Wanabodi.
Ninapenda sana hatua ya viongozi wa Chadema kuzunguka mikoani kuimarisha chama chao, ni hatua nzuri ambayo wananchi watapata nafasi kuijua vizuri Chadema ili kufanya maamuzi kama kujitoa ama kubaki ndani ya chama hicho.
Kila kikundi, chama au taasisi yeyote inapofanya mambo yake bila kuwepo na utaratibu, kuna hatari kubwa ya kutokea fujo.
Ni hatari kwa kiongozi wa chama kutofuata utaratibu wiki iliyopita Chadema walifanya mkutano wao kule Mtwara, Mbowe alimgomea (OCD) wa Nanyumbu, Mohamed Said, alipokuwa akihutubia eneo la Mangaka, OCD alimtaka Mbowe ashuke jukwaani kwa kuwa muda wa kuhutubia ulikuwa umemalizika saa 12 jioni.
Mbowe akaanza kusema Jamani OCD anataka niache kuhutubia, sasa nasema wewe OCD mimi ni mbunge na kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, hebu sikiliza usitutishe sisi, mimi simuogopi mtu yoyote awe Rais Kikwete, au Waziri Mkuu Pinda, hao nawaheshimu nao wananiheshimu, usitake kujifunzia kazi kwangu, ngoja kwanza niwaulize wananchi, mnasemaje nifunge mkutano nisifunge? Wananchi waliitikia, usifunge.
Mbowe alichotaka wananchi wamshambule OCD ili fujo itokee watu wapigwe mabomu kisha aseme kuwa polisi wanaonea wananchi, wametumia nguvu nyingi, OCD alikuwa na uwezo wa kuwaamrisha vijana wake kumshusha kwa nguvu.
Chadema msiwatumie raia wapenda amani kufanikisha malengo yenu ya kisiasa.


Reply With Quote



Follow Us Here