Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mkutano wa CCM Jangwani: CCM yafa Rasmi

    Report Post
    Page 2 of 6 FirstFirst 1234 ... LastLast
    Results 21 to 40 of 105
    1. #1
      SEBM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2012
      Posts : 339
      Rep Power : 3536
      Likes Received
      258
      Likes Given
      98

      Default Mkutano wa CCM Jangwani: CCM yafa Rasmi

      UTANGULIZI

      Wote tulisikia kwenye vyombo mbalimbali vya habari juu ya uwepo wa mkutano wa hadhara katika viwanja vya Jangwaniulioitishwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) ukiwa na maudhui ya Kutoa Msimamo Wake Juu ya Masuala Yanayogusa Mustakabali wa Taifa hususan katika maeneo makubwa matatu:

      (a) Hatma ya Maisha ya Watanzania Katika ajira, miundombinu, Reli, Barabara, umeme, bei ya bidhaa, raslimali n.k)
      (b) Mchakato wa Katiba na
      (c) Vurugu za Zanzibar

      Mkutano huu uliotegemewa kuwa na watu wengi; kwa kweli ulihudhuriwa na maelfu ya wanachamana wafuasi wa CCM ambao wengi wao waliletwa na mabasi, malori n.k. MWANZO WA MKUTANO Kabla ya kufunguliwa mkutano rasmi, kulikuwepo na utambulisho wa viongozi mbali mbali waCCM ambao walitoa salamu zao.

      Awali walielezea kwamba ule haukuwa mkutano wa mipasho, bali ulilenga kuwaambia wananchi wa CCM nini kimefanywa na Serikali ya CCM katika utekelezaji wa Ilani ya CCM.

      Miongoni mwa kauli tata zilizojitokeza ni;-

      - CCM kusifiwa kwa kuwa na wanachama wa aina mbali mbali ya watu (makundi yote) tofauti ya vyama vingine vinavyowagawa watu kidini na kikabila (Kaongea mama mmoja nimesahau jina lake)
      - Wananchi kuwaogopa wapinzani wanaozunguka nchi nzima kueneza sera zao kwa kuwa haowamefadhiliwa na wazungu/wabebari ambao wana nia ya kuja kuchukua rasilimalizetu (Mwingulu Nchemba).
      - Mbunge mmoja alisema wanataka Jamhuri ya Kaskazini na baada ya muda Mbowe akasema alikosea kusema hiyo kauli. Lakini sisi tunasema kuwa mtoto akikosea au akisema jambo basi katumwa na Baba yake na hivyo Mbunge huyo alitumwa na Baba yake – Mbowe (John Guninita)

      HOJA ZA MAWAZIRI
      Waliandaliwa mawaziri mbalimbali ambao uwepo wao ulilenga kuhakikisha wanatoa majibu kwa wananchi ya nini kimefanywa na serikali ya CCM kwa 2010 – 2015.

      Mawaziri hawa ni wasomi wenye sifa za Uprofesa (Tibaijuka, Maghembe) na Madaktari (Mwakyembe na Magufuli) na mwingine sijui elimu yale ( Wassira).

      (1) Prof. Jumanne Maghembe
      Ni Waziri mwenye dhamana ya Maji.

      - Hakuna la maana alilozungumza hususan utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwa 2010 – 2015 zaidi ya kutoa maelezo ya ‘mipango’ ya serikali na wizara yake katika kuleta maji Dar Es Salaam. Muda mwingi aliutumia kuzungumza ‘cubic meter’ za maji zitakazofika Kimara, visima anavyodhamiria kufungua 15/07/2012, na kwamba katika bajeti ya 2012/2013 kutengwa kwa hela (hajazitaja, maana bajeti haijapita, anyway) ka ajili ya kuimarisha upatikanaji wa maji.

      (2) Steven Masatu Wassira
      Ni waziri mwenye dhamana ya Uratibu na Mahusiano.

