Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: BAKWATA yatangaza rasmi waislam kugomea sensa!

    Report Post
    Page 1 of 62 12311 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 1236
    1. #1
      Kiranja Mkuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th February 2010
      Posts : 2,084
      Rep Power : 887
      Likes Received
      284
      Likes Given
      34

      Default BAKWATA yatangaza rasmi waislam kugomea sensa!

      Hawa Bakwata, wanaikomoa CCM au CUF?

      BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) limetangaza rasmi kutoshiriki sensa ya watu na makazi inayotarajiwa kufanyika nchi nzima Agosti, hadi ombi lao la kuingizwa kwa kipengele cha dini kwenye dodoso la sensa kitakapofanyiwa kazi.

      Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Amir Mkuu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Shehe Mussa Kundecha, alisema uamuzi huo umetokana na Serikali kushindwa kusikiliza upande wa Waislamu na kuamua kutokiingiza kipengele hicho.

      Alisema katika mkutano wa viongozi wa dini na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) uliofanyika Dodoma Juni 11, waliwasilisha ombi lao la kipengele cha dini kuingizwa kwenye dodoso za sensa ili kupata idadi kamili ya Watanzania kidini.

      “Kwa kweli mkutano ulikwenda vizuri, tulitoa sababu zetu za kutaka kipengele hicho kiwemo ili kuondoa utata wa sasa wa kila taasisi na dini kutoa takwimu zinazotofautiana na Kamishna wa Takwimu alipokea maombi yetu na kuahidi kuyawasilisha serikalini na kuyafanyia kazi,” alisema Shehe Kundecha.


      Alisema cha kushangaza wakati akifunga mkutano huo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Uhusiano na Uratibu, Stephen Wasira alibainisha wazi kuwa kamwe Serikali haiwezi kukiingiza kipengele hicho kwenye dodoso za sensa, kwa kuwa kinavunja umoja, amani na utulivu wa Taifa.

      Aidha, alisema katika kutetea hoja hiyo, Serikali ilitoa mifano ya nchi za Nigeria na Kenya, ambazo zimefanya sensa na kuingiza kipengele hicho kwenye dodoso, lakini kutokana na kuibuka kwa vuguvugu la kidini katika nchi hizo, hadi leo matokeo ya sensa hizo hayajatangazwa.

      Shehe Kundecha alisema Baraza hilo limepokea hoja hizo na kuzisikiliza ingawa halikubaliani nazo kwa kuwa kwa Tanzania bado zipo taasisi na madhehebu ya dini yanayotoa takwimu za kidini yakionesha idadi ya Wakristo, Waislamu na Wapagani huku umoja na amani vikiendelea kuwapo.

      “Kama tatizo ni kuvurugika kwa amani, umoja na utulivu, mbona basi vyombo hivi visivyohusika na takwimu vinatoa takwimu hizi tena hadi kwenye mitandao na Serikali kuvifumbia macho, huku kukiwa hakuna umoja wala amani iliyovunjika? Kwa nini isifanyike sensa ya kidini na kupatikana takwimu halisi?” Alihoji.

      Alisema kutokana na kauli hiyo, inaonekana wazi kuwa Serikali haijasikiliza kilio cha Waislamu kutaka kipengele cha dini kiingizwe kwenye dodoso za sensa, ili zipatikane takwimu sahihi na rasmi za Watanzania kidini.

      “Hivyo basi tunasisitiza Waislamu hatutashiriki sensa mpaka mapendekezo yetu yatakapofanyiwa kazi, tunataka idadi halisi ya Waislamu, ili nasi tujue tunawasaidiaje kimaendeleo na kidini,” alisema.

      Ustaadh Sadiki Gogo, alisema mfano uliotumiwa na Serikali kukataa ombi la kuingizwa kwa kipengele cha dini kwenye dodoso la sensa hauna nguvu, kwa kuwa umeegemea upande mmoja na kusahau nchi kama Uganda, Uingereza, Australia na Canada, ambazo katika sensa zao wanatumia kipengele cha dini na hazina matatizo.


      Hivi karibuni, Katibu Mkuu wa Shura ya Maimamu Tanzania, Shehe Ponda Issa Ponda, alisema atahakikisha Waislamu hawashiriki Sensa ya Watu na Makazi iwapo Serikali haitarudisha kipengele cha dini katika maswali wanayoulizwa wananchi.


