Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muungano

    Report Post
    Page 3 of 17 FirstFirst 1234513 ... LastLast
    Results 41 to 60 of 334
    1. #1
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,520
      Rep Power : 46715
      Likes Received
      16435
      Likes Given
      8471

      Default Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muungano



      Msitunyonye bana nyie! Msitunyonye mnatudhiri! Tuachaneni angalau tujikung’ute kidogo! Tumekuwa mafukara; mtu mwenye miaka kumi na tatu amepinda mgongo kama mtu wa miaka sabini na tano! … tunachotaka sasa hivi mtuachie tupumue!
      – Mhadhara wa Uamsho Zanzibar Machi 4, 2012.


      Nimekuwa mtetezi wa Muungano kiasi kwamba nimegundua nimebakia peke yangu. Wengine wanautetea Muungano kwa kutumia vitisho na wengine wanautetea kwa kutumia dharau. Binafsi ninaamini muungano unaweza kutetewa kwa hoja maridhiwa zenye kuonesha kuwa Zanzibar na wananchi wa Zanzibar wananufaika na wataendelea kunufaika zaidi katika Muungano kuliko nje ya Muungano. Kwamba hoja za kupinga muungano kwa madai kuwa Wazanzibari wanaonewa na kuwa Zanzibar inakaliwa kama koloni na Tanganyika haina mshiko, ni ya kupuuza na ina uwezo wa kuteka akili za watu wasiotaka kufikiria.


      Baada ya muda mrefu kuwa mtetezi pekee wa Muungano kelele za hivi karibuni zimenibadili kabisa mawazo yangu na sasa nimekuwa na nitaendelea kushakizia muungano uvunjwe ili wale wanaoitaka Zanzibar yao wapewe na ili watu wa bara tuhangaike mambo mengine kuliko kuonekana tunawakandamiza Wazanzibari. Ile hofu ya Mwalimu kiasi cha kuachilia mambo mengi ya Zanzibar kuwa tukiungana kuwa nchi moja kamili kabisa Zanzibar watajiona wamemezwa imetimia kwani pamoja na kuwapa kila kitu Zanzibar bado wapo ambao wanaona wanamezwa!


      Ni kutokana na ukweli huu kwamba hakuna kiongozi au mwanasiasa wa Tanzania awe mzee au kijana mwenye uwezo wa kuutetea Muungano kisomi na kisiasa na kuwapinga wenye hoja dhaifu ndio maana leo naendelea na hoja yangu ya kuwasaidia Wazanzibar watoke kwenye Muungano, wawe na nchi na taifa lao na zaidi ya yote waweze baada ya kutoka kwenye Muungano kuanza mahusiano mapya na bara kama nchi mbili zilizo sawa. Ninaamini tunaweza kuhusiana vizuri zaidi baada ya Zanzibar kutoka na kuwa taifa lao wenyewe kuliko ilivyo hivi sasa ambapo Muungano hauteteleki – zaidi ya kutumia vitisho vya dola.


      Tunawapenda sana ndugu zetu Wazanzibari kiasi kwamba hatutaki kuwang’ang’ania. Wapo kwao wenye kutuchukia sana kiasi kwamba hawataki hata kufikiria sisi ni ndugu zao. Wanatuangalia kwa dharau na kebeki wao wakiamini utukufu wao wa “Zanzibar” isiyokuwepo ndiyo tunu waliyonayo. Ukiwaskiliza sana baadhi ya wapinga muungano kwa kweli kabisa wamejawa chuki isiyo na kifani na chuki hiyo imezaa matunda meusi katika madhihirisho ya chuki dhidi ya watu wa Bara na Wakristu.


      Lakini kitu kimoja ambacho watu wengi hawataki kukifikiria ni kuwa hawa watu wanaopinga Muungano wao wanadai “nchi”. Sasa hakuna aliyewauliza kwamba mbona katiba ya Zanzibar imefanyiwa mabadiliko na kuitangaza kuwa Zanzibar ni nchi? Sasa kama tayari Zanzibar ni nchi wanachodai hawa ni nini? Haiwezekani kuwa wanachodai ni nchi kwani nchi tayari wanayo na Katiba ya Zanzibar inasema hivyo! Wanachotaka siyo nchi! Wanachotaka ni kuwa nje ya Muungano! Hivi ni vitu viwili tofauti.


      Ndio maana basi katika makala ya leo nataka kuwasaidia Wazanzibari hawa na wale ambao wanaamini kuwa muungano haustahili kuteteewa kwa hoja bali kwa vioja. Pendekezo langu ni njia nyepesi za Wazanzibari kujiondoa kwenye Muungano bila kufanya maandamano, mihadhara wala kuwashtumu watu wa Tanganyika. Wazanzibari wakitaka kutoka kweli kwenye Muungano wanaweza kufanya hivyo ndani ya wiki chache tu na wakawa nchi. Nina uhakika serikali ya Muungano haitotumia nguvu kuwalazimisha kubakia! Nyerere mwenyewe alishasema kuwa hawezi kuwalazimisha Wazanzibari kubakia kwenye Muungano.


      Njia ya kwanza
      Njia ya kwanza na nyepesi zaidi ya kuweza kujitoa kwenye Muungano ni kwa wananchi wa Zanzibar wakiongozwa na hawa wana- uamsho wawatake watendaji wote wa Muungano wenye asili ya Zanzibar kuachia nafasi zao mara moja na kurudi Zanzibar!


