Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Zilizokuwa Dawa za CCM, Ndizo Sumu Zinazoiua CCM!

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 59
    1. #1
      English Learner's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st January 2012
      Location : Inside the Laptop
      Posts : 254
      Rep Power : 804
      Likes Received
      269
      Likes Given
      198

      Default Dawa za CCM, Zimegeuka Sumu!

      Iwapo unaumwa, njia pekee ili upate kupona lazima upate matibabu. Na kwa wale wa imani za kileo matibabu yao ni kwa njia ya uponywaji. Lakini pia, wakati mwingine si mpaka uumwe. Unaweza kutumia dawa ili kujikinga na maradhi kabla hata hayajakufika. Kinga ni bora kuliko tiba, na pia ni vema kuswali kabla hujaswaliwa!

      Naamu! CCM inayoongoza Serikali isiyokuwa na dini, nayo toka kale inazo dawa na sindazo zake za kinga na matibabu. Miongoni mwa dawa na sindano hizo ni UMOJA wa Kitaifa, UADILIFU wa Viongozi, CHEO kama DHAMANA, na UONGOZI Bora wa Watu Kujiletea Maendeleo yao Wenyewe. Vifuko vya dawa hizi, vingi vilijumuhiswa na kufanywa kifurushi kimoja cha dawa iitwayo AZIMIO la Arusha.

      Taifa chini ya CCM lilipougua ukabila na udini, viongozi wa CCM walifanya utabibu haraka wakitumia dawa iitwayo UMOJA wa Kitaifa, rushwa na ubadhilifu wa mali ya umma punde tu ulipoibuka, wale wote waliobainika mara moja walidungwa sindano ya UADILIFU. Na mwenendo wa Serikali katika kupambana na maadui (Ujinga, Umaskini, na Maradhi) wa Taifa ilikuwa si kutembeza bakuli la kuomba misaada toka Ulaya na Amerika bali kuwatumia VIONGOZI Bora kuwaunganisha wananchi katika kuchangia vipawa, ujuzi, na mali katika kujiletea maendeleo yao kwa kutumia rasilimali za nchi yao. Na hii ndiyo ilikuwa dhana kuu ya UJAMAA na KUJITEGEMEA.

      Lakini la ajabu, leo hii, CCM ndiyo kinara wa kuchua dawa ya kubomoa UMOJA wa Kitaifa kwa kuendekeza Udini na Ukabila. Tumelishuhudia hili wakati wa Uchaguzi Mkuu na limejirudia tena katika Chaguzi Ndogo za Igunga na Arumeru. Tumeona jinsi CCM ya leo inavyoshangilia wasio-WAADILIFU kuwadunga sindano za mauti Wanaopinga RUSHWA na UBADHILIFU wa Mali za Umma. Na kubwa zaidi sote tu mashahidi, kwa CCM ya leo Cheo si DHAMANA bali BIDHAA inayonunuliwa na Matajiri ili wafanikishe mambo yao kupitia migongo ya Wapiga kura.

      CCM imefanikiwa kwa muda kugeuza matumizi ya dawa zake bila kudhurika. Habari njema ni kwamba, dawa zote sasa zimefikia ukomo wa matumizi na zimegeuka sumu tena kali. Kwa sasa, UMOJA unaanzishwa na Wananchi wenyewe kuikabili CCM. Wananchi hawakubali tena kugawanywa katika makundi ya kidini wala kikabila ili CCM ipenye kuwatawala tena. Wananchi wanawataka na wanawajua watu waadilifu. Na wanapojitokeza wanaogawa RUSHWA, wananchi wanaipokea na kuila lakini haibatilishi maamuzi yao yaliyo sahihi moyoni. Au wanaitumia hiyo pesa ya RUSHWA kumchangia mtu muadilifu wampendaye ili afikie hatma ya kuwa kiongozi wao. Hili limethibitika katika Uchaguzi Mkuu na limejirudia tena hivi karibuni huko Arumeru Mashariki. Kiongozi ambaye Wananchi wanamhitaji ni yule atakaye waongoza katika kutetea HAKI zao na kuwaunganisha KUJILETEA maendeleo. Kitendo alichokifanya Kilema mmoja huko Mwanza, cha kutoa Kuku wake wa Pasaka anadishwe katika Harambee ya kuchangia madawati iliyoongozwa na Mbunge Wenje ili naye achangie watoto kupata mazingira mazuri ya kusomea ni fundisho tosha kwa CCM na watoa RUSHWA.

