Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...

    Report Post
    Page 1 of 27 12311 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 531
    1. #1
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,737
      Rep Power : 12927
      Likes Received
      4443
      Likes Given
      7465

      Default Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...

      Nimevipima vyama vya upinzani kwenye mizania yangu ya upembuzi yakinifu na kubaini bila ya mashaka yoyote yale bado havipo tayari kimfumo kutupatia Raisi bora na hizi ndizo nondo zangu zilizonifikisha hapo..:-

      a) Vyama vyote vya upinzani vimeiga mfumo mbovu wa kidemokrasia wa ccm na vinaendeshwa kibabe-kibabe mno na huku wenzao wa ccm kuanzia 2010 walianza kujivua gamba la udikteta pale waliporuhusu wabunge wake wachaguliwe na wananchi moja kwa moja...ingawaje bado wana safari ndefu kwenye hili lakini lazima niwapongeze ccm kwa angalau kujaribu....rushwa na kuingiliwa na ngazi za juu katika maoni ya wananchi ni changamoto ambazo ccm itabidi waendelee kuzitafutia muarobaini wake.

      Kwenye hili vyama vya upinzani wapo nyuma na tumeona hata chadema bila ya kupitisha kura ya maoni kwa wapigakura wa Arusha wakitumia kauli za kidikteta kukejeli kura za wanachama wao Arusha pale kamati kuu yao ilipotengua madiwani wakaidi wa Arusha...well, chadema worshippers...that was not democracy at all...it was dictatorship.........face it now before it is too late.....Only the truth will set you free

      b) Vyama vyote vya siasa vyenye wabunge Bungeni vimekumbwa na dhoruba kali la wizi na ubadhirifu wa ruzuku ya hazina na hakuna uthibiti wa aina yoyote ile!!!!!

      Kwa mtazamo wangu kama wapinzani wameshindwa hata kusimamia kidogo ambacho tumewapa ni kwa upuuzi upi utushawishi kuwakabidhi nchi yote?

      Njaa ya viongozi wa upinzani ni kali kulikoni ya viongozi wa ccm ambao pamoja na bandubandu kweli humaliza gogo lakini ccm hawana uchu wa kututafuna kama upinzani walionao.....ccm vibosile wake wamekwisha shiba njaa siyo kali sana kwa kipimo cha malinganisho.................l ol

      c) Mchakato wa katiba mpya umenifungua macho hila na upofu wa wapinzani ambao waliipinga tume kwa vile wao hawajaweka mrija wao ndani yake na kunyonya Hazina baada ya CCM kuwaingiza kingi - au niseme mkenge? - hakuna anayehoji uhalali wa Tume ya kukusanya maoni.

      Wote wanaimba wimbo wa CCM wa ya kuwa tume tajwa haina uwalakini na sasa wamehamia kwenye mabunge mawili ambako wanaona mirija yao ni michache na kwa hiyo wanatafuta namna ya kuiongeza.

      Hii siyo demokrasia hata chembe bali ni ubinafsi tu...period. Mwanamageuzi wa kweli atadai haki hata kama yeye ni mwathirika wa hayo mageuzi siyo yule ambaye hujigeuza mpiga filimbi ya Hamelini pale anapoona masilahi yake yamepigwa na tufani kali sana...anachofanya ni kulinda tonge lake la ugali lisidondokee pabaya tu....lol hao kweli ni wababaishaji tu hawatufai kabisa.........

      USHAURI:

      Hivyo chama chochote kile cha siasa ambacho kitashirikisha wanachama wake katika kuteua viongozi watakaopeperusha bendera za vyama vyao katika ngazi zote ikiwemo ya URAISI, UBUNGE, UDIWANI hadi UENYEKITI WA KITONGOJI kina nafasi njema ya kutupatia viongozi bora...na kutumia utaratibu huohuo katika kuwavua madaraka itakuwa imepiga hatua katika demokrasia shirikishi.

      Have your say too...unaridhika na demokrasia ndani ya vyama vya siasa hasa hivi vya upinzani hata sasa kuviamini kutupatia Raisi na viongozi wengineo bora bila ya kutushirikisha grassroots?
      Last edited by Rutashubanyuma; 6th June 2012 at 12:01. Reason: spelling..................duh
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    2. Miaka 50

    3. #2
      Baija Bolobi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2009
      Location : Bosnia
      Posts : 612
      Rep Power : 719
      Likes Received
      325
      Likes Given
      0

      Default re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...

