Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Lema amjibu Kikwete, asema yupo tayari kwa lolote kuanzia sasa

    Report Post
    Page 1 of 27 12311 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 537
    1. #1
      kilewo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th February 2010
      Posts : 518
      Rep Power : 583
      Likes Received
      625
      Likes Given
      40

      Default Lema amjibu Kikwete, asema yupo tayari kwa lolote kuanzia sasa

      IKULU ILIINGILIA KESI YA UCHAGUZI. – GODBLESS LEMA.

      Ndugu Wananchi;


      Napenda kutumia nafasi hii kutoa pongezi na shukrani nyingi kwa ndugu zetu wa Arusha kwa kuwapokea vizuri na kuwakarimu vyema wageni wetu hao. Nawaomba waendelee na moyo huo mpaka watakapoondoka wote. Naomba kuwepo kwa mkutano huu kuwakumbushe umuhimu wa mji wenu kuwa tulivu. Miaka miwili iliyopita isingekuwa rahisi kwa watu au shirika kubwa la kimataifa kama Benki hii kuamua kufanya mkutano wake Arusha. Isitoshe hata sisi wenyewe tusingeshawishika kuomba au kukubali maombi ya namna hiyo. Lakini sasa imewezekana. Naomba kila mmoja wetu aweke azimio moyoni mwake la kuhakikisha kuwa hali ile haijirudii tena. Nyota ya Geneva ya Afrika lazima iendelee kuangaza. Yaliyopita si ndwele tugange yajayo . ( J.K . KIKWETE.)

      “Narudia tena , IKULU iliingilia kesi yangu ya Ubunge”.

      Mh Rais nimekusikiliza kwa makini sana ila nakupa pole kwani bado unafikiri unaongea na Tanzania ya mwaka 1961 , umesema sasa Arusha ni shwari tofauti na miaka miwili iliyopita kwani sasa kuna amani na utulivu wa kutosha ndio maana hata mkutano wa AFDB umefanyika Arusha .

      Mh Rais , najua IKULU iliingilia kesi yangu kama ilivyoonekana na ndio sababu hata Mkuu wa Mkoa wa Arusha wakati anaapisha Wakuu wa Wilaya alimpongeza Jaji kwa hukumu nzuri aliyowafurahisha wakati kesi hiyo iko mahakama ya Rufaa , lakini jambo moja la msingi ambalo huwezi kulitambua kwa sasa ni kuwa Haki na Ukweli haviwezi kushindwa na dhuluma, ubaya wala mamlaka , natambua wewe ni Rais na unayo mamalaka makubwa katika Taifa hili lakini vile vile nataka utambue kuwa huna mamlaka makubwa dhidi ya haki , utu na ukweli.

      Mh Rais hakuna Amani Duniani inayozidi Haki na usawa ,utu na ukweli , haipo na wala haitakuwepo , ndio maana kila siku nasema ni "Afadhali Vita Inayotafuta Haki na usawa kuliko Amani inayopumbaza na kudhalilisha utu wa Mwanadamu" umefurahia sana mkutano uliokupa fursa ya kutoa maneno ya kebehi na kudhihirisha ila chafu iliyofanywa na Serikali yako na kujaribu kuhadaa Umma kama ilivyo kawaida ya Serikali yako na Chama chako. Hata hivyo wakati huu kuna mambo ya msingi yakushughulikia zaidi ya kebehi na hadaa, Uchumi wa Nchi umeyumba, huduma za msingi za jamii zimepuuzwa, Mpasuko katika suala la Muungano na vururugu zinazoendelea Zanzibar, mfumuko wa bei hizi ni sababu chache ambazo haziwezi kuruhusu wakati huu kuwa wakati wa kebehi na mizaha isipokuwa kazi .

      Mh Rais, Mama Theresa, Nelson Mandela, Martin Luther Jr na Malcom X hawakuwa Wabunge kupigania haki za Nchi yao na watu wao. Sihitaji Ubunge kupigania ukweli, haki na utu, nahitaji dhamira safi, nia njema na huu utakuwa wajibu wangu mpaka nakwenda kaburini, nitakapomaliza mbio hizi najua nitapata fursa ya kutazama nyuma yangu nione nini nilifanya. Ukweli nisingependa kuona vituo vya mafuta, magorofa, magari na viwanja vingi kila kona ya Nchi bali Haki, Usawa na utu vikiwa kama nguzo ya imani ya watawala wetu watakaokuwepo. Pengine sitaishi miaka mingi sana kama utachukizwa sana na waraka wangu huu kwani Polisi, Usalama wa Taifa na Jeshi la Wananchi wanakutii wewe, hata hivyo siogopi kufa kwani nisipokufa kesho, nitakufa siku moja ambayo siijui, napenda kuishi maisha marefu nimwone mke wa mtoto wangu kama itawezekana, lakini kuliko iwezekane kwa kuishi kwa hofu ni bora ishindakane kwa kuthamini haki. Kwa hiyo kama utakuwa umekasirika sana, unaweza kufanya jambo lolote baya kwa kutumia mamlaka yako, niko tiyari sio kesho wala leo isipokuwa sasa hivi, najua IKULU imewazulumu watu wa Arusha Mbunge wao.

