Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Pinda aumbuliwa bungeni

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 36
    1. #1
      dosama's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th December 2010
      Posts : 736
      Rep Power : 573
      Likes Received
      296
      Likes Given
      1

      Default Pinda aumbuliwa bungeni

      ZIARA iliyofanywa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika Wilaya ya Maswa mkoani Simiyu, imezua tafrani jana baada ya Mbunge wa Viti Maalum, Rose Kamili (CHADEMA), kudai kuwa Mkuu wa Wilaya hiyo aliwakamata na kuwaweka ndani watendaji wa vijiji kwa kushindwa kutoa mbuzi kama zawadi kwa waziri huyo.

      Wakati akiuliza swali bungeni, bila kutaja jina, Kamili alisema mkuu huyo wa wilaya alifanya hivyo, baada ya watendaji hao kushindwa kuchangia mbuzi tisa kwa Waziri Mkuu, aliyefanya ziara mkoani humo Februari 23, mwaka huu.

      Hata hivyo, aliyekuwa mkuu wa wilaya wakati huo, ni Kapteni mstaafu, James Yamungu ambaye kwa sasa amehamishiwa Wilaya ya Serengeti, mkoani Mara.

      Swali la mbunge huyo lilimfanya Waziri Pinda, kuduwaa huku akiwa ameshika tama, na kuzua minong’ono na miguno kutoka kwa wabunge wengi.

      “Mheshimiwa Spika, ninahitaji ufafanuzi wa kisheria kwa hili la baadhi ya ma-DC, ambapo huwaagiza watendaji kufanya mambo kinyume cha sheria na pindi wasipofanya huwaweka ndani kwa muda wa siku saba.

      “Na mfano halisi ni hili lililotokea wilayani Maswa, katika ziara ya Waziri Mkuu Februari mwaka huu, katika Mkoa wa Shinyanga, ambapo mkuu huyo wa wilaya aliwaweka ndani watendaji wa kata kwa kushindwa kukusanya mbuzi tisa kwa ajili ya zawadi kwa Waziri Mkuu.”

      Swali hili lilimfanya Spika wa Bunge, Anne Makinda, kumtaka mbunge huyo kuthibitisha kwa ushahidi kutokana na jambo hilo kugusa hisia kali kwa Bunge na taifa kwa ujumla, hivyo kutaka kuleta ushahidi.

      Mbunge huyo alisema kuwa anao ushahidi, na kwamba hata jambo hilo lilitangazwa na baadhi ya runinga hapa nchini, hoja ambayo hata hivyo ilionekana kuwa nyepesi kiasi cha Spika Makinda, kuwataka wabunge kuwa makini katika maswali na hoja wanazozitoa bungeni.

      Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa TAMISEMI, Aggrey Mwanri, alisema serikali haijawahi kumwagiza mtendaji yeyote wa serikali kuchangisha wananchi kwa nguvu katika ziara za viongozi wa juu wa serikali.

      Hata hivyo, alisema hoja ya mbunge huyo si ngeni kwani iliwahi kuibuliwa na ikamlazimu aliyekuwa Waziri wa Tamisemi, George Mkuchika, kwenda hadi Maswa kuzungumza na wananchi ili kupata maelezo ya kina.

      “Baada ya kufanya mkutano na wananchi hao, ilibainika kwamba si la kweli. Lakini kama mbunge ana ushahidi mpya tunamuomba atuletee na huyo DC tutamshughulikia kwa mujibu wa sheria,” alisema Mwanri.

      Alifafanua kuwa wakuu wa mikoa na wilaya wana haki ya kuingilia kati utendaji wa ngazi za chini, zikiwemo halmashauri, ikiwa tu kuna hatari ya usalama ama mali ya taifa, vinginevyo hawaruhusiwi kuzuia ama kutoa maelezo mengine nje ya maamuzi sahihi ya kisera na kikanuni yaliyoamriwa na mamlaka za halmashauri za miji ama vijiji.

