Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

    Report Post
    Page 3 of 10 FirstFirst 12345 ... LastLast
    Results 41 to 60 of 191
    1. #1
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,507
      Rep Power : 46711
      Likes Received
      16386
      Likes Given
      8454

      Default Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Kuna maneno na kauli za baadhi ya watu wachache wakizungumza kana kwamba wanawakilisha "wengi". Utasikia mtu anayepinga Muungano anasema "Wazanzibari hatuutaki Muungano" na wakati mwingine kudai "Wazanzibari wengi hawautaki muungano". Sasa mara nyingi wanaposema "wengi" mtu wa kawaida (asiyetaka kufikiri sana) anaweza kuamini kabisa kuwa ni kweli "wengi" hawautaki Muungano.

      Mfano unaotolewa siku za hivi karibuni ni "sahihi 500,000" za wanaodaiwa "Wazanzibari" wasiotaka Muungano. Sasa kwenye mahali ambapo pana watu milioni 1.5 hivi idadi hiyo ni kubwa sana; ni theluthi moja ya watu wote wa Zanzibar. Sasa kama kweli wapo watu wengi hivi njia rahisi ya kutaka kujitoa kutoka kwenye Muungano siyo mihadhara wala hawahitaji kabisa kuwalalamikia watu wa bara au serikali ya Muungano.

      Kwa wanaokumbuka wananchi wa Zanzibar walishinikiza vyama vyao viwili vya CCM na CUF kuunda serikali ya umoja wa kitaifa na waliweza kufanya hivyo baada ya kupitisha sheria ya kura ya maoni ambayo hatimaye iliandika upya katiba ya Zanzibar. Wananchi wakaweza kujitokeza na kupiga kura ya maoni. Walifanya hivi bila kuomba kibali Muungano na kiasi cha kuweza kuandika kwenye Katiba Yao vitu ambavyo ni kinyume na Katiba ya Muungano.

      Sasa kama waliweza kufanya hili ni kitu gani kinawashinda kutaka viongozi wao wa kisiasa kuandia sheria ya kupiga kura ya maoni kama wanautaka Muungano au la? Kwa vile hoja ya kupinga MUungano inadaiwa inakubaliwa na watu wa vyama vyote ni wazi kuwa ni rahisi sana kwa watu wa Uamsho na Wazanzibari wengine kuhakikisha kuwa BLW linapokaa linaazimia kupitisha kura ya maoni kuhusu Muungano na kutaka sheria iletwe ya kuuliza swali la Muungano.

      Swali liwe rahisi tu:

      Je unataka Zanzibar ibakie kwenye Muungano wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania?

      a. Ndio ibakie - Ikibakia kero na matatizo ya Muungano kutatuliwa ifikapo Julai 1, 2014
      b. Hapana isibakie - isipobakia Zanzibar itajitoa ifikapo Julai 1, 2014



      Ijulikane mapema kuwa ikisemwa kuwa "ndio ibakie" manake ni kuwa masuala ya muundo na mfumo wa Muungano yatajadiiliwa na kushughulikiwa kwenye Katiba Mpya na yatakuwa tayari kumalizwa yote ifikapo 2014

      Na ikisemwa Hapana isibakie manae ni kuwa mazungumzo ya kuvunja Muungano yataanza na ifikapo Julai 1, 2014 Zanzibar itajitoa kwenye Muungano.

      Wazanzibar waandae kura hiyo ya maoni wao wenyewe kama walivyofanya kwenye ile ya mabadiliko ya Katiba na lolote watakaloamua Tanzania Bara WATAHESHIMU uamuzi huo.

      Ni rahisi sana kumaliza hoja ya Muungano au kutokuwepo Muungano. Yote YAMO MIKONONI MWA WAZANZIBARI. Hawahitaji kutuambia hawautaki Muungano, hatuhitaji watuambie tunawakandamiza kama wanataka kutoka kweli na siyo mikwara mbuzi njia nyeupeeeee!!! Andikeni sheria, itisheni kura ya maoni, pigeni kuchagua 'b' and then mambo yatakua yameiva ifikapo 2014 tutawasaidia kufunga mizigo.
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    2. Miaka 50

    3. #41
      Davie S.M's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Posts : 634
      Rep Power : 550
      Likes Received
      140
      Likes Given
      44

