Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Chadema wamnyemelea mbunge CUF; Lema amshangaa Membe

    Report Post
    Results 1 to 19 of 19
    1. #1
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,204
      Rep Power : 3555
      Likes Received
      3055
      Likes Given
      462

      Default Chadema wamnyemelea mbunge CUF; Lema amshangaa Membe


      Wednesday, 06 June 2012 21:15

      Geofrey Nyang’oro

      CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) jana kilizindua vuguvugu la mabadiliko (M4C) katika Mkoa wa Lindi huku kikimtaka Mbunge wa Jimbo la Lindi Mjini (CUF), Salum Barwani kujiunga na chama hicho.
      Katika siku hiyo ya kwanza, Chadema kilimnasa aliyekuwa meneja wa kampeni wa mbunge huyo, Abdallah Madebe.


      Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema mbunge huyo kwa sasa na wabunge wenzake wa CUF wamekuwa hawana sauti ya kutetea wananchi ndani ya Bunge kwa kuwa uongozi wa juu wa chama hicho umeungana na CCM.


      Mbowe alimkaribisha mbunge huyo baada ya wananchi wa Kata ya Nng’apa, kusema Barwani amefuatilia baadhi ya malalamiko yao ya muda mrefu lakini, juhudi zake zinakwamishwa na Mkuu wa Mkoa wa Lindi na madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi.


      Malalamiko mengine ya wananchi hao yalikuwa mfumuko wa bei, kukosa huduma za afya na wanafunzi kutozwa Sh20,000 kwa ajili ya ulinzi wa shule za Serikali.


      Mkazi wa Kata ya Ng’apa, Rashid Issa alimweleza Mbowe katika mkutano huo kuwa hajui hatima ya maisha yao kutokana na mfumuko wa bei unaojitokeza kila wakati huku wakiendelea kutozwa kodi katika vivuko vya mazao na fedha hizo kuishia mikononi mwa wajanja.

      Akijibu hoja hizo, Mbowe alisema maisha magumu kwa Watanzania ni matokeo ya sera mbovu za Serikali ya CCM katika kusimamia uchumi wa nchi.

      Akimzungumzia Barwani, Mbowe alisema katika mazingira ya sasa ya CUF, mbunge huyo hatakuwa na uwezo wa kuwasaidia wananchi kwa sababu viongozi wa juu wa chama hicho, akiwamo Mwenyekiti, Profesa Ibrahim Lipumba na Katibu Mkuu, Seif Sharif Hamad ndiyo wanaofanya uamuzi na ‘wamekiunganisha’ chama hicho na CCM.


      “Sina ugomvi na Barwani, ni mbunge na tunafanya naye kazi vizuri, tatizo ni misimamo ya viongozi wake wakuu. Hawa ni tatizo kwake. Ninamshauri ajitathmini na huku kwetu mlango uko wazi, anaweza kuusukuma na kuingia kwa ajili ya kuwatetea wana Lindi,” alisema Mbowe.

      Mbowe aliwataka wakazi wa Lindi kutowavumilia viongozi wazembe ambao hawawezi kuwaelezea kodi zao zimetumika vipi, wakati wao wanashindwa kupata huduma za msingi.

      Slaa na polisi
      Akizungumza katika mkutano uliofanyika katika Uwanja wa Ilulu mjini hapa, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa aliwataka polisi wasipate tabu ya kurekodi mikutano yao, bali fedha wanazonunulia kanda za kurekodia wazitumie kuboresha maisha yao.

      Dk Slaa alidai kwamba katika mikutano ya Chadema, askari wamekuwa wakijaa kwa wingi kwa lengo la kusikiliza yanayozungumzwa ili wawafikishie mabosi wao.

      “Ninyi askari mnanishangaza sana ufisadi umejaa kila sehemu, badala ya kushughulika nao ninyi mnakuja kurekodi ili mseme tunachochea vurugu...” alisema Dk Slaa.Alisema atakachoweza kuwasaidia askari ni kuhakikisha kuwa mishahara yao inaongezwa baada ya mwezi wa saba.