      Alisema haoni hoja ya msingi ya kuondoa kipengele hicho kwani uzoefu unaonesha kuwa baada ya Serikali kukiondoa, makundi yenye mwelekeo maalumu hutumia nafasi hiyo kutoa takwimu za idadi ya Waislamu, Wakristo na Wapagani.

      Pamoja na kauli ya Wasira, Mkurugenzi Mkuu wa NBS, Dk Albina Chuwa, alikataa ombi la mashehe la kujumuisha kipengele cha dini katika dodoso za maswali wakati wa sensa. Alisisitiza mbele ya viongozi wa dini mbalimbali wakiwemo mashehe kuwa maswali yanayohusu kabila na dini hayatajumuishwa kwenye dodoso kwani Serikali haipangi mipango ya maendeleo ya wananchi kwa kufuata itikadi za kidini au ukabila.

      CHANZO: HabariLeo
      takashi and Lokissa like this.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Kituko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th January 2009
      Posts : 3,717
      Rep Power : 1288
      Likes Received
      499
      Likes Given
      175

      Default Re: BAKWATA haitoshiriki zoezi la Sensa mwaka huu......!!

      Jamani, mbona sensa za Kidini ni raisi mno kuzifanya, Kama kuna dini ama dhehebu inataka kujua ina waumini wangapi kuna shida gani ya kujihesabu kwenye masinagogi na mahekalu yao?

      Issue ya Dini na wala ukabila hauna umuhimu wowote kwenye sensa, tukishajua idadi ya dini fulani ndio wengi itasaidia nini?, maana tukisema wapewe upendeleo walio wengi (Kidini) na Wasukuma nao watataka upendeleo kwa sababu nao watasema wapo wengi na hawana uwakilishi wenye uwiano

      Kwa nini Bakwata wasitafute njia ya kuwekeza kwenye mambo ya Kijamii, (shule, Vyuo, Mahospital nk)?

    4. #3
      asigwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2011
      Location : TANDHANIYA
      Posts : 4,389
      Rep Power : 1265
      Likes Received
      1210
      Likes Given
      1253

      Default Re: BAKWATA haitoshiriki zoezi la Sensa mwaka huu......!!

      kama hawataki tutawakadiria tu kama mafungu ya nyanya...
      wao kila siku ni negative ishues kwa kisingizio cha dini tu hawana chema???
      Lokissa and tedo like this.

    5. #4
      Ndahani's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd June 2008
      Location : Somewhere
      Posts : 9,647
      Rep Power : 4016
      Likes Received
      2940
      Likes Given
      5063

      Default Re: BAKWATA haitoshiriki zoezi la Sensa mwaka huu......!!

      Thanks...nini tena kitasusiwa baada ya sensa?
      We are all inventors, each sailing out on a voyage of discovery, guided each by a private chart, of which there is no duplicate. The world is all gates, all opportunities.
      Ralph Waldo Emerson

    6. #5
      Bajabiri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 9,741
      Rep Power : 2885
      Likes Received
      1115
      Likes Given
      52

      Default

      Quote By mzee wa njaa
      BAKWATA haitoshiriki zoezi la Sensa mwaka huu......!!

      Sababu ni kwamba hakuna kipengele cha DINI kitu ambacho ni dhambi na kinyume cha maadili ya Uislam...

      Nawauliza wadau kwa mujibu wa sheikh huyo ni kweli hilo suala dini kutohusishwa kwenye sensa ni dhambi kwa Uislam?????

      KUna ukweli wowote?

      Source: TV Sibuka. Taarifa ya Habari leo.
      suala la sensa lenyewe kwa ujumla wake halina tija sembuse kuweka kipengele cha dini
      Lokissa likes this.

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      Lokissa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2010
      Location : Goba
      Posts : 4,094
      Rep Power : 5808
      Likes Received
      1026
      Likes Given
      2876

      Default Re: BAKWATA haitoshiriki zoezi la Sensa mwaka huu......!!

      baadae watasema kama rais,makamu na mawaziri wajao wasipokuwa waislamu watahama nchi
      na watataka nchi ifuate mfumo wa sharia
      wanadhani JK atawapigia magoti kuwaomba washiriki.
      tutawakadiria tunajua idadi yao haizidi 40% ya watanzania wote.
      HAKUNA KUWAENDEKEZA HAWA KAMA WANATAKA WAHAMIE SOMALIA AU UARABUNI
      tedo and ha ha ha like this.
      You may know me but you have no Idea who I am !

