Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

    Report Post
    Page 10 of 10 FirstFirst ... 8910
    Results 181 to 191 of 191
    1. #1
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,518
      Rep Power : 46714
      Likes Received
      16434
      Likes Given
      8469

      Default Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Kuna maneno na kauli za baadhi ya watu wachache wakizungumza kana kwamba wanawakilisha "wengi". Utasikia mtu anayepinga Muungano anasema "Wazanzibari hatuutaki Muungano" na wakati mwingine kudai "Wazanzibari wengi hawautaki muungano". Sasa mara nyingi wanaposema "wengi" mtu wa kawaida (asiyetaka kufikiri sana) anaweza kuamini kabisa kuwa ni kweli "wengi" hawautaki Muungano.

      Mfano unaotolewa siku za hivi karibuni ni "sahihi 500,000" za wanaodaiwa "Wazanzibari" wasiotaka Muungano. Sasa kwenye mahali ambapo pana watu milioni 1.5 hivi idadi hiyo ni kubwa sana; ni theluthi moja ya watu wote wa Zanzibar. Sasa kama kweli wapo watu wengi hivi njia rahisi ya kutaka kujitoa kutoka kwenye Muungano siyo mihadhara wala hawahitaji kabisa kuwalalamikia watu wa bara au serikali ya Muungano.

      Kwa wanaokumbuka wananchi wa Zanzibar walishinikiza vyama vyao viwili vya CCM na CUF kuunda serikali ya umoja wa kitaifa na waliweza kufanya hivyo baada ya kupitisha sheria ya kura ya maoni ambayo hatimaye iliandika upya katiba ya Zanzibar. Wananchi wakaweza kujitokeza na kupiga kura ya maoni. Walifanya hivi bila kuomba kibali Muungano na kiasi cha kuweza kuandika kwenye Katiba Yao vitu ambavyo ni kinyume na Katiba ya Muungano.

      Sasa kama waliweza kufanya hili ni kitu gani kinawashinda kutaka viongozi wao wa kisiasa kuandia sheria ya kupiga kura ya maoni kama wanautaka Muungano au la? Kwa vile hoja ya kupinga MUungano inadaiwa inakubaliwa na watu wa vyama vyote ni wazi kuwa ni rahisi sana kwa watu wa Uamsho na Wazanzibari wengine kuhakikisha kuwa BLW linapokaa linaazimia kupitisha kura ya maoni kuhusu Muungano na kutaka sheria iletwe ya kuuliza swali la Muungano.

      Swali liwe rahisi tu:

      Je unataka Zanzibar ibakie kwenye Muungano wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania?

      a. Ndio ibakie - Ikibakia kero na matatizo ya Muungano kutatuliwa ifikapo Julai 1, 2014
      b. Hapana isibakie - isipobakia Zanzibar itajitoa ifikapo Julai 1, 2014



      Ijulikane mapema kuwa ikisemwa kuwa "ndio ibakie" manake ni kuwa masuala ya muundo na mfumo wa Muungano yatajadiiliwa na kushughulikiwa kwenye Katiba Mpya na yatakuwa tayari kumalizwa yote ifikapo 2014

      Na ikisemwa Hapana isibakie manae ni kuwa mazungumzo ya kuvunja Muungano yataanza na ifikapo Julai 1, 2014 Zanzibar itajitoa kwenye Muungano.

      Wazanzibar waandae kura hiyo ya maoni wao wenyewe kama walivyofanya kwenye ile ya mabadiliko ya Katiba na lolote watakaloamua Tanzania Bara WATAHESHIMU uamuzi huo.

      Ni rahisi sana kumaliza hoja ya Muungano au kutokuwepo Muungano. Yote YAMO MIKONONI MWA WAZANZIBARI. Hawahitaji kutuambia hawautaki Muungano, hatuhitaji watuambie tunawakandamiza kama wanataka kutoka kweli na siyo mikwara mbuzi njia nyeupeeeee!!! Andikeni sheria, itisheni kura ya maoni, pigeni kuchagua 'b' and then mambo yatakua yameiva ifikapo 2014 tutawasaidia kufunga mizigo.
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    2. RukaaJuu Final

    3. #181
      JokaKuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2006
      Posts : 6,841
      Rep Power : 2971
      Likes Received
      2452
      Likes Given
      3533

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By Barubaru
      Awali ya yote nakuomba radhi kwa kukosea kuliandika jina lako vilivyo. Si makusudi yangu kufanya hivyo bali ni vidole vilinipuruchuka kidogo badala kuandika D vikaweka G. Lakin nakuheshimu sana na kuliheshimu sana jina lako na michango yote humu barzani. Nakuomba radhi sana Mkandara.

