Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Ni nani alishinikiza uteuzi wa Dr. William Mgimwa kuwa waziri wa fedha?

    Report Post
    Page 1 of 9 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 170
    1. #1
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,737
      Rep Power : 12927
      Likes Received
      4438
      Likes Given
      7465

      Default Ni nani alishinikiza uteuzi wa Dr. William Mgimwa kuwa waziri wa fedha?


      Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa akionyesha begi lililobeba hotuba ya bajeti ya serikali kwa mwaka wa fedha 2012/2013, wakati akielekea kuingia katika ukumbi wa Bunge, mjini Dodoma jana. Picha na Edwin Mjwahuzi


      Jana nilijaribu kumsikiliza waziri wa fedha Dr. Mgimwa na swali lililokuwa likijirudia mara kwa mara kichwani mwangu ni hivi huyu Mheshimiwa ni mradi wa nani?

      Baada ya JK kudhalilishwa na mawaziri wake wawili wa fedha kwa maana ya utendaji duni wa Meghji na Mkullo ni dhahiri alitafuta ushauri wa nani anafaa kumsaidia kwenye wadhifa tajwa................ni nani ushauri wake JK aliuzingatia katika uteuzi tajwa?

      Wakati serikali ya JK ikikumbwa na kashfa ya CAG ya matumizi mabaya ya fedha ulikuwepo uvumi kuwa hata PM alikuwa anafikiria kujing'atua na kumwacha JK azame na merikebu yake ya TITANIC...................laki ni hakufanya hivyo ni kwa sababu zipi?

      Jingine ni kuwa wakati makabrasha ya wizara ya fedha ya bajeti yalipocheleweshwa alikuwa ni Pinda aliyemkingia kifua Dr. Mgimwa kuwa Dr. Mgimwa alikuwa na kibali cha Raisi ayapitie upya makadirio tajwa ili na yeye kwenye wadhifa wake mpya aweze kuweka michango yake.................baada ya kupitia bajeti husika sioni kama kuna jipya ukiondoa misamaha ya kodi kwa walalahoi wanaopata chini ya milioni tatu na hata hapo naona bado kuna uonevu umefanyika na nitafafanua baadaye..........

      Jingine, jipya ni kuamsha ari za usajili magari kwa majina binafsi na kuyalipia milioni 5 kila baada ya miaka 3...............hili ni kuiga marekani ambako utaratibu huu umeshamiri.................

      Mengineyo yote yaliyomo kwenye bajeti, hata Mkullo au Meghji wangelisoma hayohayo kwa hiyo sioni khoja ya Pinda ya ucheleweshwaji wa bajeti kama ina mashiko.......................

      Kwa hiyo, kama Pinda alilidanganya Bunge kwa minajili ya kumlinda Dr. Mgimwa alifanya hivyo kwa masilahi ya nani? Kwa maoni yangu binafsi, Pinda na wala siyo JK ndiye mhimili na mfadhili wa huyu waziri mpya wa fedha na Pinda anaona kavuna dume kwa sababu amekuwa akitafuta mianya ya hazina kusukuma kwa kasi maendeleo ya mkoa wa Rukwa hususani jimbo lake la uchaguzi........na Mkullo hakuwa akimsikiliza sana kwa sababu ana uhusiano wa moja kwa moja na JK uhusiano wa miaka mingi tangia akiwa NPF na JK akiwa kwenye baraza la Mwinyi........

