Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Dk 45 ITV: Kwanini wapinzani hawaalikwi humu?

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 30
    1. #1
      nexus white's Avatar
      Member Array
      Join Date : 14th October 2011
      Posts : 27
      Rep Power : 389
      Likes Received
      9
      Likes Given
      11

      Default Dk 45 ITV: Kwanini wapinzani hawaalikwi humu?

      Kwanini wapinzani hawaalikwi katika kipindi hiki, tumechoka na longolongo za hao wanaokuwepo humo, wanaongea visivyoeleweka, wanadanganya na kukataa ukweli tu, uongozi ITV tendeni haki kama kweli mna nia njema na watanzania
      Remote, Mponella, zaleo and 1 others like this.

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Filipo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Location : Kiding'a
      Posts : 6,349
      Rep Power : 18614
      Likes Received
      3508
      Likes Given
      1612

      Default re: Dk 45 ITV: Kwanini wapinzani hawaalikwi humu?

      Hicho kipindi kimekuwa kisemeo cha serikali ya magamba!

    4. #3
      Paul Kijoka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th October 2010
      Location : KIMARA, DAR
      Posts : 1,337
      Rep Power : 702
      Likes Received
      226
      Likes Given
      172

      Default re: Dk 45 ITV: Kwanini wapinzani hawaalikwi humu?

      Sisi CHADEMA tuko busy na wananchi na si kipindi cha magamba kutushambulia. Mtangazaji jana alionesha upendeleo kwa kumrudia mara nyingi waziri wa misitu.

    5. #4
      TaiJike's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th December 2011
      Posts : 1,156
      Rep Power : 606
      Likes Received
      387
      Likes Given
      347

      Default re: Dk 45 ITV: Kwanini wapinzani hawaalikwi humu?

      Ni kweli mkuu sijawahi sikia/ona kiongozi yoyote toka chama cha siasa cha upinzani, hata huyo mtangazaji hana maswali ama hoja zenye mashiko ama ukomavu kulingana na taaluma yake.
      christine ibrahim likes this.
      * Nitashangaa kama hawa Watanzania watakataa kuasi. Kwanini wasiasi? * - Julius Kambarage Nyerere


    6. #5
      fikirikwanza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th January 2012
      Posts : 642
      Rep Power : 497
      Likes Received
      149
      Likes Given
      17

      Default re: Dk 45 ITV: Kwanini wapinzani hawaalikwi humu?

      Nashukuru kwa kuanzisha uzi huu, kipindi ni kizuri lakini ukweli narudia ukweli kuwa mtangazaji anapwaya sana, wanaoalikwa wanaongoza mazungumzo nayeye anafuata nyuma, ni mara kadhaa hana uhakika na hoja zake na hivyo waalikwa baada ya kuulizwa swali, wanaligeuza wanavyotaka wao na yeye haoneshi kuwa ni mtangazaji aliyeiva kushikiria swali lake na maudhui ya swali lake, ANAPWAYA SANA MTANGAZAJI HUYU, ITV kama ina watangazaji walioelimika basi wapewe kipindi hicho.

      Wassira jana kapindisha maswali kibao harafu mtangazaji hajui la kufanya, anapunguza wasikilizaji wa kipindi badala ya kuwaongeza, swali kuhusu kuzomewa, swali kuhusu ccm kuwa makundi makundi na kushindwa 2015 mfano wake ulikuwa hoja za maige, yeye akajibu mfano wa swali (eti siwezi kumzungumzia maige) sio swali lenyewe, MTANGAZAJI alikuwa wapi???; Makundi anajibu hata vyama vingine yapo, sasa kweli hilo ndo jibu la hilo swali??? mtangazaji uwezo kiakili am very sorry unapwaya.

      Mimechukua mifano michache tu lakini kila nikisikiliza kipindi hicho mtangazaji anapwaya sana, aidha hana uwezo kielimu au kiasilia hawezi vipindi vya aina hiyo; apishe vijana wenye uwezo au abadilike sana, ajue agenda yake kwenye swali ni nini na asimamie maswali yajibiwe, ni afadhali swali likose jibu kuliko blabla tu.

