Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Tuhuma za uchomaji wa makanisa, BAKWATA wamjia juu askofu laizer

    Report Post
    Results 1 to 18 of 18
    1. #1
      BigMan's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th February 2007
      Posts : 533
      Rep Power : 733
      Likes Received
      57
      Likes Given
      10

      Default Tuhuma za uchomaji wa makanisa, BAKWATA wamjia juu askofu laizer

      BARAZA kuu la waislam nchini, BAKWATA, Mkoa wa Arusha, limemtaka Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kirutheri KKKT Dayosisi ya mkoani Arusha,Thomas Lazier, kuthibitisha madai yake aliyoyatoa hivi karibuni katika Vyombo vya habari ya kuwepo Vijana zaidi ya 300 wanaofanya mazoezi kwa ajili ya kuchoma makanisa na kuharibu mali mbalimbali zinazomilikiwa na makanisa mkoani Arusha vinginevyo Bakwata, itachukua hatua zinazostahili dhidi ya madai hayo.


      Kauli hiyo imetolewa na Shekh, wa Bakwata Mkoa wa Arusha, Shaaba Juma,alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari kufuatia taarifa zilizoandikwa katika vyombo vya habari hivi karibuni zikimnukuu AskofuThomas Laizer, wa KKKT, akiwatuhumu Vijana zaidi ya 300, wa kiislam kuwa wanakusanyika kila siku na kufanya mazoezi ya Karate,kwa kujiandaa kuchoma na kuharibu makanisa mkoani Arusha.


      Shekh, Shaaban amesema Bakwata imeshitushwa na taarifa hizo za kuwepo kundi laVijana 300 wa kiislam,wanaofanya mazoezi ya Karate, katika msikiti ambao hakuutaja jina lake aliodai kuwa upo katika Eneo la Unga limited jijini Arusha, wanaofanya mazoezi kwa ajili ya kuchoma makanisa na kuharibi mali mbaklimbali zinazomilikiwa na makanisa..


      Alisema kuwa mara baada ya kupata taarifa hiyo ya kusikitisha, aliitisha kikao na Mashekh , Maimam na walimu wa madrasa katika kata ya Unga limited ambapo viongozi hao walisikitishwa na taarifa hiyo ambayo walisema haina ukweli wowote na kama Askofu huyo anao ushahidi wakamtaka kutoa taarifa hiyo kwenye vyombo vya Ulinzi na Usalama ili ifanyiwe kazi.


      Shekh Shaaban, alisema kuwa amewasiliana na mkuu wa mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, ambae wamekubaliana kukutana siku ya Jumatano Julai 13 mwaka huu ili Askofu, huyo aweze kutoa ufafanuzi wa madai yake hayo mbele ya viongozi wa Dini na Serikali ili kupata ukweli wa madai hayo .


      “Mimi Shekh wa mkoa sina taarifa hizo ninaona taarifa hii ni ya hatari, inayolenga kuchafua Uislam na Waisam, nimefuatilia sijaona ukweli wowote kuhusu madai hayo, Kauli ya Askofu haifai kupuuzwa hata kidogo kwa sababu imetolewa na kiongozi mkubwa wa Kanisa” alisema Shehk shaaban.


      Shekh, shaaban, alisisitiza kwamba hakuna msikiti wenye Vijana 300 kama inavyodaiwa na Askofu huyo, wanaofanya mazoezi ya Karate,kwa ajili ya kuyachoma moto makanisa,na kufanya uharibifu wa mali kauli hiyo inalenga kuchonganisha Waislam na Wakiristo na serikali yao na hivyo kujenga Taswira mbaya dhidi ya Dini Kiislam.


      Akasisitiza kuwa Waislam na wasiokuwa waislam siku zote wameishi kama ndugu hivyo kauli hiyo isitumike kujenga fitina ya kuwagombanisha wananchi na kuvuruga amani na utulivu uliopo hapa nchini ambao umedumu kwa miaka mingi kwa kutambua kuwa kila mmoja ana uhuru wa kuabudu dini aitakayo.hivyo kama anazo taarifa sahihi aziwasilishe kwenye vyombo vya dola alisisitiza shehkh Shaaban.


      Hivi karibuni magazeti ya Habari leo la juni 4 na An –Nuur ya Ijumaa Juni 8 yenye vichwa vya habari tofauti yalimnukuu Askofu Laizer,ambapo gazeti la Habari leo liliandika Uamsho waibukia Dar es Salaam, wakati gazeti la An –Nuur ,likiandika Askofu Laizer, anawajua waliochoma moto makanisa hata hivyo baadhi ya viongozi wa makanisa wakiwemo mapadri, wamesema madai ya Askofu huyo yatapelekea kuwachonganisha waislam na dini zingne i kwa kuwa hakuifanyia utafiti.


