Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Bado Mizengo Pinda (PM) hajanusurika kuondoka madarakani. Hoja ya Zitto imeongezeka uthamani

    Report Post
    Results 1 to 14 of 14
    1. #1
      Nikupateje's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2009
      Posts : 855
      Rep Power : 966
      Likes Received
      544
      Likes Given
      601

      Default Bado Mizengo Pinda (PM) hajanusurika kuondoka madarakani. Hoja ya Zitto imeongezeka uthamani

      Ndugu wanabodi,

      Suala la Kamati Kuu ya CCM {CC-CCM} kutangaza kwamba imemruhusu JK alisuke upya Baraza la Mawaziri linaweza kuwa limefanikiwa kubadili upepo wa uelewa wa wananchi. Nikiangalia hata thread mbalimbali humo ninaiona hivyo.


      Sijui ni wangapi wameshagundua kwamba kwamba maamuzi ya jana ya CC-CCM yameipaisha zaidi hoja ile ya “Kutokuwa na imani na Waziri Mkuu” badala ya kui-pre-empt.

      Ambao hawajanielewa, basi badala ya kukejeli thread hii ni bora wanisome between lines.

      Kwanza tuanze na kilichofikisha yote hapa. Kilicholeteleza yote haya ni mfululizo wa report ya Mkaguzi Mkuu (CAG) ambayo chronology yake ninaipanga kama ifuatavyo:

      01: CAG ku-submit report kwa Serikali
      02: Report kuifikia kama ya Bunge
      03: Report kusomwa mbele ya Bunge
      04: Report kujadiliwa na Bunge
      05: Mwitikio wa Serikali kwa hoja za Wabunge
      06: Zitto kutaarifu ukusanyaji wa sahihi 70
      07: Zitto kukusanya sahihi 70
      08: Zitto kuwasilisha hoja na sahihi zaidi ya 70
      09: JK kuitisha CC-CCM kuitishwa kwa ajenda ikiwa ni siri
      10: CC-CCM inamruhusu JK kufumua Cabinet yake

      Tuanze kuujadili mfululizo huu kifungu cha kwanza kwa kujiuliza, je, CAG ni muajiriwa wa nani? Anawajibika kwa nani? Kazi zake zinaripotiwa kwa nani?
      Ukweli ni kwamba Executive yaani Serikali ndiyo muajiri wa CAG. Ameajiriwa kwa kukagua matumizi ya Serikali.

      CAG si muajiriwa wa Bunge. Bunge haliwezi kumfukuza kazi kama report zake hazifiki bungeni. Kinachoweza kutokea ni Bunge kuishinikiza Serikali kumshughulikia CAG na si vinginevyo.

      Hivyo, report ya CAG, kituo chake cha kwanza ni Serikalini. Wakuu wa Serikali ni Rais, Makamu, Waziri Mkuu kisha Mawaziri yaani kwa kifupi Cabinet. Kumbe, watu wa kwanza kabisa kujua kilichomo kwenye report ya CAG ni Serikali.


      Sasa tujiulize, ni hatua gani zilichukuliwa na Serikali toka siku report ya CAG ilipofika mikononi mwao kabla ya mtu mwingine nchini kuiona. Mbona tume iliyopelekea Gavana Daud Balali ilipotoa report yake hatua zilichukuliwa ndani ya masaa 24 ya kutengua ugavana wa Balali. Kumbuka report ya Balali ilikwenda moja kwa moja kwa Rais mwenyewe wakati report ya CAG inasomwa kwa ushrikiano na President, Vice na PM. Tungetarajia ubovu uliokutwa kwenye report ya CAG ushughulikiwe kwa speed zaidi kwa sababu ya ushirika huu. Lakini hakuna uwajibikaji uliotokea.

      Tuje kipengele cha pili, taratibu zetu zimeruhusu report yaCAG ifike kwenye Kamati za Bunge. Ikishakuwa kwenye Kamati tayari kundi la wanaoujua madudu yaliyomo kwenye report linaongezeka. Mwanzo walijua timu ya Cabinet, sasa wanajua wanakamati, na tetesi zinaanza kuwafikia wabunge waio wanakamati. Hadi hapa siku zimeongezeka na bado hakuna kuwajibika mtu yeyote Serikalini.

      Tunaingia sasa kipengele cha 03 cha chronology, kwamba report ya CAG inasomwa Bungeni na Mwenyekiti wa Kamati. Hapa kundi la tatu kuelewa ubovu linaongezeka yaani wabunge wasio wanakamati. Ndipo sasa na sisi wananchi na tunaelewa upotevu uliomo kwenye report ya CAG.

