Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kwanini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

    Report Post
    Page 2 of 4 FirstFirst 1234 LastLast
    Results 21 to 40 of 70
    1. #1
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,892
      Rep Power : 12961
      Likes Received
      4570
      Likes Given
      7577

      Default Kwanini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      1) Sikatai kabisa ATCL ilifanya madudu mengi sana katika nyanja zifuatazo:-

      a) uteuzi wa wakurugenzi waandamizi bila ya kufuata taratibu.

      b) Ukodishaji wa ndege kinyume na utaratibu na kulisababishia taifa hasara za mabilioni.

      Hapa na pale anakuja Waziri Mwakyembe - huyu ni mpya kabisa kutoka dukani - badala ya kuiwajibisha Bodi inayoongozwa na Mustafa Nyang'anyi yeye anawawajibisha watendaji waandamizi kazi ambayo siyo yake ni ya Bodi ya wakurugenzi.

      Mimi nilifikiri waziri shupavu atakachofanya ni kuiondoa Bodi ya wakurugenzi kwa kuhalalisha madudu lakini yeye anairuka Bodi iliyoko ndani ya uwezo wake na kuingilia kwenye majukumu ambayo yako nje ya uwezo wake na kuyafanya! Huu kweli ndiyo utawala bora?

      2) Sikatai kwenye shirika la TBS upo ushahidi wa kutosha wa ya kuwa TBS kufanya madudu makubwa ambayo yameligharimu taifa zaidi ya mabilioni 30.

      Sasa Waziri mpya kabisa naye kanunuliwa kwa bei mbaya kutoka dukani anakuja kuiagiza Bodi ya TBS kumsimamisha kazi Mtendaji Mkuu kwa minajili ya kupisha uchunguzi, kazi ambayo Bodi hiyo walipaswa waifanye na hawakuifanya.

      Kwa lugha nyingine Bodi tajwa imeshindwa kulisimamia shirika tajwa na ndiyo ilipaswa kufanya kazi na imechelea kwa sababu wazijuazo wao. Huu kweli ni utawala bora wa kuacha kuwajibisha chombo kilichoko ndani ya uwezo wa waziri na kuingilia Bodi kwenye majukumu yake?

      Sababu kubwa ya kuziweka Bodi za wakurugenzi ni kupunguza na kufifilisha wanasiasa kuendesha taasisi za umma kwa minajili ya kukidhi mahitaji yao ya muda mfupi ya kisiasa.

      Pamoja na nia nzuri ya kufuta ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka ndani ya taasisi za umma lakini mawaziri hawa wapya wa JK wanapovunja taratibu kwa visingizio kuwa lengo ni kurekebisha makosa siyo sahihi hata kidogo. Huwezi kuvunja sheria na kutumia visingizo vya kuboresha wakati wewe mwenyewe ni mkosaji tu............

      Nionavyo mimi ni kuwa hawa mawaziri wapya wa JK wanawaogopa wenyeviti wa Bodi kwa sababu hawakuwateua wao bali wameteuliwa na Raisi. wanaogopa kuhatarisha posho yao n ahivyo wanzilinda Bodi za wakurugenzi lakini wanaelewa pia ili kuulinda mlo wao lazima wachukue hatua na hivyo kusababisha huu muingiliano wa majukumu ambao unakatzwa na sheria.

      Hivyo badala ya kuwaondoa watajwa hao basi mawaziri wanawaingilia kwa kufanya yale ambayo wao mawaziri wanataka yafanyike kwa sababu zao za kisiasa na hivyo kufifilisha maana nzima ya kuwa na hizi Bodi za wakurugenzi ambazo zinatugharimu mapesa mengi sana katika kuzikarabati.


      Last edited by Rutashubanyuma; 7th June 2012 at 09:03. Reason: additional material
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."


