Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Msimamo wa Mheshimiwa Wenje juu ya Mwenyekiti wa NCCR.

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 36
    1. #1
      Gwalihenzi's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 21st October 2011
      Posts : 2,379
      Rep Power : 0
      Likes Received
      615
      Likes Given
      377

      Default Msimamo wa Mheshimiwa Wenje juu ya Mwenyekiti wa NCCR.

      Wenje achachamaa

      na Mwandishi wetu
      MBUNGE wa Nyamagana, Ezekiel Wenje (CHADEMA), amesema kamwe hatakiomba radhi Chama cha NCCR-Mageuzi kwa kuwa anaamini Mwenyekiti wa chama hicho, James Mbatia, ambaye hivi karibuni ameteuliwa kuwa mbunge na Rais Jakaya Kikwete hana ujasiri wa kuikosoa serikali.

      Wenje alitoa kauli hiyo jana alipozungumza na Tanzania Daima kuhusu tamko la Chama cha NCCR-Mageuzi kumpa mwezi mmoja kuwaomba radhi kutokana na kauli dhidi ya Mbatia kwamba chama hicho ni CCM B.

      Alisema hata wakimpa mwaka mzima, hataomba radhi kwa kuwa anaamini katika msimamo wake.
      “Naomba nitoe msimamo wangu kwamba mimi Wenje nilitoa maoni kama Wenje na si kwa niaba ya CHADEMA na kama Mtanzania mwenye haki ya kutoa maoni yake.

      “Kauli niliyosema na narudia na sijutii na sifuti ni kwamba Mbatia ambaye ni mpinzani, Mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi kuteuliwa na Rais Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa CCM kuwa mbunge, maana yake Kikwete amempa ajira ya kwenda bungeni,” alisema.

      Wenje alidai kuwa Mbatia hawezi kuwa jasiri wa kusimamia na kukosoa serikali ya Kikwete ndani ya Bunge, ambaye ndiye amempa mamlaka na ajira ya kuja bungeni.

      “Yani hapa duniani, hakuna mtu aliyewahi kuwa mkali dhidi ya bosi wake. Huu ujasiri utautoa wapi? Mimi bosi wangu ni watu wa Nyamagana walionipigia kura na CHADEMA walionipa ridhaa ya kugombea. Leo hii mimi siwezi kusimama ndani ya Bunge nikaipiga CHADEMA mkwara.

      “Hivyo hivyo wabunge wa Viti Maalumu wanafanya kazi kwa niaba ya vyama vyao. Kwa hiyo Mbatia mamlaka yake ya kuja bungeni yametokana na huruma, fadhila na utashi binafsi wa Rais Kikwete, sasa haiwezekani Mbatia kuwa na ujasiri wa kuikosoa serikali yake. Hapa ni kudanganyana na mimi kama Wenje msimamo wangu ndio huo,” alisema.

      Aidha, alikanusha madai kuwa amekiita chama hicho CCM B na kusisitiza kuwa alichosema ni kutokuwa na imani na Mbatia.

      Chama hicho, kimesema kuwa ndani ya mwezi mmoja endapo Wenje hataomba radhi kitamburuza mahakamani.


      juu
      Last edited by Gwalihenzi; 5th June 2012 at 23:19.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Losambo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2011
      Location : Katikati
      Posts : 2,346
      Rep Power : 850
      Likes Received
      688
      Likes Given
      296

      Default Re: Msimamo wa Mheshimiwa Wenje juu ya Mwenyekiti wa NCCR.

      Naunga mkono kauli ya Wenje, yale yanabaki kuwa maoni yake hinafsi na si msimamo wa CDM, na yule mbunge Machali yule dawa yake nayo inachemka 2015. M4C wakapige kambi jimboni mwake aone mtiti wake.

    4. #3
      Olaigwanani lang's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th April 2012
      Posts : 338
      Rep Power : 818
      Likes Received
      52
      Likes Given
      375

      Default Re: Msimamo wa Mheshimiwa Wenje juu ya Mwenyekiti wa NCCR.

      msimamo ni kitu kizuri sana.......!
      uwe mfano wa kuigwa.....!

    5. #4
      mwinukai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd May 2011
      Posts : 656
      Rep Power : 539
      Likes Received
      134
      Likes Given
      51

      Default Re: Msimamo wa Mheshimiwa Wenje juu ya Mwenyekiti wa NCCR.

      Hivi hata ukisema ukweli napo inabidi uombe radhi?

    6. #5
      Ruhazwe JR's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st January 2011
      Posts : 3,172
      Rep Power : 2888
      Likes Received
      776
      Likes Given
      721

      Default Re: Msimamo wa Mheshimiwa Wenje juu ya Mwenyekiti wa NCCR.

      very short and clear,wenje kajibu kwa ufasaha sana majibu yake yanajitosheleza,kwanza yanabaina kuwa ni kauli yake na si chama,pili yanapigilia msumari tamko la kwanza,tatu yanaonesha kujiamini kwake,nne yanatoa onesha mahakama ipo kwaajiri ya haki hivyo yupo tayari,tano yanaonesha Wenje anakijua anacho kisema.WAKATI NDIO SASA,UNANGOJA NIN?
      Bujigile likes this.


