Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Hivi nchi yetu iko salama kama mwaka 1978?

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 35
    1. #1
      Sangarara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 3,297
      Rep Power : 1196
      Likes Received
      1181
      Likes Given
      1554

      Default Hivi nchi yetu iko salama kama mwaka 1978?

      Wakati Nduli Amini anavamia nchi yetu mwaka 1978, Mwalimu nyerere aliweza kuwamobilize watanzania pamoja na majeshi yetu yakaingia vitani na kuweza kumuondoa Amini katika ardhi yetu.

      Nimekuwa najiuliza kwa muda sasa, kwamba iwapo itatokea nchi yetu ikavamiwa na Taifa lolote la Jirani,Je Kiongozi wetu ataweza kutumobile watanzania na kuingia vitani kupambana na adui kama ilivyotokea 1978.

      Sababu kubwa inayonipa mashaka ni kwamba, Kiongozi wetu amepoteza kabisa courage ya kutukabili wananchi wake na kutupa maelekezo, ama makaripio, ama ushauri, ama miongozi, ama ushauri n.k na hata anapopata ujasiri wa kufanya hivyo anaishia ama kwenda kujificha Studio ama kuchagua watu wachache, wazee na kuongea nao.

      Kiongozi wetu amekuwa mlalamishi kama tunavyolalamika sisi, hata pale tunapotegemea kwamba yeye ndio atatoa kauli ya mwisho juu ya swala lenye utata atafanya hivyo kwa kuchelewa sana ama anaweza kuruka kabisa hiyo issue hata kwa kusema na yeye hajui.

      Zaidi, nikiangali dissatisfaction ya wananchi wengi kwa utawala wake, napata shaka kama kweli anaweza akasikilizwa na wananchi wake,na hapa ndio panaponipa hofu zaidi, nabaki kujiuliza au anategemea kutumia nguvu za majeshi yetu peke yake ambayo at least mpaka sasa ndio sehemu kubwa ya Jamii yetu inayoonyesha kumtii.

      Kingine ni kwamba, Hii mifarakano inayojitokeza kati ya majeshi yetu na wananchi, likitokea tatizo la kiusalama inawezekana kweli makundi haya yakashirikiana kwa kufanya kazi moja pamoja?

      Kama haya hayawezekani, ni nini kinaweza kutufanya tukafikiri tuko salama dhidi ya uvamizi kutoka nje, achilia mbali dhidi ya uvamizi kutoka ndani, hapa ndio nakumbuka yaliyotokea Unguja, hivi kweli hakukuwa na mwananchi hata mmoja ambaye alipata taarifa ya mipango ya uhalifu mkubwa namna ile na kuziwasilisha kwa vyombo vya usalama?

      Kwa kweli nimejawa na wasi wasi mkubwa sana, nadhani nahitaji japo maneno ya faraja.

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Matola's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th October 2010
      Posts : 12,465
      Rep Power : 19740
      Likes Received
      5425
      Likes Given
      3612

      Default Re: Hivi nchi yetu iko salama kama mwaka 1978?

      Hakuna vita ya nchi na nchi Dunia ya leo, vita zilizobakia nia za wenyewe kwa wenyewe, hakuna Wanajeshi wowote ambao wako tayari kuvamia nchi za wengine wakati anayewadhurumu ni Raisi wao na watawala wao. Forget kuhusu vita kama ile ya Kagera.

      By the way tua asume kwamba ndio imetokea, basi tutaanza na Mkwele tutamshikiza amtoe Ridhiwani kwenda vitani kama Nyerere alivyowatoa watoto wake 3 kwenda Vitani, Andrew, Madaraka na Makongoro.
      Fredrick Sanga likes this.
      Division four point 29 = Masters Mzumbe University. Nape Nnauye is my role model.

    4. #3
      Sangarara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 3,297
      Rep Power : 1196
      Likes Received
      1181
      Likes Given
      1554

      Default Re: Hivi nchi yetu iko salama kama mwaka 1978?

      Quote By Matola
      Hakuna vita ya nchi na nchi Dunia ya leo, vita zilizobakia nia za wenyewe kwa wenyewe, hakuna Wanajeshi wowote ambao wako tayari kuvamia nchi za wengine wakati anayewadhurumu ni Raisi wao na watawala wao. Forget kuhusu vita kama ile ya Kagera.

