Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: CHADEMA wamefanya makubwa Tanzania: Tutarajie mapambazuko zaidi ya kifikra!

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 31
    1. #1
      Mbelwa Germano's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th May 2011
      Posts : 701
      Rep Power : 838
      Likes Received
      200
      Likes Given
      262

      Lightbulb CHADEMA wamefanya makubwa Tanzania: Tutarajie mapambazuko zaidi ya kifikra!

      Heshima Kwanza!

      "KAMA watu wawili wana fikra sawa na mtazamo sawa katika kila kitu cha kila jambo, basi, kuwa na uhakika kwamba ni mmojawao tu ndiye mwenye kufikiri”-Lyndon Baines Johnson (LBJ) raisi wa 36 wa Marekani (1963-1969)(Tafsiri).

      Ipo mitazamo na imani mbalimbali za kibaguzi iliyojaribu kujengwa dhidi ya vyama vya upinzani toka kuanza kwa mfumo wa vyama vyingi nchini inayolenga kudumaza changamoto za kifikra. Wapo watu wengi walioamini/wanaoamini upinzani ni njama ya kihaini, kashfa, mauaji, matusi, uzushi, au machafuko yanayoondoa dhana halisi ya kichocheo cha changamoto za demokrasia au maendeleo. Wapo baadhi ya viongozi wa kisiasa waliamini/wanaamini kwamba ukubwa wao au mali zao zinastahili kuwalinda hata wanapofanya maovu, hujifikiria wao zaidi na wanaowahusu kuliko manufaa ya taasisi au eneo waliomo na kujidanganya kwa kudhani siku zote watakuwa katika hali na nafasi waliyonayo.

      Wakati huu ambapo CHADEMA kinazidi kukubalika kwa kasi kuna baadhi ya watu wanahoji: Je hao CHADEMA wamefanya nini? Ni haki yao ya kimsingi kuhoji lakini naomba niwakumbushe: wamesahau kwamba leo hii kila jambo wanalofanya CCM wanatazama upande wa pili CHADEMA watasema nini?, wanaangalia mbele, wananchi kwa ujumla watasema nini? Nadhani sasa tuweke wigo mpana wa kifikra kutazama nini kazi ya upinzani katika kuleta ushindani wa kisiasa, kudumisha demokrasia, kuimarisha utawala bora na kujenga misingi imara zaidi ya maendeleo?

      Kwa nafasi waliyonayo CHADEMA kama chama kikubwa cha upinzani nchini wanastahili sifa na heshima kubwa. Kujenga na kuimarisha chama cha siasa si kazi lelemama, ni kazi inayohitaji UMAKINI, UVUMILIVU na UJASIRI. Kazi kubwa ya chama chochote cha upinzani ni kupima na kupinga ufanisi duni wa serikali ya chama kinachotawala na kujiweka katika nafasi ya kuaminiwa na wananchi ili kupewa ridhaa ya kuongoza na kuongeza ufanisi katika kusukuma gurudumu la maendeleo. Na haya ndio baadhi ya machache ambayo CHADEMA inafanya kama chama cha upinzani Tanzania.Tayari CHADEMA wamefanya na wanafanya, sasa tuwaulize wale wanaosema CHADEMA wamefanya nini walitaka wafanye nini?

      Bila ujasiri wa wabunge wachache wa CHADEMA kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 jamii ilikuwa imefunikwa kwenye wingu kubwa la kufungwa kufikra juu ya mustakabali wa nchi yao. Wamesahau kwamba bila CHADEMA leo hii usingesikia wimbo wa kujivua MAGAMBA ndani ya CCM.