      Ili CCM ipone na dhahama ya sumu inayoendelea kuenea mwilini mwake, lazima kwanza itapishwe na kukamuliwa sumu zote (Ubaguzi, Rushwa, Ubadhilifu, Viongozi Uchwara/wafanyabiashara, n.k) na kisha ianze upya matumizi ya dawa zake za awali (UMOJA, UADILIFU, UONGOZI BORA, CHEO kama DHAMANA). Ni makosa ya makadirio ya kisiasa kwa CCM kufikiria jinsi itakavyobaki madarakani hapo 2015. Hili jambo haliwezekani bila matumizi makubwa yaliyopitiliza ya dola yatakaambatana na umwagaji wa damu isiyo na hatia. Kadirio sahihi kwa CCM ni kufikiri nini itakuwa “Fall-Back Position” hapo 2015 na nini kiandaliwe ili baada ya hapo warudi tena madarakani ndani ya miaka mitano (5). Ni rahisi kwa CCM kurudi ndani ya muda mfupi namna hii kwa sababu, pamoja na maandalizi yanayoendelea kwenye vyama vya upinzani kushika dola, bado ni yatima wa mipango na rasilimali watu makini wa kutekeleza na kukidhi matumaini ya Wananchi ndani ya kipindi kifupi cha miaka mitano (5). Vyama vya Upinzani vimefanya na vinaendelea kufanya makosa makubwa sana kwa kuacha wananchi kuweka matumaini makubwa kupitiliza juu ya nini watakifanya wakiingia madarakani. Wamewaaminisha wanancnhi kwamba kile walichoshindwa CCM kwa miaka 54 (hapo 2015) wao watakifanikisha ndani ya miaka mitano! Kwa kosa hili, wategemee kuchukiwa haraka sana na kupingwa na wananchi hao hao watakaokuwa wamewapa ushindi. Ebu nisitoke ndani ya mada maana hii tayari ni mada nyingine kabisa.

      Nakutakia tafakuri njema.
      Last edited by English Learner; 1st June 2012 at 20:23.

    2. Miaka 50

    3. #2
      STK ONE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2011
      Location : Mpanda, Katavi Region
      Posts : 628
      Rep Power : 499
      Likes Received
      176
      Likes Given
      44

      Default Re: Zilizokuwa Dawa za CCM, Ndizo Sumu Zinazoiua CCM!

      well said, but at the end I don't think if you are right (my interpretation and analysis), but see, we have given ccm and its leaders about 50 years to rule this country instead of LEADING people to reach their EXPECTATIONS AND their dreams. Throughout all these 50 years we have seen our country going backward instead of going forward. Refer the number of industries we had in 1980s and the number of industries we have now, refer the number of unemployed people in 1980s and now days. Then see how poverty rate have increased, inflation, quality of education, number of failure students, poor health services and so many problems. All these show that we are Moving backwards instead of forward...

      Really we need changes...these changes can only be brought about by changing the ruling party. Even though we can do this, but we don't have to EXPECT dramatic changes to be brought by new party which will replace CCM. Changes can not be brought within 5 years. In normal circumstances, its impossible to build all the foundations of our nations which have been destructed by CCM within 5 years. So we have to give time the new party so that we can experience the difference....
      THANK YOU...M4C FOREVER....KEEP ON KILLING CCM AND ALL ITS MEMBER.....GOD BLESS US.

