Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mapungufu niliyoyaona pale Jangwani - muhimu CHADEMA kuyafanyia kazi

    Report Post
    Page 2 of 3 FirstFirst 123 LastLast
    Results 21 to 40 of 53
    1. #1
      Kurunzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2009
      Location : DAR ES SALAAM
      Posts : 1,956
      Rep Power : 891
      Likes Received
      386
      Likes Given
      147

      Default Mapungufu niliyoyaona pale Jangwani - muhimu CHADEMA kuyafanyia kazi

      Jana nilikuwa mmoja wa wahudhuriaji wa mkutano pale Jagwani wa M4C, ukiacha kasoro chache lakini umati wa watu hasa vijana ulikuwa na mkubwa sana, pia nilipata fursa ya kutembea kwa mąndamano kuwasindikiza viongozi kwenye ofisi za chama toka viwanja vya Jagwani (CDM SQUARE) mpaka makao makuu ya chama pale kinondoni, lengo langu la kushiriki maandamano hayo nilitaka kujua je umati hatima yao itakuwa nini na je wakifika pale Makao makuu ya chama watafanya nini vijana wamekuwa na hamasa kuu hivi?

      Hayo ndiyo mambo ambayonilitaka kupata majibu yake na kwa jibu moja ni kwamba watu hasa vijana wanataka mabadiliko na wapotayari kwa mabadiliko huwezi amini kila kijana niliona anachukuwa no. ya viongozi zilizotangazwa kwa wanaotaka kufungua matawi nilifurahi kuona watu wameliitikia kwa hamasa.

      Lakini pamoja na hayo kunamapungufu muhimu sana ambayo nimeyaona na CDM wanatakiwa kuyafanyia kazi, nitayataja machache hapa:

      1. Pamoja na muda ulikuwa finyu wa viongozi kuzungumza lakini kuna mambo ambayo hayakupangwa kwa utaratibu uliopangiliwa vema mathalani ni pale Dr. Slaa alipomtaka na kumsihi mwenyekiti kama Kiongozi wa upinzani Bungeni na kama waziri mkuu kivuli pamoja na kabineti mambo ambayo wanatakiwa wayafanyie kazi wakiwa Bungeni kwani yamekuwa kero kwa wananchi mathalani Slaa alimtaka Mbowe ashughulikie suala la watu kunyanyaswa na polisi binafsi sikusikia Mbowe akisema amesikia na atayafanyia kazi kuyafanyia kazi.

      2. Nilitegemea kupitia tungepewa tadhini japo kidogo juu ya kampeni hii M4C na vua gamba vaa gwanda imekuwa na mafakio kiasi gani, nilitegemea hata kupata tąrifa fupi ya viongozi wa Dar. tathini ya Chama hapa dar. mathalani tuna matawi mangapi, wanachama wangapi nini mahitaji yetu na kadhalika.

      3. Nilitegeme kupata hata salamu toka kwa wageni wa vyama rafiki angalau mmoja angepewa nafai ya kuzungumza akatupa hata exposure za wenzetu hapo niliona mmekuwa so conservative.

      4. Mc alifanya kazi nzuri sana ya uhamasishaji sijajua jina lake lakini alivaa ovyo sana sawa inawekana ni msanii lakini angalau angevaa sare za chama au kwa njia nyingine nadhifu lakini alionekana kama aliitwa tu kuja kufanya kazi ya u-mc tu.

      Ni hayo tu.

    2. Miaka 50

    3. #21
      MNYISANZU's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 21st October 2011
      Posts : 6,311
      Rep Power : 0
      Likes Received
      593
      Likes Given
      76

      Default Re: Mapungufu niliyoyaona pale Jangwani - muhimu CHADEMA kuyafanyia kazi

      Upande wa music ndio ulipwaya ila cha msingi ni ujumbe wa M4C.