      Inaposomwa Bungeni, Waziri Mkuu na Mawaziri wenzake, hapa si mara yao ya kwanza kujua kilichomo kama sisi na wabunge wasio wanakamati. Kwao hapa ni zaidi ya mara ya pili!
      Moyoni wanasema “upotevu waliouona kabla kabla ya wengine wote nchini, sasa unaanikwa hadharani”. Hadi hapa, siku zimeongezeka na hakuna Waziri aliyewajibika.

      Hatua ya nne sasa ni report inajadiliwa vikali na wabuunge. Ukipitia hansard, utaona si CCM au upinzani ukishinikiza njia kadhaa za kuwajibika. Hivyo, muitikio wa kuwajibika kwa mara ya kwanza unaanza kujionyesha. Si kutoka kwa Waziri Mkuu au Waziri yoyote, ambao siku zinaongezeka za kuwa kuwa wamejua kilichomo ripotini, bali unatoka kwa Wabunge.

      Point ya tano, ni reaction ya mawaziri baada ya reaction ya wabunge. Kwanza wapo mawaziri ambao wakati wa mjadala ule mkali hawakuwemo. Kuna wakati wabunge walihoji kwa nini PM hakuwemo wakati wabunge wakihoji kwa ukali. Kuna wakati wakahoji kwa nini Waziri Mkulo hakuwemo wakati wa mjadala. Waziri Lukuvi ndiye alijaribu kuzima moto kwa kueleza grounds za absence ya PM na Mkulo.

      Reaction ya mwisho ya mawaziri ni kusema, sasa wamejifunza wanaenda kuwashughulikia watendaji wabovu. Hii inatamkwa na Aggrey Mwanri na wengine kadhaa. Zitto Kabwe anahoji kuna tofauti gani na pledge ileile ya mwaka jana kuwa watawashughulikia wakati walishindwa.

      Kwa kifupi ni kwamba hapa Serikali inakiri ubovu lakini action yake si kuwajibika bali kuwawajibisha wakosefu mle reportini.

      Kabla ya kujadili kipengele cha saba cha hoja ya kutokuwa na imani na PM, napenda tukubaliane kwamba hadi hapa, unajiuliza iweje Serikali nzima iliyomtangulia kila mtanzania kujua madudu yaliyomo mle ripotini ndipo sasa ionyeshe reactio tena ya ahadi.

      Tujiulize, kwa nini Serikali kuanzia Waziri Mkuu hawakujipanga mapema kwamba wawajibishwe watu Serikalini kabla hata Bunge halijakutana ili Bunge litakapoanza wawe walau wana cha kutueleza kuwa Waziri fulani ameshawajibika, au Waziri mkuu alishauri na ushauri wake Rais anaufanya kazi. Badala yake Bunge lilianza bila kuwa na response yoyote ya kiserikali kuhusu haya. Hivyo, ukitaka kuelewa mantiki ya kumuondoa Waziri Mkuu kwa kura ni vizuri kuuangalia mpangilio huu.

      OK, sasa Zitto katangaza adhma ya kukusanya sahihi 70 kama tunavyojua. Humu nimeweka hilo kwenye section 06. Haipiti siku tatu Zitto bila kutarajia anakusanya zaidi ya signature 70 na kisha ana-submit hoja kwa Spika. Hadi hapa hoja ya Zitto ya kumuondoa Waziri Mkuu haina tena kizuizi kikatiba, inasubiri siku 14 zifike na wakati wowote itinge Bungeni mapema iwezekanavyo. Narudia ni kwa mujibu wa katiba si kwa mujibu wa JK, Makinda, Zitto, CCM, CHADEMA au wewe na mimi. Ni kwa mujibu wa Katiba.

      Sasa, wakati tunasubiri siku14, ghafla juzi tunaambiwa CC-CCM wameitana na agenda tunambiwa ni siri. Tunaweza kuwa wataalam wa kubashiri watakachoongea CC-CCM lakini ukweli ni kwamba wamesema ni siri yao hadi watakapoifanya isiwe siri.

      Jana jioni tukatangaziwa siri hiyo, kwamba CC-CCM imekubali mawaziri wang’oke. Magazeti yanaripoti jinsi mwana-CCM aitwaye Mizengo Pinda akimweleza mwana-CCM, Jakaya Kikwete azimio la wabunge wa CCM kuitaka Serikali iwawajibishe mawaziri.