      TOGETHER WE CAN BRING THE CHANGES WE NEED.....YES WE CAN.....GOD BLESS CDM..AND AL OF US...
      Lyimo and English Learner like this.
      HERI UKIMWI KULIKO CCM....BUT THE END IS ON THE WAY.....

    4. #3
      English Learner's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st January 2012
      Location : Inside the Laptop
      Posts : 254
      Rep Power : 804
      Likes Received
      269
      Likes Given
      198

      Default Re: Dawa za CCM, Zimegeuka Sumu!

      STK ONE,
      Thank you for your insightful contribution. What I'm sure of is that change is inevitable. And what I'm guessing is the magnitude and time within which that changes are expected to be vividly realized. However, that change expected under fortcoming regime are unknowingly miscalculated or deliberately hyped. Lets wait and see.
      Last edited by English Learner; 1st June 2012 at 20:27.

    5. #4
      English Learner's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st January 2012
      Location : Inside the Laptop
      Posts : 254
      Rep Power : 804
      Likes Received
      269
      Likes Given
      198

      Default

      @
      This is a good stuff for you
      I wrote it in Swahili, easily to comprehend!

      Quote By English Learner
      Iwapo unaumwa, njia pekee ili upate kupona lazima upate matibabu. Na kwa wale wa imani za kileo matibabu yao ni kwa njia ya uponywaji. Lakini pia, wakati mwingine si mpaka uumwe. Unaweza kutumia dawa ili kujikinga na maradhi kabla hata hayajakufika. Kinga ni bora kuliko tiba, na pia ni vema kuswali kabla hujaswaliwa!

      Naamu! CCM inayoongoza Serikali isiyokuwa na dini, nayo toka kale inazo dawa na sindazo zake za kinga na matibabu. Miongoni mwa dawa na sindano hizo ni UMOJA wa Kitaifa, UADILIFU wa Viongozi, CHEO kama DHAMANA, na UONGOZI Bora wa Watu Kujiletea Maendeleo yao Wenyewe. Vifuko vya dawa hizi, vingi vilijumuhiswa na kufanywa kifurushi kimoja cha dawa iitwayo AZIMIO la Arusha.

      Taifa chini ya CCM lilipougua ukabila na udini, viongozi wa CCM walifanya utabibu haraka wakitumia dawa iitwayo UMOJA wa Kitaifa, rushwa na ubadhilifu wa mali ya umma punde tu ulipoibuka, wale wote waliobainika mara moja walidungwa sindano ya UADILIFU. Na mwenendo wa Serikali katika kupambana na maadui (Ujinga, Umaskini, na Maradhi) wa Taifa ilikuwa si kutembeza bakuli la kuomba misaada toka Ulaya na Amerika bali kuwatumia VIONGOZI Bora kuwaunganisha wananchi katika kuchangia vipawa, ujuzi, na mali katika kujiletea maendeleo yao kwa kutumia rasilimali za nchi yao. Na hii ndiyo ilikuwa dhana kuu ya UJAMAA na KUJITEGEMEA.

      Lakini la ajabu, leo hii, CCM ndiyo kinara wa kuchua dawa ya kubomoa UMOJA wa Kitaifa kwa kuendekeza Udini na Ukabila. Tumelishuhudia hili wakati wa Uchaguzi Mkuu na limejirudia tena katika Chaguzi Ndogo za Igunga na Arumeru. Tumeona jinsi CCM ya leo inavyoshangilia wasio-WAADILIFU kuwadunga sindano za mauti Wanaopinga RUSHWA na UBADHILIFU wa Mali za Umma. Na kubwa zaidi sote tu mashahidi, kwa CCM ya leo Cheo si DHAMANA bali BIDHAA inayonunuliwa na Matajiri ili wafanikishe mambo yao kupitia migongo ya Wapiga kura.

