Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 21
    1. BAK
      #1
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,827
      Rep Power : 45014
      Likes Received
      8681
      Likes Given
      8666

      Default Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      Mwandishi Wetu Aprili 1, 2009

      Raia Mwema~Muungwana ni Vitendo


      Adokezwa aandae wadhamini wake

      Lengo ni kumuepusha asiende lupango


      BAADA ya kupandishwa kizimbani kwa kesi ya kusababisha ajali iliyoua watu wawili, Mwanasheria Mkuu wa zamani wa serikali Andrew Chenge, sasa anatarajiwa kufunguliwa mashitaka kuhusiana na tuhuma za rushwa katika ununuzi wa rada ya kijeshi yenye thamani Sh bilioni 40 inayomkabili na vigogo wenzake kadhaa, imefahamika.

      Habari za uhakika zimeeleza kwamba, pamoja na kuwapo juhudi kubwa za kuzuia mashitaka dhidi ya wahusika wakuu wa sakata hilo linaloigusa kwa karibu serikali ya Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, kesi hiyo itafunguliwa mahakamani wakati wowote kuanzia sasa kutokana na msukumo mkubwa wa kisiasa.

      Rada hiyo ya kijeshi iliyonunuliwa kwa Pauni za Uingereza milioni 28 , iliibua utata mkubwa lakini kasi kubwa iliongezeka baada ya makachero wa uingereza wa kitengo cha Serious Fraud Office (SFO) kubaini kuwapo kwa rushwa kubwa iliyohusisha kampuni ya Uingereza ya BAE System na wanasiasa, watendaji na wafanyabiashara wa Tanzania.

      “Hakuna kitakachozuia kushitakiwa kwa watuhumiwa wa sakata la rada akiwamo Chenge kwa kuwa kuna kila aina ya ushahidi, pamoja na kuwapo kwa vikwazo kadhaa. Wenzetu wa SFO wanafanya kazi kwa maslahi yao zaidi na hapa nyumbani kuna wanaojaribu kuwasaidia watuhumiwa, lakini ni suala la wakati tu kwa sasa,” kinaeleza chanzo chetu karibu na serikali.

      Chanzo hicho kiligusia kuwapo kwa ukabila katika kulindana kutokana na kuwa Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Elieza Feleshi na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk. Edward Hosea kutoka sehemu moja na Chenge, lakini wote wamekwisha kukanusha kupitia gazeti moja la kila wiki (si Raia Mwema) kufanya kazi kwa ukabila.

      Awali ilielezwa kwamba mwishoni mwa wiki, Chenge alijulishwa kuhusiana na maandalizi ya kesi dhidi yake, akihusishwa na rushwa ili aweze kuandaa wadhamini, lakini taarifa hizo zimekanushwa vikali na pande zote zinazohusika wakiwamo watu walio karibu na mwanasiasa huyo ambaye amekuwa gumzo kwa muda mrefu sasa kutokana na kuhusishwa kwake na sakata hilo.


      Tayari imethibitishwa pasi shaka kwamba Watanzania wane wazito wametajwa kuwa watuhumiwa wakuu wa sakata la rada, huku nyuma yao kukiwa na watendaji kadhaa wa idara na asasi nyingine za serikali walioshiriki katika mchakato huo kabla na wakati wa ununuzi wake.

      Waliotajwa moja kwa moja na nyaraka rasmi pamoja na Chenge yumo Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), Dk. Idriss Rashidi, ambaye wakati wa mchakato huo alikuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kabla ya kustaafu na kuingia katika sekta binafsi.

      Baada ya kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali wa Mkapa kwa miaka kumi, mwaka 2005 Chenge aliwania ubunge jimbo la Bariadi Magharibi kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) na kuteuliwa kuwa Waziri wa Afrika Mashariki kabla ya kuhamishiwa wizara ya Miundombinu, ambako alilazimika kujiuzulu kutokana na kashfa ya rada.

      Chenge alilazimika kujiuzulu nafasi yake baada ya kutajwa hadharani kuhusika kwake na ununuzi wa rada na kubainika kumiliki akaunti nje ya nchi yenye kiasi kikubwa cha fedha ambazo yeye aliziita kuwa ni ‘vijisenti.’

