Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kigwangalla asusa Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati kwa Kucheleweshewa Vitabu!

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 41
    1. #1
      Le Grand Alexei's Avatar
      Member Array
      Join Date : 9th November 2011
      Posts : 69
      Rep Power : 393
      Likes Received
      50
      Likes Given
      55

      Default Kigwangalla asusa Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati kwa Kucheleweshewa Vitabu!

      Kucheleweshwa vitabu vya bajeti: Kigwangalla Agomea Kujadili Bajeti Kwny Kamati! : Dr. Hamisi Kigwangalla's Round Table Kucheleweshwa vitabu vya bajeti: Kigwangalla Agomea Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati! : Dr. Hamisi Kigwangalla's Round Table # 5 mins ago

      Kumekuwa na mwenendo mbovu wa kuchelewesha nyaraka muhimu za bajeti ya serikali kwenye kamati kuanzia mwaka wa fedha unaoisha. Mwaka jana vitabu vya bajeti viligawiwa kwa wabunge wiki mbili kabla ya Bunge kuanza, kwa maana nyingine katika kipindi cha kamati kujadili na kuandaa mapendekezo kwa Bunge, kwa maana hiyo wabunge walipewa vitabu leo na kesho wakatakiwa kuanza kujadili na kutoa mapendekezo yao. Mwaka jana baadhi ya kamati ziligoma na hivyo kusababisha Spika kuitaka serikali isirudie kuchelewesha tena namna hiyo. Mwaka huu, hali ni mbaya zaidi; kamati zimepewa vitabu mwisho wa wiki ya kwanza (kati ya mbili) ya kamati. Hali hii ni kinyume na utaratibu wa kikanuni wa Bunge ambapo ingepaswa wabunge wapewe vitabu vya bajeti wiki tatu (siku 21) kabla ya tarehe ya kuanza Bunge Dodoma. Kwa maana hiyo wabunge wangekuwa wamepewa vitabu si chini ya siku saba kabla ya kuanza kwa kamati (Ukizingatia kamati hukutana wiki 2 kabla ya Bunge kuanza). Hii ingewawezesha kusoma kwa umakini na kuandaa mapendekezo ya mabadiliko ama ushauri kwenye bajeti hiyo kwa ufanisi unaopaswa.

      Kwa kucheleweshewa vitabu kiasi hiki na kwa kuzingatia ukubwa na wingi wa mavitabu haya ya bajeti ni dhahiri hakuna Mbunge mwenye spidi na uwezo wa kuisoma, kuimaliza na kuichambua bajeti hii kwa ufanisi na tija inayostahiki. Kwa maana hiyo wabunge, ambao ni jicho la wananchi kwenye bajeti na utendaji kazi wa serikali, wamenyimwa fursa ya kufanya kazi yao ipasavyo na hivyo wanalipua lipua ili mradi liende tu! Uchunguzi wangu umegundua kuwa haya yamekuwa ni mazoea. Hii inaonesha ni kwa jinsi gani mhimili wa Bunge ulivyokandamizwa na mhimili wa serikali (executive) na inaaakisi maovu na uvundo uliokuwepo kwenye serikali kwa muda mrefu bila kurekebishwa ipasavyo; kumbe ni kwa sababu mhimili Bunge ulikuwa usingizini kwa muda mrefu. Kama hii ni kwa maksudi ili kupunguza kelele na kupitisha bajeti kwa urahisi ama ni bahati mbaya nimeshindwa kuelewa, japokuwa kwa kiasi kikubwa ni harufu ya hila na inda inayotawala hali hii.

      Mimi nimeshindwa kuelewa wenzangu wanawezaje kujadili bajeti hizi bila kusoma!

      Ili kuweka wazi suala hili, na ili kuishinikiza serikali na viongozi wa Bunge kuona umuhimu wa kuwahisha vitabu ili kutoa fursa kwa wawakilishi wa wananchi kujadili bajeti kwa ufanisi na tija inayostahili, nimeamua kugoma kujadili bajeti katika ngazi ya kamati na badala yake nitajadili katika ngazi ya Bunge zima nitakapokuwa nimesoma na kuridhika kwamba ninapitisha kitu ninachokielewa. Nawashauri wabunge wenzangu waniunge mkono ili muda wa kujadili bajeti hizi katika ngazi ya kamati usogezwe mbele kwa wiki walau moja ili kutoa fursa ya kufanya kazi ya uhakika bila kulipua.
      Naelewa kuna sababu nyingi zinatolewa, kuwa eti re-shuffle ya mawaziri imesababisha kuchelewa, sawa, lakini hatuwezi ku-compromise ubora wa kazi nyeti kama kupitisha bajeti bila kutoa fursa ya kutosha kwa wabunge kujadili, kuchambua na kushauri ipasavyo.

