Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo...

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 45
    1. #1
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,733
      Rep Power : 12925
      Likes Received
      4432
      Likes Given
      7462

      Default Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo...

      Katiba ni sheria mama hivyo huwezi kutumia sheria za kawaida zinazopitishwa na wabunge kwa maana ya simple majority ya wabunge waliokamilisha koram ya siku hiyo ili kurekebisha sheria ambayo ilipitishwa kwa theluthi mbili ya wabunge kwa kila sehemu ya Muungano.

      Nimepitia jinsi Kenya walivyorekebisha katiba yao nikaelimika ya kuwa wao kwanza walikuja na muswada wa marekebisho ya katiba yao na kuweka vifungu vya kuupa utaratibu wao wa uwazi na ukweli kwa maana shirikishi nguvu kisheria ambao ulitoa mamlaka ya kuanzisha sheria za kuirekebisha katiba. Zaidi ya theluthi mbili ya wabunge walipiga kura ya kuvikubali hivyo vifungu vya kikatiba na hivyo baada ya kuifanyia marekebisho katiba yao waliweza kuunda sheria za kuunga mkono marekebisho tajwa ya kikatiba.

      Sisi tumetanguliza mkokoteni kabla ya farasi kwa maana ya kuunda sheria za kawaida kabla ya kuirekebisha sheria mama yaani katiba iliyopo ili kutoa mwanya wa hizo sheria tulizozipitisha kuirekebisha katiba ziwe hazikiuki utaratibu wa kikatiba wa kuirekebisha katiba tajwa.

      Matokeo yake sheria za marekebisho ya katiba zinapingana na muhimili wa kikatiba na ndiyo maana mchakato wake unaonekana ni batili kwa sababu haujatajwa ndani ya katiba iliyopo, hauna ushirikishi na unalenga kuzima kiu ya mabadiliko ya kweli ya kikatiba.

      Tusisahau JK and Co are mere turncoats..............si ccm manifesto au hata ngonjera za JK wakati wa kutuomba kipindi cha pili waliaahidi katiba mpya..................kwa hiyo hivi sasa wanaharakisha ili kuzima kiu ya kweli kwa kutuletea hili igizo la tasnia ya filamu babaishi.........

      Wengi ya wanaopinga sheria hii ya marekebisho ya katiba wamejikita zaidi katika kukosoa baadhi ya vifungu vyake wakati ulaini wa kufanya hivyo ni kuangalia katiba iliyopo mbona haitoi fursa za marekebisho tajwa kwa kuhusisha vyombo nje ya Bunge la Jamhuri ya Muungano?

      Mfano tu, uhalali wa hiyo tume kikatiba unatoka wapi? Haijatajwa ndani ya katiba iliyopo sasa inapata wapi uhalali wa kukusanya maoni ya kurekebisha katiba iliyopo? Ilipaswa kwanza katiba iliyopo itoe uhalali wa utaratibu huu mpya wa kutumia tume na hata hayo mabunge mawili katika kuipitisha katiba tajwa baada ya kufanyiwa marekebisho ambayo yataungwa mkono na theluthi mbili za wabunge wa pande mbili za Muungano.

      Haya hayajafanyika kwa sababu JK na wababaishi wenzie wanajua kabisa ndani ya nafsi zao ya kwamba hawana uhalali bungeni wa kupitisha utaratibu walioutumia kwa maana hawawezi kupata kuungwa mkono na theluthi mbili za wabunge na hivyo wakatafuta njia ya mkato ya kuanzisha mchakato wa kurekebisha katiba iliyopo bila ya kuzingatia katiba yetu imeweka utaratibu upi wa kuirekebisha na kwa kufanya vinginevyo wakawa wamekuja na sheria tajwa ambayo inakinzana na katiba iliyopo................huu ni ukiukwaji wa katiba iliyopo............

      Katiba iliyopo inatoa mwanya wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa tanzania kurekebisha katiba iliyopo lakini tume, mabunge ya pande mbili za Muungano na hata kura ya maoni tajwa havijatajwa.........

      Nionavyo JK na vyama vya upinzani wanafikiri ya kuwa.................the ends can justify the means.........and vice versa......."they are dead wrong"..............well keeping the politics involved at bay I can confidently argue that this constitutional process is futile abinitio..........................badi lisha katika katiba iliyopo vifungu kwanza ili ujipe mamlaka ya kuirekebisha katiba iliyopo..........acheni kutafuta njia za mkato tena za panya buku kuirekebisha katiba iliyopo...................mwishowe suala hili itabidi lifike mahakama kuu ili iamue kama kweli Bunge lina uwezo wa kikatiba wa kuunda sheria za kawaida tu.........ambazo zahitaji simple majority ya wabunge waliohudhuria kikao kile ili mradi koram tu itimie na kupitisha sheria ya kuinyambulisha katiba iliyopo ambayo ilipitishwa kwa theluthi mbili ya wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama siyo ukiukwaji wa katiba wa wazi kabisa..................?????? ????????????

