Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mbunge Zambi ashitakiwa mahakamani

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 34
    1. #1
      dm2000inter's Avatar
      Member Array
      Join Date : 27th October 2010
      Posts : 10
      Rep Power : 437
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default Mbunge Zambi ashitakiwa mahakamani

      Mbunge wa CCM Jimbo la Mbozi Mashariki, Mheshimiwa Godfrey Weston Zambi Jumatano wiki hii mjini Moshi amefunguliwa kesi ya madai na kampuni ya Lima Limited akidaiwa fidia ya shilingi 2.4 bilioni kwa tuhuma za kutoa matamshi ya kuikashifu kampuni hiyo.

      Katika gazeti la Mwanahalisi la Juni 13-19,2012, Mheshimiwa Zambi anadaiwa kutamka" Lima imekuwa ikiwashawishi wakulima kuuza kahawa mbivu kwa bei ndogo sana".

      Kampuni hiyo inamtuhumu Zambi kuanzisha kampeni mbaya dhidi ya kampuni hiyo ili kuondoa ushindani wa soko ili kuvipa fursa vikundi vya wakulima ambavyo Zambi ana maslahi navyo visipate ushindani wowote katika soko la Kahawa. K

      esi hiyo namba CC 7/2012 imefunguliwa na mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi,Eric Ng'maryo ambaye pia ni Advocate Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa.
      SpK and Kamkuki like this.

    2. RukaaJuu Final

    3. #2
      Mzee wa fund's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th October 2010
      Posts : 496
      Rep Power : 534
      Likes Received
      78
      Likes Given
      2

      Default Re: Mbunge Zambi ashitakiwa mahakamani

      Mfamaji huyo.mwache atapetape.

    4. #3
      Njoka Ereguu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th April 2012
      Posts : 503
      Rep Power : 459
      Likes Received
      167
      Likes Given
      30

      Default Re: Mbunge Zambi ashitakiwa mahakamani

      Mbona sioni tatizo la hiyo kauli, kama kweli wanafanya haki na siyo dhuluma kwa nini waogope? hapo lazima kuna ulaghai wanafanya na hivyo wameona wameumbuliwa.

      Halafu siku hizi bana Tanzania hizi kesi za kupuuzi zimezidi eti kesi 2.4 bill, yaani mtu anajitamkia tu kiasi cha fedha anachotaka. Hii laana imetoka wapi? Lengo nini kama siyo kutaka kuwanyamazisha watu wasikemee maovu kwa kuogopa kesi za billions?

      Ee Mungu iokowe nchi yangu niipendayo ya Tanzania, na mikono ya wanyanganyi hawa wasio hata na huruma wala haya.
      SpK and MAKAH like this.

    5. #4
      kanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th January 2011
      Posts : 737
      Rep Power : 571
      Likes Received
      292
      Likes Given
      410

      Default Re: Mbunge Zambi ashitakiwa mahakamani

      Ukisoma ile makala ya Mwanahalisi between line juu ya mtazamo wa Zambi utaona wazi kuwa Zambi yupo sahihi zaidi ya 100% hata kama huyu Eric anataka kutumia mahakama kumziba mdomo.Board ya kahawa wajumbe wake JK na Waziri wake wa Kilimo wamechemka kwenye uteuzi wa Board Members.Total Conflicts of interest between board members.
      SpK likes this.

    6. #5
      Sakane's Avatar
      Member Array
      Join Date : 4th June 2011
      Posts : 14
      Rep Power : 405
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default Re: Mbunge Zambi ashitakiwa mahakamani

      Tatizo ni Zambi ama alieteua Mwenyekiti na wajumbe wa Bodi, halafu tatizo lipo wapi kwakuwa sasa ni soko huria

    7. Miaka 50

    8. #6
      Ndyali's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th November 2011
      Posts : 549
      Rep Power : 488
      Likes Received
      140
      Likes Given
      3