    7. #6
      Bangoo's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 3rd November 2011
      Posts : 2,293
      Rep Power : 0
      Likes Received
      374
      Likes Given
      0

      Default Re: Msimamo wa Mheshimiwa Wenje juu ya Mwenyekiti wa NCCR.

      Kibaraka kimepewa fadhila kinataka kiombwe radhi, kwani uwongo?.

    8. #7
      mmbangifingi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th March 2011
      Posts : 2,569
      Rep Power : 858
      Likes Received
      452
      Likes Given
      2908

      Default Re: Msimamo wa Mheshimiwa Wenje juu ya Mwenyekiti wa NCCR.

      Yuko sahihi Wenje,yule Mkosamali nilimdhaniaga mtu makini kumbe hovyo kabisa no wonder ndo maana anampiga vita hata mwenzie Kafulira
      Who Jah bless, No one Curse!

    9. #8
      MANGUNGO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th August 2011
      Posts : 1,146
      Rep Power : 620
      Likes Received
      251
      Likes Given
      14

      Default Re: Msimamo wa Mheshimiwa Wenje juu ya Mwenyekiti wa NCCR.

      Moses Machari ccm B

    10. #9
      Mandingo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd September 2011
      Posts : 927
      Rep Power : 573
      Likes Received
      186
      Likes Given
      52

      Default Re: Msimamo wa Mheshimiwa Wenje juu ya Mwenyekiti wa NCCR.

      Kula 5 mbunge wangu Wenje!

    11. #10
      EL MAGNIFICAL's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th January 2011
      Location : mbeya
      Posts : 857
      Rep Power : 686
      Likes Received
      103
      Likes Given
      1

      Default Re: Msimamo wa Mheshimiwa Wenje juu ya Mwenyekiti wa NCCR.

      wabunge wengine vilaza kweli huu ni ujinga kauli aliyotoa anasema ni yake yeye kama yeye ni si chadema wakati huo huo aliyepewa madaraka ni mbatia sasa kwanini ahukumu nccr si angemsema mbatia kama mbatia lakini kwa kuwa yupo upande wa chama chenye nguvu basi imekua nongwa !
      Acheni wananchi ndo tupime !
      Inawezekana yule diwani mliyetema pale mwanza bado anakuchanganya akili !

    12. #11
      RUTARE's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 10th December 2011
      Posts : 149
      Rep Power : 406
      Likes Received
      30
      Likes Given
      108

      Default Re: Msimamo wa Mheshimiwa Wenje juu ya Mwenyekiti wa NCCR.

      Quote By mmbangifingi
      Yuko sahihi Wenje,yule Mkosamali nilimdhaniaga mtu makini kumbe hovyo kabisa no wonder ndo maana anampiga vita hata mwenzie Kafulira
      Ni Moses Machali a.k.a ccm "B"

    13. #12
      Kipimbwe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th July 2011
      Posts : 269
      Rep Power : 449
      Likes Received
      29
      Likes Given
      20

      Default Re: Msimamo wa Mheshimiwa Wenje juu ya Mwenyekiti wa NCCR.

      Ni Mosses kweli au mtu mwingine.Mosses najua huwa unapita pita humu nakuomba uwe unapima kwanza kabla yakumsikiliza mkombozi wa walima korosho(kama alivyojiita)

    14. #13
      SANING'O LOSHILU's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 19th May 2012
      Posts : 144
      Rep Power : 382
      Likes Received
      11
      Likes Given
      5

      Default Re: Msimamo wa Mheshimiwa Wenje juu ya Mwenyekiti wa NCCR.

      Naunga mkono msimamo wa wenje manake kweli hiyo kwa mbatia ni ajira sasa katika logic ya kawaida mtu hawezi kumkosoa bosi! Jamani hili hata mwenye mawazo mafupi anaelewa si kila kitu kinahitaji elimu ya chuo kikuuu!

    15. #14
      KISAKA MORIS's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd April 2012
      Posts : 367
      Rep Power : 430
      Likes Received
      30
      Likes Given
      42

      Default Re: Msimamo wa Mheshimiwa Wenje juu ya Mwenyekiti wa NCCR.

      Ha'ha'ha inamaana Mbatia japokuwa nimetoka naye kijiji kimoja bado anataka tumhesabu kuwa ni mpinzani? Ama kweli kila mtu anatafuta kula yani kwa sasa yupo CCM lakini na upande wa upinzani bado yupo. Dunia ina mambo, niliambiwa nikue niyaone sasa nimekua na ninayaona.