      - Alianza mkutano wake kwa kuwafahamisha wananchi kuwa alikuwa anamwakilisha Rais Masetu, Lesotho na baadaye kupanda ndege Johanesburg na kuwahi mkutano Jangwani.

      - Baadaye akazungumzia juu ya sababu mbali mbali zinazoleta ugumu wa maisha kwa wananchi:

      - Uchumi; hali inasababishwa na kuyumba kwa hali ya uchumi duniani.

      - Chakula; kwamba Tanzania kama nchi inalima sana na eneo lake kubwa (56%) linatumika kwa kilimo na hivyo nchi majirani za Kenya, Uganda, South Sudan huja Tanzania kubeba chakula karibu chote na hivyo Tanzania kutokuwa na chakula.

      - Kupanda kwa bidhaa za mafuta kunatokana na vita inayoendelea huko Iran na Mataifa ya Magharibi.

      - Uhaba/gharama ya sukari ; unasababishwana kuwepo kwa viwanda vichache vya sukari (alimaanisha TPC, Kagera, Mtibwa, Kilombero)na hivyo serikali inajenga viwanda vitano zaidi (hakusema kama 100% vitamilikiwa na serikali au vitakuwa tena vya makaburu, wa-madagascar n.k)

      - Umeme; hali ya matatizo ya mvua na hivyo mpango unafanyika kujenga mitambo ya gesi asilia kutoka Mtwara –Dar.

      Alimalizia wasilisho lake kwakusema kuwa kuna shule nyingi sana na ukilinganisha zamani na sasa; kuna vyuo vikuu vingi na kulikuwa na chuo kikuu chenye wanafunzi 14 wa Sheria pale Lumumba. [ukweli ni kuwa, University of East Africa (Makerere) katika kuhakikisha inapanuka, ilianzisha tawi Tanzania na wanafunzi walikuwa pale Ushirika na walikuwa wanalala Kigamboni wakati kunajengwa UDSM]

      (3) Profesa Tibaijuka: Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

      - Kimsingi sikujua hata alichokuwa anakielezea pale jukwaani zaidi ya kuzungumza kuwa alifika Dar 1970 na yeye ni Mwalimu wa UDSM (Economics) na kuwa alikuwa NJE ambako baada ya kuchuma (alimaanisha mali, ila akaja na kusema kuchuma Ujuzi) alirudi Tanzania.

      - Alisema tu kuwa kero za Ardhi Kigamboni na Kurasini zinafahamika na watazifanyia kazi; na kwenye bajeti ya 2012/2013 wametenga fedha kwa ajili ya mipango mingi ya maendeleo.

      - Zaidi pia alisema juu ya ujio wa Mji wa Kisasa wa Kigamboni utakaofanana na Dubai na Bahrain na kwamba wananchi waendelee kumpatia kero zao na kuwa kulipa pango kwamiezi 12 ni batili na uhalali ni kulipa kwa miezi 3 tu.

      (4) Dr. Harisson Mwakyembe: Waziri wa Uchukuzi.

      - Nadhani hakuwa anajua Ilani ya CCM inasemaje au pia hakujua yuko mkutanoni pale kufanya nini, maana alianza kuzungumzia kuhusu Wapinzani kuelezea MADUDU YALIYOBAINIWA NA CAG na kwamba Mamlaka makubwa kapewa CAG na Rais (sikuelewa uhusiano!).

      - Zaidi ya kuzungumza juu ya kutozwa nauli ya 1,500 Tegeta; na nauli za Kimara na kutoa namba yake ya simu (0782 24 25 26) ili tumpigie na kumpa kero kwakuwa ‘ana simu kubwa’ hakuna la maana alilozungumza.

      - Kauli zake nyingi ni zilezile za ‘mipango’ ya kufanya hiki na kile: kuwa na treni Ubungo Maziwa mpaka Stesheni; kufufua TAZARA, kusafisha Bandari. Alimalizia kwa kusema ‘ TUPENI MUDA TUNAYAFANYIA KAZI MATATIZO YENU’

      (5) Dr. John Magufuli: Waziriwa Miundo Mbinu.