      Default

      Kuna njia. Nyingi tu za kuvunja huo Muungano za Kistaarabu zinaweza fatwa kama kweli Zanzibar Hawatak Muungano ...Lakini sio Kihuni-huni kama ivi...
      Jasirii aachi Asili

      Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums

    4. #42
      Sangarara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 3,336
      Rep Power : 1205
      Likes Received
      1193
      Likes Given
      1568

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By Nyakageni
      do you think, inawezekana? Kuna tatizo lingine nalo ni faida ya magamba kwa wabunge wa bure toka Zenj! Hawawezi kukubali
      Kwani hao wabunge wa Zenji sio wazanzibar? Na mbona wote wako kimya wakati ushenzi huu ukiendelea? Nashauri Waliozanzibar waprint huu uchauri wa Mwanakijiji na kuusambaza misikiti yote Zanzibar, sababu naona uko pekee ndio kuna watu wanafikiria.

    5. #43
      Yo Yo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st May 2008
      Posts : 10,786
      Rep Power : 22905
      Likes Received
      1335
      Likes Given
      2576

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Kibunango wewe unasemaje?
      Kibunango likes this.
      ...kuwa na baba maskini ni mipango ya Mungu ila kuwa na baba mkwe maskini ni ujinga wako mwenyewe.....

    6. #44
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6154
      Likes Given
      22273

      Default

      Quote By Kiranga
      Kwa nini unafikiri swala la muungano na Zanzibar linatakiwa kupigiwa kura na Wazanzibari tu?

      Hufikiri kwamba kuna uwezekanao Wazanzibari wengi wakasema wanataka kuwa katika muungano, ila watu wa bara wakawa hawataki muungano?

      Ili kura ya maoni iwe na maana, inafaa ipigwe nchi nzima. Usichukulie for granted kwamba wabara wanautaka muungano.

      Unaweza kumaliza kura ya maoni Zanzibar bila ya kuwashirikisha watu wa bara, ukapata kura za kukubali muungano nyingi sana, only to find out kuna malalamiko kutoka kwa watu wa bara kwamba hawakushirikishwa.
      Mkuu Kiranga, sisi bara hatuna sheria ya kura ya maoni. Zanzibar tayari wanayo sheria ya kura ya maoni hivyo kwao ni straight forward.

      Hapa kwetu pia sheria hiyo italetwa baada ya kukusanywa maoni na bunge la katiba, then kura ya maoni itakuwa ndio last option kuipitisha katiba mpya!.

      Hoja ya Mwanakijiji ni very valid, maadam wamethibitisha kwa saini 500, 000 ambayo ni theluthi moja, na wanaamini Wazanzibari wengi hawautaki muungano, kwa nini wasiupinge kwa kuitumia hiyo sheria yao ya kura ya maoni na matokeo kuwa endorsed na BLW hiyo kutoa tuu azimio la utekelezaji huku bara!.

      Kama walibadili katiba yao kuunda SUK ikiwemo kuvunja cheo cha Waziri Kiongozi na badala yake kuweka hao makamo wawili, katiba ya JMT haiyatambui mabadiliko hayo. Kwa mujibu wa katiba ya JMT bado tunamtambua Waziri kiongozi ambaye hayupo na hatuwatambui hao makamo wawili kikatiba ila in reality wapo na huja huku bara na protocal inawatambua.

      NB. Nazidi kusisitiza japo muungano ni illegal before the eyes of the law kwa vile haukuwa ratified na BLW au BLM kwama ilivyotaka sheria, Wanzanzibar wanayo very valid reasons ya kujitoa kwa heshima, tena kihalali bila jinai ya uhaini kwa kuvunja muungano, wakiamua kwa kauli moja kuwa kabla ya BLW kuridhia tume yakukusanya maoni ya katiba mpya ifanye kazi Zanzibar, kwanza vile vipengele vya yale makubaliano ya muungano ambavyo vilikiukwa kwanza viridhiwe na BLW ili kuulegitimize huu muungano kule kwao Zanzibar!. Na kwa kuutumia mwanya huo then wagome kuuratify muungano hivyo muungano huu kuwa rendered illegal na legal process za kuuvunja kufuata!.

      Kwa vile Karume hakujua Kiingereza, I wala hakujua kusoma wala kuandika zaidi ya kusaini kwa dole gumba, then washeria pia wanaweza kuchalenge makubaliano before the court of law kwa kutumia kipengele kiitwacho "privity" kwa kujenga hoja kuwa wakati Karume ikitia dole gumba, hakujua anasaini nini!.