      CCM imefanikiwa kwa muda kugeuza matumizi ya dawa zake bila kudhurika. Habari njema ni kwamba, dawa zote sasa zimefikia ukomo wa matumizi na zimegeuka sumu tena kali. Kwa sasa, UMOJA unaanzishwa na Wananchi wenyewe kuikabili CCM. Wananchi hawakubali tena kugawanywa katika makundi ya kidini wala kikabila ili CCM ipenye kuwatawala tena. Wananchi wanawataka na wanawajua watu waadilifu. Na wanapojitokeza wanaogawa RUSHWA, wananchi wanaipokea na kuila lakini haibatilishi maamuzi yao yaliyo sahihi moyoni. Au wanaitumia hiyo pesa ya RUSHWA kumchangia mtu muadilifu wampendaye ili afikie hatma ya kuwa kiongozi wao. Hili limethibitika katika Uchaguzi Mkuu na limejirudia tena hivi karibuni huko Arumeru Mashariki. Kiongozi ambaye Wananchi wanamhitaji ni yule atakaye waongoza katika kutetea HAKI zao na kuwaunganisha KUJILETEA maendeleo. Kitendo alichokifanya Kilema mmoja huko Mwanza, cha kutoa Kuku wake wa Pasaka anadishwe katika Harambee ya kuchangia madawati iliyoongozwa na Mbunge Wenje ili naye achangie watoto kupata mazingira mazuri ya kusomea ni fundisho tosha kwa CCM na watoa RUSHWA.

      Ili CCM ipone na dhahama ya sumu inayoendelea kuenea mwilini mwake, lazima kwanza itapishwe na kukamuliwa sumu zote (Ubaguzi, Rushwa, Ubadhilifu, Viongozi Uchwara/wafanyabiashara, n.k) na kisha ianze upya matumizi ya dawa zake za awali (UMOJA, UADILIFU, UONGOZI BORA, CHEO kama DHAMANA). Ni makosa ya makadirio ya kisiasa kwa CCM kufikiria jinsi itakavyobaki madarakani hapo 2015. Hili jambo haliwezekani bila matumizi makubwa yaliyopitiliza ya dola yatakaambatana na umwagaji wa damu isiyo na hatia. Kadirio sahihi kwa CCM ni kufikiri nini itakuwa “Fall-Back Position” hapo 2015 na nini kiandaliwe ili baada ya hapo warudi tena madarakani ndani ya miaka mitano (5). Ni rahisi kwa CCM kurudi ndani ya muda mfupi namna hii kwa sababu, pamoja na maandalizi yanayoendelea kwenye vyama vya upinzani kushika dola, bado ni yatima wa mipango na rasilimali watu makini wa kutekeleza na kukidhi matumaini ya Wananchi ndani ya kipindi kifupi cha miaka mitano (5). Vyama vya Upinzani vimefanya na vinaendelea kufanya makosa makubwa sana kwa kuacha wananchi kuweka matumaini makubwa kupitiliza juu ya nini watakifanya wakiingia madarakani. Wamewaaminisha wanancnhi kwamba kile walichoshindwa CCM kwa miaka 54 (hapo 2015) wao watakifanikisha ndani ya miaka mitano! Kwa kosa hili, wategemee kuchukiwa haraka sana na kupingwa na wananchi hao hao watakaokuwa wamewapa ushindi. Ebu nisitoke ndani ya mada maana hii tayari ni mada nyingine kabisa.

      Nakutakia tafakuri njema.
      Last edited by English Learner; 26th June 2012 at 09:04.
      Shomari and andrews like this.

    6. #5
      dguyana's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th January 2011
      Posts : 426
      Rep Power : 508
      Likes Received
      109
      Likes Given
      66

      Default Re: Zilizokuwa Dawa za CCM, Ndizo Sumu Zinazoiua CCM!

      ukitaka kufanya biashara ya vitabu unaweza kuwa milionea ukitumia mifumo ya ccm. Ina mafunzo mengi na vituko vya kusisimua vya kukaa kwenye simulizi.


