Yule mwanasiasa mahiri na machachari katika upinzani wa kwanza kwanza yuko hai na kama yu hai yuko wapi kwa sasa na anajishughulisha na kitu gani?
Maana wakati ule alikuwa maarufu sana wakishirikana na kamanda Wilfred Rwakatare ambaye sasa yuko M4C.
Bandugu; Wenye kujua taarifa zake wazimwage hapa jamvini na walio na mawasiliano naye wamwambie siasa sasa ni M4C na kama anataka kurudi ulingoni basa amfuate Rwakatare kwenye chama makini.
kajunju.
Katika wachangiaji wooote wa hapa ni wewe tu unayeonekana unmfahamu kwa siku za karibuni. Kama unaweza kumpata fikisha ujumbe huu kwake kuwa siasa ni sawa na mtoto mdogo anayeanza kutambaa na anayetamani kutembea. Mara zote katika kujifunza kutembea hujikwaa na kuanguka mara kwa mara. Lakini katika kujikwaa na kuanguka anguka huku hakutakiwi kukata tamaa hata kidogo.
Mweleze kuwa wana JF wanamtaka sjidhirishe ksma yupo hai duniani na kwamba tundhani kuwa kwa sasa kipo chama makini zaidi ambacho yeye kitamfaa. Mwambie amuulize mwenzake Wilfred Rwakatare.
Unakumbuka alipotolewa high table Nkrumah hadi akupoteza kiatu, jamaa alikuwa mkorofi sana, watu wanamvuta aondoke yeye akashikilia meza kidogo aanguke nayo kwenye stage, i think it was 1991 or 92 kama sikosei.
He gave a prophetic truth
wakati Cuf wanataka kuchukua nchi mwaka 2000 CCM walikuja na single ya kusema Cuf ni waislamu na kwa sasa wanadai sisi Chadema ni chama cha wakristo sasa CCM nacho ni cha watu gani? Watu wakajibu mashetaaaaaniiiiii.!---Wana Kigoma.
....Pamoja na kansa ya uongozi wa CCM watu wataendelea kukichagua,au watu wanaweza wakachoka na kusema potelea mbali wakachagua chama KINGINE....Julius. Kambarage. NYERERE"
Mkuu Kimbunga umenikumbusha mbali sana zile barua za Dean of students (Manongi?) tulizopewa....tell us who intimidated you... watu wakajidai kufunguka ma-page na ma-page kumbe waliojieleza sana ndio walikuwa taget na ndio wengi waliofuatiliwa.
Feedback nami nachanga kati ya Manongi na Magimbi!
CCM na CDM vyote ni vyama vya siasa vinavyoongozwa na wanasiasa; tofauti yao kubwa ni moja kwamba kimoja kina dola kingine kinataka kushika dola.
Mtungilehi hivi sasa ni mhubiri wa Injili ya upako mahali fulani jijini DSM. Amekariri Biblia tangu Mwanzo hadi Ufunuo. Kila kitu anakiona kwa miwani ya Kibiblia. Kushindwa kwa Kikwete kuongoza nchi anaona ni mpango wa Mungu; kuibuka kwa CDM anaona ni mpango wa shetani. Kuangamia kwa TLP anasema ni fundisho maalum kutoka kwa Mungu. Lyatonga Mrema anasema ni shetani anayetumiwa na Mungu kuwapiga watanzania! Huwezi kumwelewa kirahisi. Magamba wamwendea kumtaka arudi kwenye uringo wa siasa akakataa japo ana dhiki isiyo ya kawaida. CDM wameongea naye amekataa pia. Bado anaipenda TLP lakini anasema wakati wa Mungu haijafika.
MY take: Wale wanaomfahamu na kuthamini michango yake, watoe mchango wa hiari, tutume wajumbe wakamsalimie na debe la unga ili tupate pa kuanzia maongezi naye. Ana dhiki isiyo ya kawaida.
Mkuu hebu nikumbushe huyu Maswi ndiye yule alikuwa anapenda kuvalia suruali tumboni?
Kuna siku tulikuwa pale Utawala tumegoma baada ya kumpindua Mutungirehi, tukaambiwa tuchangue watu watano watuwakilishe kwa VC yeye akawemo. Nasikia walipoingia ofisini kwanza waliombwa IDs zao pili wakaambiwa kama mnataka kuendelea na shule kawaambieni wenzenu watawanyike sasa hivi, walipotoka jamaa tumbo lilikuwa limekwisha kabisa suruali ilikuwa imeshuka karibu kudondoka.