      Naomba nikujuze kuna Muungano wa KATIBA na wa MKATABA.
      Tanganyika na Znz zimeungana KIMKATABA na hata Katiba yenu ya Muungano na hata ile ya Znz imelibainisha hilo. Kwa manaa nyingine Katiba zenu zote zinaongozwa na yale mliokubaliana tu katika muungano wenu na hilo limepelekea kila nchi kuwa na Katiba yake , Japo Tanganyika imehodhi na kuchukua madaraka kwenye muungano na yale ya Tanganyika.

      Mengi nimebainisha kwenye bandiko hapo juu kuhusu mambo mlioungana.
      Barubaru,

      ..unadai muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni wa mkataba.

      ..wenzako wa Zanzinet nao wanasema wanataka kutoka ktk muungano huu tulionao sasa hivi na kuwa na "muungano wa mkataba."

      ..sasa sisi wa-Tanganyika tuelewe vipi??
      Mzee Mwanakijiji likes this.

    4. #182
      Kiranga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th January 2009
      Posts : 14,194
      Rep Power : 41584
      Likes Received
      6094
      Likes Given
      1065

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By Barubaru
      Ahali yangu.

      Nasikitika kuona wewe Mtanzania hujui chochote kuhusu historia ya muungano wenu. nAKUSHAURI KUNA CD ZA MIHADHARA INAYOTOLEWA NA PROF ISSA SHIVJI HUKO TANZANIA na inaonyeshwa live na moja ya TV station kubwa (sijui Channel 10 au ITV) kuhusu KATIBA Mpya ya muungano. Hapo utapata darsa la historia ya Katiba ya Tanganyika, Katiba ya ZNZ na hata ya Tanzania. itakusaidia sana. Usipende kila kitu wau wakutafunie.

      Lakin lingine lazima ujue Bunge haliwezi kupitisha Katiba yoyote kwa mujibu wa sharia. Bali BUNGE LA KATIBA ndio lena jukumu hilo.


      Sikiliza uchambuzi wa Mwanasharia maarufu Dr Shivji utajifunza na kujua mengi sana kuhusu muungano wenu. Huo ni ushauri wangu kwako.

      Hujajibu swali, una-practise obfuscation.

      Sie tusiokuwa na ilmu kama yako tufafanulie.

      Kabla ya Muungano kulikuwa na Bunge la Tanzania?

      Kama halikuwapo, hiyo ratification unayosema ilifanywa na bunge la Tanzania ilifanywa muda gani? Kabla au baada ya Muungano?

      Kama ilifanywa kabla ya Muungano, bunge lilikuwapoje kabla ya nchi kuwapo?

      Kama ilifanywa baada ya Muungano, ratification gani hii inafanywa baada ya kitu kupitishwa na kupewa idhini ya bunge linalokiidhinisha chenyewe?

      Huoni mapungufu hapo?
      Nguruvi3 likes this.
      Allow others to say their say, but always say your piece, it's only right.


    5. #183
      Barubaru's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2009
      Location : Doha, Qatar
      Posts : 5,745
      Rep Power : 1920
      Likes Received
      1180
      Likes Given
      972

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By JokaKuu
      Barubaru,

      ..unadai muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni wa mkataba.

      ..wenzako wa Zanzinet nao wanasema wanataka kutoka ktk muungano huu tulionao sasa hivi na kuwa na "muungano wa mkataba."

      ..sasa sisi wa-Tanganyika tuelewe vipi??
      Labda utudadavulie.
      Tanganyika ni nini?
      Watanganyika ni akina nani?
      Je Tanganyika ni nchi? kama nchi ina Katiba, bendera na wimbo wa Taifa?.