      By the way tua asume kwamba ndio imetokea, basi tutaanza na Mkwele tutamshikiza amtoe Ridhiwani kwenda vitani kama Nyerere alivyowatoa watoto wake 3 kwenda Vitani, Andrew, Madaraka na Makongoro.
      Nashukuru kwa maneno yako ya Faraja. ila hiyo kauli yako ya kutaka kumshinikiza mkuu amuambie ridhi kwenda vitani kwanza ndio inayoniny'ong'ony'eza kabisa, maana ake wakati tunahangaika kumshinikiza maadui si tayari watakuwa wanafanya uharibifu mkubwa sana.

      Na hapa ukumbuke kwamba, kitu kilichosaidia majeshi ya tanzania kumfurumusha Nduli kutoka kampala ni dissasification waliyokuwa nayo waganda dhidi ya utawala wake, hawakuona mantiki ya kushiriki vita ile sababu hawakuwa radhi naye tena, ndio tatizo naloliona likipanuka nchini mwangu.

      Hapa ndio napoona kuna tatizo kubwa la kiusalama nchini.

    5. #4
      Ritz's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 1st January 2011
      Location : Republic of Nauru
      Posts : 18,193
      Rep Power : 12563
      Likes Received
      5760
      Likes Given
      753

      Default

      Quote By Matola
      Hakuna vita ya nchi na nchi Dunia ya leo, vita zilizobakia nia za wenyewe kwa wenyewe, hakuna Wanajeshi wowote ambao wako tayari kuvamia nchi za wengine wakati (anayewadhurumu) ni Raisi wao na watawala wao. Forget kuhusu vita kama ile ya Kagera.

      By the way tua asume kwamba ndio imetokea, basi tutaanza na Mkwele tutamshikiza amtoe Ridhiwani kwenda vitani kama Nyerere alivyowatoa watoto wake 3 kwenda Vitani, Andrew, Madaraka na Makongoro.
      (Anayewadhurumu) Anayewadhulumu...wewe utakuwa mtu wa Kamachumu au Muleba.

    6. #5
      kizomanizo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 26th January 2010
      Location : Arusha, Tanzania
      Posts : 35
      Rep Power : 480
      Likes Received
      7
      Likes Given
      1

      Default Re: Hivi nchi yetu iko salama kama mwaka 1978?

      Quote By ritz
      (Anayewadhurumu) Anayewadhulumu...wewe utakuwa mtu wa Kamachumu au Muleba.
      So does that refute his right to comment on these very forums?

    7. Miaka 50

    8. #6
      Matola's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th October 2010
      Posts : 12,465
      Rep Power : 19740
      Likes Received
      5425
      Likes Given
      3612

      Default Re: Hivi nchi yetu iko salama kama mwaka 1978?

      Quote By ritz
      (Anayewadhurumu) Anayewadhulumu...wewe utakuwa mtu wa Kamachumu au Muleba.
      Unafahamu vyema kabisa kwamba sheria na kanuni za JF ni kosa linalostahili ban ku edit comment ya member mwingine bila ridhaa yake, na kama unajiona wewe ni mahiri wa lugha ni kwanini usiende kule Jukwaa la lugha ukatowe mchango wako?
      Fredrick Sanga likes this.
      Division four point 29 = Masters Mzumbe University. Nape Nnauye is my role model.

    9. #7
      Sangarara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 3,297
      Rep Power : 1196
      Likes Received
      1181
      Likes Given
      1554

      Default Re: Hivi nchi yetu iko salama kama mwaka 1978?

      Quote By ritz
      (Anayewadhurumu) Anayewadhulumu...wewe utakuwa mtu wa Kamachumu au Muleba.
      Ritz, Nilitegemea kuona maneno yako ya faraja na sio kubrust watu kiajabu ajabu.

    10. #8
      PANAFRICA's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 4
      Rep Power : 0
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Hivi nchi yetu iko salama kama mwaka 1978?