    2. #21
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,892
      Rep Power : 12961
      Likes Received
      4570
      Likes Given
      7577

      Default Re: Kwa nini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      Waziri - KCU amemsimamisha kazi DG wa Bodi ya Pamba wakati ambao msimu unatakiwa kufunguliwa na bei ya pamba kutangazwa. System ime-paralyse hadi waziri mwenyewe anaonekana hajui cha kufanya. Bodi ilitakiwa kuwajibika kwa kushindwa kumwajibisha DG. Hii serikali sasa ndo inazidi kuwa kichekesho. Wasipostuka sijui km watafka 2015.
      @ hivi mwenyekiti wa Bodi unamsimamisha au unamwondoa kwani analindwa na sheria ipi ya ajira?
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    3. #22
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,892
      Rep Power : 12961
      Likes Received
      4570
      Likes Given
      7577

      Default Re: Kwa nini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      Hapo umenena lakini kumbuka Wenyeviti/Wakurugenzi wanateuliwa na Raisi baada ya kushauliana na Waziri wa wizara husika, tatizo linakuja pale uteuzi unakuwa niwa kisiasa kisiasa badala ya kiutendaji na ndiyo maana inakuwa vigumu kwa waziri anayeteuliwa au kuhamishiwa kwenye wizara na kuikuta bodi hiyo ya wakurugenzi ambayo mara nyingi huteuliwa kisiasa kisiasa. Waziri kisheria anakuwa amepewa madaraka ya kuiwajibisha lakini "kisiasa", anakuwa hana hayo madaraka. Hapa ndo tunarudi kwenye tatizo la Raisi kuwa na madaraka makubwa.
      masahihisho kidogo tu...........kuna baadhi ya Bodi mawaziri husika huteua wenyeviti wa bodi na wajumbe wake na kuna baadhi ni Raisi..................lakini hakuna Bodi ambayo Raisi huteua wajumbe wa Bodi hiyo ni kazi ya waziri husika..............
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    4. #23
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,892
      Rep Power : 12961
      Likes Received
      4570
      Likes Given
      7577

      Default Re: Kwa nini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      Nchi yetu inamatatizo makubwa sana kwenye governance kiasa kwamba watu hawaheshimu mipaka ya kazi zao tena. kwa ATCL haina bodi kwani ilishamaliza muda wake na sasa ni zaidi ya mwaka shirika linaendeshwa kimagumashi.
      TBS kulindana kwingi kulianzia waziri hadi bodi kwani wajumbe si kawaweka waziri.

      kinachotakiwa kifanyike kama sekta binafsi kwamba waziri angeteua wajumbe wa bodi kisha miongoni mwao wachague wenyewe mwenyekiti kisha wakabidhiwe shirika na wao ndio wafanye interview ya Mkurugenzi wa shirika(Kama hamna) ambaye atawajibika kwao. sio huu mtindo bodi kaweka waziri mkurugenzi kaweka waziri/raisi nani atawajibika kwa nani? wakurugenzi wanaviburi kwa bodi kama nini maana haijamuweka hapo.
      Mnama kwa kiwango fulani ninaafiki na hoja zako. kkwa maoni yangu badala ya waziri kuteua wajumbe tuangalie washika dau wa kila sekta watusaidie kujichagua kam awadau khalafu majina wampelekee waziri utaratibu uliopo unamlazimisha waziri achague watu kwa kukidhi mahitaji ya kisiasa tu na wala siyo kukidhi mahitaji ya taasisi husika na matokeo yake bodi hushindwa kuzidhibiti menejimenti ambazo hugeuka na kuzitawala Bodi ..............ninaafiki wajumbe wa Bodi wapewe meno ya kuchaguana nafasi ya uenyekiti lakini wajumbe watokane na wadau wa sekta husika kwa kuchaguana kutumia taratibu za wazi na zenye kuheshimu misingi ya demokrasia.........
      Mnama likes this.
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    5. #24
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,892
      Rep Power : 12961
      Likes Received
      4570
      Likes Given
      7577

