ya USA ,UK, Iran au Iraq?
Naona hukusoma vizuri hapa: his hand will be against everyone and everyone's hand against him, and he will live in hostility toward all his brothers.
Ufafanuzi wa sentensi: mchokozi ni anaye inua mkono wake dhidi ya meingine "his hand, against everypone(Waislam au mataifa ya kiislam dhidi ya wenzao) sawa? ndipo sentesi inasema and everyone's hand against himyaani kwa sababu ya uchokozi wake kila mtu atainua mkono dhidi yake (kujibu mapigo/uchokozi) wanaojibu ndio hao uliowataja akina USA, UK, Israel n.k au siyo? ndipo hapo chuki inaanza. UMEELEWA SASA
Re: Ushauri wa bure kwa BAKWATA na waislamu wenzangu wote kuhusu kususia SENSA
Nakushukuru sana ndugu yangu kwa kuangalia mambo practically. Waache kulalama. Maneno hayasaidii kitu. Kwenye somo la Mantiki (Logic) tunafundishwa kitu kinachoitwa specific difference (yaani kile kinachotofautisha kundi au kitu fulani na kingine). Kwa binadamu specific difference yetu ni rationality (uwezo wa kufanya mang'amuzi). Rationality inatutofautisha na wanyama. Ndugu zangu Waislamu muwe mnapima mambo kabla ya kuyaweka hadharani.
Re: Ushauri wa bure kwa BAKWATA na waislamu wenzangu wote kuhusu kususia SENSA
By Precise pangolin
Kuhesabiwa hiyo haiusiani na wassira tunchotaka tupate data kwaajili ya maendeleo zitatusaidia 2015 tukichukua nchi
Ebwana enhe! kumbe saa nyingine Wassira ana point enhe! ambazo mkiingia madarakani 2015 zitakusaidieni..duuh! si mchezo. Labda nikusaidie kitu kimoja..
ushauri wangu nyie CDM kubalini hiki kipengele ili mkiingia madarakani 2015 mruhusu MoU na Waislamu..kwa kuwa serikali isingekubali kuingia MoU ile ilihali hakuna umuhimu wakujua watu kwa dini zao.?
Kipengele hiki for your information ni muhimu na serikali inatumia idadi ya wakristo kwa mlango wa nyuma kuwabeba. Hivi kama Wakrosto wangekuwa ni asilimia 2% unadhani wangekubali kuingia nao ile MoU!!! akili zao nikuwa wako wengi ndio maana wakawakubalia kuwapa mabilioni ya shilingi kila mwezi.
Nilipo RED kunapelekea kutilia mashaka Uislam wako. Je unajuwa shahe ni nani? Inawezekana kweli kuwe na shahe kila mtaa huko Tanzania ?
Labda nikuulize.
Tunajuwa fika lengo kuu la sensa yenu ni kuhisabu watu.
Kwanini sasa mnaweka kipengele cha jinsia na umri wakti lengo kuu ni kujua idadi ya watu?
Kumbuka kuwa wanawake na wanaume wote ni watu na vile vile watoto, vijana na wazee wote ni watu.
Sasa kwanini msijumuishe na dini pia? je kuna gharama gani kama mtakiweka kipengele hicho?
Acheni kubaniana wenyee kwa wenyewe na kuoneana husda
Kaka baruu! Umeibukia njozini? Au ndevu zimekuzidi uzito mpaka unashindwa kuandika. Sijasema 'shahe' nimesema 'shekhe' huku kwetu ni mtu aliyebobea katika elimu ya madrasa na dini kwa ujumla. Mitaa yetu huku ni mikubwa kiasi inaweza hata kudai uhuru. Sio kama huko kwenu Zenji. Kwa taarifa yako huku bara kila mtaa haukosi shekhe.
Re: Ushauri wa bure kwa BAKWATA na waislamu wenzangu wote kuhusu kususia SENSA
By mkaliwakitaa
Nyie mbona mmezidi vya dezo sana?? kwanini msitumie pesa zenu kufanya sensa zenu..kwani wakristo wanapohesabiana huko makanisani hiyo kazi inagharamiwa na serikali?? mambo ya ajabu sana haya..hamna source of income??? taabu tupu..mahakama ya kadhi mnataka serikali ii gharamie , yaani belivers na non belivers wabebe mizigo ambayo sio yao..nani anataka pesa zake zikafanye kazi isiyo mhusu?? mahakama zenu sisi tuzigharamie...ajabu hii
Umeielewa context ya niliyoyasema?
By Barubaru
Tunajuwa fika lengo kuu la sensa yenu ni kuhisabu watu.
Kwanini sasa mnaweka kipengele cha jinsia na umri wakti lengo kuu ni kujua idadi ya watu?
Kumbuka kuwa wanawake na wanaume wote ni watu na vile vile watoto, vijana na wazee wote ni watu.
Follow Us Here