Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mchungaji Gwajima na tabiri zake: 'Tanzania Mpya' inakuja

    Report Post
    Page 3 of 10 FirstFirst 12345 ... LastLast
    Results 41 to 60 of 181
    1. #1
      Asante's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th December 2009
      Posts : 443
      Rep Power : 755
      Likes Received
      110
      Likes Given
      124

      Default Mchungaji Gwajima na tabiri zake: 'Tanzania Mpya' inakuja

      Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Kawe, Mch.Josephat Gwajima amesema Tanzania mpya yenye matumaini inakuja.

      Akihubiri Kanisani hapo leo alisema ingawa yeye ni mwana CCM na vyombo vyote vilivyotumika kwenye mkutano wa ccm Jangwani jana vilitoka Kanisani kwake, alisema chama cha siasa cha ccm kipo katika wakati mgumu na kimepoteza kabisa mwelekeo na uwezo wa kuongoza dola.

      Amewaonya wanasiasa wanaojiona ni wasafi na bado wanang'ang'ania ccm, wajue mwisho wao kisiasa upo ukingoni, aliwaonya Mwakyembe, Sita na wanasiasa wangine kuwa hali ya ccm ilivyo sasa ni sawasawa na samaki aliye ndani ya bwawa na maji ambalo linakaribia kukauka.

      "Tanzania mpya inakuja" ulikuwa ndio ujumbe wake wa leo.

      Tanzania yenye uwezo wa kukomesha rushwa inakuja.

      Tanzania yenye uwezo wa kujali afya za wananchi wake inakuja.

      Tanzania yenye uwezo wa kukomesha wizi wa mali za uma inakuja.

      Tanzania yenye uwezo wa kuwapatia vijana wake elimu bora inakuja.

      Tanzania yenye uwezo wa kuwalisha wananchi wake inakuja.

      Amewatakia wananchi wote afya njema, wapate kuipokea Tanzania mpya.

      Tanzania mpya inakuja - AMINA.

      BAADAE: Juni 14, 2012

      Quote By maitario
      Kwa wale mnaomfahamu mchungaji Gwajima mtakubaliana nami kuwa ni moja ya wachungaji wenye upako wa ajabu Tanzania na wanaozungumza mambo yaliyofunuliwa kwao na Mungu.

      Katika mahubiri yake ya Jumapili na jana jioni alisema kwamba amefunuliwa kuwa Sitta na Mwakyembe kwakuwa ni watu waadilifu watashindwa ku-survive ndani ya CCM maana watakuwa wanachukiwa sana na kuwekewa mizengwe na hivyo watajiunga CHADEMA kabla ya uchaguzi mkuu 2015. Pia alitabiri CCM inakwenda kuanguka na utawala utakaojali maslahi ya nchi kuundwa.

      Natamani mwaka 2015 ufike haraha ili tushuhudie unabii ukitimia! Ili ukubaliane na Mchungaji kuwa CCM inakwenda kuanguka, angalia kadi za CHADEMA zinavyotafutwa kama dhahabu mitaani. Kila mtu anaulizia kadi zinapatikana wapi, maji yamebadili mkondo, hakuna anayevutiwa tena na CCM

    2. Miaka 50

    3. #41
      kwamwewe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2010
      Posts : 854
      Rep Power : 5404
      Likes Received
      99
      Likes Given
      125

      Default re: "Tanzania Mpya" Inakuja: Gwajima

      Quote By Mgelukila
      Hivi akisema siyo muunini wa ccm zengwe litaanza nara aondoke ktk eneo, vifaa vya dini havina ushuru ni njia ya kulipa fadhira. Haipendezi kiongozi wa dini kuwa na chama cha siasa anatukwaza waumini. Bora iwe siri yake je! Atatendaje haki ktk kutolea maamuzi kauli za serikali ikikosea wakati ni mwanachama hata akitoa maoni yake yatakuwa ya kisiasa tu, ni mtizamo tu.
      Siasa bila dini ni uendawazimu’

      Na Lilian Nyenza


      Kanisa halitaacha kutoa mwongozo kwa watu wake hata kwa mambo ya kisiasa ukiwamo uchaguzi kwa kuwa, siasa bila dini ni sawa na uendawazimu.