      CHADEMA wamefungua minyororo ya kifikra na kuleta mapamazuko mapya. Ieleweke kwamba maendeleo yoyote ya kiuchumi na kijamii yanaanza na mapambazuko ya kifikra. "Hakuna jibu moja linaweza kutumika wakati wote na mahali pote","bila kutambua kwa utashi, kuelewa na kukubali juu ya matatizo yetu, hatuwezi kufanya maamuzi sahihi katika kudai haki za kimsingi katika jamii. Dhana ya kufikiri kwa bidii dio nyenzo muhimu ya kulinda uzalendo na uadilifu bila kuathiri utu wetu.
      “…kuchaguliwa kuunda utawala wa kuongoza nchi hakumaanishi kuchaguliwa kujitawalia mamlaka ya umma na kisha kutumia mamlaka hayo kuwakandamiza “waliokuchagua” kwa sababu tu ya kutetea maslahi binafsi badala ya maslahi ya umma”. (Katiba ya CHADEMA)

      Uwepo wa CHADEMA haulengi kugawa wananchi katika jamii yetu ili kudhoofisha maendeleo kama baadhi ya watanzania wenzetu wanavyotaka tuamini, bali ni njia ya kulinganisha sera, fikra na mitazamo katika kuchochea maendeleo.

      Think Twice...Act and react wise!
      Nara, STEIN, Mboko and 4 others like this.
      80 percent of problems are often due to 20 percent of the causes

    2. Miaka 50

    3. #2
      Babuu Rogger's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 16th November 2011
      Posts : 234
      Rep Power : 426
      Likes Received
      35
      Likes Given
      2

      Default Re: Chadema wamefanya makubwa tanzania: Tutarajie mapambazuko zaidi ya kifikra!

      List of SHAME kwa kweli tulikuwa hatuijui na hatukuwa tunajua nini kinaendelea kwa wakubwa wetu, CHADEMA KWELI M4C.
      Mbelwa Germano likes this.
      THERE AIN'T NO HIDING PLACE FROM THE FATHER OF CREATION.

    4. #3
      kitero's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st February 2012
      Location : Kaskazini
      Posts : 516
      Rep Power : 469
      Likes Received
      98
      Likes Given
      48

      Default Re: CHADEMA wamefanya makubwa Tanzania: Tutarajie mapambazuko zaidi ya kifikra!

      Siku zote sehemu ambayo hakuna upinzani/ushindani hakuna maendeleo au changamoto.Wanao wabeza upinzani ni kwajili ya maslahi yao binafsi.

      Kaskazini kulikuwa na maendeleo sababu walianza upinzani/kutofautiana na mwalimu tangia enzi za chama kimoja,Vikaja vyama vya upinzani kaskazini wakawa wakwanza kuanzisha vyama vya upinzani na ndiyo maana kukawa na maendeleo, mtu akichaguliwa ni lazima afanye maendeleo ktk jimbo lake sababu alijua wazi asipofanya kitu hawezi chaguliwa tena, ila kule kwa wenzangu na mie mtu alikuwa hajishughulishi sababu alijua akisha pata ni mpaka yeye amue kuachia ngazi na si kuwajibishwa na wanachi/upinzani na ndiyo maana mpaka leo kusini inaendelea kuwa nyuma kimaendelea na kuwa kambi ya wale wale.

      Wakidanganywa ya kuwa mkiwachagua CHADEMAupinzani watawagawa ki kanda na kidini,je mbona hao ambao hawajawagawa kidini na kikanda wamewagawa kielimu kiafya na kimaendele hawajawakataa. Kusini tafakari chukua hatua.Kusini nako ni sehemu ya tanzania tunataka upinzani na maendeleo viwepo.

    5. #4
      kanewi's Avatar
      Member Array
      Join Date : 12th June 2012
      Posts : 52
      Rep Power : 360
      Likes Received
      3
      Likes Given
      0

      Default Re: CHADEMA wamefanya makubwa Tanzania: Tutarajie mapambazuko zaidi ya kifikra!

      naona huu ujumbe ausome pia mwin'gulu nchemba.
      Mbelwa Germano likes this.

    6. #5
      mchaichai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th November 2011
      Posts : 381
      Rep Power : 457
      Likes Received
      33
      Likes Given
      25

      Default Re: CHADEMA wamefanya makubwa Tanzania: Tutarajie mapambazuko zaidi ya kifikra!