      Bajeti hii ina sifa za kulinda masilahi ya viongozi na wala siyo ya walalahoi na maeneo haya ndiyo maangalizo 10 ambayo yananifanya nije na misimamo tajwa:-

      1) Viongozi wote serikalini wanakiri kuwa makali ya maisha yameongezeka lakini ufumbuzi wao ni kulinda walichonacho au hata kujiongezea bila ya kujua kwa kufanya hivyo walikuwa wanapunguza huduma za kijamii na hivyo kumwongezea makali mlalahoi. Mishahara ya viongozi na sheria ya pensheni ya viongozi vilitakiwa vifanyiwe marekebisho makubwa ili kuondoa ubaguzi ambao unafanywa na viongozi kwenye nyanja hiyo kinyume na sheria..................haya hayakufanyika na kamwe hayatafanyika katika kipindi cha JK akiwa madarakani kwa sababu yeye mwenyewe ni matunda ya mfumo mbovu wa upatikanaji wa viongozi kwa hiyo hawezi kuwa na hisia kali ya kurekebisha mapungufu yaliyopo na hata hisia tajwa angelikuwa nazo bado hana ujuzi wa kufanya hivyo....................kwa lugha nyingine JK ni matunda ya kunukuu staili ya utendaji mbovu ya wale aliyewarithi.

      2) Kumpunguzia makali mlipa kodi mwenye kipato cha chini ya milioni 3 ni unafiki wa kupindukia. Mtumishi wa serikalini mwenye kipato kama hicho hana
      capital costs kwenye mapato yake jambo ambalo anayejiajiri anazo. Tumchukulie mama ntilie mwenye kipato cha milioni 3 kwa mwaka utakuta gharama zake za kuendesha mradi ni asilimia 70 hadi 90 ya mapato tajwa sasa ukimtoza kodi katika kiwango hicho cha chini ni dhahiri unatoza mtaji na hivyo kumwongezea adha za kufukarika. Serikali iliyo makini ingeweka wazi apataye mapato chini ya Tshs 20 millioni kwa mwaka hapaswi kulipa kodi kwa sababu hicho kiwango ni cha kumwezesha kujiajiri na kumudu gharama za maisha...............hivyo pamoja na porojo za Dr. Mgimwa bado hana hisia kali za adha ya umasikini na vyanzo vyake hapa nchini..

      3) Kodi za magari chakavu kupandishiwa umri kutoka miaka 10 hadi zaidi ya miaka 8 ni panga linalokata pande mbili: sababu za kulinda mazingira ni lazima zilinganishwe na sababu za kukuza uchumi. Dr. Mgimwa alipaswa atofautishe aina ya vyombo husika.... magari ya anasa na vifaa vyovyote vile vya anasa ni sahihi kuvitoza kodi tajwa lakini vyombo vya uzalishaji kama vya barabara, ujenzi na viwandani vilipaswa kubaki umri uleule wa miaka 10 kutokana na mchango wake katika kuinua kipato cha nchi na kuwapatia ajira raia wake. Utashangaa kufahamu zaidi ya asilimia 90 ya mitambo ya barabara inayojenga barabara zetu in umri wa zaidi ya miaka 10. Sasa ukianza kutoza kodi ya asilimia 20 kwa yule anayeagiza mitambo hiyo ambayo bado kabisa ina khali nzuri sana huo ufukara unamletea nani kama siyo mlalahoi anayetegemea kujipatia kipato kutokana na vyanzo hivyo vya uzalishaji.

      4) Bajeti kama zile zilizoitangulia bajeti hii, imeshindwa kuainisha kwa kushirikiana na CAG mianya ya kuporomoka uwajibikaji katika matumizi ya serikali. Haitoshi kwa Dr. Mgimwa kudai usimamizi wa bajeti hii utakuwa tofauti na zile zilizotanguliwa bila ya kuonyesha kwa namna zipi. mfano serikali za mitaa inabidi zimilikishwe halmashauri kwa madiwani wawe na mamlaka ya kuajiri watumishi wa ngazi zote badala ya kutegemea serikali kuu kupandikiza mamluki wao ambao ni viwavi jeshi na madiwani kubakia ni wapiga tarumbeta za hamelini. Kwenye mashirika ya umma kuna uhaja wa kubadilisha mfumo mzima wa uteuzi wa bodi na bodi kuwa na mamlaka ya mwisho ya uteuzi wa watendaji wote wakiwemo CEOs kwenye taasisi zao badala ya Ikulu kuona ni kivuno cha kupanga safu za viwavi jeshi. Bodi za wakurugenzi zinapaswa zitokane na wadau wa sekta husika ambao watapatikana kwa kupigiwa kura na washiriki wa nyanja husika hivyo kuondoa mmomonyoko wa uwajibikaji. Wenyeviti wa Bodi kuchaguliwa moja kwa moja na wajumbe wa bodi badala ya Ikulu kuwabandikia mtu ambaye hushukuriwa kwa sababu za kumlinda kisiasa bila ya kujali kama ana mchango wowote wa taasisi ambayo amekabidhiwa kuisimamia....