      Lema amshangaa Membe
      Kwa upande wake, aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alisema Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa, Bernard Membe amepoteza sifa ya kufikiria kuwa kiongozi wa nchi kutokana na kushindwa kuusaidia Mkoa wa Lindi kuondokana na umaskini.

      Alisema kama Membe angekuwa kiongozi makini, angetumia fursa yake ya kusafiri nje kila wakati kutangaza vivutio vya Mkoa wa Lindi na kuufanya uwe mji wa kitalii kama mikoa mingine inayosifika kwa utalii Tanzania.

      Mnyika awashtukia wabunge CCM
      Mbunge wa Ubungo, John Mnyika alisema kama Rais Jakaya Kikwete asipopeleka bajeti yenye kupunguza mfumuko wa bei katika Bunge lijalo, Chadema itahamasisha nguvu ya umma kumshinikiza afanye hivyo.
      Alisema kauli inayotolewa na wabunge wa CCM kuwa wataigomea Bajeti ijayo ni ya kujikosha mbele ya jamii kwa kuwa wanajua wazi kuwa hilo haliwezekani kulingana na katiba waliyonayo.

      “Hawa wanasema wataipinga Bajeti wakati wana hamu ya kupokea posho za bungeni mbona wanajidanganya kwa kuwa wakifanya hivyo Rais atavunja Bunge na kwa hofu ya matendo yao, wengi wanajua hawataweza kurudi hivyo hizo ni propaganda tu,” alisema Mnyika.

      Sugu na ajira za vijana
      Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Sugu) alisema wakati anaelekea Mtwara akiwa ndani ya ndege alijua mikoa hiyo ya kusini ni ya kupigiwa mfano kutokana na aina ya watu aliokuwa nao katika ndege, kwamba hata vijana wa Mkoa wa Lindi watakuwa wananufaika na rasilimali za mkoa huo.

      “Nilipotua nikawauliza kama vijana mnanufaika na gesi inayopatikana katika mikoa yenu? Cha ajabu mnaniambia kuwa mnachopata ni vifaa vya kukingia kifua tu.”

    2. Miaka 50

    3. #2
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,204
      Rep Power : 3555
      Likes Received
      3055
      Likes Given
      462

      Default Re: Chadema wamnyemelea mbunge CUF; Lema amshangaa Membe

      Hadi Lindi.... Mmm Mama Salma yuko wapi? Oh Anasubiri 2012 au 2013 kugombea U-NEC?

      Barwani wa CUF ni Msafi anafaa CHADEMA sio CHENGE

    4. #3
      democratic's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st November 2011
      Posts : 1,602
      Rep Power : 819
      Likes Received
      278
      Likes Given
      52

      Default Re: Chadema wamnyemelea mbunge CUF; Lema amshangaa Membe

      ccm plus cuf is equal to sisiemu bii

    5. #4
      Puppy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th October 2011
      Posts : 1,477
      Rep Power : 680
      Likes Received
      360
      Likes Given
      53

      Default Re: Chadema wamnyemelea mbunge CUF; Lema amshangaa Membe

      Who Unleashed The Dragon???

      CCM Mtajuta kumpokonya Lema majukumu na kumwacha Huru, atawabomoa kinoma

    6. #5
      mechard Rwizile's Avatar
      Member Array
      Join Date : 21st September 2011
      Posts : 90
      Rep Power : 405
      Likes Received
      52
      Likes Given
      21

      Default Re: Chadema wamnyemelea mbunge CUF; Lema amshangaa Membe

      Kwa sasa kila mbunge makini katika CCM,CUF na NCCR mageuzi anatakiwa kujiandaa na kuwaandaa wanachama wake kisaikolojia kuhamia Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( CHADEMA ) ili katika uchaguzi wa mwaka 2015 waweze kuchaguliwa. Na chama hicho kushinda uchaguzi kwa kuiangusha CCM. Inabidi wote tufanye hivyo ili kuanza hatua ya ukombozi.

      CCM ikianguka tutakuwa kumetoa funzo moja kubwa sana; kwamba chama chochote kitakachokuwa kimechaguliwa kiwe makini kutekeleza ahadi zake,vinginevyo kitapigwa chini katika uchaguzi unaofuata.

