Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

    Report Post
    Page 6 of 13 FirstFirst ... 45678 ... LastLast
    Results 101 to 120 of 254
    1. #1
      Eng. Y. Bihagaze's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 8th September 2011
      Location : Czech(but now in DAR)
      Posts : 769
      Rep Power : 5117
      Likes Received
      584
      Likes Given
      111

      Default Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%



      Kauli aliyoitoa Dr Slaa wakati wa vuguvugu la kampeni za kisiasa kwamba mfuko wa sement utakuwa Tshs 5,000, badala ya Tshs16,500 kwa sasa kwa wakazi wa DSM na zaidi ya Tshs18,000 kwa wakazi wa nje ya mji huu, nimekuwa nikizitafakari kwa kina sana kwa muda mrefu. Kutokana na Uzoefu wangu wa masuala machache alonijalia mola, nilioona kama ni sentensi ya kisiasa zaidi ya kimatendo, lakini sasa nakiri ni sentenSi makini na ya kweli. Na si 5000 tu bali pia 2,500 au 3000 kwa mfuko wa 50kgs.

      Hivi majuzi, nilikuwa namsikiliza Waziri Viwanda na Biashara Dr. Kigoda akizungumzia masuala ya Kiuchumi kwenye kipindi cha TBC asubuhi. Kauli aliyotoa Abdala Kigoda ilinifanya kile kisifa cha kuitwa Dr nikiondoe haraka na natamani nikiingia ofisini kwake nimwite Mr Abdala. Mkongwe Huyu adui mkubwa wa mabango ya “sigara ni hatari kwa Afya yako” alisema , ‘AMESIKIA” wafanya biashara wa hapa wakimweleza kwamba bei ya mfuko wa sement inayouzwa hapa ni ghali sana kulinganisha na bei ya mfuko utaouagiza kutoka India.”

      Nikawaza kama mzee huyu, waziri wetu amesikia tu, ameshindwa kufanya tathimini kutumia ziada kidogo ya akili yake iliyompelekea kuitwa DR, kwamba kama hali iko hivyo kwa India km 4,600 tu kutoka TZ, sawa na kwenda kigoma na kurudi dsm mara mbili, ana mipango gani mbadala ya kuhakikisha na hapa kwetu unafuu wa neema unaonekana kwenye gharama ya mifuko ya cement, watu tukajenga?

      Sentensi yake hiyo ilinisukumia na kuamsha mawazo yale niliyokuwa nayo awali aliyoyasema Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CHADEMA Dr Wilbroad Slaa-2010, kwamba Bei ya sement ni ghali sana, Serikali yake itaipunguza hadi kufikia Tsh5,000. Na hapo ndipo nilipoona nifanye kauchunguzi kadogo sana ambako mdau wa jamvi unaweza kunikosoa lakini uwezo wa kuchunguz kwangu ndipo ulipofikia..

      Cha kwanza nikawapigia “madalali wa wagonjwa” (india kuna watu kazi yao ni udalali wa wagonjwa, wanatengeneza dili zao kwa kuwasaka wagonjwa kutoka kwenye nchi zao kama Africa na hata penginepo kupitia mashirika mengi kama LIONS CLUB na mengineyo na kuwa connect na daktari husika na kufanya protocal zote za maandalizi na ndivyo nao wanavyopata kula ..anyway that is not ma topic)..nikawauliza wanitajie bei ya mfuko wa sement kwenye soko la kawaida .. baada ya muda wakaniambia ni Rupia 230. Rupia moja ni sawa na Tsh28.

      Kwa hiyo mfuko mmoja wa Kg 50 wa sement kule India ni sawa na Tsh 6,440 (28 x 230). Kwa Kontena la 20ft lina uwezo wa kuchukua tani 35-40, lakini meli nyingi zina standard ya kujaza 40ft kwa tani 20 tu. Sasa tani 20 ni mifuko 400 a cement. Kwa bei ya meli zinazosafirisha 40ft kwa 20ton ni dolar 400 (sawa na tzs 632,000 (1,580 x 400).. tukiacha vikodi vidogo vidogo vya asilimia 2.

      so mzigo utafika TZ kwa gharama ya (400[20ton] x 6,440[mfuko] + 632,000[Usafiri] =3,208,000 so Mifuko 400 utaifikisha Tz kwa gharama ya Tshs 3,208,000 na Mifuko 400 utainunua Tz kwenye soko letu kwa gramama ya (400 x 16,500) = 6,600,000 tofauti ya zaidi ya (6,600,000 -3,208,000) = 3,392,000 .. he he he!

