Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Tundu Lissu, kwa hili, kachemka

    Report Post
    Page 3 of 4 FirstFirst 1234 LastLast
    Results 41 to 60 of 74
    1. #1
      zimmerman's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th February 2011
      Posts : 335
      Rep Power : 486
      Likes Received
      258
      Likes Given
      66

      Default Tundu Lissu, kwa hili, kachemka

      Jana usiku nimemsikiliza kwa makini mheshimiwa Tundu Lissu kwenye kipindi cha Kipima Joto cha ITV kuhusu mada iliyosema, Je kundi la Uamsho lipo juu ya sheria? Argument ya Lissu ilikuwa kwamba fujo zote za Uamsho kuchoma moto makanisa kule Zanzibar, zisitazamwe kidini bali ziaminike zaidi kuwa ni frustrations za kisiasa hasa hasa kuhusu Muungano kwamba serikali imewaminya watu kuzungumzia uwepo au kutokuwepo kwa Muungano, bali imewapa option ya kutoa maoni ya kuuboresha.

      Akakoleza chumvi zaidi bwana Lissu pale alipotoa mifano ya Kanisa la kwanza East Africa kujengwa Zanzibar, na kwamba kule Egypt Ukristo umekuwepo more than 2, 000 years (Coptic Church), na uko kote (Zanzibar na Egypt) Waislamu walio wengi wameishi pamoja kwa amani na Wakristo walio wachache. Kwa hiyo udini wa Waislamu kuwachukia Wakristo kutokana na imani yao hauwezi kuwa hoja halisi iliyosababisha mali za Wakristo kuharibiwa hivi karibuni na Waislamu huko Egypt na Zanzibar bali siasa ndo mshtakiwa wa kwanza.

      Kwa haraka haraka unaweza ukaaminishwa na hoja hii ya Lissu pamoja na ushawishi wake wa hoja hiyo. Pamoja na kwamba mimi binafsi namkubali Lissu lakini hapa kaonyesha udhaifu mkubwa. Ni kama vile bwana Lissu kapitiwa hivi na mambo yanayoendelea ulimwenguni kuhusiana na vikundi vya aina ya Uamsho kwenye nchi zingine. Kuanzia kwa baba lao Al Qaeda, Al Shabab ya Somalia, Boko Haramu ya Nigeria, Taleban ya Pakistan na Afghanstan, na kadhalika.

      Kwa maoni yangu Uamsho ni kikundi tu cha kigaidi kama vikundi vinginevyo vyote nilivyotaja hapo juu, tofauti yake ni kwamba kipo katika hatua za kwanza za kuelekea ugaidi original. Vikundi vyote vya kigaidi hasa vile vinavyotumia uislam huwa vina jambo moja linaloviunganisha. Vyote ni fundamentalist kwenye theolojia yake na vinasukumwa na nia (kwao ni nia njema) ya kutaka kutakasa dini yao kutokana na hatari wanayohihisi kwamba nguvu za kisecular na kikiristo zinaikaba na wanataka kurudisha enzi zile za Uislam safi (sharia itawale serikali, “uchafu” wote kama bar, guest houses, na kadhalika usafishwe ili kurudisha imani halisi na iliyo safi).

      Al Qaeda kiliundwa baada ya Wamarekani kuweka bases zake za kijeshi Saudi Arabia ili kuipiga Iraq miaka ya 90, maana Osama bin Laden aliona ni aibu kwa nchi yake yenye makazi mawili matakatifu ya Allah (Mecca na Medina) kuweka bases za kijeshi, ishara ya kutawaliwa na Kafir mkuu, Marekani.Na kumbuka katika Uislamu siasa na dini haviwezi kutenganishwa, Lissu yampasa ajielimishe vizuri na theology ya Kiislamu.

