Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mpigania Uhuru na Mwasisi wa TAA, Dr. Vedastus Kyaruzi afariki dunia!

    Report Post
    Page 1 of 5 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 87
    1. #1
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,862
      Rep Power : 7377
      Likes Received
      6196
      Likes Given
      22551

      Default Mpigania Uhuru na Mwasisi wa TAA, Dr. Vedastus Kyaruzi afariki dunia!

      Kutokana na hali ya kusubiria baadhi ya wajukuu zake marehemu waishio Ulaya, mazishi ya aliyekuwa Rais wa Chama cha TAA (kabla ya kumkabidhi kiti hicho kwa Mwl. Nyerere) Dr. Vedastus Kyaruzi hayatafanyika leo (Alhamis, 24/05/2012) bali yatafanyika siku ya Jumamosi 26/05/2012 huko Kyaka kijijini Nyabihanga katika wilaya ya Missenyi
      Wanabodi,

      Nimepokea taarifa za kifo cha mmoja wa waanzilishi wa chama cha TAA na baadae TANU, Dr. Vedastus Kyaruzi kilichotokea juzi hapa jijini Dar es Salaam na mwili wake kusafirishwa leo kuelekea Bukoba kwa mazishi yatakayofanyika J.5.

      Habari hizi ni kwa mujibu wa Bw. Prosper Vedasto wa Channel Ten.

      Kwa wafuatiliaji wa historia ya siasa za Tanzania, Mzee Kyaruzi ametajwa sana katika makala za Maalim Mohamed Said kuwa yuu miongoni mwa mashujaa wa nchi hii waliosahaulika au tulio sahaulishwa na inawezekana ndio maana hata msiba wake uko low profile!.

      Nadhani nisingekutana na Bw. Prosper, msiba huu muhimu ungeweza kutupita juu kwa juu!.

      Quote By Familia
      Tunaomba tusahihishe taarifa kutoka kwa Bw. Prosper;

      Dr.Vedastus Kyaruzi amefariki jana usiku wa saa 1:20 usiku na umauti umemkuta akiwa amelazwa katika hospitali ya mkoa huko Bukoba mjini.

      Mazishi yanatarajiwa kufanyika siku ya Alhamisi ya tarehe 24 Mei,2012.
      Kwa msiomfahamu Dr. Kyaruzi, hapa anaelezewa vizuri na mwana JF mwenzetu, mpigania uhuru mwenzake!.

      Quote By Mpigania Uhuru View Post
      Wanasiasa katika jamii yetu wamekuwa wakiwachukulia madaktari kama watu ambao muda mwingi wako na wagonjwa na wajui mambo ya kijamii yanayoendelea, imefika wakati hata sitahiki zao ambazo ziko wazi katika "goverment standing order' wananyimwa bila sababu ya msingi. Mfano intern drs waliodai mshahara wao wa mwezi ambayo ni haki yao, baadae walipewa na kufukuzwa muhimbili!

      Ukweli ni kwamba drs wamehusika sana katika ukombozi wa kisiasa wa tanganyika na dunia kwa ujumla.

      Naomba nitoe mifano miwili.

      Kwanza ni Dr. Vedasto Kyaruzi ambaye alikuwa president wa TAA mwaka 1950 na katibu wake akiwa Abdulwahid Sykes. Kabla ya kuingia kwa huyu daktari TAA ilikuwa ni chama cha kijamii ambacho hakikuwa na mwelekeo wa kudai uhuru.

      Dr. huyu ndiye aliyeleta mapinduzi makubwa akiwa kama president wa TAA wakati Nyerere anakuja kujiunga na harakati za kudai uhuru msingi mkubwa ulishaandaliwa na huyu Dr. kyaruzi, kwa bahati mbaya watanganyika wengi hawajui/hawajaelezwa mchango wake i.e forgatten people.

      Mfano wa pili ni Dr. Che Guevara huyu alikuwa ni daktari na mwanamapinduzi wa ukweli ambaye amepigana vita vya msituni na kufanikisha uhuru wa CUBA, ukombozi wa DRC etc.

