Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...
Nimevipima vyama vya upinzani kwenye mizania yangu ya upembuzi yakinifu na kubaini bila ya mashaka yoyote yale bado havipo tayari kimfumo kutupatia Raisi bora na hizi ndizo nondo zangu zilizonifikisha hapo..:-
a) Vyama vyote vya upinzani vimeiga mfumo mbovu wa kidemokrasia wa ccm na vinaendeshwa kibabe-kibabe mno na huku wenzao wa ccm kuanzia 2010 walianza kujivua gamba la udikteta pale waliporuhusu wabunge wake wachaguliwe na wananchi moja kwa moja...ingawaje bado wana safari ndefu kwenye hili lakini lazima niwapongeze ccm kwa angalau kujaribu....rushwa na kuingiliwa na ngazi za juu katika maoni ya wananchi ni changamoto ambazo ccm itabidi waendelee kuzitafutia muarobaini wake.
Kwenye hili vyama vya upinzani wapo nyuma na tumeona hata chadema bila ya kupitisha kura ya maoni kwa wapigakura wa Arusha wakitumia kauli za kidikteta kukejeli kura za wanachama wao Arusha pale kamati kuu yao ilipotengua madiwani wakaidi wa Arusha...well, chadema worshippers...that was not democracy at all...it was dictatorship.........face it now before it is too late.....Only the truth will set you free
b) Vyama vyote vya siasa vyenye wabunge Bungeni vimekumbwa na dhoruba kali la wizi na ubadhirifu wa ruzuku ya hazina na hakuna uthibiti wa aina yoyote ile!!!!!
Kwa mtazamo wangu kama wapinzani wameshindwa hata kusimamia kidogo ambacho tumewapa ni kwa upuuzi upi utushawishi kuwakabidhi nchi yote?
Njaa ya viongozi wa upinzani ni kali kulikoni ya viongozi wa ccm ambao pamoja na bandubandu kweli humaliza gogo lakini ccm hawana uchu wa kututafuna kama upinzani walionao.....ccm vibosile wake wamekwisha shiba njaa siyo kali sana kwa kipimo cha malinganisho.................l ol
c) Mchakato wa katiba mpya umenifungua macho hila na upofu wa wapinzani ambao waliipinga tume kwa vile wao hawajaweka mrija wao ndani yake na kunyonya Hazina baada ya CCM kuwaingiza kingi - au niseme mkenge? - hakuna anayehoji uhalali wa Tume ya kukusanya maoni.
Wote wanaimba wimbo wa CCM wa ya kuwa tume tajwa haina uwalakini na sasa wamehamia kwenye mabunge mawili ambako wanaona mirija yao ni michache na kwa hiyo wanatafuta namna ya kuiongeza.
Hii siyo demokrasia hata chembe bali ni ubinafsi tu...period. Mwanamageuzi wa kweli atadai haki hata kama yeye ni mwathirika wa hayo mageuzi siyo yule ambaye hujigeuza mpiga filimbi ya Hamelini pale anapoona masilahi yake yamepigwa na tufani kali sana...anachofanya ni kulinda tonge lake la ugali lisidondokee pabaya tu....lol hao kweli ni wababaishaji tu hawatufai kabisa.........
USHAURI:
Hivyo chama chochote kile cha siasa ambacho kitashirikisha wanachama wake katika kuteua viongozi watakaopeperusha bendera za vyama vyao katika ngazi zote ikiwemo ya URAISI, UBUNGE, UDIWANI hadi UENYEKITI WA KITONGOJI kina nafasi njema ya kutupatia viongozi bora...na kutumia utaratibu huohuo katika kuwavua madaraka itakuwa imepiga hatua katika demokrasia shirikishi.
Have your say too...unaridhika na demokrasia ndani ya vyama vya siasa hasa hivi vya upinzani hata sasa kuviamini kutupatia Raisi na viongozi wengineo bora bila ya kutushirikisha grassroots?
Last edited by Rutashubanyuma; 6th June 2012 at 12:01.
Reason: spelling..................duh
Re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...