      Boko Haramu, tafsiri yake ni Western Education is Haram, yaani elimu ya Magharibi ni haramu, unaweza kupata hisia kwamba dini inawasukuma kusafisha kila kitu kilicho na ideals za kimagharibi ukiwemo Ukristo na ndio maana Makanisa hayatakiwi kuwepo kule kaskazini mwa Nigeria.

      Uamsho ya Zanzibar ina vichembe hivyo hivyo vya kuhisi Zanzibar inaanza kukengeuka kutoka kwenye Uislam sahihi. Muungano unachukuliwa kama culprit wa kwanza aliyesababisha Zanzibar kujaa baa, vijiwe vya kiti moto, Makanisa ya Kikristo kila shehia ya Zanzibar, watoto wa kike wa kizanzibari kuanza kuvaa kama wabara, na megineyo mengi.

      Wale wote wanaotumia hoja ya kanisa la kwanza EA kujengwa Zanzibar, wanasahau kwamba enzi zile kanisa lilelilionekana kama siyo threat kwa utamaduni wa kiislamu, after all waliosali mule ni wazungu wawili watatu pamoja na weusi wachache. Kanisa lenyewe moja. Zanzibar ya sasa imebadilika sana siku za hivi karibuni. Makanisa yameongezeka sana na hili linawatisha Wazanzibari. Maredio mengi ya FM yameanzishwa na muziki wa bongo fleva unapigwa sana ikiwemo chombeza chombeza sex stories kwenye hizo redio.

      Hili linawakera sana mafundamentalists na wanaona pa kuanzia ni Muungano kuuvunja ili wapate control kamili ya kuendesha serikali kwa kanuni zisizofungamana kwa namna yoyote na katiba ya kisecular ya serikali ya Tanganyika.

      Lissu anaweza akawa na nia nzuri ya kutofungamanisha mainstream Islam na vurugu zinazojithibisha kidini. Lakini ukweli upo pale pale kwamba Uamsho na vikundi vinginevyo vilivyopo huko Zanzibar vipo motivated zaidi na dini. Tafsiri yao ya fundamentalist Islam ya kutotenganisha dini na serikali inaweza isiwe muafaka kwa wakati huu lakini hilo ndilo linalowasukuma. Kwao Uislam Zanzibar umeingiliwa na yapaswa kuusafisha.

      Kuvunja Muungano ni hatua ya kwanza, na kama wakifanikiwa hatua zingine zitafata.
      Last edited by zimmerman; 5th June 2012 at 10:18.
      Meshili, MpendaTz, rifwima and 6 others like this.

    2. Miaka 50

    3. #41
      Hofstede's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2007
      Posts : 3,604
      Rep Power : 21342
      Likes Received
      981
      Likes Given
      988

      Default Re: Tundu Lissu, kwa hili, kachemka

      Quote By panadol
      Acha kuunga tu hoja bila kuitafakari unaunga tu hoja kwa sababu imesemwa na Lisu,kiongozi ndani ya chama chako , huo ni upofu wa mawazo fikra mgando,hujiulizi why wachome makanisa tu iweje wasichome misikiti, mali za serikali au wasichome vyote kwa pamoja? Acha upimbi amka tumia akili yako kuchanganua jambo angesema Mh Nape ungempinga ila tu kwa sababu kasema Mh Lisu unaunga tu mkono bila kuchanganua!
      Rafiki yangu panadol hunijui sikujui, JF huwa tunaongea kwa hoja ukitaka kuanza kuipima akili yangu, utashangaa kujikuta kuwa akili zako zote ulizo nazo ni sawa na 0.005% ya akili zangu. Naomba usinihusishe na Chama cha siasa mimi sina kadi ya CDM hivyo huwezi kusema ni chama changu, chama mimi ni 'Tanzania iliyo isiyokuwa na rushwa' maana ndiyo adui namba moja wa maendeleo. CDM ni chama ambacho kilichoweza kunishawishi kuwa kinaweza kabisa kuungana na chama changu (ie Tanzania isiyo na rushwa na inayoangalia wananchi kwanza kabla ya viongozi).