      Kwa kukusaidia kidogo kuhusu muungano wenu naomba nikujuze mambo mliyoungana ni haya hapa

      The initial “Union Matters†included the following eleven
      areas as Union matters:
      · The constitution and government of the United
      Republic;
      This watermark does not appear in the registered version -
      http://www.clicktoconvert.com
      · External affairs;
      · Defense;
      · Police;
      · Emergency powers;
      · Citizenship;
      · Immigration;
      · External trade and borrowing;
      · The Public service of the United Republic;
      · Income tax, corporation tax, customs and excise duties,
      and
      · Harbours, civil aviation, posts and telegraph.
      Between 1964-1977: through an amendment of the Interim
      Constitution which had reproduced the list of union matters and not
      an amendment of Acts of Union, new items were added to the list of
      Union matters giving the Union parliament and executive more
      powers.
      ADDITIONAL ARTICLES OF UNION
      Other issues added to the list to make the Union matters
      22 were:
      · All matters concern coinage, currency for the
      purposes of legal tender (including notes), banks
      (including savings banks) and all banking business;
      foreign exchange and exchange control
      · Industrial licensing and statistics
      · Higher education
      · Mineral oil resources, including crude oil and natural
      gas
      · The National Examinations Council of Tanzania and
      all matters connected with the functions of that
      Council
      · Civil Aviation
      · Research
      · Meteorology
      · Statistics
      · The Court of Appeal of the United Republic
      · Registration of political parties and other matters
      related to political parties







      Ukiwa mchoyo, usiwe mroho.

      Man Sharaf naf'sahu, fahuwa rasul

    6. #184
      Barubaru's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2009
      Location : Doha, Qatar
      Posts : 5,745
      Rep Power : 1920
      Likes Received
      1180
      Likes Given
      972

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By Kiranga
      Hujajibu swali, una-practise obfuscation.

      Sie tusiokuwa na ilmu kama yako tufafanulie.

      Kabla ya Muungano kulikuwa na Bunge la Tanzania?

      Kama halikuwapo, hiyo ratification unayosema ilifanywa na bunge la Tanzania ilifanywa muda gani? Kabla au baada ya Muungano?

      Kama ilifanywa kabla ya Muungano, bunge lilikuwapoje kabla ya nchi kuwapo?

      Kama ilifanywa baada ya Muungano, ratification gani hii inafanywa baada ya kitu kupitishwa na kupewa idhini ya bunge linalokiidhinisha chenyewe?

      Huoni mapungufu hapo?
      Sijui ahali yangu nitumie lugha gani uweze kunifahamu vizuri labda kiswahili changu kimekuwa kigumu kwako.
      Lugha yangu ya asli na ninayoitumia kila wakti ni ile inayoandikwa kutkea kulia kwenda kushoto.

      Lakin nimebainisha vizuri kabisa kwako.HUKO TANZANIA KUNA CD ZA MIHADHARA KUHUSU KATIBA MPYA INAYOONYESHWA LIVE KATIKA MOJA YA TV ZA HUKO. Inayofanywa na Prof Issa Shivji ambaye ni mwenyekiti wa kigoda cha maalim JKN.

      Kuna mihadhara mitano tu ipo kwenye CD mbili tu na nasikia zinauzwa kila pahala huko Dar es salaam. Sasa muhadhara wa Pili na Tatu umebainisha kuhusu Katiba ya Znz, Katiba ya Tanganyika na Katiba ya Muungano wa Tz. utajifunza mengi sana humo.

      Hapo utapata kusikia kila kitu kwa kiswahili mahiri cha Prof Shivji hata kama hujui kusoma utafaidika sana. Huo ndio msaada wangu kwako kukhusu suala lako.

      Nakushauri usipnde kila kitu kutafuniwa.
      Ukiwa mchoyo, usiwe mroho.

      Man Sharaf naf'sahu, fahuwa rasul

    7. #185
      Barubaru's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2009
      Location : Doha, Qatar
      Posts : 5,745
      Rep Power : 1920
      Likes Received
      1180
      Likes Given
      972

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By Allen Kilewella
      Huu ni mjadala usio na mjadala bali kitu kinachosubiri matendo ya Wazanzibari!! Kumradhi ndugu zetu tunawapenda sana lakini inaonekana sisi ndiyo kikwazo cha kufikia malengo yenu ya Kuigeuza Zanzibar kuwa Hong Kong ya Afrika Mashariki. Kuamua kuhusu hili ni nyie ndugu zetu ambao mmechoka na kero za Muungano kusema ni lini mnataka kutoka kwenye muungano huu.
      Je unajua Rules of Law?
      Je unajuwa kuwa Tanzania ni muumin wa Rules of law?

