Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

    Report Post
    Page 1 of 5 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 84
    1. #1
      Candid Scope's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 7,607
      Rep Power : 15261
      Likes Received
      3731
      Likes Given
      2868

      Default Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

      Masha: Vijana wengi hawaipendi CCM


      ALIYEKUWA Waziri wa Mambo ya Ndani na Mbunge wa Nyamagana, Lawrence Masha, amesema vijana wengi nchini hawataki CCM kwa sababu hawaoni kilichofanyika tangu kilipoanzishwa.

      Masha alisema wananchi wanahitaji kuona mabadiliko na kwamba, hali hiyo inatokana na kutosoma vizuri historia ya Tanzania. Akizungumza kwenye kipindi cha Mkasi kinachorushwa na Kituo cha Televisheni cha EATV, alisema hatua ya kutopenda chama hicho imetokana na vijana kutosoma historia.

      “Vijana wengi hawaipendi CCM, wengi wanataka mabadiliko… siyo kosa lao, hawakufundishwa. Kuna wakati nilikuwa Chuo Kikuu cha St Augustine Mwanza nazungumza, kijana mmoja akasimama akasema nyie, wazee ndiyo wanarudisha nyuma nchi. Nikaangalia nyuma nikajiuliza huyo mzee yuko wapi... Nikagundua kumbe na mimi ambaye nilikuwa najiona kijana kniko kwenye kundi la wazee” alisema Masha.

      Masha ambaye ni mtoto wa mwanasiasa mkongwe nchini, Dk Fortunatus Masha, alisema vijana wengi wanapenda mabadiliko ya haraka jambo ambalo hawalioni ndani ya CCM na kuongeza kuwa, hali hiyo inasababishwa na kutokuwapo kwa mkakati wa kuwafundisha historia ya mafanikio ya Serikali na viongozi wake.

      “Leo hii ukienda Nairobi ukitaka kitabu kuhusu maisha ya Raila Odinga utaipata, ukitaka historia ya (Daniel) Moi .. Kenyatta utaipata. Mimi kijana wangu ana miaka 17 anasoma South Africa (Afrika Kusini) alikuja hapa anaomba kitabu ili ajue Tanzania imetoka wapi,..Hakuna,” alisema Masha na kuongeza:

      “Sasa kama mtoto ambaye anataka kujua nchi yake, anakosa hata pa kuipata, nchi yake ikoje, marais waliotawala, tumefikaje hapa? Lazima waseme tumekuwa maskini kwa sababu ya chama ambacho kiko madarakani.”

      Kuhusu kushindwa kwake ubunge mwaka 2010, Masha alisema amekubali kushindwa na anaendelea na kazi zake nyingine.

      “Ukiingia kwenye uchaguzi ni sawa tu na kuingia kwenye mpira, kuna kushinda na kushindwa, kikubwa ukishashindwa kubali matokeo endelea na maisha. Tatizo watu wengi na hasa wanasiasa wenzangu hawana kazi nyingine za kufanya,” alisema Masha.

      Alipinga madai kuwa kipindi chake cha ubunge na uwaziri hakufanya lolote katika jimbo lake, badala yake alitoa mifano ya kazi alizofanya na kwamba, wanaoeneza hayo ni watu wenye fitina.

      “Sidhani kama ni kweli, unajua kwenye siasa kuna fitina imani yangu ni kwamba kazi yangu nilifanya na kazi yangu ya uwaziri niliifanya. Of course (bila shaka) kutokana na mfumo tulionao, mwenzako lazima akumalize ili akushinde,” alisema Masha na kuongeza:

      “Leo hii tunapoongelea Nyamagana kuna chuo cha polisi kimejengwa, kuna Sekondari ya Mkolani imejengwa nje ya bajeti ya Serikali… ni kutoka kwa wafadhili na marafiki, there’s a lot of works (kuna kazi nyingi).”

      Alisema alikuwa akisomesha watoto 236 kwa mshahara wake wa ubunge na kwamba, tangu alipoingia bungeni mshahara wake ulikuwa ukipelekwa jimboni kusaidia wasiokuwa na uwezo.

      “Leo hii ndiyo watu wanakumbuka, ndiyo nasema leo hii hata mke wangu na watoto wangu nao wafurahi kidogo kile ninachokipata, nipeleke kwenye maendeleo ya familia,” alisema.