      Baba wa Taifa aliundesha muungano kwa utaratibu wa "the end justifies the means". sheria, taratibu na kanuni, hazikufuatwa!.
      kwamwewe and SnowBall like this.

    7. #45
      Kibunango's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2006
      Location : Tampere
      Posts : 6,804
      Rep Power : 44130
      Likes Received
      368
      Likes Given
      1428

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By Yo Yo
      Kibunango wewe unasemaje?
      Kamanda tusitafutane...!
      Yo Yo likes this.
      Save Water Drink Beer. "Alcohol doesn't solve any problem,
      But, if you think again, neither does milk."
      Vituko Vya Zenj

    8. RukaaJuu Final

    9. #46
      Yo Yo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st May 2008
      Posts : 10,786
      Rep Power : 22905
      Likes Received
      1335
      Likes Given
      2576

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By Kibunango
      Kamanda tusitafutane...!
      haina kweeere arifu
      ...kuwa na baba maskini ni mipango ya Mungu ila kuwa na baba mkwe maskini ni ujinga wako mwenyewe.....

    10. #47
      Sangarara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 3,336
      Rep Power : 1205
      Likes Received
      1193
      Likes Given
      1568

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By Tume ya katiba
      Kwanini unaamini kuwa wasioutaka muungano ni wachache?
      Kuna mawili
      Kwanza: wangekuwa wengi wangefanya kama walivyofanya kwenye serikali ya umoja wa kitaifa.
      Pili: Kama ni wengi basi watakuwa ni wale wasiokuwa na nguvu.

      Au la, kwa moyo mkunjufu kabisa na mimi naunga mkono hoja, wafanye kama jadi yao

    11. #48
      FairPlayer's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th February 2006
      Location : UK
      Posts : 4,383
      Rep Power : 1551
      Likes Received
      456
      Likes Given
      205

      Default

      Kwani wajameni, haiwezekani by 1st of July mwaka 2012 Muungano ikawa imevunjika?



      Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums

    12. #49
      Bumpkin Billionare's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th January 2012
      Location : Msangabunyesa
      Posts : 1,280
      Rep Power : 697
      Likes Received
      557
      Likes Given
      198

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By Tume ya katiba
      Kwanini unaamini kuwa wasioutaka muungano ni wachache?
      Ni sawa na wewe unavyotaka tuamini kuwa wengi hawautaki. Mzee Mwanakijiji hajasema wengi hawautaki (na hili ndio tatizo lenu: kutopenda kusikiliza) alichosema ni kuwa jambo hili halina uhakika na njia pekee ya kupata uhakika ni kwa A au B voting.

      Ama kama unaquote namna aliyoandika, bado yupo sahihi. Idadi ya wanaopiga kelele majukwaani ni ndogo kulinganisha na idadi ya walionyamaza ambao hatujui wanasema nini
      An Idea isn't responsible for the people who believe in it.
      Donald Robert Marquis (1878 - 1937)
      American Writer


    13. #50
      mgen's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 18th November 2010
      Posts : 5,585
      Rep Power : 3945
      Likes Received
      711
      Likes Given
      148

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Hapa waZ'bar nina uhakika hawataki kuvunja muungano, wangetaka hivyo wawakilishi wa waZ'bar ambao wamewatuma kwenye Bunge la muungano wasingemzomea TS alipowaonyesha njia muafaka kabisa! Kinacho wasumbua ni UROHO Huku Z'bar wanaitaka iwe yao tu bila Tanganyika, na neema ya Tanganyika wanaitaka bila kuwekewa masharti! Fanyeni hivyo kama mtasikia kelele zao!
      Mzee Mwanakijiji likes this.

    14. #51
      Bumpkin Billionare's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th January 2012
      Location : Msangabunyesa
      Posts : 1,280
      Rep Power : 697
      Likes Received
      557
      Likes Given
      198

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By Pasco_jr_ngumi
      aaaaaaah....
      unadhani itaishia hapo??
      sisi tutapiga kura nyingine kuomba COASTAL STRIP ya 16 miles tujiunge na new ZANZIBAR REPUBLICS....
      ina maana miji yaTANGA, MTWARA, BAGAMOYO NA DSM....tutajiunga mso tuuu

      HAPO ITAKUWA NCHI IMETENGAMAA, kama sudan , waislam na bara ya wakristu...