      Sasa hivi kuna harakati nyingi za ukombozi wa jamii yetu zikioongozwa na CHADEMA.

      Madaktari nao sasa wameamua kujiunga katika vita hii. Mfano mzuri ni Mh. Zitto leo alivyojitokeza bungeni kajitokeza kuwatetea ingawa inaonekana anaweza kupata upionzani mkali kutoka vyama vingine.

      Kwa vile fikra za madaktari hawa zinaendana na fikra za CHADEMA ni ukweli usiopingika kwamba madaktari watapambana bega kwa bega kama alivyofanya dr. Che Guevara na Fidel Castro.

      Drs are people of their words, when they say it they mean it. When they are ready to die for something, they know know what death is, because they have been seeing dead people everyday!

      Hii ndio tabia ya Drs (people of their words) ambayo pinda alikuwa haijui, alifikiri akipiga mkwala, kesho watakuwa wanakanyagana kuwahi ofisini.
      Bwana Alitoa, Bwana Ametwaa,
      Jina Lake Lihimidiwe!.

      RIP Dr. Kyaruzi!.

      Pasco.

      TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

      Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali Fabian Massawe kuomboleza kifo cha Mzee Dkt.Vedastus Nshunju Kyaruzi ambaye aliaga dunia mwishoni mwa wiki kwenye Hospitali ya Mkoa wa Kagera mjini Bukoba baada ya ugonjwa wa muda mfupi.


      Katika uhai wake, Dkt. Kyaruzi ambaye alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 92 alipata kuwa Katibu Mkuu wa Vyama vya Tanganyika African Association (TAA) na Tangayika African National Union (TANU), Mwakilishi wa Kudumu wa Tanganyika katika Umoja wa Mataifa (UN), Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ulinzi na Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Watoto (UNICEF), Kanda ya Afrika, Kusini mwa Jwangwa la Sahara, akiwa na Makao yake Mjini Lagos, Nigeria.


      Katika salamu zake za rambirambi, Rais Kikwete amesema kuwa amehuzunishwa na kufadhaishwa na habari za kifo cha Balozi Kyaruzi ambaye alilitumikia Taifa la Tanzania na nchi nyingine kwa miaka mingi na kwa uaminifu,uadilifu na ufanisi mkubwa katika nafasi mbali mbali ambazo alipata kuzishikilia katika maisha yake.

      “Nimepokea habari za kifo cha Mzee Kyaruzi kwa huzuni kubwa kwa sababu ya mchango mkubwa ambao aliutoa katika maisha yake kwenye utumishi wa taifa letu kuanzia kwenye nafasi za uongozi wa kijamii na kisiasa katika vyama vya TAA na TANU hadi kwenye utumishi wa Serikali huru ya Tanganyika na kwenye Umoja wa Mataifa,” amesema Rais Kikwete katika salamu zake.

      Ameongeza Rais Kikwete: “Nakutumia wewe Mkuu wa Mkoa wa Kagera salamu za rambirambi za dhati za moyo wangu kufuatia kifo cha Mzee Kyaruzi. Nakuomba pia kupitia kwako unifikishie salamu zangu kwa wana-familia wote wa familia ya Marehemu Kyaruzi. Wajulishe kuwa niko nao katika wakati huu mgumu wa maombolezo. Naungana nao katika kuomboleza msiba huu mkubwa. Nawaomba wawe na subira katika kipindi hiki kigumu, Naungana nao katika kumwomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, ailaze peponi pema roho ya Marehemu Vedasto Nshunju Kyaruzi. Amen.”



      Imetolewa na:
      Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
      Ikulu.
      Dar es Salaam.

      24 Mei, 2012



    2. #2
      JokaKuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st July 2006
      Posts : 6,915
      Rep Power : 2990
      Likes Received
      2548
      Likes Given
      3634

      Default re: Mpigania Uhuru na Mwasisi wa TAA, Dr. Vedastus Kyaruzi afariki dunia!

      Pasco,

      ..hebu ulizia kama kama Raisi alituma rambirambi au kuna kiongozi yeyote wa serikali alitokea msibani.

      ..misiba siku hizi inatumika kisiasa. hii ni tabia ya ajabu sana nimeanza kuiona ktk awamu ya 4.