      Hii ni pamoja na majaji, wabunge, mawaziri, maafisa wa polisi na vyombo vingine vya usalama, na wantedaji wengine ambao wako kwenye Muungano. Badala ya kuililia Tanganyika kila kukicha kuwa inawabana mashehe wa Zanzibari wenye kuongoza vuguvugu la kutoka kwenye Muungano waanzishe mihadhara ya kuwataka Wazanzibari wenzao ambao wanatumikia Muungano waachilie nafasi hizo.


      Binafsi ningependekeza kama wataniruhusu waanzishe harakati hizo ili viongozi wote hawa waachilie nafasi zo ifikapo Disemba 10, 2012. Hii ni pamoja na Makamu wa Rais Ghaib Bilal, jaji mkuu na wengine.
      Hawa wote wakishawishiwa kuondoka Wazanzibari wajiandae ama kuwapatia pensheni au kuwatafutia nafasi kwenye serikali ya nchi ya Zanzibar.


      Sasa hawa wote wakikubali kuondoka kwenye nafasi zao za Muungano Zanzibar itapata wataalamu wengine wengi ambao wamekuwa wakitumikia Muungano na hivyo kujiongezea hazina ya wataalamu mbalimbali. Lakini pia itafungua ajira za Watanganyika wengi ambao wangeweza kushika nafasi zinazoshikiliwa na Wazanzibari hasa kwa vile Wazanzibari hao wako kimya na hawajitokezi kuutetea Muungano ambao wanautumikia.


      Pamoja na kuwataka viongozi wao na watendaji mbalimbali watoke kwenye Muungano katika harakati za mwanzo za Zanzibar kujitenga wana uamsho hawastahili kulalamikia Watanganyika. Hawahitaji kuendelea kuwaghilibu vijana wa Kizanzibari kuwa inanyonywa na sasa wanahitaji kupumua. Mashehe wa uamsho waende mbali zaidi katik akudai nchi yao. Waanze kuwahamasisha Wazanzibari walioko bara kuamua kuondoka bara na kurudi Zanzibar ili kuendesha shughuli zao huko.


      Watu kama kina Bakheresa wenye biashara kubwa bara itabidi watiwe hamasa waamue kuondoka bara. Siyo hawa tu bali pia wale Wapemba na Wazanzibari waliona maeneo ya ardhi Bara. Hivi ndivyo ilivyotokea Sudan ya Kusini ambapo baada ya nchi hiyo kujitenga Wasudan ya Kusini waliokuwa wanafanya kazi Khartoum waliacha kazi zao na wengi wao wameamua kurudi kwenye nchi yao kuanza kuijenga.


      Wengi tunakumbuka kuwa baada ya Rwanda chini ya Kagame kutulia kwa kiasi Wanyarwanda wengi ambao wengine waliishi kama Watanzania waliacha kazi zao na kurudi kwao Rwanda kuijenga nchi y ao. Nakumbuka baadhi ya wahadhiri kwenye taasisi mbalimbali nchini ambao tuliwadhania ni Wahaya au Waangaza walipoamua kuacha kazi zao kumbe walikuwa ni Wanyarwanda.


      Hili pia litakuwa na faida kubwa sana kwa Zanzibar kwani itapata watu wengi zaidi wenye uwezo na utajiri mkubwa na vile vile itabidi iwaandalie viwanja vipya vya kilimo na makazi maana vile vya bara itabidi waviachilie kuwapisha Watanganyika ambao wanalalamikia kukosa ardhi au kupatiwa ardhi isiy nzuri. Na pia wafanyabiashara hao wa Kizanzibari watakaporudi Zanzibar na kama watataka kuja kufanya biashara Tanganyika itabidi waje kama wawekezaji na hivyo watasaidia katika ukuaji wa uchumi wa Tanganyika kama wageni wengine. Na kama watakuwa wajanja kama wageni wengine wanaweza kutengeneza mamilioni zaidi kuliko wanavyofanya sasa kama raia wa Tanzania!


      Hivyo hilo ni jjambo la kwanza nawashauri wana uamsho; hamasisheni Wazanzibari waondoke Tanzania bara ili warudi Zanzibar ambako watapatiwa nafasi bora zaidi za ajira. Mtakapofanya hivyo, na watu wa Bara nao itabidi waanze kuondoka Zanzibar japo hapo nina uhakika kutakuwa na kazi kidogo. Watu wa Bara ni kina nani Zanzibar?


      Njia ya pili
      Kuna maneno na kauli za baadhi ya watu wachache wakizungumza kana kwamba wanawakilisha "wengi". Utasikia mtu anayepinga Muungano anasema,"Wazanzibari hatuutaki Muungano" na wakati mwingine kudai "Wazanzibari wengi hawautaki muungano". Sasa mara nyingi wanaposema "wengi" mtu wa kawaida (asiyetaka kufikiri sana) anaweza kuamini kabisa kuwa ni kweli "wengi" hawautaki Muungano.


      Mfano unaotolewa siku za hivi karibuni ni "sahihi 500,000" za wanaodaiwa "Wazanzibari" wasiotaka Muungano.
      Sasa kwenye mahali ambapo pana watu milioni 1.5 hivi idadi hiyo ni kubwa sana; ni theluthi moja ya watu wote wa Zanzibar. Sasa kama kweli wapo watu wengi hivi njia rahisi ya kutaka kujitoa kutoka kwenye Muungano siyo mihadhara wala hawahitaji kabisa kuwalalamikia watu wa Bara au Serikali ya Muungano.


      Kwa wanaokumbuka wananchi wa Zanzibar walishinikiza vyama vyao viwili vya CCM na CUF kuunda serikali ya umoja wa kitaifa na waliweza kufanya hivyo baada ya kupitisha sheria ya kura ya maoni ambayo hatimaye iliandika upya Katiba ya Zanzibar.