      Mimi naona tuko vitani kwani maana ya vita ni uharibifu wa mali na kukatisha uhai wa watu.ufisadi unaoitafuna nchi yetu ni vita kamili, kwa sabubu mali ya wananchi inaharibiwa kwa kutafunwa na watu wachache, matokeo yake watu wanakufa kwa kukosa huduma muhimu kama ilivyotokea Muhimbili na Hospitali nyinginezo kutokana na mgomo wa madakitali, ambao wanahangaika usiku na mchana huku wakiambulia kiduchu, wakati adui fisadi akiendelea kupiga balistic misile mpaka bungeni.
      wako wananchi wengi ambao wanaendelea kupoteza maisha kwa kukosa huduma muhimu kutokana na umaskini uliokithiri. Kaka funguka tuko vitani bana!

    11. #9
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,177
      Rep Power : 3549
      Likes Received
      3049
      Likes Given
      460

      Default Re: Hivi nchi yetu iko salama kama mwaka 1978?

      Oh Man... Why R we going back there again? Let us Move ON we have Major issue here... UAMSHO - Waamshwe au La?

      Wakimbie au La... Sasa ya 1978 ya Kamanyola, ya TanBond na Sabuni za Mbuni... Tuache tuishi ndugu yetu...
      Sangarara likes this.

    12. #10
      Azimio Jipya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Location : Universal Space Station
      Posts : 3,281
      Rep Power : 5414
      Likes Received
      1006
      Likes Given
      1731

      Default Re: Hivi nchi yetu iko salama kama mwaka 1978?

      Quote By Sangarara
      Wakati Nduli Amini anavamia nchi yetu mwaka 1978, Mwalimu nyerere aliweza kuwamobilize watanzania pamoja na majeshi yetu yakaingia vitani na kuweza kumuondoa Amini katika ardhi yetu.

      Nimekuwa najiuliza kwa muda sasa, kwamba iwapo itatokea nchi yetu ikavamiwa na Taifa lolote la Jirani,Je Kiongozi wetu ataweza kutumobile watanzania na kuingia vitani kupambana na adui kama ilivyotokea 1978.

      Sababu kubwa inayonipa mashaka ni kwamba, Kiongozi wetu amepoteza kabisa courage ya kutukabili wananchi wake na kutupa maelekezo, ama makaripio, ama ushauri, ama miongozi, ama ushauri n.k na hata anapopata ujasiri wa kufanya hivyo anaishia ama kwenda kujificha Studio ama kuchagua watu wachache, wazee na kuongea nao.

      Kiongozi wetu amekuwa mlalamishi kama tunavyolalamika sisi, hata pale tunapotegemea kwamba yeye ndio atatoa kauli ya mwisho juu ya swala lenye utata atafanya hivyo kwa kuchelewa sana ama anaweza kuruka kabisa hiyo issue hata kwa kusema na yeye hajui.

      Zaidi, nikiangali dissatisfaction ya wananchi wengi kwa utawala wake, napata shaka kama kweli anaweza akasikilizwa na wananchi wake,na hapa ndio panaponipa hofu zaidi, nabaki kujiuliza au anategemea kutumia nguvu za majeshi yetu peke yake ambayo at least mpaka sasa ndio sehemu kubwa ya Jamii yetu inayoonyesha kumtii.

      Kingine ni kwamba, Hii mifarakano inayojitokeza kati ya majeshi yetu na wananchi, likitokea tatizo la kiusalama inawezekana kweli makundi haya yakashirikiana kwa kufanya kazi moja pamoja?

      Kama haya hayawezekani, ni nini kinaweza kutufanya tukafikiri tuko salama dhidi ya uvamizi kutoka nje, achilia mbali dhidi ya uvamizi kutoka ndani, hapa ndio nakumbuka yaliyotokea Unguja, hivi kweli hakukuwa na mwananchi hata mmoja ambaye alipata taarifa ya mipango ya uhalifu mkubwa namna ile na kuziwasilisha kwa vyombo vya usalama?

      Kwa kweli nimejawa na wasi wasi mkubwa sana, nadhani nahitaji japo maneno ya faraja.
      sangara, umeongea jambo kubwa!!

      Ruanda karibuni itachapa Tanzania hadi mpaka wa Msumbiji ... wait and see!!