      NB:

      ..lets see kama Sheikh Mohamed Said ataandika tanzia ya Dr.Kyaruzi.
      Invisible, Ogah, Ndahani and 3 others like this.

    3. #3
      Nguruvi3's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st June 2010
      Location : Kidabashi-Dongobeshi
      Posts : 3,600
      Rep Power : 2924
      Likes Received
      5001
      Likes Given
      3073

      Default re: Mpigania Uhuru na Mwasisi wa TAA, Dr. Vedastus Kyaruzi afariki dunia!

      RIP Dr Kyaruzi,

      Inasikitisha sana kuona watu waliojitoa kwa ajili ya nchi hii wanasahaulika na hawapewi heshima stahiki.

      Historia haifichwi kwasababu hujidhihiri yenyewe!
      Last edited by Nguruvi3; 21st May 2012 at 18:49.
      Mkandara, Invisible and Ogah like this.

    4. #4
      Songoro's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th May 2009
      Posts : 2,397
      Rep Power : 0
      Likes Received
      541
      Likes Given
      24

      Default Re: Mpigania Uhuru na Mwasisi wa TAA, Dr. Vedastus Kyaruzi afariki dunia!

      Haya ndo mapungufu ya Mwl Nyerere,Aliwapoteza kwenye Historia akina Kyaruzi ili abaki pekee kwenye Historia na kuna vijitu vinaamini uhuru wa nchi hii ni matokeo ya harakati za miaka 6 i.e 1954 (kuzaliwa TANU) mpaka uhuru wa 1961, Hawajui kuwa Tanu imekuja kukamilisha kazi za wakongwe kama DR.Kyaruzi, Kwa mfano ukiwauliza vijana wasomi wa kisasa wakutajie wapigania Uhuru 10 wa nchi hii,itawachukua muda sana na kama wakijitahidi watakutajia waliokuwa mawazir wa kwanza wa Serikali wakati hao wapigania uhuru walitupwa kulleeeeeeee!!!!!! Watoto wetu hawajui kuwa Professa Babu ni Nguli wa Siasa ya Ujamaa Duniani mpaka leo wajamaaa Dunia nzima wanaadhimisha SIKU ya kifo chake kwa Mijadala yenye Afya.Buriani Dr.Kyaruzi historia ya VITABUNI umeachwa lakin kamwe vifuani mwa wapenda ukweli utadumu!
      Megawatt B and Ribosome like this.
      The Real Great thinkers should agree to disagree!

    5. #5
      BUBE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th November 2010
      Location : KIMANZICHANA
      Posts : 642
      Rep Power : 565
      Likes Received
      174
      Likes Given
      175

      Default Re: Mpigania Uhuru na Mwasisi wa TAA, Dr. Vedastus Kyaruzi afariki dunia!

      RIP Dr Vedasto Kyaruzi


    6. #6
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,862
      Rep Power : 7377
      Likes Received
      6196
      Likes Given
      22551

      Default

      Quote By JokaKuu View Post
      Pasco,

      ..hebu ulizia kama kama Raisi alituma rambirambi au kuna kiongozi yeyote wa serikali alitokea msibani.

      ..misiba siku hizi inatumika kisiasa. hii ni tabia ya ajabu sana nimeanza kuiona ktk awamu ya 4.

      NB:

      ..lets see kama Sheikh Mohamed Said ataandika tanzia ya Dr.Kyaruzi.
      Mkuu Joka Kuu, hata huyu jamaa aliyenieleza, alinieleza tuu kama by the way. Lets hope salaam za JK zitakuja!.

    7. #7
      kookolikoo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th March 2012
      Posts : 1,974
      Rep Power : 761
      Likes Received
      284
      Likes Given
      147

      Default

      Quote By Pasco View Post
      Mkuu Joka Kuu, hata huyu
      jamaa aliyenieleza, alinieleza tuu kama by the way. Lets hope salaam za
      JK zitakuja!.
      hakukuwa na press coverage ya kifo hiki!