      Wananchi wakaweza kujitokeza na kupiga kura ya maoni. Walifanya hivi bila kuomba kibali Muungano na kiasi cha kuweza kuandika kwenye Katiba Yao vitu ambavyo ni kinyume na Katiba ya Muungano.

      Sasa kama waliweza kufanya hili ni kitu gani kinawashinda kutaka viongozi wao wa kisiasa kuandia sheria ya kupiga kura ya maoni kama wanautaka Muungano au la?


      Kwa vile hoja ya kupinga MUungano inadaiwa inakubaliwa na watu wa vyama vyote ni wazi kuwa ni rahisi sana kwa watu wa Uamsho na Wazanzibari wengine kuhakikisha kuwa BLW linapokaa linaazimia kupitisha kura ya maoni kuhusu Muungano na kutaka sheria iletwe ya kuuliza swali la Muungano.


      Swali liwe rahisi tu:
      Je unataka Zanzibar ibakie kwenye Muungano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?


      a. Ndio ibakie - Ikibakia kero na matatizo ya Muungano kutatuliwa ifikapo Julai 1, 2014 na yasipotatuliwa basi kipengele cha “b” kitatimia.

      b. Hapana isibakie - isipobakia Zanzibar itajitoa kwenye Muungano ifikapo Julai 1, 2014.



      Ijulikane mapema kuwa ikisemwa kuwa "ndio ibakie", maana yake ni kuwa masuala ya muundo na mfumo wa Muungano yatajadiiliwa na kushughulikiwa kwenye Katiba Mpya na yatakuwa tayari kumalizwa yote ifikapo 2014. Baadhi ya watu ambao wamesoma hoja yangu hii ya pili wamedai – na mimi nikakubali – kuwa mwaka 2014 ni mbali sana. Hivyo, Wazanzibari wakitaka kujitenga wanaweza kuja na sheria kwenye kikao kijacho cha baraza la wawakilishi na ninapendekeza Mjumbe Jussa alete muswada wa swali la kura ya maoni ili Wazanzibari wafanye hima ya kujitoa kwenye Muungano.


      Nina uhakika wapo Watanganyika ambao watashukuru sana kwa wao pia kupewa nafasi ya kupumua kuliko kila siku kuimbiwa “Zanzibar, Zanzibar”; kama kweli inavyosemwa Muungano ni kama koti likibana unalivua ni wazi kuwa wanaobanwa na koti hilo sasa siyo Zanzibar tena bali ni watu wa bara na sasa wameamua kuwapa Wazanzibar uwezo kamili (absolute power) kujitoa kwenye Muungano bila kufanya mihadhara mingi wala kushindana na dola.
      Njia hizo hapo juu zitawasaidia Wazanzibari wanaotaka kujitoa watoke salama hasa kwa vile inaonekana hakuna Wazanzibari wanaoutaka Muungano. Watu wa Bara hatutaki kuonekana tunawang’ang’ania Wazanzibari wakati nguvu yote ya kutoka kwenye Muungano wanayo wao.


      Ni matumaini yangu serikali ya Rais Kikwete ambayo imeshindwa kujenga hoja na kuwajibu kwa hoja wana uamsho haitotumia nguvu kuzima harakati za kujitoa kwenye Muungano. Tena ningependa kabisa kutoa pendekezo kwa serikali ya Muungano kukataza kabisa Polisi na JWTZ kuingilia kati mikutano ya wanauamsho na badala yake waache kazi hiyo kwa Valentia, JKU na KMKM.


      Vikosi vya Muungano vikae pembeni kabisa kwani vitaonekana vinalazimisha watu kuupenda Muungano. Kama Muungano haupo moyoni, muungano hauwezi kuwepo ulimini! Kama watu wanataka mfumo wa Muungano au mambo fulani yabadilike basi tungeona juhudi za haraka za kutatua kero zote za Muungano badala ya hili la “subirini mkatoe maoni kwenye tume”. Watanzania wameshatoa maoni ya kutosha kuhusu Muungano kiasi kwamba kama CCM na serikali yake wangekuwa na uwezo wa kuyatatua basi wangekuwa wamekwishayatatua.


      Nidhahiri kuwa hakuna mwenye uwezo huo na sasa kilichobakia ni sote kwa pamoja kutoka Bara tuseme nasi pasi ya shaka kuwa LET ZANZIBAR GO- Iacheni Zanzibar iende.


      Itaenda wapi zaidi ya kuwa kwenye kivuli cha Tanganyika ndani au nje ya Muungano


      HUU NI MWANZO WA "LET ZANZIBAR GO MOVEMENT 2012"; Kama unaunga mkono kuwaacha Wazanzibar wajitoe kwenye Muungano weka kwenye sahihi yako "I support Let Zanzibar Go Movement 2012"! Tuwasaidie waharikishe wajitoe kwani hakuna kiongozi yeyote ambaye amekuwa na uwezo wa kuutetea Muungano kwa hoja maridhawa badala ya kutumia vitisho na mikwara.
      Last edited by Mzee Mwanakijiji; 6th June 2012 at 17:58.
      [email protected]
      The Best of Tanzanian Socio-Political Blogging - http://www.mwanakijiji.com

    2. Miaka 50

    3. #41
      Saint Ivuga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Posts : 20,740
      Rep Power : 10181
      Likes Received
      5676
      Likes Given
      12666

      Default Re: Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muung

      walipe na lile deni la umeme walilosamehewa
      Mzee Mwanakijiji likes this.
      JF the best place to be. and the POWER of God be with us all the time.