      Mbona umegeuka wakati jina lako ni "RUTASHUBANYUMA" yaani "Asiyerudi nyuma"?
      Kwa hiyo kwako wewe, CCM kuwavumilia/kuwaogopa mafisadi ndani ya chama na kuwaambia kuwa wapime na kuamua wenyewe ndiyo demokrasia?

      Ndugu yangu Ruta, hiyo unayosema kuwa demokrasia si demokrasia ni "Anarchic democrasy" ambayo inaweza kumpa uhuru baba mtu kumbaka binti yake huku ikiwanyima watu uhuru wa kuhoji hilo tendo. Think twice!
      HERI KUFIA MAWAZO YANAYOISHI KULIKO KUISHI KWA MAWAZO YALIYOKUFA.

    4. #3
      KakaKiiza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th February 2010
      Location : Here Where you see me!!
      Posts : 6,055
      Rep Power : 16331
      Likes Received
      2229
      Likes Given
      1267

      Default re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...

      Ndugu Rutashubanyuma sasa naona Noshubenyuma......Tofauti na maana ya kikwetu juu ya jina lako....

      Mimi nawasiwasi na uchambuzi wako katika siasa za hapa kwetu Tanzania kwakutumia kigezo cha chako kisichokuwa na mashiko!!CCM imekuwa madarakani nadhani zaidi ya miaka 40 Iweje leo ufananishe na chadema yenye miaka 5 ya maendeleo??CCM kwa ufupi ni madikiteta kuliko chama chochote Tanzania kwanza udikiteta wao nikatika mfumo mzima wa uongozi wa nchi kama haujatambua...

      Kifupi ni juu ya kauli za Nape alivyoenda Kusini na kumuagiza Waziri!!aliyeteuliwa na Rais!!!Hapo unaona udikiteta wapi umejikita CCM tazama walivyo kwapua mali za nchi hii!!Bado nasikitika kuwa mtazamo wako kwa upinzani siyo linganifu!!!....Nidemokrasia unaruhusiwa kuonge chochote bila kuvunja sheria!!
      Its only crazy who will be against to CDM!,only a fool who will fly CCM flag while is hungry!!

    5. #4
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,737
      Rep Power : 12927
      Likes Received
      4443
      Likes Given
      7465

      Default re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...

      Mbona umegeuka wakati jina lako ni "RUTASHUBANYUMA" yaani "Asiyerudi nyuma"?
      Kwa hiyo kwako wewe, CCM kuwavumilia/kuwaogopa mafisadi ndani ya chama na kuwaambia kuwa wapime na kuamua wenyewe ndiyo demokrasia?

      Ndugu yangu Ruta, hiyo unayosema kuwa demokrasia si demokrasia ni "Anarchic democrasy" ambayo inaweza kumpa uhuru baba mtu kumbaka binti yake huku ikiwanyima watu uhuru wa kuhoji hilo tendo. Think twice!
      MziziMkavu tupo wote mie siongelei ufisadi kwa sababu uko kwenye vyama vyote kama nilvyobaini ila ccm wao kwa vile wako madarakani ni rahisi kwa wapinzani kuibua mapungufu yao ambayo wao wakiingia madarakani leo watakuwa ni kioja nikiona jinsi ambavyo wanedesha mambo yao kwa ubinafsi mkubwa mno............

      hiyo hoja yako ya pili mie sijaielewa.................... kuhusu kugeuka mie sitetei chama chochote kile hata ccm huwa nawaangushia makombora lakini lazima niweke hadharani mapungufu ya vyama vya upinzani kuwa havipo tayari kukamata dola mpaka pale vitakapopanua demokrasia ndani ya vyama vyao na kuwa bora kuzidi ya ccm..............
      MziziMkavu, NasDaz and wahida like this.
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    6. #5
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,212
      Rep Power : 19215
      Likes Received
      8170
      Likes Given
      26659

      Default re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...

