Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Huu ndiyo Mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (Articles of Union)

    Report Post
    Page 1 of 6 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 120
    1. #1
      SubiriJibu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th June 2009
      Posts : 270
      Rep Power : 768
      Likes Received
      192
      Likes Given
      163

      Default Huu ndiyo Mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (Articles of Union)

      xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
      Wapendwa JF, mtandao uletao mabadiliko nchini,

      Kwa miaka mingi watanzania tumekuwa tukijadili mengi juu lakini hatukupata fursa pana ya kujadili Mkataba wa Muungano yaani Articles of Union uliosainiwa na Nyerere na Karume.

      Haijapita miaka mitatu tangu baadhi ya wazanzibar walipoadhimia kuupata mkataba huu wakaambiwa hauonekani, na nadhani wakajaribu waupate kule United Nations ila sikumbuki huku waliambiwaje huko.

      Tundu Lissu mwaka jana alipowasilisha Hotuba ya Kambi ya Upinzani alielezea dai la Serikali ya Tanganyika lakini akatamka wazi kuwa “hatutaki kuona picha za Nyerere na Karume wakichanganya udongo, tunataka Mkataba wa Muungano”.

      Kumbuka, miaka miwili nyuma, ni hapahapa JF wenzetu wengi walitafuta cha Julius Nyerere kiitwacho “Uongozi wetu na Hatima ya Tanganyika”. Nilipokimwaga humu jamvini kulikuwa na chereko kibao.

      Leo tena, nawaletea Mkataba wa Muungano yaani Articles of Union. Wapo wanaosema Mkataba huu ndiyo mama wa katiba zetu mbili yaani ya Muungano na ya Zanzibar. Wapo wanaosema yale mambo 11 ya Muungano yameongezwa kadhaa. Sasa mkataba huu tuuone ukweli wake.

      Ni nafasi yetu leo Jamii Forumn, tuendelee kunoyesha kuwa sisi ni “never dry thintank, tunatafiti and we dare talk openly”. Vilivyojificha tuna uwezo wa kuvifurumua vikawekwa hadharani.

      MODERATOR

      Nakumbuka thread ile ya Kitabu cha Hatima ya Tanzania iliwekwa kama “Sticky” na hivyo ikajadiliwa kwa mapana bila kupotezewa.
      Ningeomba tuwasaidie hivyohivyo wana-JF wengi kwa kui-stick hii pia, kwani naamini asilimia kubwa itakuwa ndiyo mara yao ya kwanza kuuona.

      Mkataba ni kama ifuatavyo:
      xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

      MKATABA WA MUUNGANO BAINA YA JAMHURI YA TANGANYIKA NA JAMHURI YA WATU WA ZANZIBAR


      Kwa kuwa Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar zinafahamu uhusiano wa muda mrefu watu wake na mshikamano na kukuza uhusiano huo na kuimarisha mshikamano na kukuza umoja wa watu wa Afrika, zimekutana na kutafakari Muungano wa Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar.

      Na kwa kuwa Serikali za Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar, zinapendelea ya kwamba Jamhuri hizi mbili ziungane kuwa Jamhuri moja huru moja kwa amasharti ya makubaliano yafuatayo:

      Kwa hiyo IMEKUBALIWA baina ya Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika na ya Jamhuri ya watu wa Zanzibar kama ifuatavyo:-

      I) Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar zitaungana na kuwa Jamhuri huru moja.

      II) Katika kipindi cha kuanza kwa Muungano mpaka Baraza la Kutunga katiba lililotajwa katika ibara ya (vii) litakapokutana na kupitisha katiba ya Jamhuri ya Muungano (Kuanzia hapa kitaitwa kipindi cha mpito), Jamhuri ya Muungano itaongozwa kwa masharti ya ibara ya (iii) mpaka ya (vi).