      Longa maoni yako, pia........................... ....utusaidie kutafuta sheria bora na ambazo zitahakikishia kila mtanzania maisha bora na wala siyo hizi ngonjera tupu.........

      ENGLISH VERSION AVAILABLE TOO........


      THE HYPOCRISY OF ENACTING A NEW CONSTITUTION.


      For ccm and president kikwete, it is easier to expose their hypocrisy but with the opposition it is all a different gameplan altogether to do it! Neither did the ccm manifesto of 2010 nor did Kikwete campaign trail of the same year hinted of a political will to rewrite a new constitutional order and panning out of this both CCM and Kikwete are turncoats as far as this constitutional process is concerned. Both CCM and Kikwete embraced a new constitutional process just to stay relevant in our political terrain but have neither the determination nor the political will to bequeath to us a well meaning constitution. But the opposition ranks can easily deceive many if you have been keen at following the ear deafening decibels generated by them. To their credit some opposition parties had garnished a quest for a new constitutional order into their manifesto and made that an election issue, too. After a bungled 2010 election where the real winner of presidential race was flashed out by unjust electoral system well oiled by the government in power through NEC (a national electoral body carefully handpicked by an incumbent president to do him a favour and announce him as a president –elect) and TISS ( an intelligence national body that is notorious at rigging all our post-one party elections since 1995), the opposition went berserk demanding a new constitutional order that will assure them people’s power that was perceived stolen from them by the treacherous electoral terrain.




      On their part, ccm through ministerial outbursts the impression we were getting was that the effort to rewrite the constitution was too costly and an exercise in futility. But ccm; seeing that it was getting the scissors whether from the streets or from the vociferous media waves, decided to cave in, in a manner that will protect the interests of the status quo ante. First ccm avoided to follow the law where in the hitherto constitution only the house has the power to effect the changes it deems fit. The problem for ccm were multifarious in many fronts: First almost one third of members of the House belong to the opposition bench and a number of young ccm MPs who refuse to kowtow the established party position is growing in line with the public opinion. Under this new political complexion, ccm mandarins felt insecure to follow the constitution in enacting the law that will guide the whole constitutional changing process.




      According to Rev. Mtikila v. Attorney General Case urging for independent candidates, the full bench of the Appeals court made it clear that it is only the House that has the legal power to change the constitution and if the process clearly laid down in the constitution was not followed the courts could be called to interfere and rectify the illegalities. But now ccm led constitutional process has defied the highest court of the land when it embarked to enact an act of parliament that has vitiated the constitutional onus of the House to rewrite the constitution! Out of this, unconstitutional creatures such as the presidential commission empowered to collate constitutional views, two Houses of Isles and of the United Republic of Tanzania let alone referendum leeway were enacted to confuse the electorate that we are on the right track to deliver a new order while the concomitant order was only being hacked to receive a cosmetic facelift.



      Parliament has no powers to incorporate or delegate her constitutional authority in the existing constitution and by extension cannot seek solace via a simple majority voting process to revoke what the House has enacted in the constitution through a two third majority. The solution to this archaic encroachment to the existing constitution under frivolous excuses that the ends can justify the means is out right wrong and we ought to ask the constitutional court to rectify these colossal anomalies via court injunctions pending a final determination of the main constitutional dispute.
      Last edited by Rutashubanyuma; 26th April 2012 at 13:45.
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    2. RukaaJuu Final

    3. #2
      Mvaa Tai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th August 2009
      Location : Ngudu, Mwanza
      Posts : 3,448
      Rep Power : 1187
      Likes Received
      1425
      Likes Given
      929

      Default Re: Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo............

      Quote By Rutashubanyuma
      Katiba ni sheria mama hivyo huwezi kutumia sheria za kawaida zinazopitishwa na wabunge kwa maana ya simple majority ya wabunge waliokamilisha koram ya siku hiyo ili kurekebisha sheria ambayo ilipitishwa kwa theluthi mbili ya wabunge kwa kila sehemu ya Muungano.

      Nimepitia jinsi Kenya walivyorekebisha katiba yao nikaelimika ya kuwa wao kwanza walikuja na muswada wa marekebisho ya katiba yao na kuweka vifungu vya kuupa utaratibu wao wa uwazi na ukweli kwa maana shirikishi nguvu kisheria ambao ulitoa mamlaka ya kuanzisha sheria za kuirekebisha katiba. Zaidi ya theluthi mbili ya wabunge walipiga kura ya kuvikubali hivyo vifungu vya kikatiba na hivyo baada ya kuifanyia marekebisho katiba yao waliweza kuunda sheria za kuunga mkono marekebisho tajwa ya kikatiba.