      Mkuu Rutashubanyuma Kwa Mawazo yangu mimi Ningependa Rais wa nchi asitoke chama chochote kile kiwe cha chama cha C.C.M. Au CUF au Chadema au TPL. Au NccR Mageuzi kama ningelikuwa mimi mmoja wapo wanayepanga kutunga

      Katiba ya Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania ningelitowa huo ushauri wangu. Nasema hivyo kwa sababu zangu si umeona Rais wa C.C.M. mpaka hii leo kuna maendeleo gani hapo nyumbani? zaidi ya umasikini uliojaa kila sehemu ? Sasa hata ikifika wakati wa uchaguzi ujao

      kwa mfano chama chochote kile cha upinzani kitakacho shinda hakutokuwa na mabadiliko yoyote yale ya haraka kwa sababu Rais atakaye kuwepo madarakani ndie anacho kiongoza hicho chama kilichoshinda katika uchaguzi hata Mkimlaumu vipi mabadiliko

      hayawezi kuja kwa haraka kama mnavyo mnavyotaka. Lakini ikiwa Rais hatakuwa na chama chochote kile ila tu huyo Rais kachaguliwa na Wananchi huyo Rais atakuwa hana upendeleo wowote ule kwani atakuwa ni Rais Mkweli na Muadilifu na asiyekuwa na chama chohote

      anacho kipendelea na huyo Rais akifanya kosa ni Rahisi kukosolewa au hata kujiuzulu kuliko Rais anayechaguliwa na chama kinachotawala akikosea mna mngojea mpaka wakati wa uchaguzi ndio mumng'owe madaraka yake huo ndio ushauri wangu mimi asante.
      Waberoya and Rutashubanyuma like this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      Filipo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Location : Kiding'a
      Posts : 6,362
      Rep Power : 18618
      Likes Received
      3525
      Likes Given
      1731

      Default re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...

      Kuhusu swala la madiwani wa Arusha.

      Mkuu, nadhani hapa tunatafsiri vibaya demokrasia. Tunawachagua viongozi wa kutuwakilisha. Na tunawachagua wale tunaoamini watawakilisha mawazo yetu. Madiwani wa Arusha walionekana dhahiri kuwa kuna harufu ya rushwa na wananchi walikuwa wanasema waziwazi hapa jijini. Waliposhauriwa, walipoonywa hawakusikia.

      Viongozi wetu wanajua tulichokuwa tunahitaji na kwa niaba yetu wakatimiza mahitaji yetu! Yaani wametuwakilisha kwenye ngazi ya maamuzi. Sidhani kama demokrasia ni kura ya maoni kwa kila jambo. Kuwa na viongozi wasioweza kutoa maamuzi pia ni tatizo kuliko demokrasia unayoisema.

      Ni hayo tu!

    9. #7
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,737
      Rep Power : 12927
      Likes Received
      4443
      Likes Given
      7465

      Default re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...

      Quote By KakaKiiza
      Ndugu Rutashubanyuma sasa naona Noshubenyuma......Tofauti na maana ya kikwetu juu ya jina lako....

      Mimi nawasiwasi na uchambuzi wako katika siasa za hapa kwetu Tanzania kwakutumia kigezo cha chako kisichokuwa na mashiko!!CCM imekuwa madarakani nadhani zaidi ya miaka 40 Iweje leo ufananishe na chadema yenye miaka 5 ya maendeleo??CCM kwa ufupi ni madikiteta kuliko chama chochote Tanzania kwanza udikiteta wao nikatika mfumo mzima wa uongozi wa nchi kama haujatambua...

      Kifupi ni juu ya kauli za Nape alivyoenda Kusini na kumuagiza Waziri!!aliyeteuliwa na Rais!!!Hapo unaona udikiteta wapi umejikita CCM tazama walivyo kwapua mali za nchi hii!!Bado nasikitika kuwa mtazamo wako kwa upinzani siyo linganifu!!!....Nidemokrasia unaruhusiwa kuonge chochote bila kuvunja sheria!!
      KakaKiiza......be real........ninachongelea ni mfumo wa kidemokrasia kwanza siyo kweli chadema wapo kwa miaka 5 tu walikuwepo kuanzia 1993-95 sasa hiyo ni karibu miaka 20 hivi wamefanya nini kuimarisha demokrasia ndani ya chama chao................angalia mbowe jinsi alivyojirundikia madaraka... yeye ndiye kinara bunggeni na ndani ya chama akija majukwaani anahubiri kufuta kofia mbili mbili wakati yeye kavaa tatu tau.