Umenikumbusha mbali sana mkuu. Mimi mwaka huo ndo Fresher, Nakumbuka hat Freshers' ball haijapigwa kama sikosei. Kuna jamaa mmoja alisimama akasema "Tulimchangua kidemokrasia na tumempiga kidemokrasia", akawekwa ktk kamati ya kwenda kwa Dean, waliporudi hali ilikuwa imebadilika Confidence Zero, hawataki kusikia lingine zaidi ya kutwambia RUDINI Darasani.
Ndipo akajitoleza mmoja wa wanakamati nakumbuka alikuwa anaitwa NIPASHE (utani) naye alijiita hivyo pia. Akasimulia kuwa walipofika ofisini, Professor Masenge aliwauliza kila mmoja jina halafu akapiga simu aletewe mafaili yao wao wote baada ya hapo akayaweka pamoja na wale waliokuwa wamesimamishwa. Akawaambia waje watuambie turudi darasani la sivyo watajuata kushawishi watu wagome.
Jamaa aliyekuwa anavalia suruali tumboni yupo namfahamu lakini si mpiganaji tena bali mfanya biashara fulani wa mishe mishe na mfanyakazi wa Serikali ama wakala.
Pia Kuna jamaa alisoma FOE miaka mingi alikuwa anaitwa HAROLD (?) yupo wapi siku hizi alikuwa mstari wa mbele kupanda jukwaani. Pia kuna jamaa mmoja hivi alikuwa mlemavu lakini alipanda jukwaani kumshusha Mtungirehi sijui naye kaishia wapi kwani gongo lake lilitumika katika purukshani zile.
By the way Mtungirehi alikuwa Ngwini alikuwa anaandika tarehe kwa maneno niliona tangazo lake moja likiwa hivyo, hivyo si rahisi kuja huku JF kwa wanfunzi wa wakati ule.
I am not the same person today as I was 10, 20, or 30 years ago, for I have welcomed life's changes on my heart, face, and mind.
Nilikutana nae January 2012 maeneo ya posta kwa kweli amechoka sana kiafya na kifedha huwezi amini ukimuona ila tatizo lake kubwa ni ulevi.Analewa vibaya sana.
Huenda anahitaji ushauri inaonekana kapoteza matumaini ya kisiasa.
Benedicto Mtungilehi Mtachoka. Ni mhima wa Ruhita karibu na mabira wilaya mpya ya kyerwa(karagwe) .Ni mzuri kwa maneno hovyo sana kwa vitendo na ana unafiki mkubwa sana
Umenena mkuu maana huyu alikuwa mbunge wangu miaka hiyo tukamshutukia tukapiga chini.
Nimeongea nae kwa cmu.ile cm niliyoweka hewani ni yake. Wengi walimtumia msg zenye ujumbe mbalimbali.kasema ujumbe ataufanyiakaz. Maneno ya royals aliyoyaweka niliyanote na kumsomea. Kasema tutawasiliana zaid ila anawashukuru kwa msg zenu. Kweli kaokoka na yuko dar. Nilimsisitiza atembelee jf aone lile watu wanalomzungumza liwe zuri au baya
Kweli JF haina mpinzani!!!!! Wadau nimeingia humu na hizi simulizi nimecheka hadi machozi yamenitoka maana mmenikumbusha mambo ya migomo na hasa Rev Square....nimeingia 96/97 ndio tukawa tunashangaa pale Rev Square wanafunzi walivuokuwa hawana uoga wa kuwasema viongozi wa utawala pale chuoni kwetu ilikuwa ni miujiza maana tumetoka boarding zenye nidhamu wa woga kichizi..!!!it was just soo exciting and a revealtion for many of us...ila wakati wetu hakukuwa na migomo sana sema ndio tulijifunza kuwa ukitaka haki shurti uwe jasiri kuiongelea na kuitetea...
Nimeongea nae kwa cmu.ile cm niliyoweka hewani ni yake. Wengi walimtumia msg zenye ujumbe mbalimbali.kasema ujumbe ataufanyiakaz. Maneno ya royals aliyoyaweka niliyanote na kumsomea. Kasema tutawasiliana zaid ila anawashukuru kwa msg zenu. Kweli kaokoka na yuko dar. Nilimsisitiza atembelee jf aone lile watu wanalomzungumza liwe zuri au baya
Kajunju
Wewe unastahili kufanya kazi na CIA. Ni kamanda mzuri kwa upekuzi.