      Aidha, imedaiwa kuwa tabia ya kuwalaghai vijana kuwa ni taifa la kesho, ndiyo inayowadumaza kiakili na kuwafanya watumiwe na wanasiasa kufanya fujo, badala ya kujitokeza kuongoza kwa kufuata taratibu za nchi.



      Mkurugenzi wa chama cha kifamilia cha Undugu Association Tanzania, Padri Baptiste Mapunda, alitoa kauli hiyo katika sherehe za kuuaga mwaka 2004 na kuukaribisha mwaka mpya wa 2005, zilizofanyika katika ukumbi wa Parokia ya Mt. Yosefu, Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam.



      Mkurugenzi huyo wa UNDUGU ASSOCIATION TANZANIA alisema kuwa, Tanzania imeanza kuonesha dalili mbaya za machafuko kutokana na baadhi ya watu wakiwamo wanasiasa kuweka mbele ubinafsi.

      “Tukikaa kimya huku mambo yanaharibika katika jamii; eti tuwaachie wanasiasa wafanye watakavyo, tutakuwa hatutendi wajibu wetu na hivyo, Kanisa halitaacha kusema ukweli kwa maslahi ya umma hata kama unamkera mtu. Hii ni kwa kuwa tunajua wazi kuwa siasa bila dini, ni uendawazimu ambao mtu hajui akifanyacho kwa kuwa akili yake haijatimia kiroho.” alisema.


      Aliitaka jamiii ya Kitanzania ijifunze thamani ya amani na siasa safi kutokana na hali ya amani na usalama katika nchi jirani za Rwanda na Burundi ambayo ni hatari na inasikitisha.


      Alisema vita na mauaji yanayoendelea katika nchi hizo, yanasababishwa na uroho wa madaraka wa watu wachache ambao hawajali utu wa wengine.

      Aliongeza kuwa, “Siku zote tunapaswa kukumbuka kuwa, amani na mapendo ambayo Mungu ametujalia, tunapaswa kuyaenzi sisi sote kwa kuwa siasa bila dini, ni sawa na uendawazimu.”


      Padri Mapunda aliiasa jamii kuendelea kumuomba Mungu ili azidi kuwajalia amani,upendo na utulivu uliopo sasa, kuwa uwepo hata baada ya Uchaguzi Mkuu kupita.

      Amewataka Waamini kuwaombea viongozi wanyanyasaji kama Herode, wabadilike na hivyo, kuongoza nchi kwa haki na akawasihi Watanzania kuyashinda maovu kwa kutenda yaliyo mema.



      Hata hivyo, Padri Mapunda amewatahadharisha vijana kujiepusha kutumiwa na baadhi ya viongozi wa siasa, kwa nia ya kufanya fujo katika uchaguzi.

      “Vijana mara nyingi wamekuwa wepesi wa kurubuniwa na vijizawadi vidogo vidogo, ili wafanye kile wanachokitaka wanasiasa wabinafsi. Sasa mimi nasema mkae chini na mlitafakari hilo kwa makini. Mtakao angamia ni ninyi na si wao,” alitahadharisha.



      Alisema vijana ni Taifa la leo na Taifa bila vijana limekufa, hivyo aliwasihi kuwaheshimu wazazi na walezi ili wapate kuishi maisha marefu na yenye heri duniani, kama walivyojaliwa kuuona mwaka huu mpya.



      Naye Mwenyekiti wa Umoja huo, Bw. Benjamini Komba alisema, lengo la Shirika la Undugu, ni kuiunganisha jamii, ikiwa ni pamoja na kuimarisha Ukristo katika kupata hamasa katika kazi ya umisionari, ili ijengeke roho ya umisionari wa kweli nchini Tanzania.



      Bw. Komba alisema kuwa, Shirika limekuwa na mchango mkubwa kwa jamii, kwa kuwa ni chombo cha kuelimisha jamii na kuendeleza mawasiliano na wamisionari wa Afrika ambao wapo ndani na nje ya nchi kwa lengo la kusukuma mbele kurudumu la Injili katika Taifa hili.