      Sisi tumetanguliza mkokoteni kabla ya farasi kwa maana ya kuunda sheria za kawaida kabla ya kuirekebisha sheria mama yaani katiba iliyopo ili kutoa mwanya wa hizo sheria tulizozipitisha kuirekebisha katiba ziwe hazikiuki utaratibu wa kikatiba wa kuirekebisha katiba tajwa.

      Matokeo yake sheria za marekebisho ya katiba zinapingana na muhimili wa kikatiba na ndiyo maana mchakato wake unaonekana ni batili kwa sababu haujatajwa ndani ya katiba iliyopo, hauna ushirikishi na unalenga kuzima kiu ya mabadiliko ya kweli ya kikatiba.

      Tusisahau JK and Co are mere turncoats..............si ccm manifesto au hata ngonjera za JK wakati wa kutuomba kipindi cha pili waliaahidi katiba mpya..................kwa hiyo hivi sasa wanaharakisha ili kuzima kiu ya kweli kwa kutuletea hili igizo la tasnia ya filamu babaishi.........

      Wengi ya wanaopinga sheria hii ya marekebisho ya katiba wamejikita zaidi katika kukosoa baadhi ya vifungu vyake wakati ulaini wa kufanya hivyo ni kuangalia katiba iliyopo mbona haitoi fursa za marekebisho tajwa kwa kuhusisha vyombo nje ya Bunge la Jamhuri ya Muungano?

      Mfano tu, uhalali wa hiyo tume kikatiba unatoka wapi? Haijatajwa ndani ya katiba iliyopo sasa inapata wapi uhalali wa kukusanya maoni ya kurekebisha katiba iliyopo? Ilipaswa kwanza katiba iliyopo itoe uhalali wa utaratibu huu mpya wa kutumia tume na hata hayo mabunge mawili katika kuipitisha katiba tajwa baada ya kufanyiwa marekebisho ambayo yataungwa mkono na theluthi mbili za wabunge wa pande mbili za Muungano.

      Haya hayajafanyika kwa sababu JK na wababaishi wenzie wanajua kabisa ndani ya nafsi zao ya kwamba hawana uhalali bungeni wa kupitisha utaratibu walioutumia kwa maana hawawezi kupata kuungwa mkono na theluthi mbili za wabunge na hivyo wakatafuta njia ya mkato ya kuanzisha mchakato wa kurekebisha katiba iliyopo bila ya kuzingatia katiba yetu imeweka utaratibu upi wa kuirekebisha na kwa kufanya vinginevyo wakawa wamekuja na sheria tajwa ambayo inakinzana na katiba iliyopo................huu ni ukiukwaji wa katiba iliyopo............

      Katiba iliyopo inatoa mwanya wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa tanzania kurekebisha katiba iliyopo lakini tume, mabunge ya pande mbili za Muungano na hata kura ya maoni tajwa havijatajwa.........

      Nionavyo JK na vyama vya upinzani wanafikiri ya kuwa.................the ends can justify the means.........and vice versa......."they are dead wrong"..............well keeping the politics involved at bay I can confidently argue that this constitutional process is futile abinitio..........................badi lisha katika katiba iliyopo vifungu kwanza ili ujipe mamlaka ya kuirekebisha katiba iliyopo..........acheni kutafuta njia za mkato tena za panya buku kuirekebisha katiba iliyopo...................mwishowe suala hili itabidi lifike mahakama kuu ili iamue kama kweli Bunge lina uwezo wa kikatiba wa kuunda sheria za kawaida tu.........ambazo zahitaji simple majority ya wabunge waliohudhuria kikao kile ili mradi koram tu itimie na kupitisha sheria ya kuinyambulisha katiba iliyopo ambayo ilipitishwa kwa theluthi mbili ya wabunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama siyo ukiukwaji wa katiba wa wazi kabisa..................?????? ????????????

      Longa maoni yako, pia........................... ....utusaidie kutafuta sheria bora na ambazo zitahakikishia kila mtanzania maisha bora na wala siyo hizi ngonjera tupu.........
      Tatizo la nchi yetu kila kitu kinaendeshwa kishkaji tuu, ninaamini Kikwete angeajiri washauri makini pale Ikulu ujinga wote huu usingeweza kutokea, kwasababu kila kitu kinafanywa kimtandao bila kujali sifa ndo matokeo yake haya. Nchi hii vichwa ni vingi sana tatizo siyo wanamtandao.
      Rutashubanyuma likes this.
      Mnang'oa meno ya Tembo ili mukayauze, mnang'oa meno na Kucha za Watanzania wasio na hatia ili iweje?