      Hata hivyo, Masha alisema kazi za siasa zinahitaji uvumilivu hivyo alijitahidi kuvumilia changamoto hizo kipindi chote cha uongozi wake.
      Ndahani and Ben Mugashe like this.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Candid Scope's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 7,607
      Rep Power : 15261
      Likes Received
      3731
      Likes Given
      2868

      Default Re: Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

      Nimekubaliana na majibu ya Masha pamoja na mchepuo wa maisha yake baada ya kubwagwa ubunge. Kimsingi siasa ni mchezo mchafu, ukiamua kuuendeleza unaweza kushtukia hata umekufilisi kama kama hukufanikiwa nafasi uliyogombea. Na walioshinda ndio maana wanafanya jitihada kubwa na kutumia njia haramu kurudisha gharama walizotumia kupata nafasi hizo.

      Kama nafasi inaruhusu bora kuamua kuendesha shughuli binafsi zinazokupatia lishe na kuyaendesha maisha kwa utulivu kuliko haya ya nafasi za kisiasa za kunyoosheana vidole kila kukicha bila kikomo.

    4. BAK
      #3
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,633
      Rep Power : 44971
      Likes Received
      8385
      Likes Given
      8363

      Default Re: Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

      Quote By Candid Scope
      “Vijana wengi hawaipendi CCM, wengi wanataka mabadiliko… siyo kosa lao, hawakufundishwa. Kuna wakati nilikuwa Chuo Kikuu cha St Augustine Mwanza nazungumza, kijana mmoja akasimama akasema nyie, wazee ndiyo wanarudisha nyuma nchi. Nikaangalia nyuma nikajiuliza huyo mzee yuko wapi... Nikagundua kumbe na mimi ambaye nilikuwa najiona kijana kniko kwenye kundi la wazee” alisema Masha.

      Masha ambaye ni mtoto wa mwanasiasa mkongwe nchini, Dk Fortunatus Masha, alisema vijana wengi wanapenda mabadiliko ya haraka jambo ambalo hawalioni ndani ya CCM na kuongeza kuwa, hali hiyo inasababishwa na kutokuwapo kwa mkakati wa kuwafundisha historia ya mafanikio ya Serikali na viongozi wake.
      “Leo hii ukienda Nairobi ukitaka kitabu kuhusu maisha ya Raila Odinga utaipata, ukitaka historia ya (Daniel) Moi .. Kenyatta utaipata. Mimi kijana wangu ana miaka 17 anasoma South Africa (Afrika Kusini) alikuja hapa anaomba kitabu ili nijue Tanzania imetoka wapi,..Hakuna,” alisema Masha na kuongeza:

      .

      Duh! Kwa hiyo huyu anadhani vijana wa Kitanzania wakifundishwa na kisha kupatiwa vitabu vya kusoma kuhusu historia ya nchi yetu na tumefikaje hapa tulipo basi vijana wataipenda magamba!!! Kazi kweli kweli!!!!
      Jasusi and PlanckScale like this.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    5. #4
      Nyani Ngabu's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 15th May 2006
      Location : Ikungulyabashashi
      Posts : 39,263
      Rep Power : 36770
      Likes Received
      9630
      Likes Given
      686

      Default Re: Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

      Quote By Candid Scope



      “Leo hii tunapoongelea Nyamagana kuna chuo cha polisi kimejengwa, kuna Sekondari ya Mkolani imejengwa nje ya bajeti ya Serikali… ni kutoka kwa wafadhili na marafiki, there’s a lot of works (kuna kazi nyingi).”
      There's a lot of works?
      Ndahani, PlanckScale and Sangarara like this.
      Miafrika Ndivyo Tulivyo.

    6. #5
      Janjaweed's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th January 2010
      Posts : 3,624
      Rep Power : 1129
      Likes Received
      1391
      Likes Given
      1541

      Default Re: Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

      Quote By BAK
      Duh! Kwa hiyo huyu anadhani vijana wa Kitanzania wakifundishwa na kisha kupatiwa vitabu vya kusoma kuhusu historia ya nchi yetu na tumefikaje hapa tulipo basi vijana wataipenda magamba!!! Kazi kweli kweli!!!!
      hapana, umemiss his point

      anazungumia knowledge... wakiwa na knowledge watafanya better decisions
      Candid Scope likes this.
      Kama Vipi nipotezee tu; ntakuboa....