    4. #42
      Shardcole's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th January 2012
      Posts : 4,412
      Rep Power : 1288
      Likes Received
      1034
      Likes Given
      4

      Default Re: Zanzibar ni ya Wazanzibar na si chirika na Tanganyika.

      Nyie midebwedo msio na machogo hebu msijisumbue kwani ss bara hatupo tayari kuachia koloni letu zenji kwani lina mafuta na gas..

      Chezea wabara weye....

    5. #43
      kwamwewe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2010
      Posts : 856
      Rep Power : 5406
      Likes Received
      99
      Likes Given
      125

      Default Re: Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muung

      Quote By Nguruvi3
      Pasco, JF ikinyooshewa kidole nitashangaa sana! wale wa UAMSHO waliochoma hadi nyumba za ibada hakuna aliyeshtakiwa kwa uhaini. Mzalendo.net si tu wanatoa maoni bali wana video unazopaswa kuziangalia watoto wakiwa wamelala. Ni matusi kashfa tuhuma n.k

      Tutauliza kama JF inachochea na ni uhaini,basi Jussa alitakiwa awe katika kifungo cha maisha n.k

      Naunga hoja mkono

      Let Zanzibar go, if possible July 1 2012
      MUAMUSHO WAMECHOMA nyumba za ibada hii nyimbo inaimbwa na makanisa pamoja na magazeti yao , hawana ushahidi wowote wa hilo na wanajua ni nani kachome wamebakia kujifanya kulalamika humu kwenye mitandao na kwenye magazeti yao , soma kilichotokea

      Jabir Idrissa

      KUNA uhalifu umefanywa Zanzibar. Ni katika matukio mabaya yaliyoanza usiku wa tarehe 26 Mei 2012. Watu wamechochewa kupambana na dola. Hili halijaelezwa na serikali. Polisi wamevamia nyumba za viongozi wa Uamsho na kuvunja milango huku wakiwatukana matusi ya nguoni viongozi na familia zao sambamba na kuwatishia maisha. Polisi hawajalieleza hili. Amir (kiongozi) wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu (JUMIKI), Sheikh Farid Ahmed Hadi anasema usiku wa Jumamosi hiyo, akiwa kwake, alipata taarifa anafuatwa na polisi wa kuzuia fujo (FFU).

      Akajiandaa. Mnamo saa 7.30 kweli wakafika. Wakataka mlango ufunguliwe. Hakuna aliyewatii. Wakarusha risasi hewani. Hakuna aliyetoka. Hakuna aliyepiga kelele kutokea ndani. Lakini, baada ya kuona vishindo vimezidi, Sheikh Farid akasema kwa sauti, “Nipo ndani na familia yangu tumepumzika. Kama mpo tayari, fanyeni chochote nje ila, ninaapa kwa jina la Allah, anayekuja ndani, tutakabiliana mimi sina bunduki.”

      Polisi hawakujali. Wakafyatua mabomu. Wakavunja mlango na kuvuruga walivyovikuta nje. Wakataka kuingia ndani. Wakakatazana, “hapana. Mnajua nani wamo ndani? Tuondokeni.” Wakaondoka, anasimulia Sheikh Farid. Amepata simulizi kama hizo kwa viongozi wenzake wa Uamsho. Lakini sokomoko kama lililomkuta, lilitokea nyumbani kwa naibu wake, Sheikh Azzan Khalid Hamdan, wakati mwenyewe akiwa nje ya nchi kwa matibabu.

      Sheikh Azzan aliporudi Ijumaa, akapewa taarifa na familia yake kuwa walifika polisi wa FFU na kufanya fujo. Walifyatua risasi nje, wakavunja mlango. Wakapiga mayowe ya kumtukana matusi yeye na familia. Wakaondoka. Hakutulia. Alikwenda kupiga ripoti kituo cha polisi Mfenesini, karibu na anapoishi. Wakuu wakakana kufika kwake. Wakasema askari waliomfuata walitoka Mwembemadema.
      Mwembemadema ni makao makuu ya polisi mkoa wa Mjini Magharibi.

      Hawa ndio waliotuma makachero Jumamosi ile wakamshike Ustadhi Mussa Juma Issa, mmoja wa wahadhir wakuu wa Uamsho, kipenzi cha wahudhuriaji wa mihadhara ya jumuiya hii inayohamasisha Wazanzibari kuukataa muungano.

      Wapo watu wamejitokeza kutoa ushahidi wa walivyoona polisi wanalipua nyumba na mali za vitegauchumi za raia wema, zikiwemo gari zilizoegeshwa Kisiwandui na Michenzani.

      Mwanamke anayefanya kazi shirika la ndege la Kenya Airways, gari yake iliteketezwa kwa bomu lililorushwa na polisi. Matukio yote hayo katika siku mbili – Jumamosi na Jumapili.

      Leo, taarifa zimepatikana za uhalifu wa Polisi uliofanywa Jumatatu, 28 Mei, muda mfupi baada ya watuhumiwa 30 wa fujo, walipoachiwa kwa dhamana na Mahakama ya Mwanakwerekwe, mjini Zanzibar. Kati yao wapo viongozi wawili, akiwemo Ustadhi Mussa, wa Uamsho.
      Wakati wakili wao, Abdalla Juma akiwa Mahakama ya Ardhi, Vuga, vijana wa FFU walivamia ofisi zake Amani, yapata kilomita tano kutoka Vuga. Wakapitisha mitutu ya bunduki madirishani na kufyatua risasi na mabomu ya machozi.