      III) Katika kipindi cha mpito katiba ya Jamhuri ya Muungano itakuwa katiba ya Tanganyika iliyorekebishwa ili kuweka:

      a) Chombo tofauti cha kutunga sheria na Serikali kwa ajili ya Zanzibar kwa mujibu wa sheria zilizopo za Zanzibar na vitakuwa na mamlaka ya mwisho katika Zanzibar kwa mambo yote isipokuwa yale tu yaliyo chini ya bunge na Serikali ya Jamhuri ya Muungano

      b) Nafasi ya makamo wawili wa Rais mmoja kati yao akiwa ni mkaazi wa Zanzibar atakuwa ndiye kiongozi wa Serikali iliyotajwa kwa ajili ya Zanzibar na atakuwa ndiye msaidizi mkuu wa rais wa Jamhuri ya Muungano katika utekelezaji wa kazi za Serikali kwa upande wa Zanzibar.

      c) Uwakilishi wa Zanzibar katika bunge la Jamhuri ya Muungano.

      d) Mambo mengine yatayofaa au kuhitajika ili kuipa nguvu Jamhuri ya Muungano na mkataba huu.

      IV) Mambo yafuatayo yatakuwa chini ya bunge na Serikali ya Jamhuri ya Muungano:-

      a) Katiba na Serikali ya Jamhuri ya Muungano
      b) Mambo ya nchi za nje
      c) Ulinzi
      d) Polisi
      e) Mamlaka yanayohusika na hali ya hatari
      f) Uraia
      g) Uhamiaji
      h) Mikopo na biashara ya nchi za nje
      i) Utumishi katika Jamhuri ya Muungano.
      j) Kodi ya mapato inayolipwa na watu binafsi na mashirika, ushuru wa forodha na ushuru wa bidhaa zinazotengenezwa nchini na kusimamiwa na idara ya forodha
      k) Bandari, mambo yanayohusu usafiri wa anga, Posta na Simu

      V) Bunge na Serikali vilivyotajwa vitakuwa na mamlaka ya mwisho juu ya mambo yote yahusuyo Jamhuri ya Muungano na kuongezea mamlaka juu ya mambo yote yahusuyo Tanganyika.

      Sheria zote zilizopo za Tanganyika na za Zanzibar zitaendelea kutumika katika maeneo yao bila kuathiri:-

      a) Masharti yoyote yatakayowekwa na chombo chenye mamlaka ya kutunga sheria.

      b) Masharti yatakayowekwa kwa amri ya Rais wa Zanzibar juu ya sheria yoyote inayohusu jambo lolote lililotajwa kwenye ibara ya (iv), na kufuta sheria yoyote inayolingana Zanzibar.

      c) Mabadiliko yoyote kama yataonekana yanafaa au kuhitajika ili kufanikisha Muungano na mkataba huu.

      a) Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano atakuwa ni Mwalimu J. K. Nyerere na ataongoza Serikali ya Jamhuri ya Muungano kwa kufuata masharti ya mkataba hu na kwa kusaidiwa na maofisa wengine atakaowateuwa toka Tanganyika na Zanzibar na watumishi wa Serikali zao.

      b) Makamo wa kwanza wa Rais kutoka Zanzibar aliyeteuliwa kwa kufuata marekebisho kama yalivyoelezwa na ibara ya 3, atakuwa Sheikh Abeid Karume.

      VI) Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa kukubaliana na Makamo wa Rais ambaye ni kiongozi wa serikali ya Zanzibar

      a) Atateua tume kwa ajili ya kutoa mapendekezo kwa ajili ya katiba ya Jamhuri ya Muungano.
      b) Ataitisha Baraza la kutunga katiba ikiwa na wawakilishi kutoka Tanganyika na Zanzibar katika idadi itakayoamuliwa likutane katika kipindi cha mwaka mmoja tokea kuanza kwa muungano kwa madhumuni ya kutafakarimapendekezo ya tume iliyotajwa juu na kupitisha katiba ya Jamhuri ya Muungano.

      VII) Mkataba huu utahitaji kuthibitishwa kwa kutungiwa sheria na Bunge la Tanganyika na Baraza la Mapinduzi la Jamhuri ya Watu wa Zanzibar kwa kushirikiana na Baraza lake la Mawaziri, na mkataba kupitishwa na kuundwa kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano na ya Zanzibar kwa kufuata masharti yaliyokubaliwa.

      KWA KUSHUHUDIA HAPA Julius K. Nyerere, Rais wa Jamhuri ya Tanganyika na abeid Karume, Rais wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, wametia saini nakala mbili za mkataba huu, hapa Zanzibar siku ya tarehe Ishirini na mbili ya mwezi Aprili, 1964.