      Kama wewe unaona kuchomwa makanisa ni kigezo ambacho kinaweza kumfanya Lissu awalaani waislam utakuwa umekosea sana, maana uislam haufundishi uharibifu wa mali zisizo za waislam. Wewe una uhakika gani kuwa waliochoma ni waislam?, je kesho na kesho kutwa polisi wakimkata mtu asiyekuwa muislam kuwa amechoma kanisa hilo utakubali au utakataa?. Siungi mkono uharibifu wa mali mali ziwe za kanisa au za synagogue au za msikiti. Jumping into conclusion inaonesha dhahiri kuwa wewe una 'Prejudices' na uislam na waislam na ungependa sana kila mtu aongee unavyofikiria wewe ndiyo awe sahihi, hiyo ni 'myopia' ya hali ya juu sana.

      Changia hoja acha personal attacks!
      Last edited by Hofstede; 2nd June 2012 at 15:28.
      Mzenji73 likes this.

    4. #42
      Kyindokyakombe's Avatar
      Member Array
      Join Date : 1st May 2012
      Posts : 97
      Rep Power : 375
      Likes Received
      95
      Likes Given
      2

      Default Re: Tundu Lissu, kwa hili, kachemka

      LISU hajakosea ni serikali inawapa WANANCHI frustration ndo maana.

    5. Nzi
      #43
      Nzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2010
      Location : 740 Park Avenue
      Posts : 3,325
      Rep Power : 21626
      Likes Received
      949
      Likes Given
      828

      Default Re: Tundu Lissu, kwa hili, kachemka

      Quote By zimmerman
      Boko Haramu, tafsiri yake ni Western Education is Haram, yaani elimu ya Magharibi ni haramu, unaweza kupata hisia kwamba dini inawasukuma kusafisha kila kitu kilicho na ideals za kimagharibi ukiwemo Ukristo na ndio maana Makanisa hayatakiwi kuwepo kule kaskazini mwa Nigeria.
      Mzee zimmerman, hivi huo uislamu ulikuwepo kabla ya waarabu hawajafika Afrika?! Yaani unataka kusema kwamba hao Boko Haramu wanaona uislamu ndiyo dini ya asili yao?! Kwa hiyo ideas za kimashariki ya kati na mbali ndizo sawa na ideas za ancient Africa?! Hawa jamaa hivi wanaelewa kwamba waafrika walikuwa na imani zao; kwamba uislamu na ukristo zote ni imani ngeni zilizoletwa na wavamizi - wawe wamisionari ama wafanya biashara (waarabu na waasia)?!
      "You can't make a scene if you don't have little green"-------Jim Carrey

    6. #44
      momboka's Avatar
      Member Array
      Join Date : 15th June 2011
      Posts : 16
      Rep Power : 405
      Likes Received
      0
      Likes Given
      1

      Smile Re: Tundu Lissu, kwa hili, kachemka

      lisu yupo sahihi 100%,tatizo ni muungano hapo hakuna lingino,zanzibar ni taifa la kislam na wakristo ni wakuja,hivyo wanachoma makanisa ili kuwaondoa wabara wabaki na zanzibar yao,zanzibar komaeni mpaka kieleweke,hakuna ugaidi ukiwa unadai haki yako

    7. #45
      Mcjoe's Avatar
      Member Array
      Join Date : 1st April 2012
      Posts : 51
      Rep Power : 370
      Likes Received
      10
      Likes Given
      57

      Thumbs up Re: Tundu Lissu, kwa hili, kachemka

      Nakubaliana na mheshimiwa Lissu kwa asilimia zote. Amejibu kitaalam, pengine ndio maana wengine wanapata ugumu kuelewa. Labda swali moja linaweza kusaidia katika kumuelewa. Je, mtu yeyeto anaweza kutaja mahali na wakati ambapo paliwahi kuwa na kitu kinachoitwa uislamu safi, katika maana ya kuwa dini pekee bila mchanganyiko wowote ule? Tena Lissu akisema frustration yuko sahihi kwasababu frustration haina mantiki. Ukiuliza mbona wanachoma makanisa tu, jibu ni kwamba ndiyo asili ya frustrations, mtu mwenye akili tulivu haelewi kirahisi anachofanya a frustrated person. Even the other groups that may be referred in this connection, basically they are not for doing proselytism, but they reflect a certain kind of political disillusionment. Hapa dini ni terminus operis(object) na si terminus operantis(intention). Ahsante mheshimiwa Lissu.