Jitahidi hadi aache maandiko yake hapa kupitia kwenye akaunti yako yako ya JF.
Kwa namna ya siasa ilivo sasa yeye ni mtu muhimu sana. Mwanaume hafi huku anajiona.
Dah! Kweli mmenikumbusha mbali hasa juu ya huyu traitor! Nakumbuka siku hiyo, ilikuwa vurugu mtindo mmoja. Mi sikumbuki kilichoniumiza mguuni wakati tunamvuta Mtungirehi baada ya kugoma kuachia kiti kwa usaliti wake. Kweli siku hazigandi, naona hata wewe ndugu yangu Kimbunga umekwisha kuwa Full Bawa! Pia ukinikumbusha enzi hizo Intimidation nahisi ubaridi yabisi rohoni maana jamaa walitukomoa hasa.
Nakumbuka ilikuwa jumapili mwaka 2007 nilikutana nae kwa wilfred rwakatare sinza wajiandaa kwenda kwa mrema lyatonga ,wametoka kutangaza list ya mafisadi mwembeyanga pamoja alikuwa na soksi zimetoboka miguuni,alipoongea nlijua kuna ukamanda ndani yake !
Benedicto Mtungilehi Mtachoka. Ni mhima wa Ruhita karibu na mabira wilaya mpya ya kyerwa(karagwe) .Ni mzuri kwa maneno hovyo sana kwa vitendo na ana unafiki mkubwa sana
Mkuu hebu nikumbushe huyu Maswi ndiye yule alikuwa anapenda kuvalia suruali tumboni?
Kuna siku tulikuwa pale Utawala tumegoma baada ya kumpindua Mutungirehi, tukaambiwa tuchangue watu watano watuwakilishe kwa VC yeye akawemo. Nasikia walipoingia ofisini kwanza waliombwa IDs zao pili wakaambiwa kama mnataka kuendelea na shule kawaambieni wenzenu watawanyike sasa hivi, walipotoka jamaa tumbo lilikuwa limekwisha kabisa suruali ilikuwa imeshuka karibu kudondoka.
Mkuu Feedback, aliyekuwa anavalia suruali tumboni aliitwa Ladislaus Malima, walipoingia utawala na kuchimbwa mkwala na Afisa utawala, wakati ule Prof. Masenge, yeye alipotoka aliwaambia watu kuwa 'mimi simo anayeendelea na mgomo shauri yake!', akatokomea mtaani ingawa walipofukuzwa viongozi wa kunji naye alikuwemo.
Maswi alikuwa Vice President wa Mutungirehi, wakati ule tulimwita Chacha Maswi, baada ya Mutungirehi kushushwa hightable pale Nkurumah na kuishia dispensary, Chacha alikaa mezani akatangaza 'DEMOKRASIA IMECHUKUA MKONDO WAKE, na tukaendelea na mkutano kila mtu akidahania yangeishia hapo.
Kutokana na majadiliano haya, wanaCCM wanaweza kuona kuwa Watanzania wanawajua watu mahiri, wa kawaida,wajinga, wapumbavu, wajaja na wezi bila kukosea. Inaonyesha wakati wa ubunge wake watu walimkubali na wakati wa uanafunzi wake kuna makosa aliyafanya. Hatimaye baadhi ya Watanzania wanatamani ashiriki kwenye siasa za sasa akitokea upinzani.
Nijuavyo huyu bwana ni mtu makini sana na anao uwezo wa kuona mbali na hakika ni mwanasiasa ambaye mchango wake unahitajika sana kwa sasa. Endeleeni kumshawishi na hata Chama kama CDM kinaweza kumtumia katika majukumu ya kiutendaji na kukisaidia chama katika ngazi za mkoa na wilaya kwa tiketi ya utendaji. Wanasiasa wetu katika ngazi ya wabunge na madiwani wanahitaji kusaidiwa sana katika kutimiza malengo ya kisiasa. Wakati mwingine wanahitaji hata kutungiwa ratiba ya kushiriki katika mikutano ya vijiji na kata.
Follow Us Here