      Mwanzoni nilikuwa mmoja wa waliomtetea Pinda asiwajibike kwa hoja kwamba hatujui communication yake kama PM na bosi wake President yakoje hivyo sikuwa na haki kumhukumu kwa kutomshauri. Lakini hata hivyo, bado unajiuliza kama Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, angekuwa amependekeza wateule wa Rais wawajibishwe, halafu Rais wa Tanzania akawa mbishi,
      Hiki ndicho kisa kilimfanya Julius Nyerere amsakame Waziri Mkuu, John Malecela kwamba kwa nini haku-resign kama Rais alikuwa anaelekea kumpuuza ushauri wake.

      Serikali iliposakamwa kwa tuhuma ra rushwa, yaani February 1990, Waziri Mkuu, Joseph Warioba aliamua ku-resign, na ikambidi Rais Ally Hassan Mwinyi aunde upya Serikali japo alimteua tena Warioba huyuhuyo kuwa PM na sasa wakazindua ufagio mrefu unaoitwa “fagio la chuma” la kufagia wala rushwa.

      Leo, Mizengo Pinda anashindwa kumshauri Rais kuwawajibisha wazembe serikalini, eti jana anaweza kumshauri kama mwana-CCM akifikisha azimio la wabunge wa CCM.

      Maana yake ni nini? Shinikizo na ushauri ule bado ni la wabunge na Pinda alifikisha taarifa kwa mwenyekiti wa CCM kuonyesha hali tete bungeni si kwa wabunge wa CCM tu.

      Kumbuka wakati huo, hoja ya Zitto inaendelea kukata mbuga kwa maana siku.

      HITIMISHO:

      Hivyo, hadi hapa huoni sababu ya kuendelea kuwa na Mizengo Pinda kama Waziri Mkuu wa Tanzania. Hoja ya Zitto ya kumuondoa Waziri Mkuu, inambana Waziri Mkuu aliyeshindwa kuwajibika tangu dakika alipopata report ya CAG, mapema kabla ya hata ya Kamati za Bunge.

      Kosa ninaloona kwa CCM ni kudhani kuwa azimio la jana la CC-CCM, litapunguza makali ya hoja hii kwa wananchi sasa wanaona “alichotaka Zitto ni kuwajibika, sasa mawaziri wanawajibishwa, Zitto anahitaji nini zaidi ya hilo?”.

      Wanaodhani hivyo, ukweli ni kwamba hoja ya Zitto inazidi kupanda chat. Kitendo cha mwana-CCM, Mizengo Pinda, kuonekana kulizingumza na JK mbele ya wanakamati, kinathibitisha kwamba, mwana-Serikali, Mizengo Pinda, hakuitumia nafasi hiyo wiki zilizopita kutoa ushauri huohuo aliotakiwa kuutoa kabla suala halijatinga Bungeni.

      Waziri Mkuu, Mizengo Pinda angepona hoja ya Zitto, iwapo wangeenda Bungeni tayari mawaziri hao wameshakukuliwa hatua inayotaka kutekelezwa sasa.
      Hivyo, kushusha thamani hoja ya Zitto na wenzake 70, ni kulivunja Baraza zima la Mawaziri akiwemo Waziri Mkuu (disolve) kama alivyofanya Ali Hassan Mwinyi, Feb. 1990 na Dec. 1994.

      Vinginevyo, hata JK abadili Mawaziri wote (reshuffle), akaleta wengine wapya lakini Waziri Mkuu hakuguswa na mabadiliko hayo, basi hiyo tutaiita ni reshuffle na bado hoja ya Zitto itabaki na uzito uleule yaani Waziri Mkuu aliyeshindwa kuwajibika dakika ileile ya mwanzao alipohitajika kuwajibika.

      Samahani kwa urefu wa post, imenibidi nifanye hivyo
      Last edited by Nikupateje; 28th April 2012 at 20:59. Reason: Enlerge font as rection from Matola
      Waberoya, Kikarara78 and Babkey like this.
      .."ni heri Dr. Willibrod Slaa ashinde na aingie Ikulu, kuliko Tundu Lissu kushinda ubunge na kuingia Bungeni"......Jakaya Mrisho Kikwete, Oct. 2010.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Matola's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th October 2010
      Posts : 12,514
      Rep Power : 19750
      Likes Received
      5443
      Likes Given
      3640

      Default Re: Bado Mizengo Pinda (PM) hajanusurika kuondoka madarakani. Hoja ya Zitto imeongezeka uthamani

      Hivyo vimaandishi vyako usidhani ni wote tunatumia lens kusoma, hebu edit hiyo thread yako uongeza size ya maandishi otherwise naona unatuumiza macho tu.
      Nikupateje likes this.
      Division four point 29 = Masters Mzumbe University. Nape Nnauye is my role model.