    7. RukaaJuu Final

    8. BAK
      #6
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,633
      Rep Power : 44971
      Likes Received
      8385
      Likes Given
      8363

      Default Re: Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

      Quote By Janjaweed
      hapana, umemiss his point

      anazungumia knowledge... wakiwa na knowledge watafanya better decisions
      Hiyo knowledge itatoka wapi ikiwa shule zenyewe midabwado, walimu midabwado, vifaa mbali mbali mashuleni midabwado na pamoja na kuanguka elimu yetu bado Serikali inapunguza bajeti ya Elimu!!!..
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    9. #7
      samilakadunda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th October 2011
      Posts : 792
      Rep Power : 543
      Likes Received
      102
      Likes Given
      13

      Default Re: Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

      Dah mashaaaah kama unataka kujivua gamba vile unakaribishwa waliko vijana wenzio,au ww ulisoma vitabu vya nyerere,mwinyi, mkapa na huu ni upepo tu utapita? Na huyo mwanao kasha shitukia ubabaisha wenu na ulafi wa magamba.
      PlanckScale likes this.

    10. #8
      Janjaweed's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th January 2010
      Posts : 3,624
      Rep Power : 1129
      Likes Received
      1391
      Likes Given
      1541

      Default Re: Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

      Quote By BAK
      Hiyo knowledge itatoka wapi ikiwa shule zenyewe midabwado, walimu midabwado, vifaa mbali mbali mashuleni midabwado na pamoja na kuanguka elimu yetu bado Serikali inapunguza bajeti ya Elimu!!!..
      i think that was his point....

      kusema tu vitabu haimaanish vitabu, bali elimu kwa ujumla
      Kama Vipi nipotezee tu; ntakuboa....

    11. #9
      Jasusi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th May 2006
      Posts : 10,625
      Rep Power : 2894
      Likes Received
      3845
      Likes Given
      12250

      Default Re: Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

      Mimi nadhani tatizo si kutojua historia kwa upande wa vijana wetu. Tatizo ambalo Masha hakulizungumzia ni kwamba CCM iliyopigania uhuru na kumtetea kabwela, siyo CCM hii ya leo ambayo imetamalaki kwa rushwa, matabaka ya walio nacho na kutojali raia wake.
      BAK, TIMING, PlanckScale and 3 others like this.

    12. #10
      Job K's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th October 2010
      Posts : 1,552
      Rep Power : 748
      Likes Received
      266
      Likes Given
      254

      Default

      Quote By Nyani Ngabu
      There's a lot of works?
      Hivi hicho kidhungu amesema Masha au wandishi wetu makanjanja? Eti works! Shame!

    13. BAK
      #11
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,633
      Rep Power : 44971
      Likes Received
      8385
      Likes Given
      8363

      Default Re: Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

      Quote By Janjaweed
      i think that was his point....

      kusema tu vitabu haimaanish vitabu, bali elimu kwa ujumla
      Mkuu huyu alikuwa ndani ya Serikali kwa miaka mitano hakuliona hili la elimu yetu kuwa duni na kulizungumza hadharani wakati akiwa Waziri mpaka yuko nje ya Serikali ndio analiona? Kwa maoni yangu namuona ni msanii tu ambaye sasa amekosa ulaji ndio anaziona kasoro ndani ya Serikali.
      Saint Ivuga and PlanckScale like this.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    14. #12
      Janjaweed's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th January 2010
      Posts : 3,624
      Rep Power : 1129
      Likes Received
      1391
      Likes Given
      1541

      Default Re: Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

      Quote By BAK
      Mkuu huyu alikuwa ndani ya Serikali kwa miaka mitano hakuliona hili la elimu yetu kuwa duni na kulizungumza hadharani wakati akiwa Waziri mpaka yuko nje ya Serikali ndio analiona? Kwa maoni yangu namuona ni msanii tu ambaye sasa amekosa ulaji ndio anaziona kasoro ndani ya Serikali.
      yawezekana aliona na alizungumza, ila nijuavyo mimi si kila wanachozungumza kinaenda media
      Kama Vipi nipotezee tu; ntakuboa....

    15. #13
      Candid Scope's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 7,607
      Rep Power : 15261
      Likes Received
      3731
      Likes Given
      2868

      Default Re: Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

      Quote By BAK
      Hiyo knowledge itatoka wapi ikiwa shule zenyewe midabwado, walimu midabwado, vifaa mbali mbali mashuleni midabwado na pamoja na kuanguka elimu yetu bado Serikali inapunguza bajeti ya Elimu!!!..
      Hayo ndiyo anayosema Masha, kuna kitu cha msingi ambacho vijana wamekosa. Elimu imekuwa ya mabadiliko badiliko kila mwaka, hakuna mtaala wa kudumu, kila waziri akija na yake. Sijui tuna vitabu gani vya kiada ambavyo mwanafunzi anaweza kutumia na vikarithishwa kwa wanaomfuata, kwani kesho yake mtaala utabadilika.