      Default

      Quote By kanga
      Ukisoma ile makala ya Mwanahalisi between line juu ya mtazamo wa Zambi utaona wazi kuwa Zambi yupo sahihi zaidi ya 100% hata kama huyu Eric anataka kutumia mahakama kumziba mdomo.Board ya kahawa wajumbe wake JK na Waziri wake wa Kilimo wamechemka kwenye uteuzi wa Board Members.Total Conflicts of interest between board members.
      Mkuu Kanga, sakata la Zambi na kampuni ya Lima ni la mbunge Zambi kuwa na fikra za ki-ccm yaani kuwanyonya wanyonge kwa mrija usio na huruma. Hapa Mbozi kampuni la Lima linalipa bei nzuri kuliko vikundi vya wajanja wa kiswahili, lakini kwa mashart ya kuiboresha kahawa katika vinu vyao vinavyo process kahawa mbivu. Mwanya huu unampa jeuri Zambi kutengeneza uongo mwingi dhidi ya Lima. Kiujumla wakulima wa kahawa Mbozi wanapenda kuuza kahawa yao kwa Lima, lakini Zambi kutumia ubunge wake anataka kuidhinisha wakulima wawe wananyonywa.

    9. #7
      Walikughu's Avatar
      Member Array
      Join Date : 7th December 2011
      Posts : 91
      Rep Power : 395
      Likes Received
      16
      Likes Given
      26

      Default Re: Mbunge Zambi ashitakiwa mahakamani

      Mimi Sija soma hilo Gazeti lakini ukweli ni kwamba Kampuni ya Lima Kuendelea kununua kahawa Mbichi Yaani "Cherry" huu ni wizi, kwa sababu wananunua kwa Bei ndogo sana alafu hawana mpango wowote wa kufufua zao la kahawa zaidi ya kuwaibia wana mbozi Mimi naungana na Mh. Zambi katika hili la kuwapiga vita walanguzi wa zao la kahawa katika Wilaya yetu ya Mbozi Na kwingineko.
      SpK and MAKAH like this.

    10. #8
      chuwaalbert's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th September 2010
      Posts : 295
      Rep Power : 500
      Likes Received
      52
      Likes Given
      129

      Default Re: Mbunge Zambi ashitakiwa mahakamani

      Imperialism....The Highest stage of Capitalism! Ng'maryo, Zambi wote sawa!
      SpK likes this.

    11. #9
      Ndyali's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th November 2011
      Posts : 549
      Rep Power : 488
      Likes Received
      140
      Likes Given
      3

      Default

      Quote By Sakane
      Tatizo ni Zambi ama alieteua Mwenyekiti na wajumbe wa Bodi, halafu tatizo lipo wapi kwakuwa sasa ni soko huria
      Mkuu, tatizo ni mbunge Zambi anataka kuwafadhili wanunuzi wa kizalendo ambao hawana uzalendo wanotaka kuwapunja wakulima kwa kuwapa bei ndogo. Isitoshe jamaa hawa ndiyo walio kuwa ma-cmpainer wa Zambi wakati wa uchaguzi wa ubunge, lakini kura hazikutosha ilibidi wachachue kumpa ubunge Zambi.

    12. #10
      mzee wa njaa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th June 2011
      Posts : 1,340
      Rep Power : 670
      Likes Received
      194
      Likes Given
      107

      Default Re: Mbunge Zambi ashitakiwa mahakamani

      Watu wanataka maendeleo ya nchi wengine wameona mahakamani ni sehemu inayofaa. Then mtasema Mungu anawalaani au mmejitakia wenyewe?

      Tushachoka na propaganda za uswazi kama hizi.

    13. #11
      Ndyali's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th November 2011
      Posts : 549
      Rep Power : 488
      Likes Received
      140
      Likes Given
      3

      Default

      Quote By Walikughu
      Mimi Sija soma hilo Gazeti lakini ukweli ni kwamba Kampuni ya Lima Kuendelea kununuakahawa Mbichi Yaani "Cherry" huu ni wizi, kwa sababu wananunua kwa Bei ndogo sana alafu hawana mpangowowote wa kufufua zao la kahawa zaidi ya kuwaibia wana mbozi Mimi naungana na Mh. Zambi katika hili la kuwapiga vita walanguzi wa zao la kahawa katika Wilaya yetu ya Mbozi Na kwingineko.
      Mkuu usitutukane watu wa Mbozi kana kwamba sisi tutachagua kumwuzia kahawa yetu Lima anayetupunja. Wewe na Zambi wako tuacheni soko lituamlie wapi tuuze kahawa yetu kuliko kutulazimisha tuwauzie waswahili wanaochukua kahawa yetu kwa kutukopa kutulipa inakuwa taabu.