      Huo ni unafiki ambao lazima tuusema tu bila ya kujali mapenzi ya chama...........
      zomba, MziziMkavu and Ritz like this.
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    10. #8
      Imany John's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th July 2011
      Posts : 1,971
      Rep Power : 2978
      Likes Received
      471
      Likes Given
      4

      Default

      Quote By Rutashubanyuma
      MziziMkavu tupo wote mie siongelei ufisadi kwa sababu uko kwenye vyama vyote kama nilvyobaini ila ccm wao kwa vile wako madarakani ni rahisi kwa wapinzani kuibua mapungufu yao ambayo wao wakiingia madarakani leo watakuwa ni kioja nikiona jinsi ambavyo wanedesha mambo yao kwa ubinafsi mkubwa mno............

      hiyo hoja yako ya pili mie sijaielewa.................... kuhusu kugeuka mie sitetei chama chochote kile hata ccm huwa nawaangushia makombora lakini lazima niweke hadharani mapungufu ya vyama vya upinzani kuwa havipo tayari kukamata dola mpaka pale vitakapopanua demokrasia ndani ya vyama vyao na kuwa bora kuzidi ya ccm..............
      Ccm hailiki hata ikapakwa blue band

    11. #9
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,737
      Rep Power : 12927
      Likes Received
      4443
      Likes Given
      7465

      Default re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...

      Mkuu@Rutashubanyuma Kwa Mawazo yangu mimi Ningependa Rais wa nchi asitoke chama chochote kile kiwe cha chama cha C.C.M. Au CUF au Chadema au TPL. Au NccR Mageuzi kama ningelikuwa mimi mmoja wapo wanayepanga kutunga

      Katiba ya Jamhuri ya Muungano Wa Tanzania ningelitowa huo ushauri wangu. Nasema hivyo kwa sababu zangu si umeona Rais wa C.C.M. mpaka hii leo kuna maendeleo gani hapo nyumbani? zaidi ya umasikini uliojaa kila sehemu ? Sasa hata ikifika wakati wa uchaguzi ujao

      kwa mfano chama chochote kile cha upinzani kitakacho shinda hakutokuwa na mabadiliko yoyote yale ya haraka kwa sababu Rais atakaye kuwepo madarakani ndie anacho kiongoza hicho chama kilichoshinda katika uchaguzi hata Mkimlaumu vipi mabadiliko

      hayawezi kuja kwa haraka kama mnavyo mnavyotaka. Lakini ikiwa Rais hatakuwa na chama chochote kile ila tu huyo Rais kachaguliwa na Wananchi huyo Rais atakuwa hana upendeleo wowote ule kwani atakuwa ni Rais Mkweli na Muadilifu na asiyekuwa na chama chohote

      anacho kipendelea na huyo Rais akifanya kosa ni Rahisi kukosolewa au hata kujiuzulu kuliko Rais anayechaguliwa na chama kinachotawala akikosea mna mngojea mpaka wakati wa uchaguzi ndio mumng'owe madaraka yake huo ndio ushauri wangu mimi asante.
      raisi atoke mahali popote ni sahihi hata mgombea binafsi lakini kusema asitoke kwenye vyama vya siasa hiyo itakuwa kubinya demokrasia.................... ...maendeleo ina maelezo mengi ya ndani na nje........kama raia wa utamaduni wa kubeza kazi hakuna maendeleo.....nasiye tukiri tu wavivu sana ....pita mji wowoteule angalia watu walivyofurika barabarani wengi wao hawataki kazi ..................... MziziMkavu
      MziziMkavu likes this.
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    12. #10
      Mvaa Tai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th August 2009
      Location : Ngudu, Mwanza
      Posts : 3,459
      Rep Power : 1189
      Likes Received
      1435
      Likes Given
      939

      Default re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...