      Umoja huo haujishughulishi na mambo ya siasa na hauna ubaguzi wa dini, rangi, imani wala itikadi.


      Katika sherehe hizo, Wanaundugu na watu wengine walialikwa na kuhudhuria pamoja na familia zao.

    4. #42
      CHIHAYA's Avatar
      Member Array
      Join Date : 12th March 2012
      Posts : 84
      Rep Power : 378
      Likes Received
      19
      Likes Given
      15

      Default

      Quote By MTENGE
      Ukikalia kuti kavu watu watakuambia utaanguka nahuo sio utabiri ila nimwonekano wa hili halisi inlivyo
      Like mkuu natumia cm

    5. #43
      matawi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th March 2010
      Posts : 1,437
      Rep Power : 751
      Likes Received
      122
      Likes Given
      65

      Default

      Quote By NATA
      Ndio mrithi wa shehe yahaya ?
      Kuna tofauti kati ya utabiri na analysis, huyu ametoa matokeo kutokana na anaysis ambayo ccm imebadilishiwa kibao na watanzania

    6. #44
      Albedo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th February 2008
      Posts : 4,974
      Rep Power : 1571
      Likes Received
      1075
      Likes Given
      554

      Default Re: "Tanzania Mpya" Inakuja: Gwajima

      CCM Bana

      Wamekodisha Vifaa Kanisani Halafu Wakavitumia Kuwatukana Uamsho. Astakafilulah
      "SISI SOTE NI NDUGU TATIZO NI CCM" Chris Lukosi kada wa CCM


    7. #45
      Kimbunga's Avatar
      JF Platinum Member Array
      Join Date : 4th October 2007
      Location : Kisiwani Juma
      Posts : 7,469
      Rep Power : 6166
      Likes Received
      3032
      Likes Given
      1013

      Default Re: "Tanzania Mpya" Inakuja: Gwajima

      Huyu Gwajima atakuwa na damu ya Kikenya manake huko Kenya ndio siasa zinatamalaki makanisani. Nimekuwa nikisikia viongozi wa kisiasa hasa wa CCM wakikaribishwa huko kanisani kwake na kutoa maneno ya kisiasa wakati wa Ibada. Nimewahi kuwasikia makamanda dhidi ya ufisadi, nikamsikia Nape na juzi ilikuwa zamu ya Sumaye sijui jumapili hii ilikuwa zamu ya nani. Watu si waende wasali kama tunavyozoea kwenye makanisa mengine. Manake tunaweza kuanza kusikia wanasiasa wanapewa nafasi wakati wa swala misikitini; mwisho itakuwa vurugu tu. Gwajima haitakii mema nchi hii. Hivi ana tofauti gani na Kakobe ama Mwingira au Mzee wa Upako?

    8. FemaTV & Radio

    9. #46
      Bob G's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 5th October 2011
      Location : UK Manyasi
      Posts : 1,650
      Rep Power : 715
      Likes Received
      289
      Likes Given
      36

      Default Re: "Tanzania Mpya" Inakuja: Gwajima

      Hili linajulikana kwamba ccm siku zake zinahesabika, kizuri ambacho na msifu ni kati ya wanaccm wachache wanao ujua ukweli huu kwamba ccm basi

    10. #47
      BINARY NO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th December 2011
      Posts : 549
      Rep Power : 482
      Likes Received
      136
      Likes Given
      63

      Default Re: "Tanzania Mpya" Inakuja: Gwajima

      kwanini asiwe yeye wa kwanza kutoka na anaona ufahari gani kujiita eti mwa ccm? uku ndo kujipendekeza CCM wanamavyombo chungu mzima ata mwaka 2010 walinunua system mpya za music na matangazo kila mkoa asitudandanye huyu ccm ni taasisi kubwa huyu kajipendekeza kwa serikali ya magamba kwani nae ni mcheza dili chafu anaweza kufilisiwa anytime akiwa against nao....meli ikiwa inazama utawashauri vipi wenzako wajiokoe na wewe ufe km sio unafiki?