      Default Re: Kwa nini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      Hivi kwanini taratibu sizibadilishwe ili wenyeviti/ wakurugenzi wa bodi mbali mbali wawe wanateuliwa na mawaziri wa wizara husika ili pindi waziri ama mtendaji anapo vurunda waziri aonekane wazi wazi kufanya kazi..japokua kutakua na kukingiana kifua lakini hii itawamwaga sana watendaji wa mashirika ya umma kwa kutolewa kafara na bodi za wakurugenzi..mazashit!-
      tatizo lipo palepale kwa sababu bado wanasiasa watamshinikiza kuteua mtu wao kwa sababu wanazozijua wao tu.................nionavyo bodi ziundwe na wadau wa sekta husika na kati yao wateue mwenyekiti na hapo nguvu ya wanasiasa kutuyumbisha kupitia uteuzi wa bodi utakuwa umefikia ukomo wake..................
      Mamndenyi likes this.
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    6. #25
      TIMING's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 20,203
      Rep Power : 12279
      Likes Received
      6063
      Likes Given
      6927

      Default Re: Kwa nini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      ulaji......................... ....... wameshapewa hint kwamba ulaji wao unaanzia kwenye bodi za wakurugenzi
      Rutashubanyuma likes this.
      ....Time is the wisest counselor !!!


    7. #26
      Mnama's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th October 2010
      Posts : 758
      Rep Power : 1171
      Likes Received
      180
      Likes Given
      112

      Default Re: Kwa nini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      Jamani eeeeeh Kazi itangazwe, wenye vigezo na uwezo waombe, interview ifanyike,naa aliyefaulu apewe kazi period ! huu umagumashi wa kuteuana ndio longolongo zinaanzia hapo na ubesti,undungunization dinilization na kabilarization na mengineyo yapoleta mushkeli.....

    8. #27
      Tata's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd December 2009
      Posts : 2,375
      Rep Power : 960
      Likes Received
      522
      Likes Given
      333

      Default Re: Kwa nini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      Quote By Ng'wamapalala View Post
      Sikubaliani na wewe kuhusu hili. Kuna mifano mingi tu ambayo inaonyesha kuwa wakati mwingine ni vizuri kuvunja sheria kwa manufaa ya umma katika mazingira yanayohitaji utekelezaji wa haraka ili kujipanga upya badala ya kusubiri taratibu za kisheria ambazo zinachukua muda mrefu kuzikamilisha. Kumbuka sheria zetu mara nyingi ni mbovu na zinahitaji marekebisho( sisemi kama ndiyo excuse) lakini hiyo ni sheria ya hekima na busara katika mazingira kama hayo.
      Huu mtazamo wako kuwa ni halali kuvunja sheria kwa manufaa ya umma ni wa hatari sana kwa manufaa ya umma. Hivi ni nani anatafsiri sahihi ya maslahi ya umma? Je kumwachia waziri mamlaka ya kutafsiri maslahi ya umma kisha kuchukua hatua zinazokwenda kinyume na sheria ni mwelekeo sahihi kwa utawala bora wa nchi? Vipi kama tafsiri yake itakuwa imelenga kumnufaisha yeye na watu wachache wanaomzunguka kuna "checks and balances" zipi?

      Kumbuka hata kwenye kashfa ya Richmond baadhi ya wakubwa walitumia hoja hiyohiyo ya kuvunja sheria kwa manufaa ya umma kumbe umma kwa tafsiri yao ni matumbo yao wenyewe na ya marafiki zao.

      Kwa mtazamo wangu wanachofanya hawa mawaziri ni MICRO MANAGEMENT ya taasisi zilizo chini ya wizara zao kitu ambacho siyo sahihi. Kama kwa mtazamo wao Bodi za Wakurugenzi hazifanyi kazi basi wawajibishwe wajumbe wa bodi na wenyeviti kwa madudu yanayofanyika kwenye taasisi wanazozisimamia. Kama bodi hazijateuliwa ni vyema tukajulishwa ni nini hasa kinachochelewesha uteuzi wa wajumbe na wenyeviti wa bodi hasa kwenye hii wizara ya uchukuzi? Vinginevyo ni bora ikajulikana wazi ikiwa hizi bodi hazihitajiki basi ili zifutwe kabisa na hizi taasisi zirudishwe wizarani.