      SOURCE: NIMEIKUTA KATIKA BLOG YA MWANDISHI WA HABARI WA NIPASHE INAYOFAHAMIKKA KAMA LIBENEKE LA KASKAZI
      zomba likes this.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Tume ya Katiba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2012
      Location : Chumbuni-Zanzibar
      Posts : 2,675
      Rep Power : 0
      Likes Received
      537
      Likes Given
      273

      Default re: Tuhuma za uchomaji wa makanisa, BAKWATA wamjia juu askofu laizer

      Great Shekhe.

      Laziwa tuwape nidhamu hawa viongozi wa dini wanaochonganisha waumini.

      Too bad
      zomba likes this.

    4. #3
      S.Liondo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th April 2011
      Posts : 338
      Rep Power : 476
      Likes Received
      55
      Likes Given
      6

      Default re: Tuhuma za uchomaji wa makanisa, BAKWATA wamjia juu askofu laizer

      Nampongeza sheik Shabani kwa kufuatilia ili kuhakikisha kama hali hii inayosemwa na askofu ipo au la, ikiwa ni pamoja na kuvishauri vyombo vya dola kushughulikia hilo. Ninaamini atakuwa tayari kutoa ushirikiano wa kutosha endapo hali hiyo itabainika kuwa ni kweli. Hali kadhalika, ninaamini askofu laizer atakuwa tayari kuwajibika kwa alichokisema endapo itakuwa si kweli.
      zomba likes this.

    5. #4
      Nyakageni's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st February 2011
      Posts : 5,236
      Rep Power : 1538
      Likes Received
      765
      Likes Given
      52

      Default Re: Tuhuma za uchomaji wa makanisa, BAKWATA wamjia juu askofu laizer

      udini unamea kwa kasi!

    6. #5
      sweke34's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th September 2010
      Posts : 2,493
      Rep Power : 1254
      Likes Received
      734
      Likes Given
      1240

      Default Re: Tuhuma za uchomaji wa makanisa, BAKWATA wamjia juu askofu laizer

      Quote By Tume ya katiba
      Great Shekhe.

      Laziwa tuwape nidhamu hawa viongozi wa dini wanaochonganisha waumini.

      Too bad
      Kauli ya Askofu haifai kupuuzwa hata kidogo kwa sababu imetolewa na kiongozi mkubwa wa Kanisa
      Kauli chafuchafu za akina Ponda/Basaleh/Ilunga huwa zimetolewa na viongozi wadogo wa misikiti kwa hiyo haziihitaji kuthibitishwa?
      zumbemkuu and mkufunzi wa uma like this.

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      DOUGLAS SALLU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th November 2009
      Posts : 3,598
      Rep Power : 1285
      Likes Received
      315
      Likes Given
      894

      Default Re: Tuhuma za uchomaji wa makanisa, BAKWATA wamjia juu askofu laizer

      Uchoche unaofanywa na magazeti yenu ya al nur,alhuda na redio imani mnaona sawa tu, wacheni hizo Tanzania ni ya wote Waslamu,Wakristo, waabudu mizimu na wasiokuwa na dini. Wacheni kucheza ngoma ya CCM ya kutugawa ili waendelee kutufisadi.

    9. #7
      Mdondoaji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th March 2009
      Posts : 4,722
      Rep Power : 1483
      Likes Received
      807
      Likes Given
      341

      Default Re: Tuhuma za uchomaji wa makanisa, BAKWATA wamjia juu askofu laizer

      Quote By DOUGLAS SALLU
      Uchoche unaofanywa na magazeti yenu ya al nur,alhuda na redio imani mnaona sawa tu, wacheni hizo Tanzania ni ya wote Waslamu,Wakristo, waabudu mizimu na wasiokuwa na dini. Wacheni kucheza ngoma ya CCM ya kutugawa ili waendelee kutufisadi.
      Si kama propaganda zenu za magazeti ya msemakweli, na mengineyo dhidi ya uislamu pamoja na TV na redio zenu ambazo zimeshadidia propaganda ya kuchomwa makanisa hali ya kuwa wachomaji ni nyie wenyewe. Mlishazoea sana kuwa hii nchi ya kikristo wakati hii nchi yetu sote sasa wacheni moto uwake
      zomba, mfumo and mkufunzi wa uma like this.