    8. #8
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,862
      Rep Power : 7377
      Likes Received
      6196
      Likes Given
      22551

      Default

      Quote By Nguruvi3 View Post
      RIP Dr Kyaruzi,

      Inasikitisha sana kuona watu waliojitoa kwa ajili ya nchi hii wanasahaulika na hawapewi heshima stahiki.

      Historia haifichwi kwasababu hujidhihiri yenyewe!
      Mkuu Nguruvi 3 ni kweli misiba siku hizi ni politics. Kanumba amekufa same day na former IGP Mahundi na baadae former CDF Gen. Mwita Kiaro, Bunge likasimama to observe 1 min silence kwa Kanumba, then 3 days letter ndipo Kiaro na Mahundi were just mentioned!.

      Kusema ukweli, ukiondoa ile sumu ya udini kwenye makala za Maalim Mohamed Said, they were very informative if read with open mind!.

      Ila pia nasikitika sisi waandishi hatutimizi wajibu wetu ipasavyo, watu kama hawa walitakiwa wawe documeted accordingly!.
      Ogah, Adili and Nguruvi3 like this.

    9. #9
      mashambani kwao's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th December 2011
      Posts : 369
      Rep Power : 454
      Likes Received
      52
      Likes Given
      0

      Default Re: Mpigania Uhuru na Mwasisi wa TAA, Dr. Vedastus Kyaruzi afariki dunia!

      vp mazishi yake yatatangazwa kama ya KANUMBA?

    10. #10
      jouneGwalu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Location : Studio
      Posts : 2,348
      Rep Power : 974
      Likes Received
      1320
      Likes Given
      1762

      Default Re: Mpigania Uhuru na Mwasisi wa TAA, Dr. Vedastus Kyaruzi afariki dunia!

      Quote By Nguruvi3 View Post
      RIP Dr Kyaruzi,

      Inasikitisha sana kuona watu waliojitoa kwa ajili ya nchi hii wanasahaulika na hawapewi heshima stahiki.

      Historia haifichwi kwasababu hujidhihiri yenyewe!
      Inasikitisha sana....
      Dah mzee wa watu sijui kaiacha namna gani familia yake..!

      Mungu amrehemu kamanda...

      Bado tunagharama kubwa ya kulipa katika kusahihisha historia yetu!

    11. #11
      Rweye's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th March 2011
      Posts : 2,723
      Rep Power : 963
      Likes Received
      423
      Likes Given
      0

      Default Re: Mpigania Uhuru na Mwasisi wa TAA, Dr. Vedastus Kyaruzi afariki dunia!

      Kweli akina Fundikila,Sykes,Kyaruzi n.k leo serikali zetu zinawakanyaga na kwenda kuwabeba akina Kanumba huku wakijiaibisha?

      Ndo maana CDM ina rangi nyekundu ktk bendera yake kwa ajiri ya kuenzi wapiganaji hawa na daima tutawakumbuka babu zetu wapiganaji milele yote.
      Precise pangolin likes this.

    12. #12
      Precise pangolin's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 4th January 2012
      Posts : 5,761
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1609
      Likes Given
      684

      Default Re: Mpigania Uhuru na Mwasisi wa TAA, Dr. Vedastus Kyaruzi afariki dunia!

      Quote By JokaKuu View Post
      Pasco,

      ..hebu ulizia kama kama Raisi alituma rambirambi au kuna kiongozi yeyote wa serikali alitokea msibani.

      ..misiba siku hizi inatumika kisiasa. hii ni tabia ya ajabu sana nimeanza kuiona ktk awamu ya 4.

      NB:

      ..lets see kama Sheikh Mohamed Said ataandika tanzia ya Dr.Kyaruzi.
      CCM wanaenda kwenye misiba Kama ya kanumba sio kikongwe Kama huyo wanadharau sana

    13. #13
      Kidogo chetu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2009
      Location : DAR ES SALAAM
      Posts : 478
      Rep Power : 581
      Likes Received
      53
      Likes Given
      130

      Default Re: Mpigania Uhuru na Mwasisi wa TAA, Dr. Vedastus Kyaruzi afariki dunia!

      wakati mwalimu anafika makelele Dr Vedastus alikuwa mwaka wa mwisho MEDICINE na akiwa Rais wa wanafunzi.
      Mwalumu alijua uwezo wa Kyaruzi kaitka kupambanua mambo,hivyo kumuacha achanue ilikuwa ni hatari kwake so after uhuru nchi haina wataalamu kabisa lakini Dr huyu akapelekwa ubalozi.