      Quote By MBELWA Germano
      Heshima Kwanza!..."KAMA watu wawili wana fikra sawa na mtazamo sawa katika kila kitu cha kila jambo, basi, kuwa na uhakika kwamba ni mmojawao tu ndiye mwenye kufikiri”-Lyndon Baines Johnson (LBJ) raisi wa 36 wa Marekani (1963-1969)(Tafsiri).
      Nakupongeza kaka...ni wachache wanajua lakini kwa move hii atimaye kila mtu sasa atajua maana ya vyama vya upinzani...maana cc sasa ni mabalozi kama wewe

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      Baba Clara's Avatar
      Member Array
      Join Date : 10th May 2011
      Posts : 80
      Rep Power : 423
      Likes Received
      23
      Likes Given
      38

      Default Re: CHADEMA wamefanya makubwa Tanzania: Tutarajie mapambazuko zaidi ya kifikra!

      Kwa kweli huu ujumbe wassira anatakiwa aupate ili aache kuropopka ropoka
      Mbelwa Germano likes this.

    9. #7
      Mbelwa Germano's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th May 2011
      Posts : 701
      Rep Power : 838
      Likes Received
      200
      Likes Given
      262

      Default Re: CHADEMA wamefanya makubwa Tanzania: Tutarajie mapambazuko zaidi ya kifikra!

      Kuna msemo wa kiswahili unaosema “usilolijua ni sawa na usiku wa giza”, laiti kama tungekuwa tunakumbushana mara kwa mara ule wajibu tulio nao wa kufikiri kwa bidii leo hii tungekuwa tumepata mapambazuko makubwa ya kifikra juu ya mustakabali wa nchi yetu chini ya mfumo wa vyama vingi.

      Katika nyakati hizi ambapo siasa ya Tanzania imejaa hadaa na uongo mwingi lazima wananchi na viongozi wa kisiasa waonyeshe umuhimu wa kufikiri kwa bidii na kufanya maamuzi yenye tija kwa maslahi ya nchi yetu. Tuondoe fikra za kibaguzi zinazoondoa dhana halisi ya demokrasia, haki, utu wa binadamu na utawala bora. Lazima tufikiri kwa bidii kwanini nchi yetu imezubaa kimaadili na kizalendo, nini fursa ya mtanzania? Je fursa hizo tunazitumia ipasavyo? Na nini suluhisho?

      CHADEMA wameonyesha njia sasa ni wakati wa wanawake wa Tanzania kuanza kufunga vilemba vya maarifa, Wazee wa Tanzania kuvaa kofia za hekima na busara na Vijana kuvaa kofia za fikra pevu. Tutarajie mapambazuko zaidi.
      WA-UKENYENGE likes this.
      80 percent of problems are often due to 20 percent of the causes

    10. #8
      SHIMBONONI's Avatar
      Member Array
      Join Date : 17th September 2011
      Posts : 91
      Rep Power : 406
      Likes Received
      24
      Likes Given
      35

      Default Re: CHADEMA wamefanya makubwa Tanzania: Tutarajie mapambazuko zaidi ya kifikra!

      Bravooooooo!
      Mbelwa Germano likes this.

    11. #9
      STEIN's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2010
      Location : Arusha
      Posts : 1,342
      Rep Power : 715
      Likes Received
      306
      Likes Given
      156

      Default Re: CHADEMA wamefanya makubwa Tanzania: Tutarajie mapambazuko zaidi ya kifikra!

      Mkuu tuongeze ari hii ya kuwaelezea wananchi kuhusu CDM na kikubwa ni Vijana wengi tujipambanue na CDM ili kuwa aminisha wengine
      “Problems cannot be solved by the same level of thinking that created them.”“Insanity: doing the same thing over and over again and expecting different results.”" by Albert Einstein"

    12. #10
      asigwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2011
      Location : TANDHANIYA
      Posts : 4,389
      Rep Power : 1265
      Likes Received
      1209
      Likes Given
      1253

      Default Re: CHADEMA wamefanya makubwa Tanzania: Tutarajie mapambazuko zaidi ya kifikra!

      uchambuzi wako umekaa vizuri sana na niweza kuona hata uwezo wako wa kufikiri ni mkubwa vile vile CHADEMA kama chama makini kimeweza kutoa changamoto kubwa sana kwa hawa wanaojiona wafalme wa hii nchi na kwa hili wanahitaji pongezi..kwa kawaida ukiona unaowaamini kuwa ni wakubwa wanahaha kutokana na uwepo wako basi ujue umewabana kuliko
      Mbelwa Germano likes this.