      NB: Najua mawaziri hawawezi kuwawajibisha wajumbe na wenyeviti wa bodi za taasisi za umma kwa sababu zimeshageuzwa kuwa vijiwe vya viongozi wazee waliokwishastaafu kazi na marafiki wa karibu wa mawaziri wanaowateua.

    9. #28
      Tata's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd December 2009
      Posts : 2,375
      Rep Power : 960
      Likes Received
      522
      Likes Given
      333

      Default Re: Kwa nini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      Quote By Ng'wamapalala View Post
      Sikubaliani na wewe kuhusu hili. Kuna mifano mingi tu ambayo inaonyesha kuwa wakati mwingine ni vizuri kuvunja sheria kwa manufaa ya umma katika mazingira yanayohitaji utekelezaji wa haraka ili kujipanga upya badala ya kusubiri taratibu za kisheria ambazo zinachukua muda mrefu kuzikamilisha. Kumbuka sheria zetu mara nyingi ni mbovu na zinahitaji marekebisho( sisemi kama ndiyo excuse) lakini hiyo ni sheria ya hekima na busara katika mazingira kama hayo.
      Huu mtazamo wako kuwa ni halali kuvunja sheria kwa manufaa ya umma ni wa hatari sana kwa manufaa ya umma. Hivi ni nani anatafsiri sahihi ya maslahi ya umma? Je kumwachia waziri mamlaka ya kutafsiri maslahi ya umma kisha kuchukua hatua zinazokwenda kinyume na sheria ni mwelekeo sahihi kwa utawala bora wa nchi? Vipi kama tafsiri yake itakuwa imelenga kumnufaisha yeye na watu wachache wanaomzunguka kuna "checks and balances" zipi?

      Kumbuka hata kwenye kashfa ya Richmond baadhi ya wakubwa walitumia hoja hiyohiyo ya kuvunja sheria kwa manufaa ya umma kumbe umma kwa tafsiri yao ni matumbo yao wenyewe na ya marafiki zao.

      Kwa mtazamo wangu wanachofanya hawa mawaziri ni MICRO MANAGEMENT ya taasisi zilizo chini ya wizara zao kitu ambacho siyo sahihi. Kama kwa mtazamo wao Bodi za Wakurugenzi hazifanyi kazi basi wawajibishwe wajumbe wa bodi na wenyeviti kwa madudu yanayofanyika kwenye taasisi wanazozisimamia. Kama bodi hazijateuliwa ni vyema tukajulishwa ni nini hasa kinachochelewesha uteuzi wa wajumbe na wenyeviti wa bodi hasa kwenye hii wizara ya uchukuzi? Vinginevyo ni bora ikajulikana wazi ikiwa hizi bodi hazihitajiki basi ili zifutwe kabisa na hizi taasisi zirudishwe wizarani.

      NB: Najua mawaziri hawawezi kuwawajibisha wajumbe na wenyeviti wa bodi za taasisi za umma kwa sababu zimeshageuzwa kuwa vijiwe vya viongozi wazee waliokwishastaafu kazi na marafiki wa karibu wa mawaziri wanaowateua.
      Rutashubanyuma likes this.

    10. #29
      Mzalendo Mkuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2010
      Posts : 569
      Rep Power : 556
      Likes Received
      104
      Likes Given
      288

      Default Re: Kwa nini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      Bro umeonyesha mawazo mazuri yenye nia njema na mlengo wa kimaendeleo. Nimependa hayo. Lakini kuna jambo moja dogo nalo ni kuwa MWENYEKITI WA BOARD huteuliwa na Rais na hivyo Waziri hawezi kumuondoa mwenyekiti. Jambo la msingi ni kuwa Waziri ameanza na wengine wafuate kwa kutekeleza wajibu wao. TUMPONGEZE WAZIRI KWA UJASIRI.
      Rutashubanyuma likes this.