    4. #3
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,733
      Rep Power : 12925
      Likes Received
      4432
      Likes Given
      7462

      Default Re: Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo............

      Tatizo la nchi yetu kila kitu kinaendeshwa kishkaji tuu, ninaamini Kikwete angeajiri washauri makini pale Ikulu ujinga wote huu usingeweza kutokea, kwasababu kila kitu kinafanywa kimtandao bila kujali sifa ndo matokeo yake haya. Nchi hii vichwa ni vingi sana tatizo siyo wanamtandao.
      Ezan unaamini kuwa ni kishikaji tu?
      Huoni ya kuwa hawa mafisadi wana malengo fulani ya kupitisha mambo yao kinyume na utaratibu wa kikatiba baada ya kuona ya kuwa hawana theluthi mbili za wabunge Bungeni kuhalalisha uozo wao?.........mimi ninaamini ya kuwa wanafanya kwa makusudi mazima ili kufnikisha dhamira zao......
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    5. #4
      Mpita Njia's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd March 2008
      Posts : 6,703
      Rep Power : 3255
      Likes Received
      984
      Likes Given
      754

      Default Re: Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo............

      Nakumbuka huo utaratibuw a kuanza kurekebisha katiba kwanza uloishawahi kupendekezwa na Mnyika lakini wakamuona chizi. Kwa hakika, tunachokifanjya kinaweza kugeuka kuwa shubiri huko mbele ya safari kwa kutozingatia matakwa ya kisheria kama haya. Kuna baadhi ya watu wameshaanza kuloichukulia suala hili kisisasa zaidi. Na tatizo, wananchi wengi wa Tanzania wanaburuzwa tu bila kuelewa hasa kinachotokea ni nini.
      Mathalani, kama kweli wana nia ya kuwapa watu uhuru wa kuandika katiba wanayoitaka, kwa nini waweke masharti, kwa mfanop, msizungumze kuhusu kuuvunja Muungano! Kama hisia za watu ni kutoutaka Muungano, hivi watatoa maoni gani ya maana ambayo yataifanya katiba itokane na maoni yao wakati yale wanayoyafikiria wao wamekatazwa wasiyayaseme?
      Rutashubanyuma and Mukhabarat like this.
      I assume full responsibility for my actions, except the ones that are someone else's fault.

    6. #5
      Fredrick Sanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th January 2011
      Location : Kijitonyama
      Posts : 2,982
      Rep Power : 2590
      Likes Received
      637
      Likes Given
      776

      Default Re: Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo............

      Inatia uchungu, inauma, inasikitisha, inadhalilisha lakini yetu macho.
      Rutashubanyuma likes this.
      We shall overcome, righteousness shall always prevail.

    7. Miaka 50

    8. #6
      Mungi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 23rd September 2010
      Location : Hapa!!!
      Posts : 10,177
      Rep Power : 24273
      Likes Received
      4679
      Likes Given
      2297

      Default Re: Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo............

      Quote By Rutashubanyuma
      Ezan unaamini kuwa ni kishikaji tu?
      Huoni ya kuwa hawa mafisadi wana malengo fulani ya kupitisha mambo yao kinyume na utaratibu wa kikatiba baada ya kuona ya kuwa hawana theluthi mbili za wabunge Bungeni kuhalalisha uozo wao?.........mimi ninaamini ya kuwa wanafanya kwa makusudi mazima ili kufnikisha dhamira zao......
      Ruta,
      Hii ni zaidi ya ushkaji, Rais kama Mkuu wa nchi ndiye anayetakiwa kuunda tume ya marekebisho ya Katiba.
      Rais huyo huyo ni Mwenyekiti wa chama tawala ambayo inafaidika na ubovu wa katiba tuliyonayo
      Rais huyo huyo ndiyo chanzo cha ufisadi na ubadirifu mkubwa wa mali ya umma.

      Hapo usitarajie makubwa, na kilichotokea na kinachoendelea ni kuwa mazingira yoyote ya marekebisho ya katiba yataipendelea serikali ya Mkulu.

      Kwa maoni yangu,
      Kwa kuwa serikali yetu imeamua kukumbatia dola kwa maana ya Jeshi ili wajilinde na nguvu ya wananchi, bado suala la marekebisho yoyote ya katiba au jambo lolote lenye manufaa kwa maslahi ya umma lipo mikononi mwa wananchi wa tanzania.
      Watanzania waandaliwe vya kutosha kuelewa nini wanafanyiwa na serikali iliyopo, waandaliwe elimu ya demokrasia, waandaliwe kutambua haki zao pamoja na mambo mengine.
      Baada ya hapo tulianzishe la kigeto geto kitaeleweka tu.
      Nguvu ya umma haijawahi kushindwa popote duniani, ni kiasi cha kuwaanda tu watu, na pia jeshi lielewe kuwa wanalipwa kwa kodi za watanzania wanaoonewa na kudhihakiwa na serikali ya ccm.