    10. #8
      twatwatwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th September 2011
      Posts : 838
      Rep Power : 554
      Likes Received
      94
      Likes Given
      3

      Default Re: Tuhuma za uchomaji wa makanisa, BAKWATA wamjia juu askofu laizer

      Wamezoea kuzusha hao sasa atatafuta pa kujificha
      zomba and mkufunzi wa uma like this.

    11. #9
      Mlitika's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd March 2012
      Posts : 404
      Rep Power : 516
      Likes Received
      220
      Likes Given
      314

      Default Re: Tuhuma za uchomaji wa makanisa, BAKWATA wamjia juu askofu laizer

      Mods ondoeni hii kabla hamjatulima ban wenye haki ya kukasirika kutokana na uchokozi uliotuchosha wa mashetani hawa! ONDOA HII PLZ!
      zumbemkuu likes this.

    12. #10
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14620
      Likes Received
      2841
      Likes Given
      1961

      Default Re: Tuhuma za uchomaji wa makanisa, BAKWATA wamjia juu askofu laizer

      Haya makanisa ndio yalikuwa kichocheo cha mauaji ya kimbari huko Rwanda. Huyu Askofu inabidi aoneshe ushahidi wa kauli zake.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    13. #11
      Bob G's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 5th October 2011
      Location : UK Manyasi
      Posts : 1,653
      Rep Power : 715
      Likes Received
      289
      Likes Given
      36

      Default Re: Tuhuma za uchomaji wa makanisa, BAKWATA wamjia juu askofu laizer

      Kwani serikali nayo imewakamata waliochoma makanisa? Bakwata hawana uwezo wa kumlazimisha Askofu Laizer Kuthibitisha, wao ndo wenyejukumu la kuwakamata waislamu wenzao waliochoma makanisa na kupora bia na kunywa

    14. #12
      TZ biashara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th March 2012
      Posts : 513
      Rep Power : 531
      Likes Received
      98
      Likes Given
      224

      Default Re: Tuhuma za uchomaji wa makanisa, BAKWATA wamjia juu askofu laizer

      Viongozi wa dini wanahatarisha amani katika nchi hii na wanajua kama kusema uongo ni dhambi kwasababu itakuja kuchafua hali ya hewa na itamgusa kila mwananchi.Sisi wananchi hatujui kutafakari na kujiuliza ila tunaona ufahari kuingia ktk ugonjwa mbaya au sumu kali ya ubaguzi.Mwenyezi mungu atuepushe na majanga kwasababu jipu likipasuka basi ujue usaha na damu lazima zitatoka.

      GOD BLESS TANZANIA

    15. #13
      Omulangi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th February 2008
      Posts : 726
      Rep Power : 720
      Likes Received
      132
      Likes Given
      8

      Default Re: Tuhuma za uchomaji wa makanisa, BAKWATA wamjia juu askofu laizer

      Quote By sweke34
      [SIZE=3]
      Kauli chafuchafu za akina Ponda/Basaleh/Ilunga huwa zimetolewa na viongozi wadogo wa misikiti kwa hiyo haziihitaji kuthibitishwa?
      Katika kuhitimisha mizunguko ya kongamano za ki islamu mikoa yote Shehe Ilunga pale Diamond Jubilee aliwataka waislamu kote waliko kuacha kulalamika na badala yake kuanza kuwashughulikia viongozi wa kikristo, taasisi zao na maslahi yao mbali mbali popote yalipo. Alisema viongozi wa kiislamu wanabaki na jukumu moja tu la kushughulika na yatakayo tokana na kushughulika kwao. Alisema wanachoweza kushughulikia viongozi ni kama kutafuta mawakili n.k alitoa mifano ya sehemu ambazo waislamu tayari wameshughulika kuwa ni Mwanza (uchomaji wa makanisa) Mto wa Mbu (kuuwa kwa wachungaji 2) na Morogoro kwenye shule ya sekondari. Swali ni je unaweza kuchoma makanisa na taasisi za kikristo na kuua watumishi wa Mungu bila mazoezi ya awali?? aulizwe Shehe Ilunga anaweza kutoa ufafanuzi mzuri zaidi kuliko Laizer
      Mrdash1 likes this.