    11. #30
      Elisha Ray's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th March 2012
      Posts : 278
      Rep Power : 421
      Likes Received
      74
      Likes Given
      52

      Default Re: Kwa nini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      Quote By Rutashubanyuma View Post
      1) Sikatai kabisa ATCL ilifanya madudu mengi sana katika nyanja zifuatazo:-

      a) uteuzi wa wakurugenzi waandamizi bila ya kufuata taratibu.

      b) Ukodishaji wa ndege kinyume na utaratibu na kulisababishia taifa hasara za mabilioni.

      Hapa na pale anakuja Waziri Mwakyembe - huyu ni mpya kabisa kutoka dukani - badala ya kuiwajibisha Bodi inayoongozwa na Mustafa Nyang'anyi yeye anawawajibisha watendaji waandamizi kazi ambayo siyo yake ni ya Bodi ya wakurugenzi.

      Mimi nilifikiri waziri shupavu atakachofanya ni kuiondoa Bodi ya wakurugenzi kwa kuhalalisha madudu lakini yeye anairuka Bodi iliyoko ndani ya uwezo wake na kuingilia kwenye majukumu ambayo yako nje ya uwezo wake na kuyafanya! Huu kweli ndiyo utawala bora?

      2) Sikatai kwenye shirika la TBS upo ushahidi wa kutosha wa ya kuwa TBS kufanya madudu makubwa ambayo yameligharimu taifa zaidi ya mabilioni 30.

      Sasa Waziri mpya kabisa naye kanunuliwa kwa bei mbaya kutoka dukani anakuja kuiagiza Bodi ya TBS kumsimamisha kazi Mtendaji Mkuu kwa minajili ya kupisha uchunguzi, kazi ambayo Bodi hiyo walipaswa waifanye na hawakuifanya.

      Kwa lugha nyingine Bodi tajwa imeshindwa kulisimamia shirika tajwa na ndiyo ilipaswa kufanya kazi na imechelea kwa sababu wazijuazo wao. Huu kweli ni utawala bora wa kuacha kuwajibisha chombo kilichoko ndani ya uwezo wa waziri na kuingilia Bodi kwenye majukumu yake?

      Sababu kubwa ya kuziweka Bodi za wakurugenzi ni kupunguza na kufifilisha wanasiasa kuendesha taasisi za umma kwa minajili ya kukidhi mahitaji yao ya muda mfupi ya kisiasa.

      Pamoja na nia nzuri ya kufuta ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka ndani ya taasisi za umma lakini mawaziri hawa wapya wa JK wanapovunja taratibu kwa visingizio kuwa lengo ni kurekebisha makosa siyo sahihi hata kidogo. Huwezi kuvunja sheria na kutumia visingizo vya kuboresha wakati wewe mwenyewe ni mkosaji tu............

      Nionavyo mimi ni kuwa hawa mawaziri wapya wa JK wanawaogopa wenyeviti wa Bodi kwa sababu hawakuwateua wao bali wameteuliwa na Raisi. wanaogopa kuhatarisha posho yao n ahivyo wanzilinda Bodi za wakurugenzi lakini wanaelewa pia ili kuulinda mlo wao lazima wachukue hatua na hivyo kusababisha huu muingiliano wa majukumu ambao unakatzwa na sheria.

      Hivyo badala ya kuwaondoa watajwa hao basi mawaziri wanawaingilia kwa kufanya yale ambayo wao mawaziri wanataka yafanyike kwa sababu zao za kisiasa na hivyo kufifilisha maana nzima ya kuwa na hizi Bodi za wakurugenzi ambazo zinatugharimu mapesa mengi sana katika kuzikarabati.


      ndo walikoambiwa madudu mengi yanafanyika yanayoweza kuwaharibia kazi zao bila wao wenyewe kuharibu.. ndo maana wanabadili na kuweka watu 'wao'. akija mwingine nae atabadilisha vile vile...