    9. #7
      meningitis's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th November 2010
      Location : sewahaji
      Posts : 2,918
      Rep Power : 3207
      Likes Received
      1014
      Likes Given
      149

      Default Re: BAKWATA haitoshiriki zoezi la Sensa mwaka huu......!!

      sensa ni ya raia wa tanzania sio bakwata,kwani bakwata wako wangapi?tukijua bakwata ni wangapi itatusaidia nini kwa maendeleo?
      Lokissa likes this.

    10. #8
      MwalimuZawadi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st September 2007
      Posts : 623
      Rep Power : 723
      Likes Received
      50
      Likes Given
      3

      Default Re: BAKWATA haitoshiriki zoezi la Sensa mwaka huu......!!

      Quote By Bajabiri
      suala la sensa lenyewe kwa ujumla wake halina tija sembuse kuweka kipengele cha dini
      Kweli? ...buffalo soldier... the hypocrites...
      Sent from my Nokia rinGo using JamiiForums

    11. #9
      tedo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th August 2011
      Location : uchochoroni
      Posts : 5,504
      Rep Power : 4640
      Likes Received
      1260
      Likes Given
      880

      Default Re: BAKWATA haitoshiriki zoezi la Sensa mwaka huu......!!

      Hiki kizazi cha Eshumaili kina tabu sana....... anyway tutafanyaje sasa inabidi tukaenao hivo hivo tuu labda kuna siku watabaadilika.

    12. #10
      Bob G's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 5th October 2011
      Location : UK Manyasi
      Posts : 1,661
      Rep Power : 718
      Likes Received
      291
      Likes Given
      36

      Default Re: BAKWATA haitoshiriki zoezi la Sensa mwaka huu......!!

      Sensa ni kazi ya serikali Bakwata inahusikaje? Kama Bakwata wanataka kujua waumini wao kwanini wasiwahesabu? Mbona Wakristo wanajihesabu kila siku ya IBADA

    13. #11
      Bob G's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 5th October 2011
      Location : UK Manyasi
      Posts : 1,661
      Rep Power : 718
      Likes Received
      291
      Likes Given
      36

      Default Re: BAKWATA haitoshiriki zoezi la Sensa mwaka huu......!!

      Sema wewe Kituko labda watakusikia hawa, maana kila kukicha ni malalamiko ova walikua wamezibwa mdomo na Super glew sa imebanduka. Tunalo!

    14. #12
      Matola's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th October 2010
      Posts : 12,516
      Rep Power : 19751
      Likes Received
      5449
      Likes Given
      3641

      Default Re: BAKWATA haitoshiriki zoezi la Sensa mwaka huu......!!

      Hii Habari siwezi kuiamini haina ukweli wowote, Bakwata ni tawi la CCM sasa ni kitu ambacho hakiwezekani kupingana na Serikali yao wanayoitumikia, kama kuna kauli ya namna hii imetolewa basi itakuwa ni ya yule muhuni anayeitwa Shekh Ponda ambaye yuko kwenye jumuiya nyingine ambayo haina tofauti na UAMSHO.
      Division four point 29 = Masters Mzumbe University. Nape Nnauye is my role model.

    15. #13
      ha ha ha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th December 2011
      Location : Hapahapa
      Posts : 456
      Rep Power : 466
      Likes Received
      45
      Likes Given
      71

      Default Re: BAKWATA haitoshiriki zoezi la Sensa mwaka huu......!!

      i think ubwabwa..
      Quote By Ndahani
      Thanks...nini tena kitasusiwa baada ya sensa?
      "If you find yourself in ahole, the first thing to do is stop digging"



    16. #14
      Daudi Mchambuzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th November 2010
      Posts : 6,207
      Rep Power : 2625
      Likes Received
      3000
      Likes Given
      13654

      Default

      An empty head is devil's workshop.

      Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
      Oluoch likes this.