      Quote By Rutashubanyuma
      Nimevipima vyama vya upinzani kwenye mizania yangu ya upembuzi yakinifu na kubaini ....blah....blah.............. ...:-
      Amini usiamini CCM inajukumu la kutupatia Raisi bora mwaka 2015...........
      Una haki ya kusema hivyo kwa kuwa una maoni kama great thinker, binafsi naamini hawajahi kupitisha Rais asiye bora kwa mitazamo yao.....na hao marais bora wao ndiyo wameifikisha nchi mahala hapa.....kwasababu wameshindwa binafsi naona ni heri tuwajaribishe watu wengine kwasababu....wanaweza wakafeli au kufaulu, tofauti na CCM ambayo tayari tumekuwa na uhakika wa wao kufeli miaka yoote.

      Madhaifu machache ya Vyama vya Upinzani haya halalishi udhaifu mkubwa wa CCM. Hivi kweli hii ni nchi kweli Rais wa nchi anawataka watu walioiba Mabilioni ya Shiringi wayarudishe bila adhabu na hakuna ripoti itolewayo kama wanarudisha au la na kama wamerudisha ni kwa kiasi gani.

      Rutashubanyuma
      mimi na dream CCM iondoke madarakani tuwape nafasi watu wengine nao wakishindwa basi niamini na ku-conclude kwamba Tanzania tuna Tatizo la Human resources. Nichukua uraia wa Rwanda.
      Mnang'oa meno ya Tembo ili mukayauze, mnang'oa meno na Kucha za Watanzania wasio na hatia ili iweje?

    13. #11
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,737
      Rep Power : 12927
      Likes Received
      4443
      Likes Given
      7465

      Default re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...

      Quote By Filipo
      Kuhusu swala la madiwani wa Arusha.

      Mkuu, nadhani hapa tunatafsiri vibaya demokrasia. Tunawachagua viongozi wa kutuwakilisha. Na tunawachagua wale tunaoamini watawakilisha mawazo yetu. Madiwani wa Arusha walionekana dhahiri kuwa kuna harufu ya rushwa na wananchi walikuwa wanasema waziwazi hapa jijini. Waliposhauriwa, walipoonywa hawakusikia.

      Viongozi wetu wanajua tulichokuwa tunahitaji na kwa niaba yetu wakatimiza mahitaji yetu! Yaani wametuwakilisha kwenye ngazi ya maamuzi. Sidhani kama demokrasia ni kura ya maoni kwa kila jambo. Kuwa na viongozi wasioweza kutoa maamuzi pia ni tatizo kuliko demokrasia unayoisema.

      Ni hayo tu!
      Filipo,

      Viongozi hawapaswi kutenguliwa na vikao ambavyo havikuwachagua.........kama viongozi wa matatazo basi tuulizwe siye na wala siyo kamati Kuu ya Chadema ambayo hakuna hata mpigakura wetu kule........wa jiji la Arusha..........hiyo ndiyo misingi ya demokrasia.... haiwezekani wakaazi wa nje ya jiji la Arusha watuchagulie nani anafaa kutuongoza huo ni uwakilisha haramu tu...... usiutetee...
      Filipo likes this.
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    14. #12
      Sometimes's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th December 2010
      Posts : 1,372
      Rep Power : 761
      Likes Received
      233
      Likes Given
      39

      Default re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...

      Labda wagombea watokee mbinguni!
      Rutashubanyuma likes this.

    15. #13
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,212
      Rep Power : 19215
      Likes Received
      8170
      Likes Given
      26659

      Default re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...

      Quote By Rutashubanyuma
      KakaKiiza......be real........ninachongelea ni mfumo wa kidemokrasia kwanza siyo kweli chadema wapo kwa miaka 5 tu walikuwepo kuanzia 1993-95 sasa hiyo ni karibu miaka 20 hivi wamefanya nini kuimarisha demokrasia ndani ya chama chao................angalia mbowe jinsi alivyojirundikia madaraka.................yeye ndiye kinara bunggeni na ndani ya chama akija majukwaani anahubiri kufuta kofia mbili mbili wakati yeye kavaa tatu tau.huo ni unafiki ambao lazima tuusema tu bila ya kujali mapenzi ya chama...........
      Mkuu Rutashubanyuma,