      “Majukumu ya Mkuu wa Wilaya yametajwa katika kifungu namba 14, 1 hadi 3 cha sheria za Serikali za Mikoa namba 19 ya mwaka 1997 kwamba yeye ndiye msimamizi mkuu wa serikali katika wilaya yake.


      Concern
      Hapo ni waziri mkuu je na rais huwa inakuwaje

    2. RukaaJuu Final

    3. #2
      Janjaweed's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th January 2010
      Posts : 3,626
      Rep Power : 1130
      Likes Received
      1391
      Likes Given
      1541

      Default Re: Pinda aumbuliwa bungeni

      ndio ukweli

      kuna waganga wa wilaya wanalazimika kuruhusu bajeti za afya kusaidia mbio za mwenge au hata kulipia ubwabwa wa wanasiasa
      Kama Vipi nipotezee tu; ntakuboa....

    4. #3
      Mjomba wa taifa's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 20th April 2012
      Posts : 107
      Rep Power : 379
      Likes Received
      56
      Likes Given
      0

      Default Mizengo Pinda unawakamua Masikini wenzako hadi mbuzi!!!!!

      Ni habari ya kushtua kusikia Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Pinda a.k.a mtoto wa mkulima amewakamua watoto wa wakulima wenzake tena wanaotumia jembe la mkono wilayani Maswa kwa kuchangisha mbuzi 9 kama zawadi kwake. Haijalishi ni nani aliyemwamuru Ofisa Mtendaji kutafuta mbuzi hao bali hali hiyo imedhihirisha katika ziara za wakubwa hawa zimekuwa zikiendana na kuwakamua wananchi masikini mali zao.

      Hivi kweli kiongozi kama waziri Mkuu anakosa pesa ya kununua mbuzi 9? hadi asubiri wanakijiji walazimishwe kuchanga vijisenti vyao wanavyovipata kwa tabu huku kila siku wakitawaliwa na vifo vya watoto kwa kukosa hata shilingi mia moja ya kununua PANADOL.

      Jamani! Kweli! kwelin Pinda unayafanya haya???

      Mambo haya tumeyazoea kuyaona kwa marais wasiokuwa na haya wala aibu wanapostaafu nyadhifa zao katika Chama na nchi wanachangiwa vitu mbalimbali kila mkoa bila kuhoji mali hizo zimetoka katika fungu lipi la bajeti. Tuliyashuhudia mwaka 2007 wakati Mkapa anaachia Uenyekiti taifa wa CCM.

    5. #4
      Jadi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd August 2011
      Posts : 361
      Rep Power : 467
      Likes Received
      69
      Likes Given
      7

      Default Re: Mizengo Pinda unawakamua Masikini wenzako hadi mbuzi!!!!!

      eti na Mwanri anamlazimisha mbunge alete ushahidi,kweli kazi, wao ndo walitakiwa wamchunguze DC wao,inawezekana huyu DC ni mpya anafikiri TZ bado ipo enzi za ukoloni

    6. #5
      mgeni wenu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd January 2012
      Posts : 1,157
      Rep Power : 891
      Likes Received
      578
      Likes Given
      0

      Default Re: Mizengo Pinda unawakamua Masikini wenzako hadi mbuzi!!!!!

      Nani kakwambia pinda ni maskini? Unadhani kukusanya mbuzi 9 katika kila kata kwa mikoa yote kuna maskini hapo?
      Ahh pinda Mzee wa Mbuzii kuwa na huruma basi

    7. Miaka 50

    8. #6
      Janja PORI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2011
      Posts : 662
      Rep Power : 653
      Likes Received
      86
      Likes Given
      0

      Default Re: Mizengo Pinda unawakamua Masikini wenzako hadi mbuzi!!!!!

      duuuuuuuuuuuuuuuee

    9. #7
      Elli's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 17th March 2008
      Location : Kijito-Upele
      Posts : 8,571
      Rep Power : 2551
      Likes Received
      2142
      Likes Given
      1862

      Default Re: Mizengo Pinda unawakamua Masikini wenzako hadi mbuzi!!!!!