      Kwa upande wake, Dk. Rashidi, baada ya kuondoka BoT mwaka 1998, aliingia katika sekta binafsi ikiwamo benki ya Akiba Commercial, Vodacom Tanzania na benki ya NMB kabla ya kuteuliwa tena kuongoza Tanesco aliko hadi sasa.

      Watuhumiwa wengine wawili wakuu waliotajwa ni pamoja na mtuhumiwa mkuu ambaye kwa sasa amekimbilia nje ya nchi Shailesh Pragji Vithlani na mshirika wake mkuu kibiashara Tanil Somaiya.

      Chenge, Dk. Rashidi, Vithlani na Somaiya wote wametajwa kuwa washiriki wakuu waliowaongozwa wengine katika kufanikisha biashara hiyo tata kwa upande wa Tanzania kila mmoja kwa sasa amekwisha kuchunguzwa kuhusiana na suala hilo.


      Wakati Chenge alishiriki kwa kiasi kikubwa kama Mtaalamu wa sheria, Dk. Rashidi ametajwa kushiriki kama mtaalamu na mhusika mkuu wa mambo ya fedha akiwa Gavana wa BoT.

      Taarifa zinaonesha kwamba Vithlani na Somaiya walikuwa na hati za kiapo zenye kuwapa mamlaka ya kisheria kuwakilisha kampuni iitwayo Envers Trading Corporation.

      Uchunguzi unaonyesha kwamba Envers Trading ililipwa dola za Marekani milioni 12 na kampuni nyingine iitwayo Red Diamond Trading, iliyofunguliwa mwaka 1998 katika visiwa vya Virgin ambavyo ni sehemu ya dola ya Uingereza.

      Red Diamond Trading ilikuwa na uhusiano mkubwa na kampuni iitwayo BAE Systems, ambayo ilitengeneza na kuuza rada iliyouziwa serikali ya Mkapa mwaka 2002.

      Imedaiwa kwamba Red Diamond iliweza kujinufaisha kwa kutumia mianya ya kisheria katika visiwa vidogo vya Caribbean ambako kampuni kama hiyo zinaweza kuficha taswira ya akaunti zake benki ikiwa ni pamoja na majina ya wamiliki wake.

      Akihojiwa na wapelelezi wa Uingereza, Somaiya, ambaye anamiliki kampuni ya Shivacom ya mjini Dar es Salaam, alikiri kuwa na hati zao za kiapo zenye kuwapa mamlaka ya kisheria kuwakilisha kampuni iitwayo Envers Trading Corporation kwa miezi 11.

      Somaiya alikiri katika mahojiano hayo kwamba yeye na "rafiki yake mkubwa" Vithlani wanamiliki kwa pamoja kampuni iitwayo Merlin International.

      Hata hivyo, nyaraka za SFO zinaonyesha kwamba Somaiya kupitia kwa wakili wake aliiambia Takukuru kwamba aliacha kuwa mwenye hisa na mkurugenzi wa Merlin International kipindi ambacho tayari biashara ya rada ilikuwa imekwisha kamilika.

      Kwa sasa Vithlani pekee ndiye anayetafutwa na ameshitakiwa kwa kutoa taarifa za uongo kuwa sio mmiliki wa Envers Trading na kuhusu kupokea dola 390,000 kwa biashara ya rada wakati ukweli ni kwamba alilipwa kitita cha dola milioni 12.

      Tayari makachero wa Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa Mazito ya Uingereza (Serious Fraud Office-SFO) wamekwisha kuomba ushirikiano wa wenzao wa Tanzania katika kuwahoji na kuwapekua watuhumiwa wakuu wa sakata hilo.

      Tayari SFO kwa kushirikiana na vyombo vya dola vya Tanzania, Uswisi na Ufaransa wamebaini kuwapo kwa Dola za Marekani milioni 12 (Sh. bilioni 13.8), ambazo zililipwa kwa siri kwa maofisa wa juu wa serikali kupitia Vithlani kama kamisheni, fedha zilizolipwa kupitia benki ya Uswisi.