      5) Kusahau nafasi ya michezo katika kuleta ajira na kukuza uchumi. Timu zote za daraja la juu (Premier league) la mpira wa miguu zilitakiwa zitengewe fungu la kuanzisha timu za watoto ili kuibua vipaji kama sehemu ya awali ya kuanzia. La ajabu viongozi wetu kila siku huimba soka huendelezwa na timu siyo timu ya taifa lakini ni wagumu kwenye mioyo yao kutoa fedha za shughuli hiyo nyeti katika kukuza vipaji vya michezo, kufufua uchumi na kuwapatia ajira vijana wetu. Kwa kuanzia kila timu iliyoko kwenye Premier league ingelitengewa shilingi milioni 200 kwa mwaka kwa kazi hiyo ya kukuza vipaji vya vijana na fedha hizo CAG lazima akague matumizi yake.
      Haya, huyu Dr. Mgimwa hawezi kuyafikiria kwa sababu ni kizazi kilichopitwa na wakati.

      6) (a) Upendeleo wa misamaha ya kodi zote kutofutwa kwa vigezo ambayo vinakinzana na katiba yetu ya kuondoa aina zote za ubaguzi. Katika hukumu ya KTM {Karibu Textiles Mills} mahakama zote za juu zilisema ni ukiukwaji wa katiba kutoa misamaha ya kodi kwa baadhi ya makampuni tu tena yapo kwenye sekta moja khalafu wengine mkawabagua eti kwa sababu wana mikataba yao na wengineo hawana. Mbali ya ukweli kuwa ubaguzi tajwa unatibua nguvu ya soko lakini la kuzingatiwa ni kuwa katiba iko juu ya mikataba tajwa.
      Nilidhani kama Dr. Mgimwa is the real deal angeliifuta mikataba tajwa kwa kuongozwa na hukumu za KTM ya EAC na ya CAT (TZ COURT OF APPEAL) katika kutenda haki. Lakini kwa vile, Dr. Mgimwa hakuwekwa pale kwa dhamira safi ya kulisaidia taifa bali ni kujibu tu kiu ya aliyemweka ambaye ninaamini ni Peter Mizengo Pinda basi upeo wa kuyaona haya hana na hivyo hana sifa hata moja ya kuwa Waziri kwenye nyadhifa yoyote ile kwenye baraza la mawaziri achilia mbali Wizara ya fedha.

      b) Misamaha ya kodi kwenye mahoteli ya kitalii kanda ya kaskazini haijafutwa ambayo inaigharimu nchi zaidi ya dola 20-70 milioni kwa mwaka. Sasa Dr. Mgimwa alichelewesha bajeti hii kwa nini kama...........it is business as usual, na hata huyo Pinda aliyekuwa akimtetea hivi haoni hata haya?


      What a shame!