      Pinda awakamua mbuzi? nilielewa vibaya kumbe ila wote tu ni wezi wanatofautiana tu namna na aina ya wizi

    10. #8
      Mwanaweja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th February 2011
      Posts : 3,483
      Rep Power : 1116
      Likes Received
      469
      Likes Given
      962

      Default Re: Mizengo Pinda unawakamua Masikini wenzako hadi mbuzi!!!!!

      niliisikia hii bungeni jana mbunge wa viti maalumu aliibua ni aibu kwa watendaji, waziri mkuu na serikali kwa ujumla

    11. #9
      Mwanajamii's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th March 2008
      Posts : 7,085
      Rep Power : 1810
      Likes Received
      24
      Likes Given
      13

      Default Re: Mizengo Pinda unawakamua Masikini wenzako hadi mbuzi!!!!!

      Quote By Mjomba wa taifa
      Ni habari ya kushtua kusikia Waziri Mkuu Mizengo Kayanza Pinda a.k.a mtoto wa mkulima amewakamua watoto wa wakulima wenzake tena wanaotumia jembe la mkono wilayani Maswa kwa kuchangisha mbuzi 9 kama zawadi kwake. Haijalishi ni nani aliyemwamuru Ofisa Mtendaji kutafuta mbuzi hao bali hali hiyo imedhihirisha katika ziara za wakubwa hawa zimekuwa zikiendana na kuwakamua wananchi masikini mali zao.

      Hivi kweli kiongozi kama waziri Mkuu anakosa pesa ya kununua mbuzi 9? hadi asubiri wanakijiji walazimishwe kuchanga vijisenti vyao wanavyovipata kwa tabu huku kila siku wakitawaliwa na vifo vya watoto kwa kukosa hata shilingi mia moja ya kununua PANADOL.

      Jamani! Kweli! kwelin Pinda unayafanya haya???

      Mambo haya tumeyazoea kuyaona kwa marais wasiokuwa na haya wala aibu wanapostaafu nyadhifa zao katika Chama na nchi wanachangiwa vitu mbalimbali kila mkoa bila kuhoji mali hizo zimetoka katika fungu lipi la bajeti. Tuliyashuhudia mwaka 2007 wakati Mkapa anaachia Uenyekiti taifa wa CCM.
      Hivi hili lina tofauti gani na lile la baadhi ya vyama vya siasa kuwakamua wapiga kura kwa kutembeza bakuli eti kwa madai kuwa hawana pesa, wakati tunajua wazi kuwa vinapata ruzuku, misaada toka ndani na nje ya nchi na vyanzo vingine vyingi.

    12. #10
      rosemarie's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2011
      Posts : 4,732
      Rep Power : 1367
      Likes Received
      280
      Likes Given
      142