      Imefahamika kwamba umepatikana ushahidi mzito wa kuthibitisha malipo yaliyofanywa na British Aerospace Engineering (BAE) kuwa ni hongo kwa wale waliopitisha ununuzi huo, malipo yaliyofanywa wakati wa utawala wa Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa.

      BAE ilifanya mipango miwili tofauti na Vithlani ambapo kwanza, makubaliano ilikuwa ni kusaini malipo ya kamisheni ya asilimia moja, baada ya kupitishwa kwa ununuzi wa rada wa Dola za Marekani milioni 40.

      Mwezi mmoja baada ya kupitishwa kwa ununuzi huo na serikali, BAE iliilipa kampuni ya Merlin International Ltd hapa nchini, jumla ya Dola za Marekani 400,000.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action


    2. #2
      Mfumwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2008
      Posts : 1,470
      Rep Power : 845
      Likes Received
      15
      Likes Given
      1

      Default Re: Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      Quote By Bubu Ataka Kusema
      Chenge, Dk. Rashidi, Vithlani na Somaiya wote wametajwa kuwa washiriki wakuu waliowaongozwa wengine katika kufanikisha biashara hiyo tata kwa upande wa Tanzania kila mmoja kwa sasa amekwisha kuchunguzwa kuhusiana na suala hilo.
      Dr. Rashid tumbo joto, afadhali Chenge kaanza kuzoea kufikishwa mahakamani (kesi ya kugonga watu na kuua). Hivi huyu Somaiya ndio alikuwa na kesi Kenya na imeripotiwa katorokea India?, manake huyo Somaiya aliyetoroka wanasema alikuwa anahitajika pia Tanzania. Ukifisadi utaishi kwa mashaka siku zote, "mbio za sakafuni huishia ukingoni...".

    3. #3
      Jamco_Za's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th July 2007
      Posts : 1,238
      Rep Power : 857
      Likes Received
      20
      Likes Given
      0

      Default Re: Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      Sasa nafikiri wakati wa kusema kweli umefika, chenge najua hatukubali kushitakiwa peke yake, Je Mkapa atatjwa kwenye hii kashifa kama mwanzo wa kutajwa kila sehemu anapohusika.

      Huwezi kuwatenganisha Mkapa na Chenge hata kidogo, kama chenge atashitakiwa basi Mkapa ajiandae vinginevyo moto utawaka

    4. BAK
      #4
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,827
      Rep Power : 45014
      Likes Received
      8681
      Likes Given
      8666

      Default Re: Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      Quote By Jamco_Za
      Sasa nafikiri wakati wa kusema kweli umefika, chenge najua hatukubali kushitakiwa peke yake, Je Mkapa atatjwa kwenye hii kashifa kama mwanzo wa kutajwa kila sehemu anapohusika.

      Huwezi kuwatenganisha Mkapa na Chenge hata kidogo, kama chenge atashitakiwa basi Mkapa ajiandae vinginevyo moto utawaka
      Mie bado naamini huu ni usanii tu wa kuelekea 2010 siku zote hizi walikuwa wapi? Pia kabla ya kuwashtaki wazirudishe pesa zilizo kwenye bank accounts za nje za Chenge na Idrissa huko hazina haraka iwezekanavyo.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    5. #5
      Madela Wa- Madilu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th March 2007
      Location : NORTH WEST USA
      Posts : 2,524
      Rep Power : 2445
      Likes Received
      279
      Likes Given
      286

      Default Re: Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      Kuna wakati wa kula huku umezungukwa na harufu nzuri za misosi na kuna wakati wa ulichokula kukutoka.
      Mbaya ni pale kikutokapo kupitia mdomoni na puani baada ya kukaa tumboni kwa muda wa kutosha.
      Nchi zetu bado changa sana kujua madhara yote ya kuiba fedha za wananchi.