    7. #6
      andrews's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 28th March 2012
      Posts : 1,683
      Rep Power : 0
      Likes Received
      142
      Likes Given
      76

      Default Re: Zilizokuwa Dawa za CCM, Ndizo Sumu Zinazoiua CCM!

      ​tatizo la watanzania wengi ni wavivu wa kusoma hata magazeti lakini ujumbe mzuri sana
      English Learner likes this.

    8. #7
      Blayi wa Mpwapwa's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 15th January 2012
      Posts : 106
      Rep Power : 392
      Likes Received
      41
      Likes Given
      0

      Default Re: Zilizokuwa Dawa za CCM, Ndizo Sumu Zinazoiua CCM!

      Ni kweli kabisa CCM ilikiuka utamaduni iliwojiwekea yenyewe ya kuwa na viongozi WAADILIFU kama POUL SIOZIGWA na kuruhusu kubakwa na viongozi matapeli kama akina ADEN RAGE ambao background zao hawana hata chembe za sifa za uongozi

    9. #8
      king Chuga's Avatar
      Member Array
      Join Date : 21st December 2012
      Posts : 53
      Rep Power : 333
      Likes Received
      1
      Likes Given
      1

      Default Kwa nini najisikia kukata tamaa ninaposikia jina Jakaya Mrisho Kikwete?!!!!!

      Salaam Wanabodi!

      Huyu mtu aliingia madarakani mwaka 2005 huku akituhakikishia maisha bora kwa kila mtanzania na kusema kwamba kuchekacheka kwake kuna msimamo katika mambo ya msingi!

      Jakaya Mrisho Kikwete alibeba matumaini ya watanzania maskini tena mafukara wa kutupwa akiwaahidi ahadi mbalimbali za Uongo mpaka kufikia kupata zaidi ya 80% kura zote zilizopigwa na kuwaacha mbali wapinzani wake! Ingawa mwaka 2010 zilishuka sana na kuna tetesi kwamba alishindwa uchaguzi!

      Kinachonifanya nikate tamaa na rais wangu Jakaya M.Kikwete ni kushindwa kudhibiti vitu vifuatavyo.

      (a).Deni la Taifa:
      Ndugu rais wangu JK umeshindwa kudhibiti deni hili mpaka sasa tunaambiwa linafikia trilion 20,hivi una uhakika na uhalali wa deni hilo? Mbona uko kimya? Tulikopa ili kufanya nini? Tunapewa majibu mepesi kwamba ni umeme wa gesi na maji!hivi kweli umeme na maji ndio trilioni 20? Jamani rais Kikwete unatupeleka wapi nchi hii?

      (b)Mfumuko wa bei
      kwa uzoefu nilionao sijawahi kuona mfumuko wa bei wala kusikia kwa kiwango kilichofikiwa na serikali ya awamu ya nne ya rais Jakaya Kikwete tangu uhuru,mfumuko wa bei unatisha sana ndugu Rais kikwete watu wanalalamika sana na hasa vijana na akina mama.

      (C).Udhibiti wa Rushwa.
      Hivi sasa kwenye ofisi za serikali na hasa jeshi la polisi Rushwa imekuwa ni kitu cha kawaida sana! Ukienda kupata huduma bila rushwa bila rushwa kwanza mtoa huduma anakushangaa wewe vipi kwani hujui utaratibu wa ofisi? Kwa hapo unatuambiaje watanzania!

      (d)Ufisadi wa Elimu wa baadhi ya mawaziri!
      Mawaziri kiboko na wa ajabu wametokea kipindi hiki kama vile Mulugo(Amim)kununua cheti cha mtu na bado akapata uwaziri je kuna ajenda gani hapo? Ni fadhila au ni ukada?
      (e)Mauaji ya raia wasio na hatia!
      Rais uko kimya kabisa hatujui umekusudia nini katika nchi yetu au una malengo gani kwani umekuwa ukihudhuria misiba ya wasanii tu!

