Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kukodisha Airbus ni mkataba wa kipuuzi - Mwakyembe

    Report Post
    Page 6 of 8 FirstFirst ... 45678 LastLast
    Results 101 to 120 of 147
    1. #1
      Saint Ivuga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Posts : 20,737
      Rep Power : 10180
      Likes Received
      5676
      Likes Given
      12666

      Default Kukodisha Airbus ni mkataba wa kipuuzi - Mwakyembe

      Ni mkataba wa kipuuzi ambao haujawahi kutokea. alonga Mwakyembe .. Mpaka sasa hivi serikali inadaiwa 6.9 billion shillings..
      ndege imekodiwa tumeanza kuilipia ikiwa Hungary hata kabla haijatua
      Last edited by Saint Ivuga; 8th June 2012 at 01:45.

    2. RukaaJuu Final

    3. #101
      mwakajila's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 138
      Rep Power : 387
      Likes Received
      18
      Likes Given
      4

      Default Re: Kukodisha Airbus ni mkataba wa kipuuzi - Mwakyembe

      Quote By Edson
      hivi unajua kwa nini hawa mawaziri wapya wanafumua bodoza wakurugenzi na kusimamisha wa ma CEO kwa kasi namna hii......
      hapana naomba unijuze Edson

    4. #102
      Nyangomboli's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th November 2010
      Location : Mwisenge
      Posts : 887
      Rep Power : 608
      Likes Received
      121
      Likes Given
      4

      Default

      Quote By Precise pangolin
      Huyu mzee wa Ukurutu nimekuwa simwamini tokea aseme kwenye ile ripoti yake ya Richimond kuna mambo ambayo ameficha ili serikali isianguke inamaana alitusaliti sisi wananchi. halafu turudi kwenye mada yeye ni mtaalamu wa mikataba ya kukodisha ndege?
      nakuona kama huna nidhamu na hukufunzwa maadili kwenu. Unajuaje kama hutoweza kupata ugonjwa kama huo ilihali hujamfa? Tumia bongo japo ya kimtaani taani kama hujafunzwa kwenu. Kumbuka humu wanajoin watu wenye bongo zao na si wahuni. Mwacheni Mwakyembe awasaidie kuokoa shirika.

    5. #103
      MESTOD's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th November 2010
      Posts : 2,580
      Rep Power : 949
      Likes Received
      693
      Likes Given
      131

      Default Re: Kukodisha Airbus ni mkataba wa kipuuzi - Mwakyembe

      Tanzania Tanzania, ni kosa gani ulilifanya kwa Mungu hadi uadhibiwe?

    6. #104
      Ulukolokwitanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th September 2010
      Location : ndzengelendete
      Posts : 2,595
      Rep Power : 1071
      Likes Received
      1430
      Likes Given
      261

      Default

      Quote By mwakajila
      ..

      Naomba nikusahihishe kidogo kwanza kabisa mwakyembe hakuenda redioni kama unavyosema pale ni JKIA terminal 2 na alikuwa akiongea na wafanyakazi wa ATCL hapo uwanjani..ulichosikia ni recorded sound ya tukio zima...
      La pili Mwakyembe kamuondoa Chizi si kutokana na kashfa hizo tajwa hapo juu..kashfa hizi ni zile za waliotangulia Chizi kaondolewa kwa sababu uteuzi wake unakinzana na sheria yaani kwa ufupi Uteuzi wako haupo kisheria..
      Ugonile malafyale...
      Kama utaratibu haukufuatwa kwa mtu kukaimishwa yeye kafuata utaratibu gani kumuweka binamu yake Lusajo? Mwakyembe aliugua na kulazwa India kwa karibu miezi 6 na sheria za kazi zinasema miezi mitatu ya kwanza unalipwa mshahara mzima na miezi mitatu inayofuata unapokea nusu mshahara, lakini yeye aliendelea kupokea mshahara wote kwa miezi yote aliyokuwa kitandani hafanyi kazi. Je huu sio ukiukwaji wa sheria. Masuala ya kupiga mikwala kujustify maslahi binafsi watanzania tuyakatae. Hajaeleza mpango wowote wa kuinua shirika zaidi ya longolongo ambazo hazitaleta ndege mpya wala kupunguza wafanyakazi
      trachomatis likes this.