      Uandishi wa mambo ya historia ya nchi yetu umetupiga kikumbo, ni Nyerere aliyeweza kuishi kwa kuandika mengi ya kutufunza. Marais wengi huandika mengi lakini viongozi wetu wa siku hizi wamekuwa wazururaji, sijui watapata lini nafasi ya kuandika ya kutufunza wananchi kutokana na uzoefu wao wa uongozi.

    16. #14
      TIMING's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 20,091
      Rep Power : 12253
      Likes Received
      6015
      Likes Given
      6854

      Default Re: Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

      Quote By Jasusi
      Mimi nadhani tatizo si kutojua historia kwa upande wa vijana wetu. Tatizo ambalo Masha hakulizungumzia ni kwamba CCM iliyopigania uhuru na kumtetea kabwela, siyo CCM hii ya leo ambayo imetamalaki kwa rushwa, matabaka ya walio nacho na kutojali raia wake.
      Thanks mkuu
      Jasusi likes this.
      .....Ana sifa zote, nzuri na mbaya!!!

    17. #15
      Candid Scope's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 7,607
      Rep Power : 15261
      Likes Received
      3731
      Likes Given
      2868

      Default Re: Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

      Quote By samilakadunda
      Dah mashaaaah kama unataka kujivua gamba vile unakaribishwa waliko vijana wenzio,au ww ulisoma vitabu vya nyerere,mwinyi, mkapa na huu ni upepo tu utapita? Na huyo mwanao kasha shitukia ubabaisha wenu na ulafi wa magamba.
      Binafsi nimependa uchambuzi wake, kuna mambo mazuri ya msingi ambayo ameongelea hapa, ukweli unajieleza. Hata hapa JF utakuta watu hawana nafasi ya kujadili mada, ila kutoa maneno mawili matatu ya mipasho tu. Unaweza kugundua kitu kinakosekana kwetu ambacho ni elimu. Elimu haiji peke yake ila kwa kujishughulisha kuujua ulimwengu na malimwengu. Kuna njia nyingi siku hizi, badala ya hizi network kutumika ku-browse elimu sisi tunatumia kwa ajili ya maridhio ya urafiki mitandaoni na ku-browse pics za mahaba ndo elimu wengi tunayoipenda, je itatufikisha wapi kama si kutudumaza kiakili?
      Buswelu, Saharavoice and WFM like this.

    18. #16
      MNYISANZU's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 21st October 2011
      Posts : 6,311
      Rep Power : 0
      Likes Received
      593
      Likes Given
      76

      Default Re: Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

      Hivi JK kamsahau kabisa Masha ktk ufalme wake?

    19. #17
      Candid Scope's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 7,607
      Rep Power : 15261
      Likes Received
      3731
      Likes Given
      2868

      Default Re: Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

      Quote By Job K
      Hivi hicho kidhungu amesema Masha au wandishi wetu makanjanja? Eti works! Shame!
      Jamani wengi wetu kidhungu ni lugha ya tatu kutoka mother tongue, national language na kisha hii ya kiairishi taabu tu, tunajiuma ulimi. Tuache tu.

    20. #18
      Jasusi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th May 2006
      Posts : 10,625
      Rep Power : 2894
      Likes Received
      3845
      Likes Given
      12250

      Default Re: Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

      Quote By Candid Scope
      Binafsi nimependa uchambuzi wake, kuna mambo mazuri ya msingi ambayo ameongelea hapa, ukweli unajieleza. Hata hapa JF utakuta watu hawana nafasi ya kujadili mada, ila kutoa maneno mawili matatu ya mipasho tu. Unaweza kugundua kitu kinakosekana kwetu ambacho ni elimu. Elimu haiji peke yake ila kwa kujishughulisha kuujua ulimwengu na malimwengu. Kuna njia nyingi siku hizi, badala ya hizi network kutumika ku-browse elimu sisi tunatumia kwa ajili ya maridhio ya urafiki mitandaoni na ku-browse pics za mahaba ndo elimu wengi tunayoipenda, je itatufikisha wapi kama si kutudumaza kiakili?
      Candid Scope,
      Unataka kuniambia kuwa tungekuwa na elimu bora kuliko tuliyo nayo hivi sasa vijana wetu wangeshabikia CCM? I think there is more to it than simply blaming it on education. CCM imewapoteza vijana kwa sababu kimegeuka kuwa chama cha kulaghai. Angalia ahadi alizozitoa Kikwete katika uchaguzi wa 2010. Hivi kweli unaamini Kigoma itageuzwa kuwa Dubai wakati wa utawala wa Kikwete, ambao amebakiwa na miaka mitatu tu?
      BAK and Precise pangolin like this.

