Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

    Report Post
    Page 3 of 13 FirstFirst 12345 ... LastLast
    Results 41 to 60 of 254
    1. #1
      Eng. Y. Bihagaze's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 8th September 2011
      Location : Czech(but now in DAR)
      Posts : 766
      Rep Power : 5116
      Likes Received
      583
      Likes Given
      111

      Default Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%



      Kauli aliyoitoa Dr Slaa wakati wa vuguvugu la kampeni za kisiasa kwamba mfuko wa sement utakuwa Tshs 5,000, badala ya Tshs16,500 kwa sasa kwa wakazi wa DSM na zaidi ya Tshs18,000 kwa wakazi wa nje ya mji huu, nimekuwa nikizitafakari kwa kina sana kwa muda mrefu. Kutokana na Uzoefu wangu wa masuala machache alonijalia mola, nilioona kama ni sentensi ya kisiasa zaidi ya kimatendo, lakini sasa nakiri ni sentenSi makini na ya kweli. Na si 5000 tu bali pia 2,500 au 3000 kwa mfuko wa 50kgs.

      Hivi majuzi, nilikuwa namsikiliza Waziri Viwanda na Biashara Dr. Kigoda akizungumzia masuala ya Kiuchumi kwenye kipindi cha TBC asubuhi. Kauli aliyotoa Abdala Kigoda ilinifanya kile kisifa cha kuitwa Dr nikiondoe haraka na natamani nikiingia ofisini kwake nimwite Mr Abdala. Mkongwe Huyu adui mkubwa wa mabango ya “sigara ni hatari kwa Afya yako” alisema , ‘AMESIKIA” wafanya biashara wa hapa wakimweleza kwamba bei ya mfuko wa sement inayouzwa hapa ni ghali sana kulinganisha na bei ya mfuko utaouagiza kutoka India.”

      Nikawaza kama mzee huyu, waziri wetu amesikia tu, ameshindwa kufanya tathimini kutumia ziada kidogo ya akili yake iliyompelekea kuitwa DR, kwamba kama hali iko hivyo kwa India km 4,600 tu kutoka TZ, sawa na kwenda kigoma na kurudi dsm mara mbili, ana mipango gani mbadala ya kuhakikisha na hapa kwetu unafuu wa neema unaonekana kwenye gharama ya mifuko ya cement, watu tukajenga?

      Sentensi yake hiyo ilinisukumia na kuamsha mawazo yale niliyokuwa nayo awali aliyoyasema Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CHADEMA Dr Wilbroad Slaa-2010, kwamba Bei ya sement ni ghali sana, Serikali yake itaipunguza hadi kufikia Tsh5,000. Na hapo ndipo nilipoona nifanye kauchunguzi kadogo sana ambako mdau wa jamvi unaweza kunikosoa lakini uwezo wa kuchunguz kwangu ndipo ulipofikia..

      Cha kwanza nikawapigia “madalali wa wagonjwa” (india kuna watu kazi yao ni udalali wa wagonjwa, wanatengeneza dili zao kwa kuwasaka wagonjwa kutoka kwenye nchi zao kama Africa na hata penginepo kupitia mashirika mengi kama LIONS CLUB na mengineyo na kuwa connect na daktari husika na kufanya protocal zote za maandalizi na ndivyo nao wanavyopata kula ..anyway that is not ma topic)..nikawauliza wanitajie bei ya mfuko wa sement kwenye soko la kawaida .. baada ya muda wakaniambia ni Rupia 230. Rupia moja ni sawa na Tsh28.

      Kwa hiyo mfuko mmoja wa Kg 50 wa sement kule India ni sawa na Tsh 6,440 (28 x 230). Kwa Kontena la 20ft lina uwezo wa kuchukua tani 35-40, lakini meli nyingi zina standard ya kujaza 40ft kwa tani 20 tu. Sasa tani 20 ni mifuko 400 a cement. Kwa bei ya meli zinazosafirisha 40ft kwa 20ton ni dolar 400 (sawa na tzs 632,000 (1,580 x 400).. tukiacha vikodi vidogo vidogo vya asilimia 2.

      so mzigo utafika TZ kwa gharama ya (400[20ton] x 6,440[mfuko] + 632,000[Usafiri] =3,208,000 so Mifuko 400 utaifikisha Tz kwa gharama ya Tshs 3,208,000 na Mifuko 400 utainunua Tz kwenye soko letu kwa gramama ya (400 x 16,500) = 6,600,000 tofauti ya zaidi ya (6,600,000 -3,208,000) = 3,392,000 .. he he he!

