Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Sheria ya katiba mpya kuwasilishwa kama taarifa

    Report Post
    Results 1 to 13 of 13
    1. #1
      Kakke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th December 2010
      Posts : 735
      Rep Power : 580
      Likes Received
      138
      Likes Given
      0

      Default Sheria ya katiba mpya kuwasilishwa kama taarifa

      Posted on June 11, 2012 by zanzibaryetu
      Katibu wa baraza la wawakilishi Zanzibar, Yahya Khamis Hamad

      SHERIA ya mabadiliko ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itawasilishwa kesho katika kikao cha baraza la wawakilishi kinachoanza kujadili bajeti ya mwaka wa fedha serikali ya mwaka wa fedha wa 2012/2013. Katibu wa baraza hilo, Yahya Khamis Hamad aliwaambiwa waandishi wa habari jana katika mkutano uliofanyika ukumbi wa baraza la wawakilishi, kwamba jambo la kwanza kuwasilishwa kwa wajumbe wa baraza ni sheria hiyo ambayo wananchi wanasubiri kuitolea maoni.
      “Hii itakuwa ni taarifa kwa wajumbe wa baraza la wawakilishi ambayo ni kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar kifungu 132 (2) ambayo inahitaji sheria zinazohusu muungano kuwasilishwa katika baraza” alisema Hamad.
      Hamad alisema katiba haitoi nafasi ya kujadili sheria hiyo kwani itakuwa ni taarifa kwa wajumbe wa baraza na sio kuijadili, “Hii ni kwa mujibu wa katiba lakini tusibiri litakaloweza kutokea baada ya kuwasilishwa sheria hiyo kwa sasa hatuwezi kujua nini kitatokea”.
      Katibu Hamad alisema sheria hiyo inawasilishwa katika baraza la wawakilishi katika kikao cha kesho kwa sababu ndicho kikao cha kwanza tangu bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania kupitisha sheria hiyo.
      “Waziri wa katiba na sheria wa Zanzibar Abubakar Khamis Bakari atatoa taarifa kuhusu sheria hiyo” alisema Katibu huyo.
      Akijibu suali la waandishi juu ya kuchelewa kwa kuwasilishwa sheria hiyo kwa wajumbe wa baraza la wawakilishi, Katibu huyo alisema “Bado hatujachelewa kuwapa wajumbe taarifa kwa sababu hiki ndio kikao cha kwanza” aliongeza Hamad.
      Tangu kupitishwa na bunge sheria hiyo na kusaniwa na Rais Jakaya Kikwete ilitarajiwa tume ya katiba ingeanza kazi zake ya kukusanya maoni ya katiba mpya mwezi huu, hata hivyo kikwazo kikawa ni kutowasilishwa katika kikao cha baraza la wawakilishi kama gazeti hili lilipoandika hivi karibuni.
      Akizungumzia utaratibu wa kikao hicho ambacho ni bajeti ya pili tangu kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa. Katibu alisema hakuna mswada mwengine utakaowasilishwa isipokuwa miswada ya kuidhinisha matumizi ya fedha za serikali.
      Alisema jumla ya masuali 197 yataulizwa na kupatiwa majibu na mawaziri wahusika ambapo tayari tayari matayarisho ya kikao hicho yameshakamilika ikiwemo wajumbe wote waliopo kisiwani Pemba kuwasili hapa Unguja.
      Tokea kuapishwa kwa wajumbe wa tume ya katiba Rais Kikwete wananchi wa Zanzibar wamekuwa na maoni tofauti kuhusiana na suala la kuwasilishwa sheria hiyo ya katiba katika kikao cha baraza la wawakilishi.
      Wazanzibari wengi wamekuwa na shauku kubwa wakitaka kujua kitakachotokea katika baraza hilo juu ya sheria ya katiba itakayowasilishwa na waziri wa katiba na sheria.
      Pasco likes this.


    2. #2
      Kakke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th December 2010
      Posts : 735
      Rep Power : 580
      Likes Received
      138
      Likes Given
      0

      Default Re: Sheria ya katiba mpya kuwasilishwa kama taarifa

      Ikiwa Muungano hautakiwi itakuwa Katiba? huu Muungano umekuwa kama Mwanamkke Mala.. alakuwa hajuwi kufukuzwa na kukataliwa.