      Tamko hili limetolewa na Dkt. Hamisi Kigwangalla (MB), Nzega.

    2. Miaka 50

    3. #2
      POMPO's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 12th March 2011
      Posts : 2,955
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1090
      Likes Given
      625

      Default re: Kigwangalla asusa Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati kwa Kucheleweshewa Vitabu!

      Chama chako kinasemaje? maana hukusain hoja ya kumuondoka PM, kwa madai ya chama kwanza, Je kwa hili chama hakina haja ya kuwahisha vitabu (ma kabuasha) aacha unafiki
      HKigwangalla likes this.

    4. #3
      TIMING's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 20,081
      Rep Power : 12251
      Likes Received
      6013
      Likes Given
      6847

      Default re: Kigwangalla asusa Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati kwa Kucheleweshewa Vitabu!

      kuna wakati alikandya chadema kususa, sasa ni nini hiki?
      HKigwangalla likes this.
      .....Ana sifa zote, nzuri na mbaya!!!

    5. #4
      Yetuwote's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 22nd July 2010
      Posts : 190
      Rep Power : 486
      Likes Received
      41
      Likes Given
      28

      Default re: Kigwangalla asusa Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati kwa Kucheleweshewa Vitabu!

      Amemaliza maandamano aliyoahidi? sijui ni leo?

    6. #5
      MANGUNGO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th August 2011
      Posts : 1,146
      Rep Power : 619
      Likes Received
      251
      Likes Given
      14

      Default Re: Kigwangalla asusa Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati kwa Kucheleweshewa Vitabu!

      Kakosa uwaziri anajamba tu!

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      Precise pangolin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 4th January 2012
      Posts : 5,670
      Rep Power : 1909
      Likes Received
      1563
      Likes Given
      676

      Default Re: Kigwangalla asusa Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati kwa Kucheleweshewa Vitabu!

      Kigwangalla tokea akose uwaziri kachanganyikiwa anajifanya anasoma PHD wakati anatumia majina ya watu


    9. #7
      Suzie's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th May 2010
      Posts : 1,085
      Rep Power : 0
      Likes Received
      339
      Likes Given
      309

      Default Re: Kigwangalla asusa Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati kwa Kucheleweshewa Vitabu!

      Alisemaga CDM ndio wasusaji na kuwasema vibaya sasa na yeye amekuwa CDM?

    10. #8
      Fidel80's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd May 2008
      Location : UVUNGUNI
      Posts : 19,012
      Rep Power : 9490
      Likes Received
      3123
      Likes Given
      1221

      Default Re: Kigwangalla asusa Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati kwa Kucheleweshewa Vitabu!

      Kuukosa uwaziri bado kunamsumbua akilini
      **^^+..Ukiuza Utumbo usiogope nzi..+^^**
      Chuda Raha
      Email: [email protected]

    11. #9
      HKigwangalla's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th February 2008
      Location : Dar es salaam, Tanzania
      Posts : 527
      Rep Power : 681
      Likes Received
      568
      Likes Given
      153

      Default Re: Kigwangalla asusa Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati kwa Kucheleweshewa Vitabu!

      Quote By MANGUNGO
      Kakosa uwaziri anajamba tu!
      sijawahi kuona watu wa maana kama akina Mwanakijiji wakitukana, nadhani by great thinkers, huyu ndiyo mmoja wao; lakini wewe Mangungo 'smalltime thinker' and maybe you are the opposite of smart...
      Dr. Hamisi Kigwangalla, MD, MPH, MBA
      Mabadiliko ya kweli yataletwa na sisi...!

    12. #10
      HKigwangalla's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th February 2008
      Location : Dar es salaam, Tanzania
      Posts : 527
      Rep Power : 681
      Likes Received
      568
      Likes Given
      153

      Default Re: Kigwangalla asusa Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati kwa Kucheleweshewa Vitabu!

      Quote By Fidel80
      Kuukosa uwaziri bado kunamsumbua akilini
      kwani nilitegemea kuupata ama ni nyie mliokuwa mnaweweseka kuhusu mimi kupewa uwaziri?
      Dr. Hamisi Kigwangalla, MD, MPH, MBA
      Mabadiliko ya kweli yataletwa na sisi...!

    13. #11
      HKigwangalla's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th February 2008
      Location : Dar es salaam, Tanzania
      Posts : 527
      Rep Power : 681
      Likes Received
      568
      Likes Given
      153

      Default Re: Kigwangalla asusa Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati kwa Kucheleweshewa Vitabu!