    4. SG8
      #22
      SG8's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th December 2009
      Location : DSM
      Posts : 2,558
      Rep Power : 4177
      Likes Received
      771
      Likes Given
      730

      Default Re: Mapungufu niliyoyaona pale Jangwani - muhimu CHADEMA kuyafanyia kazi

      Ni vizuri kufanyia kazi changamoto... Wengi wetu tumeshindwa kujikosoa.
      "Tumefika hapa kutokana na udhaifu wa Rais Kikwete,Uzembe wa Bunge na Upuuzi wa CCM"

    5. #23
      Mussa Haruni's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 1st April 2012
      Posts : 7
      Rep Power : 361
      Likes Received
      3
      Likes Given
      0

      Default Re: Mapungufu niliyoyaona pale Jangwani - muhimu CHADEMA kuyafanyia kazi

      jamani si kila mtu anayekosoa ana nia mbaya..kuna namna ya kuboresha kulingana na mtizamo wake..upande wangu nimeona kuna point fulan aliposema au kudai tathimini..ni lugha tu aliyotumia cha msingi naona alilenga kitu kinaitwa baseline survey..hii hufanyika unapotaka kufanya jambo anatakiwa kuwa na data za wakati huo hii itakusaidia kufanya ufuatiliaji(monitoring) na baadae tathimini(evaluation) yote haya kukuwezesha kujua kama upo katika mstari sahihi na mwisho je umefanikiwa?

    6. #24
      Kurunzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2009
      Location : DAR ES SALAAM
      Posts : 1,956
      Rep Power : 891
      Likes Received
      386
      Likes Given
      147

      Default

      Quote By Pasco
      Mkuu Kurunzi, hongera kwa kuwa bold na kuleta ukosoaji wa CDM in a constructive criticism. Sisi tuliofanya hivyo kule nyuma, tuliishia kutukanwa!.

      Pia nawapongeza wana Chadema kwa yote, they are growing up for the better! This time hawajatukana!.

      Amini msiamini, critique ndio inayojenga chama imara kuliko pongezi za sifa na mapambio!.

      Pasco.
      Ni kweli Pasco, tupo CDM kukijenga hata mahali nilipo nakijenga kwakukosoa na kupongeza lakini kwa sasa tunelekekea kuchukua nchi ni lazima tujipange vema ili tusiwape maadui pakusemea.

    7. #25
      daGoldFather's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 6
      Rep Power : 361
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Mapungufu niliyoyaona pale Jangwani - muhimu CHADEMA kuyafanyia kazi

      Nafikiri mtoa mada uko sahihi kabisa umetoa very simple but important constructive critisism.

      Binafsi tathmin yangu ni kwamba mkutano huo ulikuwa more of a PR event kitu nnachokubaliana nacho kabisa kutokana na hali halisi ya chama kinavokua, hivo hayo uliyoyasema yalitakiwa kuzingatiwa.

      Nafikiri wahusika wameyasikia na watayafanyia kazi

      Binafsi natamani kuona umakini kwa vyama vyote au vingi vyao maana vyama vitakapokuwa makini sera zetu kama nchi zitakuwa bora na maisha yetu yataboreka sana

      Niachie hapa kwa leo.

    8. RukaaJuu Final

    9. #26
      Mwita Maranya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2008
      Location : Ikorongo Game Reserve
      Posts : 7,989
      Rep Power : 12010
      Likes Received
      5319
      Likes Given
      5144

      Default

      Quote By naggy
      uko sahihi kamanda. mimi pia napenda wawe wanatangaza hela zinazopatikana wakipitisha mchango. ni hela ya umma hiyo,wapenda mageuz.
      Sio jambo rahisi kufanyika majumuisho na kutangaziwa mapato hapo hapo. Taarifa inatolewa baadaye kadri taarifa sahihi zinavyokuwa zimekusanywa.

    10. #27
      Kurunzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2009
      Location : DAR ES SALAAM
      Posts : 1,956
      Rep Power : 891
      Likes Received
      386
      Likes Given
      147

      Default

      Quote By kichomiz
      Utu si mavazi,na utendaji kazi si mavazi,Weredi na kujituma ndi vitu muhimu,
      Tafuta kasoro nyingine.
      Je mwanao akija nyumbani amevaa kimini mbele ya wageni unalisemeaje hilo?