      JE MZEE MWANAKIJIJI KUNA K2 UMEJIFUNZA HAPA?????
      Kabla hizi ILLUSIONS zako hazijatokea, Unguja na Pemba zitakuwa zimeshatengana. Kutapatikana Watumbatu na Washirazi watakaolumbana juu ya nani ana haki ya kuitawala Jamhuri ya Zanzibar.

      Labda ujiunge na Jamhuri ya Watu wa Kojani.
      Mzee Mwanakijiji likes this.
      An Idea isn't responsible for the people who believe in it.
      Donald Robert Marquis (1878 - 1937)
      American Writer


    15. #52
      mkomatembo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th December 2011
      Location : Bweleo
      Posts : 1,019
      Rep Power : 637
      Likes Received
      228
      Likes Given
      1269

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By Pasco_jr_ngumi
      aaaaaaah....
      unadhani itaishia hapo??
      sisi tutapiga kura nyingine kuomba COASTAL STRIP ya 16 miles tujiunge na new ZANZIBAR REPUBLICS....
      ina maana miji yaTANGA, MTWARA, BAGAMOYO NA DSM....tutajiunga mso tuuu

      HAPO ITAKUWA NCHI IMETENGAMAA, kama sudan , waislam na bara ya wakristu...

      JE MZEE MWANAKIJIJI KUNA K2 UMEJIFUNZA HAPA?????
      Aiseee umenikosha roho yangu wewe! yaani umenifanya niazne kuota mchanamchana
      Mzee Mwanakijiji likes this.
      Reply With Quote

    16. #53
      tpmazembe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th January 2012
      Posts : 351
      Rep Power : 443
      Likes Received
      44
      Likes Given
      57

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By Kiranga
      1. Bila ya kupiga kura ya maoni nchi nzima huwezi kujua wabara wanautaka muungano au hawautaki. Kwamba wamelalamika au hawajalalamika hapo nyuma is irrelevant.Usipowashirikisha unaacha mwanya wa mzozo ambao unaweza kuzibwa kirahisi tangu mwanzo. Ukitaka kuondoa feelings za kwamba muungano uko one sided itabidi kura ipigwe pande mbili zote.

      2. Mfano wa Quebec hata mimi niliufikiria.Lakini haupo appropriate hapa kwa sababu Quebec ni jimbo la Canada lililokuwa linaamua kwamba libaki Canada au lijitoe. Zanzibar si jimbo la Tanzania, ni a quasi-state within a state.

      3. Ukipiga kura ya maoni nchi nzima, Zanzibar wakasema wanataka Muungano, bara wakasema hawataki, muungano unavunjwa.Point ya kupiga kura ya maoni nchi nzima ni kupata maoni ya wananchi wa nchi nzima, kwa maana muungano unawahusu wananchi wa nchi nzima, si Wazanzibari tu.Huwezi kuita hii situation stalemate. Stalemate itatokea iwapo kura za maoni zitakataa na kukubali muungano kwa 50% kote bara na visiwani. Kitakachotakiwa kuendeleza muungano kiwe simple majority on both sides.

      Moja ya matatizo tunayoyaona katika muungano wetu sasa hivi ni hii habari ya kufanya mambo nusunusu au juu juu. Kama kuupitisha muungano kibungebunge bila a thorough process iliyowahusisha wananchi wote directly.

      Sasa tushaona hili ni tatizo.Tunatakiwa tujifunze. Tusitake kurudia makosa kwa kufanya swala la muungano liamuliwe na upande mmoja tu wa muungano.

      Tutawapa msemo watu wa bara wanaosema Wazanzibari wanapendelewa.
      waznz ndio walalamikaji katika muungano huu,hakuna haja ya kupoteza pesa kupiga kura nchi nzima, kama hao waznz wakisema wanautaka basi utaendelea na waache chokochoko,kama wao hawautaki utavunjika,hiyo haina hata haja ya kuwauliza wabara maana wautake wasiutake kama waznz wameukataa utavunjikaa tu na wao tu wanatosha.
      Mzee Mwanakijiji likes this.

    17. #54
      Kiranga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th January 2009
      Posts : 14,153
      Rep Power : 41575
      Likes Received
      6055
      Likes Given
      1057

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By tpmazembe
      waznz ndio walalamikaji katika muungano huu,hakuna haja ya kupoteza pesa kupiga kura nchi nzima, kama hao waznz wakisema wanautaka basi utaendelea na waache chokochoko,kama wao hawautaki utavunjika,hiyo haina hata haja ya kuwauliza wabara maana wautake wasiutake kama waznz wameukataa utavunjikaa tu na wao tu wanatosha.
      Utajuaje Wazanzibari ndio walalamikaji bila kuomba maoni ya watu wa bara? If JF is any indication kuna watu wa bara wengi tu hawaupendi muungano pia.