      Sisi tuliambiwa tutakula Nyasi, wao watanyea debe.
      MYPEOPLE PERISH FOR LACK OF KNOWLEDGE. HOSEA 4:6


    6. #6
      Dark City's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th October 2008
      Location : Roaming
      Posts : 11,756
      Rep Power : 23596
      Likes Received
      7123
      Likes Given
      11534

      Default Re: Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      Quote By Bubu Ataka Kusema
      Mie bado naamini huu ni usanii tu wa kuelekea 2010 siku zote hizi walikuwa wapi? Pia kabla ya kuwashtaki wazirudishe pesa zilizo kwenye bank accounts za nje za Chenge na Idrissa huko hazina haraka iwezekanavyo.
      Mkuu BAK,

      Mbona kila siku nawaambia kuwa hii ni michezo ya kuigiza? Hata wakipelekwa mahakama hatafungwa mtu. Siku ikitokea hivyo labda JK awe ametupwa nje ya Ikulu. Na afadhali mzee wa watu Dr Salimu aliukosa urais. Sijui angefanyaje na haya madudu!

    7. #7
      Madela Wa- Madilu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th March 2007
      Location : NORTH WEST USA
      Posts : 2,524
      Rep Power : 2445
      Likes Received
      279
      Likes Given
      286

      Default Re: Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      Kabla onyesho halijaanza ni lazima kuandaa jukwaa.
      Jukwaa linaandaliwa.
      Onyesho likianza hakuna kurudi nyuma.

      Vita kali ya kukatilia mbali tabaka tawala siku zote huanza wakati wa Amani.
      Wakati wa Amani Tabaka tawala hudhani Amani ndiyo mlinzi wao mwaminifu.
      Ukianzisha Vita ya namna hiyo wakati wa Machafuko hutofanikiwa kwani wanatabaka watakuwa macho wakikusubiri.
      MYPEOPLE PERISH FOR LACK OF KNOWLEDGE. HOSEA 4:6

    8. #8
      Semilong's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th March 2009
      Posts : 1,614
      Rep Power : 1255
      Likes Received
      92
      Likes Given
      112

      Default Re: Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      watu wa mkapa wanakamatwa sasa hivi ,
      je watu wa kikwete (RA,EL) watakamatwa baada ya kikwete kutoka madarakani
      You can not keep 40m people quite forever....
      one year one month one day they will wake up..........

    9. #9
      Zogwale's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 10th July 2008
      Posts : 6,127
      Rep Power : 6510
      Likes Received
      1248
      Likes Given
      536

      Default Re: Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      Jamani BAK hii haikuwa habari kwa ajili ya Fools Day??? Huwa najihadhari kupeleka kitu makini cha kweli kwenye media siku ya FOOLS. Sasa tuhakikishie kama hii habari ya jana 1st April si ya Fools. Aotherwise, kama ni kweli hi hatua njuri japo always ni mass attraction but matokea zero.

    10. #10
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,862
      Rep Power : 7377
      Likes Received
      6195
      Likes Given
      22546

      Default Re: Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      Wana JF, niliwahi kusema huko nyuma, serikali inakurupukia mahakamani ili kujenga cheap popularity na watu, lakini baadhi ya kesi zenyewe, hazina legal merit. hata hiyo kesi ya vithlani is nothing. hii kesi ya radar is anoher nothing. Naomba muamini msiamini, hawana cha kufikisha mahakamani.
      Uthibitisho kama kagoda kaanzisha kampuni hewa, kalamba bilioni 40. akaifuta hiyo kampuni, hivyo kagoda is non existance hakuna wa kumshitaki. lakini zile fedha, yaani hizo bilioni 40, ziliingizwa kwenye accounts za watu na makampuni ya ukweli. kama hili la wazi limeshindikana, litakuwa hili la ada ambalo ni la siri.
      Chenge fedha ni zake. bila link zimetokaje BAE zikamfikia, then its nothing na hakuna kesi yoyote, labda serikali iifungue tuu ili kuongeza kura za 2010.

    11. #11
      catimwa's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 2nd April 2009
      Posts : 4
      Rep Power : 0
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      sijaelewa vizuri mchakato mzima wa unuzi wa rada mwaka 2002, je mwaweza kunisaiia utaratibu uliotakiwa kufuatwa ili chenge na wenzanke wasiwe watuhumiwa?