    14. #12
      Walikughu's Avatar
      Member Array
      Join Date : 7th December 2011
      Posts : 91
      Rep Power : 395
      Likes Received
      16
      Likes Given
      26

      Default Re: Mbunge Zambi ashitakiwa mahakamani

      Quote By Ndyali
      Mkuu usitutukane watu wa Mbozi kana kwamba sisi tutachagua kumwuzia kahawa yetu Lima anayetupunja. Wewe na Zambi wako tuacheni soko lituamlie wapi tuuze kahawa yetu kuliko kutulazimisha tuwauzie waswahili wanaochukua kahawa yetu kwa kutukopa kutulipa inakuwa taabu.
      Mimi sijawatukana ila wewe ndiye unaye taka matusi, Ngoja nikupe shule kidogo kahawa ya cherry unauza kwa lima kiasi cha sh.200 kwa kilo ambayo ukichukua kilo 5 za cherry ni sawa na kilo 1 ya kahawa kavu yani Parchments, hapo either mnakuwa mmeshaachana na lima kwa sh.1000 tu.

      Ambayo unakuwa umelipwa yeye akienda kuuza sokoni wastani wa kili moja tena parchment ni sawa na $ 3.5 kwa kilo hilo ni soko la Moshi bado hajachakachua ule mtindo wa kujinnulia kahawa yake na kuipeleka nje ya nchi, cha msingi ni kuwa hata kama soko unataka liwe forced na demand and supply lazima kuwa na sheria ambazo zitasimamiwa na serikali maana yake ni kwamba ukiwaacha hawa wafanyabiashara peke yao watakaa na kupanga bei.

      Mwisho wa siku atakaye umia ni Mkulima, kuhusu hivyo vikundi vya kahawa ni sawa baadhi ni kero lakini vingine vinafanya vizuri na naomba usije ukasema mimi na Mh. Zambi tunakula pamoja kama unavyo taka kujipambanua hapo kuna wizi labda wewe binafsi kuwe na maslahi unayoyapata kupitia lima maana tunawafahamu sana kwa uchakachuaji wenu wa kahawa kwa kumwibia mkulima.
      MAKAH likes this.

    15. FJM
      #13
      FJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 7,179
      Rep Power : 2569
      Likes Received
      5331
      Likes Given
      4587

      Default Re: Mbunge Zambi ashitakiwa mahakamani

      Nimesoma articles mbili kuhusiana na hii saga. Mwanahilisi na Mwananchi. Yangu mimi ni maswali mawili tu:

      1. Kwa nini Lima wananunua kahawa mbichi (cherry)?

      2. Uteuzi wa Board unazingatia nini?

    16. #14
      MAMA POROJO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2007
      Posts : 4,858
      Rep Power : 1844
      Likes Received
      592
      Likes Given
      413

      Default Re: Mbunge Zambi ashitakiwa mahakamani

      Wacha mahakama itatupatia majibu

    17. #15
      Walikughu's Avatar
      Member Array
      Join Date : 7th December 2011
      Posts : 91
      Rep Power : 395
      Likes Received
      16
      Likes Given
      26

      Default Re: Mbunge Zambi ashitakiwa mahakamani

      Quote By FJM
      Nimesoma articles mbili kuhusiana na hii saga. Mwanahilisi na Mwananchi. Yangu mimi ni maswali mawili tu:

      1. Kwa nini Lima wananunua kahawa mbichi (cherry)?

      2. Uteuzi wa Board unazingatia nini?
      Ananunua kahawa mbichi ili ajifaidishe, ananunua kwa bei ndogo na kisha kuiuza kwa bei kubwa.

      Kuhusu Uteuzi wa Board Nadhani kuna vigezo ambavyo vimewekwa na wizara ya kilimo ili kuwapata hao wakurungezi bodi ya kahawa na hizo nafasi hasa mkurungenzi mtendaji huwa inatangazwa na wenye sifa wanaomba.