      Mungu Ibariki Tanzania
      Rutashubanyuma likes this.
      "Peace is not simply about the absence of violence. It is defined by the presence of fundamental liberties and the prevalence of economic opportunities."

    9. #7
      Kigarama's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd April 2007
      Location : Manzese kwa Mfuga Mbwa
      Posts : 2,359
      Rep Power : 16278
      Likes Received
      974
      Likes Given
      703

      Default Re: Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo...

      Hebu kwanza tujiulize sisi tunahitaji Katiba mpya au Uongozi mpya? Maana nimesikia mara nyingi ikisemwa "kama katiba ikirekebishwa, CCM lazima ishindwe".

      Mimi naungana Jenerali Ulimwengu kwamba tuchambue yale mambo ambayo wanasiasa wapenda madaraka wanayaona kwamba ndiyo "katiba" na tuyarekebishe na tuwaache wao wanagombania madaraka wakati sisi tunatafuta muafaka wa Kitaifa.

      Hoja kama tume huru ya Uchaguzi, mgombea huru (siyo binafsi), matokeo ya kura za Uraisi kuhojiwa mahakamani,haki ya kutangaza matokeo ya awali,jinsi ya kujiandikisha,kupiga,kuhesabu na kutangaza matokea ya uchaguzi ni mambo ambayo tunaweza hata kwa kutumia bunge hili hili tulilonalo tukayarekebisha na kuwapa "wanasiasa" wanachokitaka na sisi tukapata nafasi ya kutunga katiba mpya kwa manufaa ya nchi yetu.

      Eti kwa miezi kumi na nane tunatafuta muafaka wa kitaifa kwa taifa lililo na umri zaidi ya miaka 45, haya ni maskhara!!
      UKIDHANI WEWE SI MWENDAWAZIMU PIMA KWANZA UHUSIANO WAKO NA MACHIZI!!

    10. #8
      Mtambuzi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 29th October 2008
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 6,094
      Rep Power : 27014
      Likes Received
      8231
      Likes Given
      17325

      Default Re: Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo...

      Quote By Kigarama
      Hebu kwanza tujiulize sisi tunahitaji Katiba mpya au Uongozi mpya? Maana nimesikia mara nyingi ikisemwa "kama katiba ikirekebishwa, CCM lazima ishindwe".

      Mimi naungana Jenerali Ulimwengu kwamba tuchambue yale mambo ambayo wanasiasa wapenda madaraka wanayaona kwamba ndiyo "katiba" na tuyarekebishe na tuwaache wao wanagombania madaraka wakati sisi tunatafuta muafaka wa Kitaifa.

      Hoja kama tume huru ya Uchaguzi, mgombea huru (siyo binafsi), matokeo ya kura za Uraisi kuhojiwa mahakamani,haki ya kutangaza matokeo ya awali,jinsi ya kujiandikisha,kupiga,kuhesabu na kutangaza matokea ya uchaguzi ni mambo ambayo tunaweza hata kwa kutumia bunge hili hili tulilonalo tukayarekebisha na kuwapa "wanasiasa" wanachokitaka na sisi tukapata nafasi ya kutunga katiba mpya kwa manufaa ya nchi yetu.

      Eti kwa miezi kumi na nane tunatafuta muafaka wa kitaifa kwa taifa lililo na umri zaidi ya miaka 45, haya ni maskhara!!
      Well said.......................Na kikubw ana kuruhusiwa kwa wagombea binafsi.................
      Rutashubanyuma likes this.

    11. #9
      Entrepreneur's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th June 2011
      Posts : 911
      Rep Power : 586
      Likes Received
      479
      Likes Given
      153

      Default Re: Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo...

      Suala hili lilionekana mwanzo, na ninakumbuka hata kwenye kongamano la UDASA pale UDSM lilijadiliwa. Mh. Myika JJ alisema atapeleka hoja bungeni ili katiba ifanyiwe marekebisho kwanza kabla ya mchakato wa hii sheria ya mabadiliko kuanza kwani ukianza bila matakwa ya Kikatiba mchakato wote utakiuka katiba iliyopo kama wewe unavyosema.

      Cha kushangaza ni kwamba ile hoja imepotea kiajabu ajabu na hakuna mtu aliyejisumbua kuhoji huko Bungeni. Shukrani kwako kwa kuihoji huku uraian
      Last edited by Entrepreneur; 26th April 2012 at 11:31.
      Rutashubanyuma likes this.
      “The first method for estimating the intelligence of a ruler is to look at the men he has around him.” ― Niccolò Machiavelli, The Prince

    12. #10
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,733
      Rep Power : 12925
      Likes Received
      4432
      Likes Given
      7462

      Default Re: Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo...