      (F)Malumbano ya kidini.
      Kulizungumzia hili inatakiwa kuwa na moyo mgumu sana,malumbano haya yameanza na kukua kwa kasi awamu hii ya nne,Je nchi inaelekea wapi?

      Inanikatisha tamaa sana ninapowaza mambo hayo,je wewe mwana Jf una maoni gani? hii ni kwa mustakabali wa Nchi yetu.karibuni.!

    10. #9
      Wimana's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th June 2012
      Posts : 1,053
      Rep Power : 558
      Likes Received
      284
      Likes Given
      180

      Default Nathubutu kusema; hatujawahi kupata Serikali dhaifu kama hii!

      Watetezi wa Serikali ya JK, watadai Rais ni msikivu, watadai Rais ni muumini wa demokrasia na utawala bora!
      Mimi nasema, hatujapata kuwa na Serikali dhaifu kama hii tangu Uhuru, ingawa imeingia madarakani wakati kodi inakusanywa zaidi, hazina ikiwa imenona zaidi.
      Ni awamu ambayo sheria haziheshimiwi, WaTz hawaviamini vyombo vya dola, na ufisadi umeota mizizi zaidi, uongozi na kuteuliwa uongozi kunaitwa "kuula".
      Nathubutu kusema kuwa iwapo tutapata Serikali kama hii 2015 hali itakuwa mbaya zaidi.
      Doroth, Kiwi, measkron and 3 others like this.

    11. #10
      englibertm's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st May 2009
      Posts : 1,315
      Rep Power : 776
      Likes Received
      578
      Likes Given
      10

      Default Re: Nathubutu kusema; hatujawahi kupata Serikali dhaifu kama hii!

      wanaotetea si wakombi tu wanadhani watapewa shafu.
      measkron likes this.

    12. #11
      Father of All's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2012
      Posts : 3,093
      Rep Power : 1045
      Likes Received
      1830
      Likes Given
      3343

      Default Re: Nathubutu kusema; hatujawahi kupata Serikali dhaifu kama hii!

      Hiyo ndiyo sirikali ya Jakaya Kikwete chaguo la Mungu kuwaudhi watanzania ili wajikomboe. Kuna kipindi kila shari huwa na neema na kila neema huwa na shari. Ni suala la waathirika kutathmini na kujitathmini na kuamua the way forward. Tusimlaumu Kikwete bali tutumie udhaifu wake kujikomboa na kuikomboa nchi yetu. Mbona nchi nyingine wameweza? Nani alituroga tuishie kulalamika badala ya kufanya kweli?
      Quote By Wimana
      Watetezi wa Serikali ya JK, watadai Rais ni msikivu, watadai Rais ni muumini wa demokrasia na utawala bora!
      Mimi nasema, hatujapata kuwa na Serikali dhaifu kama hii tangu Uhuru, ingawa imeingia madarakani wakati kodi inakusanywa zaidi, hazina ikiwa imenona zaidi.
      Ni awamu ambayo sheria haziheshimiwi, WaTz hawaviamini vyombo vya dola, na ufisadi umeota mizizi zaidi, uongozi na kuteuliwa uongozi kunaitwa "kuula".
      Nathubutu kusema kuwa iwapo tutapata Serikali kama hii 2015 hali itakuwa mbaya zaidi.

    13. #12
      artorius's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th January 2012
      Posts : 529
      Rep Power : 478
      Likes Received
      100
      Likes Given
      0

      Default Re: Nathubutu kusema; hatujawahi kupata Serikali dhaifu kama hii!

      serikali legelege
      measkron likes this.

    14. #13
      Mzee wa Rula's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th October 2010
      Posts : 6,385
      Rep Power : 12714
      Likes Received
      2195
      Likes Given
      1820

      Default Re: Nathubutu kusema; hatujawahi kupata Serikali dhaifu kama hii!