      Mh Rais ninajua wazi njama zote na hasira hizi zinaweza kuwa zimetokana hasa na mkutano tuliokaa Osterbay Dar mimi na wewe kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 hata hivyo sikupuuza maongezi yetu isipokuwa nilichagua kufuata dhamira yangu na wito wangu wa utumishi wa kweli katika Jimbo langu na Nchi yangu.

      Mh Rais nimekuelewa na Wananchi wamekuelewa kila mahali , wewe ni Rais unayo mamlaka makubwa na mimi ni mwananchi mamlaka yangu makubwa ni kwa mke wangu tu , sina Polisi wala Usalama wa Taifa lakini nitawaomba wanyonge wafunge na kusali tuone kama mamlaka yako inaweza kushindana na haki na ukweli .

      Mh Rais “Mtu anaweza kuzini kwa siri lakini hawezi kuugua ukimwi kwa siri” Serikali na Chama cha Mapinduzi kimepuuza watu na haki zao kwa muda mrefu , lakini wakati umefika ambapo hawatapuuzwa tena hata hivyo kwa kauli yako hii naamnini haiwezi kuwafundisha kazi majaji wa mahakama ya rufaa .

      ONLY TIME WILL TELL”.


      GODBLESS .J. LEMA.



    2. #2
      Rejao's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th May 2010
      Location : Long Street
      Posts : 8,775
      Rep Power : 25659
      Likes Received
      3353
      Likes Given
      2881

      Default re: Lema amjibu Kikwete, asema yupo tayari kwa lolote kuanzia sasa

      Jamani CDM msaidieni huyu mtu wenu. Naona kama hayuko sawa!

    3. #3
      DALLAI LAMA's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 21st February 2012
      Posts : 3,122
      Rep Power : 0
      Likes Received
      741
      Likes Given
      0

      Default re: Lema amjibu Kikwete, asema yupo tayari kwa lolote kuanzia sasa

      Lema napenda unavyojiamini
      Papizo, The Fixer, AZIMIO and 2 others like this.

    4. #4
      Bajabiri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 9,741
      Rep Power : 2888
      Likes Received
      1115
      Likes Given
      52

      Default re: Lema amjibu Kikwete, asema yupo tayari kwa lolote kuanzia sasa

      Dah,,,,hahahahahha..........na baki naasama mdomo tu hapa....wanasiasa bhana,,,,,,leo yote yapo wazi,,,kumbe mlikaa Oysterbay?????shabassssh...... ..

    5. #5
      Bajabiri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 9,741
      Rep Power : 2888
      Likes Received
      1115
      Likes Given
      52

      Default re: Lema amjibu Kikwete, asema yupo tayari kwa lolote kuanzia sasa

      Uko wapi Rweyemamu????njoo ujibu hapa.......hatutaki ubishi
      Sangarara likes this.


    6. #6
      only83's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th October 2010
      Location : Dodoma-Mjengoni
      Posts : 4,202
      Rep Power : 1859
      Likes Received
      1445
      Likes Given
      1560

      Default re: Lema amjibu Kikwete, asema yupo tayari kwa lolote kuanzia sasa

      Kauli za kamanda Godbless Lema zinachochea kupigania haki, hakika huyu jamaa ni chachu ya mabadiliko kwa kizazi hiki...Endelea kamanda, bora kufa ukiwa unapigania haki na utu wa mwanadamu kuliko kuishi miaka 100 ya udhalimu na ujambazi. Godbless Lema ni mwanamapinduzi wa kweli hakika kauli zake zinachochea kupigania haki.

      Mungu Ibariki Tanzania, Mungu ibariki CHADEMA, Mungu mbariki Godbless Lema.
      Tulianza na MUNGU, tunaendelea na MUNGU, tutamaliza na MUNGU.
      "Problems can not be solved by the same level of thinking that created them"
      "Matatizo hayawezi kutatuliwa na uwezo ule ule mdogo wa watawala wa CCM walioyasababisha"




    7. #7
      Ruppy karenston's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th June 2011
      Posts : 396
      Rep Power : 486
      Likes Received
      69
      Likes Given
      26

      Default re: Lema amjibu Kikwete, asema yupo tayari kwa lolote kuanzia sasa

      Nimependa maneno ya Lema, haki daima hushinda dhuluma!

    8. #8
      Kasheshe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th June 2007
      Location : Bububu
      Posts : 3,630
      Rep Power : 1351
      Likes Received
      196
      Likes Given
      344

      Default re: Lema amjibu Kikwete, asema yupo tayari kwa lolote kuanzia sasa

      Aisee... Kumbe hotuba ya JK ilitaja mtu... kweli simple people real have problems....
      Waberoya and wantuzu like this.