      Nakumbuka huo utaratibuw a kuanza kurekebisha katiba kwanza uloishawahi kupendekezwa na Mnyika lakini wakamuona chizi. Kwa hakika, tunachokifanjya kinaweza kugeuka kuwa shubiri huko mbele ya safari kwa kutozingatia matakwa ya kisheria kama haya. Kuna baadhi ya watu wameshaanza kuloichukulia suala hili kisisasa zaidi. Na tatizo, wananchi wengi wa Tanzania wanaburuzwa tu bila kuelewa hasa kinachotokea ni nini.
      Mathalani, kama kweli wana nia ya kuwapa watu uhuru wa kuandika katiba wanayoitaka, kwa nini waweke masharti, kwa mfanop, msizungumze kuhusu kuuvunja Muungano! Kama hisia za watu ni kutoutaka Muungano, hivi watatoa maoni gani ya maana ambayo yataifanya katiba itokane na maoni yao wakati yale wanayoyafikiria wao wamekatazwa wasiyayaseme?
      kwa vile bunge limekataa kurekebisha katiba kuruhusu mchakato wa kuirekebisha katiba ukubalike basi ni mahakama tu ndiyo msuluhishi wa mwisho.............haiwezakni watu wakatafuta majibu mepesi kwa mswali magumu.......
      kibunda likes this.
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    13. #11
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,733
      Rep Power : 12925
      Likes Received
      4432
      Likes Given
      7462

      Default Re: Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo...

      Suala hili lilionekana mwanzo, na ninakumbuka hata kwenye kongamano la UDASA pale UDSM lilijadiliwa. Mh. Myika JJ alisema atapeleka hoja bungeni ili katiba ifanyiwe marekebisho kwanza kabla ya mchakato wa hii sheria ya mabadiliko kuanza kwani ukianza bila matakwa ya Kikatiba mchakato wote utakiuka katiba iliyopo kama wewe unavyosema.

      Cha kushangaza ni kwamba ile hoja imepotea kiajabu ajabu na hakuna mtu aliyejisubua kuhoji huko Bungeni. Shukrani kwako kwa kuihoji huku uraian
      twende mahakamani tusimamishe huu upuuzi wote khalafu wakajipange kwa upya kabisa................wajue TZ ina wenyewe
      kibunda likes this.
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    14. #12
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,733
      Rep Power : 12925
      Likes Received
      4432
      Likes Given
      7462

      Default Re: Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo...

      Well said.......................Na kikubw ana kuruhusiwa kwa wagombea binafsi.................
      maudhui ya kipi kiwepo kwenye katiba au kisiweko yaje baadaye kwanza utaratibu lazima uingizwe kwenye katiba kwanza........
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    15. #13
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,733
      Rep Power : 12925
      Likes Received
      4432
      Likes Given
      7462

      Default Re: Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo...

      Hebu kwanza tujiulize sisi tunahitaji Katiba mpya au Uongozi mpya? Maana nimesikia mara nyingi ikisemwa "kama katiba ikirekebishwa, CCM lazima ishindwe".

      Mimi naungana Jenerali Ulimwengu kwamba tuchambue yale mambo ambayo wanasiasa wapenda madaraka wanayaona kwamba ndiyo "katiba" na tuyarekebishe na tuwaache wao wanagombania madaraka wakati sisi tunatafuta muafaka wa Kitaifa.

      Hoja kama tume huru ya Uchaguzi, mgombea huru (siyo binafsi), matokeo ya kura za Uraisi kuhojiwa mahakamani,haki ya kutangaza matokeo ya awali,jinsi ya kujiandikisha,kupiga,kuhesabu na kutangaza matokea ya uchaguzi ni mambo ambayo tunaweza hata kwa kutumia bunge hili hili tulilonalo tukayarekebisha na kuwapa "wanasiasa" wanachokitaka na sisi tukapata nafasi ya kutunga katiba mpya kwa manufaa ya nchi yetu.

      Eti kwa miezi kumi na nane tunatafuta muafaka wa kitaifa kwa taifa lililo na umri zaidi ya miaka 45, haya ni maskhara!!
      kigarama uko sahihi.................wasisin gizie katiba mpya kukwepa kutekeleza majukumu yao.............ili kwenda uchaguzi ujao tunahitaji minimum refroms kama hizo ulizozitaja................... ..lakini la katiba mpya twende nalo polepole...............na dawa yao ni kuweka injunction utaratibu huu wote mahakamani hadi suala hili la kimsingi limepatiwa ufumbuzi.........
      Kigarama and kibunda like this.
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    16. #14
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,733
      Rep Power : 12925
      Likes Received
      4432
      Likes Given
      7462

      Default Re: Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo...