      Serikali inayoendekez propaganda na kutake advantage ya ujinga wa Watanzania siku wakijanjaruka nchi hii haitatawalika.

      Deni la taifa linaongezeka kwa kasi kama speed ya ndege ya Fastjet kutoka Dia - Kia na wananchi bado tunachekelea.

    15. #14
      Wimana's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th June 2012
      Posts : 1,053
      Rep Power : 558
      Likes Received
      284
      Likes Given
      180

      Default

      Quote By Father of All
      Hiyo ndiyo sirikali ya Jakaya Kikwete... Kuna kipindi kila shari huwa na neema na kila neema huwa na shari. Ni suala la waathirika kutathmini na kujitathmini na kuamua the way forward. Tusimlaumu Kikwete bali tutumie udhaifu wake kujikomboa na kuikomboa nchi yetu. Mbona nchi nyingine wameweza? Nani alituroga tuishie kulalamika badala ya kufanya kweli?
      Maandamano ya Mtwara, ni ujumbe kuwa hata wale waliodhaniwa kuwa vilaza wameshajua udhaifu wa serikali hii.
      Father of All and BHULULU like this.

    16. #15
      Wimana's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th June 2012
      Posts : 1,053
      Rep Power : 558
      Likes Received
      284
      Likes Given
      180

      Default

      Quote By Mzee wa Rula
      Serikali inayoendekez propaganda na kutake advantage ya ujinga wa Watanzania siku wakijanjaruka nchi hii haitatawalika.

      Deni la taifa linaongezeka kwa kasi kama speed ya ndege ya Fastjet kutoka Dia - Kia na wananchi bado tunachekelea.
      Si umeona watu wa Mtwara juzi? Ni ishara mbaya.
      Serikali inayowaza kututawala kutumia hata hila za propaganda za kutugawa kidini na kikabila.

    17. #16
      GunzInTheAir's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th May 2011
      Posts : 301
      Rep Power : 469
      Likes Received
      21
      Likes Given
      24

      Default Re: Nathubutu kusema; hatujawahi kupata Serikali dhaifu kama hii!

      Quote By Wimana
      Maandamano ya Mtwara, ni ujumbe kuwa hata wale waliodhaniwa kuwa vilaza wameshajua udhaifu wa serikali hii.
      kilaza mkubwa wewe

    18. #17
      Wimana's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th June 2012
      Posts : 1,053
      Rep Power : 558
      Likes Received
      284
      Likes Given
      180

      Default

      Quote By GunzInTheAir
      kilaza mkubwa wewe
      Mkuu sina nia mbaya, ndio maana nimetumia "waliodhaniwa". Hata kwenye ujumbe wao kwa Serikali, wametumia maneno yanayofanana na hayo.

    19. #18
      Chiya Chibi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th July 2011
      Location : Penye Oxygen
      Posts : 441
      Rep Power : 487
      Likes Received
      102
      Likes Given
      12

      Default Re: Nathubutu kusema; hatujawahi kupata Serikali dhaifu kama hii!

      Ukweli uko waz, hatuna haja ya kujadili sana, na tusitegemee kitu kipya kwa miaka hii iliyobaki..! Ila tusichoke kupiga kelele, mana tukinyamaza nchi ndo itauzwa kabisa.!

    20. #19
      Ikwanja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th July 2011
      Posts : 553
      Rep Power : 508
      Likes Received
      106
      Likes Given
      48

      Default Re: Nathubutu kusema; hatujawahi kupata Serikali dhaifu kama hii!

      aliposema Mnyika wengi hamkuelewa, afadhali wewe umeokoka leo. hii serikali ni dhaifu

    21. #20
      kigoda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th October 2012
      Posts : 664
      Rep Power : 464
      Likes Received
      99
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By GunzInTheAir
      kilaza mkubwa wewe
      wewe ndio kilaza unakurupuka bila kuelewa hata kinaongelewa nini gamba we.

    Page 1 of 3 123 LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...