      Hawakujali wafanyakazi waliokuwa ndani. Ni mchana kweupe. Hapana, ni mchana wa mola muumba mbingu na ardhi siku ya kazi, Jumatatu. Ipo taarifa ya Chama cha Wanasheria wa Zanzibar (ZLS) kulalamikia kitendo hicho. Wamemtumia barua Kamishna wa Polisi wa Zanzibar, Mussa Ali Mussa, na kumtaka asake wahusika na kuwashitaki.

      ZLS wamekiita kitendo hicho cha makusudi kilicholenga kutisha mawakili wasiwe imara katika kazi yao ya kutetea wananchi wanaposhitakiwa. Polisi wanatuhumiwa sasa kushiriki vitendo vya uhalifu katika kipindi kilekile ambacho wao wanatuhumu Uamsho kuzusha ghasia mjini Zanzibar.

      Ninayaeleza haya ili kukumbusha historia ya kisiasa Zanzibar inayochefua. Siasa za maridhiano zilizoanza kustawi tangu 2010 mwishoni, zinachafuliwa kwa nguvu. Ni kama zilivyokuwa zikipandikizwa na kustawishwa siku zile za giza, mara tu mfumo wa siasa za vyama vingi, siasa za ushindani, uliporudishwa chini ya sheria ya Tanzania.

      Sasa wapo wasiotaka amani Zanzibar idumu. Wapo. Pengine wanampenda Amani Abeid Karume, kiongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Shariff Hamad, ambao walizijenga, bali wanachukia matunda ya maridhiano.

      Polisi. Polisi. Polisi. Polisi. Polisi. Polisi. Polisi. Polisi. Polisi. Hapana; si peke yao.

      Kwa jumla, vyombo vya dola, vya dola, vya dola. Dola, dola, dola, dola, dola, dola, dola, dola, dola. Vyote vilitajwa kupandikiza chuki kwa wananchi, mgongo ukiwa vyama vingi na uimara wa CUF. Visima vikapakwa kinyesi, ofisi za umma zikawashwa kwa viberiti na makanisa yakachomwa kiajizi. Kanisa linawashwa, dakika mbili tu hao walinzi wamefika.

      Ushetani ule ukakoma pale wananchi wa Shengejuu, kaskazini Pemba, walipovizia usiku kutafuta nani hasa wakihusika na vitendo vile vya kiharamia. Waliokutwa mpaka leo Polisi hawajawataja.

      Ni askari polisi na mashushushu ndani ya Landrover iliyosheheni madumu ya petroli, mapipa ya kinyesi na viberiti vya kuwashia mabomu ya chupa.

      Kutaka kuzubaisha umma wa Watanzania na ulimwengu, IGP Omari Mahita akaunda kikosi kuchunguza. Akamteua Robert Manumba, kachero aliyekuwa msaidizi mkuu wa DCI Adadi Rajabu, kukiongoza.

      Alitaka wachunguze chimbuko, sababu na wahusika wa milipuko ile ya kishetani pamoja na vitendo haramu vya kupaka kinyesi madarasa na kukimwaga kwenye visima vya maji wanayotumia wananchi.

      Tangu wakati ule, karibu miaka kumi sasa, si DCI Manumba ambaye sasa ndiye DCI, si IGP Mahita wala serikali iliyotoa ripoti ya uchunguzi huo.

      Wananchi waseme nini hapo?

      Lakini kwa sababu wahusika walijulikana na kufikia kukamatwa Shengejuu, zile fitna kuwa CUF walikuwa wahusika, zilifutika.
      Tungalinao wakorofi wasiopenda maridhiano.

      Wahafidhina ndani ya CCM wameibuka upya wakitaka kuharibu amani na utulivu. Hawawezi kuitaja CUF moja kwa moja maana wanashirikiana nacho kuendesha serikali.


      Wametafuta pa kuingilia – Uamsho. Kwa kuwa taasisi hii imechukua jukumu la kupigania haki za wananchi wasioridhishwa na mwenendo wa muungano, wanawapakazia kuwa wanavunja amani.

      Kumbe bado kuujadili Muungano wa Tanzania ni uhaini. Pamoja na serikali kuruhusu Watanzania watoe maoni yatakayotumika kuandika katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, watawala hawapendi watu wafikiri tofauti na wao.


      Tunaona kila viongozi wa polisi wanavyojitahidi kupotosha ukweli wa kilichotendeka mjini Zanzibar, ile dhamira yao ya kupotosha inawarudia. Wanatajwa baada ya kuonekana wazi wakivamia na kuharibu mali ikiwemo ofisi za wanasheria.

      Mpanga ubaya mwisho humrudia. Hawajajisafisha, wamejiumbua. Na ndiyo matokeo ya polisi nchini kushabikia siasa. Wanasubiriwa watamshika nani mchoma makanisa. Bado watafute ushahidi kuthibitisha kesi ya watu 30, pamoja na wafadhili wa Uamsho.

    6. #44
      majorbuyoya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st April 2012
      Posts : 663
      Rep Power : 2613
      Likes Received
      183
      Likes Given
      238

      Default Re: Zanzibar ni ya Wazanzibar na si chirika na Tanganyika.

      nyie uzao wa watumwa ebu pumzikeni sasa, kila siku kelele tu!!. Dunia gani itakayowasikia nyie, hivi mnadhani Zanzibar huko nje wanaitambua kuwa ni nchi? Hata mkiandamana nchi za nje wanajua kuwa kitongoji kimojawapo ndani ya Tanzania ndo kimeandamana.

