Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: CHADEMA yawa gumzo Mtwara

    Report Post
    Page 5 of 10 FirstFirst ... 34567 ... LastLast
    Results 81 to 100 of 193
    1. #1
      Molemo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Posts : 8,457
      Rep Power : 10882
      Likes Received
      3822
      Likes Given
      426

      Default CHADEMA yawa gumzo Mtwara

      Wakazi wa manispaa ya Mtwara wamepokea kwa furaha kubwa taarifa za ujio wa CDM katika mikoa ya kusini.Wananchi mbalimbali waliohojiwa wamesema wamekuwa wakiisikia CDM kupitia vyombo mbalimbali vya habari na hasa mambo makubwa wabayofanya viongozi wake Dr Slaa,Mbowe na wabunge wa chama hicho.Wameapa kukipokea kwa kishindo chama hicho huku wakiapa kurudisha kadi za CCM na kusimika bendera za CDM mpaka ndani ya vyumba vyao.Mzee mmoja akiongea kwa uchungu alisema anaamini CDM itawakomboa na vuguvugu lao la M4C hasa katika zao la korosho.Ameahidi mikoa ya kusini kuwa ngome kuu ya CDM kama mikoa ya kanda ya ziwa na kaskazini.
      Source:Majira Jumanne

      ------------------------------------------------------------------------
      UPDATES.....1

      Mkurugenzi wa habari na uenezi-CDM John Mnyika ametangaza rasmi operesheni ya M4C kwa mikoa ya kusini itaanza tarehe 28/05/2012 na itadumu kwa wiki mbili ambapo maelfu ya wananchi wanatarajiwa kuvua Gamba na kuvaa Gwanda.

      -------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
      UPDATES...2

      MBOWE, SLAA KUONGOZA OPERESHENI KUSINI

      Awamu mpya ya operesheni ya Chadema inayolenga kuhamaisha umma kuleta mabadiliko na uwajibikaji serikalini iliyopangwa kufanyika katika mikoa ya Kanda ya Kusini, itaanza rasmi Mei 28, mwaka huu, katika Mkoa wa Mtwara.

      Akizungumza na NIPASHE jana, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika, alisema operesheni hiyo itaongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, Freeman Mbowe.

      Alisema wengine watakaoongoza operesheni hiyo, ni Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa pamoja na wabunge wa chama hicho na kwamba, itahitimishwa katika mkoa wa Lindi.

      Kwa mujibu wa Mnyika, operesheni hiyo imelenga kushughulikia mambo matatu; la kwanza likiwa ni kusimamia uwajibikaji katika ngazi zote za serikali, ili kuhakikisha changamoto zote zinazolikabili taifa zinashughulikiwa.

      Mnyika ambaye pia ni Mbunge wa Ubungo, alisema jambo la pili litakaloshughulikiwa na operesheni hiyo, ni kutoa elimu ya kisiasa kwa umma kuhusu mchakato wa mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

      Alisema jambo la tatu, litakuwa ni kujenga organaizesheni ya chama mijini na vijijini katika mikoa hiyo.


      Source:Nipashe Jumanne.


      -----------------------------
      More Updates

      Makamanda wa CDM wakiongozwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe na Katibu Mkuu Dr Wilbroad Slaa wameondoka leo kuelekea mikoa ya Mtwara na Lindi kwa operesheni itakayotikisa ukanda wote wa kusini.Jumla ya makamanda wote walioondoka ni 60 ambapo watasambaa vijiji vyote kufungua matawi, ofisi za chama kata mbalimbali,kutoa elimu ya uraia kuhusu katiba na kuhutubia mikutano kila kata na kijiji.
      Last edited by Molemo; 27th May 2012 at 15:58.

