Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kauli ya Dr. Slaa kuhusu hoja za ccm Jangwani - CCM mna majibu ya tuhuma hizi??

    Report Post
    Page 1 of 4 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 71
    1. #1
      Honolulu's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 19th January 2012
      Posts : 720
      Rep Power : 0
      Likes Received
      285
      Likes Given
      0

      Default Kauli ya Dr. Slaa kuhusu hoja za ccm Jangwani - CCM mna majibu ya tuhuma hizi??

      WAKATI CCM, ikihaha kujaza watu kwenye mkutano wake, Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Wilbroad Slaa, amekidhihaki chama hicho kuwa hakiwezi kuendelea kutawala nchi kwa kuwalipia nauli, kuwabeba na kuwapa posho watu wanaokwenda kwenye mikutano.
      Slaa, alisema ilani ya chama chochote makini inapaswa kuonekana machoni mwa wananchi na siyo kusemwa kama ambavyo Rais Jakaya Kikwete na timu yake ndani ya CCM wanavyofanya.

      Kauli hiyo aliitoa jana katika Uwanja wa Likangala wilayani Ruangwa mkoani Lindi wakati akihutubia mkutano wa hadhara, huku akitanabaisha kuwa wafuasi wanaokipenda chama chao hawawezi kubebwa na magari kwenda kwenye mikutano kwa kulipiwa nauli.
      Dk. Slaa alikuwa akijibu matamshi mbalimbali yaliyokuwa yakitolewa na viongozi wa CCM katika mkutano wao wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam na kurushwa moja kwa moja na vituo vya redio na runinga.

      Alisema mawaziri wa CCM wamekuwa makasuku kwa kushindwa kutathmini kauli zao za awali, ambazo hazijatekelezwa na kwamba sasa wanakuja na hoja nyingine zisizotekelezeka.

      Akiwachambua baadhi ya mawaziri na kuanza na Jumanne Maghembe, alisema kuwa anapaswa akumbuke miaka zaidi ya kumi iliyopita serikali ilikuja na mkakati wa kilimo cha umwagiliaji na kusema imeshapata kiasi cha dola milioni 12 za Marekani kwa ajili ya shughuli hiyo.
      “Tunataka watuambie hizi fedha zimeenda wapi mpaka sasa wanakuja na kauli nyingine, hivi hakumbuki tulikaa katika ukumbi wa mikutano wa Pius Msekwa wakatuambia hizi fedha zipo, sasa zimeenda wapi?” alihoji Dk. Slaa.
      Kuhusu ujenzi wa barabara kilomita 11,000 zilizoelezwa na Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, Slaa alisema huo ni upuuzi kwa kufananisha hali hiyo na mahitaji mazima ya nchi.


      Alisema fedha zilizoibwa na watumishi wa serikali ya CCM ni nyingi kuliko hivyo wanavyojinadi kuwa wamefanya, na kuitaka serikali ieleze dola milioni 1.5 zilizokutwa katika akaunti ya mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge (CCM) zimefanyiwa nini.

      Alibainisha kuwa, Serikali ya CCM inapaswa kutolea maelezo fedha za chenji ya rada zimefanya nini wakati katika mahesabu ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) hazionekani kutumika.


      Kuhusu kauli ya Steven Wassira kuwa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Freeman Mbowe atalaaniwa kwa kuwa baba yake aligombea uhuru na Mwalimu Nyerere, Dk. Slaa alisema viongozi hao walisimama kwa ajili ya kuwatetea Watanzania na kama watasimama leo kuna hatari ya kuwachapa viboko viongozi wa CCM kwa kushindwa kuendeleza malengo waliyofikia.

      Naye Mbowe alisema anamsikitikia Wassira kwa kile alichoeleza kuwa, anashindwa kusimamia hata utendaji wa nafasi yake na badala yake anahangaika kuropoka kila wakati mambo yasiyo na tija kwa taifa.
      Alibainisha kuwa, Wassira si saizi yake kwenye majukwaa ya kisiasa kwa sababu hana hadhi ya kupigania ukombozi wa kweli, hivyo akamtaka awatafute watu wenye hadhi yake.

