WANA FORUM TUWE WAUNGWANA NA TUJADILI KISOMI BILA UNAFIKI!!!!!!!!!!!!!!!!
Tuna zaidi ya wiki moja tunajadili suala la sensa na kipengele cha dini. naomba niulize kisha nijibu maswali yafuatayo;
1- Sensa ni nini?
sensa ni zoezi la kuhesabu watu wakazi katika eneo husika likisimamiwa na chombo halali kilicho na dhamana ya kufanya hivyo. Aghalabu, sensa ya kitaifa hufanyika kila baada ya miaka kumi.
2- Lengo la sensa ni nini?
Lengo kuu la sensa ni kujua idadi ya watu kiumri, kijinsia, kimakzi ktk eneo husika, kikazi(ajira) na kidini (hapa ndiyo penye utata)
3-Kipengele cha dini kiliwahi kuwekwa kwenye dodoso ya sensa hapa nchini?
ndiyo. sensa za mwaka 1957 na 1967 zilikua na kipengele cha dini
4-Kipengele hicho cha dini kilichangia kuvunja amani nchini?
hapana hakijawahi kusababisha uvunjifu wa amani kwa kuwekwa kwenye sensa?
5- Kwa nini kiliondolewa? na nani?
sababu hazijulikani lakini nadhani rais wa kwanza alikiondoa ktk dodoso ya sensa ya tatu 1977 kwa kuhofia jambo moja. Sensa zote mbili zilionesha Waislamu ni wengi hapa nchini. hali halisi ikaonesha kuwa Waislamu ni wachache sana katika ajira za sekta ya umma (serikalini). ikumbukwe kuwa Waislamu waliogopa kupeleka watoto wao katika shule za kikoloni (wazungu) wakihofia watabadilishwa dini. hali hii ikafanya idadi ya wasomi waislamu kuwa ndogo. Mwalimu Nyerer hakuzuia Waislamu kusoma. ni khofu wa wazee wenyewe wa Kiislamu. naweza kusema walikosea na kwa upande mwengine walikua sahihi. Vile mwalimu alikua mwana saikolojia, aliona HATARI ya kuwa na watu wengi hapa nchini wenye asilimia kiduchu ktk idara za serikali. JAMBO LA KWANZA, BILA KULISHAURI BUNGE, MWL AKAAGIZA KIMYAKIMYA KIONDOLEWE KIPENGELE CHA DINI KTK SENSA.
simlaumu mwalimu katika hili. ALITAKA KULINDA UMAJO WA NCHI. narudia tena. ni wazee wenyewe wa kiislamu ndiyo walihofia watoto wao kubadilishwa dini wakisomesha ktkt shule za misheni.
kama mnavoelewa, mtu akiwa na cheo ofisini, anapopata habari ya ajira HUMFAHAMISHA NDUGU YAKE AU JAMAA WA KARIBU AU RAFIKI YAKE. bila kutarajiwa, kadri miaka ilivyozidi, wakristo wakawa wameshamiri maofini kwa asilimia kubwa sana. NAMLAUMU BABA WA TAIFIA KWA JAMBO MOJA. baada ya kugundua hatari iliokuepo, angejitahidi kufanya mkakati maalumu wa kuwasomesha waislamu wachache na kuwasimika ktk ajira ya umma ili kulazimisha ongezeko la idadi yao. nadhani hili hakulifanya! hali imeendelea hivyo hadi hii leo.
6-KWA NINI AKINA PONDA WANALALAMIKA?
sasa hivi ukienda kwenye ofisi za serikali kama TRA, VYEO VYA JUU POLISI (kuwepo said mwema juu kabisa siyo kigezo tosha), VYEO VYA JUU JESHINI, WIZARA ZOTE ZA SERIKALI .... nk utakuta ofisi zimekaa kama parokia fulani. wakristo watupu (najua hili kwa wakristo ama hawasilioni au wanaliona na wanalijua). wapo waislamu ambao wamesoma (japo hawajawafikia wakristo) lkn waislamu walio wengi wanapata rizki katika biashara, muziki, mpira, uvuvi, kilimo, umachinga na kazi ngumu kama kusukuma mikokoteni na kubeba mizigo (hawajui wala kunusa WHITE COLAR JOBS). vijana wengi wa kiislamu wnabwiya unga. wanaishia la saba! kaka zao wanashindwa kuwasaidia kwa SABABU HAWAMO SERIKALINI. HAWANA MSHAHARA WA MWISHO WA MWEZI. wasomi waislamu hili wanaliona na wanalijua. AKINA PONDA WANAONA ILI UNFAIR TREATMENT iliyokuepo kipindi cha mwalimu imetapakaa na kukua hadi hii leo. kwa anae jua maana ya govt adminstrtve strcture pamoja na local gvt system, hawezi kuema ooohhh mbona rais na makamu ni waislamu? thats nothing! kwenye wizara na halmashauri nchini waislamu ni chini ya asilimia 9. hawakutaka wenyewe. serikali kama mzazi haikuweka mkakati wa kukosoa kosa lililofanywa na wazee kuogopa shule za kimisheni (sina uhakika kama ni kosa kwa sababu kweli baadhi walibadilishwa au walilazimika kutumia majina ya kikristo ili wakasome. bob makani ni mmoja wao).
7-MADAI YA PONDA NI YAPI?
ponda anasema "enough is enough. tutumie sensa kama gia ili tujue idadi kisha yaje madai ya kuuliza mbona waislamu ni asilimia 35, 40 50 au 55 lakini kwenye ajira asilimia 9!!!!!!!?" NI BOMU AMBALO LIPO NA LITAPASUKA. NATABIRI KUWA kama kipengele cha dini hakitawekwa, waislamu watatafuta haki ya uwiano kiajira kwa njia ambazo zitavunja amani.
USAHURI WANGU
NI wakati muafaka tuache kuweka majivu kwenye moto tukidhani umezimika. UKWELI NI KWAMBA KIJANA WA KIISLAMU ANAPOKWENDA SERIKALINI KUOMBA KAZI, hujihisi kwa anakwenda parokiani. na akitaja jina la kiislamu, huangaliwa na walakini. hili jambo linawasononesha waislamu kuwa hivyo katika nchi yao licha ya kupigania UHURU WA NCHI HII NA KUMPOKEA NYERERE DSM NA KUMKABIDHI TAA KISHA TANU
nimeandika kwa nia njema. nitafurahi nikijibiwa kwa hoja bila ya ushabiki wa kidini wala matusi
Follow Us Here