      Sasa kwa misingi hiyo. Je Znz wana nafasi hapo kujadili muungano wenu?

      Jipambanue na kuona ukweli wa muungano wenu ni kunieleza upenyo upo wapi kwa mujibu wa katiba yenu ya muungano kwa Znz kujadili muungano?

      J unajua Bunge la muungano waliwahi kutoa hoja ya kudai serikali ya Tanganyika? Jee iliishiaje?

      Kama ukijibu hayo utajua ninakusudia nini katika darsa yangu kwako.

      Ukiwa mchoyo, usiwe mroho.

      Man Sharaf naf'sahu, fahuwa rasul

    8. Miaka 50

    9. #186
      warea's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 22nd January 2010
      Posts : 242
      Rep Power : 523
      Likes Received
      52
      Likes Given
      20

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By zomba
      Unasema halafu unajichangana mwenyewe "japo si wote", Sasa na wa Zanzibari ni wote?

      Historia ipi yetu inayotuonesha tunapenda Muungano? Nyerere ndiye aliyeshabikia Biafra ijitenge na Nigeria, Nyerere alihitilafiana na Nkurumah aliyetaka Afrika moja, Nyerere ndiye alivunja East African Community. Sasa hiyo ndio historia ya kupenda muungano?

      Kwa Zanzibar nia siyo kuwa na Muungano ni a ni kuifanya Zanzibar iwe mkoa wa Tanzania, kama ilivyo mengine. Ni kitu hakiwezekani.

      Njia moja ya kuuboresha muungano ni kuanza upya kuutazama kwa matakwa ya wengi na kwa kisheria zilizo wazi. Na sasa ni wakati muafaka tukielekea kwenye katiba mpya, si kama ulivyo sasa, Muungano wa kuburuzwa na Nyerere na Karume ambao haujafata wala hauna kanuni na sheria.

      Simple solution:

      1) Serikali ya Zanzibar, ambayo haitaingilia kabisa mambo ya Tanganyika.

      2) Serikali ya Tanganyika ambayo haitaingilia kabisa mambo ya Zanzibar.

      3) Serikali ya Muungano ambayo itakuwa inashughulikia mambo ya Muungano tu.
      Nakuunga mkono. Nashangaa MM anadai kuwa wabara hawajawahi kukataa muungano huu uliopo. Kundi la wabunge wa G55 miaka ile ilikuwa inadai nini? Bora kila nchi iwe na serikali yake ndipo tuwe na serikali ya muungano.

      Suala la muungano lingejadiliwa kwa kirefu kama watu wote, bara nza visiwani, wangepewa nafasi ya kutoa maoni yao!
      zomba and kwamwewe like this.

    10. #187
      Kiranga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th January 2009
      Posts : 14,194
      Rep Power : 41584
      Likes Received
      6094
      Likes Given
      1065

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By Barubaru
      Sijui ahali yangu nitumie lugha gani uweze kunifahamu vizuri labda kiswahili changu kimekuwa kigumu kwako.
      Lugha yangu ya asli na ninayoitumia kila wakti ni ile inayoandikwa kutkea kulia kwenda kushoto.

      Lakin nimebainisha vizuri kabisa kwako.HUKO TANZANIA KUNA CD ZA MIHADHARA KUHUSU KATIBA MPYA INAYOONYESHWA LIVE KATIKA MOJA YA TV ZA HUKO. Inayofanywa na Prof Issa Shivji ambaye ni mwenyekiti wa kigoda cha maalim JKN.

      Kuna mihadhara mitano tu ipo kwenye CD mbili tu na nasikia zinauzwa kila pahala huko Dar es salaam. Sasa muhadhara wa Pili na Tatu umebainisha kuhusu Katiba ya Znz, Katiba ya Tanganyika na Katiba ya Muungano wa Tz. utajifunza mengi sana humo.

      Hapo utapata kusikia kila kitu kwa kiswahili mahiri cha Prof Shivji hata kama hujui kusoma utafaidika sana. Huo ndio msaada wangu kwako kukhusu suala lako.

      Nakushauri usipnde kila kitu kutafuniwa.
      Barubaru,

      Naona wewe unayetaka arguments zako zifanywe na CD za mihadhara ndiye unayependa kutafuniwa.