    8. #46
      Sangarara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 3,370
      Rep Power : 1212
      Likes Received
      1214
      Likes Given
      1591

      Default Re: Tundu Lissu, kwa hili, kachemka

      Quote By Papaeliopaulos
      Sikubaliani na hoja yako hata kidogo. Ili watu waweze kuishi katika jamii moja jambo la msingi sio kufuata matakwa au imani ya mtu mwingine ili uweze kukaa naye kwa amani. ukishafanya hivyo tayari umekuwa "MTUMWA"
      Jambo la kuzingatia ni kuheshimu uhuru wa mtu mwingine. Mwana falsafa mmoja alisema kuwa "katika msongamano wa watu mwisho wa uhuru wako ni pale linapoanzia bega la mwenzako" Tafsiri yake ni kuwa katika jamii inayoheshimu uhuru wa watu uhuru wako wa kufanya mambo ni kwa kiwango kile tu ambacho hutamuathiri jirani yako.
      Kwa hiyo basi tukisema kuwa ili tuishi nao ni lazima tukubaliane na matakwa yao ni dhahiri kuwa tutakuwa watumwa wao. wewe unasema kuwa kwenu mmekubaliana kuku lazima achinjwe kiislamu ili kuwaridhisha, ni sawa ila ukumbuke halitaishia hapo.
      - kesho watasema lazima mavazi uvae kwa mujibu wa dini ya kiislamu utakubali?
      -Halafu mkikubali watakuja na hili; bar, guest house nk zivunjwe kwa kuwa haziendani na imani yao. tukikubali watasema sheria za nchi hazifai bali sharia za kiislam ndio zifuatwe na watu wote hili ni pamoja na kufanya mashauri yote (ya waislamu na wasio waislamu) kwenye mahakama ya kadhi ili tuweze kukaa nao kwa amani
      Mwisho watasema hata raisi lazima awe shehe maana kwa mujibu imani yao hawawezi kutawaliwa na kafri.

      Mimi nafikiri uhuru wa kiraia ni muhimu zaidi, kila mtu afanye mambo yake ili mradi asifunje sheria ya nchi ambayo inatuunganisha wote na sheria hii ilinde haki na uhuru wa kila mmoja bila kujali imani.
      Twende Taratibu Kiongozi.
      Usiongee kwa namna ambayo inamaanisha kwamba sheria zetu ni kamilifu bila chembe ya mapungufu, moja ya mapungufu makubwa ya sheria zetu ni poor penetration kwenye jamii zetu, jamii zetu nyingi zinajiendesha bila ufahamu wa kuwapo kwa sheria, na serikali yetu haijawahi kuchukumua maamuzi ya dhati ya kupropagate sheria za nchi yetu ili ziweze kuwa enforced nchi nzima, vyombo vyetu vya usimamizi wa sheria vinavyanya kazi kwa kuvizia, sheria inaonekana kuwapo baada ya kosa kutokea, hata washitakiwa wengi kwenye mahakama zetu wanashitakiwa kwa mujibu wa sheria wasizozifahamu, kwa hiyo unaposema watu waishi kwa mujibu wa sheria nashindwa kukuelewa unamaanisha nini exactly?