      Katika chaguzi zilizotangulia hasa kuanzia mwaka 1995, CCM kimekuwa kiomba huruma ya wapiga kura kwa madai kuwa kitajirekebisha, baada ya kuonewa huruma na kuchaguliwa kinageuka na kuanza kusema sera zetu zinakubalika na wapinga kura wana imani nacho.

      Sasa wakati umefika wa ndama kurejea kwa mama yake. Mheshimiwa Baruan upo hapo! Mheshimiwa Kafulila upo? Mheshimiwa Mkosamali unasikia, Mheshimiwa Mwakyembe unasikia? Tafakari na chukua hatua.

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      Shardcole's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 15th January 2012
      Posts : 4,393
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1032
      Likes Given
      4

      Default Re: Chadema wamnyemelea mbunge CUF; Lema amshangaa Membe

      Peoples..........

    9. #7
      tara's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 5th June 2012
      Posts : 188
      Rep Power : 388
      Likes Received
      61
      Likes Given
      96

      Default Re: Chadema wamnyemelea mbunge CUF; Lema amshangaa Membe

      Imenikumbusha ishu ya Kagawa na Sir Alex furguson.........

    10. #8
      mwigo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 8th May 2012
      Posts : 45
      Rep Power : 364
      Likes Received
      15
      Likes Given
      14

      Default Re: Chadema wamnyemelea mbunge CUF; Lema amshangaa Membe

      slaa amepopolewa alipo anza kumzushia MTATIRO huko nanyumbu, nasasa mmeishiwa kabisa na sera za kuzungumza, kilicho baki ni CUF CUF CUF, HMNA JIPYA NYIE CUF KIBOKO YENU, kila kitu mna kazi ya kuiga tu.

    11. #9
      Shembago's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th August 2011
      Posts : 294
      Rep Power : 450
      Likes Received
      41
      Likes Given
      26

      Default Re: Chadema wamnyemelea mbunge CUF; Lema amshangaa Membe

      Kazi bado inaendelea hitimisho kuchukua Nchi 2015

    12. #10
      asigwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2011
      Location : TANDHANIYA
      Posts : 4,388
      Rep Power : 1264
      Likes Received
      1208
      Likes Given
      1253

      Default Re: Chadema wamnyemelea mbunge CUF; Lema amshangaa Membe

      Quote By mwigo
      slaa amepopolewa alipo anza kumzushia mtatiro huko nanyumbu, nasasa mmeishiwa kabisa na sera za kuzungumza, kilicho baki ni cuf cuf cuf, hmna jipya nyie cuf kiboko yenu, kila kitu mna kazi ya kuiga tu.
      gamba at work for his daily bread

    13. #11
      mtotowamjini's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd April 2012
      Location : None of Your Business
      Posts : 4,532
      Rep Power : 1263
      Likes Received
      1109
      Likes Given
      28

      Default Re: Chadema wamnyemelea mbunge CUF; Lema amshangaa Membe

      nawaonea huruma mawaziri na bajeti zao za mwaka huu...maana akina zitto lazima walianzishe huko bungeni
      Every saint has a past, every sinner has a future' ...Oscar Wilde

      One man's good fortune is another man's misfortune


    14. #12
      Filipo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Location : Kiding'a
      Posts : 6,349
      Rep Power : 18614
      Likes Received
      3508
      Likes Given
      1612

      Default

      Quote By mwigo
      slaa amepopolewa alipo anza kumzushia MTATIRO huko nanyumbu, nasasa mmeishiwa kabisa na sera za kuzungumza, kilicho baki ni CUF CUF CUF, HMNA JIPYA NYIE CUF KIBOKO YENU, kila kitu mna kazi ya kuiga tu.
      Mbona sijaona mahali Dr (PhD) Slaa amezungumza habari ya cuf!? Ngoja nitafute miwani!