      - Pamoja na kwamba tangu awali nilitegema kusikia idadi yakilometa za lami zinazojengwa na majina ya makampuni, sikutegemea kufahamu kuwa kipaji chake kingine ni kufahamu lugha mbali mbali za Kitanzania.

      - Aliendelea tu kutaja kilometa za Lami zinazowekwa huku akitoa ulinganisho wa kilometer za lami tangu uhuru (6,500) hadi sasa (11,154) tofauti la kauli ya awali ya Wassira kuwa uhuru kulikuwa na barabara 3 tu (Dar – Moro. Hii naijua ina kama 200kms; Tanga - Korogwe ; kama 101kms na Arusha – Moshi; kama 90kms.)

      - Alizungumza pia kuwa bajeti hii ya 2012/2013 imepanga kutekeleza miradi mingi ya maendeleo ya barabara. Labda tukio la kusisimua ni kuwa, wakati akiwa anaendelea kuongea (huku ikijionyesha dhahiri kuna kitu anakisubiria), Magufuli alitangaza kuwa ameongea kwa muda mrefu na amemaliza muda wake lakini anatambua kuwa kuna watu wanataka kurudisha kadi za CCM (akabadili ghafla na kusema za vyama vingine) waziwasilishe.

      Katika hali ya kushangaza, waliibuka watu wa umri mmoja (vijana wa kike na kiume wa umri wa miaka 28 – 33), na ambao walionekana wakiwa wanafahamiana kabla (au kukaa pamoja kabla), na waliokuwa wakicheza wimbo mmojakwa umahiri walirudisha kadi. Kadi hazikuonekana na wala hawakujitokeza katika kuzungumza kwa nini ‘walihama huko walikotoka’ na kujiunga na CCM.

      HITIMISHO

      - Lazima nikiri, kwa kusikia na kutazama yaliyosemwa na CCM katika mkutano wao leo, ni dhahiri kuwa CCM imefikia mwisho wake kwa kuwa imeshindwa kuwapa majibu sahihi watanzania juu ya shida zao na namna serikali ya CCM ilivyoweza kuwakwamua wananchi na mipango yake thabiti ijayo katika kuhakikisha kila kitu kinakuwa sawa.

      - Pamoja na kuwa Kinana alikuja kuelezea kuwa mada nyingine mbili (Katiba na Zanzibar) zitawasilishwa na Kamati/Halmashauri kuu kwaKamati ya Warioba, lakini ukweli ni kuwa walikosa majibu ya kuridhisha.

      - Mwanzoni walisema hawako pale kujibu hoja za vyama vingine au kuweka mipasho, lakini kauli zao zilijidhihirisha kuwa hawakuwa na la maana la kusema/kuwaambia wananchi (mfano, salamu ya ‘vyama vingine vidogo’ hoyee, ya Magufuli, Mbowe arudi kuuza Pombe, CCM wataweka lami na CHADEMA waandamane kwenye hizo lami n.k)

      - Kimsingi ni kama vile tulikuwa kwenye mkutano wa kampeni, kusikiliza ahadi za nini chama kitafanya na wala si nini kimefanywa na serikali ndani ya 2010 – 2015.

      - Walichokifanya mawaziri hawa, wasomi, ni upotezaji wa muda wa wananchi na upotevu wa rasilimali za Taifa kwani wangeweza kuongea waliyoongoea kwa kuwaambia tu manaibu waziri wao wazungumze na wahariri au wazee wa Dar Es Salaam na si kama walivyofanya.

      CCM Imejivua nguo rasmi leo; CCM Imekufa Rasmi
      Last edited by SEBM; 9th June 2012 at 20:06.


