Mh wewe ni waziri ambaye umeteuliwa juzi tu, inawezekana haujui nini kinaendelea ndani ya wizara yako. Sisi kama watanzania ni muda mrefu sana tumeilalamikia serikali yetu kuwa tunahitaji ndege kwa ajili ya safari za anga.
Ni juzi tu Katibu mkuu wako alitamka maneno kuwa ndege hiyo isiruke mpaka itemize mashart yote.hali ya kuwa ndege imetimiza masharti yanayotakiwa kuruka. Je katibu mkuu alikuwa na dhamira gani kuizuia ndege isiruke? Kama mdau wa usafiri wa anga ilitustua sana kuona katibu mkuu ambaye ndie mtendaji wizarani na mtegemewa na wananchi ndio anakuwa mtu wa kwanza kuikwamisha ndege ya watanzania isifanye kazi.
Wiki mbili baadae baada ya ndege ile aina ya B 737 – 500 kuanza safari zake DAR- JRO- MWZ-DAR tukasikia ndege ile imepokea vitisho kuwa itafanyiwa hujuma. Ni wiki moja sasa tangu vitisho hivo vitolewe, na leo tunaona DIRECT MR. CHIZI ambaye ndio ameisimamia ndege ile mpaka kuileta hapa nchini amesimamishwa kazi.
Kuna haja gani ya kumuondoa MR CHIZI katika nafasi ambaye tumeona matunda yake? Au ni kwa vile alikaidi amri ya katibu mkuu wake ya kutoiondoa ndege kwa visingizio kuwa haijatimiza mashart? Hali ya kuwa imetimiza? Au kosa lake ni kuisimamia hii ndege mpaka ikapatikana? Au ni kwa vile yeye katibu mkuu hakushirikishwa ipasavyo katika kuileta ndege hii?? Nina maswali mengi ya kujiuliza kuhusu huyu katibu mkuu na namna alivyo mfukuzisha kazi mr chizi.Kiukweli katibu mkuu anakitu kimejificha nyuma yake kuhusu hii ndege na ATCL kwa ujumla.
Mh Mwakyembe hujuma kwa ndege zina fanyika katika mazingira tofauti, katika kile katibu mkuu alidai kuwa “tutaona itafika wapi” sasa ndio ameanza kwa kukushawisi wewe ili kumsafisha DIRECTOR CHIZI ambaye ameileta kisha na ndege hiyo kurudi kwao ili yeye KATIBU MKUU anufaike anavyonufaika katika makampuni mengine ya NDEGE ambayo yanamtumia kuisambaratisha ndege hii.
Tuna wasi wasi na katibu mkuu huyu ambaye inaonekakana yupo nyuma ya kikundi Fulani ambacho kina mtumia ili kuiua ndege hii ambayo inatumika kufanya safari za ndani ya nchi.
Sisi kwetu hii ni hujuma kubwa ambayo imefanywa na kiongozi wetu wa serikalini bila kuangalia maslahi ya taifa na badala yake anaangalia maslahi yake binafsi.
Kama waziri wa wizara husika tunaomba ukae na wadau mbali mbali wa secta ya anga ikiwemo AIR TANZANIA ili upate maoni yao.Hatuja pendezwa na hatujafurahia maamuzi ya katibu mkuu huyo kukushawishi kumsimamisha kazi DIRECTOR CHIZI.
Ahsaante sana
Madau.

Reply With Quote


Follow Us Here