    12. #12
      catimwa's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 2nd April 2009
      Posts : 4
      Rep Power : 0
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      expected procurement officer

    13. #13
      Shishye's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2009
      Location : On earth
      Posts : 270
      Rep Power : 579
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      Quote By Bubu Ataka Kusema
      Mie bado naamini huu ni usanii tu wa kuelekea 2010 siku zote hizi walikuwa wapi? Pia kabla ya kuwashtaki wazirudishe pesa zilizo kwenye bank accounts za nje za Chenge na Idrissa huko hazina haraka iwezekanavyo.
      Ninachojua mimi ni kuwa hii kesi inachunguzwa na waingereza wenyewe na ndio drivers (kama sivyo naomba nisahihishwe) otherwise ingeshatupiliwa mbali na kusahaulika siku nyingi au basi imeisha. At any point JK hana credits za kujipa kwenye hili maana hata baada ya evidence zote hizo hajamchukulia hatua zozote za kinidhamu. Hata kama uchunguzi bado unaendelea, sababu hiyo hiyo iliyomtoa kwenye uwaziri ilitakiwa kumtoa kwenye uongozi mwingine wowote, sio kwa hiari, bali mkuu wake kushupaa. This never and will never happen.

      Sina hakika though kwamba hawa washtakiwa wakitakiwa mahakamani kesi zitaendeshwa kwa sheria na vyombo gani - JK na wafuasi wake watakuwa na influence gani for Chenge, maana hao waingereza watakuwa wanaifuatilia pia. Ninachojua pia ni kwamba ukitaka kumwona mtanzania alivyo mchapa kazi, mpe bosi wa kizungu!

    14. BAK
      #14
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,827
      Rep Power : 45014
      Likes Received
      8681
      Likes Given
      8666

      Default Re: Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      Quote By Dark City
      Mkuu BAK,

      Mbona kila siku nawaambia kuwa hii ni michezo ya kuigiza? Hata wakipelekwa mahakama hatafungwa mtu. Siku ikitokea hivyo labda JK awe ametupwa nje ya Ikulu. Na afadhali mzee wa watu Dr Salimu aliukosa urais. Sijui angefanyaje na haya madudu!
      Mkuu DC, ahsante sana Mkuu. Kauli yako ni kweli kabisa maana hakuna dalili zozote za kupandishwa kizimbani fisadi Chenge alias Mzee wa Vijisenti labda ni mmoja wa wale ambao 'nchi itawaka moto' kama wakipandishwa kizimbani. Kweli CCM imeshika 'utamu'
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    15. #15
      Chief's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th June 2006
      Posts : 960
      Rep Power : 860
      Likes Received
      99
      Likes Given
      232

      Default Re: Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      Na kesi ya akina Lukaza imeishia wapi? Haitajwi siku hizi. Hizi kesi zote kwei ni usanii mtupu.

    16. #16
      Manitoba's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 8th July 2008
      Posts : 248
      Rep Power : 607
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default Re: Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      Quote By Pasco
      Wana JF, niliwahi kusema huko nyuma, serikali inakurupukia mahakamani ili kujenga cheap popularity na watu, lakini baadhi ya kesi zenyewe, hazina legal merit. hata hiyo kesi ya vithlani is nothing. hii kesi ya radar is anoher nothing. Naomba muamini msiamini, hawana cha kufikisha mahakamani.
      Uthibitisho kama kagoda kaanzisha kampuni hewa, kalamba bilioni 40. akaifuta hiyo kampuni, hivyo kagoda is non existance hakuna wa kumshitaki. lakini zile fedha, yaani hizo bilioni 40, ziliingizwa kwenye accounts za watu na makampuni ya ukweli. kama hili la wazi limeshindikana, litakuwa hili la ada ambalo ni la siri.
      Chenge fedha ni zake. bila link zimetokaje BAE zikamfikia, then its nothing na hakuna kesi yoyote, labda serikali iifungue tuu ili kuongeza kura za 2010.
      Tuchukulie kwamba majambazi yameanzisha kampuni ya ulinzi, yakaajiri vijana na kuwafanyisha mazoezi, kisha kwenda kuvamia benki na kuiba na hatimaye kuifuta kampuni. Kwa hiyo logic yako hiyo then hakuna wa kumshtaki kwasababu kampuni ni non-existance.