    12. #31
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,892
      Rep Power : 12961
      Likes Received
      4570
      Likes Given
      7577

      Default Re: Kwa nini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      Jamani eeeeeh Kazi itangazwe, wenye vigezo na uwezo waombe, interview ifanyike,naa aliyefaulu apewe kazi period ! huu umagumashi wa kuteuana ndio longolongo zinaanzia hapo na ubesti,undungunization dinilization na kabilarization na mengineyo yapoleta mushkeli.....
      Mnama ukoi sahihi tunahitaji kwenye katiba mpya kuweka vigezo vya namna utumishi wa umma utakavyokuwa ukiendesha shughuli zake kwa taratibu za uwazi na shirikishi ili kuondoa upendele o unaotokana na kujuana...........
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    13. #32
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,892
      Rep Power : 12961
      Likes Received
      4570
      Likes Given
      7577

      Default Re: Kwa nini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      Jamani eeeeeh Kazi itangazwe, wenye vigezo na uwezo waombe, interview ifanyike,naa aliyefaulu apewe kazi period ! huu umagumashi wa kuteuana ndio longolongo zinaanzia hapo na ubesti,undungunization dinilization na kabilarization na mengineyo yapoleta mushkeli.....
      serikali imekuwa kama shamba la bibi, vile..lol
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    14. #33
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,892
      Rep Power : 12961
      Likes Received
      4570
      Likes Given
      7577

      Default Re: Kwa nini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      Bro umeonyesha mawazo mazuri yenye nia njema na mlengo wa kimaendeleo. Nimependa hayo. Lakini kuna jambo moja dogo nalo ni kuwa MWENYEKITI WA BOARD huteuliwa na Rais na hivyo Waziri hawezi kumuondoa mwenyekiti. Jambo la msingi ni kuwa Waziri ameanza na wengine wafuate kwa kutekeleza wajibu wao. TUMPONGEZE WAZIRI KWA UJASIRI.
      MZALENDO MKUU 2 mimi nachelea kumpongeza waziri kwa kutotumia bodi yake ifanye kazi hata kama muda umeisha alipaswa aiongezee muda hadi nyingineyo itakapoteuliwa................ ........asitumie loopholes kufanya atakavyo...........
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    15. #34
      Njowepo's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 26th February 2008
      Location : Santiago
      Posts : 7,779
      Rep Power : 22095
      Likes Received
      1044
      Likes Given
      857

      Default Re: Kwa nini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      Hayo ndo madhara ya kumrundikia raisi madaraka!
      Imagine bodi zote zilizopo yeye kateua ivi atakuwa na umakini gani kama sio kuvurunda tuu ktk uteuzi ofcourse excluding zama za Nyerere
      WB Tanzania lead economist Jacques Morisset said the GDP doubled in 10 years, but it has failed to produce any significant decline in poverty levels.

    16. #35
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,892
      Rep Power : 12961
      Likes Received
      4570
      Likes Given
      7577

      Default Re: Kwa nini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      Huu mtazamo wako kuwa ni halali kuvunja sheria kwa manufaa ya umma ni wa hatari sana kwa manufaa ya umma. Hivi ni nani anatafsiri sahihi ya maslahi ya umma? Je kumwachia waziri mamlaka ya kutafsiri maslahi ya umma kisha kuchukua hatua zinazokwenda kinyume na sheria ni mwelekeo sahihi kwa utawala bora wa nchi? Vipi kama tafsiri yake itakuwa imelenga kumnufaisha yeye na watu wachache wanaomzunguka kuna "checks and balances" zipi?

      Kumbuka hata kwenye kashfa ya Richmond baadhi ya wakubwa walitumia hoja hiyohiyo ya kuvunja sheria kwa manufaa ya umma kumbe umma kwa tafsiri yao ni matumbo yao wenyewe na ya marafiki zao.