      7) Eneo ambalo humgusa mlalahoi moja kwa moja ni eneo la kodi. Kodi ya VAT ya asilimia 18 imesaidia sana katika kufifilisha soko la ajira. Hawa wakubwa wakisha kulamba hela yetu pale hazina hukimbilia kudai haya ni makusanyo ya serikali na kusahau hata siye ambao hatujaajiriwa serikalini nao ni sehemu hiyo hiyo ya serikali. Serikali yoyote ambayo haisikilizi kukua kwa gharama za maisha na uhaba wa vyanzo vya uzalishaji hiyo serikali siyo sikivu hata kama ikidai vinginevyo.

      a) Kwa kuanzia VAT ilipaswa kupunguzwa kutoka asilimia 18 hadi 15 ili kuhamasisha waajiri wakuze soko la ajira na kuongeza ushindani wa bidhaa zetu kwenye soko la dunia. Mapato ya serikali kuyaongeza siyo kuongeza viwango vya kodi tu bali kuwa na kiwango cha kodi ambacho kitahamasisha tija na uzalishaji. Hili tuendelee kulidai kwani ni haki yetu kukataa kuburutwa bila ya siye kutaka katika ufukara wa kujitakia.

      b) VAT ya EWURA na REA, kwenye umeme ni ya kuondoa tena kinatakiwa kiwe kitendo cha haraka sana. Hivi huo umeme wa vijijini hata ukipelekwa ni nani kule atakayeweza kuumudu gharama zake kama hata wakaazi wengi wa mijini naona wamerudishwa kwenye vibatali tu? Kiujumla wakaazi wa mijini wana uwezo wa kumudu gharama za maisha zaidi ya wale wa vijijini na kama mfupa umemshinda mzee fisi je nani atauweza?

      c) Kila Halmashauri ilipaswa kutengewa 7% ya VAT kwenda moja kwa moja kwenye shughuli zao badala ya kutegemea hisani ya serikali kuu au udanganyifu wa mfuko wa jimbo ambao nao ni kituko kwani siyo shirikishi hata chembe. Serikali kuu ingelibaki na 8% ya makusanyo ya VAT kwa minajili ya kusawazisha maeneo ambayo yana mapato madogo na hivyo kuleta maendeleo yenye uwiano mzuri. Mfumo wa mgawanyo uliopo unaipa serikali kuu hususani DSM upendeleo wa kila kitu na hivyo kuacha mikoa ya pembezoni kuwa nyuma sana kimaendeleo. Huu ndiyo mtazamo mpya wa kulikwamua taifa kutoka hapa lilipo hadi kwenda kwenye maendeleo kwa kila mtanzania..................... ...azma ambayo ianaelekea ni tamu wakati wa kuomba kura lakini ni chungu katika kuitekeleza..............

      Hivi huyu Dr. Mgimwa anaelewa nchi hii inatoka wapi, iko wapi na yaelekea wapi? Kama siyo mbabaishaji tu?


      8) Kukwepa kufuta road tolls za magari makubwa. Kila mahali alipokuwa akihalalisha kupanda kwa kodi, Dr. Mgimwa alikuwa anajificha kwenye kichaka cha EAC na sheria zake. Bajeti ya jana ya Kenya wamefuta vizuizi vyote vya barabarani vikiwemo vya tozo za magari makubwa, usafirishaji wa vyakula n.k .......................sasa hayo maigizo ya EAC mbona hayakufika kwenye kufuta road tolls ambazo zinatajirisha watu wachache badala ya kulitajirisha taifa?????????????..........Ku husu uzito wa magari ni udhibiti wa idadi ya matairi ya nyuma la gari au load axles unatosha kabisa kuhakikisha magari yetu hayazidi tani stahiki. Kenya wao lori lenye axles 3 tu ndizo zinaruhusiwa kwenye barabara zao. Sasa ukiisha kulisimamia hilo huu uchafu wa road tolls ambazo zinaongeza mrundikano wa bidhaa na kuchelewesha huduma kwa jamii huku zikimwongezea mlaji gharama zisizorejesheka ni wa nini kama siyo kulinda ajira na ufisadi wa watoto wa vigogo ambao ndiyo wamerundikwa kwenye vituo vya matozo tajwa?