      Pamoja na yote hayo unayoyasema lakini kwa sasa C.C.M. imezeeka tunataka chama kingine chochote kije kitawale mkuu hatupo sisi Urusi tupo Afrika Mashariki hatupo Zimbambwe tupo Tanzania Mkuu tunataka mabadiliko na Maendeleo C.C.M. tangu iundwe sasa yapata miaka 35 hakuna Maendeleo yoyote yale Chama cha C.C.M kimesha pitwa na wakati tungoje chama kingine Tuyavue Mkuu Magamba tuvae People in Power Mkuu kila lilio na Mwanzo halikosi kuwa na mwisho. Waswahili wamesema Ngoma ikivuma sana mwisho hupasuka C.C.M hu ndio mwisho wao imekalia kuti kavu mkuu samahani kama nitakukwaza.
      Rutashubanyuma and jouneGwalu like this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    16. #14
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,737
      Rep Power : 12927
      Likes Received
      4443
      Likes Given
      7465

      Default re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...

      Quote By Ezan
      Una haki ya kusema hivyo kwa kuwa una maoni kama great thinker, binafsi naamini hawajahi kupitisha Rais asiye bora kwa mitazamo yao.....na hao marais bora wao ndiyo wameifikisha nchi mahala hapa.....kwasababu wameshindwa binafsi naona ni heri tuwajaribishe watu wengine kwasababu....wanaweza wakafeli au kufaulu, tofauti na CCM ambayo tayari tumekuwa na uhakika wa wao kufeli miaka yoote.

      Madhaifu machache ya Vyama vya Upinzani haya halalishi udhaifu mkubwa wa CCM. Hivi kweli hii ni nchi kweli Rais wa nchi anawataka watu walioiba Mabilioni ya Shiringi wayarudishe bila adhabu na hakuna ripoti itolewayo kama wanarudisha au la na kama wamerudisha ni kwa kiasi gani.

      Rutashubanyuma
      mimi na dream CCM iondoke madarakani tuwape nafasi watu wengine nao wakishindwa basi niamini na ku-conclude kwamba Tanzania tuna Tatizo la Human resources. Nichukua uraia wa Rwanda.
      Ezan sijasema marasis wa CCM waliotangulia walikuwa bora ila sasa wanayo nafasi ya kutupatia raisi bora kama watapanua wigo la demokrasia.......ungelikuwa umenielewa ungelifahamu hao wote waliotangulia walikuwa ni bomu kwa sababu wanachama wa kawaida wa ccm hawakushiriki katika kuchagua kiongozi bora...
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    17. #15
      MziziMkavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2009
      Location : European Union
      Posts : 22,212
      Rep Power : 19215
      Likes Received
      8170
      Likes Given
      26659

      Default re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...

      Quote By Rutashubanyuma
      Ezan sijasem marasis wa ccm waliotangulia walikuwa bora ila sasa wanayo nafasi ya kutupatia raisi bora kama watapanua wigo la demokrasia.......ungelikuwa umenielewa ungelifahamu hao wote waliotangulia walikuwa ni bomu kwa sababu wanachama wa kawaida wa ccm hawakushiriki katika kuchagua kiongozi bora............. Ezan
      Hawezi Rais Bora kutoka tena C.C.M. You Forget it. Tunataka Rais atoke sehemu yoyote ile sio tena Rais atoke C.C.M imesha zeeka Mkuu .............................. .. Rutashubanyuma
      Rutashubanyuma and jouneGwalu like this.
      Only Do What Your Heart Tells You




      Allah
      Has Not Revealed A Disease without Treatment....
      (Prevention is Better Than Cure) Email Address yangu hii [email protected]

    18. #16
      Mvaa Tai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th August 2009
      Location : Ngudu, Mwanza
      Posts : 3,459
      Rep Power : 1189
      Likes Received
      1435
      Likes Given
      939

      Default re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...