    18. #16
      matengo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 1st June 2011
      Posts : 24
      Rep Power : 408
      Likes Received
      1
      Likes Given
      2

      Default Re: Mbunge Zambi ashitakiwa mahakamani

      Hatua iliyochukuliwa na Lima naipongeza ili iwe fundisho kwa yeyote atakayetumika kwa kulipwa vijisenti au kupigania wadhamini wake wa uchaguzi. Mheshimiwa Zambi amejidhihirisha wazi kuwa ana maslahi binafsi tena pengine huu ni ushahidi wa maneno ya mh. Kafulila mbunge wa Kasulu kuwa anapenda rushwa(Soma Mwanahalisi ya tarehe 13/06/2012).

      Biashara ya kahawa mbichi inafanyika Tanzania nzima na hakuna mgogoro, hata Mbozi biashara hiyo imekuwa ikifanyika tangu mwaka 2006 na hatukuwahi kumsikia Mh. Zambi akilalamika. Matatizo yalianza mwaka 2008 baada ya kuingia Mkurugenzi Mkuu mpya wa Bodi ya kahwa Bw. A. Kumburu. Huyu mkurugenzi ndiye aliyefuta leseni za Red Cherry kwa maagizo toka maboss wake wa zamani Technoserve(Bado ni maboss wake wa siri). Alifanya hivi kinyume cha taratibu kwa vile maamuzi ya kuruhusu kuwepo leseni ya Red Cherry yalitoka baada ya vikao kati ya Wizara mbili za kilimo na uwekezaji pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri Mbozi na Bodi ya Kahawa. Hivyo ili kufuta leseni ilibidi apate kwanza kibali cha waziri mwenye dhamana.

      Baadae yakaendelea malalamiko toka kampuni ya Lima kwani waliwekeza kwa mwaliko wa serikali ili kuboresha zao la kahawa lipate bei nzuri katika soko la dunia. Serikali iliona kuna sababu za msingi wakaruhusu leseni itolewe.

      Kuhusu kuandaa kanuni mpya uliandaliwa mchakato wa kuhusisha wadau ambapo mwezi wa sita 2011 kilifanyika kikao cha baadhi ya wadau chini ya uenyekiyti wa Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya kahawa. Kikao hiki kilipitisha leseni ya kununua kahawa mbivu itolewe. Mwenyekiti alikubali kwa vile wajumbe walimzidi tena kibaya zaidi katika kikao hicho mabosi wake wa kwenye mabano wakishuhudia na mh. Zambi naye pia alikuwapo.

      Baada ya njama za Bw. Kumburu kugonga mwanga ndipo akaanza mkakati wa kuwatumia akina Mh. Zambi ambaye kwenye hicho kikao wala hakuonekana kupinga biashara ya Red Cherry. Hatujui alimshawishi kwa njia hipi labda ni pamoja na kutumia njia alizotaja mh. Kafulila. Bw. Kumburu kinyume cha maamuzi ya wadau aliandika barua wizarani kupinga biashara ya Red Cherry.

      Sasa baada ya kuona Waziri wa Kilimo amejua ukweli na kuruhusu leseni ndipo mh. Zambi akaendesha kampeini aondolewe wizara ya Kilimo na hasa akitegemea atamwokoa Kumburu ambaye anaendesha Bodi ya Kahawa bila ya kufuata sheria. Waziri alipobadilishwa akategemea sasa Bodi mpya itakuwa kama bodi ya zamani imfumbie macho Adolf Kumburu kinyume chake Bodi mpya ikaonyesha ina nia ya kumaliza matatizo ndani ya sekta ndogo ya kahawa.

      Mkutano mkuu wa wadau wa kahawa Morogoro uliazimia itolewe lesni ya kununua kahawa mbivu ili mkulima mwenyewe ndiye aamue kama auze au aache. Huu pia ndio ulikuwa msimamo wa waziri mkuu alipoenda Mbeya.

      Sasa unyonyaji anaosema Mh. Zambi uko wapi? Au anataka kusema Lima itakuwa inashika bunduki kuwalazimisha wakulima wapeleke kahawa kwenye vinu vyao. Kama Zambi anaona kuuza kahawa mbivu ni kuwanyonya wakulima kwa nini asifanye kazi kuwaelimisha wasimuuzie Lima ili Lima ikiona inakosa kahawa iache biashara hiyo yenyewe.

      Mh. Zambi anajua akifanya hivyo kwa kuwaahidi wakulima bei ya juu mwisho wake watakapouza wakakuta bei imeporomoka watamuua hivyo hawezi kufanya hilo.