      Mifuko 400, ukiinunua India na kuiuza TZ Tsh 10,000 tu kwa mfuko utapata Tshs (10,000 x 400)= 4,000,000 na kutengeneza faida chap ya (4,000,000-3,208,000)=792,000.

      Biashara ya haraka sana na mifuko itagombaniwa kama njugu na wewe unaifanya biashara yako yote ukiwa nyumbani nyuma ya laptop yako tu na simu ya mkononi basi.

      Nikaenda mbali kidogo na kujiuliza kwanini India cement ni bei rahisi. Nikagundua kwamba, kasheshe kubwa ya kutengenza sement iko kwenye maandalizi yake hasa hasa uzalishaji wa vijiwe vidoho vigumu sana vinavyoitwa Clinker. Mchakato wa Kutengeneza malighafi hii clinker ndio mgumu na ghali zaidi. Kwa utafiti mfupi nilioufanya nimegundua utengenezaji wa Clinker Kule India Ni Ghali sana Kulinganisha na hapa kwetu TZ. Nilibahatika kutembelea kiwanda cha Lafarge Mbeya Cement maarufu kwa kutengeneza Cement ya Mnyama (TEMBO CEMENT). --Simba ni Tanga na Twiga ni DSM.

      Mchakato wa Kutengeneza Clinker unaanzia kwenye machimbo ya miamba geu yenye vichambuzi (ingredients na Ore mbalimbali) miamba hii hutoka machimboni na kuingizwa kwenye ngome ya mapondo (Crushers) ambapo hupondwa na kuwa miamba midogo mithili ya kokoto na kuzukumizwa kwenye mkanda, na vile vile huchimbwa udongo wa mfinyanzi nao hukimbizwa kwenye mkanda wake mwingine kwa viwango vyao.

      Mikanda hii miwili huingizwa kwenye ngome kubwa ya mapondo na kusagwa kwa kuchanganywa kiasi cha kuwa vumbi, hapa ndipo kiasi kikubwa cha Vumbi huzalishwa, kutokana na shughuli pevu inayofanyika. Vumbi hili hudhibitiwa sana ila kiasi kidogo hutolewa nje na kuwa wingu zito sana la Vumbi hatari kwa mazingira. Vumbi hukusanywa kwenye Kiwiko kikubwa na kirefu sana nadhani ndio point ndefu kuliko zote kwenye kiwanda cha simenti, kinachoitwa Cyclone. Cyclone Hili hupokea vumbi hilo na kulisafirisha likahifadhiwe kweye maghala makubwa (Silos) Sasa Vumbi hili laini ndio malighafi ya kutengenezea hizo Clinker.

      Vumbi hili hukimbizwa kwenye kinu kikubwa (KILN). Na huko huchomwa kwenye jotoridi la takriban nyuzijoyo 1400. Udongo huyeyushwa na kuchangamana. Chanzo cha moto huwa ni makaa ya mawe ambayo hupondwa na kuwa vumbi kisha husukumwa kwa upepo wenye gandamizo kubwa na kuzalisha moto kama jehanam ya ajabu sana ndani ya jiko hilo. Moto ule (Carbon) na udongo huo ukijumlisha na mzunguko wa jiko lenyewe, manake linachoma huku linazunguka basi huzaa vijiwe vidogo vyeusi vinavyoitwa Clinker.

      Clinker hizo hupozwa kwenye ghala (hydrous)na baadae hukimbizwa kwenye mpipa mkubwa unaozunguka wenye magololi ya chuma na vikwazo ndani yake, huko clinker hugongwagongwa na kuwa vumbi laini sana ambalo huchanganywa na vumbi jingine linaloitwa gypsum (udongo unaochimbwa Tanga) na hapo kutoa vumbi ambalo likipata maji hukauka na kuwa jiwe linaloitwa CEMENT.