      Default Pinda aumbuliwa bungeni

      ZIARA iliyofanywa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda katika Wilaya ya Maswa mkoani Simiyu, imezua tafrani jana baada ya Mbunge wa Viti Maalum, Rose Kamili (CHADEMA), kudai kuwa Mkuu wa Wilaya hiyo aliwakamata na kuwaweka ndani watendaji wa vijiji kwa kushindwa kutoa mbuzi kama zawadi kwa waziri huo.Wakati akiuliza swali bungeni, bila kutaja jina, Kamili alisema mkuu huyo wa wilaya alifanya hivyo, baada ya watendaji hao kushindwa kuchangia mbuzi tisa kwa Waziri Mkuu, aliyefanya ziara mkoani humo Februari 23, mwaka huu.Hata hivyo, aliyekuwa mkuu wa wilaya wakati huo, ni Kapteni mstaafu, James Yamungu ambaye kwa sasa amehamishiwa Wilaya ya Serengeti, mkoani Mara.Swali la mbunge huyo lilimfanya Waziri Pinda, kuduwaa huku akiwa ameshika tama, na kuzua minong’ono na miguno kutoka kwa wabunge wengi.“Mheshimiwa Spika, ninahitaji ufafanuzi wa kisheria kwa hili la baadhi ya ma-DC, ambapo huwaagiza watendaji kufanya mambo kinyume cha sheria na pindi wasipofanya huwaweka ndani kwa muda wa siku saba.“Na mfano halisi ni hili lililotokea wilayani Maswa, katika ziara ya Waziri Mkuu Februari mwaka huu, katika Mkoa wa Shinyanga, ambapo mkuu huyo wa wilaya aliwaweka ndani watendaji wa kata kwa kushindwa kukusanya mbuzi tisa kwa ajili ya zawadi kwa Waziri Mkuu.”Swali hili lilimfanya Spika wa Bunge, Anne Makinda, kumtaka mbunge huyo kuthibitisha kwa ushahidi kutokana na jambo hilo kugusa hisia kali kwa Bunge na taifa kwa ujumla, hivyo kutaka kuleta ushahidi.Mbunge huyo alisema kuwa anao ushahidi, na kwamba hata jambo hilo lilitangazwa na baadhi ya runinga hapa nchini, hoja ambayo hata hivyo ilionekana kuwa nyepesi kiasi cha Spika Makinda, kuwataka wabunge kuwa makini katika maswali na hoja wanazozitoa bungeni.Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa TAMISEMI, Aggrey Mwanri, alisema serikali haijawahi kumwagiza mtendaji yeyote wa serikali kuchangisha wananchi kwa nguvu katika ziara za viongozi wa juu wa serikali.Hata hivyo, alisema hoja ya mbunge huyo si ngeni kwani iliwahi kuibuliwa na ikamlazimu aliyekuwa Waziri wa Tamisemi, George Mkuchika, kwenda hadi Maswa kuzungumza na wananchi ili kupata maelezo ya kina.“Baada ya kufanya mkutano na wananchi hao, ilibainika kwamba si la kweli. Lakini kama mbunge ana ushahidi mpya tunamuomba atuletee na huyo DC tutamshughulikia kwa mujibu wa sheria,” alisema Mwanri.Alifafanua kuwa wakuu wa mikoa na wilaya wana haki ya kuingilia kati utendaji wa ngazi za chini, zikiwemo halmashauri, ikiwa tu kuna hatari ya usalama ama mali ya taifa, vinginevyo hawaruhusiwi kuzuia ama kutoa maelezo mengine nje ya maamuzi sahihi ya kisera na kikanuni yaliyoamriwa na mamlaka za halmashauri za miji ama vijiji.“Majukumu ya Mkuu wa Wilaya yametajwa katika kifungu namba 14, 1 hadi 3 cha sheria za Serikali za Mikoa namba 19 ya mwaka 1997 kwamba yeye ndiye msimamizi mkuu wa serikali katika wilaya yake.

      Tanzania daima
      ccm inakufa,asante mungu umesikia kilio chetu!!!!!!!

    13. #11
      Mwanajamii's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th March 2008
      Posts : 7,085
      Rep Power : 1810
      Likes Received
      24
      Likes Given
      13

      Default Re: Mizengo Pinda unawakamua Masikini wenzako hadi mbuzi!!!!!

      Quote By Mwanaweja
      niliisikia hii bungeni jana mbunge wa viti maalumu aliibua ni aibu kwa watendaji, waziri mkuu na serikali kwa ujumla
      Na wale wanaotembezaga bakuli wakati wa kambeni nao walikuwemo.

    14. #12
      Mwanajamii's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th March 2008
      Posts : 7,085
      Rep Power : 1810
      Likes Received
      24
      Likes Given
      13

      Default Re: Mizengo Pinda unawakamua Masikini wenzako hadi mbuzi!!!!!

      Quote By Elli
      Pinda awakamua mbuzi? nilielewa vibaya kumbe ila wote tu ni wezi wanatofautiana tu namna na aina ya wizi
      Si afadhali za pinda zinafahami zinakwenda wapi, zile zinazochangishwaga kwenye mikutano ya kampeni kwa bakuli huwa zinakwenda wapi jamani?