      Kipindi ni cha maswali yenye utata/magumu sio maswali ambayo kila mtu analojibu haitakuwa na maana kabisa; aandae maswali vigongo yenye manufaa kwa TZ, aombe yajibiwe, asimamie swali lijibiwe sio mtu atunge lake harafu aanze kujibu.
      Last edited by fikirikwanza; 5th June 2012 at 10:15.
      Mahoo, andrewk, Remote and 2 others like this.

    7. Miaka 50

    8. #6
      Edwine Mugarula's Avatar
      Member Array
      Join Date : 28th October 2010
      Posts : 15
      Rep Power : 437
      Likes Received
      2
      Likes Given
      32

      Default re: Dk 45 ITV: Kwanini wapinzani hawaalikwi humu?

      Ahsante kwa kuweka thread hii jamvini, mimi nimewahi ku-comment mara kadhaa juu ya uboreshaji wa kipindi hiki. Kama ni viongozi wawe wale wote wanaowajibika kwa wananchi, si wale tu walio serikalini! Kama ITV ingelikuwa ni ya serikali, hapo sawa.

      Kama ni viongozi wa kisiasa, si hao tu walio serikalini. Lakini pia wangeshirikisa hata viongozi wa dini (wazungumzie mambo kitaifa na ya jumla tu), viongozi wa mashirika ya umma na yasiyo ya umma, n.k.

      Wakati mwingine huwa naingiwa na mashaka na huyu Seleman Semunyu, kwamba huenda ana ajenda fulani nao, kwa mfano hata kama kipindi hicho kilibuniwa kwa ajili ya mawaziri tu, ni kigezo gani anachotumia kumwalika waziri fulani hata mara 4, wakati kuna ambaye hayawahi kualikwa hata mara moja?!

      Na ukifuatilia hao wanaoitwa mara kwa mara, kila inapotokea huwa wamekuja (sijui niite kuoshwa) mara yakuwepo uvumi wa kuchafuliwa na matukio kadhaa, lakini kingine kinatia mashaka, ni pale anapokuja mtu fulani, anaulizwa swali wakati wa kujibu, anaonekana dhahiri akisoma majibu yaliyoandaliwa kwenye "note book" na majibu yake huyasoma kwa mtiririko wa namna alivyoandaa, yaani ukurasa mmoja baada ya mwingine, je hii haijengi mashaka kuwa huwa kunakuwepo mawasiliano kati ya hao wawili? Ni mtizamo wangu, I might be wrong!

    9. #7
      Mkeshaji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th January 2011
      Location : This is Anfield
      Posts : 3,634
      Rep Power : 1372
      Likes Received
      1091
      Likes Given
      318

      Default re: Dk 45 ITV: Kwanini wapinzani hawaalikwi humu?

      Quote By Filipo
      Hicho kipindi kimekuwa kisemeo cha serikali ya magamba!
      Wakishaona mambo taiti tu basi wanakimbilia huko.
      You'll never walk alone - LFC.

    10. #8
      Olaigwanani lang's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th April 2012
      Posts : 333
      Rep Power : 816
      Likes Received
      52
      Likes Given
      373

      Default Re: Dk 45 ITV: Kwanini wapinzani hawaalikwi humu?

      huyo chipanzee hana jipya, hata wakimwita mara kumi hapoo.....
      christine ibrahim likes this.

    11. #9
      Apolonary's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th August 2011
      Location : SAN DIEGO COMMUNITY
      Posts : 1,456
      Rep Power : 682
      Likes Received
      249
      Likes Given
      30

      Default Re: Dk 45 ITV: Kwanini wapinzani hawaalikwi humu?

      ni lazima watu itv kama ilivyo haifungamani na chama chochote cha siasa. Ni chombo cha raia wote sasa ukisema chama fulani kiende kufanya interview kuna wengne hawataridhika

    12. #10
      Bajabiri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 9,741
      Rep Power : 2884
      Likes Received
      1115
      Likes Given
      52

      Default

      Quote By Filipo
      Hicho kipindi kimekuwa kisemeo cha serikali ya magamba!
      exactly,,,,ni asasi yao ya kuletea propaganda,,,,,,

    13. #11
      7son's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 24th May 2012
      Posts : 129
      Rep Power : 377
      Likes Received
      22
      Likes Given
      2

      Default Re: Dk 45 ITV: Kwanini wapinzani hawaalikwi humu?