    7. #45
      kwamwewe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2010
      Posts : 856
      Rep Power : 5406
      Likes Received
      99
      Likes Given
      125

      Default Re: Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muung

      Quote By Mzee Mwanakijiji
      Pasco, Muungano uliridhiwa Zanzibar kama ulivyoridhiwa Tanganyika na vyombo halali vilivyokuwa na uwezo wa kufanya hivyo na ambavo bado vipo. Wanaosema kwamba Muungano haukuridhiwa Zanzibar wanaandika historia upya; hawajui historia na hawataki kuijua. Na Wazanzibari wengi hawajui kuwa muungano uliridhiwa kihalali kabisa. Ndio maana wengine tunaona huo muda wa kuwafundisha watu historia hatuna; kama wanataka kuondoka wafunge mizigo, mapakacha na waende; kuna mamia ya Watanganyika walio tayari kushika nafasi zao ambazo wanazishikilia bara.
      haya mbona unayaandika hapa tu huwezi weka muhadhara ukawaambia watu haya ??? unakimbilia JF na Magazetini tu !!!

      Mbona waliokuwemo katika system tokea kuundwa Huo Muungano , wengine wahai wanasema vyengine???
      Mzee Mwanakijiji likes this.

    8. RukaaJuu Final

    9. #46
      kwamwewe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2010
      Posts : 856
      Rep Power : 5406
      Likes Received
      99
      Likes Given
      125

      Default Re: Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muung

      Quote By Nyumbu-
      Let Zanzibar GO! GO Go. Zanzibar!
      Unfortumetelly though, who is a Zanzibari?
      the one who wants his country Zanzibar
      Mzee Mwanakijiji likes this.

    10. #47
      Nguruvi3's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st June 2010
      Location : Kidabashi-Dongobeshi
      Posts : 3,438
      Rep Power : 2887
      Likes Received
      4802
      Likes Given
      2865

      Default Re: Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muung

      Ndugu yangu Kwamwewe, uhalifu wa kuchoma moto umetokea mara 25. Siyo SMZ au UAMSHO wanaokanusha.
      Watanganyika wamechomwa moto na wahalifu wameachiwa huru.
      Hili la kuchoma moto linatokana na uchochezi wa lugha za 'Wakristo na muungano'
      Ni mwendawzaimu peke yake atakayesikiliza hadithi za 'Alshabaab' za kukanusha upuuzi.

      Huko tumeshatoka na sasa tunasema
      Let Zanzibar Go!

      Tuna vijana wetu kwa maelfu sasa wanjipanga kuchukua nafasi zao halali ndani ya nchi yao siku Wazanzibar watakapobeba mizigo.

      Wazaznzibar walikuja na mabegi na wanapaswa kuondoka na mabegi na Watanganyika pia walioko huko wataondoka na mabegi. Hakuna Mzanzibar aliyekuja na nyumba au ardhi.

      Let Zanzibar go sasa haina kurudi nyuma.
      Hakuna serikali 3, mkataba wala ushirikiano. Ushirikiano ni kama ule wa Kenya au Malawi

      It is time, we're tired. Let Zanzibar go!
      The mantra should be Let Zanzibar go.

    11. #48
      kwamwewe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2010
      Posts : 856
      Rep Power : 5406
      Likes Received
      99
      Likes Given
      125

      Default Re: Zanzibar ni ya Wazanzibar na si chirika na Tanganyika.

      Quote By adolay
      ya wazanzibar wenye asili ya mwarabu au watu weusi kama watanganyika? We unaonaje?
      mwenye asili ya mwalabu ni pengo na shayo maana ndiyo wimbo wanaowaimbisha huo

    12. #49
      kwamwewe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2010
      Posts : 856
      Rep Power : 5406
      Likes Received
      99
      Likes Given
      125

      Default Re: Zanzibar ni ya Wazanzibar na si chirika na Tanganyika.

      Quote By majorbuyoya
      nyie uzao wa watumwa ebu pumzikeni sasa, kila siku kelele tu!!. Dunia gani itakayowasikia nyie, hivi mnadhani zanzibar huko nje wanaitambua kuwa ni nchi? Hata mkiandamana nchi za nje wanajua kuwa kitongoji kimojawapo ndani ya tanzania ndo kimeandamana.
      wewe ungalikuwa mtumwa hata mimi ningalikutoa bure maana huna thamani yoyote huwezi kuuzika maana uwezo wa kufikiri huna

    13. #50
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6154
      Likes Given
      22279

      Default

      Quote By Mzee Mwanakijiji
      Pasco, Muungano uliridhiwa Zanzibar kama ulivyoridhiwa Tanganyika na vyombo halali vilivyokuwa na uwezo wa kufanya hivyo na ambavo bado vipo. Wanaosema kwamba Muungano haukuridhiwa Zanzibar wanaandika historia upya; hawajui historia na hawataki kuijua. Na Wazanzibari wengi hawajui kuwa muungano uliridhiwa kihalali kabisa. Ndio maana wengine tunaona huo muda wa kuwafundisha watu historia hatuna; kama wanataka kuondoka wafunge mizigo, mapakacha na waende; kuna mamia ya Watanganyika walio tayari kushika nafasi zao ambazo wanazishikilia bara.
      Mkuu Mzee Mwanakijiji, with due respect, Muungano uliridhiwa bara tuu na sio Zanzibar!.

      Sio lazima kila mkataba uwe ni wa maandishi, lakini mkataba wowote wa ardhi, land au pango, lazima uwe wa maandishi!. Wewe unaweza kununua gari na kumzawadia mpenzi/mke/ ndugu au mzazi kwa kauli tuu na ukawa ni mkataba halali!.