    2. Miaka 50

    3. #81
      Red Scorpion's Avatar
      Member Array
      Join Date : 1st February 2012
      Posts : 83
      Rep Power : 385
      Likes Received
      13
      Likes Given
      65

      Default re: CHADEMA yawa gumzo Mtwara

      Quote By MtamaMchungu
      Hiyo itakuwa ngumi ya pua kwa CCM.
      nimeipenda hiyo

    4. #82
      OSOKONI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th October 2011
      Posts : 3,647
      Rep Power : 1113
      Likes Received
      1001
      Likes Given
      761

      Default re: CHADEMA yawa gumzo Mtwara

      Quote By ritz
      Point ya maana kwako ikoje? Haya sio maneno yangu ni maneno ya Mbunge wa Chadema Nassari ndio alisema Chadema kujitenga mie utanionea bure labda ungemwambia mbunge wako.

      Halafu mie naitwa Ritz wa JF hayo mambo yenu ya kupeanda vyeo vya kinafiki eti great thinkers wala mie siitaji mkuu wangu itaneni tu nyie Pro-Chadema JF.
      afadhali umekiri kuwa sio great thinker hilo limenionyesha uwezo wako wa kufikiri ni mdogo nimekusamehe! Swala la Nassary lilishatolewa maelezo na mh. Mbowe na yeye mwenyewe Nassary kwenye press conference lakini wewe kulileta hapa kiushabiki ndio maana nimekuambia ongea point ya maana! JF ni mahali pa fikra pana na mjadala mtambuka na ujenzi wa hoja sio ushabiki wa kwenye magazeti ya udaku!
      Narrow minded people discuss people,common minded people discuss events great minded people discuss ideas!!!

    5. #83
      NasDaz's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th May 2009
      Location : Ushenzini
      Posts : 3,123
      Rep Power : 5358
      Likes Received
      1477
      Likes Given
      1686

      Default re: CHADEMA yawa gumzo Mtwara

      Jambo lipo dhahiri, kwamba CHADEMA watalazimika kufanya kazi ya ziada ili waweze kukubalika maeneo ya pwani! Iwe ni matunda ya propaganda au vinginevyo, tayari taswira ya CHADEMA machoni mwa watu wengi haioneshi utaifa kama ilivyo kwa CCM! Inawezekana kabisa kwamba CCM kikaonekana ni very CORRUPT, lakini linapokuja suala la muonekano wa kitaifa, CCM is far better than CHADEMA and even CUF!

      Hili, halikuja kwa bahati! Ni dhahiri kwamba, propaganda za CCM zimesaidia kujenga taswira hiyo ya CHADEMA kuonekana enzi zile kwamba ni chama cha Wachaga, ikaja kuwa cha Kikristo na sasa cha kikanda! Kwa bahati mbaya sana, ama kwa makusudi ama kwa ukosefu wa weledi wa kile kinachosemwa “Think All Before You Speak, But Don’ Speak All Before You Think”, imetokea mara kadhaa kauli za viongozi wa CHADEMA kuleta mshabihiano wa yale yanayosemwa na wapinzani wa CHADEMA!! Mbaya zaidi, kosa ambalo lilitokea kwa CUF limerejea CHADEMA! Wakati CUF kikituhumiwa kwamba ni Chama Cha Waislamu, ikatokea Waislamu wengi wakajiunga na Chama hicho na tangu hapo hata mamo ya CUF yakakaa Kiislamu Islamu! Ilikuwa ni jamo la kawaida kwenda kwenye mikutano ya CUF na kukuta full Barkhashia!! Hivyo hivyo, wapo Watanzania wengi tu hivi sasa ambao wanajikuta wanaiunga mkono CHADEMA kwa ajili tu ya Ukristo wao! Hata hapa JF, ukiangalia Wakristo ambao wamekubuhu kwa udini, utakuta ni watetetzi wakubwa wa CHADEMA! Si hilo, utakuta members wengi humu JF ambao Signatures zao ni vifungu vya Biblia, basi wengi wao kama sio wote ni watetezi wakubwa wa CHADEMA! Mara nyingi member hawa hata michango yao utakuta inaegemea zaidi kwenye udini udini kuliko Siasa za kawaida hata kama hoja inayojadiliwa ni ya kisiasa! Members hawa, wanatia kinyaa na wanachangia kwa kiasi kikubwa kuifanya CHADEMA ionekane dhahiri ni chama cha Wakristo!