    11. #28
      Kurunzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2009
      Location : DAR ES SALAAM
      Posts : 1,956
      Rep Power : 891
      Likes Received
      386
      Likes Given
      147

      Default

      Quote By Kassim Awadh
      Nadhani jambo zuri kuwa na more critics kuliko kupongeza ili wahusika warekebishe na kufanya bora zaidi Mikoa mingine,,
      Tumeshakuwa watu wazima lazima tukubali chałages ndani na nje ya chama.

    12. #29
      kanganyoro's Avatar
      Member Array
      Join Date : 22nd June 2011
      Posts : 85
      Rep Power : 418
      Likes Received
      21
      Likes Given
      1

      Default Re: Mapungufu niliyoyaona pale Jangwani - muhimu CHADEMA kuyafanyia kazi

      Hakuna haja ya kutaja idadi ya wanachama, kimbunga kitaonekana mwaka 2015. Leo nimemsikia MzeePeter kisumo ambaye ni mwenyekiti wa baraza la wadhamini la ccm kwamba ccm ina wanachama milioni 5 lakini wamesahau kuwa tangu operation ya vua gamba vaa gwanda ianze wanaccm wengi wamehamia cdm.

    13. #30
      Kurunzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2009
      Location : DAR ES SALAAM
      Posts : 1,956
      Rep Power : 891
      Likes Received
      386
      Likes Given
      147

      Default

      Quote By Mussa Haruni
      jamani si kila mtu anayekosoa ana nia mbaya..kuna namna ya kuboresha kulingana na mtizamo wake..upande wangu nimeona kuna point fulan aliposema au kudai tathimini..ni lugha tu aliyotumia cha msingi naona alilenga kitu kinaitwa baseline survey..hii hufanyika unapotaka kufanya jambo anatakiwa kuwa na data za wakati huo hii itakusaidia kufanya ufuatiliaji(monitoring) na baadae tathimini(evaluation) yote haya kukuwezesha kujua kama upo katika mstari sahihi na mwisho je umefanikiwa?
      Naamini tathimini hiyo itapelekea mimi nma we tujue ni wapi tunapaswa kuongeza nguvu.

    14. #31
      Mapi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2011
      Posts : 571
      Rep Power : 0
      Likes Received
      142
      Likes Given
      141

      Default Re: Mapungufu niliyoyaona pale Jangwani - muhimu CHADEMA kuyafanyia kazi

      mkuu samahan, ninawiwa kusema hoja zako nyepesi kuliko uji wa futari

    15. #32
      Kurunzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2009
      Location : DAR ES SALAAM
      Posts : 1,956
      Rep Power : 891
      Likes Received
      386
      Likes Given
      147

      Default

      Quote By kanganyoro
      Hakuna haja ya kutaja idadi ya wanachama, kimbunga kitaonekana mwaka 2015. Leo nimemsikia MzeePeter kisumo ambaye ni mwenyekiti wa baraza la wadhamini la ccm kwamba ccm ina wanachama milioni 5 lakini wamesahau kuwa tangu operation ya vua gamba vaa gwanda ianze wanaccm wengi wamehamia cdm.
      Hapana records na takwimu nimuhimu kwani mapambano yetu haihitaji kificho kwani ni dhairi na

    16. #33
      Kurunzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2009
      Location : DAR ES SALAAM
      Posts : 1,956
      Rep Power : 891
      Likes Received
      386
      Likes Given
      147

      Default

      Quote By Mapi
      mkuu samahan, ninawiwa kusema hoja zako nyepesi kuliko uji wa futari
      Pole zipite vizuri

    17. #34
      Gwankaja Gwakilingo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th January 2012
      Location : Masoko Busisya
      Posts : 1,199
      Rep Power : 609
      Likes Received
      326
      Likes Given
      32