      Hebu Watanganyika mujitao Watanzania na kujinata muna kila rasilimali na makeke, hamujuwi kukataliwa? nyinyi nikungangangania tu, aibu tena kwenu .

      Kila Mtanganyika macho yamewatoka kuona Wazanzibar hawawataki, jee kwani kabla ya Muungano mulikuwa munaishi vipi?
      Pasco and Kilasara like this.

    3. #3
      Nyakageni's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st February 2011
      Posts : 5,570
      Rep Power : 1610
      Likes Received
      816
      Likes Given
      52

      Default

      Quote By Kakke View Post
      Ikiwa Muungano hautakiwi itakuwa Katiba? huu Muungano umekuwa kama Mwanamkke Mala.. alakuwa hajuwi kufukuzwa na kukataliwa.

      Hebu Watanganyika mujitao Watanzania na kujinata muna kila rasilimali na makeke, hamujuwi kukataliwa? nyinyi nikungangangania tu, aibu tena kwenu .

      Kila Mtanganyika macho yamewatoka kuona Wazanzibar hawawataki, jee kwani kabla ya Muungano mulikuwa munaishi vipi?
      povu jingi. Tumia na elimu ya darasani basi

    4. #4
      kwamwewe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2010
      Posts : 907
      Rep Power : 5419
      Likes Received
      105
      Likes Given
      132

      Default Re: Sheria ya katiba mpya kuwasilishwa kama taarifa

      Quote By Nyakageni View Post
      povu jingi. Tumia na elimu ya darasani basi
      povu mnalo nyinyi tena la kule......maana humu kila mmoja roho juu

      Kila Mtanganyika macho yamewatoka kuona Wazanzibar hawawataki, jee kwani kabla ya Muungano mulikuwa munaishi vipi?

    5. #5
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,862
      Rep Power : 7377
      Likes Received
      6196
      Likes Given
      22551

      Default

      Quote By Kakke View Post
      Ikiwa Muungano hautakiwi itakuwa Katiba? huu Muungano umekuwa kama Mwanamkke Mala.. alakuwa hajuwi kufukuzwa na kukataliwa.

      Hebu Watanganyika mujitao Watanzania na kujinata muna kila rasilimali na makeke, hamujuwi kukataliwa? nyinyi nikungangangania tu, aibu tena kwenu .

      Kila Mtanganyika macho yamewatoka kuona Wazanzibar hawawataki, jee kwani kabla ya Muungano mulikuwa munaishi vipi?
      Kakee ni kweli Muungano ni kama ndoa, Tanganyika ndio Bwana na Zanzibar ndio bibi, sisi wanaume wa bara hatuna utamaduni wa kuacha mke, tena mwanamke mwenyewe mzuri kama Zanzibar, kamwe hatuachi!.

      Hizi chokochoko ni visa vya mke kutingisha kibiriti ili ampime mumewe kama kweli anapendwa, huyo ni mke anayetafuta tuu mapenzi akiyapata kisawa sawa, atatulia!.

      Ila pia kuna aina ya visa vya mke aliyepata bwana mwingine!. Tumesikia fununu mmepata bwana mwingine wa Kiarabu ndio maana sisi machogo mnatuona hatuna maana hata baada ya kukutunza na kukuhudumia kwa kila kitu yapata miaka 48 sasa!.

      Maadam mshenga wenu BLW amekuja, dai basi hiyo talaka yenu tukupeni tuachane kwa usalama ila hala hala msije kujuta!. Msiache mbachao kwa msala upitao na siku zote, mkataa pema pabaya panamwita!. Msubirieni tuu mjukuu majuto!.


    6. #6
      kwamwewe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2010
      Posts : 907
      Rep Power : 5419
      Likes Received
      105
      Likes Given
      132

      Default Re: Sheria ya katiba mpya kuwasilishwa kama taarifa

      Quote By Pasco View Post
      Kakee ni kweli Muungano ni kama ndoa, Tanganyika ndio Bwana na Zanzibar ndio bibi, sisi wanaume wa bara hatuna utamaduni wa kuacha mke, tena mwanamke mwenyewe mzuri kama Zanzibar, kamwe hatuachi!.