      Harakati za CHADEMA nazo zinazua mashaka mengine! Hata uendaji wa Kusini hivi sasa unaonekana ni kama tu katika kuzima kelele za wapinzani wao kwamba CHADEMA ni chama cha kikanda na chama cha Wakristo! Mbwembwe za CHADEMA kwenda kusini hazijaanza leo….na hata kama wataenda bado hawana hamasa kiasi hicho! Molemo, ametuletea habari za gazeti la Majira…..CHADEMA tuliowazoea si wa kusuiri Majira waandike stori kisha waje hapa kui-paste! Safari, imekosa hamasa!

      Kama ilivyo ugumu kwa CUF kukubalika Bara ndivyo hivyo hivyo CHADEMA watakavyopata ugumu wa kukubalika Pwani ingawaje wapo wapumbavu watakaosema kwamba watu wa pwani hawana uelewa! Yaani leo hii Mmasasi ambae anaishi kwa kuhamahama awe na uelewa kuliko mtu aliye-settle sehemu moja!
      I am a free thinker! It's only my free thinking that leads me, to what am commenting. Thus, I've no doubt that today I can be your fellow but tomorrow your enemy, and the agent between us being my comments!! So, If today we agree with cheers, tomorrow we'd not disagree with jeers!


    6. #84
      STEIN's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2010
      Location : Arusha
      Posts : 1,343
      Rep Power : 715
      Likes Received
      306
      Likes Given
      156

      Default re: CHADEMA yawa gumzo Mtwara

      Quote By ritz
      Point ya maana kwako ikoje? Haya sio maneno yangu ni maneno ya Mbunge wa Chadema Nassari ndio alisema Chadema kujitenga mie utanionea bure labda ungemwambia mbunge wako.

      Halafu mie naitwa Ritz wa JF hayo mambo yenu ya kupeana vyeo vya kinafiki eti great thinkers wala mie siitaji mkuu wangu itaneni tu nyie Pro-Chadema JF.
      Ukitofautiana sana na watu basi mwisho wa siku lazima utakuwa na matatizo... Kama ukiona katika watu kumi 8 au 9 wanakupinga basi ujue hayo mawazo yako hayafai... Najua inawezekana wewe hili unalielewa lakini kwa sababu ya maslahi binafsi unashindwa kufanya maamuzi sahihi.
      “Problems cannot be solved by the same level of thinking that created them.”“Insanity: doing the same thing over and over again and expecting different results.”" by Albert Einstein"

    7. #85
      Nabwada's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 5th April 2012
      Posts : 121
      Rep Power : 384
      Likes Received
      33
      Likes Given
      1

      Default

      Quote By Pasco_jr_ngumi
      Ukweli unaumaaaaaa......
      Wachaga wana ubaguzi xana!!!!! Hata marehem baba yangu pale Mikindani aliniambiaaaa..... CDM hamtaweza kukubalika milele!!!!!!


      Pili huku kuna waislam tupu, na ule udini mmechemka!!!!! Niko huku Lipwidi, Mtwara Vijijin nalimaaaa!!!!
      kama kweli unaishi Lipwidi basi unamatatizo makubwa kwenye kufikiri.Uchaga sio Ugonjwa ni Kabila ambalo anazaliwa anakuta wazazi wake wanalo.Mbona Mtwara kuna M bunge Viti maalumu Mama Wambura ni Mkulya.Upoandika jamvini usifikiri Mtu wa Mtwara uko peke yako ili udanganye watu humu.