      Ukweli ni kwamba Jamii zetu zinaongozwa na mila na desturi fulani fulani, na kwa bahati mbaya sana sheria nyingi zilizopo sasa hazireflect mira na desturi hizi,na ni mila na desturi hizi ndio zimeweza kuzihifadhi jamii zetu katika mazingira ya amani ya utulivu mpaka kufikia sasa, kumbuka kwamba, Mwalimu Nyerere aliona matatizo yanayoweza kujitokeza katika jamii yetu kwa uwapo wa vikabila vingi vingi, ndio maana alitumia nguvu na uwezo wake wote kuhakikisha kwamba elimu ya kuwawezesha watanzania kuishi bila kubaguana kwa misingi ya ukabila, rangi na dini inaingia akilini mwa kila mtanzania, hakuna sheria na maandishi hayo hayawezi kuitwa sheria kwa mtazamo wa kibinaadamu ambayo yanawaelekeza binaadamu kuishi kwa amani na utulivu. ndio maana nikalazimika kufanya reference kwenye maandiko ya kwenye biblia kwa namna yanayohimiza wakisristo kuishi na watu wa jamii zingine.

      Hivyo hili sio swala la kisheria, ni swala la mila na desturi, na katika hili narudia tena, tunalazimika kujitune na matakwa ya jamii ya kiislamu,sasa wewe unakuza mambo, unadai kuheshimu mila na desturi za kiislamu ni sawa na kuwa mtumwa kwa uislamu au waislamu, unasisitiza kuheshimu uhuru wa mtu mwingine bila kuvunja sheria, sina nia ya kukushambulia, lakini sina namna ingine ya kuelezea kwamba hii ni hurka ya ushindani usio na maana yoyote ile, nimekueleza kwamba sisi mtaani kwetu ilikuwa na taratibu zetu kwa kuku kuchinjwa na muislamu, msingi ni kwamba if possible nao waje tujumuike nao kwenye chakula, kinyume cha hapo ni kufanya maandalizi ya chakula katika namna ambayo unajuwa jirani yako hawezi kukitumia, kwa nini uweke vikwazo kwenye chakula?
      Mzenji73 likes this.

    9. #47
      Suzie's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th May 2010
      Posts : 1,087
      Rep Power : 0
      Likes Received
      339
      Likes Given
      309

      Default

      Quote By panadol
      Huyo Lisu kuchemsha ni kawaida yake anafanya siasa kwa jazba anatafuta umaarufu kama wa Mh Zito au Mh Mbowe au Mh Dr Slaa kwa nguvu mara nyingi uropoka na kuteleza huyu jamaa hafai kuwa kiongozi mkubwa atatupeleka shimoni,wewe jiulize kuna mahusiano gani kutaka muungano ujadiliwe na kuchoma makanisa kwa nini wasichome misikiti au mali za serikali,hapo Tundu kachemsha sana tuongee ukweli tusiweke siasa manake kuna mijitu mingine itamtetea kwa sababu ni kiongozi wa chama chao ebu tuweke itikadi zetu kando tujadili ukweli wa jambo hili vinginevyo tukiwa tunajadili jambo kimtazamo wa kisiasa hatutafika ata kidogo,Mh Lisu katika hili kachemsha ata wachungaji na wananchi mbalimbali wamemshangaa!
      Sawa mimi nitamtetea sababu ni wa chama changu, embu mlete huyo wa chama chako amung'unye tumsikie na wewe umtetee.

      Tatizo lao ni kweli lahusu Muungano na wao wanaamini bila muungano wakristo wasingekuwepo na wao wanashambulia kiunganishi kimojawapo cha Muungano. ***** dot ukuda

    10. #48
      sir.JAPHET's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th May 2012
      Posts : 609
      Rep Power : 475
      Likes Received
      90
      Likes Given
      45

      Default Re: Tundu Lissu, kwa hili, kachemka

      mtoa hoja.. Thread n kilaza tuu.. Hukumuelewa komando lissu vizuri akakuacha njia panda.. Take care

    11. #49
      jogi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th September 2010
      Posts : 4,041
      Rep Power : 1225
      Likes Received
      982
      Likes Given
      247

