Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

By
Barubaru
Sijui ahali yangu nitumie lugha gani uweze kunifahamu vizuri labda kiswahili changu kimekuwa kigumu kwako.
Lugha yangu ya asli na ninayoitumia kila wakti ni ile inayoandikwa kutkea kulia kwenda kushoto.
Lakin nimebainisha vizuri kabisa kwako.HUKO TANZANIA KUNA CD ZA MIHADHARA KUHUSU KATIBA MPYA INAYOONYESHWA LIVE KATIKA MOJA YA TV ZA HUKO. Inayofanywa na Prof Issa Shivji ambaye ni mwenyekiti wa kigoda cha maalim JKN.
Kuna mihadhara mitano tu ipo kwenye CD mbili tu na nasikia zinauzwa kila pahala huko Dar es salaam. Sasa muhadhara wa Pili na Tatu umebainisha kuhusu Katiba ya Znz, Katiba ya Tanganyika na Katiba ya Muungano wa Tz. utajifunza mengi sana humo.
Hapo utapata kusikia kila kitu kwa kiswahili mahiri cha Prof Shivji hata kama hujui kusoma utafaidika sana. Huo ndio msaada wangu kwako kukhusu suala lako.
Nakushauri usipnde kila kitu kutafuniwa.
Barubaru,
Naona wewe unayetaka arguments zako zifanywe na CD za mihadhara ndiye unayependa kutafuniwa.
Kama umezielewa jibu swali langu dogo tu, ama sivyo utaonekana umepotoka, umeonyeshwa ulipopotoka, halafu huna hata uungwana wa kukubali kwamba umepotoka.
Pia naona unapenda sana kufanya assumption kwamba wewe peke yako ndiye uliye mbali na Tanzania na wengine wote tuko Tanzania na tunaweza kuzipata kwa urahisi hizo CD, wengine tuko Alaska tunachimba mafuta huku kama wewe huko, CD tutaipata wapi?
Bottom line, umekwepa kujibu swali, umeogopa challenge.
Bunge la Tanzania liliwezaje ku ratify muungano wa Tanzania? Hili jambo ni sawa na kusema mwanao wa kumzaa mwenyewe ndiye aliyetia sahihi cheti chako cha kuzaliwa siku uliyozaliwa, mwanao angewezaje kutia sahihi cheti chako cha kuzaliwa siku uliyozaliwa wewe wakati siku uliyozaliwa wewe yeye alikuwa hajazaliwa?
Last edited by Kiranga; 11th June 2012 at 16:00.
Allow others to say their say, but always say your piece, it's only right.
Follow Us Here