      Taifa lillopoteza Utu wake na kuwa lege lege kabisa ... ni kama "mwanamke aliyevaa kwa kutojiheshimu" ... anashawishi kumjaribu... na kila mtu anajihisi kumjaribu .. You know what guys ...soon tutajaribiwa ni kiinchi kidogo kabisa cha jirani ... NA BILA UTU WA TAIFA hakuna uzalendo na hapo ndipo utakuja gundua NGUVU YA UTU WA TAIFA vs SILAHA NZITO ZA TAIFA ... silaha is nothing kama hatuna UTU na uadilifu wake wote kwenye ngazi zote za Uogozi wa Jamii na Taifa kwa ujumla wake!!

      Huu ujumbe ni wa muhimu kuliko wengi wanvyodhania ... MUNGU IBARIKI TANZANIA ILIYOPOTEZA UZALENDO WOTE sasa ni debe tupu!!!
      Sangarara and JingalaFalsafa like this.
      Never Get Angry; Never Make Threat; Reason With People;
      "Napenda the logic of the words because in some ways it says about individual-not to use emotions-when scrutinizing something, whether it involves you or not" ...-by AshaDiii @ Jamiiforums 26th July 2011.


    13. #11
      Sangarara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 3,297
      Rep Power : 1196
      Likes Received
      1181
      Likes Given
      1554

      Default Re: Hivi nchi yetu iko salama kama mwaka 1978?

      Quote By Azimio Jipya
      sangara, umeongea jambo kubwa!!

      Ruanda karibuni itachapa Tanzania hadi mpaka wa Msumbiji ... wait and see!!

      Taifa lillopoteza Utu wake na kuwa lege lege kabisa ... ni kama "mwanamke aliyevaa kwa kutojiheshimu" ... anashawishi kumjaribu... na kila mtu anajihisi kumjaribu .. You know what guys ...soon tutajaribiwa ni kiinchi kidogo kabisa cha jirani ... NA BILA UTU WA TAIFA hakuna uzalendo na hapo ndipo utakuja gundua NGUVU YA UTU WA TAIFA vs SILAHA NZITO ZA TAIFA ... silaha is nothing kama hatuna UTU na uadilifu wake wote kwenye ngazi zote za Uogozi wa Jamii na Taifa kwa ujumla wake!!

      Huu ujumbe ni wa muhimu kuliko wengi wanvyodhania ... MUNGU IBARIKI TANZANIA ILIYOPOTEZA UZALENDO WOTE sasa ni debe tupu!!!
      Au hatujawahi kuwa wamoja wala wazalendo?

    14. #12
      Sangarara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 3,297
      Rep Power : 1196
      Likes Received
      1181
      Likes Given
      1554

      Default Re: Hivi nchi yetu iko salama kama mwaka 1978?

      Quote By PANAFRICA
      Mimi naona tuko vitani kwani maana ya vita ni uharibifu wa mali na kukatisha uhai wa watu.ufisadi unaoitafuna nchi yetu ni vita kamili, kwa sabubu mali ya wananchi inaharibiwa kwa kutafunwa na watu wachache, matokeo yake watu wanakufa kwa kukosa huduma muhimu kama ilivyotokea Muhimbili na Hospitali nyinginezo kutokana na mgomo wa madakitali, ambao wanahangaika usiku na mchana huku wakiambulia kiduchu, wakati adui fisadi akiendelea kupiga balistic misile mpaka bungeni.
      wako wananchi wengi ambao wanaendelea kupoteza maisha kwa kukosa huduma muhimu kutokana na umaskini uliokithiri. Kaka funguka tuko vitani bana!
      Mbona sioni kama Rais anatuunganisha katika vita hivi? Au kuna kitu sielewi, Huyu ni Rais wa Watanzania au Kiongozi wa serikali?

    15. #13
      JingalaFalsafa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th April 2012
      Location : Africa.
      Posts : 336
      Rep Power : 425
      Likes Received
      211
      Likes Given
      80

      Default

      Quote By Azimio Jipya
      sangara, umeongea jambo kubwa!!

      Ruanda karibuni itachapa Tanzania hadi mpaka wa Msumbiji ... wait and see!!