      ITV wanatakiwa watafute mtu anayeweza kuhoji vizuri, yule mtangazaji wa sasa anabaki anashangaa haeleweli hata kitu, ndo mana Mkapa huwa hataki kuongea nao mana wako shallow mno
      christine ibrahim likes this.

    14. #12
      Bajabiri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 9,741
      Rep Power : 2884
      Likes Received
      1115
      Likes Given
      52

      Default

      Quote By Olaigwanani lang
      huyo chipanzee hana jipya, hata wakimwita mara kumi hapoo.....
      hahahahaaa........mr Gombe

    15. #13
      Ngalikivembu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th October 2010
      Location : Geostationary Earth Orbit
      Posts : 511
      Rep Power : 10611
      Likes Received
      152
      Likes Given
      117

      Default Re: Dk 45 itv: Kwanini wapinzani hawaalikwi humu?

      Quote By fikirikwanza
      Nashukuru kwa kuanzisha uzi huu, kipindi ni kizuri lakini ukweli narudi ukweli kuwa mtangazaji anapwaya sana, wanaoalikwa wanaongoza mazungumzo nayeye anafuata nyuma, ni mara kadhaa hana uhakika na hoja zake na hivyo waalikwa baada ya kuulizwa swali, wanaligeuza wanavyotaka wao na yeye haoneshi kuwa ni mtangazaji akiyeiva kushirikia swali lake na maudhui ya swali lake, ANAPWAYA SANA MTANGAZAJI HUYU, ITV kama ina watangazaji walioelimika basi wapewe kipindi hicho.

      Wassira jana kapindisha maswali kibao harafu mtangazaji hajui la kufanya, anapunguza wasikilizaji wa kipindi badala ya kuwaongeza, swali kuhusu kuzomewa, swali kuhusu ccm kuwa makundi makundi na kushindwa 2015 mfano wake ulikuwa hoja za maige, yeye akajibu mfano wa swali sio swali, MTANGAZAJI alikuwa wapi???; Makundi anajibu hata vyama vingine yapo, sasa kweli hilo ndo jibu la hilo swali??? mtangazaji uwezo kiakili am very sorry umapwaya.

      Mimechukua mifano michache tu lakini kila nikisikiliza kipindi hicho mtangazaji anapwaya sana, aidha hana uwezo kielimu au kiasilia hawezi vipindi vya aina hiyo; apishe vijana wenye uwezo au abadilike sana, ajue agenda yake kwenye swali ni nini na asimamie maswali yajibiwe, ni afadhali swali likose jibu kuliko blabla tu.