      Alisema katika hali ya sasa, CCM haioni mahaba ya wananchi, hivyo wanajitahidi kukusanya watu katika maeneo mbali mbali ya nchi ikiwa ni pamoja na kununua kadi za CHADEMA kwa ajili ya kujiaminisha mbele ya wananchi.

      “Hawa watu vipi, wana nini sijui kwa kuwa wanatunga uongo wanauaminisha umma na mwisho wa siku wanauamini huo uongo walioutunga kama ambavyo wamefanya leo kule Jangwani,” alisema Mbowe.

      Source: Tanzania Daima


    2. #2
      STIDE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st September 2011
      Posts : 822
      Rep Power : 563
      Likes Received
      275
      Likes Given
      0

      Default Re: Kauli ya Dr. Slaa kuhusu hoja za ccm Jangwani - CCM mna majibu ya tuhuma hizi??

      Yap!! Dr wa ukweli amenena!! Yaani over compyuta!! Big up Dr!! Ccm na wakuda wake wooote njooni na majibu yenye ujazo!!

      I'll be back.

    3. #3
      Yericko Nyerere's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2010
      Location : Kigamboni, DSM
      Posts : 4,965
      Rep Power : 23055
      Likes Received
      3012
      Likes Given
      315

      Default Re: Kauli ya Dr. Slaa kuhusu hoja za ccm Jangwani - CCM mna majibu ya tuhuma hizi??

      Hawana majibu kabisa, kwanza hata sasa hivi uwafuate na kuwauliza waliyozungumza jana jangwani nakuhakikishia hakuna atakae kumbuka,

      Hawatakumbuka kwakuwa mioyo yao ilipingana na uongo wao!

    4. #4
      Radhia Sweety's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th August 2011
      Posts : 1,413
      Rep Power : 0
      Likes Received
      691
      Likes Given
      4

      Default Re: Kauli ya Dr. Slaa kuhusu hoja za ccm Jangwani - CCM mna majibu ya tuhuma hizi??

      CCM ikifikia mnaanza kujibishana badala ya kufanya kazi basi siku zenu za kuishi uongozini zinahesabika. Kwahiyo badala ya kufanya kazi nyie mtazunguka kila mkoa Chadema ilikopita?
      TELO and Precise pangolin like this.

    5. #5
      MNYISANZU's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 21st October 2011
      Posts : 6,311
      Rep Power : 0
      Likes Received
      593
      Likes Given
      76

      Default Re: Kauli ya Dr. Slaa kuhusu hoja za ccm Jangwani - CCM mna majibu ya tuhuma hizi??

      Dr Slaa ana akili mile 1000,000,000,000 zaidi ya magamba yote!


    6. #6
      MESTOD's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th November 2010
      Posts : 2,621
      Rep Power : 960
      Likes Received
      707
      Likes Given
      131

      Default Re: Kauli ya Dr. Slaa kuhusu hoja za ccm Jangwani - CCM mna majibu ya tuhuma hizi??

      Inasikitisha sana chama kikongwe kila wakati kukaa na ku copy ya chadema. Hivi ccm, hamuwezi nadi sera zenu bila maji taka?
      Kujibu hoja za chadema iwe ni kutekeleza ahadi, na yale yote mnayosema mmeyafanya yaendane na hali halisi ya mapato yetu.

    7. #7
      kaburungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th March 2011
      Posts : 354
      Rep Power : 567
      Likes Received
      56
      Likes Given
      67

      Default Re: Kauli ya Dr. Slaa kuhusu hoja za ccm Jangwani - CCM mna majibu ya tuhuma hizi??

      Moja ya mbinu inayotumia serikali ya CCM ni kuhadaa wananchi kwa kuibua ahadi. nzuri zinazosikika vizuri masikioni mwa watanzania.

      Wanasahau kile walichohaidi jana au juzi kimetekelezwa au la bahati mbaya sana kwa CCM na serikali yake ni kwamba, watanzania wa leo ufahamu wao uko juu na hii ni kutokana na kazi nzuri inayoendelea kufanywa na CDM.