      Kama umezielewa jibu swali langu dogo tu, ama sivyo utaonekana umepotoka, umeonyeshwa ulipopotoka, halafu huna hata uungwana wa kukubali kwamba umepotoka.

      Pia naona unapenda sana kufanya assumption kwamba wewe peke yako ndiye uliye mbali na Tanzania na wengine wote tuko Tanzania na tunaweza kuzipata kwa urahisi hizo CD, wengine tuko Alaska tunachimba mafuta huku kama wewe huko, CD tutaipata wapi?

      Bottom line, umekwepa kujibu swali, umeogopa challenge.

      Bunge la Tanzania liliwezaje ku ratify muungano wa Tanzania? Hili jambo ni sawa na kusema mwanao wa kumzaa mwenyewe ndiye aliyetia sahihi cheti chako cha kuzaliwa siku uliyozaliwa, mwanao angewezaje kutia sahihi cheti chako cha kuzaliwa siku uliyozaliwa wewe wakati siku uliyozaliwa wewe yeye alikuwa hajazaliwa?
      Last edited by Kiranga; 11th June 2012 at 16:00.
      Allow others to say their say, but always say your piece, it's only right.


    11. #188
      JokaKuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2006
      Posts : 6,841
      Rep Power : 2971
      Likes Received
      2452
      Likes Given
      3533

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By Barubaru
      Sijui ahali yangu nitumie lugha gani uweze kunifahamu vizuri labda kiswahili changu kimekuwa kigumu kwako.
      Lugha yangu ya asli na ninayoitumia kila wakti ni ile inayoandikwa kutkea kulia kwenda kushoto.

      Lakin nimebainisha vizuri kabisa kwako.HUKO TANZANIA KUNA CD ZA MIHADHARA KUHUSU KATIBA MPYA INAYOONYESHWA LIVE KATIKA MOJA YA TV ZA HUKO. Inayofanywa na Prof Issa Shivji ambaye ni mwenyekiti wa kigoda cha maalim JKN.

      Kuna mihadhara mitano tu ipo kwenye CD mbili tu na nasikia zinauzwa kila pahala huko Dar es salaam. Sasa muhadhara wa Pili na Tatu umebainisha kuhusu Katiba ya Znz, Katiba ya Tanganyika na Katiba ya Muungano wa Tz. utajifunza mengi sana humo.

      Hapo utapata kusikia kila kitu kwa kiswahili mahiri cha Prof Shivji hata kama hujui kusoma utafaidika sana. Huo ndio msaada wangu kwako kukhusu suala lako.

      Nakushauri usipnde kila kitu kutafuniwa.
      Barubaru,

      ..mimi nadhani hiyo mihadhara ya Prof.Shivji inawafaa zaidi watu wenye interest na mambo ya sheria-sheria.

      ..mimi naomba utueleze in a layman language faida za muungano kwa wa-Tanganyika ni nini?

      ..naomba utueleze kwanini tubakie kwenye muungano, au kwanini tuondoke ktk muungano.

    12. #189
      Barubaru's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2009
      Location : Doha, Qatar
      Posts : 5,745
      Rep Power : 1920
      Likes Received
      1180
      Likes Given
      972

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By Kiranga
      Barubaru,

      Naona wewe unayetaka arguments zako zifanywe na CD za mihadhara ndiye unayependa kutafuniwa.

      Kama umezielewa jibu swali langu dogo tu, ama sivyo utaonekana umepotoka, umeonyeshwa ulipopotoka, halafu huna hata uungwana wa kukubali kwamba umepotoka.

      Pia naona unapenda sana kufanya assumption kwamba wewe peke yako ndiye uliye mbali na Tanzania na wengine wote tuko Tanzania na tunaweza kuzipata kwa urahisi hizo CD, wengine tuko Alaska tunachimba mafuta huku kama wewe huko, CD tutaipata wapi?

      Bottom line, umekwepa kujibu swali, umeogopa challenge.

