Mkuu
Chesty, hapa ni kama unatwanga maji kwenye kinu..
ruta,
Waberoya et al...hawako peke yao. Mshuhudie na huyu anayeitwa
zomba;
Hawa ni wa kuwaacha tu ...si watu wa kuhangaika nao, Tsunami ya Chadema itawasomba tu. Eti CCM kuwasomba watu kwenye malori na kuwapa posho ili wahudhurie mikutano, ni haki yake kwani inatumia uwezo wake mkubwa wa kifedha. Eti chama cha kidemokrasia hakitakiwi kuchukua hatua dhidi ya wanachama wake kata kama wanasinginya katiba kwa maslahi binafsi.
Ndio maana CCM imekuwa kimbilio la wahalifu kwani huko kuna kulindana, mhalifu gani atamchukulia hatua mhalifu mwenzake? Matokeo yake wezi wanabembelezwa warudishe walichokwiba, mafisadi wanaokumbatiwa wasije wakaiyumbisha dola na wauaji wa raia wanazawadiwa kwa kupandishwa vyeo. CCM inawahimiza wananchi kuuza utu wao kwa sinia la pilau, kipande cha kanga na kopo la chumvi.
Sasa CCM imefikia hatua ambayo imetekwa nyara na wahalifu na mtu yeyote mwenye nia ya kuwatetea wananchi ndiye mbaya, hatakiwi humo. Vyombo vya kuwalinda wananchi na mali zao vimegeuka na kuwa vya kidhalilishaji dhidi ya raia wema wanaopinga uonevu. Tazama Chama hiki cha Kifisadi kinavyotetewa humu na baadhi ya wachangiaji hadi mtu anathubutu kuanzisha mada kama hii kukitetea.
Lakini linalosikitisha kuliko yote ni kuwa kina wanazi ambao pamoja na shida zote hizi na jitihada za Chadema kuwaelimisha wameshindwa kufunguka macho. Ni kama wamelogwa vile, wana imani kuwa kilichooza bado kina ubani, wana imani kuwa ipo siku mlafi atashiba na kuacha tabia yake ya ulafi, wana imani kuwa aliyeonja nyama ya binadamu ataacha...! Lakini siku ya kiama inakuja na hilo wakae wakilijua.
Follow Us Here