      Watanzania wa leo wanaujasiri wa kuhoji,kudadisi utekelezaji wa yale walohaidiwa mwanzo na kizuri zaidi washaelewa nani mchawi wao.

      Nawasilisha.

    8. #8
      Precise pangolin's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 4th January 2012
      Posts : 5,761
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1609
      Likes Given
      684

      Default Re: Kauli ya Dr. Slaa kuhusu hoja za ccm Jangwani - CCM mna majibu ya tuhuma hizi??

      Quote By Radhia Sweety View Post
      CCM ikifikia mnaanza kujibishana badala ya kufanya kazi basi siku zenu za kuishi uongozini zinahesabika. Kwahiyo badala ya kufanya kazi nyie mtazunguka kila mkoa Chadema ilikopita?
      Mama naona siku hizi umebadilika !!!!
      Jasusi likes this.

    9. #9
      STIDE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st September 2011
      Posts : 822
      Rep Power : 563
      Likes Received
      275
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Precise pangolin View Post
      Mama naona siku hizi umebadilika !!!!
      Mkuu, hivi ndie huyu au ID zinaelekeana!? Maana nahisi kama yule kimeo alikuwa anaitwa R. Sweke au!?

    10. #10
      DOWN SYNDROME's Avatar
      Member Array
      Join Date : 8th June 2012
      Posts : 18
      Rep Power : 357
      Likes Received
      6
      Likes Given
      3

      Default Re: Kauli ya Dr. Slaa kuhusu hoja za ccm Jangwani - CCM mna majibu ya tuhuma hizi??

      CMD ni chama makini sana!

    11. #11
      hans79's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th May 2011
      Posts : 1,673
      Rep Power : 806
      Likes Received
      163
      Likes Given
      0

      Default Re: Kauli ya Dr. Slaa kuhusu hoja za ccm Jangwani - CCM mna majibu ya tuhuma hizi??

      Ukweli utajulikana tu waache waendelee na mipasho yao hawa nyinyiemu, unafanya mkutano huku unatangaza ya kuwa wasanii hawa watakuwepo. Je hao kuwepo kwao kunasaidia nini?

    12. #12
      democratic's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st November 2011
      Posts : 1,606
      Rep Power : 824
      Likes Received
      279
      Likes Given
      53

      Default Re: Kauli ya Dr. Slaa kuhusu hoja za ccm Jangwani - CCM mna majibu ya tuhuma hizi??

      viva dokta,viva mbowe,viva cdm
      Kama damu inakusisimka unapoona haki ya mtu ikipokwa na uko tayari kuitetea kwa gharama yeyote, basi hakika wewe ni Comrade wangu-Che Guevara.


    13. #13
      christine ibrahim's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2012
      Posts : 2,897
      Rep Power : 948
      Likes Received
      473
      Likes Given
      440

      Default Re: Kauli ya Dr. Slaa kuhusu hoja za ccm Jangwani - CCM mna majibu ya tuhuma hizi??

      yaan nyinyiem + plus Nape ni janga la kitaifa

    14. #14
      Crashwise's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd October 2007
      Location : Safarini
      Posts : 13,490
      Rep Power : 19248
      Likes Received
      4229
      Likes Given
      3379

      Default

      Quote By Precise pangolin View Post
      Mama naona siku hizi umebadilika !!!!
      ulitegemea mtoto mzuri kama radhia angeendelea kuwa ccm mpka lini kaiona nuru...kuishabikia au kuiunga mkono ccm lazima uwe na akili ya maiti..huoni hata akina faizafox,mwita25

    15. #15
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 16,053
      Rep Power : 14671
      Likes Received
      2957
      Likes Given
      2099

      Default Re: Kauli ya Dr. Slaa kuhusu hoja za ccm Jangwani - CCM mna majibu ya tuhuma hizi??

      Kilomita zaidi ya 11,000 kwa kipindi cha Kikwete tu ni upuuzi? huyu mzee kweli hamnazo.