      Baada ya chochezi hilo nikapeleleza na utengenezji wa Clinker kule India, ambapo mawe hununuliwa, mfinyanzi hununuliwa na zaidi ya hayo wao huchoma kwa kutumia mafuta ambapo ni gharama sana sisi tunatumia makaa ya mawe ambayo kusini ni mengi tu..

      Ukiangalia mchakato huo HAPA KWETU, Miamba geu iko mingi na bure kabisa, Makaa ya Mawe Tunayo Kusini ya Kumwaga tu, Gypsum ni udongo unaopatikana Tanga mwingi sana na Bure tu. Sasa nani katuroga mpaka Cement isiwe na bei ya Tsh 2500 au 3000 tu????!!!????

      Nikagundua gharama Kubwa za Cement ni Unyonyaji tu, Viwanda vingi vinaendesha mataifa ya nje na si tanzania. Mfano waholanzi hawa Lafarge wanamlipa MZUNGU Technician tu mwenye certificate ya ufundi karibia Dola 8,500 sawa na (8500 x 2580) = Tshs 13,400,000/=kama mshahara wake mwezi, wakati Mhandisi Mtanzania mwenye Jiwe lake moja au mawili, aliyekokotoa shule ngumu ya FoE na term system that time, na kuvivuka vikwazo vyote vya kina Prop Chambega, Luhanga , Masuha Nk ambaye ndiye mkuu wa sekta mojawapo labda project manager, au Chief Electrical, mechanical, Civil nk kiasi cha Tsh 820,000 kwa mwezi. Usawa uko wapi?. Wakati huyu fundi wa kizungu maelekezo na miongozo ya kazi anaipata kwa Mtanzania huyu ambaye ni meneja wa kitengo husika. Hivi usawa uko .. kama Fundi tu anakula madolali yote hayo je Eng wa kizungu, je Chief of DPt je manager je CO wa kizungu anajichotea mangapi.. kama hiyo haitoshi je wanajilipia kwenye serikali yao kiasi gani kwa External security, BIMA, INSUARANCE nk (maana huduma hizi zote wanajitegmezea huko kwao) na kiasi gani wanarundika kwenye mabenki yao na kuimarisha uchumi wao?

      Fedha nyingi na Utajiri Mwingi wazawa hawafaidi, tunanyonywa na kukubali kunyonyeka. Kiwanda sio Inshu kubwa, Serikali ikiamua kujenga Kiwanda hiki ni kazi nyepesi na laini sana. Kama Hawa wazungu wanaleta makandamizi haya basi tuwaalike Wajerumani waliowajengea hawa waholanzi na wengineo viwanda waijengee serikali kupitia vichwa makini chini ya PSRC ikaendesha kiwanda hiki kwa ukombozi wa wananchi wake. INAWEZEKANA..

      Alamsik..!!


      NB: Kwa muda wako jisomee:

      Tanzania: Cement sh 5,000 yawezekana!

      &k
      Maisha BORA: Songea mfuko wa cement sh 20, 000 per bag!
      ...

      Quote By Ukana Shilungo
      you are real brialiant,uchambuzi safi kabisa,mbeya cement kiwanda cha songwe Injinia mwandamizi Maro ni alikuwa injinia mkuu toka kiwanda kinajengwa mpaka kinaanza uzalishaji,aliacha kazi kwa ajili ya mzungu asiyejua kazi kulipwa Milioni 13 ili hali yeye akipokea milioni 1.5,alipatwa na uchungu akaacha kazi.meneja mkuu Diyami alimshauri Mkapa kutobinafisisha kiwanda cha Songwe ila mkapa hakusikia,kwa hiyo bei ya saruji ingeweza kuwa nafuu tatizo ni ufisadi toka kwa hawa wageni tuliowapa viwanda kwa bei ya kutupa,lengo ni kupata super profit,so THE MISSION OF CAPITALIST WHEREVER THEY ARE IS EXPLOITATION by any means,hivyo saruji kuuzwa 5000 kama alivyosema Dr slaa ni kweli,kweli tupu.
      Last edited by Eng. Y. Bihagaze; 13th June 2012 at 21:03.
      Invisible, BAK, Small Boy and 59 others like this.