    15. #13
      Tuyuku's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Posts : 658
      Rep Power : 560
      Likes Received
      139
      Likes Given
      16

      Default Re: Pinda aumbuliwa bungeni

      najisikia kutukana

    16. #14
      Crashwise's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd October 2007
      Location : Safarini
      Posts : 13,133
      Rep Power : 14290
      Likes Received
      4019
      Likes Given
      3281

      Default

      Quote By Kengemumaji
      Si afadhali za pinda zinafahami zinakwenda wapi, zile zinazochangishwaga kwenye mikutano ya kampeni kwa bakuli huwa zinakwenda wapi jamani?
      za pinda huwa zinaenda wapi na hizo wanazo changishwa wakati wakapeni ni hiari au lazima kama ilivyojionyesha kwa pinda

    17. #15
      Ringo Edmund's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th May 2010
      Location : MDAWI
      Posts : 3,671
      Rep Power : 1361
      Likes Received
      885
      Likes Given
      586

      Default Re: Pinda aumbuliwa bungeni

      hivi kumbe tanzania kuna waziri mkuu?
      au ni jina kama majina mengine?mdogo wangu anaitwa god lakini halina uhusiano na mungu.
      ​kusema ni fedha na kusikilizwa ni zahabu.

    18. #16
      Elli's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 17th March 2008
      Location : Kijito-Upele
      Posts : 8,571
      Rep Power : 2551
      Likes Received
      2142
      Likes Given
      1862

      Default Re: Mizengo Pinda unawakamua Masikini wenzako hadi mbuzi!!!!!

      Mmmhh mi si msemaji wa CDM japo ni mwanachama wa CDM
      Quote By Kengemumaji
      Si afadhali za pinda zinafahami zinakwenda wapi, zile zinazochangishwaga kwenye mikutano ya kampeni kwa bakuli huwa zinakwenda wapi jamani?
      ...but what MAN is entirely without Evil intent in the Silence of his Soul???

    19. #17
      kajembe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 419
      Rep Power : 516
      Likes Received
      101
      Likes Given
      116

      Default Re: Mizengo Pinda unawakamua Masikini wenzako hadi mbuzi!!!!!

      Quote By Kengemumaji
      Na wale wanaotembezaga bakuli wakati wa kambeni nao walikuwemo.
      Lakini wao wananchi wananchangia kwa hiari tu na kupenda sera zao maana siyo za wizi na kukumbatia mafisadi,wanaonekana ni wakombozi wa kweli! na wala hawafungwi jela wasipotoa!

    20. #18
      Dabudee's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 30th May 2012
      Posts : 129
      Rep Power : 377
      Likes Received
      13
      Likes Given
      0

      Default Re: Pinda aumbuliwa bungeni

      Huko siyo kuchangishwa bali ni kunyang'anywa. Lakini haya ni mambo yanayofanywa bila kificho sehemu nyingi nchini.Uonevu na dhuluma hizi haziwezi kwisha bila magamba kupumzishwa moja kwa moja.

    21. #19
      Saint Ivuga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Posts : 20,739
      Rep Power : 10180
      Likes Received
      5676
      Likes Given
      12666

      Default Re: Pinda aumbuliwa bungeni

      mbuzi wa kutambika nini hao?
      JF the best place to be. and the POWER of God be with us all the time.

    22. #20
      Negotiator's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 9th August 2010
      Posts : 301
      Rep Power : 510
      Likes Received
      36
      Likes Given
      36

      Default Re: Mizengo Pinda unawakamua Masikini wenzako hadi mbuzi!!!!!

      Quote By Kengemumaji
      Hivi hili lina tofauti gani na lile la baadhi ya vyama vya siasa kuwakamua wapiga kura kwa kutembeza bakuli eti kwa madai kuwa hawana pesa, wakati tunajua wazi kuwa vinapata ruzuku, misaada toka ndani na nje ya nchi na vyanzo vingine vyingi.
      tofauti ni kua hawa wa ccm wamelazimishwa na waliposhindwa kufanya hivyo wakaswekwa ndani, isitoshe hawa wanalazimishwa kumpa waziri mkuu zawadi wakati wale wa M4C huchangia harakati za ukombozi bila shuruti na tena hakuna hatua zozote zinazochukuliwa iwapo mtu hajisikii kuchangia kwa hiari yake.
      '

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...