    7. #105
      Precise pangolin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 4th January 2012
      Posts : 5,698
      Rep Power : 1915
      Likes Received
      1596
      Likes Given
      677

      Default Re: Kukodisha Airbus ni mkataba wa kipuuzi - Mwakyembe

      Quote By Nyangomboli
      nakuona kama huna nidhamu na hukufunzwa maadili kwenu. Unajuaje kama hutoweza kupata ugonjwa kama huo ilihali hujamfa? Tumia bongo japo ya kimtaani taani kama hujafunzwa kwenu. Kumbuka humu wanajoin watu wenye bongo zao na si wahuni. Mwacheni Mwakyembe awasaidie kuokoa shirika.
      Sasa kwavile wewe unampenda unataka na mimi niwe upande wako kwani kuwa na bongo ni kumpenda Mwakyembe?
      trachomatis likes this.

    8. Miaka 50

    9. #106
      Prisoner 46664's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th December 2010
      Posts : 1,120
      Rep Power : 651
      Likes Received
      593
      Likes Given
      1564

      Default

      Quote By Kasheshe
      Jamani.... ya Airbus... si basi sasa ... si tuendelee mbele... au ndio hivyo tuchukue hizo ndio deliverables zako Dr. Mwakyembe... kiongozi mzuri ni yule ana-kubali hali halisi aliyoikuta na kuanza na strategy zake....
      Mfano kama nikiwa rais wa hii nchi,halafu nikanyonga watu kama wewe..hata bila kuwasikiliza sana,potelea mbali..bado nitakwenda mbinguni
      Kasheshe and trachomatis like this.

    10. #107
      wikolo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th October 2010
      Posts : 454
      Rep Power : 526
      Likes Received
      131
      Likes Given
      60

      Default Tutaishi na Ufisadi wa Namna Hii Hadi Lini?

      Hebu angalia hapo ambapo wino umekolezwa. Hivi kweli sare moja inunuliwe kwa dola karibu 50,000?

      Mwakyembe alipuka tena



      WAZIRI wa Uchukuzi, Dk. Harison Mwakyembe, ameendelea kuwasha moto ndani ya Shirika la Ndege (ATCL) ambapo jana aliweka bayana sababu kadhaa za kutengua uteuzi wa aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo, Paul Chizi.


      Akizungumza na wafanyakazi wa shirika hilo katika karakana ya uwanja wa ndege jijini Dar es Salaam, Mwakyembe alisema kamwe hawezi kufanya kazi na watendaji wabovu na kuwataka wale walioumizwa na maamuzi yake kuacha kazi mara moja.
      Huku akionyesha kukasirika, waziri huyo aliapa kuendelea kufukuza watendaji wengine zaidi watakaobainika kwenda kinyume na sheria.
      Akitaja sababu zilizomwondoa Chizi, alisema kuwa uteuzi wake haukuzingatia tarartibu za utumishi wa umma.


      “Chizi katika ripoti yake ya uzoefu wa kazi inaonekana kuwa alishastaafu kwa mujibu wa sheria ambapo kwa wafanyakazi wa aina yake kuna taratibu za kuwaajiri, hivyo anatakiwa azifuate ili kuajiriwa tena,” alisema.


      Mbali na hilo, sababu nyingine iliyomponza mkurugenzi huyo ni kuingia mkataba wa kukodi ndege bila ridhaa ya serikali wala wizara husika.


      Hata hivyo, Dk. Mwakyembe alipotakiwa aeleze kwa nini mkurugenzi huyo alifanya hivyo, alisema anaogopa kusema kwani huenda akazidi kuibua mjadala zaidi katika taifa.


      “Inasikitisha sana kuona kuwa ilifika mahali watu wakaona shirika ni mali yao na kufanya maamuzi vile wanavyotaka huku wakisahau kwamba wananchi wanaliangalia shirika hilo linavyouawa,” alisema.


      Alisema kuwa serikali mbali na kutoridhia pia ukodishwaji huo haukufuata taratibu za manunuzi ya umma kwani ndege hiyo ilinunuliwa nchini Liberia ambako bidhaa zote chakavu ‘mikweche’ kama baiskeli, pikipiki na ndege zimekuwa zikipelekwa huko na nchi zilizoendelea.