    2. Miaka 50

    3. #41
      Edson's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2009
      Posts : 7,308
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1799
      Likes Given
      433

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Quote By Henge
      Asante mkuu hata kama umeniongezea hasila!

      wenzako wameamua kujenga 2016.... nadhani unajua nani atakuwa anashika madaraka ya nchi hii
      I'm Naturaly Evasive..

    4. #42
      Edson's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2009
      Posts : 7,308
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1799
      Likes Given
      433

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Quote By S.Liondo
      Kwa hii taarifa yako mkuu, basi uduni wa maisha tulionao watanzania ni wa kujitakia wenyewe, tena kwa kuukumbatia kwa mapenzi makubwa kiasi cha kushindwa kuihukumu CCM kupitia sanduku la kura. Hakuna maendeleo ya maana hapa Tanzania mpaka kuwe na mabadiliko ya maana katika serikali inayotawala.

      ni wakujitakia mkuu tena kwa asilimia zote....
      I'm Naturaly Evasive..

    5. #43
      Rasib's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd April 2012
      Posts : 322
      Rep Power : 421
      Likes Received
      32
      Likes Given
      7

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Walahhi tenah! Mi na nyinyiemu 2015, mungu aendelee kumpa nguvu mheshimiwa rais, Dr. Wilbroad Slaa..AMeN

    6. #44
      Yo Yo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st May 2008
      Posts : 10,786
      Rep Power : 22905
      Likes Received
      1335
      Likes Given
      2576

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      ooh man JF is back....well analytical and constructive thread ever
      ...kuwa na baba maskini ni mipango ya Mungu ila kuwa na baba mkwe maskini ni ujinga wako mwenyewe.....

    7. #45
      mozes's Avatar
      Member Array
      Join Date : 11th January 2012
      Posts : 56
      Rep Power : 382
      Likes Received
      5
      Likes Given
      1

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Nazdi kupata hasira na serikal ilioko madarakan! 'wananchi wasiopiga kura ndio wanaowachagua viongoz wasiofaa' lazma 2badilike jaman

    8. FemaTV & Radio

    9. #46
      nyondoloja's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 10th November 2010
      Posts : 147
      Rep Power : 1141
      Likes Received
      22
      Likes Given
      0

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      mkuu asante kwa uchambuzi umesomeka

    10. #47
      Bhbm's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st October 2009
      Posts : 650
      Rep Power : 616
      Likes Received
      151
      Likes Given
      0

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Safi sana mkuu, good analysis

    11. #48
      bensonlifua92's Avatar
      Member Array
      Join Date : 9th December 2010
      Posts : 82
      Rep Power : 444
      Likes Received
      32
      Likes Given
      32

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Salma kwa uchambuzi na utafiti ulofanya una haki ya kusema ulosema hasa kuwa bei ya cement yaweza shuka hadi chini ya 5,000/- ya Ki-TZ. I salute you and you deserve my (our) respect!!! Wewe ni GREAT THINKER...!!!

      Viongozi mlo madarakani endeleeni kubisha tu ila ipo siku mambo yatageuka na watakuja watu makini washike serikali na ndo wata-prove kuwa inawezekana na nyie kama mtakuwa hai au wana wenu watakuja ona aibu kuwa why nyie mlitunyonya na kutukandamiza watanzania kwa maisha magumu na nyie ndo muishi kwenye maisha bora kwa kila mnyonyaji na Fisadi!!

      Mtu mmoja nilisoma kitabu chake nikiwa shule enzi hizo, alimsimulia mtu mmoja aitwaye Rashidi kama sikosei ambaye alikuwa Kuli bandarini...kwa shida alizo kuwa anazipata alihitimisha hivi..."YANA MWISHO HAYA".

      So hata ufisadi ulokubuhu nao Una mwisho wake na OLE WENU MAFISADI NA WANYONYAJI WOTE WA TAIFA HILI...Wakati ukifika Mtalia na kusaga meno....