      9) Ukuaji wa deni la taifa Dr. Mgimwa aliuchukulia kimzahamzaha tu na hakuna maelezo ya kutosha kuelezea ni kwa sababu zipi taifa limebebeshwa mzigo wa deni la trilioni 5 tu wakati Mkapa anamkabidhi Jk nchi na khalafu deni hilo lipande khadi trilioni 8 mwaka 2009 na leo lifikie trilioni 22 (Kwa fedha za kitanzania)? Tathmini ya nani alikopa na kwa idhini ya nani inabidi ijulikane sasa na hata CAG sijui yuko wapi kutathmini hilo na badala yake anatumia muda mwingi kuwabana halmashauri ambao mapato yao ni kiduchu. Dr. Mgimwa kama angelikuwa makini angelianzisha sheria ya kuhakikisha bunge ndilo lenye mamlaka ya kupitisha mikopo yote ya serikalini. Hatukumchagua Raisi aende Ikulu kufanya atakavyo bila ya kuwajibika kwa yeyote. Haya madeni yatalipwa na wajukuu zetu na vilembwekazi hata hatujui hizo fedha zilifanya nini na aliyekuwa aziidhinisha alifanya hivyo kwa mashinikizo ya akina nani...........

      10) BOT imekuwa haitazamwi juu ya vyanzo vyake vya mapato na matumizi na imekuwa kinara wa ufisadi ambao hata CAG huwa anaufumbia macho. Wakati umefika mapato na matumizi ya BOT yakawekwa wazi na ile sheria ya kulizuia bunge kudhibiti BOT ikafutwa na kurejesha BOT mikononi mwa udhibiti wa Bunge......................

      Kwa haraka haraka, Dr. Mgimwa ni bomu na tusitishike na kauli zake za kujiamini..mara nyingi matapeli ndivyo walivyo.............na nimpa D minus kwenye maandalizi ya bajeti inayomjali mnyonge....................... ........have your say too.

      Last edited by Rutashubanyuma; 17th June 2012 at 12:21. Reason: spelling, additional points
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    2. Miaka 50

    3. #2
      Ndahani's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd June 2008
      Location : Somewhere
      Posts : 9,647
      Rep Power : 4016
      Likes Received
      2940
      Likes Given
      5063

      Default Re: Ni nani alishinikiza uteuzi wa Dr. William Mgimwa kuwa waziri wa fedha?

      Why dont we wait until 2015? Is there anything new now? Au ndio mambo ya kuweka zabibu mpya kwenye kiriba cha kale....
      We are all inventors, each sailing out on a voyage of discovery, guided each by a private chart, of which there is no duplicate. The world is all gates, all opportunities.
      Ralph Waldo Emerson

    4. #3
      Kongosho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st March 2011
      Location : Location loading...
      Posts : 25,268
      Rep Power : 13086
      Likes Received
      14147
      Likes Given
      15016

      Default Re: Ni nani alishinikiza uteuzi wa Dr. William Mgimwa kuwa waziri wa fedha?

      Mmmmmh, jukwaa la presha.
      Rutashubanyuma and Mamndenyi like this.
      No matter how hot your anger is, it can not cook yams-Nigeria

    5. #4
      Maundumula's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th November 2010
      Posts : 5,003
      Rep Power : 3112
      Likes Received
      1369
      Likes Given
      5780

      Default Re: Ni nani alishinikiza uteuzi wa Dr. William Mgimwa kuwa waziri wa fedha?

      Nakubaliana na wewe juu ya kupunguza Kodi, ila mimi nafikiri kwa kipindi tulichonacho hiki cha ukosefu wa ajira wangetoa punguzo maalum la kodi kwa yale makampuni ya size ya kati ambayo kazi zake labour intensive na wanaoajiri watu kuanzia 3000 na kuendelea ili waje wawekeze hapa pengine ingesaidia vijana. Labda ni wakati wa kulifikiria hili na kutangaza Tanzania duniani kwamba makampuni ya aina hiyo yanaweza kunufaika kwa kuwekeza hapa kwetu.