      Quote By Suzie
      Alisemaga CDM ndio wasusaji na kuwasema vibaya sasa na yeye amekuwa CDM?
      sijawahi kusema hvyo, wewe ni mwongo ukizeeka utakuwa ...............
      Dr. Hamisi Kigwangalla, MD, MPH, MBA
      Mabadiliko ya kweli yataletwa na sisi...!

    14. #12
      HKigwangalla's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th February 2008
      Location : Dar es salaam, Tanzania
      Posts : 527
      Rep Power : 681
      Likes Received
      568
      Likes Given
      153

      Default Re: Kigwangalla asusa Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati kwa Kucheleweshewa Vitabu!

      Quote By Precise pangolin
      Kigwangalla tokea akose uwaziri kachanganyikiwa anajifanya anasoma PHD wakati anatumia majina ya watu
      watu wengine mna wivu sana. kuhusisha kusoma kwangu Ph.D na haya masiasa yenu ya kitoto ni fallacy. sasa inahusika vipi hapa? acha wivu bro. Kama unaweza kusoma Ph.D na wewe nenda kasome tu its a good thing, ofcoz kama una uwezo! Maana ile ni uanazuoni na siyo blah blah kama hizi siasa unazofanya hapa, maana hata wewe unafanya na unajiona una hoja kweli, pengine ukijifananisha na mimi unajiona uko juu sana na mimi ni mchovu sana...kumbe ukute wewe hata kugombea tu huo ubunge hujawahi kujaribu, ukute hata kuchukua risk ya kuacha kazi tu na kuanzisha biashara yako hujawahi kufanya, hata ku-indulge in a challenge ya ku-pursue Ph.D hujawahi....
      Dr. Hamisi Kigwangalla, MD, MPH, MBA
      Mabadiliko ya kweli yataletwa na sisi...!

    15. #13
      HKigwangalla's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th February 2008
      Location : Dar es salaam, Tanzania
      Posts : 527
      Rep Power : 681
      Likes Received
      568
      Likes Given
      153

      Default Re: Kigwangalla asusa Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati kwa Kucheleweshewa Vitabu!

      Quote By MANGUNGO
      Kakosa uwaziri anajamba tu!
      Bora mimi, hivi wewe ungeishia nini?...
      Dr. Hamisi Kigwangalla, MD, MPH, MBA
      Mabadiliko ya kweli yataletwa na sisi...!

    16. #14
      UmkhontoweSizwe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th December 2008
      Posts : 2,010
      Rep Power : 933
      Likes Received
      552
      Likes Given
      319

      Default Re: Kigwangalla asusa Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati kwa Kucheleweshewa Vitabu!

      Kigwangala, acha kujibishana na watu ambao badala ya kujadili mantiki ya hoja yako ya kususia hiyo bajeti kwa sababu ulizozitoa, wao wanaanza kutukana tu. Wewe ni kiongozi wa jamii kwa ngazi ya kitaifa, jaribu kuepuka mipasho isiyo na tija kwako. Jikite zaidi kwenye kutetea hoja yako ya ususiaji. Ikiwezeka usaidie kuwaelewesha ugumu wa kujadili bajeti bila kusoma.
      HKigwangalla and Saint Ivuga like this.
      "Power tends to corrupt, and absolute power corrupts absolutely." (Lord Acton, 1887)

    17. #15
      English Learner's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st January 2012
      Location : Inside the Laptop
      Posts : 251
      Rep Power : 804
      Likes Received
      268
      Likes Given
      197

      Default

      Quote By HKigwangalla
      watu wengine mna wivu sana. kuhusisha kusoma kwangu Ph.D na haya masiasa yenu ya kitoto ni fallacy. sasa inahusika vipi hapa? acha wivu bro. Kama unaweza kusoma Ph.D na wewe nenda kasome tu its a good thing, ofcoz kama una uwezo! Maana ile ni uanazuoni na siyo blah blah kama hizi siasa unazofanya hapa, maana hata wewe unafanya na unajiona una hoja kweli, pengine ukijifananisha na mimi unajiona uko juu sana na mimi ni mchovu sana...kumbe ukute wewe hata kugombea tu huo ubunge hujawahi kujaribu, ukute hata kuchukua risk ya kuacha kazi tu na kuanzisha biashara yako hujawahi kufanya, hata ku-indulge in a challenge ya ku-pursue Ph.D hujawahi....
      This is a TRUTH and 100% a FACT to most JF members who blow the trumpet of critique.

      It is simple to condemn, critize, etc and most fool do
      HKigwangalla likes this.

    18. #16
      Saint Ivuga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Posts : 20,652
      Rep Power : 10162
      Likes Received
      5648
      Likes Given
      12664

      Default Re: Kigwangalla asusa Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati kwa Kucheleweshewa Vitabu!