      Alieleza kukerwa na kitendo cha watendaji wa shirika hilo kujinunulia magari ya kifahari wakati serikali ilitoa fedha ili shirika lifufuke.


      “Maana inashangaza iweje idara na kampuni ndogo zinaweza kujiendesha na kusimama zenyewe lakini ATCL imekuwa ikibebwa hadi leo pamoja na kuwa na wafanyakazi wazuri ambao wakienda kufanya kazi katika makampuni mengine wanafanya vizuri,” alihoji.


      Alisema kuwa serikali inajua wako mawakala wa makampuni ya ndege binafsi, wanaodhani wataiua ATCL kumbe wanajiua wenyewe, na hivyo kuwaonya akisema kama bado wapo ni bora waondoke wenyewe kabla hajawaondosha.


      Alisema yuko tayari kufikishwa mahakamani kwa ajili ya suala hilo kwani wanaofanya hivyo ni sawa na kuchezea sebuleni kwake.


      Akifafanua zaidi madudu ndani ya ATCL, Mwakyembe alisema kuwa fedha za bima ya ndege iliyodondoka mkoani Kigoma takriban dola bilioni saba, tatu za awali zililipwa na iliagizwa ziingizwe katika akaunti ya Shirika Hodhi la Mashirika ya Umma(CHC) lakini watendaji wakafanya kinyume.


      “Watendaji hao hawakufanya hivyo na kuamua kuziingiza katika akaunti ya ATCL, ambapo kati ya fedha hizo tumekuta dola bilioni mbili na dola bilioni moja zilizosalia hazijulikani zilipopelekwa,” aliongeza.


      Waziri huyo aligusia pia hatua ya baadhi ya maafisa kwenda nchini China na kukaa huko takriban siku 45 kwa ajili ya kusimamia sare za wafanyakazi, jambo ambalo alidai ni ufujaji wa fedha za umma kwa kugharamia sare moja dola 49,900.


      Kuhusu ajira ndani ya ATCL, Dk. Mwakyembe alisema kuna waajiriwa wengi waliokwishastaafu na pia ajira mpya zilitolewa bila kufuata tararibu ikiwemo kutangaza nafasi zilizopo ili wenye sifa washindane.


      Alisema kuwa badala yake watu wamekuwa wakipeana ajira hizo kwa kufahamina na kuacha wale walio na sifa, jambo alilodai kuwa walikuwa wameamua kufukuza menejimenti yote, lakini wakahisi wangekosa kumbukumbu za urushwaji ndege.
      “Baada ya kupitia baadhi ya mafaili ya watendaji hao tulikuta mwenye afadhali ni Kaimu Mkurugenzi huyu niliyemteua, Kapteni Lusajo Lazaro,” alisema.


      Aliwaonya wanaozusha kuwa ametumia ukabila kumteua mkurugenzi huyo, akidai kuwa amebebwa na sifa pamoja na uwezo wake kiutendaji.

      Waziri huyo alisema kuwa wameunda tume ambayo anaamini itakuja na majibu mazuri yatakayoliwezesha shirika hilo kusonga mbele.


      Aliwataka wafanyakazi waliobaki, kuchapa kazi ili kumrahisishia pale anapoomba fedha serikalini aeleweke na kuongeza kwamba tayari wameshakabidhiwa sh bilioni 4.9 kutoka hazina kwa ajili ya matengenezo ya ndege.


      Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Shirika hilo aliahidi kuyafanyia kazi yale yote waziri huyo aliyowaagiza, na kutimiza malengo ndani ya miezi mitatu waliyopewa.


      Kwa niaba ya wanafanyakazi hao, Nelson Kalinga, alisema kusuasua kwa ATCL kumechangiwa na serikali kutowasikiliza wafanyakazi, kwani tangu awali walipinga kununuliwa kwa ndege hiyo ya Air Bus, ambapo waliandamana na kuandika barua wizarani lakini hawakusikilizwa.