    12. #49
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Halafu hiyo hesabu yako mfuko mmoja ni shillingi ngapi? ukiweka gharama za usafiri wa meli (zilizo sawa, hiyo ya dola 400 kwa container la futi 40 ni porojo), gharama za bandari? usafiri wa nchi kavu? gharama za kuhifadhi (storage)? gharama za kuuza (sales cost)? kwi kwi kwi teh teh teh, bado ni elfu tano tu kwa mfuko? sasa wewe mbona juu huko kwa gharama porojo na unauza 10,000 kwa mfuko? umempita bei Slaa kwa 100%, sasa nani porojo zaidi wewe, au yeye?
      Last edited by zomba; 13th June 2012 at 21:02.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    13. #50
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 15,822
      Rep Power : 14621
      Likes Received
      2842
      Likes Given
      1961

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Mambumbu ni wengi sana Tanzania, wanasifia uongo! hizo ndio shule za kina mtakatifu. Tukiwaambia mnasaidiwa na NECTA mnakataa, mmeshazitazama hizo hesabu za bi Salma lakini au mnachekelea kama misukule tu?
      Last edited by zomba; 13th June 2012 at 21:02.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    14. #51
      PRISCUS JR's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 3rd October 2011
      Location : Mwanza Rock City
      Posts : 165
      Rep Power : 419
      Likes Received
      107
      Likes Given
      34

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Dada naomba ruhusa niprint utafiti huu niusambaze mtaani kwa gharama yangu nikuatribute tafadhali.

    15. #52
      CHIMPONGO's Avatar
      Member Array
      Join Date : 6th February 2012
      Posts : 29
      Rep Power : 373
      Likes Received
      3
      Likes Given
      1

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Hongera sana kwa uchambuzi makini, wacha Kigoda na serekali wasome labda wataelewa pia TBC wanaweza kukanusha makala zao

    16. #53
      mkizungo's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 6th April 2012
      Posts : 249
      Rep Power : 408
      Likes Received
      47
      Likes Given
      298

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      asante mkuu kwa info,,,,,,,,hatuna utashi kwa vile hatuna uzalendo,,,,chadema valien njuga mambo haya,,,kampen futa nyumba za tope na nyasi tz au op makazi bora,,,

    17. #54
      Bigirita's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th February 2007
      Location : Under a mango tree
      Posts : 11,256
      Rep Power : 3042
      Likes Received
      3038
      Likes Given
      4125

      Default

      Ubaya ni kwamba ndugu zetu wakina Nape huwezi kuwaona huku waki reason kwa issue badala ya propaganda.

      Wakina rejao wao wanajua mambo laini laini tu!

    18. #55
      Ginner's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th May 2011
      Posts : 618
      Rep Power : 530
      Likes Received
      120
      Likes Given
      7

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Mheshimiwa, kwa maana iyo ni nafuu zaidi kuagiza contena la cement toka nje kwaajili ya ujenzi kuliko kununua hapa nchini..kama option hii ipo kwann tuna endelea kung'ang'ana na cement za hapa nchini au serikali inakata kodi ya juu mno kwenye iyo

    19. #56
      Kituko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th January 2009
      Posts : 3,706
      Rep Power : 1286
      Likes Received
      489
      Likes Given
      173

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Uchambuzi mzuri sana, na ni kweli hilo linawezekana kabisa
      na kwa kuongezea tu, bei inawezaje kuwa sawa nchi zima? yaani kama Dar ni 5000 basi na Kigoma, Lindi na Shinyanga bei inakuwa hiyohiyo ya 5000tsh

      Kwa nchi zenye kujali raia wake na kuwapunguzia kasi ya ugumu wa maisha, utaratibu unaotumika ni wa kuwapa punguzo la kodi na kuwashushia bei ya mafuta kwa wasafirishaji wote wanaopewa tenda ya kusafirisha hiyo cement kwenda mikoa husika, mwenye roli anayepeleka cement Morogoro anakuwa na kiwango chake cha kodi na bei yake ya mafuta ambayo itakuwa juu kidogo kuliko ya yule anayepeleka Kigoma ama mwanza, utaratibu huu unasaidia sana kwa kuweka uwiano sawa wa bei kwa nchi nzima

    20. #57
      blea's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 14th November 2011
      Location : URU ONGOMA MAMBA
      Posts : 239
      Rep Power : 427
      Likes Received
      48
      Likes Given
      145

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Yawezekana kama viongozi wetu wataacha ulafi uliopitiliza. Wamekula wameshiba bado wanajitapisha ili waendelee kula huku wananchi wa kawaida wakiteseka kwa njaa na umasikini uliokithiri. Hawana aibu kabisa wameshatufanya misukule yao wao na familia zao wakineemeka kwa jasho letu.AIBU YAO MILELE

    21. #58
      STEIN's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2010
      Location : Arusha
      Posts : 1,342
      Rep Power : 715
      Likes Received
      306
      Likes Given
      156

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Mkuu kwanza nashukuru kwa shule kubwa uliyotupa.., Mimi naamini kabisa kila kitu kinawezekana ila kama unavyosema TZ kila kitu ni Udalali ambao unaanzia kwa waziri hadi watendaji wa chini.