    9. #9
      dosama's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th December 2010
      Posts : 736
      Rep Power : 577
      Likes Received
      296
      Likes Given
      1

      Default re: Lema amjibu Kikwete, asema yupo tayari kwa lolote kuanzia sasa

      Pamoja sana mkuu

    10. #10
      mshikachuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2010
      Posts : 2,358
      Rep Power : 904
      Likes Received
      435
      Likes Given
      2288

      Default re: Lema amjibu Kikwete, asema yupo tayari kwa lolote kuanzia sasa

      Duuh maneno mazito sana haya!...yaani yamejaa hekima,busara na hoja ya nguvu. Hongera sana Lema.
      Mlingwa likes this.

    11. #11
      Kasheshe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th June 2007
      Location : Bububu
      Posts : 3,630
      Rep Power : 1351
      Likes Received
      196
      Likes Given
      344

      Default re: Lema amjibu Kikwete, asema yupo tayari kwa lolote kuanzia sasa

      Something is Wrong with Lema... time will tell.

    12. #12
      silie's Avatar
      Member Array
      Join Date : 1st September 2011
      Posts : 14
      Rep Power : 396
      Likes Received
      2
      Likes Given
      2

      Default re: Lema amjibu Kikwete, asema yupo tayari kwa lolote kuanzia sasa

      Quote By DALLAI LAMA View Post
      Lema napenda unavyojiamini
      Mungu yu nawe,na haki ya kila mwananchi inaweza kucheleweshwa,lakini itakuja tu!!!

    13. #13
      magosha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th April 2012
      Posts : 351
      Rep Power : 431
      Likes Received
      36
      Likes Given
      9

      Default re: Lema amjibu Kikwete, asema yupo tayari kwa lolote kuanzia sasa

      Mh Rais “Mtu anaweza kuzini kwa siri lakini hawezi kuugua ukimwi kwa siri” Serikali na Chama cha Mapinduzi kimepuuza watu na haki zao kwa muda mrefu , lakini wakati umefika ambapo hawatapuuzwa tena hata hivyo kwa kauli yako hii naamnini haiwezi kuwafundisha kazi majaji wa mahakama ya rufaa .

    14. #14
      Mzee wa Rula's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th October 2010
      Posts : 6,517
      Rep Power : 24928
      Likes Received
      2234
      Likes Given
      1829

      Default re: Lema amjibu Kikwete, asema yupo tayari kwa lolote kuanzia sasa

      Duuuuh hapa lazima tifu lizuke tena baina ya Ikulu na Lema, JK kalianzisha tena.


    15. #15
      andrews's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 28th March 2012
      Posts : 1,683
      Rep Power : 0
      Likes Received
      143
      Likes Given
      76

      Default re: Lema amjibu Kikwete, asema yupo tayari kwa lolote kuanzia sasa

      SALVA RWEYEMAMU UKAE DAR HUKOHUKO BAADA 2015 MAANA UKIJA BUKOBA UTATUELEZA KWANINI UMETUUZA KWA JAKAYA,NAPE NAE MWISHO NI 2015

    16. #16
      Comi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd October 2011
      Posts : 1,031
      Rep Power : 596
      Likes Received
      164
      Likes Given
      2

      Default

      Duh, katika kauli hii kuna mengi sana yaliyojificha

    17. #17
      Kiby's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th November 2009
      Posts : 3,540
      Rep Power : 1201
      Likes Received
      605
      Likes Given
      33

      Default re: Lema amjibu Kikwete, asema yupo tayari kwa lolote kuanzia sasa

      Sisi ni wafungwa wa kweli haki na usawa. Na hatutalala hadi vitu hivi vimetamalaki katika jamii yetu sasa na kwa vizazi vijavyo. Mwenye kuthulumu atafurikishwa na kimbunga cha ghadhabu ya Mungu na mwenye haki hata mafuriko yajapofurika kwa kiwango cha kusukwasukwa, bwana atainua kiwango dhidi yake. Bendera ya mwenye haki itapepea juu ya maji ya mafuriko daima, wala kamwe haitakaa izame ndani ya hayo maji yaliyofurika.
      .
      MVUMBUZI and cicy like this.

    18. #18
      Babkey's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th December 2010
      Posts : 2,045
      Rep Power : 929
      Likes Received
      406
      Likes Given
      167

      Default re: Lema amjibu Kikwete, asema yupo tayari kwa lolote kuanzia sasa

      Mh!! Nahisi baridi ghafla!
      Haya, ndio siasa hiyo.

    19. #19
      Mohamed Ngwasu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 11th May 2011
      Posts : 171
      Rep Power : 445
      Likes Received
      27
      Likes Given
      70

      Default re: Lema amjibu Kikwete, asema yupo tayari kwa lolote kuanzia sasa

      du mie hoi.

    20. #20
      Mwanajamii's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th March 2008
      Posts : 7,085
      Rep Power : 1814
      Likes Received
      24
      Likes Given
      13

      Default re: Lema amjibu Kikwete, asema yupo tayari kwa lolote kuanzia sasa

      uchaguzi arusha ufanyike ili lema akatwe kilimi limi rasmi
      Le Grand Alexei likes this.

    Page 1 of 27 12311 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...