      Taifa lillopoteza Utu wake na kuwa lege lege kabisa ... ni kama "mwanamke aliyevaa kwa kutojiheshimu" ... anashawishi kumjaribu... na kila mtu anajihisi kumjaribu .. You know what guys ...soon tutajaribiwa ni kiinchi kidogo kabisa cha jirani ... NA BILA UTU WA TAIFA hakuna uzalendo na hapo ndipo utakuja gundua NGUVU YA UTU WA TAIFA vs SILAHA NZITO ZA TAIFA ... silaha is nothing kama hatuna UTU na uadilifu wake wote kwenye ngazi zote za Uogozi wa Jamii na Taifa kwa ujumla wake!!

      Huu ujumbe ni wa muhimu kuliko wengi wanvyodhania ... MUNGU IBARIKI TANZANIA ILIYOPOTEZA UZALENDO WOTE sasa ni debe tupu!!!
      Pamoja sana mkuu.
      Mifumo tuliyojichagulia kutusimamia ndio adui wa kwanza katika hili. Imejinga chuki na visasi baina yetu, imefanya mtu ajifikirie binafsi badala ya umma, hatuwezi kujenga utaifa katika hili. Tumelubuniwa na demokrasia, tukafurahia kinachoitwa UHURU-HAKI. Leo mtu haoni ajabu kuweka mikate store hali jirani yake hajala siku ya pili...kwenye mikutano ya hadhara(iwe ya dini, siasa, uchumi nk) anajitunisha kifua mbele...na kujiita mzalendo-mtanzania. Kwao taifa ni ramani yake na jina tu, akishavipenda hivyo imetosha. Amesahau kuwa taifa halikamiliki pasi kuwa na watu....na ndio hao majirani zake.
      Leo itokee vita watoto wa Lowasa, Kikwete, Mengi nk. hatutowaona kushika japo kisu vitani, watakwea mapipa kwenda ng'ambo. Sasa kwanini kapuku mie nijitolee kufa kwa maslahi ya watu wachache wabnafsi? Haiingii akilini. Sitoacha kusema "HAKI ZA BINADAMU" ni mtego mbaya sana unaoleta na kupalilia unyonge wetu.
      Mungu wetu anaita.

    16. #14
      Sangarara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 3,297
      Rep Power : 1196
      Likes Received
      1181
      Likes Given
      1554

      Default Re: Hivi nchi yetu iko salama kama mwaka 1978?

      Quote By JingalaFalsafa
      Pamoja sana mkuu.
      Mifumo tuliyojichagulia kutusimamia ndio adui wa kwanza katika hili. Imejinga chuki na visasi baina yetu, imefanya mtu ajifikirie binafsi badala ya umma, hatuwezi kujenga utaifa katika hili. Tumelubuniwa na demokrasia, tukafurahia kinachoitwa UHURU-HAKI. Leo mtu haoni ajabu kuweka mikate store hali jirani yake hajala siku ya pili...kwenye mikutano ya hadhara(iwe ya dini, siasa, uchumi nk) anajitunisha kifua mbele...na kujiita mzalendo-mtanzania. Kwao taifa ni ramani yake na jina tu, akishavipenda hivyo imetosha. Amesahau kuwa taifa halikamiliki pasi kuwa na watu....na ndio hao majirani zake.
      Leo itokee vita watoto wa Lowasa, Kikwete, Mengi nk. hatutowaona kushika japo kisu vitani, watakwea mapipa kwenda ng'ambo. Sasa kwanini kapuku mie nijitolee kufa kwa maslahi ya watu wachache wabnafsi? Haiingii akilini. Sitoacha kusema "HAKI ZA BINADAMU" ni mtego mbaya sana unaoleta na kupalilia unyonge wetu.
      Mungu wetu anaita.
      Maneno yako ni mazito sana mkuu, yamenipiga na kunichana kabisa, unanifanya nijiulize kama, Tanzania ni kitu halisia au ni matokeo ya art.