      Mfano the same inatokea kwenye Sukari, Unga nk...

      Tufike mahali kama Dr Anasema inwezekana Mfuko wa Cement kuwa 5000/=, Elimu Bure, Afya Bure etc Tumpe hii Nchi atuonyeshe the wengine wafuate... Tatizo hapa ni CCM na Mafisasi wanatumia sana Pesa ili kupotosha ukweli huu...

      Mimi namwamini sana huyu Mzee... Nakumbuka Mara ya kwanza wakati anagombea ubunge kule Karatu alisema... Kusambaza maji viji vyote vya Karatu inawezekana, Kupunguza kodi ya kichwa kutoka 5000 hadi 2000 inawezekana, Wanafunzi wa karatu kusoma bure inawezekana, Kila kijiji kuwa na Dispensary inawezekana... Wakati jamaa wa CCM anahubiri maji hakuna TZ nzima si karatu tu...

      Watu wa Karatu wakaona isiwe taabu.. Wakampa Ubunge pamoja na halimashauri... Unajua alifanyaje? Kwanza alifuatilia kodi ya kichwa inakusanywa kiasi gani kwa mwaka, akakuta zaidi ya 80% inatumika kwenye process ya ukusanyaji.

      Simply akasema kama atatengeneza kodi ndogo ambayo watu watailipa wenyewe then amemaliza Kazi ndiyo ikawa 2000/= na 500/= kwa ajili ya kuwasomesha wanafunzi kutoka olevel hadi Alevel.

      Badala yake wakazi wa Halimashauri zinazoizunguka Karatu wakawa wanalipa kodi zao Karatu. Mapato yakawa mengi ndiyo CCM wakaamua kuifuta.


      Sasa ni muda wa kuangalia tusichague tena hawa wazee wa mades tuchagu Rais mwenye IQ, I mean Ram, HDD pamoja na Processor speed kubwa ambaye si Rahisi kumdanya sikufichi hata mchwa na vipandikizi Pale CDM vinashindwa kufanya kazi pale CDM kwa sababu ya huyu Mzee.

      Mtu mwingine ambaye namkubali ni Freeman Mbowe huyu bwana anastahili kuwa kwenye nafasi ya Juu maana hata Nyerere alijua hili kabla hajafariki, IQ yake ni kubwa huwezi kukuta mahali ukawakusanya interlectuls kama alivyofanya kule marekani then ukawaambia nataka tufanye QA session kwa maana yeye atoe maelezo then wao wamwuulize maswali na majibu na tumeona ameweza kuwa convince wote na badala yake sasa ni balaa tupu CCM wanahaha.
      “Problems cannot be solved by the same level of thinking that created them.”“Insanity: doing the same thing over and over again and expecting different results.”" by Albert Einstein"

    22. #59
      kitero's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st February 2012
      Location : Kaskazini
      Posts : 516
      Rep Power : 469
      Likes Received
      97
      Likes Given
      48

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Kunaambao mpaka leo hawajui kwanini watanzania ni maskini.

    23. #60
      Kibanga Ampiga Mkoloni's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th August 2007
      Location : Here! here!
      Posts : 4,768
      Rep Power : 1628
      Likes Received
      1185
      Likes Given
      1701

      Default Re: Dr. Slaa: Mfuko wa cement utakuwa Tshs 5,000.. Ni KWELI 100%

      Well said sister!
      Hili hata kwa NONDO na BATI linawezekana, Kwani halina tofauti na NGUZO ya TANESCO kuuzwa 1 Milioni.
      For the Holy Quran says in Sura 42, verse 41: 'All those who fight when oppressed incur no guilt, but Allah shall punish the oppressor, Come the day.

    Page 3 of 13 FirstFirst 12345 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...