      Mwenyekiti wa Bodi yuko sahihi kwa kutamka kuwa mwenye uhuru wa kuchagua ni mkulima. Jukumu la kumwelimisha mwenendo wa soko ili mkulima afanye maamuzi sahihi ndilo linatakiwa kutekelezwa na serikali na wala siyo kuzuia baadhi ya masoko.

      Sasa Mh. Zambi aliyeenda Morogoro na wenzake kuhakikisha wanalazimisha kuzuia biashara ya kahawa mbivu ambayo yeye anaipinga Mbozi ili izuiliwe nchi nzima( Kwingine kote inafanyika) kugonga mwamba akaja na ajenda mpya ya kumpinga mwenyekiti mpya wa Bodi na wajumbe wake.

      Swali la kujiuliza alipata je ubunge mtu asiyekubali maoni ya wengi. Au anaogopa kutema pesa alizoahidiwa na wafidhili wake akiwemo Adolph ambaye anamtumia ili Bodi yote ingolewe yeye aendelee kuedesha shirika la umma kama mali yake.

      Huku ni kujidanganya kwa vile matatizo ya Kumburu hayawezi kuisha kwa kufukuza viongozi wake, kinyume chake matatizo ndani ya sekta ya kahawa yanaweza kuisha kama Kumburu chanzo ch
      muchetz likes this.

    19. #17
      Belik's Avatar
      Member Array
      Join Date : 15th June 2012
      Posts : 10
      Rep Power : 352
      Likes Received
      3
      Likes Given
      0

      Default Re: Mbunge Zambi ashitakiwa mahakamani

      naomba kusema kuwa naenda kutafuta data halisia ila haya yote yanasababishwa na Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Kahawa Bw Adolph Kumburu akiwasaidia wazungu kummaliza mkulima waziri wa kilimo chukua hatua haraka
      MAKAH likes this.

    20. #18
      OSOKONI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th October 2011
      Posts : 3,632
      Rep Power : 1110
      Likes Received
      1001
      Likes Given
      756

      Default Re: Mbunge Zambi ashitakiwa mahakamani

      Quote By Njoka Ereguu
      Mbona sioni tatizo la hiyo kauli, kama kweli wanafanya haki na siyo dhuluma kwa nini waogope? hapo lazima kuna ulaghai wanafanya na hivyo wameona wameumbuliwa.

      Halafu siku hizi bana Tanzania hizi kesi za kupuuzi zimezidi eti kesi 2.4 bill, yaani mtu anajitamkia tu kiasi cha fedha anachotaka. Hii laana imetoka wapi? Lengo nini kama siyo kutaka kuwanyamazisha watu wasikemee maovu kwa kuogopa kesi za billions?

      Ee Mungu iokowe nchi yangu niipendayo ya Tanzania, na mikono ya wanyanganyi hawa wasio hata na huruma wala haya.
      Wangekuwa wameogopa wasingefungua kesi! mahamani ndipo mahali sahihi pa kupata ukweli , utakuwa au huelewi katiba au unaidharau unaposema kesi za kipuuzi! kikatiba kila mtu anapohisi hajatendewa haki mahali pa kuipata haki hiyo ni mahakamani! Kama Zambi au hiyo kampuni ipo sahihi ni kazi ya mahakama kutafsiri na kama fidia iliyoombwa ni sahihi au sio pia ni wajibu wa mahakama kutafsiri! Inaonekana una maslahi binafsi na hii kesi ndio maana umeanza ku rule out kabla hata hearing haijaanza!!
      Narrow minded people discuss people,common minded people discuss events great minded people discuss ideas!!!

    21. #19
      Mwanaweja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th February 2011
      Posts : 3,481
      Rep Power : 1116
      Likes Received
      469
      Likes Given
      958

      Default Re: Mbunge Zambi ashitakiwa mahakamani

      ngoja tusubiri tuone nani mkweli mahakama tendeni haki

    22. #20
      jogi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th September 2010
      Posts : 4,023
      Rep Power : 1220
      Likes Received
      981
      Likes Given
      247

      Default Re: Mbunge Zambi ashitakiwa mahakamani

      Wakulimaaaaaaa, mnalima mkishavuna mnamuachia mnunuzi awapangie bei ya mazao yenu!!!! ndiyo maana ujinga umefungamanishwa nanyi.

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...