    21. #19
      TIMING's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 20,091
      Rep Power : 12253
      Likes Received
      6015
      Likes Given
      6854

      Default Re: Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

      Quote By MNYISANZU
      Hivi JK kamsahau kabisa Masha ktk ufalme wake?
      MASHA ANA ufalme wa kumtosha, hahitaji JK... pia uelewe JK ana less than 50% influence kwenye serikali iliyo madarakani

      wewe unaangalia juu, kazi zote zipo local government....

      komaa-komaa ujue maisha,

      inatia aibu sana mtu kama muhingo, a well seasoned journalist anakubali kuwa DC, what a waste!!

      tubadilike, we can sustain our families bila hata political appointments
      Jasusi, BAK and Candid Scope like this.
      .....Ana sifa zote, nzuri na mbaya!!!

    22. #20
      Candid Scope's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 7,607
      Rep Power : 15261
      Likes Received
      3731
      Likes Given
      2868

      Default Re: Masha athibitisha Vijana wengi hawaipendi CCM

      Quote By Jasusi
      Candid Scope,
      Unataka kuniambia kuwa tungekuwa na elimu bora kuliko tuliyo nayo hivi sasa vijana wetu wangeshabikia CCM? I think there is more to it than simply blaming it on education. CCM imewapoteza vijana kwa sababu kimegeuka kuwa chama cha kulaghai. Angalia ahadi alizozitoa Kikwete katika uchaguzi wa 2010. Hivi kweli unaamini Kigoma itageuzwa kuwa Dubai wakati wa utawala wa Kikwete, ambao amebakiwa na miaka mitatu tu?


      Thanks Jasusi, elimu ni pana na wala tuizungumzayo hatumaanishi ya vitabuni tu na wewe unafahamu fika juu ya niongeleacho. Mfano makamanda wa Chadema wanavyozunguka nchi nzima kutoa somo la uraia kwa wananchi na jinsi wananchi wanavyowaelewa na kuitikia kiasi cha kubadili kabisa wimbi la mtazamo wa kisiasa za mageuzi nchini mwetu. Hii ni moja wapo ya elimu ambayo wananchi wameikosa na CCM imefanya kila jitihada kuwanyima kwa ajili ya wachache wabaki kuwa katika nafasi wanazotaka bila kunyoshewa vidole na wananchi.

      Serikali haijawa na mfumo wa kuwafunda watu namna ya kutoa elimu ya kujitegemea kama enzi za awamu ya kwanza ambapo vijijini kulikuwa na msukumo wa kujitegemea na watu baada ya kuhitimu shule walikuwa na mwelekeo wa uzalishaji vijijini. Leo elimu hiyo imekosekana, vijana toka vijijini baada ya kuhitimu shule wanakimbilia mijini. Ukiona vijana walivyojaa mijini huwezi kuamini wanakula nini na wanaajiriwa wapi na ndio maana wako waitikiaji wazuri sana kwenye mihadhara kwa kuwa hawana cha kufanya. Nenda vijiji wamebaki vijana wachache wana ambao nao wengi wanatafuta nafasi ya kwenda mijini na vijiji vimebaki makazi ya wazee tu.

      Amini nisemayo kwani nimefanya utafiti na kushuhudia hali ilivyo vijijni na mijini. Shule za kata zimesaidia kuwashika walio mashuleni kubaki huko, na wakishahitimu wanatimkia mijini, ni dalili ya kukosa somo la elimu ya kujitegemea ambalo nio muhimu kwa mazingira ya kujiajiri vijijini ingawa nako kuna changamoto nyingi zinazotokana na kukosekana kwa miundo mbinu mbalimbali na kukosekana kwa utility.
      Jasusi, Buswelu and WFM like this.

    Page 1 of 5 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...