    17. #15
      David webb's Avatar
      Member Array
      Join Date : 20th November 2011
      Posts : 56
      Rep Power : 390
      Likes Received
      22
      Likes Given
      16

      Default re: BAKWATA yatangaza rasmi waislam kugomea sensa!

      Sensa ya mwaka 1957 ya kikoloni kipengele cha kuonesha dini kilikuwepo na ndio kinachoonesha takwimu waislamu wangapi na wakristo wangapi, na ukiangalia mwaka huo 1957 waislamu walikuwa ni 65%.

      Baada ya hapo sensa zote zilizofuata kipengele cha dini kilifutwa; ajabu leo hii watu wanasema wakristo wapo wengi kuliko waislamu kwa takwimu zipi ikiwa kipengele cha kuorodhesha watu dini zao hakipo.

      Pili ni kwanini wanaogopa kuhesabu watu kwa kutumia kigezo cha dini? Wengi watasema wanaogopa udini, hii hoja ni dhaifu maana nchi nyingi duniani sensa zinahebabiwa kwa mtindo wakujua idadi ya watu na dini zao ni asilimia ngapi katika nchi hizo.

    18. #16
      Sideeq's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th December 2009
      Posts : 1,603
      Rep Power : 800
      Likes Received
      213
      Likes Given
      0

      Default re: BAKWATA yatangaza rasmi waislam kugomea sensa!

      Ninatumaini kuwa maamuzi ya Waislamu yataheshimiwa katika nchi ya Kidemokrasia kama Tanzania.

    19. #17
      Shine's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th February 2011
      Posts : 9,197
      Rep Power : 2431
      Likes Received
      948
      Likes Given
      378

      Default

      Quote By Sideeq
      Ninatumaini kuwa maamuzi ya Waislamu yataheshimiwa katika nchi ya Kidemokrasia kama Tanzania.
      Maamuzi ya kupinga sensa? Itakuwa ni ujinga usiopingika kama unakuwa ni mnafiki wa mambo yenye maendelea bila sababu yeyote ya msingi ntashindwa hata kuwashangaa na hata wewe unaewasapot
      Jasusi, MIGNON, andate and 2 others like this.

    20. #18
      Jasusi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th May 2006
      Posts : 10,626
      Rep Power : 2894
      Likes Received
      3845
      Likes Given
      12256

      Default re: BAKWATA yatangaza rasmi waislam kugomea sensa!

      Quote By David webb
      Sensa ya mwaka 1957 ya kikoloni kipengele cha kuonesha dini kilikuwepo na ndio kinachoonesha takwimu waislamu wangapi na wakristo wangapi, na ukiangalia mwaka huo 1957 waislamu walikuwa ni 65%.

      Baada ya hapo sensa zote zilizofuata kipengele cha dini kilifutwa; ajabu leo hii watu wanasema wakristo wapo wengi kuliko waislamu kwa takwimu zipi ikiwa kipengele cha kuorodhesha watu dini zao hakipo.

      Pili ni kwanini wanaogopa kuhesabu watu kwa kutumia kigezo cha dini? Wengi watasema wanaogopa udini, hii hoja ni dhaifu maana nchi nyingi duniani sensa zinahebabiwa kwa mtindo wakujua idadi ya watu na dini zao ni asilimia ngapi katika nchi hizo.
      Sensa ya mwaka 1957 haikuonyesha idadi ya Waislamu kuwa 65%. Pia kuna sensa iliyofuata 1967 pia ina takwim inayoonyesha idadi ya Waislamu na Wakristo. Kwa hiyo si sahihi unaposema kuwa baada ya 1957 sensa zote zilizofuata zilifuta kipengele kinachoonyesha dini za watu.

    21. #19
      Mgongo wa paka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd October 2011
      Posts : 397
      Rep Power : 465
      Likes Received
      23
      Likes Given
      0

      Default re: BAKWATA yatangaza rasmi waislam kugomea sensa!

      ni vizuri sana kwanini utoe kipengele cha dini?
      mwongozo likes this.

    22. #20
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,269
      Rep Power : 3568
      Likes Received
      3074
      Likes Given
      464

      Default re: BAKWATA yatangaza rasmi waislam kugomea sensa!

      yeah Waislamu walikuwa wengi, Msisahau pia Wapagani au Wanaoamini Dini za kienyeji walikuwa wengi sana...

    Page 1 of 62 12311 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...