      Hiyo argument yako huwa inatumika sana siku hizi. Mimi sio mwanasheria, lakini hainiingii akilini. Kama wewe ni muhasibu na kwa makusudi ukaisaidia kampuni yako kuiba, then nadhani wewe binafsi sio shahidi tu bali ni mshiriki kamilifu wa wizi huo. Hata kama ulitumwa na bosi wako ukaibe.

      Kufanya kazi kwa niaba ya kampuni hakukupi wewe immunity ya kuvunja sheria za nchi. Tena kwa maslahi yako binafsi. Ingekuwa hivyo mbona kila mwizi duniani angekuwa anaunda kampuni ambayo anaivunja baada ya wizi kufanyika.

      Na nadhani hilo la linki ya pesa zilizoenda kwenye hiyo account ya Chenge umeliona mikoni chini miguu juu. Sio kwamba walianza na account ya Chenge na kuanza kushangaa fedha hizo zimetoka wapi. Ni kwamba walikutana na account ya Chenge wakati wana-trace fedha za rada zilienda wapi. Kwa hiyo hakuna linki ya kutafuta. I stand to be corrected.
      There are only 10 types of people in the world. Those that understand binary, and those that don't.

    17. #17
      Mpita Njia's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd March 2008
      Posts : 6,751
      Rep Power : 3269
      Likes Received
      991
      Likes Given
      785

      Default Re: Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      Quote By Bubu Ataka Kusema
      Mkuu DC, ahsante sana Mkuu. Kauli yako ni kweli kabisa maana hakuna dalili zozote za kupandishwa kizimbani fisadi Chenge alias Mzee wa Vijisenti labda ni mmoja wa wale ambao 'nchi itawaka moto' kama wakipandishwa kizimbani. Kweli CCM imeshika 'utamu'
      Hivi hamjabaini tu kuwa habari yenyewe ni ya April 1
      I assume full responsibility for my actions, except the ones that are someone else's fault.

    18. #18
      Jamco_Za's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th July 2007
      Posts : 1,238
      Rep Power : 857
      Likes Received
      20
      Likes Given
      0

      Default Re: Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      Yes it was april fools, ndio maana hajapandishwa kizimbani mpaka leo.

    19. #19
      S. S. Phares's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2006
      Posts : 3,042
      Rep Power : 1251
      Likes Received
      16
      Likes Given
      119

      Default Fresh Twist: Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      Fresh mystery on Chenge`s billions




      By Guardian on sunday team



      23rd August 2009



      Email




      Print




      Comments









      Andrew John Chenge



      The source of Andrew John Chenge’s $1.5million(Sh2.1bilion) found in his offshore bank account in Jersey, last year, remains a mystery as local investigators failed to connect the dots on whether the billions are part of the radar’s kickback pays amounting to $12million. But, as the mystery about the source of Chenge’s billions deepens, the UK’s Serious
      Fraud Office (SFO) still strongly believes that $1.5million (Sh2.1billion) found in the offshore bank account of Tanzania’s former Attorney General and Cabinet minister last year, is part of the radar’s kickback pays.

      The fresh twist on the source of the money sharpens the contradiction between the two credible institutions currently investigating the radar scam – SFO and the local Prevention and Prevention of Corruption Bureau (PCCB).
      By-products of the contradiction include deeper controversy, wider mystery and bigger confusion over who actually pocketed the huge kickback pays from radar paymaster Sailesh Vithlani.

      According to a reliable source within the PCCB, the anti-graft agency has failed to establish whether the Chenge billions are part of the radar’s kickback pays or not. The move cast a bleak a future on the much-awaited case that has drawn public attention since the revelation that the UK’s BAE System paid a total of $12million to Vithlani.