      Default

      Quote By Angel Msoffe
      %kubwa ya wazanzibar wazawa ni waislam, na wakristo wengi walioko zanzibar ni wahamiaji toka bara, kuwachomea makanisa, baa, nyumba ni ishara ya kuwafukuza warudi kwao bara, na yote hii inatokana na wazanzibari kutokuuhitaji muungano.
      Hivi Enjo, kwa kumbukumbu zako ukristo na uislamu ni upi ulianza duniani? nia yangu ni kupima nani mvamizi, nani kati yao anajua maana ya IMANI!!!!

    12. #50
      Tume ya Katiba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2012
      Location : Chumbuni-Zanzibar
      Posts : 2,690
      Rep Power : 0
      Likes Received
      542
      Likes Given
      273

      Default Re: Tundu Lissu, kwa hili, kachemka

      Quote By Mungi
      ​@zimmerman
      Ninachoamini ni kwamba Tundu yupo sahihi, na wanaochoma makanisa kule zanzibar siyo Kikundi cha Uamsho, bali vijana wa Dr. Shein ili wazanzibari na jamii iseme hawa jamaa wanachoma makanisa.
      Hata mimi mwanzoni nilidhani kwamba waliochoma makanisa ni Uamsho, kumbe siyo!
      @kwa mara ya kwanza nimeanza kukuamini kuwa wewe ni great thinker.
      Mzenji73 and Mungi like this.

    13. #51
      jogi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th September 2010
      Posts : 4,041
      Rep Power : 1225
      Likes Received
      982
      Likes Given
      247

      Default

      Quote By Nzi
      Mzee zimmerman, hivi huo uislamu ulikuwepo kabla ya waarabu hawajafika Afrika?! Yaani unataka kusema kwamba hao Boko Haramu wanaona uislamu ndiyo dini ya asili yao?! Kwa hiyo ideas za kimashariki ya kati na mbali ndizo sawa na ideas za ancient Africa?! Hawa jamaa hivi wanaelewa kwamba waafrika walikuwa na imani zao; kwamba uislamu na ukristo zote ni imani ngeni zilizoletwa na wavamizi - wawe wamisionari ama wafanya biashara (waarabu na waasia)?!
      Kwa kumkumbusha ourstory not history, ni kuwa IN THE BEGINING AFRIKA WAS CALLED ALKEBULAN- MEANS THE LAND OF THE BLACKS, kwa hili kuna sababu ya kuwahusudu wapagani kwani hawakulazimishi uelewa wao uwe wako pia hasa kwa maswala ya imani.

    14. #52
      gwavara's Avatar
      Member Array
      Join Date : 5th April 2012
      Posts : 37
      Rep Power : 367
      Likes Received
      5
      Likes Given
      8

      Default Re: Tundu Lissu, kwa hili, kachemka

      Quote By magenyi
      hata mimi nakuunga mkono kwa asilimia 100 kwani busara alizotumia mh lissu ndiyo hiyo na hakuna nyingine
      namuunga mkono lissu mnataka aseme halafu mpotoshe kama mlivyopotosha kauli ya mzee mtei.shame on you magamba

    15. #53
      sokwambi's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 27th April 2012
      Posts : 5
      Rep Power : 358
      Likes Received
      1
      Likes Given
      3

      Default Re: Tundu Lissu, kwa hili, kachemka

      hivi wewe na elimu yako ya kuunga unga unaweza kumzidi tundu lisu? walikolalia ccm ndiko cdm walikoamkia.kwa nini itv hawakuita vyama vingine

    16. #54
      idawa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th January 2012
      Posts : 4,690
      Rep Power : 3353
      Likes Received
      1249
      Likes Given
      474

      Default Re: Tundu Lissu, kwa hili, kachemka

      Lissu alikua sahihi, japo wenzetu dini na siasa vinakwenda sambamba lakini lengo lao kuu la vurugu ni siasa kwa maslai ya dini..!lakini kaa ukijua wazanzibar wakilala wakiamuaka wanawaza uarabuni.!