    17. #15
      JingalaFalsafa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th April 2012
      Location : Africa.
      Posts : 336
      Rep Power : 425
      Likes Received
      211
      Likes Given
      80

      Default

      Quote By Sangarara
      Maneno yako ni mazito sana mkuu, yamenipiga na kunichana kabisa, unanifanya nijiulize kama, Tanzania ni kitu halisia au ni matokeo ya art.
      Sio Tanzania pekee, ni Afrika yote ni matokeo ya sanaa kubwa. Wanacheza na akili zetu, ni sanaa ya hali ya juu kabisa, watu wamekaa chini na kuumiza vichwa mno ili kuendeleza unyonge wetu kwa maslahi yao, wamefanya analysis, speculations, synsthesis, innovations nk kutuingiza mtegoni. Cha kushangaza sisi tunachukulia mambo rahisi rahisi tu, eti kujipanga kwenye misululu mirefu na kwa wingi kuleta mabadiliko kwenye kiboksi cha kura. TUMEROGWA, NA TUNAKENUA MENO BADO. Ni lazima tukae chini tuumize vichwa mara mbili ya vile walivyoumiza wao. UBUNIFU HAUJAWAI KUFIKA MWISHO, TUNAWEZA. Nguvu yetu ni UMOJA na KUTHUBUTU. Kiboksi cha kura hakiwezi kumaliza "mental slavery" vichwani mwetu, ila kuupalilia tu. MUNGU WETU ANAITA!

    18. #16
      Sangarara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 3,297
      Rep Power : 1196
      Likes Received
      1181
      Likes Given
      1554

      Default Re: Hivi nchi yetu iko salama kama mwaka 1978?

      Quote By JingalaFalsafa
      Sio Tanzania pekee, ni Afrika yote ni matokeo ya sanaa kubwa. Wanacheza na akili zetu, ni sanaa ya hali ya juu kabisa, watu wamekaa chini na kuumiza vichwa mno ili kuendeleza unyonge wetu kwa maslahi yao, wamefanya analysis, speculations, synsthesis, innovations nk kutuingiza mtegoni. Cha kushangaza sisi tunachukulia mambo rahisi rahisi tu, eti kujipanga kwenye misululu mirefu na kwa wingi kuleta mabadiliko kwenye kiboksi cha kura. TUMEROGWA, NA TUNAKENUA MENO BADO. Ni lazima tukae chini tuumize vichwa mara mbili ya vile walivyoumiza wao. UBUNIFU HAUJAWAI KUFIKA MWISHO, TUNAWEZA. Nguvu yetu ni UMOJA na KUTHUBUTU. Kiboksi cha kura hakiwezi kumaliza "mental slavery" vichwani mwetu, ila kuupalilia tu. MUNGU WETU ANAITA!
      Unamaanisha kwamba hata watawala tulionao ni moja wa maadui wakubwa wa maendeleo yetu ya Kifikra na kiuchumi? ndio maana sasa hakuna kiongozi anaweza akatuelezea muungano wa tanganyika na zanzibar bila kutumia vitisho? na sahihi kabisa kuamini kwamba kwa muda mrefu watu wachache wametumia opportunity ya ujinga wetu kujineemesha huku wakitumbaza kwamba sisi ni wamoja? thanks to the expanding gap between the rich and the poor, sababu sasa hata dhamira zetu halisi japo ni primitive lakini zinadhihirika, no wonder why the president is very unconfortable to approach us.
      Profesa likes this.

    19. #17
      Azimio Jipya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Location : Universal Space Station
      Posts : 3,281
      Rep Power : 5414
      Likes Received
      1006
      Likes Given
      1731

      Default Re: Hivi nchi yetu iko salama kama mwaka 1978?