      Source: Tanzania Daima

    11. #108
      Mnama's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th October 2010
      Posts : 737
      Rep Power : 1163
      Likes Received
      174
      Likes Given
      108

      Default Re: Kukodisha Airbus ni mkataba wa kipuuzi - Mwakyembe

      Natural justice......................

    12. #109
      Mnama's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th October 2010
      Posts : 737
      Rep Power : 1163
      Likes Received
      174
      Likes Given
      108

      Default Re: Kukodisha Airbus ni mkataba wa kipuuzi - Mwakyembe

      Quote By Kichoncho
      mwakyembe anachapa kazi lakini ushauri wake kwa chizi juu ya kupokea malipo ya insurance nje ya account za atcl,hauku-sound ki- professional
      Ha haaa usishangae sana hawa ndio wachakachuaji wenyewe ,hana tofauti na UDA .huo ushauri ulikuwa wa hovyo kabisa kwani dawa ya deni ni kulipa sio kupitisha hela pembeni pembeni.

    13. Aza
      #110
      Aza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd February 2010
      Location : popote
      Posts : 1,421
      Rep Power : 718
      Likes Received
      119
      Likes Given
      263

      Default Re: Kukodisha Airbus ni mkataba wa kipuuzi - Mwakyembe

      tungelikua na mawaziri nusu ktk wizara tulizonazo wenye misimamo na kutetea nchi,tungefika mbali sana sana
      yani nimesikitishwa kwa jinsi hii ATCL na akina chizi walivofanya,jamani ndege hata haijaja watu wamechakachua?ivi tunaitakia nini hii nchi?hawa waliopewa madaraka si watanzania wezetu?wazee ni noma sana kweli nimeamini!!

      na aliyemchagua chizi na wale wakurugenzi nae achunguzwe ana lake jambo si bure,watu wanakula kwa kupitia ATCL
      natamani tu lisiwepo hili shirika sioni sababu linatunyonya tu
      A 'parliament' is not only made up of our dear politicians,but is also a group of owls.
      The greedy people are the victims to the evil people.

    14. #111
      mechard Rwizile's Avatar
      Member Array
      Join Date : 21st September 2011
      Posts : 90
      Rep Power : 406
      Likes Received
      52
      Likes Given
      21

      Default Re: Mwakyembe afunguka

      Quote By sem2708
      Mh.Mwakyembe wewe piga kazi kwa nguvu zote,iga mfano wa mh.magufuli,maadam dhamira yako ni njema hata wapinge namna gani wewe utang'aa tuu! Maombi ya watanzania yanatafuta mtu kama wewe...Mungu anatafuta mtu atakayesimama sehemu iliyobomoka.... hao wanaokupinga ni mafisadi ama wanafaidika na mafisadi.
      endelea mbele mkuu.
      Katika eneo ambalo ninamuunga mkono Rais msaafu wa mwaka 2015 nipale alipomteuwa Dr Harrison Mwakyembe kuwa waziri wa uchukuzi. Ninaamini atatusaidia sana. Kaza uzi.

    15. #112
      Kifimbocheza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th August 2008
      Posts : 345
      Rep Power : 620
      Likes Received
      12
      Likes Given
      0

      Default Re: Kukodisha Airbus ni mkataba wa kipuuzi - Mwakyembe

      Mwakyembe

      Piga kazi achana na hao Wasomi lkn ni Wezi wa Mali za Taifa hili

      Hongera sana na Kaza Buti hivyo2

    16. #113
      Chesty's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th August 2009
      Posts : 1,053
      Rep Power : 705
      Likes Received
      156
      Likes Given
      23

      Default Re: Kukodisha Airbus ni mkataba wa kipuuzi - Mwakyembe

      Quote By mwakajila
      hapana naomba unijuze Edson
      Moja ya sababu ni kutekeleza maagizo ya Kikwete wakati wa kuwateua mawaziri wapya, alisema sasa wanakwenda kuwashughulikia watendaji wa mashirika wanaosababisha mawaziri wa Kikwete kulalamikiwa na kisha kuondolewa.

      Kwa hiyo ni mkakati maalum sio wa kumaliza ufisadi Tanzania bali kulipiza kisasi. CCM na mkulu wake hawana nia ya dhati ya kuung'oa wizi na ubadhirifu kwa sababu ndio unaowastawisha.