      Default Re: Mapungufu niliyoyaona pale Jangwani - muhimu CHADEMA kuyafanyia kazi

      Tutatazama wapi tulijikwaa na sio tulipo angukia dosari hazikwepeki
      kwa pamoja ni lazima twende mbali zaidi ya maneno yetu...........039.mac

    18. #35
      Candid Scope's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 7,606
      Rep Power : 15261
      Likes Received
      3731
      Likes Given
      2867

      Default Re: Mapungufu niliyoyaona pale Jangwani - muhimu CHADEMA kuyafanyia kazi

      Kwanza nikupongeze kwa kazi nzuri uliyofanya, Ninyi ndio tunawahitaji.

      Hapa tupo watu wa tabaka mbalimbali, maono mbalimbali, viwango vya kufikiri na kuona mbalimbali, uwezo wa kujenga hoja kwa viwango mbalimbali, uchambuzi wa masuala ya kisiasa na kijamii mbalimbali. Kwa aliye msomi au mzoefu wa kusoma tukio na yaliyojilia kisha kutoa hitimisho atakuwa amekuelewa fika. Kuna wanaochangamkia mipasho na kuna wanaopenda uchambuzi yakinifu.

      Kasoro ulizoziainisha ni za msingi, wahusika wanatakiwa kuzifanyia kazi. Ipo siku wakishika dola hawatakiwi kufanya kazi kwa propaganda. Wananchi wanahitaji kujua hatu ambazo chama kimefikia katika jitihada zake za kuiamsha jamii, na ni mategemeo ya takwimu hata za matukio na takwimu za matarajio siku zijazo zina umuhimu wa kujenga kujiamini na kuamsha zaidi ari ya watu kuitikia na kufikia malengo.

      Wawapo jukwaani kawaida yao kila mmoja huwa na yake ya kuongea, na katu hawaweki kumbukumbu ya aliyemtangulia ameongea nini kwa minajili ya kama anatakiwa kutolea ufafanuzi, au kupokea pendekezo, hayo ni mambo muhimu, kwani ukiwa kiongozi unapotoa hotuba inabidi ijibu yale yaliyoongelewa na viogozi wa chini yako ambao wamekutangulia kutoa hotuba za utangulizi.

      Jambo moja ambalo nimekubali wameshalifanyia kazi ni ila hamaki ya kujibu hoja jukwaani na kuzitolea maamuzi. Mkutano wa pale Jangwani ambapo wamepabatiza jina la Chadema Square pamoja na shinkizo la watu wengi licha ya vyombo vya habari, matamko yaliyotangulia na baadaye kusukumwa na wahudhuriaji wa mkutano ule kutolea tamko kuhusu Shibuda, busara ilitawala na kuongelea kwa mbali sana bila kuonyesha kuligusa moja kwa moja na kuhitimisha kwamba vikao vitalifanyia kazi. Hiyo ndiyo busara inayotakiwa na ndio ukomavu wa kuongoza nchi. Papara husababisha mwanya wa mipasuko.

      Nataraji ushauri wako umesikika na wameusikia, nategemea wataufanyia kazi, kwani kujenga nyumba si kazi ya siku moja, na ni mambo mengi yanayofanya nyumba ikamilike. Wengine wanamaliza kujenga nyumba kwa miezi na wengine kwa miaka hata hivyo kuna baadhi wanaishi ndani ya nyumba ambayo baadhi yatakamilika kwa muda wanapoishi. Bado wana nafasi ya kuyafanyia kazi nataraji nafasi nyingine tutaona mabadiliko ya kuziba mapungufu yaliyojitokeza.

    19. #36
      Dennis_elisha's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 1st April 2012
      Location : Ubungo
      Posts : 7
      Rep Power : 361
      Likes Received
      1
      Likes Given
      1

      Default

      Quote By Kurunzi

      4. Mc alifanya kazi nzuri sana ya uhamasishaji sijajua jina lake lakini alivaa ovyo sana sawa inawekana ni msanii lakini angalau angevaa sare za chama au kwa njia nyingine nadhifu lakini alionekana kama aliitwa tu kuja kufanya kazi ya u-mc tu.