      Quote By JingalaFalsafa
      Pamoja sana mkuu.
      Mifumo tuliyojichagulia kutusimamia ndio adui wa kwanza katika hili. Imejinga chuki na visasi baina yetu, imefanya mtu ajifikirie binafsi badala ya umma, hatuwezi kujenga utaifa katika hili. Tumelubuniwa na demokrasia, tukafurahia kinachoitwa UHURU-HAKI. Leo mtu haoni ajabu kuweka mikate store hali jirani yake hajala siku ya pili...kwenye mikutano ya hadhara(iwe ya dini, siasa, uchumi nk) anajitunisha kifua mbele...na kujiita mzalendo-mtanzania. Kwao taifa ni ramani yake na jina tu, akishavipenda hivyo imetosha. Amesahau kuwa taifa halikamiliki pasi kuwa na watu....na ndio hao majirani zake.
      Leo itokee vita watoto wa Lowasa, Kikwete, Mengi nk. hatutowaona kushika japo kisu vitani, watakwea mapipa kwenda ng'ambo. Sasa kwanini kapuku mie nijitolee kufa kwa maslahi ya watu wachache wabnafsi? Haiingii akilini. Sitoacha kusema "HAKI ZA BINADAMU" ni mtego mbaya sana unaoleta na kupalilia unyonge wetu.
      Mungu wetu anaita.
      JingalaFalsafa, Ukishautupa mfumo uliojijenga kwa dhati ndani ya uasili na haki za binadamu, chochote kingine kinachofuatia hapo kinamfaa nini binadamu? Nani kasema, Kitaamfaa vipi wakati kimesha potoka kuanzia kwenye shina?

      Kama ubinaadamu haki zake na ukamilifu wake kijamii sio sera ya jamii na Taifa kimatendo, mtu akimkimbiza albino kama swala anavyokimbizwa na chui na akadakwa akafanywa kitoweo na mkubwa huyo kajipatia rizki akayaita hayo maendelo nanai atauliza? Aulizwe kwa msingi upi sasa wa ubinadamu au Unyama? Kwani kutwaa mikate tele na kuifungia stoo huku jirani anakufa kunatofautiana vipi na kumuanagamiza albino na kudai hayo ni maendeleo!

      Kwani kupewa Magari 5 ya kifahari na mtoto kupelekwa shule ulaya na kuachia vitalu vya thamani ya mamilioni kwa mwekezaji, machimbo ya almasi nk huko si sawa na kumuangamiza albino!?

      Lakini hilo linafanyika na madai ni kuwa wanatumia haki na uhuru wao! Mfumo unaruhusu na "mahesabu" yanaonyesha Taifa limeendeela na kusonga mbele! Huku ubinafsi ukishamiri na kusambaratisha Umoja ambao ndio msingi wa utu wetu.

      Mwaka 1978 hatukuwa tumefikia "kiwango cha chini kama cha leo cha ubinadamu" ambao ndio uasili unatutofautisha na swokwe wa manyara na tumbili wa serengeti! Lakini wanadai wana PhD na zimeogezeka sasa kuliko huko tulipotoka!! Na Taifa linasonga mbele na tunakubalika kimataifa ... Nonsense!!

      Kwa mtizamo huo ni msukumo gani wa kulitetea Taifa kama kichapo alichokipata Nduli!!! Kwani katika upofu uliotanda fikra, kauli na matendo silahaya yaweza kuonekana kuwa ni vifaru na ndege na wala sio NGUVU YA UMMOJA NA UBINNADA WETU nyuma ya silaha hizo!! Kwani huyo nduli hakuwa na silaha??

      Leo? Kwani adui yuko nje ya nchi! Hata akija hawa amabao wameshaisaliti nchi watampinga? Kwa ubinaadamu na Utu Upi??? Kwani hawajamuunga mkono bado? Vita ya kutetea Uasili wako kama ubinaadamu, utu na nidhamu katika hayo ikishakushinda ..Utashinda Vita ipi nyingine!!!?
      JingalaFalsafa likes this.
      Never Get Angry; Never Make Threat; Reason With People;
      "Napenda the logic of the words because in some ways it says about individual-not to use emotions-when scrutinizing something, whether it involves you or not" ...-by AshaDiii @ Jamiiforums 26th July 2011.


    20. #18
      Azimio Jipya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Location : Universal Space Station
      Posts : 3,281
      Rep Power : 5414
      Likes Received
      1006
      Likes Given
      1731

      Default Re: Hivi nchi yetu iko salama kama mwaka 1978?