      Kigwa achana na kujibu matusi ya watu wapotezee ...
      JF the best place to be. and the POWER of God be with us all the time.

    19. #17
      HKigwangalla's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th February 2008
      Location : Dar es salaam, Tanzania
      Posts : 527
      Rep Power : 681
      Likes Received
      568
      Likes Given
      153

      Default Re: Kigwangalla asusa Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati kwa Kucheleweshewa Vitabu!

      Quote By UmkhontoweSizwe
      Kigwangala, acha kujibishana na watu ambao badala ya kujadili mantiki ya hoja yako ya kususia hiyo bajeti kwa sababu ulizozitoa, wao wanaanza kutukana tu. Wewe ni kiongozi wa jamii kwa ngazi ya kitaifa, jaribu kuepuka mipasho isiyo na tija kwako. Jikite zaidi kwenye kutetea hoja yako ya ususiaji. Ikiwezeka usaidie kuwaelewesha ugumu wa kujadili bajeti bila kusoma.
      unajua kuna watu wa hovyo sana humu JF na wamezoea kuona wakitukana viongozi na viongozi wakiwaacha, sasa mimi huwa siwaachi kwa kuwa nimo humu na ninajibu hoja kwa hoja, tusi kwa tusi (japokuwa situkani moja kwa moja ) kama wao. Hakuna anayejibu hoja ama hata kuchangia. Jambo nililopost kwenye blog yangu ni la msingi sana kwa mustakabali wa Taifa lkn leo hapa watu wanaleta hoja za kitoto (kisa eti kiongozi mzuri na shujaa ni yule anayeleta vurugu, anayepinga serikali muda wote nk). Mimi imejifunza uongozi kabla hata sijaenda shule na ninajua kufanya mambo yatakayowafurahisha na yatakayowachukiza ninaowaongoza lakini siku zote kwa kuwa nina ethics za uongozi siwezi kufanya maamuzi ya hovyo kwa kuwa nataka kusifiwa, nitafanya yale ya ukweli - yakiwafurahisha sawa, yakiwachukiza sawa, na huo ndio uongozi shupavu na unaofaa---kuwa na ujasiri wa kusema ukweli muda wote
      Dr. Hamisi Kigwangalla, MD, MPH, MBA
      Mabadiliko ya kweli yataletwa na sisi...!

    20. #18
      Saint Ivuga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Posts : 20,652
      Rep Power : 10162
      Likes Received
      5648
      Likes Given
      12664

      Default Re: Kigwangalla asusa Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati kwa Kucheleweshewa Vitabu!

      Sio kila kitu tubishe ..kwa siku moja ama mbili mtu atasomaje na kuelewa kilichomo? Na inawezekana ndio maana kuna madudu mengi yanapitishwa san=babu ya ujanja ujanja kwenye sehemu nyeti na za muhimu ..hapa naona kigwa kakataa kuwapa ushirikiano tunamdhihaki ila kafanya jambo la msingi
      kwa kucheleweshewa vitabu kiasi hiki na kwa kuzingatia ukubwa na wingi wa mavitabu haya ya bajeti ni dhahiri hakuna mbunge mwenye spidi na uwezo wa kuisoma, kuimaliza na kuichambua bajeti hii kwa ufanisi na tija inayostahiki.
      JF the best place to be. and the POWER of God be with us all the time.

    21. #19
      English Learner's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st January 2012
      Location : Inside the Laptop
      Posts : 251
      Rep Power : 804
      Likes Received
      268
      Likes Given
      197

      Default

      A single qn to HK and other social media Policians; why are you increasingly mendering JF? If you managed to come and respond to both, senseble and stupid critiques then why failed to personally bring this realese as you did in other networks?

    22. #20
      HKigwangalla's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th February 2008
      Location : Dar es salaam, Tanzania
      Posts : 527
      Rep Power : 681
      Likes Received
      568
      Likes Given
      153

      Default Re: Kigwangalla asusa Kujadili Bajeti Ngazi ya Kamati kwa Kucheleweshewa Vitabu!

      Quote By English Learner
      This is a TRUTH and 100% a FACT to most JF members who blow the trumpet of critique.

      It is simple to condemn, critize, etc and most fool do
      sure. hapa wengi hawafanyi 'critique' bali 'criticism'; maana critique ni ya kuanazuoni zaidi na ni nzuri maana mnachambua kwa kina pros and cons na siyo kukosoa one sided tu
      Dr. Hamisi Kigwangalla, MD, MPH, MBA
      Mabadiliko ya kweli yataletwa na sisi...!

    Page 1 of 3 123 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...