      Quote By Rutashubanyuma
      Ezan sijasem marasis wa ccm waliotangulia walikuwa bora ila sasa wanayo nafasi ya kutupatia raisi bora kama watapanua wigo la demokrasia.......ungelikuwa umenielewa ungelifahamu hao wote waliotangulia walikuwa ni bomu kwa sababu wanachama wa kawaida wa ccm hawakushiriki katika kuchagua kiongozi bora............. Ezan
      Ulichosema ni kwamba CCM inajukumu hilo, hukusema wana nafasi ya kutupatia Rais bora kama ni suala la nafasi kila chama kina nafasi, ila kwasababu CCM imepewa hiyo nafasi miaka mingi na haijaitumia vizuri uwezekano wa kupewa nafasi hiyo tena ni mdogo sana watu tupo tayari ku-take risk kwa chama kingine hata TLP
      Mnang'oa meno ya Tembo ili mukayauze, mnang'oa meno na Kucha za Watanzania wasio na hatia ili iweje?

    19. #17
      Omonto wa-hene's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 150
      Rep Power : 390
      Likes Received
      39
      Likes Given
      37

      Default re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...

      Quote By Rutashubanyuma
      MziziMkavu tupo wote mie siongelei ufisadi kwa sababu uko kwenye vyama vyote kama nilvyobaini ila ccm wao kwa vile wako madarakani ni rahisi kwa wapinzani kuibua mapungufu yao ambayo wao wakiingia madarakani leo watakuwa ni kioja nikiona jinsi ambavyo wanedesha mambo yao kwa ubinafsi mkubwa mno............

      hiyo hoja yako ya pili mie sijaielewa.................... kuhusu kugeuka mie sitetei chama chochote kile hata ccm huwa nawaangushia makombora lakini lazima niweke hadharani mapungufu ya vyama vya upinzani kuwa havipo tayari kukamata dola mpaka pale vitakapopanua demokrasia ndani ya vyama vyao na kuwa bora kuzidi ya ccm..............
      Sikubaliani asilani na hoja za Watanzania wengi wenye uoga wa kubadili mfumo wa utawala kwa maelezo chapwa eti heri tuendelee na wezi hawa hawa tuliowazoea (Chama Cha Magamba) kuliko kuleta wezi wapya wa Upinzani. Astaghfilullah!! Hivi ndo kusema wizi ni sifa kuu ya Watanzania? Kwamba kila anayeingia madartakani lazima aibe?

      Kama hivi ndivyo bado tunadhani ipo haja ya kuwabadili 'wezi' kwa sababu wapinzani wana sera ya kuunda serikali ndogo na hivyo kupunguza mianya ya wizi kuliko hawa Chama Cha Magamba ambao ukubwa wa serikali hauelezeki maana wapo viongozi rasmi na wasio rasmi. Wasio rasmi ni kama watoto, mashemeji, vidosho, mabest, makada, nyumba mbhoke.......Na woote hawa ni wezi kama alivyobainisha Rutashubanyuma

    20. #18
      Sangarara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 3,370
      Rep Power : 1212
      Likes Received
      1214
      Likes Given
      1591

      Default re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...

      wengine tunaamini katika mfumo wa kidicteta ndugu yangu, na katika hili ninaamini kwamba mfumo wa kimocrasia sisi tumerukia gari kwa mbele, mfumo wa kidemocrasia unaambatana na elimu, ni katika jamii zilizoelimika pekee ambako asilimia kubwa ya wananchi wanafanya rational decisions ndiko wanakofaidika na mfumo wa kidemocrasia.

      Moja ya tatizo la democrasia ni kama ulilolionyesha wewe, kwamba umefumbia macho matatizo yoooote ambayo CCM imelifikisha Taifa letu na kuangalia weaknesses za kuhesabu za wapinzani kisha umeamua kwamba CCM ni bora zaidi ya wapinzani, katika hili umejiweka kundi moja na wale wanaofanya maamuzi baada ya kula wali na kugombania kanga.

    21. #19
      james chapacha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd April 2012
      Posts : 478
      Rep Power : 455
      Likes Received
      102
      Likes Given
      24

      Default re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...

      Rutashubanyuma WAGAISA,chonka wagaima omugusha!



      ,
      Rutashubanyuma likes this.

    22. #20
      Ndallo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st October 2010
      Location : LaRusa
      Posts : 4,146
      Rep Power : 6368
      Likes Received
      1489
      Likes Given
      423

      Default re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...

      Sasa nimshagundua nini maana ya kuwa na mgombea binafsi!
      Rutashubanyuma likes this.
      '' Mtu ni Utu sio Kitu''

    Page 1 of 27 12311 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...