      Bunge la Tanzania liliwezaje ku ratify muungano wa Tanzania? Hili jambo ni sawa na kusema mwanao wa kumzaa mwenyewe ndiye aliyetia sahihi cheti chako cha kuzaliwa siku uliyozaliwa, mwanao angewezaje kutia sahihi cheti chako cha kuzaliwa siku uliyozaliwa wewe wakati siku uliyozaliwa wewe yeye alikuwa hajazaliwa?
      Pole sana ahali yangu kwa sio tu kupitwa na wakti lakin pia kupitwa na technology ya kugundua dunia ni kama kijiji mimi na wewe na wengine tupo nje ya Tz lakin tunajuwa mengi zaidi kuliko pengine mtu aliye kule Bukoli Geitaau Pujini Pemba. Nakushauri SKULI ni kitu bora sana kwa mwan'Adam yoyote kwa minajili sio tu ya kusoma lakin msingi wake mkuu ni KUELIMIKA. Vile kujenga mahusiano na watu ni jambo jema sana.

      Nakushauri tena CD zipo nyingi sana huko TZ hususan Dar es Salaam na hata Znz. Mwambie ndugu, jamaa ahata marafiki zako ndani ya JF wakununulie kisha wazitie posta utazipata na kujifunza mengi sana. Lakin pia hata kwa ku search kwenye mtandao kuhusu historia ya katiba ya TZ itakusaidia na vile vile kusoma vitabu mbalimbli itakusaidia sana kujifunza mengi KULIKO kukalia kuwa nipo mbali na Tz hivyho lazima kila kitu utafuniwe.

      Kwa upeo wangu nimeshafafanua zaidi na zaidi kwenye post mbalimbali humu na sina muda wala wakti wa kurejea tena ni wajib wako kutafuta na kujisomea kwa nia ya kuelewa zaidi na zaidi kuhusu Muungano wenu.

      Nakupa pole sana.

      Ukiwa mchoyo, usiwe mroho.

      Man Sharaf naf'sahu, fahuwa rasul

    13. #190
      Barubaru's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2009
      Location : Doha, Qatar
      Posts : 5,745
      Rep Power : 1920
      Likes Received
      1180
      Likes Given
      972

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By JokaKuu
      Barubaru,

      ..mimi nadhani hiyo mihadhara ya Prof.Shivji inawafaa zaidi watu wenye interest na mambo ya sheria-sheria.

      ..mimi naomba utueleze in a layman language faida za muungano kwa wa-Tanganyika ni nini?

      ..naomba utueleze kwanini tubakie kwenye muungano, au kwanini tuondoke ktk muungano.
      Jokakuu,

      Awali ya yote jina lako JokaKuu linanikumbusha mbali sana. Kulikuwa na mshairi mmoja maarufu sana huko Tanzania akitokea Tabora jina lake alikuwa akiitwa Juma Maganga. na jina lake la ushairi akiitwa JokaKuu. Hongera sana.

      Lakin nilipenda kukujuza kama ulinisoma nilipomwambia MM ambaye ni mtoa mada hii kuwa huwezi kuujadili muungano wenu pasi na kuwa na elimu ya ziada ya Sharia. Kwani pamoja na kuwa Muungano wenu ni wa KIMKATABA lakin umefuata taratibu za Kisharia zzaidi kwa upande wa Tanganyika. Na unafuata msingi ya Katiba yenu ambayo inaongozwa na Mkataba wenu wa Muungano.

      Hivyo kwa njia yoyote huwezi kuacha sharia kuujadili muungano wenu.

      Kuhusu suala lako la pili. Hapo nilifafanua kwa kina sana kuhusu madhil na dhulma wanazofanyiwa wa Znz kutokana na muungano wenu katika bandiko la NINI FAIDA ZA MUUNGANO KWA ZNZ. fuatilia uzi huo utaona nimebainisha kwa kina sana humo. Na nimeanzia na historia ya nchi zenu na makovu ya ukoloni kwa pande zote mlizorithi.

      Kama kuna ziada basi Bismillah


      Ukiwa mchoyo, usiwe mroho.

      Man Sharaf naf'sahu, fahuwa rasul

    14. #191
      WA MAMNDENII's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 5th June 2010
      Location : mamndeni
      Posts : 245
      Rep Power : 504
      Likes Received
      16
      Likes Given
      8

      Default Re: Kama kweli Wazanzibari "wengi" wanataka watoke kwenye Muungano mbona ni rahisi sana...