      At least katika mfumo wake wa sasa.
      Mzee Mwanakijiji likes this.
      Allow others to say their say, but always say your piece, it's only right.


    18. #55
      Kiranga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th January 2009
      Posts : 14,153
      Rep Power : 41575
      Likes Received
      6055
      Likes Given
      1057

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By Pasco
      Mkuu Kiranga, sisi bara hatuna sheria ya kura ya maoni. Zanzibar tayari wanayo sheria ya kura ya maoni hivyo kwao ni straight forward.

      Hapa kwetu pia sheria hiyo italetwa baada ya kukusanywa maoni na bunge la katiba, then kura ya maoni itakuwa ndio last option kuipitisha katiba mpya!.

      Hoja ya Mwanakijiji ni very valid, maadam wamethibitisha kwa saini 500, 000 ambayo ni theluthi moja, na wanaamini Wazanzibari wengi hawautaki muungano, kwa nini wasiupinge kwa kuitumia hiyo sheria yao ya kura ya maoni na matokeo kuwa endorsed na BLW hiyo kutoa tuu azimio la utekelezaji huku bara!.

      Kama walibadili katiba yao kuunda SUK ikiwemo kuvunja cheo cha Waziri Kiongozi na badala yake kuweka hao makamo wawili, katiba ya JMT haiyatambui mabadiliko hayo. Kwa mujibu wa katiba ya JMT bado tunamtambua Waziri kiongozi ambaye hayupo na hatuwatambui hao makamo wawili kikatiba ila in reality wapo na huja huku bara na protocal inawatambua.

      NB. Nazidi kusisitiza japo muungano ni illegal before the eyes of the law kwa vile haukuwa ratified na BLW au BLM kwama ilivyotaka sheria, Wanzanzibar wanayo very valid reasons ya kujitoa kwa heshima, tena kihalali bila jinai ya uhaini kwa kuvunja muungano, wakiamua kwa kauli moja kuwa kabla ya BLW kuridhia tume yakukusanya maoni ya katiba mpya ifanye kazi Zanzibar, kwanza vile vipengele vya yale makubaliano ya muungano ambavyo vilikiukwa kwanza viridhiwe na BLW ili kuulegitimize huu muungano kule kwao Zanzibar!. Na kwa kuutumia mwanya huo then wagome kuuratify muungano hivyo muungano huu kuwa rendered illegal na legal process za kuuvunja kufuata!.

      Kwa vile Karume hakujua Kiingereza, I wala hakujua kusoma wala kuandika zaidi ya kusaini kwa dole gumba, then washeria pia wanaweza kuchalenge makubaliano before the court of law kwa kutumia kipengele kiitwacho "privity" kwa kujenga hoja kuwa wakati Karume ikitia dole gumba, hakujua anasaini nini!.

      Baba wa Taifa aliundesha muungano kwa utaratibu wa "the end justifies the means". sheria, taratibu na kanuni, hazikufuatwa!.
      Inaonekana hapa Bunge la Tanganyika lili ratify, lakini hakuna document yoyote ya ku ratify muungano kutoka Zanzibar

      http://www.zanzinet.org/files/legality_union.pdf pp 30/31

      One can make an argument kwamba muungano hauhitaji kura ya maoni bara kwa sababu ulishakuwa ratified na bunge la Tanganyika. Although the best ratification would have been involving the people directly.

      One can also make an argument that so much has changed since then it deserves an fresh, all encompassing, all inclusive second look.

      Muungano ukipigiwa kura ya maoni pande zote ndipo tutapata jibu la kudumu.
      Mzee Mwanakijiji likes this.
      Allow others to say their say, but always say your piece, it's only right.


    19. #56
      MachoMakavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th February 2008
      Posts : 348
      Rep Power : 646
      Likes Received
      36
      Likes Given
      11

      Default

      Timing ya hizi kelele za UAMSHO na Mombasa kutaka kujitoa Kenya inanipa walakini!

      Kuna kitu nyuma ya pazia! Tutajua soon!
      Mzee Mwanakijiji likes this.