    4. #3
      Gambas's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th November 2011
      Location : Malimbe, Nyegezi Mwanza
      Posts : 955
      Rep Power : 2449
      Likes Received
      191
      Likes Given
      17

      Default

      Quote By Matola
      Hivyo vimaandishi vyako usidhani ni wote tunatumia lens kusoma, hebu edit hiyo thread yako uongeza size ya maandishi otherwise naona unatuumiza macho tu.
      dah! Wabongo jamani. Kakuelewa nadhani.

    5. #4
      oyaoya's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 4th March 2012
      Posts : 194
      Rep Power : 402
      Likes Received
      32
      Likes Given
      15

      Default Re: Bado Mizengo Pinda (PM) hajanusurika kuondoka madarakani. Hoja ya Zitto imeongezeka uthamani

      Mkuu, zipo tetesi WM aliwasilisha hoja ya kuwawajibisha mawaziri na watendaji husika kabla, (mbona hujaweka kwny hizo stages?) ikajibiwa "ni upepo tu, utapita"
      Wakuu, ikumbukwe si ishu zote za kiutendaji serikalini zinaanikwa hadharani, hivyo kinadharia (km ulivyowasilisha) hoja ya Zitto itatimizwa kwa kuwawajibisha wahusika kwa kuwa ndiyo lengo kuu la hoja na si kumwajibisha WM kwa kuwa yeye mwenyewe Zitto alikiri anampenda MP na anamheshimu isipokuwa wahusika wakiwajibishwa watakuwa wamemuokoa MP.

    6. #5
      Kimbunga's Avatar
      JF Platinum Member Array
      Join Date : 4th October 2007
      Location : Kisiwani Juma
      Posts : 7,478
      Rep Power : 6168
      Likes Received
      3054
      Likes Given
      1017

      Default Re: Bado Mizengo Pinda (PM) hajanusurika kuondoka madarakani. Hoja ya Zitto imeongezeka uthamani

      Mkuu oyaoya usemayo ni kweli. Zitto hakumtaka waziri mkuu. Hoja ya Zitto ilikuwa mawaziri wanaotuhumiwa wajiuzulu na kama hawatajiuzulu basi wanamuweka rehani PM na wabunge watamchukulia hatua PM kwa kuwa wana uwezo naye. Hivyo kama mawaziri wataondoka Zitto atakuwa ametimiza lengo lake. Japo sioni Mtoto wa MKulima akibaki.
      Lakini pia mtoa hoja amesisitiza kuwa hoja ya kutokuwa na imani na PM inasubiri kujadiliwa na kwa mujibu wa katiba lazima ijadiliwe. Ukweli ni kwamba taarifa ikishapelekwa kwa spika basi spika ana uwezo wa kukubali ama kukataa hoja kuwasilishwa; kwa mujibu wa Katiba.

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      Raia Fulani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th March 2009
      Posts : 9,255
      Rep Power : 2623
      Likes Received
      1291
      Likes Given
      834

      Default Re: Bado Mizengo Pinda (PM) hajanusurika kuondoka madarakani. Hoja ya Zitto imeongezeka uthamani

      asante kwa uchambuzi mwanana ndugu yetu

    9. #7
      Greard's Avatar
      Member Array
      Join Date : 23rd December 2010
      Posts : 58
      Rep Power : 437
      Likes Received
      13
      Likes Given
      0

      Default Re: Bado Mizengo Pinda (PM) hajanusurika kuondoka madarakani. Hoja ya Zitto imeongezeka uthamani

      nimejitahidi kusoma lkn siku nyingine jifunze kuandika thread fopi
      Nikupateje likes this.