      Mifuko 400, ukiinunua India na kuiuza TZ Tsh 10,000 tu kwa mfuko utapata Tshs (10,000 x 400)= 4,000,000 na kutengeneza faida chap ya (4,000,000-3,208,000)=792,000.

      Biashara ya haraka sana na mifuko itagombaniwa kama njugu na wewe unaifanya biashara yako yote ukiwa nyumbani nyuma ya laptop yako tu na simu ya mkononi basi.

      Nikaenda mbali kidogo na kujiuliza kwanini India cement ni bei rahisi. Nikagundua kwamba, kasheshe kubwa ya kutengenza sement iko kwenye maandalizi yake hasa hasa uzalishaji wa vijiwe vidoho vigumu sana vinavyoitwa Clinker. Mchakato wa Kutengeneza malighafi hii clinker ndio mgumu na ghali zaidi. Kwa utafiti mfupi nilioufanya nimegundua utengenezaji wa Clinker Kule India Ni Ghali sana Kulinganisha na hapa kwetu TZ. Nilibahatika kutembelea kiwanda cha Lafarge Mbeya Cement maarufu kwa kutengeneza Cement ya Mnyama (TEMBO CEMENT). --Simba ni Tanga na Twiga ni DSM.

      Mchakato wa Kutengeneza Clinker unaanzia kwenye machimbo ya miamba geu yenye vichambuzi (ingredients na Ore mbalimbali) miamba hii hutoka machimboni na kuingizwa kwenye ngome ya mapondo (Crushers) ambapo hupondwa na kuwa miamba midogo mithili ya kokoto na kuzukumizwa kwenye mkanda, na vile vile huchimbwa udongo wa mfinyanzi nao hukimbizwa kwenye mkanda wake mwingine kwa viwango vyao.

      Mikanda hii miwili huingizwa kwenye ngome kubwa ya mapondo na kusagwa kwa kuchanganywa kiasi cha kuwa vumbi, hapa ndipo kiasi kikubwa cha Vumbi huzalishwa, kutokana na shughuli pevu inayofanyika. Vumbi hili hudhibitiwa sana ila kiasi kidogo hutolewa nje na kuwa wingu zito sana la Vumbi hatari kwa mazingira. Vumbi hukusanywa kwenye Kiwiko kikubwa na kirefu sana nadhani ndio point ndefu kuliko zote kwenye kiwanda cha simenti, kinachoitwa Cyclone. Cyclone Hili hupokea vumbi hilo na kulisafirisha likahifadhiwe kweye maghala makubwa (Silos) Sasa Vumbi hili laini ndio malighafi ya kutengenezea hizo Clinker.

      Vumbi hili hukimbizwa kwenye kinu kikubwa (KILN). Na huko huchomwa kwenye jotoridi la takriban nyuzijoyo 1400. Udongo huyeyushwa na kuchangamana. Chanzo cha moto huwa ni makaa ya mawe ambayo hupondwa na kuwa vumbi kisha husukumwa kwa upepo wenye gandamizo kubwa na kuzalisha moto kama jehanam ya ajabu sana ndani ya jiko hilo. Moto ule (Carbon) na udongo huo ukijumlisha na mzunguko wa jiko lenyewe, manake linachoma huku linazunguka basi huzaa vijiwe vidogo vyeusi vinavyoitwa Clinker.

      Clinker hizo hupozwa kwenye ghala (hydrous)na baadae hukimbizwa kwenye mpipa mkubwa unaozunguka wenye magololi ya chuma na vikwazo ndani yake, huko clinker hugongwagongwa na kuwa vumbi laini sana ambalo huchanganywa na vumbi jingine linaloitwa gypsum (udongo unaochimbwa Tanga) na hapo kutoa vumbi ambalo likipata maji hukauka na kuwa jiwe linaloitwa CEMENT.