    16. #14
      Omulangi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th February 2008
      Posts : 726
      Rep Power : 720
      Likes Received
      132
      Likes Given
      8

      Default Re: Tuhuma za uchomaji wa makanisa, BAKWATA wamjia juu askofu laizer

      KENYA: TWO CHRISTIAN PASTORS BURNED TO DEATH AFTER VISITING MUSLIM FAMILY [Excerpts]

      "The umbrella body of evangelical churches and a human rights organization have condemned the lynching of two pastors at Jomvu in Mombasa early this week.

      Federation of Evangelical and Indigenous Christian Churches of Kenya asked the police to pursue the case up to the end, with the culprits arrested and charged in court.

      On Thursday, the federation's national chairman, Mr Joseph Methu, said punishment of killers of the two clerics in a case of mistaken identity should be used as an example to those who spearhead crime.

      "Time has come for the government to enforce the law and bring to book those who participated in the act that saw innocent pastors on a preaching mission burnt to death," said Mr Methu...

      As police continue with their investigations, there are conflicting reports by the church and Jitoni residents in Jomvu, where the two pastors were lynched.

      The pastor in charge of Melchidizek Church, Mr Samuel Wainaina, said the owner of the home the clerics visited was converted into a Christian a few weeks.

      His family, however, dismissed the conversion claim.

      Ms Mapenzi Abdalla, one of the members of Mr Mutana Nyandu's family, said they were all Muslims and no one had converted to Christianity as claimed by Pastor Wainaina.

      (Anthony Kitimo, [Kenya] Daily Nation, 5/17/2012)

    17. #15
      sweke34's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th September 2010
      Posts : 2,493
      Rep Power : 1254
      Likes Received
      734
      Likes Given
      1240

      Default Re: Tuhuma za uchomaji wa makanisa, BAKWATA wamjia juu askofu laizer

      Quote By Omulangi
      Katika kuhitimisha mizunguko ya kongamano za ki islamu mikoa yote Shehe Ilunga pale Diamond Jubilee aliwataka waislamu kote waliko kuacha kulalamika na badala yake kuanza kuwashughulikia viongozi wa kikristo, taasisi zao na maslahi yao mbali mbali popote yalipo. Alisema viongozi wa kiislamu wanabaki na jukumu moja tu la kushughulika na yatakayo tokana na kushughulika kwao. Alisema wanachoweza kushughulikia viongozi ni kama kutafuta mawakili n.k alitoa mifano ya sehemu ambazo waislamu tayari wameshughulika kuwa ni Mwanza (uchomaji wa makanisa) Mto wa Mbu (kuuwa kwa wachungaji 2) na Morogoro kwenye shule ya sekondari. Swali ni je unaweza kuchoma makanisa na taasisi za kikristo na kuua watumishi wa Mungu bila mazoezi ya awali?? aulizwe Shehe Ilunga anaweza kutoa ufafanuzi mzuri zaidi kuliko Laizer
      Uzao wa 'kijakazi' unasikitisha sana...

    18. #16
      Mngendalyasota's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 22nd January 2011
      Posts : 138
      Rep Power : 449
      Likes Received
      40
      Likes Given
      0

      Default Re: Tuhuma za uchomaji wa makanisa, BAKWATA wamjia juu askofu laizer

      Quote By sweke34
      Uzao wa 'kijakazi' unasikitisha sana...
      Ila ni hatari. MUNGU HUYU BWANA ALIUMBA WANADAMU NA KUWATOFAUTISHA KIFIKRA ILI WATAMBUE MEMA NA MABAYA!

    19. #17
      Ngalikihinja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st September 2009
      Posts : 4,393
      Rep Power : 1440
      Likes Received
      976
      Likes Given
      96

      Default

      Quote By Mdondoaji
      Si kama propaganda zenu za magazeti ya msemakweli, na mengineyo dhidi ya uislamu pamoja na TV na redio zenu ambazo zimeshadidia propaganda ya kuchomwa makanisa hali ya kuwa wachomaji ni nyie wenyewe. Mlishazoea sana kuwa hii nchi ya kikristo wakati hii nchi yetu sote sasa wacheni moto uwake
      Wa jino kwa jino utawajuwa tu

    20. #18
      Mdondoaji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th March 2009
      Posts : 4,722
      Rep Power : 1483
      Likes Received
      807
      Likes Given
      341

      Default Re: Tuhuma za uchomaji wa makanisa, BAKWATA wamjia juu askofu laizer

      Quote By Ngalikihinja
      Wa jino kwa jino utawajuwa tu
      Kwani wana tofauti gani na wa sumu kwa sumu? Mnaleta propaganda zenu hapa mnadhani hatuwaelewi? Kizazi cha dot com kitawatoa jasho subirini tu!

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...