    8. #86
      samstevie's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 11th November 2011
      Posts : 195
      Rep Power : 420
      Likes Received
      31
      Likes Given
      14

      Default re: CHADEMA yawa gumzo Mtwara

      Quote By Pasco_jr_ngumi
      Mmechemka, hii ni ngome ya CCM !!!!!! Tangu lini Mmakonde aolewe na Mchaga???
      Brother hata Mwanza mimi niliamini kuwa Ni CCM tu ndiyo wenye ngome but things have been changed to history. So lets wait

    9. #87
      Kalumbesa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th November 2010
      Location : Shamba
      Posts : 867
      Rep Power : 604
      Likes Received
      267
      Likes Given
      120

      Default re: CHADEMA yawa gumzo Mtwara

      Quote By Rejao
      Tunakumbushi mlichokisema na end result yake! na mtwara itakuwa hivyo hivyo...
      Kwa watu wanaolewa mwenendo wa CDM na uducteta uliopo, hawawezi kukishobokea CDM.
      Am happy watu wa Pwani ni waelewa na wanajua kupima mambo kabla ya kukurupukia vitu!
      Hivi uducteta ndio nini?

    10. #88
      Nabwada's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 5th April 2012
      Posts : 121
      Rep Power : 384
      Likes Received
      33
      Likes Given
      1

      Default

      Quote By Rejao
      Hata Uzini ilikuwa hivi hivi..
      Natafuta comment ya Slaa hapa JF siku wawalipoenda Uzini.
      Nafikiri wote mliona CDM walichoambulia kule!!
      usichanganye mambo UZINI ilikuwa wakati wa uchaguzi,alafu huko tunajua kuwa kuna mahusiano ya kiutawala kati ya CUF na CCM .CHADEMA wanakuja kukiimarisha chama Kusini.Karibuni sana CHADEMA.

    11. #89
      Nabwada's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 5th April 2012
      Posts : 121
      Rep Power : 384
      Likes Received
      33
      Likes Given
      1

      Default

      Quote By Rejao
      Tunakumbushi mlichokisema na end result yake! na mtwara itakuwa hivyo hivyo...
      Kwa watu wanaolewa mwenendo wa CDM na uducteta uliopo, hawawezi kukishobokea CDM.
      Am happy watu wa Pwani ni waelewa na wanajua kupima mambo kabla ya kukurupukia vitu!
      wewe unatudhihaki sisi watu wa Pwani unatuöa ni Maamuma tu,hutoamini kitakachotokea Mtwara.

    12. #90
      NasDaz's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th May 2009
      Location : Ushenzini
      Posts : 3,123
      Rep Power : 5358
      Likes Received
      1477
      Likes Given
      1686

      Default re: CHADEMA yawa gumzo Mtwara

      Quote By STEIN
      Ukitofautiana sana na watu basi mwisho wa siku lazima utakuwa na matatizo... Kama ukiona katika watu kumi 8 au 9 wanakupinga basi ujue hayo mawazo yako hayafai... Najua inawezekana wewe hili unalielewa lakini kwa sababu ya maslahi binafsi unashindwa kufanya maamuzi sahihi.
      Jambo la msingi ni hoja na sio idadi ya watu!! Wajuzi wa mambo huku Uswahilini wanatuambia kwamba nyani mmoja ana akili nusu ya ile aliyonayo binadamu; lakini haimaanishi kwamba pakiwepo nyani 72 ndo watakuwa na akili 36, la hasha....bali ni ile ile nusu!!

      Si hivyo, ukiangalia sana basi utagundua kwamba kitu ambacho kinashabikiwa na wengi basi kina walakini! KWANINI?! Wanadamu huwa hatuna silika ya kuumiza kichwa na kutafuta ukweli na badala yake tunalazimika kukikubali kile kilicho rahisi kwetu kukimeza au kile ambacho wahubiri wake wakuu wana uwezo wa kuteka hisia za wengi! Angalia suala la uwepo wa mungu.....wengi tunaamini, lakini ukilitafakari "crtically" unakutana na walakini kibao!! Tunaogopa kuhoji critically kwavile tunaambiwa tutakufukuru kwa kumchimba chimba yule (mungu)tunayemwamini!