      Kipindi ni cha maswali yenye utata/magumu sio maswali ambayo kila mtu analojibu haitakuwa na maana kabisa; aandae maswali vigongo yenye manufaa kwa TZ, aombe yajibiwe, asimamie swali lijibiwe sio mtu atunge lake harafu aanze kujibu.
      Kwa hakika nashukuru sana ulinitangulia kuanzisha uzi huu leo.Nilipanga kuandika juu ya kipindi kwa kadiri nilivyokitazama jana. Ki ukweli mimi si mtazamaji wa kipindi hicho toka kiwe hewani nasikia tu fulani kaongea hiki. Na nilisoma maoni ya Karugendo gazetini siku moja akikosoa kipindi hiki.Jana wakati natafuta vipindi vya kutazama nikamwona wasira na semunyu wakiwa wanaanza tu mazungumzo yao.Nikashawishika kutazama nimsike wasira anaongea nini. Mapungufu(japo si kiswahili sanifu) niliyoyaona ni kama yafuatayo;
      1. Mtangazaji hajiandai kumhoji mhusika.Kwanini?Sikuliona swali la kiujuzi alilioulizwa Wasira. Hata maswali aliyoulizwa wasira mengine alikuwa hajibu au kupindisha swali alilioulizwa na mtangazaji anamwacha tu.Hang'ang'anii swali lake lipewe jibu.Mfano swali kuhusu siasa za vyama vingi, mahusiano yakoje hivi sasa reference Semunyu akitoa ile ya Arumeru.Hili Wasira hakujibu akarukia kwingine na kusema ya Arumeru achana nayo.
      2. Semunyu ana woga wa kuuliza swali la kuudhi.Mtangazaji siku zote hasa katika vipindi kama vile vya mahajiano anatakiwa aondoe woga wa kuuliza swali la kumkasirisha au kumuudhi anayemhoji.Chukua mfano wa makundi ndani ya CCM.Wasira swali hili badala ya kuuliza akarukia kumhoji mtangazaji, chama kipi hakina makundi nitajie.Akaanza, CUF wanamakundi, Chadema wana makundi.Hapa Wasira alikazania sana.Chadema kina kundi la Mbowe, Slaa na Zitto, wewe hujui hili.Hapa nikaona kuna upungufu kwa mwandishi.Hakutaka kumdadisi hayo makundi ni yepi wala kumlazimisha kujibu hoja aliyoulizwa ndani ya ccm.
      3. Kwa jana, niliona, Wasira alikuwa naonekana ni mwenye dukuduku na kisilani hasa na chadema, kwani maswali mengi aliyohojiwa alikuwa anakimbilia aidha kukitaja chadema au kukilaumu au kukikebehi chadema.Chukua mfano wa swala la kuvuana magamba ndani ya ccm.Badala ya kujibu swali kama alivyotakiwa akarukia kusema chadema wana endesha change sijui change ya nini?anahoji.Change ya kurudi nyuma au kwenda mbele maana zote ni change.
      Hapa kiufupi Wasira nilivyomsoma ni kuwa hafurahishwi na kampeni ya chadema bali ana hasira nayo.
      4. Semunyu anapaswa kuwabadilisha au kuwaleta watu wawili awe anawahoji.Mfano kama jana alitakiwa kwa vile kamleta waziri wa mahusiano, alipaswa pia amlete mtu mmoja toka kwenye vyama vya siasa aweze kusema kama mahusiano ya vyama vya siasa ni mazuri au la.Au ushauri mwingine ni kuwa aite na vyama vya siasa badala ya kuwaleta mawaziri ambao wanaongea kusifia serikali zaidi.Mfano aliyoongea wasira yanapaswa kujibiwa pia na wengine hasa wale aliowagusa.
      Hayo ni baadhi tu niliyoyaona.
      zaleo and christine ibrahim like this.
      AN EMPTY STOMACH IS NOT A GOOD ADVISER. Albert Einstein
      POVERTY IS THE PARENT OF REVOLUTION AND CRIME. Aristotle

    16. #14
      sawabho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2011
      Location : Miyakojima
      Posts : 1,792
      Rep Power : 775
      Likes Received
      415
      Likes Given
      121

      Default Re: Dk 45 ITV: Kwanini wapinzani hawaalikwi humu?

      Ingekuwa vizuri Mtangazajia aandae maswali, halafu asimamie majibu, kama akiona Muhusika anayeenda nje ya mada amrekebisha na kumrudisha kwenye mada. Mara nyingi Mtangazaji anamwachia Mhusika kujieleza anavyotaka mpaka mtangazaji anashtuka muda umeisha !!! Hata hivyo, inavyoonekana na ndivyo ilivyo yale maswali sio ya papo kwa hapo kwa sababu Mhusika anasoma kutoka kwenye taarifa iliyoandaliwa na ikiwa ni pamoja na takwimu mbali mbali. Hii inatia shaka kama mtu anayehojiwa ana uelewa na jambo analojibu kwa sababu anasoma majibu ambayo tayari yameendaliwa. Kama hiyo ndiyo kazi yake, kwa nini asiongee bila kusoma ? Kipindi kiwe Live na kuruhusu maswali kutoka kwa watazamaji.
      zaleo likes this.
      INAWEZEKANA, TIMIZA WAJIBU WAKO