      Hizi chokochoko ni visa vya mke kutingisha kibiriti ili ampime mumewe kama kweli anapendwa, huyo ni mke anayetafuta tuu mapenzi akiyapata kisawa sawa, atatulia!.

      Ila pia kuna aina ya visa vya mke aliyepata bwana mwingine!. Tumesikia fununu mmepata bwana mwingine wa Kiarabu ndio maana sisi machogo mnatuona hatuna maana hata baada ya kukutunza na kukuhudumia kwa kila kitu yapata miaka 48 sasa!.

      Maadam mshenga wenu BLW amekuja, dai basi hiyo talaka yenu tukupeni tuachane kwa usalama ila hala hala msije kujuta!. Msiache mbachao kwa msala upitao na siku zote, mkataa pema pabaya panamwita!. Msubirieni tuu mjukuu majuto!.
      Kwani hii ni ndoa au raping???
      Pasco likes this.

    7. #7
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,862
      Rep Power : 7377
      Likes Received
      6196
      Likes Given
      22551

      Default Re: Sheria ya katiba mpya kuwasilishwa kama taarifa

      Sio rape bali ni ndoa ya mkeka ambapo upande mmoja wa kidume Tanganyika ndio iliridhia kwa kuleta posa huko kupitia kwa mshenga Karume ambapo barua ya posa ilikubaliwa, japo mke hakuulizwa anataka mahari ya kiasi ili aridhie rasmi kuolewa na Tanganyika bali ndoa ilifungwa rasmi ile tarehe 26 April, 1964, na tarehe 27 April, 1964, mshenga Karume alimleta rasmi mke na kumkabidhi kwa Tanganyika pale Karimjee!.

      Kisheria ndoa ya upande mmoja sio halali ila ili kuibatilisha ilibidi mke aliyeolewa bila ridhaa yake, kugoma kutimiza masharti ya ndoa ile ikiwemo kutotoa huduma za kindoa hivyo kuonyesha kuikataa ndoa ile batil!.

      Kitendo cha mke kujituliza tuli ndani ya ndoa, hiyo ndoa ikawa "consumated" na mpaka leo mke hajaomba rasmi kutoka ndani ya ndoa ile, ni uthibitishi kuwa yule mke aliiridhia ndoa ile kwa kukaa kimya hivyo ndoa hiyo kupata uhalali kwa kutumia "the law of limitation".

      Kukubali kwa kukaa kimya ni moja ya mila nzuri za Kiafrika kwa binti mwenye adabu njema kukaa kimya anapoombwa penzi ila ukimshika mkono kumpeleka chumbani huja bila kulazimishwa na mle ndani nguo huvua mwenyewe, kitandani alipanda mwenyewe na miguu pia alifungua mwenyewe!. Hivyo hiyo sio rape!.

      Hizi chokochoko za vile vitimbakwiri zinaketwa kwa sababu ametokea bwana wa kiarabu na kutaka kumfitinisha mke kwa kumkumbushia kuwa hawakupokea mahari!, eti yeye ataleta majunia ya dhahabu kama mahari!. Sasa hivyo vitimbakwiri ndivyo vinamchokoa dada yao aombe talaka ili wao wapate mali!.

      Kwa taarifa tuu dada yao kapenda kwa dhati, kajituliza kwenye ndoa hivyo fitina zao ni bure tuu!.
      thereitis likes this.

    8. #8
      Fredrick Sanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th January 2011
      Location : Kijitonyama
      Posts : 2,988
      Rep Power : 2594
      Likes Received
      641
      Likes Given
      777

      Default Re: Sheria ya katiba mpya kuwasilishwa kama taarifa

      Duhh mimi ni mtanganyika, lakini naipenda sana Zanzibar. Sitakubali muungano uvunjike. Siku hizi hata usingizi sipati. Beautiful aisland of Africa
      Last edited by Fredrick Sanga; 12th June 2012 at 11:32.
      Pasco and thereitis like this.
      We shall overcome, righteousness shall always prevail.