    13. #11
      Mbelwa Germano's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th May 2011
      Posts : 701
      Rep Power : 838
      Likes Received
      200
      Likes Given
      262

      Default Re: CHADEMA wamefanya makubwa Tanzania: Tutarajie mapambazuko zaidi ya kifikra!

      Quote By STEIN
      Mkuu tuongeze ari hii ya kuwaelezea wananchi kuhusu CDM na kikubwa ni Vijana wengi tujipambanue na CDM ili kuwa aminisha wengine
      Moja ya sifa kuu ya kijana ni kupenda kujua vitu tafauti tofauti kwa maana ya kutopenda kuishi kwa mazoea. Tofauti kati ya kijana na kijana haitokani na umri tu bali ni pamoja na utofauti wa kifikra katika kukabiliana na changamoto mbalimbali.

      Angalizo: Tusikubali kufanywa kama ndege waendao mtegoni wakati wanamuona mtegaji kwasababu tu ya tamaa ya mali au kama ng’ombe waendaye machinjoni wakati wanamuona mchinjaji. Lazima tujenge utamaduni wa kuchagua viongozi wa kisiasa wanaohubiri mipango na kutekeleza wakipata nafasi ya kushika madaraka ya nchi, tuachane na ushabiki usiokuwa na tija, hakuna binadamu anayezaliwa na chama cha siasa.
      80 percent of problems are often due to 20 percent of the causes

    14. #12
      masopakyindi's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 5th July 2011
      Posts : 3,746
      Rep Power : 4197
      Likes Received
      1009
      Likes Given
      416

      Default Re: CHADEMA wamefanya makubwa Tanzania: Tutarajie mapambazuko zaidi ya kifikra!

      Kimsingi hata CHADEMA wakichukua nchi -Mungu apishili mbali- watakuwa na matatizo pengine makubwa zaidi hata kuliko ya CCM.
      Kioganaizesheni bado CHADEMA ni cha mtoto kwa CCM, na bado kuna sehemu nyingi tu nchi ambako CHADEMA haijulikani.

      Lazima tuelewe ukweli kuwa umaarufu wa CHADEMA ni kutokana na MAKOSA ya CCM na si sera mbadala na nzuri za CDM.
      Hilo ni jambo la msingi sana na CHADEMA wasisahau hilo.
      Kimsingi CCM walipoteza touch na wananchi baada ya kuanza kukumbatia matajiri.
      Walipokifikisha chama cha CCM matajiri hao, leo CCM inajuta-lakini walionywa hawakusikia.
      Pamoja na wizi, kashfa ambazo hazijashughulikiwa umaarufu wa uongozi wa CCM umetia wananchi mashaka.
      Hilo ndo kosa kubwa la CCM.

      Kwa hiyo CHADEMA msije kubweteka, CCM waijisahihisha makosa yao bado sera za chama hiki zinaeleweka ukilonganisha na CHADEMA.

      Kwa hiyo CDM usipime nguo kabla mwana hajazaliwa.
      Mbelwa Germano likes this.

    15. #13
      Mbelwa Germano's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th May 2011
      Posts : 701
      Rep Power : 838
      Likes Received
      200
      Likes Given
      262

      Default Re: CHADEMA wamefanya makubwa Tanzania: Tutarajie mapambazuko zaidi ya kifikra!

      Quote By masopakyindi
      Kimsingi hata CDM wakichukua nchi -Mungu apishili mbali- watakuwa na matatizo pengine makubwa zaidi hata kuliko ya CCM.
      Kioganaizesheni bado CDM ni cha mtoto kwa CCM, na bado kuna sehemu nyingi tu nchi ambako CDM haijulikani.