    17. #55
      BinMgen's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th June 2008
      Posts : 1,484
      Rep Power : 854
      Likes Received
      110
      Likes Given
      229

      Default

      Lisu yuko saws, uchomaji wa makanisa kunaueezekano mkubwa ikawa ccm wamefanya hivyo ili kuizima hoja ya kupinga muungano inayoongozwa na uamsho.

    18. #56
      Waberoya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd August 2008
      Location : Busia-Uganda
      Posts : 5,948
      Rep Power : 1742
      Likes Received
      1518
      Likes Given
      2835

      Default Re: Tundu Lissu, kwa hili, kachemka

      kisiasa yuko sahihi kabisa amesema kuokoa cdm, hasa nyakati hizi mbaya

      kihalisia wale jamaa hawaupendi ukristo
      You are not supposed to be so blind with patrotism that you cant face reality. Wrong is wrong no matter who says it. Malcom X

    19. RC.
      #57
      RC.'s Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th May 2012
      Posts : 349
      Rep Power : 422
      Likes Received
      30
      Likes Given
      16

      Default

      Quote By Matola
      Kwenye keyboard ya computer kila button ina kazi yake, wacha kutetea ujinga, wewe ndio mvivu wa kufahamu. Binafsi siwezi hata kupoteza muda wangu na kujiumiza macho kusoma thread ya namna hii isiyokuwa na mpangilio.
      Kama hujaisoma mbona unachangia? bwana ee kama unaweza unaruhusiwa kuedit sio issue kuaibishana hapa.mi napita tu.

    20. RC.
      #58
      RC.'s Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th May 2012
      Posts : 349
      Rep Power : 422
      Likes Received
      30
      Likes Given
      16

      Default

      Quote By panadol
      Huyo Lisu kuchemsha ni kawaida yake anafanya siasa kwa jazba anatafuta umaarufu kama wa Mh Zito au Mh Mbowe au Mh Dr Slaa kwa nguvu mara nyingi uropoka na kuteleza huyu jamaa hafai kuwa kiongozi mkubwa atatupeleka shimoni,wewe jiulize kuna mahusiano gani kutaka muungano ujadiliwe na kuchoma makanisa kwa nini wasichome misikiti au mali za serikali,hapo Tundu kachemsha sana tuongee ukweli tusiweke siasa manake kuna mijitu mingine itamtetea kwa sababu ni kiongozi wa chama chao ebu tuweke itikadi zetu kando tujadili ukweli wa jambo hili vinginevyo tukiwa tunajadili jambo kimtazamo wa kisiasa hatutafika ata kidogo,Mh Lisu katika hili kachemsha ata wachungaji na wananchi mbalimbali wamemshangaa!
      tuliza munkari bro na ondoa bias zako za u ccm utaelimika zaidi.

    21. #59
      babykailama's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 5th March 2012
      Posts : 226
      Rep Power : 409
      Likes Received
      227
      Likes Given
      77

      Default Re: Tundu Lissu, kwa hili, kachemka

      Hakuna kuchemka. Hatutaki watu walete vurugu nchini kwa kisingizio cha kutopewa nafasi ya kujadiana. Wape nafasi na ikiwezekana wapewe wanachotaka kama ni wengi (majority) ndipo tutaheshimiana mbele ya safari. Wabara ndio tungepaswa kulaumu soma hapa nilisema.

      http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la...toujadili.html
      Pa shoka hapaingii kisu

    22. #60
      idawa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th January 2012
      Posts : 4,690
      Rep Power : 3353
      Likes Received
      1249
      Likes Given
      474

      Default Re: Tundu Lissu, kwa hili, kachemka

      tatizo wazanzibar wanajhisi ni waarabu.

    Page 3 of 4 FirstFirst 1234 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...