      Therefore, achana na udikteta wa fikra....acha watu wafikirie vile wanavyoamini ni RIGHT na sio wafikirie vile amavyo wewe na wenye imani kama yako mngependa wengine wote wafikirie!
      I am a free thinker! It's only my free thinking that leads me, to what am commenting. Thus, I've no doubt that today I can be your fellow but tomorrow your enemy, and the agent between us being my comments!! So, If today we agree with cheers, tomorrow we'd not disagree with jeers!


    13. #91
      Ritz's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 1st January 2011
      Location : Republic of Nauru
      Posts : 18,357
      Rep Power : 12597
      Likes Received
      5872
      Likes Given
      781

      Default

      Quote By OSOKONI
      afadhali umekiri kuwa sio great thinker hilo limenionyesha uwezo wako wa kufikiri ni mdogo nimekusamehe! Swala la Nassary lilishatolewa maelezo na mh. Mbowe na yeye mwenyewe Nassary kwenye press conference lakini wewe kulileta hapa kiushabiki ndio maana nimekuambia ongea point ya maana! JF ni mahali pa fikra pana na mjadala mtambuka na ujenzi wa hoja sio ushabiki wa kwenye magazeti ya udaku!
      Wewe kweli kauzu yani ukiwa mshabiki wa Chadema humu JF ndio great thinkers halafu kazi yako ni kuisifia Chadema ndio unakuwa unaongea pointi?

    14. #92
      Ritz's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 1st January 2011
      Location : Republic of Nauru
      Posts : 18,357
      Rep Power : 12597
      Likes Received
      5872
      Likes Given
      781

      Default

      Quote By STEIN
      Ukitofautiana sana na watu basi mwisho wa siku lazima utakuwa na matatizo... Kama ukiona katika watu kumi 8 au 9 wanakupinga basi ujue hayo mawazo yako hayafai... Najua inawezekana wewe hili unalielewa lakini kwa sababu ya maslahi binafsi unashindwa kufanya maamuzi sahihi.
      Mkuu mie sio mtumwa wa akili nasimamia mawazo yangu...halafu nakukumbusha JF sio mali ya Chadema ni jukwaa huru.
      NasDaz, Rejao and SIERA like this.

    15. #93
      Molemo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Posts : 8,457
      Rep Power : 10882
      Likes Received
      3822
      Likes Given
      426

      Default

      Quote By ritz
      Mkuu mie sio mtumwa wa akili nasimamia mawazo yangu...halafu nakukumbusha JF sio mali ya Chadema ni jukwaa huru.
      Mkuu wangu unajaribu kuukimbiza upepo.Maoni ya wadau ndani ya JF ndiyo uthibitisho tosha M4C haikamatiki tena.Count my words!
      Precise pangolin likes this.

    16. #94
      G. Activist's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 3rd November 2010
      Location : United Kingdom
      Posts : 209
      Rep Power : 475
      Likes Received
      45
      Likes Given
      124

      Default re: CHADEMA yawa gumzo Mtwara

      Huu ndio uzuri wa kuanza na Mungu na kutenda kazi kwa kumshirikisha Mungu.
      Wao wana wakuu wa Wilaya, wakuu wa Mikoa, wana Jeshi ila sisi tuna Mungu!!!!
      Duh njema sana hiyo.....!!!!
      You can't beat the history, but you can shape the future.

    17. #95
      Ritz's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 1st January 2011
      Location : Republic of Nauru
      Posts : 18,357
      Rep Power : 12597
      Likes Received
      5872
      Likes Given
      781

      Default

      Quote By Molemo
      Mkuu wangu unajaribu kuukimbiza upepo.Maoni ya wadau ndani ya JF ndiyo uthibitisho tosha M4C haikamatiki tena.Count my words!
      Mkuu wangu Tanzania kuna watu zaidi ya milioni 40 JF kuna members 70,000 na kuna zaidi ya Multiple ID's 40,000 Members hai unaweza kukuta wapo 20,000 tu Chadema wape members 15,000 hawa ndio wanawawakilisha Watanzania milioni 45? Ha haa haaa haaaa haaaaaa!