      Lakini kama una land yako, ukiamua kumzawadia yoyote, hata ukimzawadia kwa kauli, lazima maandishi yafuatie ndio yatakayo halalisha hiyo kauli!.

      Mzizi asili haswa wa muungano ni kauli, ya Nyerere na Karume.

      Nyerere " Sisi ni ndugu, kwa nini tusiungane?".
      Karume " Tuungane, wewe rais. mimi makamo".

      Shughuli ilianza na kumalizika in a split of a second!.

      Kwa vile hizi ni nchi mbili tofauti zenye uhuru wake na zote ni Jamuhuri huru, kauli pekee haitoshi kuziunganisha, lazima kufuata taratibu, sheria na kanuni ili kuhalalisha nia na kauli hizo, ndipo zikaandaliwa hizo articles of union!.

      Articles zile japo zilikosa sifa ya kisheria ya kuutwa mkataba "contract" kutokana na tatizo la kisheria liitwalo "privity of contract", articles zile zilikuwa na sifa zote za kuitwa ' international treaty" kuunganisha nchi mbili, na ili any international treaty kupata uhalali na nguvu ya kisheria, ni lazima treaty hiyo iwe ratified na mabunge ya nchi husika!.

      Ratification is a process ambayo hufanywa kwa procedures maalum na kufanywa in writing!.

      Bunge la Tanzania lilifuata sheria, taratibu na kanuni zote ku ratify zile articles of union kwa maandishi!.

      Zanzibar, walikuwa ndio kwanza wametoka kwenye mapinduzi, hivyo hawakuwa na bunge, Baraza la Mapinduzi ndilo lililokuwa kila kitu!. Lilipaswa kuziridhia zile articles of union kwa ratification ambayo hufanywa kwa maandishi!. Vikao vyote vya BLM vina hansard, lakini hilo halikufanyika na hakuna kumbukumbu yoyote ya maandishi kwamba ratification ilifanyika!.

      Kisheria Muungano ni wa bara tuu, ndio maana Dourado alipomtonya Jumbe kuhusu Zanzibar kutouratify muungano na wakataka kuweka mambo sawa, Jumbe alishughulikiwa ipasavyo!.

      Tumewanyanyasa sana, its about time now, we just lets them go!
      Mzee Mwanakijiji likes this.

    14. #51
      Tume ya Katiba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2012
      Location : Chumbuni-Zanzibar
      Posts : 2,690
      Rep Power : 0
      Likes Received
      542
      Likes Given
      273

      Default Re: Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muung

      Quote By Pasco

      Kisheria Muungano ni wa bara tuu, ndio maana Dourado alipomtonya Jumbe kuhusu Zanzibar kutouratify muungano na wakataka kuweka mambo sawa, Jumbe alishughulikiwa ipasavyo!.!
      Muumini wa sera ya majimbo, hili neno, umetumia taaluma yako leo at least.
      Natumai shule ulioitoa MMKJ ameielewa!

    15. #52
      Shardcole's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th January 2012
      Posts : 4,412
      Rep Power : 1288
      Likes Received
      1034
      Likes Given
      4

      Default

      Quote By kwamwewe
      wewe ungalikuwa mtumwa hata mimi ningalikutoa bure maana huna thamani yoyote huwezi kuuzika maana uwezo wa kufikiri huna
      ndio madhara ya elimu ahela hyo... Wazenji vilaza kweli...

    16. #53
      mshikachuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2010
      Posts : 2,346
      Rep Power : 899
      Likes Received
      429
      Likes Given
      2283

      Default Re: Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muung

      Mmh! nakula nondo tu hapa....sitii neno lolote leo ila najifunza vitu fulani kupitia uzi huu wa Mwanakijiji.
      Wale wenzangu na mimi wa Mzalendo.net nawaombeni njooeni huku muangalie watu wanavyojua kujenga
      hoja za nguvu! siyo nyinyi kazi yenu kushupalia udini tu kwenye mtandao wenu wa Mzalendo.net na ham
      jui kujenga hoja. Back to the topic....tuendelee wana jamvi- nawasoma taratiiiiibu!
      Mzee Mwanakijiji likes this.

    17. #54
      Nonda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th November 2010
      Location : Gongo La Mboto
      Posts : 5,834
      Rep Power : 1866
      Likes Received
      939
      Likes Given
      367

      Default Re: Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muung

      Quote By Pasco
      Mkuu Mzee Mwanakijiji, with due respect, Muungano uliridhiwa bara tuu na sio Zanzibar!.

      Kwa vile hizi ni nchi mbili tofauti zenye uhuru wake na zote ni Jamuhuri huru, kauli pekee haitoshi kuziunganisha, lazima kufuata taratibu, sheria na kanuni ili kuhalalisha nia na kauli hizo, ndipo zikaandaliwa hizo articles of union!.

      Articles zile japo zilikosa sifa ya kisheria ya kuutwa mkataba "contract" kutokana na tatizo la kisheria liitwalo "privity of contract", articles zile zilikuwa na sifa zote za kuitwa ' international treaty" kuunganisha nchi mbili, na ili any international treaty kupata uhalali na nguvu ya kisheria, ni lazima treaty hiyo iwe ratified na mabunge ya nchi husika!.

      Ratification is a process ambayo hufanywa kwa procedures maalum na kufanywa in writing!.

      Bunge la Tanzania lilifuata sheria, taratibu na kanuni zote ku ratify zile articles of union kwa maandishi!.