    6. #5
      +255's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st January 2012
      Posts : 1,089
      Rep Power : 590
      Likes Received
      207
      Likes Given
      0

      Default Re: Ni nani alishinikiza uteuzi wa Dr. William Mgimwa kuwa waziri wa fedha?

      Kama wewe ambavyo haujaona kipya kwenye bajeti, ndivyo na mimi sijaona kipya ulichoandika..
      Kama bajeti zetu huwa ni za ku-copy bajeti za nyuma sidhani ka kuna mtu anaweza kufanya analysis mpya kuhusu hiyo bajeti.

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,737
      Rep Power : 12927
      Likes Received
      4438
      Likes Given
      7465

      Default Re: Ni nani alishinikiza uteuzi wa Dr. William Mgimwa kuwa waziri wa fedha?

      Why dont we wait until 2015? Is there anything new now? Au ndio mambo ya kuweka zabibu mpya kwenye kiriba cha kale....
      Ndahani..2015 to do what ...........kama hata upinzani hususani cdm hawazioni hizi khoja kama ni za msingi kwa kuinua maisha ya MTZ?
      Mziba likes this.
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    9. #7
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,737
      Rep Power : 12927
      Likes Received
      4438
      Likes Given
      7465

      Default Re: Ni nani alishinikiza uteuzi wa Dr. William Mgimwa kuwa waziri wa fedha?

      Kama wewe ambavyo haujaona kipya kwenye bajeti, ndivyo na mimi sijaona kipya ulichoandika..
      Kama bajeti zetu huwa ni za ku-copy bajeti za nyuma sidhani ka kuna mtu anaweza kufanya analysis mpya kuhusu hiyo bajeti.
      +255 pole sana kama huoni jipya na wakati meingi mapya yapo lakini hayana tija kwa mlalahoi.....na kukwepa kuchangi kwa madai bajeti ni ileile......................ni kujinyima nafasi ya kutoa mchango wa mawazo kuliendeleza taifa letu.....
      Mziba, lutamyo and MICHAEL JOHN like this.
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    10. #8
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,737
      Rep Power : 12927
      Likes Received
      4438
      Likes Given
      7465

      Default Re: Ni nani alishinikiza uteuzi wa Dr. William Mgimwa kuwa waziri wa fedha?

      Nakubaliana na wewe juu ya kupunguza Kodi, ila mimi nafikiri kwa kipindi tulichonacho hiki cha ukosefu wa ajira wangetoa punguzo maalum la kodi kwa yale makampuni ya size ya kati ambayo kazi zake labour intensive na wanaoajiri watu kuanzia 3000 na kuendelea ili waje wawekeze hapa pengine ingesaidia vijana. Labda ni wakati wa kulifikiria hili na kutangaza Tanzania duniani kwamba makampuni ya aina hiyo yanaweza kunufaika kwa kuwekeza hapa kwetu.
      Maundumula.......................inapoku ja VAT huwezi kumbagua yeyote yule..........katiba inakataza.........na hao wakubwa wafikiri hata wanalipa? Wangekuwa wanalipa basi khali yetu ingelikuwa ni nafuu sana.....ila viwavi jeshi wachache tuliowapa dhamana ndiyo wananufaika pekee yao........
      Maundumula likes this.
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    11. #9
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,737
      Rep Power : 12927
      Likes Received
      4438
      Likes Given
      7465

      Default Re: Ni nani alishinikiza uteuzi wa Dr. William Mgimwa kuwa waziri wa fedha?

      Mmmmmh, jukwaa la presha.
      Kongosho kila kitu ni presha tupu hakuna unafuu mahali popote pale.............
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    12. #10
      Maundumula's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th November 2010
      Posts : 5,003
      Rep Power : 3112
      Likes Received
      1369
      Likes Given
      5780

      Default Re: Ni nani alishinikiza uteuzi wa Dr. William Mgimwa kuwa waziri wa fedha?