      Anyway Rest In Peace DR ,ulijenga misingi ambayo leo imekuwa nguzo ya uhuru na amani ya nchi yetu

    14. #14
      mayenga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th September 2009
      Posts : 1,596
      Rep Power : 817
      Likes Received
      320
      Likes Given
      447

      Default Re: Mpigania Uhuru na Mwasisi wa TAA, Dr. Vedastus Kyaruzi afariki dunia!

      RIP Mzee,ulikuwa muumini mzuri,Mungu akupokee katika ufalme wake.

    15. #15
      Mapi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2011
      Posts : 571
      Rep Power : 0
      Likes Received
      142
      Likes Given
      141

      Default Re: Mpigania Uhuru na Mwasisi wa TAA, Dr. Vedastus Kyaruzi afariki dunia!

      R.I.D Dr. Kweli nimeyaona ya kina kina ngugi wanamawazo mapana. A man like ths kfo chake kina run low profile hivi!!! TANZANIA HAYA MAKOSA TUTAYALIPA.

    16. #16
      Mag3's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 31st May 2008
      Posts : 3,575
      Rep Power : 1816
      Likes Received
      2521
      Likes Given
      2548

      Default Re: Mpigania Uhuru na Mwasisi wa TAA, Dr. Vedastus Kyaruzi afariki dunia!

      RIP Dr. Vedastus Kyaruzi, ulikuwa Mtanganyika aliyeshiriki na Watanganyika wengine bila kujali tofauti zao zozote zile kupigania uhuru wa Tanganyika. Daima utakumbukwa.
      Shwari likes this.
      The true sign of intelligence is not knowledge but imagination.
      Education is what remains after one has forgotten what one has learned in School
      -Albert Einstein.


    17. #17
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 16,045
      Rep Power : 14670
      Likes Received
      2954
      Likes Given
      2093

      Default Re: Mpigania Uhuru na Mwasisi wa TAA, Dr. Vedastus Kyaruzi afariki dunia!

      Quote By Nguruvi3 View Post
      RIP Dr Kyaruzi,

      Inasikitisha sana kuona watu waliojitoa kwa ajili ya nchi hii wanasahaulika na hawapewi heshima stahiki.

      Historia haifichwi kwasababu hujidhihiri yenyewe!
      Mohamed Said kamkumbuka huyu na wengine kwenye maandiko yake. Cha kushangaza wengi hufikiri historia ya nchi hii imeanzia kwa Nyerere. Why?

    18. #18
      MAMA POROJO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2007
      Posts : 4,907
      Rep Power : 1857
      Likes Received
      626
      Likes Given
      421

      Default Re: Mpigania Uhuru na Mwasisi wa TAA, Dr. Vedastus Kyaruzi afariki dunia!

      RIP Dr. Kyaruzi!.

    19. #19
      Alexism's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th August 2011
      Location : Iringa Municipal TZ
      Posts : 843
      Rep Power : 569
      Likes Received
      119
      Likes Given
      18

      Default Re: Mpigania Uhuru na Mwasisi wa TAA, Dr. Vedastus Kyaruzi afariki dunia!

      Omulangira Vedast Kyaruzi mungu akupokee kwa amani.Kyaruzi was one of the first Tanganyikan intellectual trained at Makerere in Uganda and he headed TAA from 1950 to 1953.R.I.P.

    20. #20
      Mwita Maranya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2008
      Location : Ikorongo Game Reserve
      Posts : 8,335
      Rep Power : 12084
      Likes Received
      5562
      Likes Given
      5420

      Default Re: Mpigania Uhuru na Mwasisi wa TAA, Dr. Vedastus Kyaruzi afariki dunia!

      Pole kwa familia ya mpiganaji wa kweli, mtanganyika mzalendo Dr. Kyaruzi.

    Page 1 of 5 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...