By Mwita Maranya
Huwezi kulinganisha hoja zinazotolewa na wabunge wa chadema na wale wa ccm. Unatambua kwamba ccm wanatumia wingi wao bungeni kupitisha maamuzi lakini kwa hoja chadema inawagaragaza. Mfano wa hivi karibuni ni sheria ya mchakato wa katiba mpya, uliona shughuli ya chadema!
si kwamba hakui hili anajua kabisa isipokuwa anajiazimsha kubishi....kila kitu anakiona na anakijua...kuna mahali nimemwambia aina hii ya ubishi na ujinga unaitwa invincible ignorance akasema namtukana matusi ya nguini.....
thead yake imejaa kufikirika na anachanganya mambo sana..kwa kifupi huyu jama haijui siasa
Edson kama uwezo hawana nifanyaje? Mbeleko za kuwabeba cdm zimenikatia............lol
Rutashubanyuma Chuki yako kwa Chadema imekupofusha wala huoni kabisa.
Kuna chama kinachopenda mbereko zaidi ya ccm? Polisi, usalama wa ccm na kubwa lao tume ya uchaguzi.
Chadema imekuwa ikijitegemea kwa kusimama yenyewe bila msaada wa yeyote. Sasa wachambuzi uchwara mnajaribu kujenga hoja legelege dhidi yake.
Viongozi hawapaswi kutenguliwa na vikao ambavyo havikuwachagua.........kama viongozi wa matatazo basi tuulizwe siye na wala siyo kamati Kuu ya Chadema ambayo hakuna hata mpigakura wetu kule........wa jiji la Arusha..........hiyo ndiyo misingi ya demokrasia.... haiwezekani wakaazi wa nje ya jiji la Arusha watuchagulie nani anafaa kutuongoza huo ni uwakilisha haramu tu...... usiutetee...
Ok! Hapo nimekupata sawasawa!kumbe una maana kuwa kuwe na election mara mbili?ya kumweka mtu madarakani,na kumtoa mtu madarakani!!!!hiyo ndiyo demokrasia unayoona sahihi?Tanzania itakuwa nchi ya kwanza duniani kuwa na demokrasia ya ki hivyo! Je na hao tuliowachagua kutuwakilisha watafanya kazi gani? Ptuuuu
si kwamba hakui hili anajua kabisa isipokuwa anajiazimsha kubishi....kila kitu anakiona na anakijua...kuna mahali nimemwambia aina hii ya ubishi na ujinga unaitwa invincible ignorance akasema namtukana matusi ya nguini.....
thead yake imejaa kufikirika na anachanganya mambo sana..kwa kifupi huyu jama haijui siasa
Kweli kabisa huyu msisiem anauona ukweli dhahiri shairi lakini kwa makusudi kabisa anaamua kubisha.
Alivyo na misifa ya kijinga anajiona yeye kasoma kuliko wanachadema.
Kama kusoma kwenyewe ndio kuwa na mawazo ama akili kama hii ni bora mtu usisome kabisa.
Mara ajiite political analyst mara ajiite mwanasheria. Yani ni ujanja ujanja tu!
Ezan sijasema marasis wa CCM waliotangulia walikuwa bora ila sasa wanayo nafasi ya kutupatia raisi bora kama watapanua wigo la demokrasia.......ungelikuwa umenielewa ungelifahamu hao wote waliotangulia walikuwa ni bomu kwa sababu wanachama wa kawaida wa ccm hawakushiriki katika kuchagua kiongozi bora...