      Lazima tuelewe ukweli kuwa umaarufu wa CDM ni kutokana na MAKOSA ya CCM na si sera mbadala na nzuri za CDM.
      Hilo ni jambo la msingi sana na CDM wasisahau hilo.
      Kimsingi CCM walipoteza touch na wananchi baada ya kuanza kukumbatia matajiri.
      Walipokifikisha chama cha CCM matajiri hao, leo CCM inajuta-lakini walionywa hawakusikia.
      Pamoja na wizi, kashfa ambazo hazijashughulikiwa umaarufu wa uongozi wa CCM umetia wananchi mashaka.
      Hilo ndo kosa kubwa la CCM.

      Kwa hiyo CDM msije kubweteka, CCM waijisahihisha makosa yao bado sera za chama hiki zinaeleweka ukilonganisha na CDM.

      Kwa hiyo CDM usipime nguo kabla mwana hajazaliwa.
      Jambo la muhimu tunalopaswa kutambua ni kwamba, kila binadamu anafanya makosa lakini hatupaswi kujiridhisha na makosa yetu bila kutumia fikra zetu kutafuta ufumbuzi mkubwa kusahihisha makosa yetu. Ukweli hautaki kupuuzwa hivyo tusijidanganye wenyewe na kujiridhisha kana kwamba matatizo na shida zetu hazihitaji fikra za juu zilizojaa hekima, ubunifu, uadilifu na busara.

      Vilevile tunapaswa kutambua kwa dhati kwamba kutambua ukweli ndio njia ya kuamsha fikra na kuamini matendo chanya, kukubali ukweli wa maisha na kupambana kubadilika kuelekea kwenye mafanikio zaidi, hivyo lazima tutazame kwa ukaribu changamoto za nyakati.
      80 percent of problems are often due to 20 percent of the causes

    16. #14
      uwemba1's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 102
      Rep Power : 380
      Likes Received
      23
      Likes Given
      3

      Default

      Quote By mchaichai
      nakupongeza kaka...ni wachache wanajua lakini kwa move hii atimaye kila mtu sasa atajua maana ya vyama vya upinzani...maana cc sasa ni mabalozi kama wewe
      mkuu heshima mbele umechangia vizuri lkn unacopy story yoote unaboa wengine tunatumia cm so ni usumbufu
      unataka
      Mbelwa Germano likes this.

    17. #15
      masopakyindi's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 5th July 2011
      Posts : 3,746
      Rep Power : 4197
      Likes Received
      1009
      Likes Given
      416

      Default Re: CHADEMA wamefanya makubwa Tanzania: Tutarajie mapambazuko zaidi ya kifikra!

      Quote By MBELWA Germano
      Jambo la muhimu tunalopaswa kutambua ni kwamba, kila binadamu anafanya makosa lakini hatupaswi kujiridhisha na makosa yetu bila kutumia fikra zetu kutafuta ufumbuzi mkubwa kusahihisha makosa yetu. Ukweli hautaki kupuuzwa hivyo tusijidanganye wenyewe na kujiridhisha kana kwamba matatizo na shida zetu hazihitaji fikra za juu zilizojaa hekima, ubunifu, uadilifu na busara.

      Vilevile tunapaswa kutambua kwa dhati kwamba kutambua ukweli ndio njia ya kuamsha fikra na kuamini matendo chanya, kukubali ukweli wa maisha na kupambana kubadilika kuelekea kwenye mafanikio zaidi, hivyo lazima tutazame kwa ukaribu changamoto za nyakati.
      Mkuu unamwaga filosofia ambayo kila mtu mwenye hekima anaifahamu.

      Bado hujajibu counter argument yangu kuwa CDM in capitalize kisiasa kwa makosa ya CCM na si vinginevyo.
      Makosa ya CCM hata wanaCCM wanaya fahamu, na kwa hivi sasa inaelekea CCM imexinduka kutoka kwenye usingizi mzito wa kiitikadi.