      Baada ya chochezi hilo nikapeleleza na utengenezji wa Clinker kule India, ambapo mawe hununuliwa, mfinyanzi hununuliwa na zaidi ya hayo wao huchoma kwa kutumia mafuta ambapo ni gharama sana sisi tunatumia makaa ya mawe ambayo kusini ni mengi tu..

      Ukiangalia mchakato huo HAPA KWETU, Miamba geu iko mingi na bure kabisa, Makaa ya Mawe Tunayo Kusini ya Kumwaga tu, Gypsum ni udongo unaopatikana Tanga mwingi sana na Bure tu. Sasa nani katuroga mpaka Cement isiwe na bei ya Tsh 2500 au 3000 tu????!!!????

      Nikagundua gharama Kubwa za Cement ni Unyonyaji tu, Viwanda vingi vinaendesha mataifa ya nje na si tanzania. Mfano waholanzi hawa Lafarge wanamlipa MZUNGU Technician tu mwenye certificate ya ufundi karibia Dola 8,500 sawa na (8500 x 2580) = Tshs 13,400,000/=kama mshahara wake mwezi, wakati Mhandisi Mtanzania mwenye Jiwe lake moja au mawili, aliyekokotoa shule ngumu ya FoE na term system that time, na kuvivuka vikwazo vyote vya kina Prop Chambega, Luhanga , Masuha Nk ambaye ndiye mkuu wa sekta mojawapo labda project manager, au Chief Electrical, mechanical, Civil nk kiasi cha Tsh 820,000 kwa mwezi. Usawa uko wapi?. Wakati huyu fundi wa kizungu maelekezo na miongozo ya kazi anaipata kwa Mtanzania huyu ambaye ni meneja wa kitengo husika. Hivi usawa uko .. kama Fundi tu anakula madolali yote hayo je Eng wa kizungu, je Chief of DPt je manager je CO wa kizungu anajichotea mangapi.. kama hiyo haitoshi je wanajilipia kwenye serikali yao kiasi gani kwa External security, BIMA, INSUARANCE nk (maana huduma hizi zote wanajitegmezea huko kwao) na kiasi gani wanarundika kwenye mabenki yao na kuimarisha uchumi wao?

      Fedha nyingi na Utajiri Mwingi wazawa hawafaidi, tunanyonywa na kukubali kunyonyeka. Kiwanda sio Inshu kubwa, Serikali ikiamua kujenga Kiwanda hiki ni kazi nyepesi na laini sana. Kama Hawa wazungu wanaleta makandamizi haya basi tuwaalike Wajerumani waliowajengea hawa waholanzi na wengineo viwanda waijengee serikali kupitia vichwa makini chini ya PSRC ikaendesha kiwanda hiki kwa ukombozi wa wananchi wake. INAWEZEKANA..

      Alamsik..!!


      NB: Kwa muda wako jisomee:

      Tanzania: Cement sh 5,000 yawezekana!

      &k
      Maisha BORA: Songea mfuko wa cement sh 20, 000 per bag!
      ...

      Quote By Ukana Shilungo
      you are real brialiant,uchambuzi safi kabisa,mbeya cement kiwanda cha songwe Injinia mwandamizi Maro ni alikuwa injinia mkuu toka kiwanda kinajengwa mpaka kinaanza uzalishaji,aliacha kazi kwa ajili ya mzungu asiyejua kazi kulipwa Milioni 13 ili hali yeye akipokea milioni 1.5,alipatwa na uchungu akaacha kazi.meneja mkuu Diyami alimshauri Mkapa kutobinafisisha kiwanda cha Songwe ila mkapa hakusikia,kwa hiyo bei ya saruji ingeweza kuwa nafuu tatizo ni ufisadi toka kwa hawa wageni tuliowapa viwanda kwa bei ya kutupa,lengo ni kupata super profit,so THE MISSION OF CAPITALIST WHEREVER THEY ARE IS EXPLOITATION by any means,hivyo saruji kuuzwa 5000 kama alivyosema Dr slaa ni kweli,kweli tupu.
      Last edited by Eng. Y. Bihagaze; 13th June 2012 at 21:03.
      Invisible, BAK, Small Boy and 59 others like this.

    2. Miaka 50

    3. #101
      bg_dg_dy's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 27th February 2009
      Location : Dsm - Tz
      Posts : 223
      Rep Power : 565
      Likes Received
      27
      Likes Given
      1

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Well analysed!