Naona sasa JF imeshakuwa kijiwe cha propaganda. Baada ya kuisoma thread yako na utetesi wako, jambo moja nimeligundua, kwamba unataka kutufanya kuwa sisi Wtz wote bado ni wadanganyika. Hapa hashawishiki mtu kwa hoja za mchumia tumbo kama wewe. Kitendo cha kushaushi watu kuamini kuwa ccm kinaweza kutuletea rais bora 2015 kinaonyesha jinsi usivyo mzalendo, usivyokuwa na uchungu na rasili mali za nchi hii. Unataka kutuaminisha kuwa ukiwa na ng'ombe wako ukampa mtu uliyemwamini anywe maziwa na amtunze na kila ndama atakayezaliwa amtunze ili waongezeke ili mwisho wa siku maziwa mengi yapatikane na watu wote waweze kupata yakutosha. Yule mtu anageuka na kuwa upande mmoja anakuwa kupe kunyonya damu ya yule ng'ombe, na kwa upande mwingine anamkamua yule ng'ombe mpaka damu. Na maziwa anayoyakamua anakunywa akishashiba badala ya kuwapa nduguzeke yeye anatoko na kwenda kijiji cha jirani na kuwaambia njooni mchukuwe maziwa safi yasiyogoshiwa kwa bei iliyosawa na bure. Halafu kila ndama anayezaliwa anamchinja na kugawana nyama na marafiki zake, kitu kinyume na makubaliano na yule mwenye ng'ombe. Je, unataka kudanganya kwa unafiki wako kuwa pamoja na kubaini makosa hayo yote utaendelea kumuamini huyo mtu na kumpenda, na kuendelea kumtunza huyo ng'o pamoja na kuwa umempa nafasi ya kujirudi lakini ameshindwa kufanya hivyo? Kama jibu lako ni ndiyo basi wewe si dhani kama we ni mtz, nahisi utakuwa mwaalishababu fulani, usiyeitakia nchi hii mema!!!
Ezan sijasema marasis wa CCM waliotangulia walikuwa bora ila sasa wanayo nafasi ya kutupatia raisi bora kama watapanua wigo la demokrasia.......ungelikuwa umenielewa ungelifahamu hao wote waliotangulia walikuwa ni bomu kwa sababu wanachama wa kawaida wa ccm hawakushiriki katika kuchagua kiongozi bora...
Naona sasa JF imeshakuwa kijiwe cha propaganda. Baada ya kuisoma thread yako na utetesi wako, jambo moja nimeligundua, kwamba unataka kutufanya kuwa sisi Wtz wote bado ni wadanganyika. Hapa hashawishiki mtu kwa hoja za mchumia tumbo kama wewe. Kitendo cha kushaushi watu kuamini kuwa ccm kinaweza kutuletea rais bora 2015 kinaonyesha jinsi usivyo mzalendo, usivyokuwa na uchungu na rasili mali za nchi hii. Unataka kutuaminisha kuwa ukiwa na ng'ombe wako ukampa mtu uliyemwamini anywe maziwa na amtunze na kila ndama atakayezaliwa amtunze ili waongezeke ili mwisho wa siku maziwa mengi yapatikane na watu wote waweze kupata yakutosha. Yule mtu anageuka na kuwa upande mmoja anakuwa kupe kunyonya damu ya yule ng'ombe, na kwa upande mwingine anamkamua yule ng'ombe mpaka damu. Na maziwa anayoyakamua anakunywa akishashiba badala ya kuwapa nduguzeke yeye anatoko na kwenda kijiji cha jirani na kuwaambia njooni mchukuwe maziwa safi yasiyogoshiwa kwa bei iliyosawa na bure. Halafu kila ndama anayezaliwa anamchinja na kugawana nyama na marafiki zake, kitu kinyume na makubaliano na yule mwenye ng'ombe. Je, unataka kudanganya kwa unafiki wako kuwa pamoja na kubaini makosa hayo yote utaendelea kumuamini huyo mtu na kumpenda, na kuendelea kumtunza huyo ng'o pamoja na kuwa umempa nafasi ya kujirudi lakini ameshindwa kufanya hivyo? Kama jibu lako ni ndiyo basi wewe si dhani kama we ni mtz, nahisi utakuwa mwaalishababu fulani, usiyeitakia nchi hii mema!!!
Re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...
Kaka Rutashubanyumaasante sana kwa maelezo yako mimi ni mnazi mkubwa sana wa CCM na ninakiri kuna mapungufu ndani ya chama. pamoja na mapungufu yake hanifanyi mimi niichukie CCM. CCM ndio chama pekee ambacho mtu huwezi kutabiri Rais ajae atakuwa nani tofauti na CUF na CDM wagombea wao wanajulikana tena akitokea mwanachama mwingine anataka kugombea atapata habari yake kawaulizeni akina Zito. Mbowe yeye hata kukosolewa ndani ya chama ni balaa lazima tu atakutoa kundini shahidi marehemu Chacha Wangwe. Sasa tujiulize Kiongozi ambae hapendi kukoselewa ndani ya chama je itakuje akipewa nchi?