    2. #21
      Barnabas Shadrack's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd July 2011
      Posts : 2,061
      Rep Power : 815
      Likes Received
      186
      Likes Given
      12

      Default Re: Mkutano wa CCM Jangwani: CCM yafa Rasmi

      Ccm wafe au wasife hawani impact yoyote katika maisha yangu na ya watanzania wengi.
      The unseen is illustrated by the seen.

    3. #22
      Capt Tamar's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th December 2011
      Posts : 1,840
      Rep Power : 1066
      Likes Received
      447
      Likes Given
      1

      Default

      Quote By Ngarenaro View Post
      Acha upotoshaji wakati mwingine si lazima sana kuchambua mambo ya CCM, ambayo ni dhahiri yapo nje ya uwezo wako, ukweli ni kwamba umeupindisha ukweli na umepotosha kwa kiasi kikubwa yale yaliyozungumza kwenye Mkutano wa leo.
      Watu wazima wakiongea uwe unanyamaza kimya!!ngarenaro na jangwani wapi na wapi? Au ni wivu wa kutosombwa na malori kwenda karatu kula ubwabwa kama ilivyokuwa kipindi cha kampeni, tatizo lenu warangi wengi wa ngarenaro ni uvivu, na ujinga!

      Kwenda zako huko.

    4. #23
      tanira1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th November 2011
      Posts : 661
      Rep Power : 515
      Likes Received
      114
      Likes Given
      99

      Default Re: Mkutano wa CCM Jangwani: CCM yafa Rasmi

      Quote By Ngarenaro View Post
      Acha upotoshaji wakati mwingine si lazima sana kuchambua mambo ya CCM, ambayo ni dhahiri yapo nje ya uwezo wako, ukweli ni kwamba umeupindisha ukweli na umepotosha kwa kiasi kikubwa yale yaliyozungumza kwenye Mkutano wa leo.
      acha ushamba wewe siku hizi dunia ni kijiji kimoja kila mtu ameona na kusikia kwangu mimi mtoa mada hakuwa biased amesema kilichojiri wewe kwa ugonjwa wa kupenda hujaona hata pumba moja ya mkutano ule gamba mkubwa wewe

      ''MIAKA HAMSINI(51) YA UVUMILIVU''​

    5. #24
      Makala Jr's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th August 2011
      Posts : 1,949
      Rep Power : 890
      Likes Received
      405
      Likes Given
      0

      Default Re: Mkutano wa CCM Jangwani: CCM yafa Rasmi

      Msishangae,hata mwanza walipokuja kujilopokea watu walibebwa kwenye malori na mabasi.Walipewa wali nyama,walickiliza maneno ya kwenye khanga ya Vicky Kamata na Suma Lee.Lakini ulipofika uchaguzi wa kata ya Kirumba tukawafundisha demokrasia hadi wakachukia na kuwakata mapanga wabunge wetu.Hawa magamba wamekengeuka kwa asilimia kubwa ndo maana wanahangaika majukwaani.Mi naamini sera zikitekelezwa wananchi wataona wenyewe siyo kuonyeshwa kwenye majukwaa.Ama kweli,mbio za panya huishia sakafuni.

    6. #25
      Ms Judith's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th December 2010
      Posts : 2,542
      Rep Power : 972
      Likes Received
      851
      Likes Given
      584

      Default Re: Mkutano wa CCM Jangwani: CCM yafa Rasmi

      wapendwa,

      kwanza nakushukuru sana mleta mada ( SEBM) kwa kutuchambulia na kutuletea kwa muhtasari yote yaliyojiri. ubarikiwe sana mpendwa

      matumizi ya pesa kwenye siasa ni kitu kibaya sana. kila anayeng'ara katika ccm alitumia pesa kuwa hapo alipo. matokeo yake wanasiasa wa kweli wamefunikwa na hawachomozi kwa kukosa pesa ama kwa kulinda maadili wakajizuia kutoa rushwa.