      Zanzibar, walikuwa ndio kwanza wametoka kwenye mapinduzi, hivyo hawakuwa na bunge, Baraza la Mapinduzi ndilo lililokuwa kila kitu!. Lilipaswa kuziridhia zile articles of union kwa ratification ambayo hufanywa kwa maandishi!. Vikao vyote vya BLM vina hansard, lakini hilo halikufanyika na hakuna kumbukumbu yoyote ya maandishi kwamba ratification ilifanyika!.

      Kisheria Muungano ni wa bara tuu, ndio maana Dourado alipomtonya Jumbe kuhusu Zanzibar kutouratify muungano na wakataka kuweka mambo sawa, Jumbe alishughulikiwa ipasavyo!.

      Tumewanyanyasa sana, its about time now, we just lets them go!
      Mkuu hapo nilipoweka rangi nyekundu umechanganya madawa/ umefanya madudu.

      Isomeke Bunge la Tanganyika lilifuata sheria na katika kufuata sheria pia ilivunja sheria kwani baada ya sheria ile Bunge la Tanganyika halikukaa tena kama Bunge la Tanganyika. Nani aliwapa uwezo wa kuiua serikali ya Tanganyika na Bunge la Tanganyika?

      Pia isomeke Muungano ni wa Tangayika tu. Hakuna nchi iliyoitwa bara au inayoitwa bara. Usifuate siasa za kisanii/ mazingaombwe.

      Jikumbushe jina la Muungano. Lilikuwa ni Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na lilipofupishwa likawa Jamhuri ya Muungano wa TanZanIA.
      Mazingaombwe/ kiini macho tu ndio yataleta neno bara.

      Sio nia yangu kuanzisha mjadala katika hili lakini tusiwachanganye wananchi na wasomaji wa JF.

      Let us call spade a spade!

    18. #55
      Chilisosi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th October 2008
      Posts : 1,703
      Rep Power : 0
      Likes Received
      375
      Likes Given
      459

      Default Re: Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muung

      Huu muungano wa kupe na ng'ombe wapi na wapi. kupe anataka kujitenga lakini ng'ombe ambaye ndio tanganyika unakataa badala ya kushangilia. mie naunga mkono. GO ZENJI GO! RASILIMALI ZENU ZA UROJO NA KARAFUU HATUZITAKI ACHILIA MBALI HAYO MAFUTA MNAYODAI YAPO. na wakiondoka mipaka iimarishwe kwa sababu mie nawaona kama somalia tu hakuna tofauti
      Mzee Mwanakijiji likes this.

    19. #56
      majorbuyoya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st April 2012
      Posts : 663
      Rep Power : 2613
      Likes Received
      183
      Likes Given
      238

      Default Re: Zanzibar ni ya Wazanzibar na si chirika na Tanganyika.

      Quote By kwamwewe
      wewe ungalikuwa mtumwa hata mimi ningalikutoa bure maana huna thamani yoyote huwezi kuuzika maana uwezo wa kufikiri huna
      Niwe mtumwa kwani mimi nimekuambia ni Mzanzibar??. Wewe huoni watumwa jinsi wasivyojiamini kila siku kelele tu kuwa wanaonewa.

    20. #57
      Saint Ivuga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Posts : 20,740
      Rep Power : 10181
      Likes Received
      5676
      Likes Given
      12666

      Default Re: Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muung

      Mwanakijiji kwenye hii clip una la kusema tena?ni kwamba watu wanataka nchi yao ambayo mmeikalia kimabavu..
      Mzee Mwanakijiji likes this.
      JF the best place to be. and the POWER of God be with us all the time.

    21. #58
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,520
      Rep Power : 46715
      Likes Received
      16435
      Likes Given
      8471

      Default Re: Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muung

      Quote By Pasco
      Mkuu Mzee Mwanakijiji, with due respect, Muungano uliridhiwa bara tuu na sio Zanzibar!.
      Pasco na wewe umeendelea kuamini porojo kuwa 'muungano haukuridhiwa Zanzibar'; chombo halali cha Zanzibar (siyo Karume tu kama wengi mnavyotaka tuamini ) kiliridhia muungano. Wanaosema muungano haukuridhiwa Zanzibar wanakana historia.
      [email protected]
      The Best of Tanzanian Socio-Political Blogging - http://www.mwanakijiji.com

    22. #59
      timbilimu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd September 2010
      Location : DSM
      Posts : 2,672
      Rep Power : 977
      Likes Received
      584
      Likes Given
      10

      Default Re: Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muung

      Sioni sababu ya kuendelea kuwabembeleza Wazanzibari. Mtoto akitaka wembe mpe umkate! Hatutaki watu wa kujitoa mhanga kujiripua huku Tanganyika kisa ni wapigania uhuru wa Zanzibar. Watimue! Tunashindwa kupumua!
      Chilisosi likes this.

    23. #60
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,520
      Rep Power : 46715
      Likes Received
      16435
      Likes Given
      8471

      Default Re: Let Zanzibar Go! - Kwanini Zanzibar hawahitaji kuwashawishi Watanganyika ili watoke kwenye Muung

      Quote By Saint Ivuga
      Mwanakijiji kwenye hii clip una la kusema tena?ni kwamba watu wanataka nchi yao ambayo mmeikalia kimabavu..
      Nope nililolisema ndio nimelisema. Sasa hivi malalamiko yao ya kutawaliwa, kunyonywa, kunyanyaswa hayana msingi tena. Wakitaka kutoka njia ndio hizo tumeziweka wazi wao tu waamue ili wataitumia.
      Saint Ivuga likes this.
      [email protected]
      The Best of Tanzanian Socio-Political Blogging - http://www.mwanakijiji.com

    Page 3 of 17 FirstFirst 1234513 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...