      Sera za CCM zitabaki kuwa safi na kungwa mkono na wananchi walio wengi-arimradi CCM wakijipanga vizuri, na hili naona wameliona.
      Hekima peke yake hailiwi balikuifanyia kazi hekima hiyo ndio jambo la msingi.

      Sera za CDM bado ni kitendawili na nasisitiza kuwa CCm ikijipanga CDM itakuwa haina hoja ya msingi.
      Kinachowaunganisha CDM ni makosa ya CCM na si sera za CDM.
      Mbelwa Germano likes this.
      "If you don't know where you are going, any road will get you there-nowhere”

    18. #16
      Kobello's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th February 2011
      Posts : 2,950
      Rep Power : 1660
      Likes Received
      1109
      Likes Given
      191

      Default Re: CHADEMA wamefanya makubwa Tanzania: Tutarajie mapambazuko zaidi ya kifikra!

      Lengo la upinzani ni kuchukua madaraka, kama bado hawajachukua basi wakae tu uani, barazani wawaachie wazee wa kazi.
      masopakyindi likes this.
      Keeping quiet is a war crime.

    19. #17
      Sun Tzu's Avatar
      Member Array
      Join Date : 2nd March 2010
      Posts : 75
      Rep Power : 593
      Likes Received
      20
      Likes Given
      10

      Default Re: CHADEMA wamefanya makubwa Tanzania: Tutarajie mapambazuko zaidi ya kifikra!

      Mbelwa Germano,

      CHADEMA is Evanescent, it only flourishes now due some weaknesses within CCM. The moment CCM get her act together, CHADEMA will take a back seat that is the truth:-)
      Mbelwa Germano likes this.
      "In time of war, when truth is so precious, it must be protected by a bodyguard of lies." Winston Churchill

    20. #18
      Mbelwa Germano's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th May 2011
      Posts : 701
      Rep Power : 838
      Likes Received
      200
      Likes Given
      262

      Default Re: CHADEMA wamefanya makubwa Tanzania: Tutarajie mapambazuko zaidi ya kifikra!

      Quote By Sun Tzu
      Mbelwa Germano,

      CHADEMA is Evanescent, it only flourishes now due some weaknesses within CCM. The moment CCM get her act together, CHADEMA will take a back seat that is the truth:-)
      And the true democracy will start to prevail

      Hata Democrat wanapata nguvu kutokana na makosa ya Republican and viceversa, ninachosisitiza kwenye uzi wangu ni Watanzania kupevuka kisiasa na kufikiri nje ya boksi, ukweli ni kwamba CCM hakiwezi kutawala daima na CHADEMA hawawezi kupendwa milele. Vileviele kumbuka leo hii Tanzania tuna vyama vya siasa zaidi ya 18, lakini ni vichache tu vimeweza kustahimili siasa za ushindani nchini na usifikiri kwamba CDM hapa kilipo fika ni kazi lelemama.

      "Wapo watu wengi walioamini/wanaoamini upinzani ni njama ya kihaini, kashfa, mauaji, matusi, uzushi, au machafuko yanayoondoa dhana halisi ya kichocheo cha changamoto za demokrasia au maendeleo"

      Sasa watanzania wameamka na kuanza kuelewa nini maana ya mfumo wa vyama vingi tofauti na nyuma kutokana na hayo makosa uliyosema ya CCM kwa kusahau itikadi yake wakati kinaanzishwa na kukumbatia ufisadi.
      80 percent of problems are often due to 20 percent of the causes

    21. #19
      Mbelwa Germano's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th May 2011
      Posts : 701
      Rep Power : 838
      Likes Received
      200
      Likes Given
      262

      Default Re: CHADEMA wamefanya makubwa Tanzania: Tutarajie mapambazuko zaidi ya kifikra!

      Quote By masopakyindi
      Mkuu unamwaga filosofia ambayo kila mtu mwenye hekima anaifahamu.

      Bado hujajibu counter argument yangu kuwa CDM in capitalize kisiasa kwa makosa ya CCM na si vinginevyo.
      Makosa ya CCM hata wanaCCM wanaya fahamu, na kwa hivi sasa inaelekea CCM imexinduka kutoka kwenye usingizi mzito wa kiitikadi.