      hao waliozungumza wote, hakuna hata mmoja aliyepiga siasa pekee kupata nafasi aliyonayo. naweza kuhitimisha kuwa hao wote si mifano ya kuigwa kisiasa na kimaadili na hata siasa yenyewe hawaijui! hivyo haishangazi kuona wakizungumza kama wapinzani wakati chama chao kiko madarakani kwa nusu karne sasa!

      hawa ndio magamba halisi waoapaswa kujipima na ujiondoa chamani ama waondolewe! kwa kweli wamenisikitisha sana

      mbarikiwe sana wapendwa

      Glory to God!
      Mtu awaye yote asiyempenda BWANA, na awe amelaaniwa. MARAN ATHA!!!
      (1 Wakorintho 16:22)


    7. #26
      mfereji maringo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th November 2010
      Posts : 862
      Rep Power : 607
      Likes Received
      141
      Likes Given
      47

      Default Je haya yaligusiwa ktk mkutano wa ccm leo?

      Wadau Habari?
      Leo sikupata muda wa kusikiliza viongozi wakihutubia katika mkutano wa CCM viwanja vya Jangwani naskia kunaitwa siku hizi CHADEMA SQUARE naomba kwa aliesikiliza asinambie wamezungumzia nini? Naomba kama kuna mzungumzaji yeyote kati yao amegusia jambo lolote kati ya mambo yafuatayo, na labda atanisaidia kama ataniambia wamelizungumziaje?
      1. Wizi wa kagoda Agriculture, Deep Green, Buhemba EPA, je wamedokeza chochote kuhusu wizi huu?

      2. Vipi jamani wamegusia kuhusu Uuzwaji wa nyumba za serikali? Vipi wamesema lini watazirudisha? Au wanadhani hatuzihitaji?

      3. Vipi kuhusu Mikataba mibovu ya madini tayari wameirekebisha?

      4. Kuhusu huduma mbovu za jamii wamezungumzia mipango yeyote ya kuiboresha?

      5. Twiga vipi waliosafirishwa kuna yeyote aliyefikishwa mahakamani?

      Ni hayo tu kwa sasa, nasubiri majibu wadau

    8. #27
      sweke34's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th September 2010
      Posts : 2,493
      Rep Power : 1259
      Likes Received
      734
      Likes Given
      1240

      Default Re: Mkutano wa CCM Jangwani: CCM yafa Rasmi

      Quote By Honolulu View Post
      CCM imeishaujua ujinga wa watanzania na ndio maana inawatongoza na inapowapata inawatumia ipasavyo.

      Inawahadaa watanzania mithili ya mvulana anayemtafuta msichana!!! Inawatongoza kwa vitisheti vya njano na vikofia vya kijani; Inawapa lifti; inawalisha wali kuku; inawatumbuiza kwa taarabu; inawaahidi maisha bora na kisha inawahonga elfu tano!! Kwa ulaini wananchi wanakubali kufanya mapenzi na CCM. Wanapewa mimba. Wanazaa ufukara na kisha CCM inawatelekeza kwa maisha duni!

      Nionavyo mimi:

      Watanzania wakiteseka na mazingaombwe ya ugumu wa maisha ni sawa tu!! Ni haki yao!! Waendelee tu kutaabika kwa kuwa dhiki, mahangaiko na ufukara wanavitaka wenyewe!!
      Tafadhali bana...kabla ya kila neno 'watanzania' anza na 'baadhi ya'...unakuwa unatutusi sana ukitujumuisha sote na takataka za CCM...!

    9. #28
      Concrete's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2011
      Posts : 1,741
      Rep Power : 987
      Likes Received
      461
      Likes Given
      0

      Default Re: Mkutano wa CCM Jangwani: CCM yafa Rasmi

      Ni aibu kwa chama kikongwe kama CCM kufanya mkutano wa kisanii kabisa kama huu.
      Hii ni mbinu ya secretarieti ya Mukama kujifanya inafanyakazi kukwepa lawama,mambo kama haya alifanya sana Makamba senior chama kikapoteza mwelekeo naona wakina Nape wanarudia usanii uleule ili chama kife kabisa.