    9. #9
      Fredrick Sanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th January 2011
      Location : Kijitonyama
      Posts : 2,988
      Rep Power : 2594
      Likes Received
      641
      Likes Given
      777

      Default Re: Sheria ya katiba mpya kuwasilishwa kama taarifa

      Serikali Tatu zitatatua migogoro
      Pasco likes this.
      We shall overcome, righteousness shall always prevail.

    10. #10
      Power G's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 20th April 2011
      Location : Msoga Kijijini
      Posts : 2,432
      Rep Power : 1001
      Likes Received
      801
      Likes Given
      275

      Default Re: Sheria ya katiba mpya kuwasilishwa kama taarifa

      Quote By Fredrick Sanga View Post
      Serikali Tatu zitatatua migogoro
      Mkuu tukiwa na serikali 3 haitatua migogoro kwa sababu wazenji wataanza kulalamika kwamba serikali ya muungano inaipendelea serikali ya Tanganyika (kumbuka sasa kwamba huu utakuwa uke wenza), hivyo kusababisha kuendelea kuwa na kero zisizokwisha. Nadhani suluhisho sahihi na la kudumu ni Serikali moja au Kila mtu kushika lake.
      thereitis likes this.
      TANZANIA ITAJENGWA NA WENYE MOYO NA KULIWA NA WENYE MENO KAMA AKINA EL, JK, EC na RA

    11. #11
      thereitis's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Location : Arusha
      Posts : 237
      Rep Power : 484
      Likes Received
      24
      Likes Given
      60

      Default Re: Sheria ya katiba mpya kuwasilishwa kama taarifa

      Quote By Fredrick Sanga View Post
      Serikali Tatu zitatatua migogoro
      Sanga kwa hili sikubaliani nawe. serikali tatu zitsababisha muungano kufa maana kila serikali itajali mambo yake hivyo kusahau mambo ya muungano. Nafikiri serikali moja ndilo suluhisho la kunusuru ndoa hii
      Kilasara likes this.

    12. #12
      thereitis's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Location : Arusha
      Posts : 237
      Rep Power : 484
      Likes Received
      24
      Likes Given
      60

      Default Re: Sheria ya katiba mpya kuwasilishwa kama taarifa

      Quote By Power View Post
      Mkuu tukiwa na serikali 3 haitatua migogoro kwa sababu wazenji wataanza kulalamika kwamba serikali ya muungano inaipendelea serikali ya Tanganyika (kumbuka sasa kwamba huu utakuwa uke wenza), hivyo kusababisha kuendelea kuwa na kero zisizokwisha. Nadhani suluhisho sahihi na la kudumu ni Serikali moja au Kila mtu kushika lake.
      Mkuu nakubaliana na wewe 100%

    13. #13
      Kilasara's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 21st December 2008
      Posts : 538
      Rep Power : 642
      Likes Received
      89
      Likes Given
      141

      Default Re: Sheria ya katiba mpya kuwasilishwa kama taarifa

      Quote By thereitis View Post
      Sanga kwa hili sikubaliani nawe. serikali tatu zitsababisha muungano kufa maana kila serikali itajali mambo yake hivyo kusahau mambo ya muungano. Nafikiri serikali moja ndilo suluhisho la kunusuru ndoa hii
      Nakubaliana na wanaosema serikali tatu zitazidisha malumbano baina ya Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Zanzibar; na hatimaye kuvunja Muungano. Kama serikali moja haitatakiwa na Zanzibar, basi ndoa itavunjika.

      Tujuavyo ni kwamba Wazanzibari kadhaa hawautaki Muungano na wamediriki hata kupeleka ujumbe Umoja wa Mataifa kuomba Umoja huo uingilie. Wengi wetu wa Bara tunadhani pia sio lazima tuwe na Muungano, na kwamba maendeleo yetu Tanganyika yangesonga mbele kwa kasi zaidi kwa kuachana na Zanzibar.

      Kwa hiyo Tume ya Katiba ipendekeze kura ya maoni kwa wananchi wa Zanzibar na kwa wananchi wa Tanganyika. Endapo mmoja kati ya Zanzibar au Tanganyika hataki Muungano, basi Tume iandike Katiba mbili: moja ya Tanganyika na ingine ya Zanzibar. Tusilazimishe upande wowote kuwa ktk Muungano.
      thereitis likes this.

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...