    20. #57
      KIDUNDULIMA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th August 2010
      Posts : 559
      Rep Power : 556
      Likes Received
      73
      Likes Given
      244

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Mwanakijiji kwa idadi ya watu umepotosha kidogo. Kama Zanzibar inawatu 1.5 million wenye haki ya kupiga kura ni wangapi? unataka kuniambia kuwa wote hao 1.5 million ni wapiga kura? Kama sio wote wapiga kura, sahihi za watu 500,000 ni asilimia ngapi ya wapiga kura wote. Na ukishapata % ndipo utuambia kuwa ni wachache au ni wengi
      Mzee Mwanakijiji likes this.

    21. #58
      Borakufa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th May 2011
      Location : Tohell
      Posts : 1,164
      Rep Power : 642
      Likes Received
      260
      Likes Given
      207

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Kwa mazingira yapi tuaweza kuachiwa kufanyi hivi mwanakjj anavyoshuari! Wao walishapiga mstari kuwa kuhusu muungano hakuna kitakachobadilika zaidi ya ulivyo labda kutolewe mawazo ya kuuboresha! sasa unafikiri watatuacha tuuvuke mstari waliokwisha upiga!
      Busara ni kufanya jambo kwa wakati sahihi na sehemu sahihi! busara yako mwanakjj haina msaada kwetu sisi kwa wakati huu!
      Mzee Mwanakijiji likes this.

    22. #59
      nderingosha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th March 2011
      Posts : 820
      Rep Power : 1449
      Likes Received
      440
      Likes Given
      119

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Ningependa kujua TOR watakazotumia tume ya katiba kama zitakua zimelizungumziaje swala la mjadala wa uwepo/kutokuwepo kwa muungano...maana kama sikosei wakati wa kuikabidhi kazi tume rais alisema swala la uwepo/kutokuwepo muungano halina mjadala...Sasa baada ya hizi vurugu zenj nimeanza kusikia rhetorics toka kwa hawa marais wa pande zote...Jk na dr.Shein ...kuwa hili suala lijadiliwe kwenye tume ya katiba..Swali langu ni je..tume ya katiba wataliingiza kwenye TOR zao swala la uwepo/kutokuwepo kwa muungano?????..maana kwa mazoea hapa TZ..ni rahisi sana kwa viongozi kusema mambo...lakini utekelezaji huwa hamna....Navyojua swala la muundo wa serikali litakuwepo kwenye TOR za tume ya katiba...Ni jambo la msingi sana kwa sasa....wakati wa fujo hizi za zenj..hawa tume ya katiba wachukue kila kitu kinacholalamikiwa na wazanzibari sasa hivi wakiingize kwenye TOR zao ili wapate maoni ya wazanzibari wote ...na itakapofika wakati wa ile final kura ya maoni ya katiba kwa nchi nzima(referendum) hili jambo nalo lipigiwe kura.......yaani kiwepo kipengele pekee kitakachohusisha kura ya uwepo/kutokuwepo kwa muungano.....maana sioni njia ya haraka tuliyo nayo kama nchi ya jinsi ya kushughulikia hii issue.....maana hawa jamaa wazenj naona wamefanya nao timing wakati huu kabla tume haijaanza kazi ili hili swala lishughulikiwe kipekee.......nadhani this is the time to do it.....
      Last edited by nderingosha; 4th June 2012 at 18:24.
      Mzee Mwanakijiji likes this.
      ....real change begins with PEOPLE.......

    23. #60
      kombo1's Avatar
      Member Array
      Join Date : 27th May 2012
      Posts : 11
      Rep Power : 354
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By Mzee Mwanakijiji
      Kuna maneno na kauli za baadhi ya watu wachache wakizungumza kana kwamba wanawakilisha "wengi". Utasikia mtu anayepinga Muungano anasema "Wazanzibari hatuutaki Muungano" na wakati mwingine kudai "Wazanzibari wengi hawautaki muungano". Sasa mara nyingi wanaposema "wengi" mtu wa kawaida (asiyetaka kufikiri sana) anaweza kuamini kabisa kuwa ni kweli "wengi" hawautaki Muungano.

      Mfano unaotolewa siku za hivi karibuni ni "sahihi 500,000" za wanaodaiwa "Wazanzibari" wasiotaka Muungano. Sasa kwenye mahali ambapo pana watu milioni 1.5 hivi idadi hiyo ni kubwa sana; ni theluthi moja ya watu wote wa Zanzibar. Sasa kama kweli wapo watu wengi hivi njia rahisi ya kutaka kujitoa kutoka kwenye Muungano siyo mihadhara wala hawahitaji kabisa kuwalalamikia watu wa bara au serikali ya Muungano.