    10. MTK
      #8
      MTK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th April 2012
      Posts : 931
      Rep Power : 4495
      Likes Received
      300
      Likes Given
      330

      Default Re: Bado Mizengo Pinda (PM) hajanusurika kuondoka madarakani. Hoja ya Zitto imeongezeka uthamani

      Good food for thought; kwa maono mengine ni kwamba PM pia alichukua attitude ya kusema kwamba ni upepo tu wa kisiasa utapita ili watanzania na wabunge wao washushe munkari hadi alipomsikia Mr. 2 akimwambia hiki ni kimbunga na destination ni yeye. unajua watu kama hawa kina PM ambao wamegeuza siasa kuwa taaluma ili waendelee kuganga njaa ni tatizo kubwa sana kwa nchi zinazoendelea na hasa ukizingatia na mifuma ya utawala na taasisi zetu.
      Itapendeza kama wabunge wetu wata push forward ili PM awajibike kivyake, hakuna sababu ya kumuonea huruma kama yeye hajionei huruma, falsafa ya "Funika kikombe mwanaharamu apite si faraja kwa taifa letu hata kidogo, PM purpots to be a devout and practicing Catholic lakini bado anacondone ubadhirifu kama huu!

    11. #9
      mkurugenz's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Posts : 200
      Rep Power : 400
      Likes Received
      15
      Likes Given
      16

      Default Re: Bado Mizengo Pinda (PM) hajanusurika kuondoka madarakani. Hoja ya Zitto imeongezeka uthamani

      pm anaweza kuwa sasha kama reshafle itakuwa na tija vinginevyo budgetary parliament litamsumbua

    12. #10
      Nikupateje's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2009
      Posts : 855
      Rep Power : 966
      Likes Received
      544
      Likes Given
      601

      Default Bado Mizengo Pinda (PM) hajanusurika kuondoka madarakani. Hoja ya Zitto imeongezeka uthamani

      Quote By Kimbunga
      Mkuu oyaoya usemayo ni kweli. Zitto hakumtaka waziri mkuu. Hoja ya Zitto ilikuwa mawaziri wanaotuhumiwa wajiuzulu na kama hawatajiuzulu basi wanamuweka rehani PM na wabunge watamchukulia hatua PM kwa kuwa wana uwezo naye. Hivyo kama mawaziri wataondoka Zitto atakuwa ametimiza lengo lake. Japo sioni Mtoto wa MKulima akibaki.
      Lakini pia mtoa hoja amesisitiza kuwa hoja ya kutokuwa na imani na PM inasubiri kujadiliwa na kwa mujibu wa katiba lazima ijadiliwe. Ukweli ni kwamba taarifa ikishapelekwa kwa spika basi spika ana uwezo wa kukubali ama kukataa hoja kuwasilishwa; kwa mujibu wa Katiba.
      Mkuu Kimbunga, hapo kwenye red. Hoja ikishakamilisha masharti ya kikatiba, hakuna kipengele chochte cha Katiba au Kanuni za Bunge kinachompa Spika uwezo mwingine wa kuikataa isifikishwe Bungeni.

      Kilichobaki ni mtoa hoja kuiondoa kama ameridhika na hatua zilizochukuliwa. Kumbuka sekeseke la G55 kudai Serikali ya Tanganyika ambapo licha ya Nyerere kupiga kelele Wabunge waliondoa hoja yao baada ya Zanzibar kujitoa kwenye OIC na wakaja na hoja nyingine mpya kabisa ya kura ya maoni.

      Spika akijipa uwezo usio ndani ya katiba, basi anajitakia matatizo yeye mwenyewe ya kukiuka katiba. Kumbuka aliyapata matatizo haya alipodanganya kuwa Tundu Lissu kashtakiwa kwa mauaji akasamehewa halafu ajitumbukize kwa jingine.

      Kosa la kuvunja katiba ni kosa la uhaini ambao hauna mjadala unatakiwa utoke kwenye kiti ulichokalia kwani kiapo chako ilikuwa ni kulinda katiba na si kuivunja.
      .."ni heri Dr. Willibrod Slaa ashinde na aingie Ikulu, kuliko Tundu Lissu kushinda ubunge na kuingia Bungeni"......Jakaya Mrisho Kikwete, Oct. 2010.

    13. #11
      Nikupateje's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2009
      Posts : 855
      Rep Power : 966
      Likes Received
      544
      Likes Given
      601

      Default Re: Bado Mizengo Pinda (PM) hajanusurika kuondoka madarakani. Hoja ya Zitto imeongezeka uthamani

      Quote By oyaoya
      Mkuu, zipo tetesi WM aliwasilisha hoja ya kuwawajibisha mawaziri na watendaji husika kabla, (mbona hujaweka kwny hizo stages?) ikajibiwa "ni upepo tu, utapita"
      Wakuu, ikumbukwe si ishu zote za kiutendaji serikalini zinaanikwa hadharani, hivyo kinadharia (km ulivyowasilisha) hoja ya Zitto itatimizwa kwa kuwawajibisha wahusika kwa kuwa ndiyo lengo kuu la hoja na si kumwajibisha WM kwa kuwa yeye mwenyewe Zitto alikiri anampenda MP na anamheshimu isipokuwa wahusika wakiwajibishwa watakuwa wamemuokoa MP.
      Mkuu, wasilisho langu humu JF si kwa mtizamo wa kinadharia bali ni kwa mujibu wa Katiba. Zitto hakuwasilisha hoja yake kwa mujibu wa tetesi au nadharia yake. Ingekuwa ni nadharia basi hoja yake ingetupiliwa mbali dakika ileile ilipopokelewa.