    16. #15
      Gsana's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th August 2010
      Location : Dar es salaam
      Posts : 2,233
      Rep Power : 890
      Likes Received
      217
      Likes Given
      30

      Default Re: Msimamo wa Mheshimiwa Wenje juu ya Mwenyekiti wa NCCR.

      nataka nimuone siku ya kwanza bungen braza jemu atakataa upande gani,upande wa mwenyekiti bosi wake,au upande wa wapinzani?kwa kuwa anaenda kumwakilisha mwenyekiti wa ccm yafaa aitwe ccm A negative! Pia hatoweza kushiriki vikao vya wabunge wapinzani,na hatoweza kuingia vikao ya wabunge ccm. Namshauri viikitishwa vikao vya wabunge kivyama,yy asiende ukumbi wa msekwa wala wa kiongoz wa upinzani bali amtafute chibuda wakacheze golf au mchezo wa kufukuza panzi nje mpaka vikao vya wabunge halali vihishe! Mbatia ccm A negative!
      Bujigile likes this.

    17. #16
      Gsana's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th August 2010
      Location : Dar es salaam
      Posts : 2,233
      Rep Power : 890
      Likes Received
      217
      Likes Given
      30

      Default

      Quote By EL MAGNIFICAL
      wabunge wengine vilaza kweli huu ni ujinga kauli aliyotoa anasema ni yake yeye kama yeye ni si chadema wakati huo huo aliyepewa madaraka ni mbatia sasa kwanini ahukumu nccr si angemsema mbatia kama mbatia lakini kwa kuwa yupo upande wa chama chenye nguvu basi imekua nongwa !
      Acheni wananchi ndo tupime !
      Inawezekana yule diwani mliyetema pale mwanza bado anakuchanganya akili !
      ni bora mbunge kilaza kuliko mwandishi taahira!ni wapi mbunge ametamka nccr kuwa ccm b kama si ww mwenye mchango wa kilaza?

    18. #17
      democratic's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st November 2011
      Posts : 1,602
      Rep Power : 819
      Likes Received
      278
      Likes Given
      52

      Default Re: Msimamo wa Mheshimiwa Wenje juu ya Mwenyekiti wa NCCR.

      Naona fahari kuishi jimbo hili la nyamagana,sijawahi kuijutia kura yangu ya ubunge,Viva E.D.Wenje

    19. #18
      Duble Chris's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th May 2011
      Posts : 2,341
      Rep Power : 873
      Likes Received
      382
      Likes Given
      309

      Default Re: Msimamo wa Mheshimiwa Wenje juu ya Mwenyekiti wa NCCR.

      Quote By EL MAGNIFICAL
      wabunge wengine vilaza kweli huu ni ujinga kauli aliyotoa anasema ni yake yeye kama yeye ni si chadema wakati huo huo aliyepewa madaraka ni mbatia sasa kwanini ahukumu nccr si angemsema mbatia kama mbatia lakini kwa kuwa yupo upande wa chama chenye nguvu basi imekua nongwa !
      Acheni wananchi ndo tupime !
      Inawezekana yule diwani mliyetema pale mwanza bado anakuchanganya akili !
      soma vizuri makala yake between lines utaelewa tu nadhani hapa umekurupuka
      frustration is given by expectationdivide by
      outcome
      ie
      frustration = expectation/outcome


    20. #19
      Mkwanda's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 6th April 2012
      Posts : 123
      Rep Power : 384
      Likes Received
      14
      Likes Given
      0

      Default Re: Msimamo wa Mheshimiwa Wenje juu ya Mwenyekiti wa NCCR.

      Machali nilikua namkubali sna,kuna kipindi nilijua ni mbunge wa chadema badae nikagundua ni nccr nikasema kumbe nccr bado kuna majembe,he!ckuamini namna ambavyo akitetea ujinga live,nimepoteza imani na MOSES MACHALI kabisa hata kusoma upepo ameshndwa?safi sana kamanda WENJE.

    21. #20
      agatony8l's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th October 2010
      Posts : 392
      Rep Power : 513
      Likes Received
      89
      Likes Given
      52

      Default Re: Msimamo wa Mheshimiwa Wenje juu ya Mwenyekiti wa NCCR.

      Quote By Mkwanda
      Machali nilikua namkubali sna,kuna kipindi nilijua ni mbunge wa chadema badae nikagundua ni nccr nikasema kumbe nccr bado kuna majembe,he!ckuamini namna ambavyo akitetea ujinga live,nimepoteza imani na MOSES MACHALI kabisa hata kusoma upepo ameshndwa?safi sana kamanda WENJE.
      Nami nilijua huyu mtu ni mpambanaji na nilikuwa namkubali sana lakini jinsi siku zinavyokwenda naanza kuona ni kama anategemea fadhila fulani toka kwa mwenyekiti wake wa chama kwani amekuwa mstari wa mbele kumtetea. Kiujumla namuunga mkono Mh. Wenje kwa kauli yake na msimamo aliouonhyesha. Kwa kweli hata mtoto wa darasa la kwanza anaweza kujumlisha moja na moja akapata mbili. Anatakiwa ajibu hoja je Mh. Mbatia ni mbunge wa upinzani au wa chama tawala???? Je anaweza kupinga kwa nguvu zote hoja kandamizi za magamba???? Hayo ndo maswali ya msingi. Yawafanyie kazi ili kutuprove Wrong sio kupoteza muda kwenda mahakamani.

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...