      ……………………………………………………………………………… …………………….
      Umepitishwa na Bunge siku ya tarehe Ishirini na Tano ya Aprili, 1964.


      ……………………………………………………………………………… …………………….
      Pius Msekwa, Karani wa Bunge

      ……………………………………………………………………………… …………………….
      Adam Sapi Mkwawa, Spika
      25 Aprili 1964

      xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
      SOURCE:

      1: {THE PATNERSHIP, ISBN: 9789987880553, pg. 156, Author: Aboud Jumbe, }

      2: {Zanzibar hadi mwaka 2000: ISBN: 9789987898015, pg. 201, Author: Ali Shaaban Juma}
      xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx
      Last edited by SubiriJibu; 6th May 2012 at 04:30.
      ...Kanisa halijawahi kumtuhumu Dr. Slaa kwa wizi wa hela za ujio wa Papa...{Jude Thaddaues O.F.M. Cap, Archbishop of Mwanza and President of Tanzania Episcopal Conference (TEC), March 20, 2012}

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      SURUMA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd March 2011
      Posts : 1,460
      Rep Power : 705
      Likes Received
      342
      Likes Given
      346

      Default

      Quote By SubiriJibu
      xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

      Wapendwa JF, mtandao uletao mabadiliko nchini,


      Kwa miaka mingi watanzania tumekuwa tukijadili mengi juu lakini hatukupata fursa pana ya kujadili Mkataba wa Muungano yaani Articles of Union uliosainiwa na Nyerere na Karume.

      Haijapita miaka mitatu tangu baadhi ya wazanzibar walipoadhimia kuupata mkataba huu wakaambiwa hauonekani, na nadhani wakajaribu waupate kule United Nations ila sikumbuki huku waliambiwaje huko.

      Tundu Lissu mwaka jana alipowasilisha Hotuba ya Kambi ya Upinzani alielezea dai la Serikali ya Tanganyika lakini akatamka wazi kuwa “hatutaki kuona picha za Nyerere na Karume wakichanganya udongo, tunataka Mkataba wa Muungano”.


      Kumbuka, miaka miwili nyuma, ni hapahapa JF wenzetu wengi walitafuta cha Nyerere kiitwacho “Uongozi wetu na Hatima ya Tanganyika”.
      Nilipokimwaga humu jamvini kulikuwa na chereko kibao.

      Leo tena, nawaletea Mkataba wa Muungano yaani Articles of Union. Wapo wanaosema Mkataba huu ndiyo mama wa katiba zetu mbili yaani ya Muungano na ya Zanzibar. Wapo wanaosema yale mambo 11 ya Muungano yameongezwa kadhaa. Sasa mkataba huu tuuone ukweli wake.

      Ni nafasi yetu leo Jamii Forumn, tuendelee kunoyesha kuwa sisi ni “never dry thintank, tunatafiti and we dare talk openly”. Vilivyojificha tuna uwezo wa kuvifurumua vikawekwa hadharani.


      MODERATOR
      Nakumbuka thread ile ya Kitabu cha Hatima ya Tanzania iliwekwa kama “Sticky” na hivyo ikajadiliwa kwa mapana bila kupotezewa.
      Ningeomba tuwasaidie hivyohivyo wana-JF wengi kwa kui-stick hii pia, kwani naamini asilimia kubwa itakuwa ndiyo mara yao ya kwanza kuuona.

      IDUMU JF:

      Mkataba ni kama ifuatavyo:
      Asante sana kwa hii nondo! JF kweli kiboko; nimo katika kundi la wale akina Thomas wasioamini-i thought kweli document hii haipatikani!
      SubiriJibu likes this.

    4. #3
      makeyzan's Avatar
      Member Array
      Join Date : 13th June 2011
      Posts : 54
      Rep Power : 412
      Likes Received
      11
      Likes Given
      4

      Default Re: Huu ndiyo Mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (Articles of Union)

      heee....ngoja nilale kwnza nikiamka nitaisoma vizuri.
      SubiriJibu likes this.