    10. #29
      Crashwise's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd October 2007
      Location : Safarini
      Posts : 13,470
      Rep Power : 19244
      Likes Received
      4189
      Likes Given
      3368

      Default Re: Je haya yaligusiwa ktk mkutano wa ccm leo?

      utasubiri jibu mpaka yesu atarudi, hatamimi sijasikiliza lakini wote waliokuwepo hakuna mwenye uthubutu wa kuyaongelea...

    11. #30
      Kibanga Ampiga Mkoloni's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th August 2007
      Location : Here! here!
      Posts : 5,094
      Rep Power : 1778
      Likes Received
      1269
      Likes Given
      1710

      Default Re: Mkutano wa CCM Jangwani: CCM yafa Rasmi

      Quote By Ngarenaro View Post
      Acha upotoshaji wakati mwingine si lazima sana kuchambua mambo ya CCM, ambayo ni dhahiri yapo nje ya uwezo wako, ukweli ni kwamba umeupindisha ukweli na umepotosha kwa kiasi kikubwa yale yaliyozungumza kwenye Mkutano wa leo.
      Sasa si uandike ukweli?
      For the Holy Quran says in Sura 42, verse 41: 'All those who fight when oppressed incur no guilt, but Allah shall punish the oppressor, Come the day.

    12. #31
      magosha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th April 2012
      Posts : 351
      Rep Power : 430
      Likes Received
      36
      Likes Given
      9

      Default Re: Mkutano wa CCM Jangwani: CCM yafa Rasmi

      ccm ishakufa zamani inasubiri kuzikwa tuu.

    13. #32
      Froida's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th May 2009
      Posts : 3,854
      Rep Power : 1343
      Likes Received
      758
      Likes Given
      153

      Default Re: Mkutano wa CCM Jangwani: CCM yafa Rasmi

      CCM kushindana na chadema wanajitia aibu mkutano haukuwa na hamasa yeyote wale wa mama na mikorogo yao unawaona walivyochoka ,Mawaziri hawana hata mfupa wa kujiamini walikuwa wanaonyesha uoga,Vitisho Mwakyembe analalamika eti atatimua wapi hivi nani amewambiya kutisha wafanya kazi kutaongeza tija,wakati chama chao ndio msuka raketi ya wizi
      Kinana Msomali mwizi wa pembe za ndovu,msafirisha wanyama hai,mleta wasomali nchini alshabaab eti ana nguvu hata ya kusema wapinzani hawana safu ya kuongoza CCM wamelala usingizi kweli ,wanadhani wataendelea kuiba kura tunawaambia safari hii tutapiga kura na kuilinda hawakujiandaa kabisa

    14. #33
      jingalao's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th October 2011
      Location : kikonga
      Posts : 738
      Rep Power : 535
      Likes Received
      129
      Likes Given
      27

      Default Re: Mkutano wa CCM Jangwani: CCM yafa Rasmi

      ccm walidhani hukumu itatolewa kwa kuangalia namba ya wahudhuriaji kumbe ni ujumbe kwa waliofika na wasiofika.ni fedheha ya hali ya juu.

      KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA

    15. #34
      Ruttashobolwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd February 2012
      Posts : 13,779
      Rep Power : 19847
      Likes Received
      4407
      Likes Given
      1715

      Default Re: Je haya yaligusiwa ktk mkutano wa ccm leo?

      Nape amegusia kuhusu kufungua band na lusinde. Na mipasho ili tawala pamoja na mwanachama mmoja kusisitiza hawataki mipasho,lakini nape hakumuelewa.

      Wassira alisema alikuwa south kwenye sherehe.

    16. #35
      Dar_Millionaire's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 6th August 2008
      Posts : 173
      Rep Power : 589
      Likes Received
      25
      Likes Given
      175

      Default Re: Mkutano wa CCM Jangwani: CCM yafa Rasmi

      Mkuu SEBM,

      Umesahau ishu moja ya msingi kabla ya kutangaza kifo cha CCM.