      Sera za CCM zitabaki kuwa safi na kungwa mkono na wananchi walio wengi-arimradi CCM wakijipanga vizuri, na hili naona wameliona.
      Hekima peke yake hailiwi balikuifanyia kazi hekima hiyo ndio jambo la msingi.

      Sera za CDM bado ni kitendawili na nasisitiza kuwa CCm ikijipanga CDM itakuwa haina hoja ya msingi.
      Kinachowaunganisha CDM ni makosa ya CCM na si sera za CDM.

      Nimefurahi kwamba wewe binafsi unakiri kwamba CCM kina matatizo lakini unafikiri ni kwa nini hayo makosa yameshindwa kuvipandisha chati UDP, CHAUSTA, NLD n.k na iwe CHADEMA. Na mimi sikuanzisha mada ili kushambulia CCM zaidi ya kueleza nafasi ya vyama vya upinzani ikiwepo CHADEMA katika kuleta mapambazuko ya kifikra nchini.


      Nimeshaandika "...bila CHADEMA leo hii usingesikia wimbo wa kujivua MAGAMBA ndani ya CCM" na sijaona hizo unazoziita argument zako ambazo sijazijibu. Rudi kwenye mada, bado ni mwepesi sasa kujenga arguments zenye mashiko.
      80 percent of problems are often due to 20 percent of the causes

    22. #20
      masopakyindi's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 5th July 2011
      Posts : 3,746
      Rep Power : 4197
      Likes Received
      1009
      Likes Given
      416

      Default Re: CHADEMA wamefanya makubwa Tanzania: Tutarajie mapambazuko zaidi ya kifikra!

      Quote By MBELWA Germano

      Nimefurahi kwamba wewe binafsi unakiri kwamba CCM kina matatizo lakini unafikiri ni kwa nini hayo makosa yameshindwa kuvipandisha chati UDP, CHAUSTA, NLD n.k na iwe CHADEMA. Na mimi sikuanzisha mada ili kushambulia CCM zaidi ya kueleza nafasi ya vyama vya upinzani ikiwepo CHADEMA katika kuleta mapambazuko ya kifikra nchini.


      Nimeshaandika "...bila CHADEMA leo hii usingesikia wimbo wa kujivua MAGAMBA ndani ya CCM" na sijaona hizo unazoziita argument zako ambazo sijazijibu. Rudi kwenye mada, bado ni mwepesi sasa kujenga arguments zenye mashiko.
      Mkuu wewe si mwanafunzi mzuri wa historia.

      Dont try to give Cdm credit for what it is not.

      Kujivua gamba ndani ya CCM haikuanzia na CHADEMA na haitaishia na chama hicho.

      Soma vizuri on the Rules of Social Contradictions katika jamii.

      Unawakumbuka Christopher Mtikila na Mapalala? Mababa wa upinzani wa kisiasa?

      Walimpinga hata Mwalimu Nyerere at the pain ya kuswekwa kizuizini,na walikuwepo wengine.

      CHADEMA wameflourish baada ya wao kuruhusiwa kuishi kisiasa. Kwa mtu ambaye ni mgeni katika siasa hataweza kukumbuka kuwa hapo nyuma palokuwepo kitu similar na kujivua gamba.

      Soma historia ya CCM na utaona kulikuwepo na OPERATION TUJISASAHIHISHE,KUNG'ATUKA, UFAGIO Wa CHUMA- hatua maalum zilizochukuliwa ili kukinusuru chama cha Mapinduzi.
      Hayo yote yalitokana na shinikizo toka NDANI ya CCM, na wala si chama kingine cha siasa, ambavyo havikuwepo anyway.

      CHADEMA is right now only riding a wave of social discontent into the unknown, and when the water is calm, sink it will!
      Last edited by masopakyindi; 16th June 2012 at 17:14.
      Sun Tzu likes this.
      "If you don't know where you are going, any road will get you there-nowhere”

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...