Hakika CDM ikipewa nchi basi ndo itakuwa kwisheni kwa watz
Re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...
Ruta,
Hoja zako hazina hoja ni vioja tu. Hivi hiyo demokrasia ya ndani ya ccm ambayo inaweza kutuletea viongozi bora kuliko upinzni ni upi? Kitu cha kwanza uelewe ndani ya ccm hiyo demokrasi haiwezi kumleta kiongozi bora. Kiongozi bora manake unamwongelea mtu asiye na makundi na wezi, asiyependa rushwa, ambaye atafanya uchaguzi pasipo kuhonga na akishindwa atakubali matokeo. Ambaye atatimua wezi popote walipokuwepo na kurejesha madaraka kwa wananchi badala ya kuhodhiwa na serikali kuu hasas rais. Can ccm do that? BIG NO.
Kwa kifupi kiongozi bora unayemwongelea na kumchora hapa alitakiwa miaka ya sabini na siyo hii miaka ya 2010... .
Ujue watanzania tunataka kiongozi wa watu na atakayekubali kusimama na watu na kusimamiwa na taasisi imara za serikali. Kinachotakiwa sasa ni watu au chama kitakachojenga taasisi hizi na mazingira hayo. Hii ni katiba mpya inayoendesha serikali kupitia ridhaa ya wananchi. ccm wanapatikana kwenye hiyo picha? ndio maana nakwambia mawazo yako ni ya miaka ya 70 na yanapitwa mbali hata na uwezo wa madiwani wa Arusha unaowaona hawan uwezo wa kujenga hoja kama wewe.
Hatuwaweki tena CDM kama Miungu jinsi walivokuwa ccm. Kitu cha kuzingatia CDM wamesimama na sisi kuweka mfumo huo tunaoutaka ambao utawabana hata wao na wakikosea wanaondoka. Hiyo ligi ccm hawana ubavu wa kuicheza tena.
Kusema hakuna demokrasi ya ndani ya CDM. Who cares about that **** demokracy? We care about common good of the our country tanzania? Tutaaangalia nani anarepresent common good. Kama wanafuata katiba ya chama chao haina shida. Si kwamba demokrasi ya ndani ya chama ndo kitatatulea kiongozi bora that is BIG WRONG, prove it with the fact that with all democracy if applied ccm will still bring the worst president, because ccm with all dirties arround it will never produce good leadership. Kitu kitakachotuletea kiongozi bora is WHAT THEY STAND FOR. and we know what CDM stand for so don't come here n try to confuse us with these low arguments.
Re: Amini usiamini, CCM ina jukumu la kutupatia Rais bora mwaka 2015...
Halafu mtu mzima kuwa mnafki vbaya kweli hvi unajita mara mwanakijji na mara.... Tumekundua umetumwa na magamba kwa hyo umechelewa mno umekumbuka shuka kumekucha subiri 2015 uone rais toka chadema
Viongozi hawapaswi kutenguliwa na vikao ambavyo havikuwachagua.........kama viongozi wa matatazo basi tuulizwe siye na wala siyo kamati Kuu ya Chadema ambayo hakuna hata mpigakura wetu kule........wa jiji la Arusha..........hiyo ndiyo misingi ya demokrasia.... haiwezekani wakaazi wa nje ya jiji la Arusha watuchagulie nani anafaa kutuongoza huo ni uwakilisha haramu tu...... usiutetee...
mkuu nijuavyo uongozi wa chadema HAUKUTENGUA udiwani wao. Madiwani hao WALIFUKUZWA uanachama.
Hakuna elimu yoyote hapa kumejaa chuki, majungu, husda, wivu na mashudu!
Kama ni elimu basi ni kwenu watumwa wa nape!
Hivi na wewe kumbe unamuogopa Nape kwa taarifa yako wewe pamoja na Nape mie nawaweka kwenye kundi moja wote mnatumwa tu...wewe ni kiongozi wa Chadema nakushangaa unavyomuogopa Nape wakati Nape ni kijana mdogo tu watu tunamtuma sokoni.
Nape hana nguvu zozote za kisiasa Tanzania zaidi ya kubebwa na JK, sasa nyie mnamuogopa kweli Nape kila post lazima umtaje.
Follow Us Here