      - Leo wamejitokeza wanawake wengi kuliko ule mkutano wa CHADEMA. In fact CHADEMA wanawake walikuwa ni kama hawapo kabisa. Hii ni nguzo muhimu sana ya uhai wa chama.

      - Na kwenye taarifa ya mtandao wa chama wanasema wana matawi kama 600 Dar es Salaam, na wanachama/wakereketwa 400,000. Sina uhakika na numbers, lakini ni kweli kuwa CCM bado wana mtandao mkubwa wa matawi.

    17. #36
      Endeleaaa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Posts : 560
      Rep Power : 710
      Likes Received
      125
      Likes Given
      43

      Default Re: Mkutano wa CCM Jangwani: CCM yafa Rasmi

      Quote By Ngarenaro View Post
      Acha upotoshaji wakati mwingine si lazima sana kuchambua mambo ya CCM, ambayo ni dhahiri yapo nje ya uwezo wako, ukweli ni kwamba umeupindisha ukweli na umepotosha kwa kiasi kikubwa yale yaliyozungumza kwenye Mkutano wa leo.
      Tuandikie yaliyo sahihi basi, sio kupinga tu.

      Kwa taarifa yako watu tumefuatilia kwa makini, hicho anachosema huyo mdau ni sawa kabisa. CCM has very limited ruling time. hayo tulisikia na kuyaona leo ni dalili tosha kuwa kifo chao kimekaribia kabisa.

      Wameshindwa kuelewa Siasa na Muziki sio mbinu tena kwa sasa. wanamuziki wenyewe wanakuja na playback kuashiria huwa hata hawana maandalizi.

      CCM your Days for rulling this TZ are numbered.
      1. HARNESS THE POWER OF CHANGE, 2. FACE REALITY!, 3. MANAGING LESS IS MANAGING BETTER
      4. CREATE A VISION AND THEN GET OUT OF THE WAY

    18. #37
      Mantuntunu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Posts : 109
      Rep Power : 459
      Likes Received
      9
      Likes Given
      20

      Default Re: Mkutano wa CCM Jangwani : CCM Yafa Rasmi

      Quote By Communist View Post
      Wasira hajui kama kuna viti vinaitwa index. Yeye alikuwa anasoma tarakimu tu. Nyingine zilionyesha kushuka kwa ratio kati yake na ongezeko la idadi ya watu. CCM inakufa.
      CCM ilishakufa zamani

    19. #38
      Ng'wanangwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th August 2010
      Posts : 6,016
      Rep Power : 1656
      Likes Received
      1138
      Likes Given
      419

      Default Re: Mkutano wa CCM Jangwani: CCM yafa Rasmi

      Quote By SEBM View Post




      - Kimsingi ni kama vile tulikuwa kwenye mkutano wa kampeni, kusikiliza ahadi za nini chama kitafanya na wala si nini kimefanywa


      Nukta!
      CCM HAIKUBALIKI ...TUSHIRIKIANE KUITOKOMEZA...

      REST IN PEACE, DR.D.D. HAULE...Wema hawana Maisha

    20. #39
      CHEMPO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th November 2011
      Location : A TOWN
      Posts : 369
      Rep Power : 1936
      Likes Received
      58
      Likes Given
      19

      Default Re: Je haya yaligusiwa ktk mkutano wa ccm leo?

      Ukipewa nauli unaweza uliza?watu walikuwa picnic usiwaze sana hawawezi kuongelea mambo hayo

    21. #40
      Kasimba G's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 19th January 2011
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 917
      Rep Power : 609
      Likes Received
      277
      Likes Given
      265

      Default Re: Mkutano wa CCM Jangwani: CCM yafa Rasmi

      naombea mtizamo wa kiccm uendelee, yaani wizi wao na ufujaji ili walio wavivu wa kufikiri wajue wajibu wao kama waTZ!

    Page 2 of 6 FirstFirst 1234 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...