      Kwa wanaokumbuka wananchi wa Zanzibar walishinikiza vyama vyao viwili vya CCM na CUF kuunda serikali ya umoja wa kitaifa na waliweza kufanya hivyo baada ya kupitisha sheria ya kura ya maoni ambayo hatimaye iliandika upya katiba ya Zanzibar. Wananchi wakaweza kujitokeza na kupiga kura ya maoni. Walifanya hivi bila kuomba kibali Muungano na kiasi cha kuweza kuandika kwenye Katiba Yao vitu ambavyo ni kinyume na Katiba ya Muungano.

      Sasa kama waliweza kufanya hili ni kitu gani kinawashinda kutaka viongozi wao wa kisiasa kuandia sheria ya kupiga kura ya maoni kama wanautaka Muungano au la? Kwa vile hoja ya kupinga MUungano inadaiwa inakubaliwa na watu wa vyama vyote ni wazi kuwa ni rahisi sana kwa watu wa Uamsho na Wazanzibari wengine kuhakikisha kuwa BLW linapokaa linaazimia kupitisha kura ya maoni kuhusu Muungano na kutaka sheria iletwe ya kuuliza swali la Muungano.

      Swali liwe rahisi tu:

      Je unataka Zanzibar ibakie kwenye Muungano wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania?

      a. Ndio ibakie - Ikibakia kero na matatizo ya Muungano kutatuliwa ifikapo Julai 1, 2014
      b. Hapana isibakie - isipobakia Zanzibar itajitoa ifikapo Julai 1, 2014



      Ijulikane mapema kuwa ikisemwa kuwa "ndio ibakie" manake ni kuwa masuala ya muundo na mfumo wa Muungano yatajadiiliwa na kushughulikiwa kwenye Katiba Mpya na yatakuwa tayari kumalizwa yote ifikapo 2014

      Na ikisemwa Hapana isibakie manae ni kuwa mazungumzo ya kuvunja Muungano yataanza na ifikapo Julai 1, 2014 Zanzibar itajitoa kwenye Muungano.

      Wazanzibar waandae kura hiyo ya maoni wao wenyewe kama walivyofanya kwenye ile ya mabadiliko ya Katiba na lolote watakaloamua Tanzania Bara WATAHESHIMU uamuzi huo.

      Ni rahisi sana kumaliza hoja ya Muungano au kutokuwepo Muungano. Yote YAMO MIKONONI MWA WAZANZIBARI. Hawahitaji kutuambia hawautaki Muungano, hatuhitaji watuambie tunawakandamiza kama wanataka kutoka kweli na siyo mikwara mbuzi njia nyeupeeeee!!! Andikeni sheria, itisheni kura ya maoni, pigeni kuchagua 'b' and then mambo yatakua yameiva ifikapo 2014 tutawasaidia kufunga mizigo.
      Nyinyi Watanganyika ndio msioruhusu kuitishwa kwa kura hiyo kwani huyu Raisi wenu Kikwete hata anapinga Muungano usijadiliwe katika katiba hiyo mpya. Vingine hawa viongozi wetu wa Zanzibar wote wanaogopa kuitisha kura hiyo ya maoni kwani wote ni vibaraka wa vyama vyao ambavyo vyote viko mikononi kwa Watanganyika. Usidanganyike kura hile ya maoni ilifanyika kwa ruhusa ya CCM na mataifa makubwa ya nje waliotaka Zanzibar kuwe na usalama. Hapo awali Rais Aboud Jumbe alipoonesha tuu kwamba anataka kuwe na serikali tatu, mara moja aliitwa Dodoma na kufukuzwa kazi. Zanzibar tunataka uhuru wetu na hii katiba mpya tutaikubali iwapo muungano utakuwa kama hule wa mfumo wa nchi za ulaya magharibi vinginevyo sote wazanzibari tutaukataa mpaka milele. Angalia watu waliojitokeza kupinga muungano, wengi wao ni vijana hii inaonyesha tatizo hili litaendelea kwa muda mrefu sana mpaka zanzibar iwe huru.
      Mzee Mwanakijiji and takashi like this.

    Page 3 of 10 FirstFirst 12345 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...