      Ruta,
      Hii ni zaidi ya ushkaji, Rais kama Mkuu wa nchi ndiye anayetakiwa kuunda tume ya marekebisho ya Katiba.
      Rais huyo huyo ni Mwenyekiti wa chama tawala ambayo inafaidika na ubovu wa katiba tuliyonayo
      Rais huyo huyo ndiyo chanzo cha ufisadi na ubadirifu mkubwa wa mali ya umma.

      Hapo usitarajie makubwa, na kilichotokea na kinachoendelea ni kuwa mazingira yoyote ya marekebisho ya katiba yataipendelea serikali ya Mkulu.

      Kwa maoni yangu,
      Kwa kuwa serikali yetu imeamua kukumbatia dola kwa maana ya Jeshi ili wajilinde na nguvu ya wananchi, bado suala la marekebisho yoyote ya katiba au jambo lolote lenye manufaa kwa maslahi ya umma lipo mikononi mwa wananchi wa tanzania.
      Watanzania waandaliwe vya kutosha kuelewa nini wanafanyiwa na serikali iliyopo, waandaliwe elimu ya demokrasia, waandaliwe kutambua haki zao pamoja na mambo mengine.
      Baada ya hapo tulianzishe la kigeto geto kitaeleweka tu.
      Nguvu ya umma haijawahi kushindwa popote duniani, ni kiasi cha kuwaanda tu watu, na pia jeshi lielewe kuwa wanalipwa kwa kodi za watanzania wanaoonewa na kudhihakiwa na serikali ya ccm.

      Mungu Ibariki Tanzania
      niaafiki na hii misimamo namna rahisi ya kuwashtua hawa wababaishaji ni kuwawekea court injunction hadi suala la kimsingi litakapopatiwa ufumbuzi.......
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    17. #15
      Entrepreneur's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th June 2011
      Posts : 911
      Rep Power : 586
      Likes Received
      479
      Likes Given
      153

      Default Re: Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo...

      Quote By Rutashubanyuma
      twende mahakamani tusimamishe huu upuuzi wote khalafu wakajipange kwa upya kabisa................wajue TZ ina wenyewe
      Naunga mkono hoja kwa asilimia 100.
      “The first method for estimating the intelligence of a ruler is to look at the men he has around him.” ― Niccolò Machiavelli, The Prince

    18. #16
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,733
      Rep Power : 12925
      Likes Received
      4432
      Likes Given
      7462

      Default Re: Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo...

      Suala hili lilionekana mwanzo, na ninakumbuka hata kwenye kongamano la UDASA pale UDSM lilijadiliwa. Mh. Myika JJ alisema atapeleka hoja bungeni ili katiba ifanyiwe marekebisho kwanza kabla ya mchakato wa hii sheria ya mabadiliko kuanza kwani ukianza bila matakwa ya Kikatiba mchakato wote utakiuka katiba iliyopo kama wewe unavyosema.

      Cha kushangaza ni kwamba ile hoja imepotea kiajabu ajabu na hakuna mtu aliyejisubua kuhoji huko Bungeni. Shukrani kwako kwa kuihoji huku uraian
      tuifufue hoja tajwa katika mahakama kuu hawa akina mnyika wao ni nguvu ya soda tu..........kuna maana gani ya kuanzisha hoja khalafu ushindwe kuitetea mahakamani kama unaona bungeni umeelemewa?
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    19. #17
      Mpita Njia's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd March 2008
      Posts : 6,703
      Rep Power : 3255
      Likes Received
      984
      Likes Given
      754

      Default Re: Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo...

      Quote By Kigarama
      Hebu kwanza tujiulize sisi tunahitaji Katiba mpya au Uongozi mpya? Maana nimesikia mara nyingi ikisemwa "kama katiba ikirekebishwa, CCM lazima ishindwe".

      Mimi naungana Jenerali Ulimwengu kwamba tuchambue yale mambo ambayo wanasiasa wapenda madaraka wanayaona kwamba ndiyo "katiba" na tuyarekebishe na tuwaache wao wanagombania madaraka wakati sisi tunatafuta muafaka wa Kitaifa.

      Hoja kama tume huru ya Uchaguzi, mgombea huru (siyo binafsi), matokeo ya kura za Uraisi kuhojiwa mahakamani,haki ya kutangaza matokeo ya awali,jinsi ya kujiandikisha,kupiga,kuhesabu na kutangaza matokea ya uchaguzi ni mambo ambayo tunaweza hata kwa kutumia bunge hili hili tulilonalo tukayarekebisha na kuwapa "wanasiasa" wanachokitaka na sisi tukapata nafasi ya kutunga katiba mpya kwa manufaa ya nchi yetu.