      Quote By Mzee Mwanakijiji
      Kuna maneno na kauli za baadhi ya watu wachache wakizungumza kana kwamba wanawakilisha "wengi". Utasikia mtu anayepinga Muungano anasema "Wazanzibari hatuutaki Muungano" na wakati mwingine kudai "Wazanzibari wengi hawautaki muungano". Sasa mara nyingi wanaposema "wengi" mtu wa kawaida (asiyetaka kufikiri sana) anaweza kuamini kabisa kuwa ni kweli "wengi" hawautaki Muungano.

      Mfano unaotolewa siku za hivi karibuni ni "sahihi 500,000" za wanaodaiwa "Wazanzibari" wasiotaka Muungano. Sasa kwenye mahali ambapo pana watu milioni 1.5 hivi idadi hiyo ni kubwa sana; ni theluthi moja ya watu wote wa Zanzibar. Sasa kama kweli wapo watu wengi hivi njia rahisi ya kutaka kujitoa kutoka kwenye Muungano siyo mihadhara wala hawahitaji kabisa kuwalalamikia watu wa bara au serikali ya Muungano.

      Kwa wanaokumbuka wananchi wa Zanzibar walishinikiza vyama vyao viwili vya CCM na CUF kuunda serikali ya umoja wa kitaifa na waliweza kufanya hivyo baada ya kupitisha sheria ya kura ya maoni ambayo hatimaye iliandika upya katiba ya Zanzibar. Wananchi wakaweza kujitokeza na kupiga kura ya maoni. Walifanya hivi bila kuomba kibali Muungano na kiasi cha kuweza kuandika kwenye Katiba Yao vitu ambavyo ni kinyume na Katiba ya Muungano.

      Sasa kama waliweza kufanya hili ni kitu gani kinawashinda kutaka viongozi wao wa kisiasa kuandia sheria ya kupiga kura ya maoni kama wanautaka Muungano au la? Kwa vile hoja ya kupinga MUungano inadaiwa inakubaliwa na watu wa vyama vyote ni wazi kuwa ni rahisi sana kwa watu wa Uamsho na Wazanzibari wengine kuhakikisha kuwa BLW linapokaa linaazimia kupitisha kura ya maoni kuhusu Muungano na kutaka sheria iletwe ya kuuliza swali la Muungano.

      Swali liwe rahisi tu:

      Je unataka Zanzibar ibakie kwenye Muungano wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania?

      a. Ndio ibakie - Ikibakia kero na matatizo ya Muungano kutatuliwa ifikapo Julai 1, 2014
      b. Hapana isibakie - isipobakia Zanzibar itajitoa ifikapo Julai 1, 2014



      Ijulikane mapema kuwa ikisemwa kuwa "ndio ibakie" manake ni kuwa masuala ya muundo na mfumo wa Muungano yatajadiiliwa na kushughulikiwa kwenye Katiba Mpya na yatakuwa tayari kumalizwa yote ifikapo 2014

      Na ikisemwa Hapana isibakie manae ni kuwa mazungumzo ya kuvunja Muungano yataanza na ifikapo Julai 1, 2014 Zanzibar itajitoa kwenye Muungano.

      Wazanzibar waandae kura hiyo ya maoni wao wenyewe kama walivyofanya kwenye ile ya mabadiliko ya Katiba na lolote watakaloamua Tanzania Bara WATAHESHIMU uamuzi huo.

      Ni rahisi sana kumaliza hoja ya Muungano au kutokuwepo Muungano. Yote YAMO MIKONONI MWA WAZANZIBARI. Hawahitaji kutuambia hawautaki Muungano, hatuhitaji watuambie tunawakandamiza kama wanataka kutoka kweli na siyo mikwara mbuzi njia nyeupeeeee!!! Andikeni sheria, itisheni kura ya maoni, pigeni kuchagua 'b' and then mambo yatakua yameiva ifikapo 2014 tutawasaidia kufunga mizigo.
      mkuu mjj nakubaliana na wewe kwa mapendekezo yako hii ya kulazimisha ndoa na wakati mmoja wa wanandoa anahisi kutotendewa haki hata familia itakayozaliwa itakuwa na mfarakano tupu na dalili watoto waliozaliwa na WANAUAMSHO, jamani wazenji wapewe nchi yao ili tuikomboe TANGANYIKA yetu
      Barubaru likes this.

    Page 10 of 10 FirstFirst ... 8910

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...