    5. #4
      palalisote's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th August 2010
      Location : WA HAPAHAPA
      Posts : 2,061
      Rep Power : 2038
      Likes Received
      928
      Likes Given
      3824

      Default Re: Huu ndiyo Mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (Articles of Union)

      Quote By SURUMA
      Asante sana kwa hii nondo! JF kweli kiboko; nimo katika kundi la wale akina Thomas wasioamini-i thought kweli document hii haipatikani!
      muda mwingine usinukuu post yote

    6. #5
      SubiriJibu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th June 2009
      Posts : 270
      Rep Power : 768
      Likes Received
      192
      Likes Given
      163

      Default Re: Huu ndiyo Mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (Articles of Union)

      Quote By SURUMA
      Asante sana kwa hii nondo! JF kweli kiboko; nimo katika kundi la wale akina Thomas wasioamini-i thought kweli document hii haipatikani!
      Asante Mkuu,

      Sorry utaona reply yako nime-edit. Si kubadilisha content, bali ni kwa sababu nimeitayarisha kwa kui-type kwenye document nyingine nikapata matatizo wakati naikopi kwenye browser ya JF online.

      P'se bear with me that.
      palalisote likes this.
      ...Kanisa halijawahi kumtuhumu Dr. Slaa kwa wizi wa hela za ujio wa Papa...{Jude Thaddaues O.F.M. Cap, Archbishop of Mwanza and President of Tanzania Episcopal Conference (TEC), March 20, 2012}

    7. Miaka 50

    8. #6
      Tony Almeda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th September 2011
      Location : C.T.U
      Posts : 395
      Rep Power : 467
      Likes Received
      117
      Likes Given
      37

      Default Re: Huu ndiyo Mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (Articles of Union)

      Ndio maana wanakataa tusiujadili........!
      Kwa kuwa una mapungufu mengi.

      palalisote likes this.
      WAMETHUBUTU, HAWAWEZI LAKINI WANASONGA MBELE

    9. #7
      Asprin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 8th March 2008
      Location : Psychiatric Ward
      Posts : 25,439
      Rep Power : 32075
      Likes Received
      14541
      Likes Given
      22033

      Default

      Quote By SURUMA
      Asante sana kwa hii nondo! JF kweli kiboko; nimo katika kundi la wale akina Thomas wasioamini-i thought kweli document hii haipatikani!
      Mkuu kuquote post ndefu namna hii ni usumbufu kwa wasomaji hasa ambao wako via mobile.
      Kigogo likes this.

    10. #8
      Asprin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 8th March 2008
      Location : Psychiatric Ward
      Posts : 25,439
      Rep Power : 32075
      Likes Received
      14541
      Likes Given
      22033

      Default Re: Huu ndiyo Mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (Articles of Union)

      Bunge lililopitisha mkataba tar 25/4, lilikuwa la Tanganyika peke yao au lilihusisha wazanzibari? Sijaona sehemu spika wa Zenji akitajwa.

    11. #9
      RedDevil's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th April 2009
      Location : Hapa Hapa
      Posts : 1,455
      Rep Power : 803
      Likes Received
      269
      Likes Given
      512

      Default Re: Huu ndiyo Mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (Articles of Union)

      Ndiyo kwisha habari hapo? Duh, inabidi kutafakari kweli uhalali wa huu muungano aka "bomu la muungano"
      "Never argue with stupid people, they will drag you down to their level and then beat you with experience" Mark Twain

    12. #10
      tempo_user1's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 7th September 2010
      Posts : 127
      Rep Power : 466
      Likes Received
      11
      Likes Given
      0

      Default Re: Huu ndiyo Mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (Articles of Union)

      Tatizo sio mkataba wenyewe, tatizo ni kwamba mkataba haukufwatwa tangu mwanzo wake. ulichokiweka hapa ni mkataba ambao ulijadiliwa na bunge la Tanganyika. mkataba ulitaka pia bunge la Zanziba liujadili na kuupitisha ndipo usainiwe kuwa sheria rasmi ya kuanzisha Jamhuri ya Tanganyika na Zanzibar. kwa upande wa Zanzibar hawakupata fursa hiyo kwani hata bunge halikuwepo. na pia hakuna ushahidi wowote kwamba bunge la Zanzibar liliwahi kukaa na kupitisha mkataba huo, hivyo hata kama mkataba ni mzuri kiasi gani - unakosa uhalali wa kisheria.
      mkomatembo and MAKAWANI like this.