      Kinachosubiriwa sasa ni siku 14 zitimie kwa mujibu wa katiba na si kwa mujibu wa matakwa ya binadamu anayeitwa Anne Makinda, Jakaya Kikwete au wewe au mimi au hata Zitto mwenyewe.

      Kila kitu hadi hatua tuliyopo na na tunayoelekea ni kwa mujibu wa katiba.

      Kinachoweza kuiondoa hoja ile wakati wowote sasa au baadaye ni kitendo cha Zitto mwenyewe kwenda kuichoma isiendelee na utaratibu unaoelezwa ndani ya katiba.

      Ukilijua hilo, ukaijua katiba basi taona ni wapi tunaelekea kwa mujibu wa katiba na si kwa mujibu wa tetesi au mtizamo wa Zitto, mimi, wewe au yule.
      .."ni heri Dr. Willibrod Slaa ashinde na aingie Ikulu, kuliko Tundu Lissu kushinda ubunge na kuingia Bungeni"......Jakaya Mrisho Kikwete, Oct. 2010.

    14. #12
      Nikupateje's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2009
      Posts : 855
      Rep Power : 966
      Likes Received
      544
      Likes Given
      601

      Default Re: Bado Mizengo Pinda (PM) hajanusurika kuondoka madarakani. Hoja ya Zitto imeongezeka uthamani

      Quote By Greard
      nimejitahidi kusoma lkn siku nyingine jifunze kuandika thread fopi
      Hatusingiziwi tunapoambiwa watanzania tu wavivu wa kusoma vitabu.
      .."ni heri Dr. Willibrod Slaa ashinde na aingie Ikulu, kuliko Tundu Lissu kushinda ubunge na kuingia Bungeni"......Jakaya Mrisho Kikwete, Oct. 2010.

    15. #13
      Khakha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th July 2009
      Posts : 960
      Rep Power : 694
      Likes Received
      209
      Likes Given
      81

      Default

      Quote By Nikupateje
      Mkuu Kimbunga, hapo kwenye red. Hoja ikishakamilisha masharti ya kikatiba, hakuna kipengele chochte cha Katiba au Kanuni za Bunge kinachompa Spika uwezo mwingine wa kuikataa isifikishwe Bungeni.

      Kilichobaki ni mtoa hoja kuiondoa kama ameridhika na hatua zilizochukuliwa. Kumbuka sekeseke la G55 kudai Serikali ya Tanganyika ambapo licha ya Nyerere kupiga kelele Wabunge waliondoa hoja yao baada ya Zanzibar kujitoa kwenye OIC na wakaja na hoja nyingine mpya kabisa ya kura ya maoni.

      Spika akijipa uwezo usio ndani ya katiba, basi anajitakia matatizo yeye mwenyewe ya kukiuka katiba. Kumbuka aliyapata matatizo haya alipodanganya kuwa Tundu Lissu kashtakiwa kwa mauaji akasamehewa halafu ajitumbukize kwa jingine.

      Kosa la kuvunja katiba ni kosa la uhaini ambao hauna mjadala unatakiwa utoke kwenye kiti ulichokalia kwani kiapo chako ilikuwa ni kulinda katiba na si kuivunja.
      niko kwa mobile otherwise ningekutwangia LIKE ya nguvu mkuu.
      Nikupateje likes this.

    16. #14
      Saas's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2011
      Posts : 270
      Rep Power : 455
      Likes Received
      74
      Likes Given
      57

      Default Re: Bado Mizengo Pinda (PM) hajanusurika kuondoka madarakani. Hoja ya Zitto imeongezeka uthamani

      Mkuu nimefurahi kwa uchambuzi wako makini pia naona itakuwa haina maana kama Kikwete ata dissolve Baraza la Mawaziri halafu akamuacha Pinda kwenye post ya Uwaziri Mkuu huyu naye anapaswa kuondolewa

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...