    4. #102
      Chakunyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th April 2011
      Location : Masasi
      Posts : 751
      Rep Power : 561
      Likes Received
      134
      Likes Given
      283

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Uchambuzi mzuri big up!

    5. #103
      MSEZA MKULU's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 22nd July 2011
      Posts : 169
      Rep Power : 429
      Likes Received
      58
      Likes Given
      213

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Naunga mkono.

      Baada ya uchaguzi wote wameanza maandalizi ya uchaguzi ujao. Wananchi tumebaki yatima, hakuna kiongozi hata mmoja mwenye kuweza kufikilia kama weye mkuu.

      Thnks ubarikiwe
      The most powerful moral influence is example

    6. #104
      Bob G's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 5th October 2011
      Location : UK Manyasi
      Posts : 1,659
      Rep Power : 717
      Likes Received
      291
      Likes Given
      36

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Mimi nawashauri watanzania wote waipige chini hii ccm ili wote tumiliki nyumba bora wote kwa kununua Mfuko 1 wa cement kwa shs 5,000/

    7. #105
      Dr.kapama's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 12th November 2011
      Posts : 156
      Rep Power : 411
      Likes Received
      22
      Likes Given
      15

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      In government,i need peopke like you bhana...big up japo inatia uchungu,hasara ya Tsh 15000/= nzima for nothing...

    8. RukaaJuu Final

    9. #106
      Godwinnko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2012
      Location : Moshi
      Posts : 484
      Rep Power : 669
      Likes Received
      111
      Likes Given
      64

      Default

      Quote By zomba
      Hapo bado upo India halafu uulete Tanzania uuze kwa bei ya Slaa ya 5,000/= kwi kwi kwi teh teh teh!
      huyu zomba naona hajasoma vizuri hii thread..naomba uuweke utanzania pembeni alaf usome tena utaona salma ameonesha tofauti ya utengenezaji huko india na hapa tz..raw materials wanazo tumia kule wanazinunua lakini sisi tunazo hapahapa nchini
      fredmlay likes this.

    10. #107
      sammosses's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th January 2011
      Location : Shinyanga
      Posts : 912
      Rep Power : 604
      Likes Received
      168
      Likes Given
      238

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      big up sana mama,tatizo hii ni Danganyika state,na Wadanganyika wamekubali kudanganyika kwa kila jambo.Tujifunze kwa wenzetu wa Kenya,hawakubali kuburuzwa na watawala walafi wa madaraka.Angalia Zambia kilo moja ya sembe ikipanda watu wanaingia barabarani lakini sisi vichwa vya wendawazimu kial fisadi ana jifunzia kuibia.

    11. #108
      Godwinnko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2012
      Location : Moshi
      Posts : 484
      Rep Power : 669
      Likes Received
      111
      Likes Given
      64

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      mods nadhani hii thread inastahili kuwekwa kama sticky..!

    12. #109
      webondo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2012
      Location : Chini ya mwembe
      Posts : 1,167
      Rep Power : 589
      Likes Received
      178
      Likes Given
      381

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Hakika hawa watu wanatufanya mapimbi sana.

    13. #110
      Capt Tamar's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th December 2011
      Posts : 1,707
      Rep Power : 1036
      Likes Received
      414
      Likes Given
      1

      Default

      Quote By zomba
      Hicho kiwanda si kilikuwa cha umma mkashindwa kukiendesha? kachukuwa singa singa, mambo swaafi kabisa. Ndio maana mkaambiwa maendeleo ya mtu huletwa na yeye mwenyewe. Nyinyii mlishindwa nini tena umma mzima, singa-singa mmoja kaweza. Aibu.
      Sema vizuri!chama lako hilo la majizi ndilo lililoendekeza ulafi mpaka likakosa hela ya kununulia Mifuko!!ambayo ndiyo material pekee inayoingia kutoka nje ya geti,aibu gani hii mmetuletea watanzania?nakuombea kwenye jeneza la ccm nawe uwepo ndani yake,na mfe kwa aibu kama yule masikini muliyemdhulumu anavyoishi kwa aibu.