    11. #48
      Fredrick Sanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th January 2011
      Location : Kijitonyama
      Posts : 2,982
      Rep Power : 2589
      Likes Received
      637
      Likes Given
      776

      Default Re: "Tanzania Mpya" Inakuja: Gwajima

      Hii ni saa ya Ufufuo na Uzima. Mmewafanya watu kuwa misukule kwa miaka 50. Sasa nyota zao zimerudi. Tanzania mpya inakuja. Neno la hekima sasa litoke M4C.
      Gerald likes this.

    12. #49
      Fredrick Sanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th January 2011
      Location : Kijitonyama
      Posts : 2,982
      Rep Power : 2589
      Likes Received
      637
      Likes Given
      776

      Default Re: "Tanzania Mpya" Inakuja: Gwajima

      Inakuja kabisa.
      We shall overcome, righteousness shall always prevail.

    13. #50
      Mercyless's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 449
      Rep Power : 448
      Likes Received
      90
      Likes Given
      575

      Default Re: "Tanzania Mpya" Inakuja: Gwajima

      Quote By Asante
      Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Kawe, Mch.Josephat Gwajima amesema Tanzania mpya yenye matumaini inakuja.

      Akihubiri Kanisani hapo leo alisema ingawa yeye ni mwana CCM na vyombo vyote vilivyotumika kwenye mkutano wa ccm Jangwani jana vilitoka Kanisani kwake, alisema chama cha siasa cha ccm kipo katika wakati mgumu na kimepoteza kabisa mwelekeo na uwezo wa kuongoza dola.

      Amewaonya wanasiasa wanaojiona ni wasafi na bado wanang'ang'ania ccm, wajue mwisho wao kisiasa upo ukingoni, aliwaonya Mwakyembe, Sita na wanasiasa wangine kuwa hali ya ccm ilivyo sasa ni sawasawa na samaki aliye ndani ya bwawa na maji ambalo linakaribia kukauka.

      "Tanzania mpya inakuja" ulikuwa ndio ujumbe wake wa leo.

      Tanzania yenye uwezo wa kukomesha rushwa inakuja.

      Tanzania yenye uwezo wa kujali afya za wananchi wake inakuja.

      Tanzania yenye uwezo wa kukomesha wizi wa mali za uma inakuja.

      Tanzania yenye uwezo wa kuwapatia vijana wake elimu bora inakuja.

      Tanzania yenye uwezo wa kuwalisha wananchi wake inakuja.

      Amewatakia wananchi wote afya njema, wapate kuipokea Tanzania mpya.

      Tanzania mpya inakuja - AMINA.
      Aaaaameeeeeen!!!!!!!!!!!

    14. #51
      IKHOIKHOI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th January 2012
      Location : Bustani ya Eden
      Posts : 344
      Rep Power : 436
      Likes Received
      34
      Likes Given
      34

      Default Re: "Tanzania Mpya" Inakuja: Gwajima

      sipendi kuyaamini haya niliyoyasoma hapa, kumbe magamba walienda kuazima vipaza sauti kanisani?? kweli magamba ni magamba tuuu
      ora et labora

    15. #52
      lyimoc's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 20th February 2011
      Posts : 140
      Rep Power : 445
      Likes Received
      9
      Likes Given
      4

      Default Re: "Tanzania Mpya" Inakuja: Gwajima

      R i p ccm mafuriko yanakuja yatasomba kila aina ya uchafu ndani ya nchi yetu nayo itakua safi

    16. #53
      RICH OIL SHEIKH's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd January 2012
      Location : NEWALA/QATAR/DAR ES SALAAM
      Posts : 800
      Rep Power : 532
      Likes Received
      123
      Likes Given
      40

      Default Re: "Tanzania Mpya" Inakuja: Gwajima

      Kaona ishu za misukule hazilipi kaamia kwenye siasa: HIVI LILE ZOEZI LAKE LA KUMFUFUA AMINA CHIFUPA LILIFANIKIWA?
      Once more into the fray
      Into the last good fight I’ll ever know
      Live or die on this day
      Live or die on this day

    17. #54
      democratic's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st November 2011
      Posts : 1,601
      Rep Power : 818
      Likes Received
      278
      Likes Given
      51

      Default Re: "Tanzania Mpya" Inakuja: Gwajima

      Quote By NATA
      Ndio mrithi wa shehe yahaya ?
      kuwaambia watu ukweli sio utabiri
      Kama damu inakusisimka unapoona haki ya mtu ikipokwa na uko tayari kuitetea kwa gharama yeyote, basi hakika wewe ni Comrade wangu-Che Guevara.