      Kwa mtazamo wangu wanachofanya hawa mawaziri ni MICRO MANAGEMENT ya taasisi zilizo chini ya wizara zao kitu ambacho siyo sahihi. Kama kwa mtazamo wao Bodi za Wakurugenzi hazifanyi kazi basi wawajibishwe wajumbe wa bodi na wenyeviti kwa madudu yanayofanyika kwenye taasisi wanazozisimamia. Kama bodi hazijateuliwa ni vyema tukajulishwa ni nini hasa kinachochelewesha uteuzi wa wajumbe na wenyeviti wa bodi hasa kwenye hii wizara ya uchukuzi? Vinginevyo ni bora ikajulikana wazi ikiwa hizi bodi hazihitajiki basi ili zifutwe kabisa na hizi taasisi zirudishwe wizarani.

      NB: Najua mawaziri hawawezi kuwawajibisha wajumbe na wenyeviti wa bodi za taasisi za umma kwa sababu zimeshageuzwa kuwa vijiwe vya viongozi wazee waliokwishastaafu kazi na marafiki wa karibu wa mawaziri wanaowateua.
      Tata uko sahihi hakuna aliyejuu ya sheria........................ .waziri anayekaidi sheria analenga kuleta vurugu na upendeleo sehemu ya kazi kwa manufaa yake binafsi tu...........hakuna utaifa kwa yeyote anayejichukulia sheria mkononi.........
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    17. #36
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,892
      Rep Power : 12961
      Likes Received
      4570
      Likes Given
      7577

      Default Re: Kwa nini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      Hayo ndo madhara ya kumrundikia raisi madaraka!
      Imagine bodi zote zilizopo yeye kateua ivi atakuwa na umakini gani kama sio kuvurunda tuu ktk uteuzi ofcourse excluding zama za Nyerere
      Njowepo uko kwenye mstari hapo.............katiba mpya kama itakuwepo basi haya majeraha inabidi iyatibu..........
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    18. #37
      Precise pangolin's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 4th January 2012
      Posts : 5,761
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1609
      Likes Given
      684

      Default Re: Kwanini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      Ndio kwenye ulaji

    19. #38
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,892
      Rep Power : 12961
      Likes Received
      4570
      Likes Given
      7577

      Default Re: Kwa nini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      ulaji......................... ....... wameshapewa hint kwamba ulaji wao unaanzia kwenye bodi za wakurugenzi
      TIMING Bodi za wakurugenzi zimekuwa ni nafasi nyingine ya wanasiasa kujaza wapambe zao na hata mahawala hujazwa huko wakapate mshiko wa kulea familia zao...........
      TIMING likes this.
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    20. #39
      Njowepo's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 26th February 2008
      Location : Santiago
      Posts : 7,779
      Rep Power : 22095
      Likes Received
      1044
      Likes Given
      857

      Default Re: Kwanini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      Ebu imagine mtu kama Msekwa yuko kwenye sijui bodi gani sijui ila nijuacho iyo bodi inadeal na utalii!
      HUyu mtu toka miaka ya 1960 yuko serikalini ana kipi kipya mpaka anaendelea kuwemo.
      Ukifuatilia sana bodi ni kwa ajili ya kulipana fadhira na vijiwe vy washikaji wa mkuu wa nchi
      WB Tanzania lead economist Jacques Morisset said the GDP doubled in 10 years, but it has failed to produce any significant decline in poverty levels.

    21. #40
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,892
      Rep Power : 12961
      Likes Received
      4570
      Likes Given
      7577

      Default Re: Kwa nini mawaziri wapya wa JK wanaingilia Bodi za wakurugenzi?

      ulaji......................... ....... wameshapewa hint kwamba ulaji wao unaanzia kwenye bodi za wakurugenzi
      tunakazi kubwa katika kuirekebisha nchi hii.....................tujiki te katika kuangalia kwa makini mfumo mzima wa uendeshaji nchi badala ya kuwa watumwa wa vyama vya siasa...............
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    Page 2 of 4 FirstFirst 1234 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...