      Ni hayo tu.
      Kama sijakosea, MC anaitwa JOHN MREMA, mkurugenzi bunge na halmashauri chadema, pia 2010 aligombea ubunge jimbo la vunjo na augustine mrema. Ni jembe la ukweli, labda mkuu ulipendelea avae sare but for me namkubali sana kamanda kama makamanda wengine licha ya alivyokua amevaa.

      BTW; thanx for constructive critism, WATAYAFANYIA KAZI coz huwa wanapita huku.

    20. #37
      alan's Avatar
      Member Array
      Join Date : 20th February 2012
      Posts : 17
      Rep Power : 369
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default Re: Mapungufu niliyoyaona pale Jangwani - muhimu CHADEMA kuyafanyia kazi

      Tunapokosolewa tukubali usimwangalie ni nani anayekukosoa hii itatufanya tujenge kilicho bora zaidi

    21. #38
      Duble Chris's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th May 2011
      Posts : 2,340
      Rep Power : 872
      Likes Received
      382
      Likes Given
      309

      Default Re: Mapungufu niliyoyaona pale Jangwani - muhimu CHADEMA kuyafanyia kazi

      haya ni makosa madogo sana ya kibinadamu na yanarekebishika, asante
      frustration is given by expectationdivide by
      outcome
      ie
      frustration = expectation/outcome


    22. #39
      fikirikwanza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th January 2012
      Posts : 642
      Rep Power : 498
      Likes Received
      149
      Likes Given
      17

      Default Re: Mapungufu niliyoyaona pale Jangwani - muhimu CHADEMA kuyafanyia kazi

      Siku CHADEMA itaacha kufanya makosa madogo madogo itakuwa sio chama cha siasa tena bali mwakilishi wa mungu duniani; Ni lazima makoso madogo madogo yatokea kibinadamu.

      Tunachokataa CCM ni kufanya makosa makubwa makubwa mfululizo bila hata haya, tunakufa na umaskini wakati wanasema maisha bora, tunashiriki ubepari wakati wanasema siasa za ujamaa. Kama huamini moja ya makosa makubwa ya CCM ni katiba ya zanz, ambayo wao ndo waliingia mwafaka na CUF, wakajipoendekeza kwa kusema zanz ni nchi; wanawadanganya watanzania kwa umaarufu wa muda mfupi, kama zanz ni nchi basi CCM & CUF ndo walivunja muungano tangu siku hiyo. Inachofanya Tanganyika ni kutoa ulinzi kwa Znz kama USA kwa Afghanistan etc, Makosa mengine ni Bilal kuwa Makamu wa rais wa Tanganyika wakati ni Mzanzibar, zanz si ni nchi??? inamaana Tanzania ndo Tanganyika, Zanz ni Zanz.

      Kosa jingine la CCM vyeo kwa upendeleo, mtu yuko masomoni anapewe cheo, Mbunge anakuwa RC au DC tumelalamika sana tangu 2006 au 7 huko Ukerewe mtoto wa primaty school alimuuliza Lowassa inakuwaje ktk upungufu wa ajira mtu mmoja napewa vyeo lukuki??? Hili nalo linajirudia bila huruma kwa Mtanzania.

      EPA, Richmond yanajirudia kila siku huku wahusika wakila bata. na mengine mengi unayoyajua.

    23. #40
      NICE LAMECK's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 209
      Rep Power : 401
      Likes Received
      26
      Likes Given
      37

      Default Re: Mapungufu niliyoyaona pale Jangwani - muhimu CHADEMA kuyafanyia kazi

      Ni mawazo mazuri yafanyiwe kazi nia ni kuchukua Serikali 2015 na tusisite kukosoa ndipo tutaimalika zaidi peoplessss power.

    Page 2 of 3 FirstFirst 123 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...