    18. #96
      NasDaz's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th May 2009
      Location : Ushenzini
      Posts : 3,123
      Rep Power : 5358
      Likes Received
      1477
      Likes Given
      1686

      Default re: CHADEMA yawa gumzo Mtwara

      Quote By Molemo
      Mkuu wangu unajaribu kuukimbiza upepo.Maoni ya wadau ndani ya JF ndiyo uthibitisho tosha M4C haikamatiki tena.Count my words!
      A Very Wrong Analysis!!
      I am a free thinker! It's only my free thinking that leads me, to what am commenting. Thus, I've no doubt that today I can be your fellow but tomorrow your enemy, and the agent between us being my comments!! So, If today we agree with cheers, tomorrow we'd not disagree with jeers!


    19. #97
      Molemo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Posts : 8,457
      Rep Power : 10882
      Likes Received
      3822
      Likes Given
      426

      Default

      Quote By ritz
      Mkuu wangu Tanzania kuna watu zaidi ya milioni 40 JF kuna members 70,000 na kuna zaidi ya Multiple ID's zaidi ya 40,000 Members hai unaweza kukuta wapo 20,000 tu Chadema wape members 15,000 hawa ndio wanawawakilisha Watanzania milioni 45? Ha haa haaa haaaa haaaaaa!
      Mkuu wangu moja na moja huwa mbili.Nakuhakikishia CDM haikamatiki tena.Mlizoea kuwadanganya vijana sasa wamebadilika wanataka mageuzi.Ritz nikuambie kinachoipeleka CDM Ikulu ni kushindwa kwenu kuboresha maisha ya watanzania.Ni hilo tu.Kila leo ni afadhali ya jana.Watu wanaishi maisha ya shida.Tembea vijijini uone.CDM sasa imebaki ndiyo tegemeo lao pekee.Ni kama mtu anayekata roho atakavyofurahi akipata mponyaji.Na ndivyo kwa watanzania sasa kwamba kwa maisha yao ni sawa na watu wanaokata roho na mponyaji wao ni CDM.Porojo hazina nafasi tena kama CCM mnavyotaka iwe.

    20. #98
      Molemo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Posts : 8,457
      Rep Power : 10882
      Likes Received
      3822
      Likes Given
      426

      Default

      Quote By NasDaz
      A Very Wrong Analysis!!
      You are not among GT which means I will never argue with you!

    21. #99
      Ileje's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th December 2011
      Posts : 1,045
      Rep Power : 584
      Likes Received
      406
      Likes Given
      107

      Default re: CHADEMA yawa gumzo Mtwara

      Kwa hali kama hii nani ataendelea kuishabikia CCM!

      UBOVU WA BARABARA YA KWENDA MTWARA

      [IMG]file:///C:/Users/user/AppData/Local/Temp/msohtml1/01/clip_image001.jpg[/IMG]

      Gari Toyota Fuso likiwa limenasa katika tope kwenye Barabara ya Kilwa eneo la Ndundu Somanga hivi karibuni, barabara hiyo imeharibika vibaya kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.
      Never give up your right!

    22. #100
      NasDaz's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th May 2009
      Location : Ushenzini
      Posts : 3,123
      Rep Power : 5358
      Likes Received
      1477
      Likes Given
      1686

      Default re: CHADEMA yawa gumzo Mtwara

      Quote By Molemo
      You are not among GT which means I will never argue with you!
      Ndo tatizo lenu hilo pro-CHADEMA, GT ni yule anaewaza ki-CHADEMA CHADEMA hata kama anachokiongea hakina mashiko!! Kwenu nyinyi, GT ni yule anayeshikiwa akili zake na wapiga proganda za kisiasa hususani CHADEMA! For the second time, YOU'RE VERY WRONG!! Am Free Thinker Broda, check out my Signature!!!!
      Rejao likes this.
      I am a free thinker! It's only my free thinking that leads me, to what am commenting. Thus, I've no doubt that today I can be your fellow but tomorrow your enemy, and the agent between us being my comments!! So, If today we agree with cheers, tomorrow we'd not disagree with jeers!


    Page 5 of 10 FirstFirst ... 34567 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...