      Quote By JingalaFalsafa
      Sio Tanzania pekee, ni Afrika yote ni matokeo ya sanaa kubwa. Wanacheza na akili zetu, ni sanaa ya hali ya juu kabisa, watu wamekaa chini na kuumiza vichwa mno ili kuendeleza unyonge wetu kwa maslahi yao, wamefanya analysis, speculations, synsthesis, innovations nk kutuingiza mtegoni. Cha kushangaza sisi tunachukulia mambo rahisi rahisi tu, eti kujipanga kwenye misululu mirefu na kwa wingi kuleta mabadiliko kwenye kiboksi cha kura. TUMEROGWA, NA TUNAKENUA MENO BADO. Ni lazima tukae chini tuumize vichwa mara mbili ya vile walivyoumiza wao. UBUNIFU HAUJAWAI KUFIKA MWISHO, TUNAWEZA. Nguvu yetu ni UMOJA na KUTHUBUTU. Kiboksi cha kura hakiwezi kumaliza "mental slavery" vichwani mwetu, ila kuupalilia tu. MUNGU WETU ANAITA!
      Mental slavery nalo ni eneo pana lilisahaulika! Likiachwa kutatuliwa na elimu ya kawaida ya darasani ...lakini ni kweli elimu ya darasa la kwanza hadi la mwisho juu kabisa linamweza kukabili tatizo hili?

      Maana leo wasomi wakubwa wametanda nchi nzima ...Tanzania na Africa wana shahada zote zilizopo anazotakiwa kuwa nazo msomi ... lakini Babu yake alipewa shanga akaachia kisiwa kizima chenye ardhi kubwa kwa MKOLONI mwekezaji wa enzi hizo. Msomi huyo huyo leo hii anjengewa nyumaba moja self contained na kigari anaaachia Mgodi mzima wa almasi!

      Kasoma sawa!! Lakini Fikra kweli ziko Timamu na kamilifu?

      Kweli aatwaeza kupigania Taifa lake kwenye vita ya vifaru na ndege za anagani au hata vita ya kisiasa na kiuchumi? Vita ipi ataweza Mtanzania kama huyu ...!!

      Turudi nyuma tutizame upya maana ya elimu!

      Elimu ya KIAKILI PEKE yake haitatufikisha Kuna elimu nyingine ..ELIMU YA UBINAADAMU NA UTU WA MTU!
      Never Get Angry; Never Make Threat; Reason With People;
      "Napenda the logic of the words because in some ways it says about individual-not to use emotions-when scrutinizing something, whether it involves you or not" ...-by AshaDiii @ Jamiiforums 26th July 2011.


    21. #19
      Lavie's Avatar
      Member Array
      Join Date : 3rd April 2012
      Posts : 61
      Rep Power : 371
      Likes Received
      15
      Likes Given
      0

      Default Re: Hivi nchi yetu iko salama kama mwaka 1978?

      Bora tuvamiwe ili tujiunge na wavamizi kung'oa CCM na magamba yake.

    22. #20
      Sangarara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 3,297
      Rep Power : 1196
      Likes Received
      1181
      Likes Given
      1554

      Default Re: Hivi nchi yetu iko salama kama mwaka 1978?

      Quote By Azimio Jipya
      Mental slavery nalo ni eneo pana lilisahaulika! Likiachwa kutatuliwa na elimu ya kawaida ya darasani ...lakini ni kweli elimu ya darasa la kwanza hadi la mwisho juu kabisa linamweza kukabili tatizo hili?

      Maana leo wasomi wakubwa wametanda nchi nzima ...Tanzania na Africa wana shahada zote zilizopo anazotakiwa kuwa nazo msomi ... lakini Babu yake alipewa shanga akaachia kisiwa kizima chenye ardhi kubwa kwa MKOLONI mwekezaji wa enzi hizo. Msomi huyo huyo leo hii anjengewa nyumaba moja self contained na kigari anaaachia Mgodi mzima wa almasi!

      Kasoma sawa!! Lakini Fikra kweli ziko Timamu na kamilifu?

      Kweli aatwaeza kupigania Taifa lake kwenye vita ya vifaru na ndege za anagani au hata vita ya kisiasa na kiuchumi? Vita ipi ataweza Mtanzania kama huyu ...!!

      Turudi nyuma tutizame upya maana ya elimu!

      Elimu ya KIAKILI PEKE yake haitatufikisha Kuna elimu nyingine ..ELIMU YA UBINAADAMU NA UTU WA MTU!
      Unamaana sisi bado ni slaves as far as our thinking is concerned??

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...