    14. #111
      Shine's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th February 2011
      Posts : 9,187
      Rep Power : 2429
      Likes Received
      946
      Likes Given
      377

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Ktk hili kaonyesha yeye siyo kilaza kama mwenzake j!

    15. #112
      tanira1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th November 2011
      Posts : 614
      Rep Power : 502
      Likes Received
      111
      Likes Given
      91

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Quote By Negotiator
      Asante Salma uchambuzi makini. ndo maana najiuliza nani katuloga?
      tumelogwa na vitishet na vikanga na vikofia vya ccm no 1

      ''MIAKA HAMSINI(51) YA UVUMILIVU''​

    16. #113
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Quote By olyset net
      Sema vizuri!chama lako hilo la majizi ndilo lililoendekeza ulafi mpaka likakosa hela ya kununulia Mifuko!!ambayo ndiyo material pekee inayoingia kutoka nje ya geti,aibu gani hii mmetuletea watanzania?nakuombea kwenye jeneza la ccm nawe uwepo ndani yake,na mfe kwa aibu kama yule masikini muliyemdhulumu anavyoishi kwa aibu.
      Chama ndio wanaendesha kiwanda? kwani hujui viwanda vyote vya umma vilianza kufa kabla havijaingiza faida? kuna mali ya dhulma ikaendelea?
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    17. Nzi
      #114
      Nzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2010
      Location : 740 Park Avenue
      Posts : 3,317
      Rep Power : 21624
      Likes Received
      927
      Likes Given
      823

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Quote By SALMA2015

      Nikaenda mbali kidogo na kujiuliza kwanini India cement ni bei rahisi. Nikagundua kwamba, kasheshe kubwa ya kutengenza sement iko kwenye maandalizi yake hasa hasa uzalishaji wa vijiwe vidoho vigumu sana vinavyoitwa Clinker. Mchakato wa Kutengeneza malighafi hii clinker ndio mgumu na ghali zaidi. Kwa utafiti mfupi nilioufanya nimegundua utengenezaji wa Clinker Kule India Ni Ghali sana Kulinganisha na hapa kwetu TZ. Nilibahatika kutembelea kiwanda cha Lafarge Mbeya Cement maarufu kwa kutengeneza Cement ya Mnyama (TEMBO CEMENT). --Simba ni Tanga na Twiga ni DSM.

      SALMA2015, nilikuwa naelewa kwamba Twiga Cement uimport clinker toka nje ya nchi ili kufidia mahitaji yao ya clinker. Sijui kama wameanza kutengeneza clinker ya kutosheleza mahitaji pale kiwandani (ingawa nafahamu walikuwa wana mpango wa kuboresha uzalishaji wa clinker katika KILN No. 3) . Na nakumbuka mara kwa mara wamekuwa wakilalamika juu ya gharama kubwa za uzalishaji zinazochangiwa na uagizaji wa clinker toka nje.

      Pia kuna hili suala la Portland and Pozzolana Cements; hiyo portland (imechukua jina hilo kutokana na kufananishwa na jiwe linaloitwa portland, jiwe linalopatikana katika kisiwa kidogo cha Portland kilichopo Uingereza) cement ndiyo maarufu kuliko pozzolana (pia jina lake linatokana na eneo linaloitwa Pozzuoli lililoko Italia, ambako ndipo inasemekana majivu jivu ya ki-pozzolanic ndipo yalichimbwa na kugundulika kwanza) cement.

      Sasa hiyo pozzolana cement inasemwa kuwa ni imara zaidi ya portland cement; kwa kuwa pozzolana cement pale inapokuwa ngumu (imekauka vizuri) ina sifa ya kutofyonza na kutopitisha maji kwa kiwango (lower porosity) kikubwa kama portland cement, sifa ambayo inafanya iwe imara pia dhidi ya kuvunjikavunjika (breaking into fragments/small pieces). Na sasa nasikia makampuni makubwa duniani yanachanganya pozzolanic materials na portland cement katika kufaidika na sifa za cement hizo mbili.

      Hii pozzolana inapatikana kwa wingi sana Mbeya na pia maeneo ya karibu na Mlima Meru (tena kulikuwa na mradi wa kuchimba na kutumia majivu ya volcano yaliyokuwa yanapatikana karibu na Mlima Meru miaka ya 1970). Sasa sielewi kwanini viwanda vyetu havitumii hii pozzolana katika kuzalisha simenti, sijaweza kufahamu shida ya pozzolana, labda kama kuna mdau anaelewa, anaweza kunisaidia.