    18. #55
      democratic's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st November 2011
      Posts : 1,601
      Rep Power : 818
      Likes Received
      278
      Likes Given
      51

      Default Re: "Tanzania Mpya" Inakuja: Gwajima

      Quote By Gagnija
      Anakiri kuwa mwanaCCM ingawa anawaonya kina Mwakyembe wasing'ang'anie huko! Yeye anahofia nini, kwa nini asianze yeye kutoka ?
      wewe unadhani na yeye anatumia kamasi kama nyie magamba,yaaani aseme hayuko ccm ili mbomoe kanisa lake kuwa liko kwenye njia ya umeme au ni hifadhi ya barabara..........thubutuuuuuu uuuuuuuuuuu
      Kama damu inakusisimka unapoona haki ya mtu ikipokwa na uko tayari kuitetea kwa gharama yeyote, basi hakika wewe ni Comrade wangu-Che Guevara.


    19. #56
      Dr.Mbura's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 30th June 2009
      Posts : 117
      Rep Power : 526
      Likes Received
      41
      Likes Given
      0

      Default Re: "Tanzania Mpya" Inakuja: Gwajima

      Quote By Mkiliman
      Gwajima ndio mkodishaji wa vyombo vya muziki na matangazo kwaajili ya mkutano wa CCM?
      HAKUKODISHA VYOMBE BALI ALIWAPA CCM bure tena akatoa angalizo kwa CCM kuwa CHADEMA wakija kuazima vyombe yeye atawapa kwa ahiyo CCM wasilalamike

    20. #57
      Communist's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st June 2012
      Location : Ubungo
      Posts : 2,712
      Rep Power : 2263
      Likes Received
      599
      Likes Given
      783

      Default Re: "Tanzania Mpya" Inakuja: Gwajima

      Treni la ufufuo na uzima sasa linataka kufufua watanganyika. Kumbukeni ushirikina umezidi huko magambaz. Hii nchi ilizindikwa kuzimu. Saa ya Ufufuo na uzima imefika, Treni le ufufuo limeweka gea ya M4C, na bahati mbaya breki zimekata. CCM kaeni mkao wa Baru.
      Simple life is healthier than egoism.

    21. #58
      chuki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2011
      Posts : 519
      Rep Power : 518
      Likes Received
      49
      Likes Given
      36

      Default Re: "Tanzania Mpya" Inakuja: Gwajima

      Freemason at work!
      Huyo Mchungaji ni Freemason.
      CHADEMA NI FREEMASON.
      WAMEANZISHA MTANDAO WA KIGAIDI.

    22. #59
      Ngambo Ngali's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th April 2009
      Posts : 2,567
      Rep Power : 1027
      Likes Received
      529
      Likes Given
      398

      Default Re: "Tanzania Mpya" Inakuja: Gwajima

      Quote By Shine
      Mambo mengine siyo utabiri bali hata mwelekeo wa mambo unaonyesha!
      Sawa kabisa, huwezi kutabiri kuwa ikifika saa kuminambili jua litazama na giza litaingia.
      Injustice anywhere is a threat to justice everywhere.

    23. #60
      obseva's Avatar
      Member Array
      Join Date : 23rd March 2009
      Posts : 74
      Rep Power : 531
      Likes Received
      20
      Likes Given
      0

      Default Re: "Tanzania Mpya" Inakuja: Gwajima

      GOD bless Tanzania, GOD bless Gwajima and GOD Bless Israel
      .

    24. Study Abroad
    Page 3 of 10 FirstFirst 12345 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...