    17. #15
      andrewk's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th April 2010
      Posts : 2,224
      Rep Power : 906
      Likes Received
      283
      Likes Given
      59

      Default Re: Dk 45 ITV: Kwanini wapinzani hawaalikwi humu?

      Hicho kipindi ni cha kipuuzi kabisa, dunia ya sasa unaweka kipindi recorded? maana utakuta juma pili anaanza kurusha dondo kwa yaliyongelewa. maana yake watakuwa waneongea Alhamis au ijumaa, wakafanya editing kwa siku 2-3 ndio wanarusha jumatatu! sasa hapo unasikiliza nini hapo?
      christine ibrahim likes this.

    18. #16
      Precise pangolin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 4th January 2012
      Posts : 5,670
      Rep Power : 1909
      Likes Received
      1563
      Likes Given
      676

      Default Re: Dk 45 ITV: Kwanini wapinzani hawaalikwi humu?

      Wananchi wenyewe wa vijini umeme hawana sijui hiyo TV wanaangaliaje badala ya kuzunguka huko vijijini wanakaa kwenye A/C za studio za TV tu pambaf
      christine ibrahim likes this.

    19. #17
      Tewe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th January 2008
      Posts : 450
      Rep Power : 670
      Likes Received
      63
      Likes Given
      12

      Default Re: Dk 45 ITV: Kwanini wapinzani hawaalikwi humu?

      Kimsingi jamaa anaboa, hadhi ya kipindi ilitakiewa kufanana na hard talk ya BBC lakini semunyu amebaki kuwa msikilizaji tu hadi huwa natamani kuzima tv, afadhili angepewa hata fatma nyangasa au mzee masako huenda kingechangamka
      christine ibrahim likes this.

    20. #18
      zaleo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th December 2011
      Posts : 791
      Rep Power : 535
      Likes Received
      234
      Likes Given
      528

      Default Re: Dk 45 ITV: Kwanini wapinzani hawaalikwi humu?

      Quote By nexus white
      Kwanini wapinzani hawaalikwi katika kipindi hiki, tumechoka na longolongo za hao wanaokuwepo humo, wanaongea visivyoeleweka, wanadanganya na kukataa ukweli tu, uongozi ITV tendeni haki kama kweli mna nia njema na watanzania

      Huilo nalo ni neno.

    21. #19
      zaleo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th December 2011
      Posts : 791
      Rep Power : 535
      Likes Received
      234
      Likes Given
      528

      Default Re: Dk 45 ITV: Kwanini wapinzani hawaalikwi humu?

      Quote By andrewk
      Hicho kipindi ni cha kipuuzi kabisa, dunia ya sasa unaweka kipindi recorded? maana utakuta juma pili anaanza kurusha dondo kwa yaliyongelewa. maana yake watakuwa waneongea Alhamis au ijumaa, wakafanya editing kwa siku 2-3 ndio wanarusha jumatatu! sasa hapo unasikiliza nini hapo?

      Enheeee, ndio upuuzi huohuo twataka wapinzani wauonyeshe na kuupinga. Ni vizuri kuwapo na wapuuzi kwenye jamii, maana hao watatusaidia kupata kitu cha upuuzi tutakachokizungumzia na hatimaye kuondoa upuuzi katika jamii.

    22. #20
      Godwinnko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2012
      Location : Moshi
      Posts : 484
      Rep Power : 669
      Likes Received
      111
      Likes Given
      64

      Default Re: Dk 45 ITV: Kwanini wapinzani hawaalikwi humu?

      all in all ITV inastahili pongez..kila siku m4c katika newz..

    Page 1 of 2 12 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...