    13. #11
      Mzalendo Mkuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2010
      Posts : 547
      Rep Power : 547
      Likes Received
      91
      Likes Given
      285

      Default Re: Huu ndiyo Mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (Articles of Union)

      wewe ni Jembe. Tunafurahi kuyaona haya.

    14. #12
      Jumakidogo's Avatar
      R I P Array
      Join Date : 16th July 2009
      Location : DOM & DAR
      Posts : 1,868
      Rep Power : 1176
      Likes Received
      390
      Likes Given
      42

      Default Re: Huu ndiyo Mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (Articles of Union)

      Sasa huu ni mkataba? Au utani?

    15. #13
      Makame's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd January 2008
      Posts : 513
      Rep Power : 680
      Likes Received
      57
      Likes Given
      23

      Default Re: Huu ndiyo Mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (Articles of Union)

      Aliyeleta hio ametoa kwenye kitabu cha aboud jumbe mwinyi 'the partnership - thirty turbulent years of the union'

      kisheria hio sio document yenyewe kwa kuwa:-

      1. Hau jatiwa saini na spika wala katibu wa bunge.

      2. Haujatiwa saini na yeyote mwenye mamlaka anayewakilisha jamhuri ya tanganyika na jamhuri ya zanzibar

      wanasheria wataongezea
      kibogo likes this.
      God made Man, Man made Money, Money made man mad!

    16. #14
      Kongosho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st March 2011
      Location : Location loading...
      Posts : 25,141
      Rep Power : 13061
      Likes Received
      14087
      Likes Given
      14889

      Default Re: Huu ndiyo Mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (Articles of Union)

      ndo hii tu au kuna document nyingine?

    17. #15
      Praff's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 9th March 2012
      Posts : 137
      Rep Power : 390
      Likes Received
      11
      Likes Given
      0

      Default Re: Huu ndiyo Mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (Articles of Union)

      Im still in dilemma.

    18. #16
      SALOK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th September 2011
      Location : Some where!!
      Posts : 1,169
      Rep Power : 620
      Likes Received
      222
      Likes Given
      207

      Default Re: Huu ndiyo Mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (Articles of Union)

      Nashukuru kukiona kile kinachoitwa mkataba wa muungano sijapatapo kuuona kabla wala sikufikiria siku moja ningeuona.
      Ahsante sana jf. Ahsante sana mleta mada!
      Ng'wanangwa likes this.

    19. #17
      kaburungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th March 2011
      Posts : 353
      Rep Power : 562
      Likes Received
      56
      Likes Given
      67

      Default Re: Huu ndiyo Mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (Articles of Union)

      Wajemeni mbona hayo mambo11 mi siyaoni,,,kah!!! mweee!

    20. #18
      Yericko Nyerere's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2010
      Location : Kigamboni, DSM
      Posts : 4,498
      Rep Power : 22956
      Likes Received
      2812
      Likes Given
      312

      Default Re: Huu ndiyo Mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (Articles of Union)

      Japokuwa sio ndio mkatba halisi, lakini mambo yote muhimu yapo, naamini utaamusha ufahamu wa wahafidhina mgando wa muungano huu batili!

    21. #19
      ITEGAMATWI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th January 2012
      Posts : 1,666
      Rep Power : 776
      Likes Received
      421
      Likes Given
      826

      Default Re: Huu ndiyo Mkataba wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar (Articles of Union)

      Alaaaah!!Kumbe ndiyo maana kila kukicha wimbo ni ule ule wa kero za muungano!Kwakweli viongozi wetu hawajatutendea haki hata kidogo!!Nitaendelea kuwalaumu hata huko huko makaburini walipo!

    22. #20
      Yericko Nyerere's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2010
      Location : Kigamboni, DSM
      Posts : 4,498
      Rep Power : 22956
      Likes Received
      2812
      Likes Given
      312

      Default

      Quote By kaburungu
      Wajemeni mbona hayo mambo11 mi siyaoni,,,kah!!! mweee!
      Duuuh hivi ulitaka mpaka iandikwe 1,2,3 au a,b,c huzioni ndugu? Unaniangusha mkuu!
      Ng'wanangwa and kaburungu like this.

    Page 1 of 6 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...