      Eti kwa miezi kumi na nane tunatafuta muafaka wa kitaifa kwa taifa lililo na umri zaidi ya miaka 45, haya ni maskhara!!
      Waache wacheze makida, wakileta mchezo tutakutana kwenye kura ya maoni
      Rutashubanyuma likes this.
      I assume full responsibility for my actions, except the ones that are someone else's fault.

    20. #18
      Rutashubanyuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th September 2010
      Location : Arusha
      Posts : 38,733
      Rep Power : 12925
      Likes Received
      4432
      Likes Given
      7462

      Default Re: Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo...

      Waache wacheze makida, wakileta mchezo tutakutana kwenye kura ya maoni
      kuraya maoni haijatajwa kwenye katiba kwa hiyo tukiwaruhusu kufika huko tutakuwa tunahalalisha ukiukwaji wa sheria na hiyo katiba itakuwa ni batili kutokana na ubatili wa utaratibu uliotumika......
      John 14:14 " If you ask anything in My Name, I will do it"

      John 14:15 "If you love Me, keep My commandments."

    21. #19
      Mukhabarat's Avatar
      Member Array
      Join Date : 9th March 2012
      Posts : 83
      Rep Power : 379
      Likes Received
      23
      Likes Given
      6

      Default Re: Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo...

      kwa sheria ya mabadiliko ya katiba kukataza wananchi wasijadili kuhusu kuwepo kwa muungano au la ila kwa nia ya kuuboresha tu huko ni kuminya uhuru wa kutoa maoni, na sheria hii inalazimisha kuwepo kwa muungano na kuwepo kwa serikali ya mapinduzi zanzibar, kwa hiyo hapo mwananchi anabakia na maoni ya serikali tatu au mbili kama zilivyo sasa, maana yake ni kuyaweka jela mawazo ya watu kwa kuwachagulia mambo ya kusema badala ya kuwaacha waseme wanavyotaka! serikali inaogopa nini kuwapa watu uhuru wa kutoa mawazo yao bila kuwapangia cha kusema? je kweli katiba hii itakuwa na haki ya kuitwa imeandikwa na wananchi wenyewe? tatizo ni nini iwapo mwisho wa siku watu watapiga kura ya maoni, mchakato huu ni sawa na mwalimu kuwachagulia wanafunzi topics 4 kutoka kwenye syllabus yenye topics 10 baadae anawapa mtihani kutokana na hizo topics 4 alizowafundisha halafu wakifaulu huo mtihani aseme wamefuzu kumbe si kweli kwa sababu ili wafuzu walitakiwa wawe na uelewa wa topics zote kumi za kwenye mtaala huo.
      Katiba mpya inaweza ikaja lakini naamini haitotatua sintofahamu ya muungano ndo maana mimi naungana na wazanzibari wanaotaka kwanza kura ya maoni kuhusu muungano halafu ndo tujadili katiba kwa maana matokeo ya kura ya maoni ndo yatakayoamua kama tunahitaji katiba ya muungano au vinginevyo.
      NB: KASHESHE ZA MUUNGANO ZITAENDELEA KUWEPO
      Rutashubanyuma likes this.

    22. #20
      Dark City's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th October 2008
      Location : Roaming
      Posts : 11,568
      Rep Power : 23554
      Likes Received
      6987
      Likes Given
      11340

      Default Re: Sheria ya marekebisho ya katiba imekiuka katiba iliyopo...

      Ta Ruta,


      Binafsi nilishasema kuwa JK na serikali yake hawana nia njema kwenye suala la katiba mpya. Toka mwanzo, Waziri Kombani na AG walikuwa wanajikanyaga kwani hawakujua kitu gani wananchi wanataka. Hata JK mwenyewe hakujua pia na alikiri hayo mbele ya vingozi wa CHADEMA.

      Hata Wabunge walipoptisha mswada wa hii sheria kwa mara ya kwanza, nilionga na baadhi yao na kuwaeleza kuwa wangetumia busara kidogo kujielimisha ni kitu gani hasa wananchi wanahitaji. Badala yake, viongozi wetu wameendekeza ushabiki.

      Kwa hapa tulipofika, tunahitaji akina Mtikila kuchukua hatua ili kutuepusha na huu usanii ambao unaweza kutuletea matatizo makubwa huko mbele ya safari.
      Rutashubanyuma likes this.
      "WE ALWAYS DON'T CHANGE UNTIL THE COST OF STAYING THE SAME EXCEEDS THE COST OF CHANGE....LOOKING BEYOND THE 31 OKTOBA 2010 LANDMARK"

      Retired Maj Gen DC (1947)...[email protected]

    Page 1 of 3 123 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...