      Rutashubanyuma,

      Basi angalau Income Tax tungewapunguzia ili waone umuhimu wa kuajiri watu wengi. Mfno tukilete kampuni 10 kila moja ikawa imeajiri vijana 3000 huoni hata wizi utapungua dsm?
      Mziba and Rutashubanyuma like this.

    13. #11
      Mungi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 23rd September 2010
      Location : Hapa!!!
      Posts : 10,186
      Rep Power : 24275
      Likes Received
      4681
      Likes Given
      2300

      Default Re: Ni nani alishinikiza uteuzi wa Dr. William Mgimwa kuwa waziri wa fedha?

      Quote By Ndahani
      Why dont we wait until 2015? Is there anything new now? Au ndio mambo ya kuweka zabibu mpya kwenye kiriba cha kale....
      why do we wait until 2015? something must be done to rescue the majority!
      "Peace is not simply about the absence of violence. It is defined by the presence of fundamental liberties and the prevalence of economic opportunities."

    14. #12
      Nicas Mtei's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st December 2010
      Location : Shamba
      Posts : 8,651
      Rep Power : 32147
      Likes Received
      5004
      Likes Given
      5175

      Default

      Quote By Kongosho
      Mmmmmh, jukwaa la presha.
      huku BAN ni za kumwaga. Wapo Mods 6
      Mungi, LiverpoolFC and Dotworld like this.

    15. #13
      Ndahani's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd June 2008
      Location : Somewhere
      Posts : 9,647
      Rep Power : 4016
      Likes Received
      2940
      Likes Given
      5063

      Default Re: Ni nani alishinikiza uteuzi wa Dr. William Mgimwa kuwa waziri wa fedha?

      Quote By Rutashubanyuma
      Ndahani..2015 to do what ...........kama hata upinzani hususani cdm hawazioni hizi khoja kama ni za msingi kwa kuinua maisha ya MTZ?
      Rutashubanyuma, There is nothing we can do in between. This is it trust me. Maana mageuzi gani yatakayofanyika yenye uwezo wa kubadili mwelekeo? Wakati si lazima suluhisho liwe limetoka chadema, changamoto yetu ni kupata presidential material wa ukweli....Awe ametokea wapi si hoja kubwa kama uwezo wake wa kuongoza
      Rutashubanyuma likes this.
      We are all inventors, each sailing out on a voyage of discovery, guided each by a private chart, of which there is no duplicate. The world is all gates, all opportunities.
      Ralph Waldo Emerson

    16. #14
      Ndahani's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd June 2008
      Location : Somewhere
      Posts : 9,647
      Rep Power : 4016
      Likes Received
      2940
      Likes Given
      5063

      Default Re: Ni nani alishinikiza uteuzi wa Dr. William Mgimwa kuwa waziri wa fedha?

      Hizi kodi zinaelekezwa zaidi kwa vikampuni vidogo vidogo vyenye uhai mdogo kuliko multinations kama za madini etc
      Mziba likes this.
      We are all inventors, each sailing out on a voyage of discovery, guided each by a private chart, of which there is no duplicate. The world is all gates, all opportunities.
      Ralph Waldo Emerson

    17. #15
      IGWE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2011
      Location : Blue Plaza Building-Arusha
      Posts : 5,108
      Rep Power : 3263
      Likes Received
      1247
      Likes Given
      1201

      Default Re: Ni nani alishinikiza uteuzi wa Dr. William Mgimwa kuwa waziri wa fedha?

      Huyu waziri ni mradi mwingine wa wakubwa wake.....if you read between lines you will get what i mean mkuu
      "We should learn to help others,not only in our prayer but also in daily life,if we cannot help them_then,the least thing we can do is to desist from harming them"

    18. #16
      Mungi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 23rd September 2010
      Location : Hapa!!!
      Posts : 10,186
      Rep Power : 24275
      Likes Received
      4681
      Likes Given
      2300

      Default Re: Ni nani alishinikiza uteuzi wa Dr. William Mgimwa kuwa waziri wa fedha?

