Kama Mungu yupo, kweli atakua anaona dhamira yangu dhidi yako kaka yangu. Nimekua nikifikiria sana kwamba kwa matatizo yaliyoikuta haki nchi hii katika jimbo lako yanaweza kukufanya ukajutiat kuwa mkweli na mpambanaji dhidi ya udhalimu wenye ncha kali namna hii kaka yangu!
Kukuambia usiogope, pole, usisikitike, usihuzunike, hongera, na mengine mengi naona kama haitoshi!!. Wakikutana viongozi wawili au watatu wa serikali kwa ngazi yeyote kupitia CCM, wanasemezana namna ya kuondoa makucha ya Lema shingoni mwa ccm.
Na kwa jinsi ulivyo chimbia makucha, kukutoa itakugarimu kama ulivyohisi tayari ili kunusuru CCM. Garama utakazoingia nipamoja na kutoa milimita nyingi za hymoglobine kuloanisha udongo au sakafu kaka yangu!
Mimi nimeajiriwa na hii serikali ila umenijaza hasira mpaka nafikiria kuacha kazi niingie kwenye harakati za kukutetea wewe pamoja na wanasiasa wengine walio hatarini. Usirudi nyuma, maliza safari yako kishujaa, kwani hata ungaliishi miaka 100, usingaliepuka mauti ndugu yangu lema!
Wanakuogopa kama panya wengi kwa paka mmoja kwa kapaka kadogo kamoja. Endelea kufuta tabasamu lako kwa 'injustices tanzania' maana sasa wanalaumu mama alokuzaa! ¤wana jf just say (yes or no) to this topic.

Reply With Quote


Follow Us Here