    15. #13
      mwigo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 8th May 2012
      Posts : 45
      Rep Power : 364
      Likes Received
      15
      Likes Given
      14

      Default Re: Chadema wamnyemelea mbunge CUF; Lema amshangaa Membe

      Quote By Filipo
      Mbona sijaona mahali Dr (PhD) Slaa amezungumza habari ya cuf!? Ngoja nitafute miwani!
      ULIZA UAMBIWE kila koner issue ni CUF badala wazungumzie matatizo ya watu wa kusini. hata yeye atakueleza. na operasion yao imeishia leo baada ya wakati mgumuuuuuuuuuuuu

    16. #14
      mwigo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 8th May 2012
      Posts : 45
      Rep Power : 364
      Likes Received
      15
      Likes Given
      14

      Default Re: Chadema wamnyemelea mbunge CUF; Lema amshangaa Membe

      Quote By asigwa
      gamba at work for his daily bread
      inakula kwenu hiyo maana baadaya kukosa mtu wa kuwapa mambo ya kuongea mmemukosa sasa mnabaki kukashifu vyama vya wenzenu tu, hamadi ndio alikuwa anawapa mambo ya kuhusu ufisadi sasa kafukuzwa hamna jipya tuone kama mtatoa, mtaishia hivo hivo tuuuuuuuuuu. hata penye ukweli mnapinga haoooooooooooooo

    17. #15
      Mr. Bigman's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th May 2011
      Posts : 573
      Rep Power : 624
      Likes Received
      103
      Likes Given
      57

      Default

      Quote By nngu007
      Hadi Lindi.... Mmm Mama Salma yuko wapi? Oh Anasubiri 2012 au 2013 kugombea U-NEC?

      Barwani wa CUF ni Msafi anafaa CHADEMA sio CHENGE
      Barwani aje Cdm,Lindi Municipal itapaa
      nngu007 likes this.

    18. #16
      asigwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2011
      Location : TANDHANIYA
      Posts : 4,388
      Rep Power : 1264
      Likes Received
      1208
      Likes Given
      1253

      Default Re: Chadema wamnyemelea mbunge CUF; Lema amshangaa Membe

      Quote By mwigo
      inakula kwenu hiyo maana baadaya kukosa mtu wa kuwapa mambo ya kuongea mmemukosa sasa mnabaki kukashifu vyama vya wenzenu tu, hamadi ndio alikuwa anawapa mambo ya kuhusu ufisadi sasa kafukuzwa hamna jipya tuone kama mtatoa, mtaishia hivo hivo tuuuuuuuuuu. hata penye ukweli mnapinga haoooooooooooooo
      maneno yako kama ya kwenye kanga za mipasho zinazouzwa pale mataa wa kongo...
      CHADEMA NI CHAMA MAKINI sana..na sa izi tumevamia KUSINI sasa nyie na SPOUSESwenu CUF inabidi mfe pamoja si au mtatumia ile kauli yenu ya "KUTOTENGANA MPAKA KIFO KIWATENGANISHE??"

    19. #17
      Mr. Bigman's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th May 2011
      Posts : 573
      Rep Power : 624
      Likes Received
      103
      Likes Given
      57

      Default

      Quote By mwigo
      ULIZA UAMBIWE kila koner issue ni CUF badala wazungumzie matatizo ya watu wa kusini. hata yeye atakueleza. na operasion yao imeishia leo baada ya wakati mgumuuuuuuuuuuuu
      Hii huja wakati magamba na jamaa zao yanapopata moto!

    20. #18
      Comi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd October 2011
      Posts : 962
      Rep Power : 578
      Likes Received
      156
      Likes Given
      2

      Default Re: Chadema wamnyemelea mbunge CUF; Lema amshangaa Membe

      Kama barca vile

    21. #19
      Noboka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th November 2011
      Posts : 493
      Rep Power : 2248
      Likes Received
      153
      Likes Given
      23

      Default Re: Chadema wamnyemelea mbunge CUF; Lema amshangaa Membe

      “Nilipotua nikawauliza kama vijana mnanufaika na gesi inayopatikana katika mikoa yenu? Cha ajabu mnaniambia kuwa mnachopata ni vifaa vya kukingia kifua tu.”
      Sugu anakufanya ufikiri hasa, nakumbuka hata lile suala la Twiga alivyomuuliza Maige awaeleze aliwezaje kumuingiza Twiga na ulefu wote kwenye ndege!
      Kwa watu wa kusini huu ni wakati wao kukombolewa, kila la kheri kwao!

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...