      Sasa kwa mtazamo huo, ni hakika kwamba kama viwanda vyetu vikiweza kutumia hii pozzolana katika uzalishaji wa simenti, basi naamini kwa kiwango kikubwa bei za simenti zitashuka sana. Na hivyo kupelekea wazo la Slaa kuwa linalotekelezeka.
      "You can't make a scene if you don't have little green"-------Jim Carrey

    18. #115
      twatwatwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th September 2011
      Posts : 840
      Rep Power : 556
      Likes Received
      96
      Likes Given
      3

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Mawazo ya upinzani ni yakuogopa kama ukoma hata kama yana ukweli

    19. #116
      Mopalmo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th November 2010
      Posts : 425
      Rep Power : 518
      Likes Received
      51
      Likes Given
      43

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Kwanza saluti sana kwa mleta mada,ameleta mjadala wa muhimu sana hapa,wale wenye akili mgando za kimagamba ndio hawaamini kua cement inaweza uzwa kwa bei hiyo.mimi kitu kimoja kimenishangaza cement ya pakistan inauzwa bei moja na ya tz na ubora ni wa juu kuliko hata ya tz,hapa kuna tatizo tutafakari na tuchukue hatua tuwakatae wanaokumbatia wawekezaji wanyonyaji hii si enzi ya binadam kuishi nyumba ya udongo juu mpaka chini kama wanyama,Mungu alituambia tuje kuitawala dunia na vyote vilivyomo

    20. #117
      ndinga's Avatar
      Member Array
      Join Date : 1st April 2012
      Posts : 95
      Rep Power : 379
      Likes Received
      12
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By zomba
      Halafu hiyo hesabu yako mfuko mmoja ni shillingi ngapi? ukiweka gharama za usafiri wa meli (zilizo sawa, hiyo ya dola 400 kwa container la futi 40 ni porojo), gharama za bandari? usafiri wa nchi kavu? gharama za kuhifadhi (storage)? gharama za kuuza (sales cost)? kwi kwi kwi teh teh teh, bado ni elfu tano tu kwa mfuko? sasa wewe mbona juu huko kwa gharama porojo na unauza 10,000 kwa mfuko? umempita bei Slaa kwa 100%, sasa nani porojo zaidi wewe, au yeye?
      Hivi inakuingia akilini cement inatengenezwa km 17 inauzwa zaidi ya sehemu ya km 800.fanya nawewe utafiti wako so kupinga kila kitu.
      fredmlay likes this.

    21. #118
      fredmlay's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th April 2008
      Posts : 1,516
      Rep Power : 868
      Likes Received
      265
      Likes Given
      934

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Vitu makini kama hivi vikisemwa na wengine mara utasikia habari za udini, ukanda, upadri nk.. kweli watanzania utafikiri tumelogwa, hakika inawezekana cement kuuzwa kwa bei ya chini hata chini ya 5000.
      A wise man will make more opportunities than he finds:

    22. #119
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Kabla ya miaka 5 Kikwete alishasema anashughulikia hili tatizo la simenti na naam, hivi karibuni tutaona ushindani mkubwa kwani kuna viwanda vipya vinne sehemu tofauti Tanzania viko katika ujenzi, vingine vimeshaanza mpaka uzalishaji wa majaribio.

      Tegemeeni kushuka kwa bei ya simenti lakini sio kwa kiwango cha Bi Salma cha 2,500/= kwa mfuko wa kilo 50 au cha Slaa cha 5,000/= huko ni kujidanganya.
      mzeelapa likes this.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    23. #120
      fredmlay's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th April 2008
      Posts : 1,516
      Rep Power : 868
      Likes Received
      265
      Likes Given
      934

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Umaskini wetu unasababishwa na mibwege kama akina zomba.. hebu fikiri serikali ikiwa na watendaji wa aina ya zomba unatarajia nini kama si kuyumba kama tuyumbavyo?
      A wise man will make more opportunities than he finds:

    Page 6 of 13 FirstFirst ... 45678 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...