      Amesha jiuliza, Mkoloni, Nyerere, Mwinyi na Kikwete na yeye akiwemo hukohuko kabla ya ujio wa Kikwete walitengeneza kilo mita ngapi? jumlisha zote pamoja na za Slaa, uone kama zinafika hata nuzu za hii miaka 7 tu ya Kikwete.

      Kumbuka, ukitoa mkoloni, Nyerere miaka 24 KM ngapi? Mwinyi (na Slaa akiwepo)? Mkapa ngapi? Kiwete zaidi ya KM 11,000.

      Amma kweli akutukanae hakuchagulii tusi.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    16. #16
      STIDE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st September 2011
      Posts : 822
      Rep Power : 563
      Likes Received
      275
      Likes Given
      0

      Default Re: Kauli ya Dr. Slaa kuhusu hoja za ccm Jangwani - CCM mna majibu ya tuhuma hizi??

      Mmh!! Crashwise inamaana FF alishaiona nuru!!? Mwita25 huyo nakumbuka alishaanza kuujua ukweli japo unafiki ulimtatiza, lakini huyu mwingine siwezi amini, na KAMA ni kweli basi CHADEMA LEVEL NYINGINE zaidi ya ninavoijua!!

    17. #17
      trachomatis's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th June 2011
      Location : Dar es Salaam,Tanzania.
      Posts : 3,460
      Rep Power : 1099
      Likes Received
      484
      Likes Given
      235

      Default

      Quote By Yericko Nyerere View Post
      Hawana majibu kabisa, kwanza hata sasa hivi uwafuate na kuwauliza waliyozungumza jana jangwani nakuhakikishia hakuna atakae kumbuka,

      Hawatakumbuka kwakuwa mioyo yao ilipingana na uongo wao!
      Mimi najiuliza iweje Serikali ijieleze mbele ya wanachama wake na si wananchi wake? Huu ni utumiaji mbaya wa madaraka kwa chama kuyahodhi kiasi hicho. Na nadhani hii move ni kama vile wanajifunga wenyewe goli katika harakati za kuokoa mpira.

    18. #18
      Mwanaweja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th February 2011
      Posts : 3,520
      Rep Power : 1128
      Likes Received
      480
      Likes Given
      1065

      Default Re: Kauli ya Dr. Slaa kuhusu hoja za ccm Jangwani - CCM mna majibu ya tuhuma hizi??

      Dr. ulichonena hakina upinzani kinahitaji majibu yakina na si longolongo za kuongea maneno matupi majukwaani ccm ni serikali inatakiwa kutenda na wala sio kuongea sana bila vitendo. hawa wa meishiwa kabisa na ndio mwisho wa kutawala wajiandae kwenda kukaa uhamishoni maana nawatamani sana nje yahapo wote wataishia gerezani na maisha yaliyobaki watayamalizia gerezani.

    19. #19
      mbumbumbu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th December 2010
      Location : Nyasamba, Shinyanga vijijini
      Posts : 471
      Rep Power : 527
      Likes Received
      75
      Likes Given
      13

      Default

      Quote By DOWN SYNDROME View Post
      CMD ni chama makini sana!
      Mkuu CMD bado kuanzishwa Tanzania, kwa sasa tuna CDM.

      Asante!

    20. #20
      Lambardi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th February 2008
      Location : KITAANI ZAIDI
      Posts : 4,588
      Rep Power : 1814
      Likes Received
      666
      Likes Given
      0

      Default Re: Kauli ya Dr. Slaa kuhusu hoja za ccm Jangwani - CCM mna majibu ya tuhuma hizi??

      Watanzania wanataka hoja zijibiwe na ugumu wa maisha udhibitiwe hasa mazao ya chakula ya ndani!!!sio kutupa vijembe kama taarabu,watu wameshaamka wanapoteza pesa zao bure maana watanzania wa leo sio wa jana kamwe,watashangaa sana naona kuna nusu ya wabunge watakosa ubunge mwaka 2015 sababu ya kutojali matatizo ya wananchi!!!

    Page 1 of 4 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...