      “We haven’t received any credible evidence linking Chenge’s billions to the radar deal…but that doesn’t mean it is the end of the road, ”a senior official of the PCCB investigation team told The Guardian on Sunday under conditions of anonymity.

      “His file is still pending as we try to tie the dots together, but so far , we haven’t found a direct link of his billions to the radar kickback payments.”
      But contacted on Friday, the SFO official close to the investigation emphatically maintained that “there’s clear evidence that the billions are part of the radar’s deal until proven otherwise.”

      Speaking to The Guardian on Sunday over the phone, the SFO official who earnestly requested anonymity said, “What you are telling me is news to me…we have every clear evidence to prove that this was part of the radar deal; but if someone claims that there’s no link then he should wait for our final report.”

      SFO version

      In March last year, UK investigators probing the controversial $40m BAE radar deal claimed that ex-Infrastructure Minister Cheyo received $1.5m (2.1bn/-) in kickbacks from the deal through a slush fund he set up in the UK island of Jersey.

      According to SFO’s draft, Chenge received payments through six credit transfers between June 19, 1997, and April 17, 1998, while he was serving as Attorney General.

      The SFO draft further claimed that, the monies were paid to account No.59662999 owned by Franton Investment Limited through Bank Code No 204505 of Barclays Bank Plc. The SFO proved beyond reasonable doubt that Chenge owns Franton Investment— a registered company that appears to have been established primarily to facilitate the transfer of the money.
      According to information provided by the Jersey Authority, the $1.5m was transferred from a Frankfurt branch of Barclays Bank to Chenge’s account at a Jersey branch.

      Chenge resigned last year after the SFO’s revelations that he had $1.5m in his offshore bank account suspected to have been obtained from the $12m payoff that broker Sailesh Vithlani took from BAE System, the UK’s biggest arms supplier.

      He is alleged to have told his banker that the $1.5m was professional earnings from his work as a lawyer, but later contradicted himself, saying the money was a combination of inheritance and family savings, adding that 25 percent of the money belonged to his wife.

      The SFO believes that Vithlani had made payments to Tanzanian public officials in a position of influence in the BAE System contract negotiations, in which he brokered the purchase of military radar at an inflated price and skimmed a cut for himself and those who aided him in committing the crime.

      UK investigators also believe that Chenge was one of the top people to receive a payoff from Vithlani because without the AG’s agreement, the financing package for the radar could not have gone through.

      The AG’s office under Chenge was required to comment on and approve the financing package to purchase the radar deal, for which Tanzania was forced to borrow from the Barclays Bank Plc. The $12m back-door payment to Vithlani, Chenge and others, represented 30 percent of the contract value.

      In the wake of the saga, Chege shocked the public by casually remarking that the money in question was “vijisenti”, which loosely translates as “peanuts”.




      SOURCE: GUARDIAN ON SUNDAY


      My Take: Corruption On Top of Corruption..!! Tanzania..!!!

    20. #20
      Nemesis's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th February 2008
      Posts : 2,667
      Rep Power : 1522
      Likes Received
      34
      Likes Given
      94

      Default Re: Chenge aandaliwa mashitaka ya rada

      zile pesa ni za meremeta siyo rada, hapo Chenge kishashinda kiulaini tu. Unajua kwanini? kwasababu hawataki kuifunua meremeta, mambo ni funika kikombe mwanaharamu apite.

    Page 1 of 2 12 LastLast

    Similar Topics

    1. SFO: Hivi ndivyo Chenge alihusika kashfa ya rada!
      By mundele in forum Jamii Intelligence
      Replies: 69
      Last Post: 11th August 2012, 00:35
    2. Jamani issue ya rada na chenge vipi?
      By hittler in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 0
      Last Post: 22nd July 2011, 09:47
    3. KICHEFU CHEFU:SAKATA LA RADA:Kina Ndugai wataka kina Chenge washitakiwe
      By Tonge in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 6
      Last Post: 6th July 2011, 14:48
    4. Replies: 40
      Last Post: 16th February 2011, 10:25
    5. TAKUKURU: Chenge hahusiki na tuhuma za RADA
      By nickname in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 137
      Last Post: 23rd November 2010, 19:19

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...