      Quote By Kongosho
      Mmmmmh, jukwaa la presha.
      Mkuu huku haikufai, kakimbilie EM EM YU
      Kongosho likes this.
      "Peace is not simply about the absence of violence. It is defined by the presence of fundamental liberties and the prevalence of economic opportunities."

    19. #17
      Kongosho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st March 2011
      Location : Location loading...
      Posts : 25,268
      Rep Power : 13086
      Likes Received
      14147
      Likes Given
      15016

      Default Re: Ni nani alishinikiza uteuzi wa Dr. William Mgimwa kuwa waziri wa fedha?

      Huku sipapendi maana watu wanapiga makelele afu kura hawapigi, Wizi mtupu
      Tunapandishana mori afu wanakimbia vitani, ya nini wanitoe na kitaulo ndani?

      PAYE inanifanya hata biya sinywi tena
      Quote By Mungi
      Mkuu huku haikufai, kakimbilie EM EM YU
      Ndahani, Mziba and Rutashubanyuma like this.
      No matter how hot your anger is, it can not cook yams-Nigeria

    20. #18
      Mungi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 23rd September 2010
      Location : Hapa!!!
      Posts : 10,186
      Rep Power : 24275
      Likes Received
      4681
      Likes Given
      2300

      Default Re: Ni nani alishinikiza uteuzi wa Dr. William Mgimwa kuwa waziri wa fedha?

      Quote By Kongosho
      Huku sipapendi maana watu wanapiga makelele afu kura hawapigi, Wizi mtupu
      Tunapandishana mori afu wanakimbia vitani, ya nini wanitoe na kitaulo ndani?

      PAYE inanifanya hata biya sinywi tena
      Mkuu usikate tamaa kwa hilo, katika 100 utakaowapigia kelele utavuna angalau samaki wakuridhisha, wengine ndo hivyo tena.
      Rutashubanyuma likes this.
      "Peace is not simply about the absence of violence. It is defined by the presence of fundamental liberties and the prevalence of economic opportunities."

    21. #19
      Rogie's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 22nd November 2010
      Location : Darul Islamia
      Posts : 1,918
      Rep Power : 1146
      Likes Received
      486
      Likes Given
      334

      Default Re: Ni nani alishinikiza uteuzi wa Dr. William Mgimwa kuwa waziri wa fedha?

      In fact, nowhere where I see this government has any plans to the poor of this country rather to make life more difficult. Taxes we pay is very much still has been just words. No politician now is concentrate on this. very heartening.
      Rutashubanyuma likes this.
      "You have your people,and I have mine"
      [email protected]

    22. #20
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,737
      Rep Power : 12927
      Likes Received
      4438
      Likes Given
      7465

      Default Re: Ni nani alishinikiza uteuzi wa Dr. William Mgimwa kuwa waziri wa fedha?

      Rutashubanyuma,

      Basi angalau Income Tax tungewapunguzia ili waone umuhimu wa kuajiri watu wengi. Mfno tukilete kampuni 10 kila moja ikawa imeajiri vijana 3000 huoni hata wizi utapungua dsm?
      @ la muhimu ni kuwa kodi ya VAT ishuke kutoka 18% hadi 15% na kodi za EWURA na REA ziondolewe mara moja.......................... hatua hizi zitamupunguzia mlalahoi kero nyingi...............maana zinagusa sekata zote na asiwepo anayelipa kodi ya mapato kama mapato yake kwa mwaka ni chini ya Tshs 20 millions...................... tukubailane yeyote anayepata chini ya kiwango hicho ni masikini na siyo mtu tena wa kushinikizwa alipe tena kodi..............
      Mziba likes this.
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    Page 1 of 9 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...