    17. #114
      MachoMakavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th February 2008
      Posts : 348
      Rep Power : 646
      Likes Received
      36
      Likes Given
      11

      Default

      Mbona tulishawapigia sana kelele humu hawakuchukua hatua! Hadi Mwakyembe afanye jitihada binafsi!

    18. #115
      MESTOD's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th November 2010
      Posts : 2,580
      Rep Power : 949
      Likes Received
      693
      Likes Given
      131

      Default Re: Kukodisha Airbus ni mkataba wa kipuuzi - Mwakyembe

      Tanzania Tanzania, ni kosa gani ulilifanya kwa Mungu hadi uadhibiwe?

    19. #116
      trachomatis's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th June 2011
      Location : Dar es Salaam,Tanzania.
      Posts : 3,460
      Rep Power : 1095
      Likes Received
      484
      Likes Given
      235

      Default Re: Kukodisha Airbus ni mkataba wa kipuuzi - Mwakyembe

      Kumjudge Mwakyembe kama anayetafuta cheap popularity... Anyways,time will tell...
      Revolution is not an apple that falls when it is ripe... You have to make it fall! [Che Guevara]

    20. #117
      mwakajila's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 138
      Rep Power : 387
      Likes Received
      18
      Likes Given
      4

      Default Re: Kukodisha Airbus ni mkataba wa kipuuzi - Mwakyembe

      Quote By Chesty
      Moja ya sababu ni kutekeleza maagizo ya Kikwete wakati wa kuwateua mawaziri wapya, alisema sasa wanakwenda kuwashughulikia watendaji wa mashirika wanaosababisha mawaziri wa Kikwete kulalamikiwa na kisha kuondolewa.

      Kwa hiyo ni mkakati maalum sio wa kumaliza ufisadi Tanzania bali kulipiza kisasi. CCM na mkulu wake hawana nia ya dhati ya kuung'oa wizi na ubadhirifu kwa sababu ndio unaowastawisha.


      mmmmmh haya kaka

    21. #118
      Safari_ni_Safari's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Location : Kibaruani
      Posts : 12,014
      Rep Power : 24158
      Likes Received
      4735
      Likes Given
      2652

      Default Re: Kukodisha Airbus ni mkataba wa kipuuzi - Mwakyembe

      Quote By Precise pangolin
      Huyu mzee wa Ukurutu nimekuwa simwamini tokea aseme kwenye ile ripoti yake ya Richimond kuna mambo ambayo ameficha ili serikali isianguke inamaana alitusaliti sisi wananchi. halafu turudi kwenye mada yeye ni mtaalamu wa mikataba ya kukodisha ndege?
      Yeye ni mwanasheria......na Mtanzania pia....halafu ndugu lower the tone please!

      Soki Ozali Mwasi Yaka, Soki Ozali Mobali Koya Te


    22. #119
      Precise pangolin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 4th January 2012
      Posts : 5,698
      Rep Power : 1915
      Likes Received
      1596
      Likes Given
      677

      Default Re: Kukodisha Airbus ni mkataba wa kipuuzi - Mwakyembe

      Quote By Safari_ni_Safari
      Yeye ni mwanasheria......na Mtanzania pia....halafu ndugu lower the tone please!
      Nimekuelewa Mkuu
      Safari_ni_Safari likes this.

    23. #120
      davidie's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2011
      Posts : 328
      Rep Power : 450
      Likes Received
      48
      Likes Given
      5

      Default Re: Kukodisha Airbus ni mkataba wa kipuuzi - Mwakyembe

      Quote By edson
      kuondolewa kwa chizi ni kutokana na mikataba mibovu, ajira yake haikufata taratibu au kushindwa kusimamia shirika?

      Hivi mnamwamini mwakyembe??
      unataka tukuamini wewe? Kwa lipi kubwa ulilolifanya? Au hiyo kauli yako ya kupinga kila jambo? Kama rais wako kamuamini na kumpa cheo wewe ni nani? Inawezekana hata mjumbe wa nyumba kumi haujawahi kupewa sasa tukuamini kwa lipi? Acha chokochoko na majungu.

    Page 6 of 8 FirstFirst ... 45678 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...